Elections 2015 Dr. John Pombe Magufuli anafaa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania

Elections 2015 Dr. John Pombe Magufuli anafaa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania

“Ni jamii iliyochoka na kuchakaa; ni jamii iliyooza na kuchoma pua kwa harufu ya uvundo wa rushwa na kujaza nzi wakubwa wa rangi ya Kijani, Ni jamii yenye ufisadi na ukandamizaji; ni jamii isiyojua mbele wala nyuma, ni jamii iliyokosa dira”. Bunge lipo kwa jina tu kwa sababu limewekwa kwapani na watawala; Madaraka ya Rais ni makubwa kwa kiwango cha kupora demokrasia: Utajiri wa nchi upo mikononi mwa kikundi kidogo cha “wateule” na watawala kilichowageuza wananchi wadunda kazi wasiofaidi jasho lao. Na pale maandamano ya wanawake, wanaume na vijana wenye njaa yanapopita karibu na Makazi ya Wenye nacho,Malodilofa husimama ghorofani, wakawatazama na kuuliza, “kulikoni?”. Na walipoambiwa kwamba yalikuwa ya “malofa” wenye njaa waliokosa mkate wa kila siku, wao walijibu: “Kama ni hivyo, kwa nini wasile nyasi na mihogo?”Vijana wanaangamia kwa kukosa maarifa mashuleni na wanaishia kubwia "unga" ambao ni biashara pendwa ya Malodilofa,vijana wasanii wenye vipaji mbalimbali wanageuka ombaomba na wakati wa Kampeni wanakuwa "lulu" kwa kutumika kujaza “nyomi” katika mikutano,wakulima wanazeeka kwa kazi ngumu mashambani na kukosa pembejeo za kisasa na mazao yao yanaishia kukopwa kwa bei ndogo ajabu,wavuvi wanachomewa nyavu zao walizonunua kwa wafanyabiashara wajanja wenye meno,wawindaji wa vitoweo wanaambiwa ni majangili huku tembo wakiuwawa kwa tama ya meno yao na twiga wakipandishwa ndege kwenda ulaya na Asia..Dah! wagonjwa wanakufa huku wamelala mzungu wanne sakafuni mahospitalini kwa kukosa madawa,wakina mama wanajifungulia vichochoroni kwa ubovu wa barabara, Na wanapoona malofa wanawapigia kelele kwa madai yao sahihi wanaamuru majeshi ya ndugu zao wanyonge wawapige mabomu ya machozi na kuwaua na kuwasababishia vilema vya maisha na kuwatesa waandishi wa habari zao za kilofa.Watawala wetu hivi leo wanatuhumiwa kumiliki mabilioni ya fedha wanayomiliki huku wakiyaita ni “vijisenti”, au “fedha ya mboga”, wakati kipato cha Watanzania walio wengi ni chini ya shilingi mia nane kwa siku. Wananchi wanapopiga kelele kugugumia bei kubwa ya kivuko wanaambiwa “Wapige mbizi” na pale ndege ya Rais na rada chakavu inaponunuliwa kwa pesa nyingi zenye asilimia kumi za wajanja wanaambiwa “Ni heri wale nyasi”…Pamoja na mikakati mikubwa na yakutumia fedha na rasilimali nyingi za walala hoi kwa ajili ya kuvuruga "Mabadiliko" kwa kuwanunua wanasiasa uchwara na kuwakashfu kuwa ni “wapumbavu,amlofa na mbumbumbu”. Wakati umefika,chama kilichokuwa na dhamana ya haya yote kipumzishwe,ili kijitafakari,kitakapokuja kwa mara nyingine (MUNGU akikijaalia) kije kikiwa kamili....Kwa wakati huu,nathubutu kusema,Naichagua UKAWA,...sio kwa sababu za uimara wa CDM,CUF,NLD,NCCR MAGEUZI ama Uimara wa UKAWA la hasha!!Ila ni kwa sababu ya udhaifu wa CCM na ahadi ilizoshindwa kuzitekeleza kwa miaka 54 mfululizo.“ALUTA Continua, Victoria Ascerta”.... “The Struggle Continues, Victory is Certain”; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!! ≠HapaNimakwenziTu!!
 
Aliyekutuma kuandika gazeti mwambie watanzania wameamua kuchagua Lowassa.

Ellyson, mchango wako ungekuwa na mshiko kama ungewaambia wana jamvini ubora wake Lowasa kama alivyofanya mtoa mada. Majibu mepesi kama hili lako ni la ushabiki tu hupati wa kukuunga mkono labda wenye mtizamo kama wako.

Lowasa mimi nilimkubali alipokuwa madarakani. Lowasa sikumpenda alipokiuka taratibu za Chama chake (kilichompa hadhi aliyo nayo sasa) za kutia nia ya kugombea hadi akafungiwa kwa miezi kadhaa na bado alipofunguliwa alikaidi tena. Lowasa simpendi tena sasa kwa sababu hatabiliki. Kuna maswali kadhaa yanayoulizwa na hayatolewi majibu na yeye, wapambe wake, waliomsitiri baada ya kukatwa CCM na wala wewe shabiki yake! Kwa nini hakuondoka mapema CCM? Kwa nini aligombea tena CCM, na wenzake waliokatwa, kama CCM ni chama kibovu hivyo kwa jinsi wanavyokikandia kwenye kampeni zao leo? Yapo maswali mengi kuhusu Lowasa na wenzake yasiyo na majibu. Ukimya ni dhahiri yanayosemwa ni kweli na kweli tupu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
“Ni jamii iliyochoka na kuchakaa; ni jamii iliyooza na kuchoma pua kwa harufu ya uvundo wa rushwa na kujaza nzi wakubwa wa rangi ya Kijani, Ni jamii yenye ufisadi na ukandamizaji; ni jamii isiyojua mbele wala nyuma, ni jamii iliyokosa dira”. Bunge lipo kwa jina tu kwa sababu limewekwa kwapani na watawala; Madaraka ya Rais ni makubwa kwa kiwango cha kupora demokrasia: Utajiri wa nchi upo mikononi mwa kikundi kidogo cha “wateule” na watawala kilichowageuza wananchi wadunda kazi wasiofaidi jasho lao. Na pale maandamano ya wanawake, wanaume na vijana wenye njaa yanapopita karibu na Makazi ya Wenye nacho,Malodilofa husimama ghorofani, wakawatazama na kuuliza, “kulikoni?”. Na walipoambiwa kwamba yalikuwa ya “malofa” wenye njaa waliokosa mkate wa kila siku, wao walijibu: “Kama ni hivyo, kwa nini wasile nyasi na mihogo?”Vijana wanaangamia kwa kukosa maarifa mashuleni na wanaishia kubwia "unga" ambao ni biashara pendwa ya Malodilofa,vijana wasanii wenye vipaji mbalimbali wanageuka ombaomba na wakati wa Kampeni wanakuwa "lulu" kwa kutumika kujaza “nyomi” katika mikutano,wakulima wanazeeka kwa kazi ngumu mashambani na kukosa pembejeo za kisasa na mazao yao yanaishia kukopwa kwa bei ndogo ajabu,wavuvi wanachomewa nyavu zao walizonunua kwa wafanyabiashara wajanja wenye meno,wawindaji wa vitoweo wanaambiwa ni majangili huku tembo wakiuwawa kwa tama ya meno yao na twiga wakipandishwa ndege kwenda ulaya na Asia..Dah! wagonjwa wanakufa huku wamelala mzungu wanne sakafuni mahospitalini kwa kukosa madawa,wakina mama wanajifungulia vichochoroni kwa ubovu wa barabara, Na wanapoona malofa wanawapigia kelele kwa madai yao sahihi wanaamuru majeshi ya ndugu zao wanyonge wawapige mabomu ya machozi na kuwaua na kuwasababishia vilema vya maisha na kuwatesa waandishi wa habari zao za kilofa.Watawala wetu hivi leo wanatuhumiwa kumiliki mabilioni ya fedha wanayomiliki huku wakiyaita ni “vijisenti”, au “fedha ya mboga”, wakati kipato cha Watanzania walio wengi ni chini ya shilingi mia nane kwa siku. Wananchi wanapopiga kelele kugugumia bei kubwa ya kivuko wanaambiwa “Wapige mbizi” na pale ndege ya Rais na rada chakavu inaponunuliwa kwa pesa nyingi zenye asilimia kumi za wajanja wanaambiwa “Ni heri wale nyasi”…Pamoja na mikakati mikubwa na yakutumia fedha na rasilimali nyingi za walala hoi kwa ajili ya kuvuruga "Mabadiliko" kwa kuwanunua wanasiasa uchwara na kuwakashfu kuwa ni “wapumbavu,amlofa na mbumbumbu”. Wakati umefika,chama kilichokuwa na dhamana ya haya yote kipumzishwe,ili kijitafakari,kitakapokuja kwa mara nyingine (MUNGU akikijaalia) kije kikiwa kamili....Kwa wakati huu,nathubutu kusema,Naichagua UKAWA,...sio kwa sababu za uimara wa CDM,CUF,NLD,NCCR MAGEUZI ama Uimara wa UKAWA la hasha!!Ila ni kwa sababu ya udhaifu wa CCM na ahadi ilizoshindwa kuzitekeleza kwa miaka 54 mfululizo.“ALUTA Continua, Victoria Ascerta”.... “The Struggle Continues, Victory is Certain”; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!! ≠HapaNimakwenziTu!!

Ufafanuzi wa kina kuhusu matatizo ya Taifa ketu👍✌. Naomba umalizie kwa kutufafanulia namna na jinsi hayo mabadiliko yataletwa na UKAWA chini ya mamluki kutoka CCM? Laiti wangetoka mapema pasipo kukatwa kungekuwa na hoja ya msingi? Lauti viongozi wa UKAWA wangeendelea na mikakati yao ya kuleta mabadiliko bila mamluki, mimi na wenye mtizamo kama wangu, bila shak ningewaunga mkono.
 
Mgombea mteule wa CCM, Mh Magufuli ameonyesha uwezo wa hali ya juu kiutendaji akiwa waziri zaidi ya Mzee Lowasa katika kipindi chake akiwa waziri. Mh Magufuli ameonesha uthubutu katika majukumu yake ktka wizara alizopita. Wote hawa wawili wamelitumikia taifa hili katika nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Uwaziri. Kati ya hawa wawili mmoja ambaye ni Magufuli kote alikopita ameweka record ya kipekee kiasi cha kuwafanya wananchi wengi kutamani apewe majukumu makubwa zaidi.

Mh Makufuli, amekua tunu hata wizara nyingine alizokwenda nakumfanya ang'are zaidi tofauti na mzee Lowasa katika wizara zote alizopita hakuna jipya alilolifanya zaidi ya kuacha malalamiko ya kero mbalimbali. Mh Magufuli ndiye aliyeokoa upotevu wa magari ya miradi ya serikali ambayo watumishi wengi walikua wakijimilikisha magari hayo na kuyatumia vibaya kwakua yalikua na namba za kiraia na baadae akaanzisha program kuweka namba mpya za magari yote ya serikali, Mh Makufuli akiwa wizara ya ujenzi watanzania tumempongeza sana na kwa juhudi,uboreshaji wa miundo mbinu kama barabara za kisasa, hakika huyu ndio kiongozi tunaemhitaji kwa sasa.

Mh Magufuli alipambana na wavuvi haramu waliokua wanatumia mabomu na nyavu haramu ijapokua wengine wachache walimchukia lakini wanaichi wengi tumempongeza kwa kazi nzuri hata akiwa wizara ya mifugo

Magufuli mara nyingi ameonekana akiwa sites mbalimbali za ujenzi akisimamia shughuli zinazofanyika iwe usiku au mchana akishirikiana na sisi wanainchi.Hakika huyu ndiye kiongozi tunaehitaji kwa sasa.

Jimboni kwake Mh Magufuli kupo vizuri barabara za lami,shule,ujenzi vituo bora vya afya na amekuwa karibu sana na wanainchi wake ukilinganisha na babu yetu Lowasa kule Monduli. Babu katika kipindi chake wizarani ametumia fulsa hiyo kujilimbikizia mali,kufanya biashara haramu na mataifa ya Ulaya, alijikita katika kutengeneza makundi yasiyokuwa na tija kwetu sisi wanainchi na zaidi kutuongezea umasikini.Kama wazalendo tujiulize huyu babu anaedai kuchukia umasikini,katengeneza ajira ngapi kwa vijana wa Monduli?

Zaidi ya maigizo anayofanya makanisani na misikitini,atueleze ni bodaboda wangapi kawapa mitaji zaidi ya kuwaburuza hususani wale wasiojitambua,vijana wengi wa kimasai kawapa fursa kiasi gani zaidi ya kukimbilia Dar es Salaam?. Kwa miaka zaidi ya 20 akiwa kiongozi hajaonesha nia ya dhati ya kumkomboa kijana,ataweza vipi kwa sasa na uzee unaomkabili ukiachilia maradhi anayokabiliana nayo. Alipokua waziri Mkuu Wafuasi wake wamekua wakimpongeza sana kwamba anamaamuzi magumu ambayo kama ni shule za kata zimechangiwa na wanainchi chini ya ilani ya chama cha CCM,yeye alikuwa na jukumu la kusimamia zoezi hilo tu.

Jimboni kwake kwenyewe hakuna maendeleo yeyote yale maisha ni magumu sana kuliko majimbo mengine.

Zaidi ya kujilimbikizia mali hakuna jipya alilofanya mzee Lowasa pamoja na kupendwa na bodaboda wachache wasiojitambua maana ukiwauliza kwanini wanampenda w atakujibu basi tumempenda tu" Ahahahaaaa mwengine watakujibu kuwa wanataka mabadiliko sasa hebu jiulize mabadiliko gani atakayokuletea wakati Jimboni kwake kwenyewe ni njaa tu!!!

huu uchafu na upumbavu wa aina hii wapelekee ukoo wako sio sisi wapenda mabadiliko.

lowassa ndiyo rais wako
 
Unaweza kuwa sawa kwamba Magufuli kamzidi Lowassa kiutendaji. Ila sina hakika na usahihi wa vigezo unavyotumia.

Twende mbele zaidi; kwa jinsi maelezo yanayotolewa kumhusu Magufuli na jinsi kampeni yake inavyoendeshwa, picha inayojitokeza ni kuwa Magufuli ndiye aliyekuwa mtendaji bora kuliko wote ndani ya serikali ya CCM (akiwemo Lowassa). Kampeni yake inatueleza ni yeye tu ndiye mwenye uwezo wa kukigeuza chama na serikali yake vitumikie wananchi wanyonge! Yaani kabla ya yeye kuwa rais tumekuwa na tuna hali mbaya. Yaani hata harakati za Katibu Mkuu kushambulia uozo serikalini na kujituma kupiga tofali, kupanda mpunga, kupiga cherehani, n.k. hazikufikisha ujumbe.

Hii aina ya maneno iko sawa kweli? Binafsi, wako watu ndani ya serikali ya CCM naoheshimu utendaji wao sana tu lakini kwa vile hawasikiki kwenye media ni kama vile hawapo. Wengine nimeshawapa ushauri wa ki-Nigeria: "you must talk big - o!" Lakini hawana hulka hiyo. Hivyo, leo tumebakia na mtendaji mashuhuri mmoja tu! Sawa?
 
Mgombea mteule wa CCM, Mh Magufuli ameonyesha uwezo wa hali ya juu kiutendaji akiwa waziri zaidi ya Mzee Lowasa katika kipindi chake akiwa waziri. Mh Magufuli ameonesha uthubutu katika majukumu yake ktka wizara alizopita. Wote hawa wawili wamelitumikia taifa hili katika nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Uwaziri. Kati ya hawa wawili mmoja ambaye ni Magufuli kote alikopita ameweka record ya kipekee kiasi cha kuwafanya wananchi wengi kutamani apewe majukumu makubwa zaidi.

Mh Makufuli, amekua tunu hata wizara nyingine alizokwenda nakumfanya ang'are zaidi tofauti na mzee Lowasa katika wizara zote alizopita hakuna jipya alilolifanya zaidi ya kuacha malalamiko ya kero mbalimbali. Mh Magufuli ndiye aliyeokoa upotevu wa magari ya miradi ya serikali ambayo watumishi wengi walikua wakijimilikisha magari hayo na kuyatumia vibaya kwakua yalikua na namba za kiraia na baadae akaanzisha program kuweka namba mpya za magari yote ya serikali, Mh Makufuli akiwa wizara ya ujenzi watanzania tumempongeza sana na kwa juhudi,uboreshaji wa miundo mbinu kama barabara za kisasa, hakika huyu ndio kiongozi tunaemhitaji kwa sasa.

Mh Magufuli alipambana na wavuvi haramu waliokua wanatumia mabomu na nyavu haramu ijapokua wengine wachache walimchukia lakini wanaichi wengi tumempongeza kwa kazi nzuri hata akiwa wizara ya mifugo

Magufuli mara nyingi ameonekana akiwa sites mbalimbali za ujenzi akisimamia shughuli zinazofanyika iwe usiku au mchana akishirikiana na sisi wanainchi.Hakika huyu ndiye kiongozi tunaehitaji kwa sasa.

Jimboni kwake Mh Magufuli kupo vizuri barabara za lami,shule,ujenzi vituo bora vya afya na amekuwa karibu sana na wanainchi wake ukilinganisha na babu yetu Lowasa kule Monduli. Babu katika kipindi chake wizarani ametumia fulsa hiyo kujilimbikizia mali,kufanya biashara haramu na mataifa ya Ulaya, alijikita katika kutengeneza makundi yasiyokuwa na tija kwetu sisi wanainchi na zaidi kutuongezea umasikini.Kama wazalendo tujiulize huyu babu anaedai kuchukia umasikini,katengeneza ajira ngapi kwa vijana wa Monduli?

Zaidi ya maigizo anayofanya makanisani na misikitini,atueleze ni bodaboda wangapi kawapa mitaji zaidi ya kuwaburuza hususani wale wasiojitambua,vijana wengi wa kimasai kawapa fursa kiasi gani zaidi ya kukimbilia Dar es Salaam?. Kwa miaka zaidi ya 20 akiwa kiongozi hajaonesha nia ya dhati ya kumkomboa kijana,ataweza vipi kwa sasa na uzee unaomkabili ukiachilia maradhi anayokabiliana nayo. Alipokua waziri Mkuu Wafuasi wake wamekua wakimpongeza sana kwamba anamaamuzi magumu ambayo kama ni shule za kata zimechangiwa na wanainchi chini ya ilani ya chama cha CCM,yeye alikuwa na jukumu la kusimamia zoezi hilo tu.

Jimboni kwake kwenyewe hakuna maendeleo yeyote yale maisha ni magumu sana kuliko majimbo mengine.

Zaidi ya kujilimbikizia mali hakuna jipya alilofanya mzee Lowasa pamoja na kupendwa na bodaboda wachache wasiojitambua maana ukiwauliza kwanini wanampenda w atakujibu basi tumempenda tu" Ahahahaaaa mwengine watakujibu kuwa wanataka mabadiliko sasa hebu jiulize mabadiliko gani atakayokuletea wakati Jimboni kwake kwenyewe ni njaa tu!!!

Ndugu UNAJISUMBUA BURE MAANA UNAJICHOSHA KWA KUAANDIKA GAZETI KUBWA ILIHALI #WATANZANIA TUSHAAMUA NA UNASAHAU KUWA "MTU MMOJA(MAGUFULI)" HAWEZI BADILISHA CHOCHOTE AKIWA KATIKA SERIKALI YA CCM MAANA MAGUFULI ANAGOMBEA URAIS NA SIO UWAZIRI NA UJUE KWAMBA RAIS NI TAASISI HIVYO LAZIMA AFANYE KAZI NA MAWAZIRI ILI NCHI ISONGE MBELE TATIZO KUBWA ZAIDI NI HAO MAWAZIRI WENU SASA AMBAO NDO "MIZIGO ILIYOSHINDIKANA(BY KATIBU MKUU WA CCM-KINANA)"...HIVYO TUMESHAAMUA KUWA HATUMUITAJI MAGUFULI TUNATAKA MTU ATAKAYEKUJA NA SERIKALI MPYA YA UKAWA TUONE UFANISI WAO NA SIO TENA HIYO SERIKALI YA CCM YENU AMBAYO NI ILEILE NA VIONGOZI WAKE MIZIGO WALEWALE...NA UTAMBUE TUNAKWENDA KUCHAGUA KIONGOZI NA SIO MENEJA...AMBAPO MTU PEKEE ANAYEFAA KWA UWONGOZI NI LOWASSA NA SIO HUYO MENEJA WENU MAGUFULI ANAYEONGOZWA NA MANAGEMENT NYUMA YAKE(KIKWETE NA MKAPA)...ALAFU ACHA UONGO UNAPOSEMA ETI MONDULI HAKUNA MAENDELEO WAKATI MONDULI TULIIONA KWENYE KIPINDI MAALUMU CHA ITV IKIWA NA MAJI MAJUMBANI KWA WANAMONDULI,LAMI NA SHULE KADHAA ZA SECONDARY...SASA EBU TUAMBIE CHATO KWA MAGUFULI WENU KUNA NINI???...EBU ONENI "MAWAZIRI WENU MIZIGO HAO" WANALALA TUU BUNGENI...ALAFU NDO WAKAFANYE KAZI NA MAGUFULI WALETE MAENDELEO YAPI HAYO???"...Teh!Teh! Teh!
 

Attachments

  • Wasira Usingizi.jpg
    Wasira Usingizi.jpg
    7.3 KB · Views: 227
  • wasira_akifuatilia.jpg
    wasira_akifuatilia.jpg
    8.8 KB · Views: 225
Lowassa mkasa, Magufuli kafulia.

Mmoja hajajibu tuhuma za Richmond, mwingine kauzia nyumba za serikali mpaka mchepuko ambao haukuwa ukufanya kazi serikalini.

Twaaafwaaa.
 
Think beyond don't undermine Tanzanians there isn't even a single day when the ruling system of CCM will faver its citizens. % Mti ni ule ule ambao matunda yake ni yale yale ya siku zote .Lakini ukae ukijua kuwa kwenye mti wa mkuyu huwezi vuna maembe. MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YAKO WAPI, BADALA YAKE NI KILA KITU KUPANDA BEI WAKATI KIPATO KIMESIMAMA.NITAFURAHI KUONA CCM IMEBAKI CHAMA CHA UPINZANI. MOLA UWE PAMOJA NASI DAIMA AMEENI CHANGESSSSSSSSssssssss
 
Acha ndoto ya mchana wajukuu zetu wasije piga viboko makaburi yetu kwasababu ya kufanya uchaguzi kwa uzoefu , kuwa na fikra zinazoishi lowasa ndo mkombozi wako .tangu 1961 waliopata uhuru ni viongozi wa ccm wao kila siku ni sherehe harafu raia shida tu ,acha kupotosha umma .andaa maisha yako na wanao kupitia ukawa =na uhuru wa pili tanzania 2015 kutoka kwa mkoloni ccm.
 
Hata kkuwa mwenyeki wenu hatoshi Kwa katiba ya ccm
Lazima November mfanye uchaguz wa mwenyekit baada ya magufur kupigwa dobo na lowassa 25October
Kwa sababu mtamuona hatoshi
 
Hakuweza ku-perform vizuri kukamata meli ya nje bila utafiti na kuingizia taifa hasara ya bilioni 2

kushindwa kulipa pesa za wakandarasi na kusababishia taifa deni la bilioni 900 sasa ame perform wapi

vizuri. Watu mnaongea bila kufanya utafiti na wala hamjui maana ya kufanya vizuri.aliachisha watu

kazi wasio na hatia halafu akashindwa kuwaomba msamaha
 
Magufuli hafai hata kwa dawa. Magufuli ana gombea urais kwa lengo la kuwa mlinzi wa mafisadi wa CCM na si kwa lengo la kuwa rais wa watanzania. Hafai hata kidogo.
 
Back
Top Bottom