Dola zimeadimika kwasababu wageni wanavuna fedha za miradi kuliko wazawa

Dola zimeadimika kwasababu wageni wanavuna fedha za miradi kuliko wazawa

Inategemea na time frame, not miradi yote tunaweza fanya kwa style hiyo.
Although ninwazo zuri
Ni lazima yote kufanya hivyo.Kama tumepiga marufuku kuchimba Madini mkakati bila kufanya value addition ndani ya Nchi hilo la wakandarasi ni very minor ,na miradi ya hivyo ratio iwe 60% vs 40% au hata 50% vs 50% kabisa
 
kama ulikua hujui nikwambie tu kuwa hao wakandarasi wa bongo ni tia maji sana, wengi wao ni wezi na hawako punctual kwenye kazi zao, uvivu [kazi ya mwezi itakamilika ndani ya mwaka kwa visingizio vingi sana] - talking from experience.
Shida kubwa kwa wakandarasi wazalendo ni kucheleweshewa malipo. Ukishapewa malipo ya mwanzo hayo madai mengine haulipwi kwa muda wa siku 28 kadri ya mikataba baada ya tathmini ya kazi iliyokwishakamilika. Wanasingizia pesa haijatoka wizarani. Pia wizarani wanatoa kipaumbele kwa wa nje maana watashtaki ila wa hapa ukishtaki mwisho wa kupewa tenda. Hivyo ulipaji ndio unaochelewesha kazi kwa wakandarasi wazalendo. Kama ni uongo kila mwaka bajeti wanasema kuna madai ya wakandarasi. INAKUWAJE PAWE NA MADAI AMBAYO NI KAZI ZILIZOPIMWA NA KUHITAJIKA KULIPWA KWA MUDA WA MKATABA MPAKA MADAI HAYO YAWEKWE KWENYE BAJETI WAKATI TAYARI PESA ILIKUWEPO KATIKA MWAKA UNAOISHA KABLA YA BAJETI? HIVYO TUNAJIFICHA KWA WAKANDARASI WAZALENDO JUU YA UKOSEFU WA PESA. MASIKINI MPAKA WENGINE WANABANWA NA MABENKI WALIYOKOPA. WAKANDARASI NA WALIPAJI WANALIELEWA HILI.
 
Kila siku tunalia kuhusu kuadikika Kwa Dola licha ya juhudi za kukuza Uchumi lakini hakuna ambae anajadili jambo Hilo Kwa kuangalia sababu za msingi.

Mojawapo ya vitu vinavyosababisha kuadikika Kwa Dola Nchini no hizo hapa 👇

1. Kuwapa kazi za Ujenzi wakandarasi wa kigeni badala ya wazawa Kwa visingizio vya hawana uwezo na uzoefu(wageni hulipwa Kwa Dola)

2. Kuagiza bidhaa nyingi ambazo tunaweza Kuzalisha wenyewe ndani ya mwaka eg maziwa,ngano,Mafuta ya kula,sabuni,vyakula vya mifugo,mbegu nk

3. Kukwamisha uwekezaji kutoka Nje kutokana na mitizamo ya siasa za ujamaa(kusema Nchi imeuzwa Kwa Waarabu,kuwa na sera ambazo hazitabiriki,Urasimu wa Kiserikali na Rushwa) eg miradi ya Lindi LNG na Liganga imekwama kutokana na siasa uchwara.

---
WAGENI WAVUNA FEDHA ZA MIRADI KULIKO WAZAWA

SERIKALI imesema asilimia kubwa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inawanufaisha wageni kutoka nje ya nchi kuliko wazawa.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema bungeni Dodoma kuwa sababu kubwa inayochangia hali hiyo ni uwezo mdogo wa makandarasi wa ndani wa kifedha, mitambo na wataalamu hivyo inakuwa vigumu kwao kushindana kwenye zabuni za kazi na makandarasi kutoka nje hasa kampuni za Kichina.

Bashungwa amesema hayo akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/25 bungeni Dodoma jana. Alisema kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Usajili wa Makandarasi, kati ya miradi 36,839, wazawa walitekeleza miradi 35,351 sawa na asilimia 95.9 ya miradi hiyo.

Hata hivyo, Bashungwa amesema miradi iliyotekelezwa na wazawa ni midogomidogo yenye thamani ya Sh trilioni 23.749, sawa na asilimia 38.5 ya thamani ya miradi yote iliyosajiliwa na kutekelezwa katika kipindi hicho ambayo ni Sh trilioni 61.638.

“Hivyo, makandarasi wa nje ambao ni takribani asilimia 4.1 walitekeleza miradi michache yenye thamani kubwa (asilimia 61.5 ya thamani ya miradi yote),” amesema Bashungwa.

Kwa mujibu wake, kuna kampuni 14,800 za ndani za makandarasi, za ushauri wa wahandisi ni 252 na kampuni za wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ni 461.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Naunga mkono wazo la Bashungwa kuanza kuwaamini Wakandarasi Wazawa.Sheria hii isiishie Wizara ya Ujenzi pekee Bali Taasisi zote.Tanzania sio Mali ya Wachina pekee.
Wizara zimekaliwa na watu wenye uwezo duni na vibaka!
 
Hapo Sumbawanga ujenzi wa Mradi wa Tactic km 12 kapewa Mchina wakati Sumry anaweza.

Mbeya Jiji km 15 kapewa Mchina wakati Wazawa wapo .

Huu upumbavu ukome mara Moja.
Wakandarasi wa ndani wenyewe wakipewa kazi mnawapiga hamwalipi kwa wakati huo uwezo wa kimitaji na mitambo anaupata vipi.

Mkandarasi anapewa kazi anafanya kwa tabu sana halafu analipwa baada ya miaka 10 toka akamilishe mradi na hela yenyewe anaipata kwa kugawana na wahuni walioko kwenye mfumo.
 
Wakandarasi wa ndani wenyewe wakipewa kazi mnawapiga hamwalipi kwa wakati huo uwezo wa kimitaji na mitambo anaupata vipi.

Mkandarasi anapewa kazi anafanya kwa tabu sana halafu analipwa baada ya miaka 10 toka akamilishe mradi na hela yenyewe anaipata kwa kugawana na wahuni walioko kwenye mfumo.
Kwa sababu sera haikuwa inawapa kipaombele ila Kwa Sasa yote hayo yatakuwa addressed.

Najua hujui kwamba Kuna Samia Infrastructure bond imeanzishwa Kwa Ajili ya wakandarasi kupata pesa na dhamana za kazi.
 
uchumi wa maframe

nchi ya kichuuzi

unatategemea kupata dola kweli

nyie wazawa biashara zenu mabar,na usanii kukata mauno

ova
 
Tunamtakia tuwajengee uwezo wa ndani kwanza baadae wamikua wataenda Nje.
Nje wana viwango vya juu sana? So swali langu bado hata wakienda nje je watatekeleza kwa viwango vya kwao?

Nafikiri ni vema wakawa attached kwenyenmakampuni ya nje, wapate uzoefu kwanza kabla ya kurudi nyumbani
 
Kila siku tunalia kuhusu kuadikika Kwa Dola licha ya juhudi za kukuza Uchumi lakini hakuna ambae anajadili jambo Hilo Kwa kuangalia sababu za msingi.

Mojawapo ya vitu vinavyosababisha kuadikika Kwa Dola Nchini no hizo hapa 👇

1. Kuwapa kazi za Ujenzi wakandarasi wa kigeni badala ya wazawa Kwa visingizio vya hawana uwezo na uzoefu(wageni hulipwa Kwa Dola)

2. Kuagiza bidhaa nyingi ambazo tunaweza Kuzalisha wenyewe ndani ya mwaka eg maziwa,ngano,Mafuta ya kula, sabuni, vyakula vya mifugo, mbegu nk

3. Kukwamisha uwekezaji kutoka Nje kutokana na mitizamo ya siasa za ujamaa(kusema Nchi imeuzwa Kwa Waarabu,kuwa na sera ambazo hazitabiriki,Urasimu wa Kiserikali na Rushwa) eg miradi ya Lindi LNG na Liganga imekwama kutokana na siasa uchwara.

---
WAGENI WAVUNA FEDHA ZA MIRADI KULIKO WAZAWA

SERIKALI imesema asilimia kubwa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inawanufaisha wageni kutoka nje ya nchi kuliko wazawa.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema bungeni Dodoma kuwa sababu kubwa inayochangia hali hiyo ni uwezo mdogo wa makandarasi wa ndani wa kifedha, mitambo na wataalamu hivyo inakuwa vigumu kwao kushindana kwenye zabuni za kazi na makandarasi kutoka nje hasa kampuni za Kichina.

Bashungwa amesema hayo akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/25 bungeni Dodoma jana. Alisema kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Usajili wa Makandarasi, kati ya miradi 36,839, wazawa walitekeleza miradi 35,351 sawa na asilimia 95.9 ya miradi hiyo.

Hata hivyo, Bashungwa amesema miradi iliyotekelezwa na wazawa ni midogomidogo yenye thamani ya Sh trilioni 23.749, sawa na asilimia 38.5 ya thamani ya miradi yote iliyosajiliwa na kutekelezwa katika kipindi hicho ambayo ni Sh trilioni 61.638.

“Hivyo, makandarasi wa nje ambao ni takribani asilimia 4.1 walitekeleza miradi michache yenye thamani kubwa (asilimia 61.5 ya thamani ya miradi yote),” amesema Bashungwa.

Kwa mujibu wake, kuna kampuni 14,800 za ndani za makandarasi, za ushauri wa wahandisi ni 252 na kampuni za wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ni 461.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Naunga mkono wazo la Bashungwa kuanza kuwaamini Wakandarasi Wazawa.Sheria hii isiishie Wizara ya Ujenzi pekee Bali Taasisi zote.Tanzania sio Mali ya Wachina pekee.
Tukikwambia ccm ni laana ya hili taifa ndo uwe unatuelewa
 
Nje wana viwango vya juu sana? So swali langu bado hata wakienda nje je watatekeleza kwa viwango vya kwao?

Nafikiri ni vema wakawa attached kwenyenmakampuni ya nje, wapate uzoefu kwanza kabla ya kurudi nyumbani
Lazima wapate uzoefu kutoka hapa ndio wataenda Nje.Wachina waliopata uzoefu kwao
 
Back
Top Bottom