DP World Washusha Meli yenye Kontena 4,000 Dar Port. Meneja TPA asema ni matokeo ya uwekezaji, adai huo ni Mwanzo tu

DP World Washusha Meli yenye Kontena 4,000 Dar Port. Meneja TPA asema ni matokeo ya uwekezaji, adai huo ni Mwanzo tu

Mleta mada hacha kuleta sifa ili tusifie utuone chawa au wajinga

leta taarifa kamili hy meli inaitwaje? Inamilikiwa na nchi gani au kampuni gani?

imetoka wapi na inaenda wapi baada ya kutoka tz

tusije kufurahia kumbe imeleta silaha na vifaru kwaajiri ya M23 Alafu 2027 waje wavamie tz kwa kutumia hzo silaha
 
Gallus amesema bandari ya Dar es Salaam imefanya maboresho katika kina cha maji na ununuzi wa vitendea kazi vya kisasa.
Haya wameyafanya hao DP World unaowasifia kabla hata hawajaanza kazi, au kwa kazi hiyo moja ya kuleta hiyo meli?

Una haraka ya nini, tupe mrejesho wa utendaji kazi wao baada ya mwaka mmoja, siyo sasa.
Wananchi wetu wenyewe walikwisha onyesha ufanisi, hata kabla ya hao DPWorld kuja hapo.
 
Screenshot_20240623-031940.png
 
Iweje leo makasha 4000 mseme haijawahi kutokea? Acheni siasa za bei rahisi na ishatia nanga meli mwaka juzi ilikua na makontena 6000, acheni siasa za bei rahisi kwenye bandari mmevuruga tunawakalia kimya mnatuona mafara, mara gawio wakati tpa ishawahi kutoa gawio kubwa miaka mingi ilopita kuliko gawio lenu
 
Hivi we jamaa timamu kweli? au hata ni mtanzania mwenzetu.

Wewe na huyo ‘bi-tozo’ hata mlisoma makubaliano yaliyopitishwa na bunge na kuelewa ni nini wanatakiwa kufanya ili kuongeza ufanisi bandarini.

Kwenye mkataba ambao bunge liliotumia watu kadhaa kuutetea. Maswala ya phase 1 hao DP hawajaanza hata huo uwekezaji wenyewe kama sehemu maboresho ni vipi unaweza wapa credit ya mafanikio kama umesoma ule mkataba.
 
JPM alivyoweka hela hapo kuongeza kina na no of berth hakukusudia kuwapa Bandari DP world, kina na idadi ya Berth ilikuwa project kipindi cha JPM matokeo yake Bandari kapewa Muarabu.

Hii sio mara ya kwanza Bandari ya Dar es salaam kupokea Meli yenye container 4000.
Maersk Cubango ilishawahi kudock hapo na Container 4000, Waziri wa uchukuzi akiwa Mwakyembe.

Karne ya 21 Taifa lenye watu zaidi ya 60mil na kupata Uhuru 1961 linapiga kelele eti kupokea Meli ya container 4000, hahahaha, tembea uone huo ni uwezo wa Bandari ndogo kabisa Japan
 
Haya Sasa DP World wameanza kufanya Yao Dar Port Kwa kuleta meli kubwa zaidi ,urefu zaidi ya mita 300👇👇


Kampuni ya DP World iliyoingia ubia na Serikali kwa ajili ya uwekezaji kwenye bandari ya Dar es Salaam imeingiza meli ya kwanza yenye urefu wa mita 294.12 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji na maboresho yanayofanywa na kampuni hiyo katika kuendesha bandari hiyo.

Hayo yameelezwa na meneja mizigo mchanganyiko wa Mamlaka ya Bandari nchini TPA, Abed Galusi.

My Take
Kasi ya kuondoa mzigo ili.kuepusha Msongamano itaendana? 👇👇
Meli kubwa ya MSC ADU V iliyobeba makasha 4,000 imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam, ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa meli yenye mzigo mkubwa wa makontena kuwasili Tanzania.

MSC ADU V iliyotengenezwa mwaka 2005 ina urefu wa mita 294.12 unaokaribiana na viwanja vitatu vya mpira wa miguu imetia nanga leo Jumamosi Juni 22, 2024.

Akizungumza na wanahabari Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Abeid Gallus amesema ujio wa meli hiyo umetokana na maboresho yaliyofanyika katika bandari hiyo na uwekezaji wa Kampuni ya DP- World.

Gallus amesema bandari ya Dar es Salaam imefanya maboresho katika kina cha maji na ununuzi wa vitendea kazi vya kisasa.

Amesema mwanzo kulikuwapo na kina cha mita nane hadi 12.7 sasa hivi kipo 14.5 chenye uwezo wa kuingiza meli yenye urefu wa mita 305 na kina 13.5.

"Hii ni historia kwetu hapo mwanzoni tulikuwa tunaingiza meli zenye urefu wa mita 267, tumeongeza uwezo wa bandari yetu ya Dar es Salaam katika uingizaji wa meli.

"Uwezo wa utendaji kazi wa bandari ya Dar es Salaam utazidi kuimarika zaidi kwa sababu hivi sasa tuna mwekezaji mpya DP World aliyeanza kazi na mabadiliko yameonekana mfano ni meli hii kubwa,"amesema Gallus.

Gallus amefafanua kuwa katika usafirishaji ukipokea meli kubwa unaongeza kiwango cha mizigo unaokuja katika bandari husika sambamba na kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo.

Pia Soma
- Bandari ya Dar es salaam yazidi kupokea meli kubwa duniani


Kwa kifupi, or in summery, DP world wanapongezwa kwa kuongeza kina cha maji kwa 2 miters.
 
Back
Top Bottom