Donald Trump apatikana na hatia ya makosa yote 34 katika kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya

Sikujua kama Marekani ina figisu kama za Afrika!
Madaraka na uongozi yana vita sana.
1. Marekani wanatumia mfumo wa jury,
2. Mwendesha mashitaka wa jimbo hateuliwi na Rais au gavana bali anachaguliwa na raia wapiga kura
3. Jaji lazima athibitishwe na seneti,
 
Mkuu,kwani hajakutwa na hayo mashtaka aliyotuhumiwa nayo,ameonewa?

Wenzetu si Sheria za zipo vyema, basi akate rufaa.
 

kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya​


Umebadili headline lakini bado umechemka, bado unahangaika kuelewa kilichomtia hatiani, bado unatuingiza mkenge.

Trump hajapatikana na hatia ya kutaka kuficha kuhusu hela alizompatia pornstar ili akae kimya.

Ukimlipa changudoa ili akutunzie siri ya kulala nae sio kesi mahala popote duniani.

Dunia ya tatu na waandishi wetu masikini ya Mungu, tunatia huruma.
 
Huyo mzee kaitingisha sana establishment ya Marekani...waliojiona wao ndo familia za siasa zote kazitingisha....
Establishment ya Marekani ni ipi?
Wakina nani waliojiona wao ndo familia za siasa zote?
 
Marekani bado ina wabaguzi wengi sana hasa vijijini ambao hawakufurahia ushindi wa Obama. Trump aliibuka kiongozi wa kupinga uhalali wa Obama hadharani na hata alipoanza kampeini za kişi asa kete yake kubwa ikawa ni siasa zenye mlango wa ubaguzi. Hivyo wabaguzi wote wakawa wafuasi wake wakajichnganya na walokole waliofurahia ubavu I wake dhidi ya waislamu pamoja na republicans wote ambao walimwona amevuta wapiga kura ambao zamani walikuwa hawapigi kura
 
Trump alianzisha conspiracy Obama hajazaliwa Marekani na kwamba ni Muislamu
 
Taifa la demokrasia duniani leo hii Mahakma imemtia hatiani Rais mstaafu wa Marekani D.Trumph kwa makosa 34 yanayo daiwa ni ya mchongo, yenye lengo la kumaliza kisiasa.

kama ni kweli, je mataifa mengine yanajifunza nini kutoka Taifa kubwa la Marekani?

ingekuwa hapa kwetu Tz mpinzani amefungwa kwa makosa ya jinai ingeonekana vp?
kuna jambo la kujifunza kutokana na hukumu ya Trumph.
 
Trump anatakiwa kuwa jela. Bado kesi ya kuondoka na nyaraka za siri na kwenda nazo kwake alipoachia urais. Bado kesi ya kuchochea vurugu za January 6 2021(Laiti yule mwendesha mashtaka asingekuwa mpunbavu). Bado kesi ya kudanganya kuhusu mali zake. Ni mhalifu sugu. Hana tofauti na Zuma.
 
Makosa ya mchongo? Mimi najua kosa moja alimpa hela kahaba (ili asiseme kuwa alimgegeda) Stormy Daniels kuptia msaidizi wake Cohen, ambayo ni tuhuma ya kweli. Tujifunze kwa wenzetu hakuna aliye juu ya sheria.
 
Makosa ya mchongo? Mimi najua kosa moja alimpa hela kahaba (ili asiseme kuwa alimgegeda) Stormy Daniels kuptia msaidizi wake Cohen, ambayo ni tuhuma ya kweli. Tujifunze kwa wenzetu hakuna aliye juu ya sheria.
Kwaiyo tuhuma ni kumchakata pornstar au kutumia hela yake kumuhonga pornstar
 
Trump amehukumiwa kuchakachua nyaraka za kibiashara kuficha malipo kwa porn star(mcheza filamu za ngono) aliyefanya naye mapenzi ili kumnyamazisha na kufanikisha matokeo ya uchaguzi yawe na faida kwake.

Kuingilia uchaguzi kwa namna hii Marekani ni kosa kubwa sana, hairuhusiwi kulipa watu ili wakufichie siri zako mbaya kwa wapiga kura na kukuwezesha kushinda uchaguzi.
 
Kwa kumkuta na hatia kwa mashtaka yote 34, hiyo yatoa mwanya kwa mawakili wake kukata rufaa ambayo yaweza kupunguza hatua hizo na kisha hukumu nzima kuangaliwa upya.
Kukata rufaa ni haki yake tu hata kama angekutwa na hatia kwa kosa 1, kukutwa na hatia na makosa yote 34 na jurors 12 bila kutofautiana inaonyesha jinsi gani ushahidi wa kumtia hatiani ulivyokuwa mzito.
 
Hata hakujitahidi kuficha. Alificha chooni🤣
 
Hush money trial daah
Mimi mtu wa mahenge huku Iringa ndani ndani nitaelewa nini?
 
Usijichetue akili,

Majaji na waendesha mashitaka wa Tanzania wanapatikanaje??

Tanzania mnatumia mfumo wa jurors?

Umewahi kusikia Marekani kiongozi wa kisiasa anaamuru kwa polisi/FBI mtu kukamatwa au kuwekwa rumande?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…