Donald Trump apatikana na hatia ya makosa yote 34 katika kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya

Donald Trump apatikana na hatia ya makosa yote 34 katika kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya

Sikujua kama Marekani ina figisu kama za Afrika!
Madaraka na uongozi yana vita sana.
1. Marekani wanatumia mfumo wa jury,
2. Mwendesha mashitaka wa jimbo hateuliwi na Rais au gavana bali anachaguliwa na raia wapiga kura
3. Jaji lazima athibitishwe na seneti,
 
Marekani ishageuka kuwa banana republic. Democrats wameiharibu nchi!

Absolutely garbage case. Total embarrassment for the American justice system.

Ipo siku na wao [Democrats] yatawatokea puani.

Now I want Trump to win in November.

Sipendi kabisa uonevu wa aina yoyote ile, hususan wa kisiasa.

Weaponizing the justice system to hurt your political opponents is the hallmark of a banana republic!!

Tofauti ya Democrats na CCM ni nini? 🤣

Shameful.
Mkuu,kwani hajakutwa na hayo mashtaka aliyotuhumiwa nayo,ameonewa?

Wenzetu si Sheria za zipo vyema, basi akate rufaa.
 

kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya​


Umebadili headline lakini bado umechemka, bado unahangaika kuelewa kilichomtia hatiani, bado unatuingiza mkenge.

Trump hajapatikana na hatia ya kutaka kuficha kuhusu hela alizompatia pornstar ili akae kimya.

Ukimlipa changudoa ili akutunzie siri ya kulala nae sio kesi mahala popote duniani.

Dunia ya tatu na waandishi wetu masikini ya Mungu, tunatia huruma.
 
Huyo mzee kaitingisha sana establishment ya Marekani...waliojiona wao ndo familia za siasa zote kazitingisha....
Establishment ya Marekani ni ipi?
Wakina nani waliojiona wao ndo familia za siasa zote?
 
Huyo mzee kaitingisha sana establishment ya Marekani...waliojiona wao ndo familia za siasa zote kazitingisha....Ukimuona kisiasa ni kama hana wafuasi na kumbe anawafuasi.
Wanamtafuta mpaka basi....mara impeachment, mara majahaba, mara mambo ya kodi, yaani hawampumzishi.Angekua mtu mwepesi kihisia aliishakimbia mchezo zamani sana.
Huyu mzee kuna kitu anacho maana sio kwa kumsumbua hivi
Marekani bado ina wabaguzi wengi sana hasa vijijini ambao hawakufurahia ushindi wa Obama. Trump aliibuka kiongozi wa kupinga uhalali wa Obama hadharani na hata alipoanza kampeini za kişi asa kete yake kubwa ikawa ni siasa zenye mlango wa ubaguzi. Hivyo wabaguzi wote wakawa wafuasi wake wakajichnganya na walokole waliofurahia ubavu I wake dhidi ya waislamu pamoja na republicans wote ambao walimwona amevuta wapiga kura ambao zamani walikuwa hawapigi kura
 
Marekani bado ina wabaguzi wengi sana hasa vijijini ambao hawakufurahia ushindi wa Obama. Trump aliibuka kiongozi wa kupinga uhalali wa Obama hadharani na hata alipoanza kampeini za kişi asa kete yake kubwa ikawa ni siasa zenye mlango wa ubaguzi. Hivyo wabaguzi wote wakawa wafuasi wake wakajichnganya na walokole waliofurahia ubavu I wake dhidi ya waislamu pamoja na republicans wote ambao walimwona amevuta wapiga kura ambao zamani walikuwa hawapigi kura
Trump alianzisha conspiracy Obama hajazaliwa Marekani na kwamba ni Muislamu
 
Taifa la demokrasia duniani leo hii Mahakma imemtia hatiani Rais mstaafu wa Marekani D.Trumph kwa makosa 34 yanayo daiwa ni ya mchongo, yenye lengo la kumaliza kisiasa.

kama ni kweli, je mataifa mengine yanajifunza nini kutoka Taifa kubwa la Marekani?

ingekuwa hapa kwetu Tz mpinzani amefungwa kwa makosa ya jinai ingeonekana vp?
kuna jambo la kujifunza kutokana na hukumu ya Trumph.
 
Trump anatakiwa kuwa jela. Bado kesi ya kuondoka na nyaraka za siri na kwenda nazo kwake alipoachia urais. Bado kesi ya kuchochea vurugu za January 6 2021(Laiti yule mwendesha mashtaka asingekuwa mpunbavu). Bado kesi ya kudanganya kuhusu mali zake. Ni mhalifu sugu. Hana tofauti na Zuma.
 
Makosa ya mchongo? Mimi najua kosa moja alimpa hela kahaba (ili asiseme kuwa alimgegeda) Stormy Daniels kuptia msaidizi wake Cohen, ambayo ni tuhuma ya kweli. Tujifunze kwa wenzetu hakuna aliye juu ya sheria.
 
Makosa ya mchongo? Mimi najua kosa moja alimpa hela kahaba (ili asiseme kuwa alimgegeda) Stormy Daniels kuptia msaidizi wake Cohen, ambayo ni tuhuma ya kweli. Tujifunze kwa wenzetu hakuna aliye juu ya sheria.
Kwaiyo tuhuma ni kumchakata pornstar au kutumia hela yake kumuhonga pornstar
 
Mkuu, hii kesi leo wazee wa baraza wamemtia hatiani Donald Trump kwa makosa yote 34 ya kughushi nyaraka kuhusiana na pesa alozitoa kwa yule mwanamke zinoitwa "Hush Money".

Hivyo akiwa madarakani akawezesha nyaraka kughushiwa yaani kuchakachua na kurekebisha mahesabu kwamba fedha alozilipa ama ni ndogo au hakikuwepo kabisa,

Hivyo hii kesi yahusu Hush Money au Hush Money Trial.

NB
Hizi fedha za hash au Hush Money ni zile fedha unozilipa kwa mchepuko ili asije kutoa siri/taarifa zako nje au kumfunga mdomo pale siri au taarifa hizo zinapoleta dhahama kwako au familia yakop na mstakabali mzima wa maisha yako.
Trump amehukumiwa kuchakachua nyaraka za kibiashara kuficha malipo kwa porn star(mcheza filamu za ngono) aliyefanya naye mapenzi ili kumnyamazisha na kufanikisha matokeo ya uchaguzi yawe na faida kwake.

Kuingilia uchaguzi kwa namna hii Marekani ni kosa kubwa sana, hairuhusiwi kulipa watu ili wakufichie siri zako mbaya kwa wapiga kura na kukuwezesha kushinda uchaguzi.
 
Kwa kumkuta na hatia kwa mashtaka yote 34, hiyo yatoa mwanya kwa mawakili wake kukata rufaa ambayo yaweza kupunguza hatua hizo na kisha hukumu nzima kuangaliwa upya.
Kukata rufaa ni haki yake tu hata kama angekutwa na hatia kwa kosa 1, kukutwa na hatia na makosa yote 34 na jurors 12 bila kutofautiana inaonyesha jinsi gani ushahidi wa kumtia hatiani ulivyokuwa mzito.
 
Tatizo kubwa la Trump ni majivuno na kiburi chake.

Kilichomponza Trump ni ego yake. Kosa la kwanza la kumlipa mwanamke afiche siri siyo siyo crime, linakuwa crime tu kama lilifanyika ili kuficha kosa jingine. Sasa hapo kwenye ufichaji wa kosa jingine ndipo ego ya trump ilipompoza kwani iliwezekana kabisa kumlipa bila kuhusisha na uchaguzi ila akagtumia njia za kuwadharau waliokuwa wanamsaidia, na ndio waliomtosa.

Ukifuatia kosa la documents liliko mahakama ya Miami, nayo utagundua pia kuwa ni ego yake ndiyo iliyomletea matatizo. Idara ya kumbukumbu ilimwomba makaratasi matatu tu: (a) Barua aliyoachiwa na Obama (b) Barua aliyoandikiwa na Kim Jong Il (c) ramani iliyokuwa inatumika kuonyesha njia ya Hurricane Dorian. Lakini yeye kwa ego yake akawasumbua kwa zaidi ya mwaka mzima mpaka wakatumia amri ya mahakama na mwishowe kuvamia nyumbani kwa na kukuta document nyingi za serikali ambazo hakutakiwa kuwa nazo ambazo alikuwa anajitahidi sana kuzificha.

Baada ya kujikuta kuwa kosa lake dogo la ego limezaa tatizo kubwa kisheria, yeye anageuza kuwa la kisiasa na majuzi tu anasema kuwa Biden aliamuru FBI watumie deadly force kumkamata na kusahahu kuwa issue ilikuwa ni idara ya nyaraka za serikali.
Hata hakujitahidi kuficha. Alificha chooni🤣
 
Mkuu, hii kesi leo wazee wa baraza wamemtia hatiani Donald Trump kwa makosa yote 34 ya kughushi nyaraka kuhusiana na pesa alozitoa kwa yule mwanamke zinoitwa "Hush Money".

Hivyo akiwa madarakani akawezesha nyaraka kughushiwa yaani kuchakachua na kurekebisha mahesabu kwamba fedha alozilipa ama ni ndogo au hakikuwepo kabisa,

Hivyo hii kesi yahusu Hush Money au Hush Money Trial.

NB
Hizi fedha za hash au Hush Money ni zile fedha unozilipa kwa mchepuko ili asije kutoa siri/taarifa zako nje au kumfunga mdomo pale siri au taarifa hizo zinapoleta dhahama kwako au familia yakop na mstakabali mzima wa maisha yako.
Hush money trial daah
Mimi mtu wa mahenge huku Iringa ndani ndani nitaelewa nini?
 
Taifa la demokrasia duniani leo hii Mahakma imemtia hatiani Rais mstaafu wa Marekani D.Trumph kwa makosa 34 yanayo daiwa ni ya mchongo, yenye lengo la kumaliza kisiasa.

kama ni kweli, je mataifa mengine yanajifunza nini kutoka Taifa kubwa la Marekani?

ingekuwa hapa kwetu Tz mpinzani amefungwa kwa makosa ya jinai ingeonekana vp?
kuna jambo la kujifunza kutokana na hukumu ya Trumph.
Usijichetue akili,

Majaji na waendesha mashitaka wa Tanzania wanapatikanaje??

Tanzania mnatumia mfumo wa jurors?

Umewahi kusikia Marekani kiongozi wa kisiasa anaamuru kwa polisi/FBI mtu kukamatwa au kuwekwa rumande?
 
Back
Top Bottom