Donald Trump Pamoja na kupigwa Risasi na Kujeruhiwa lakini hapiti kwenye vyombo vya habari kuichafua Marekani kama alivyofanya Lissu kwa Tanzania

Mjifunze kuwa wazalendo kwa Taifa letu na kuacha kuwa waropokaji hovyo hovyo.Embu niambie kwanini Trump hajakwenda kuishtaki Marekani na kutaka iwekewe vikwazo vya kiuchumi?
Sasa hivi ni ngumu kutofautisha uzalendo na ujinga. Ni sawa na mzazi amlawiti mtoto wake, kisha ifanywe siri maana hiyo ni kuwa mzalendo wa familia.

Marekani unaenda kuishitaki kwa nani wakati ina sheria zenye nguvu? Naona unatoa mifano irrelevant.
 
Si ndiyo nakuona wewe mbwiga niende mahakamani kabla DPP hajafungua kesi wewe zinakutosha kweli?
Kwa hiyo unasubiri Dpp afungue kesi ndio upeleke ushahidi wako? Vipi asipofungua kesi? Utaendelea kukaa na ushahidi wako chumbani kwako?
 
Kwa hiyo unasubiri Dpp afungue kesi ndio upeleke ushahidi wako? Vipi asipofungua kesi? Utaendelea kukaa na ushahidi wako chumbani kwako?
Wewe ni mpumbavu usiwe unaongea mambo yaliyo juu ya uwezo wako wa utambuzi, unajidhalilisha sana. Kwani kazi ya kupeleleza na kufungua mashitaka anafanya nani, au unafikiri ushahidi unapelekwa mahamani kama barua ya posa iliyoletwa kwa wazazi wako wakati unaposwa? Punguza shobo ndiyo maana huteuliwi kwa ubwege wako huu. Umeleta hoja hii ambayo maudhui yakehailingani kabisa ya suala la shambulio la Lissu na shambulio la Trump na kila kakupinga na kukelimisha lakini wewe umekazania , huna akili, kama huna kazi ya kufanya kale maparachichi uchukue ngozi yako ya mbuzi utandike ulale.
 
Hongera Sanaaaa kwa mchango wako.
 
Sijasoma andiko lako, lakini tofauti ni kwamba hata kama aliempiga risasi Trump angekimbia, uhakika wa kumkamata ni zaidi ya 100% na angeshtakiwa.
Lakini huku kwetu mpaka leo muhusika wa Lisu hajakamatwa mwaka wa 7 sasa na hajulikani.
 
..wale walinzi wa serikali ya USA wanaoitwa secret service wangekuwa wameondolewa halafu Trump akapigwa risasi kungekuwa na tuhuma mbaya sana.

..au Kamera zilizokuwa eneo la tukio zingechomolewa na vyombo vya serikali, na kufanikisha mlenga shabaha asijulikane, Trump angetoa tuhuma na lawama nzito sana kwamba serikali imejaribu kumuua.
 
Lakini,si kwa hapa Domdom.
-hajawa wa kwanza kupigwa risasi.
-kifo ni kifo.
-drama za kujiteka nk wa kadhaa zinazokirihisha.
 
Lakini,si kwa hapa Domdom.
-hajawa wa kwanza kupigwa risasi.
-kifo ni kifo.
-drama za kujiteka nk wa kadhaa zinazokirihisha.

..kuna tofauti kubwa ktk mwenendo wa vyombo vya dola ktk tukio la Trump ukilinganisha na la Tundu Lissu.

..Bunge la Marekani limemuita na kumhoji Mkuu wa taasisi inayohusika na kulinda viongozi wakuu, Trump akiwa mmoja wapo.


..baada ya mahojiano hayo Mkuu wa secret service alilazimika kujiuzulu kwasababu wa uzembe wa waliokuwa chini yake ilipelekea Trump akashambuliwa.

..kwenye tukio la Tundu Lissu ni nani amechukuliwa hatua? Kwanini aliyeondoa walinzi hajakamatwa leo ni mwaka wa 7 tangu tukio litokee?
 
Mkuu JokaKuu kwanza hongera kwa maelezo yaliyonyooka.

Leo nilikaa nikajiuliza kwa majirani hapo deputy IGP , Gilbert Masengeli aliyekataa wito wa mahakama mara 7 hatimaye mahakama ikamuonyesha nguvu yake hatimaye akapanda kizimbani na kuomba radhi .

Je najiuliza mahakama za Tanzania zina nguvu gani kama zimeshindwa kumpandisha kizimbani askari wa cheo cha chini tu kama Fatma Kigondo kwa tuhuma za kukodi genge la wabakaji, kesi katupiwa DPP hatimaye kaitupilia mbali huku vyombo vya habari vikiogopa kumuadress mtuhumiwa kwa majina yake wakiishia kusema " kesi ya afande yafutwa".

Kwa matukio ya awamu ya 5 kwa nchi inayofuata utawala wa sheria Simon Sirro lazima angepandishwa kizimbani.
 
Unadhani ni nani atawajibika/kuwajibika kwa udhalimu wanaofanyiwa wakinzani wa kisiasa Tanzania ikiwa bado nje ya CCM wengine wanaonekana/kuoneshwa kama wahaini,wapotofu,si wazalendo(eti upande wa pili.Neno la kipumbavu kwa kila anayelitumia)kwa wananchi wasio na uelewa mpana wa siasa za ushindani?
 
Mwambie ukweli huyu pimbi hajielewi kabisa!
 
Tanzania inaongozwa na wapuuzi wakubwa sana!
 
Luca acha mifananisho isiyokuwa na uhai ndani yake,ungeanza na machimbuko ya sababu za matukio hayo mawili,halafu ungekuja na majumuisho wa hayo mambo mawili.
 
Luca acha mifananisho isiyokuwa na uhai ndani yake,ungeanza na machimbuko ya sababu za matukio hayo mawili,halafu ungekuja na majumuisho wa hayo mambo mawili.
Soma tena uelewe andiko langu.Lissu ni mropokaji, mkurupukaji,mbwatukaji na mtu mwenye mihemuko na utoto mwingi sana.
 
Kwa ulinganisho huu wewe jamaa upeo wako ni mdogo sana
 
Mjifunze kuwa wazalendo kwa Taifa letu na kuacha kuwa waropokaji hovyo hovyo.Embu niambie kwanini Trump hajakwenda kuishtaki Marekani na kutaka iwekewe vikwazo vya kiuchumi?
Kumbuka Biden alisemaje baada ya shambulio na tuambie mwendazake alisemaje baada ya shambulio halafu linganisha, usiwe mvivu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…