Hivi karibuni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini ya makubaliano ya awali ya mkataba wa mradi wa kuchakata na kusindika gesi asilia na kampuni za Equinor ya Norway na Shell ya Uingereza.
Rais Samia amesema mradi huo ni wa kimkakati kwa nchi ambao utakapokamilika utaingizia nchi mapato na kuinua uchumi. Mradi huu pia utazalisha ajira na kuchangia katika kujenga uwezo wa watanzania kupitia mafunzo, elimu, kuinua teknolojia na utafiti.
Dondoo za mradi huu:
Hadi kufikia mwezi Mei, 2022, jumla ya futi za ujazo trilioni 57.54 za gesi asilia ziligunduliwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini
Kati ya hizo, jumla ya futi za ujazo trilioni 47.13 ni katika vitalu vilivyopo katika kina cha bahari na futi za ujazo trilioni 10.41 ni katika maeneo ya nchi kavu, ugunduzi wa kiasi hiki kikubwa cha gesi asilia ulifanyika kwa ushirikiano wa Serikali na Makampuni.
Utekelezaji wa mradi huu katika Mkoa wa Lindi utafanyika sambamba na uendelezaji wa miundombinu kwenye mkondo wa juu ili kuwezesha kuvuna rasilimali hiyo. Mradi huu mkubwa utabadilisha sura na taswira ya uchumi wa nchi yetu.
Eneo ambalo mtambo utajengwa tayari limeshajulikana na kuwekwa katika miliki ya Serikali kwa kuwalipa fidia ya takriban Shilingi bilioni 5.71 wananchi 642 waliokuwa wakazi wa maeneo hayo.
Mradi huu unatarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi, kuiongezea Serikali mapato, kuongeza ajira na kuongeza uwezo wa Watanzania kitaaluma.
Kati ya miaka minne hadi sita ya ujenzi wa mradi huu kunatarajiwa kuwa na ajira 10,000 na baada ya kukamilika kwa ujenzi, ajira za kudumu zitakuwa 500.
Rais Samia amesema mradi huo ni wa kimkakati kwa nchi ambao utakapokamilika utaingizia nchi mapato na kuinua uchumi. Mradi huu pia utazalisha ajira na kuchangia katika kujenga uwezo wa watanzania kupitia mafunzo, elimu, kuinua teknolojia na utafiti.
Dondoo za mradi huu:
Hadi kufikia mwezi Mei, 2022, jumla ya futi za ujazo trilioni 57.54 za gesi asilia ziligunduliwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini
Kati ya hizo, jumla ya futi za ujazo trilioni 47.13 ni katika vitalu vilivyopo katika kina cha bahari na futi za ujazo trilioni 10.41 ni katika maeneo ya nchi kavu, ugunduzi wa kiasi hiki kikubwa cha gesi asilia ulifanyika kwa ushirikiano wa Serikali na Makampuni.
Utekelezaji wa mradi huu katika Mkoa wa Lindi utafanyika sambamba na uendelezaji wa miundombinu kwenye mkondo wa juu ili kuwezesha kuvuna rasilimali hiyo. Mradi huu mkubwa utabadilisha sura na taswira ya uchumi wa nchi yetu.
Eneo ambalo mtambo utajengwa tayari limeshajulikana na kuwekwa katika miliki ya Serikali kwa kuwalipa fidia ya takriban Shilingi bilioni 5.71 wananchi 642 waliokuwa wakazi wa maeneo hayo.
Mradi huu unatarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi, kuiongezea Serikali mapato, kuongeza ajira na kuongeza uwezo wa Watanzania kitaaluma.
Kati ya miaka minne hadi sita ya ujenzi wa mradi huu kunatarajiwa kuwa na ajira 10,000 na baada ya kukamilika kwa ujenzi, ajira za kudumu zitakuwa 500.