DPP, IGP, DG TISS, DG- PCCB nyie ndiyo mnapaswa kuchukua hatua dhidi ya ufisadi

Stuxnet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
13,417
Reaction score
23,310
Tumesikia namna Rais anavyolalamika kuhusu ufisadi sehemu mbalimbali. Hata PM Majaliwa naye tulimsikia last week akiwa ziaranya mkoa wa Mara.

Nauliza DPP, IGP, DG-TISS na DG TAKUKURU mnasubiri nini kuchukua hatua sitahiki dhidi ya watumishi ambao wametajwa kwenye hizo tuhuma?

 
kuwa mstahimilivu kua na subra....
 
Alivyokuwa anawaomba kwa maneno matamu ya rafudhi laini ya kizanzibari hakuna atakayeacha kuiba kwa ile lugha tamu anayotumia.
 
Huyu Rais tumepatikana safari hii. Halafu anataka tena 2025. Mungu tutetee
 
Kama raisi anachukua hatua gani kuonyesha mfano?

Mkubwa analalama bila kuchukiua hatua, je hizo taasisi zitafanya nini?
Akisema tu maana yake tayari ni maagizo !!
Inapaswa wanaohusika waanze upelelezi wakati huo huo !
Rais sio kazi yake kupeleleza kumfikisha mtuhumiwa Mahakamani na kisha kumfunga au kumwachia mtuhumiwa huru !

Mimi ninavyofahamu ni kwamba Rais akitamka kitu kama hicho maana yake ni kwamba ameshatoa go ahead ya wasaidizi wake waanze kazi. !
That’s it !🙏
 
Duh 🙄 !
 
GREED/URAFI ni nini?

Ni tamaa kubwa ya kichoyo/uchoyo, kwenye kitu flani kama ve utajili, nguvu(madaraka), chakula.

(Anajifikiria yeye na familia yake kwenye maslahi ya taifa badala ya maslahi ya taifa na wana taifa wote kwa ujumla.)

Mfano;
Watumishi wa umma nchini Tanzania wameendekeza sana greed/urafi mpaka umekua juu ya kanuni za kitumishi serikalini.

Kama hali ndio hivyo ilivyo sasa nani atawachunga hawa? Hawa si ndio huwa wanaambiwa wakalitizame na hili sasa itakuwaje?
 
Mkuu funguka zaidi tuujue huo mkoa, hii ndiyo namna tutaisadia nchi yetu kufichua uovu through JF
 
Ndicho ninachomaanisha, atoe kauli.
 
Tumesubiri sana mpaka kazi ya CAG inakuwa USELESSView attachment 2934292
kua mstahimilivu, kuwa mwenye subra....

mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali anawajibika kikatiba kubainisha matumizi ya serikali, na Rais pia anawajibika kwa wanainchi kwa mujibu wa sheria na katiba ya Tanzania..

kwa ufupi wanatekeleza wajibu wao kikamilifu...
 
CAG ndo 'meini stelingi' ndo kubwa la maadili maana anaingiaga laivu kukagua Hadi a/c za wahusika.
CAG kama haoni Hela nyiiingi zinaibwa vile asemavyo prezdaa maana yake ameshindwa kazi anapaswa kujiuzulu!!
"CAG AJIUZULU HARAKA SANA KAMA KWELI ANAMHESHIMU RAIS NA NCHI KIUJUMLA"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…