Elections 2015 Dr. John Pombe Magufuli anafaa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania

Elections 2015 Dr. John Pombe Magufuli anafaa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania

Lowassa fisadi tu ranchi zote kauza na zingine kajibinafsisha, bila Masaburi alikuwa anauza UDA kwa bei chee, Mtwara na alilamba hela za misaada ya mafuriko kwenye kitengo cha maafa mwaka 1992. alikatisha mkataba wa dawasco kisa, alikataliwa 10% aliyoomba. Lowassa ni mwizi wala sio wa kumwonea haya hata kidogo.
 
Pole sana mkuu. Ila kwa sasa kila mtu ameshajua anamchagua nani. Wala hakuna mtu atakayebadilika tena. Hayo uliyoandika hayana maana tena, yaani yameshapitwa na wakati. Kwa muda uliobaki wa lowassa watabaki kwa lowassa hata lolote limfike.
Wewe acha ujinga usione aibu kusema au kukubali ukweli. Jenga hoja kamanda maana maelezo yako hayawezi hata mshawishi mtu akabadili mawazo.
Kila kukicha viongozi wa chadema wanajitoa wanarudi ccm hivi hayo huoni. Kila kikucha wanachama wanapungua wewe unasema eti tumeshaamua. Unaishi dunia gani? Labda wewe na famikia yako usiwasemee wengine. Tafakari msitujazie simu zetu kwa idea na kijinga.
Tafuta mbinu mbadala za kurudisha imani kwa wananchi
 
Lowasa ni hatari kwa mustakabali mwema wa taifa letu. Amekuwa akipita akifanya kampeni na kuwadanganya watanzania atawaondolea umaskini, atawapa magari, pikipiki kuwajengea nyumba, kuwaondolea kodi, kuwasomesha bure hadi chuo kikuu, kuwapa vijana ajira na kwamba nchi hii itakuwa ya asali na maziwa. Huyu ni hatari na wakuogopa kama ukimwi. Mwaka 2005 alifanya hayahaya alipokuwa ccm kwa kuaminisha umma kuwa maisha bora kila mtanzania ili JK aweze kupigiwa kura kwa asilimia 100. Baadae alipoppewa U PM ukamshinda kwa richmond. Ni hatari sana japo anayomengi aliyoyafanya yakiwemo ya kujikabidhi ranchi za ngombe za taifa, na jana imeelezwa uuzwaji wa UDA bado suala la kiwanja na ujenzi wa jengo umoja wa vijana ccm mnazimoja jinsi alivyotaka kulipiga juu kwa juu.

Ni hatari japo vijana wa tanzania hawataki kuelezwa jinsi mtu huyu alivyohatari kwa mustakabali mwema wa nchi yetu. Tuwaache naamini baada ya miaka 5 kama atapewa nchi watabaki wakilia.
 
Lowasa ni hatari kwa mustakabali mwema wa taifa letu. Amekuwa akipita akifanya kampeni na kuwadanganya watanzania atawaondolea umaskini, atawapa magari, pikipiki kuwajengea nyumba, kuwaondolea kodi, kuwasomesha bure hadi chuo kikuu, kuwapa vijana ajira na kwamba nchi hii itakuwa ya asali na maziwa. Huyu ni hatari na wakuogopa kama ukimwi. Mwaka 2005 alifanya hayahaya alipokuwa ccm kwa kuaminisha umma kuwa maisha bora kila mtanzania ili JK aweze kupigiwa kura kwa asilimia 100. Baadae alipoppewa U PM ukamshinda kwa richmond. Ni hatari sana japo anayomengi aliyoyafanya yakiwemo ya kujikabidhi ranchi za ngombe za taifa, na jana imeelezwa uuzwaji wa UDA bado suala la kiwanja na ujenzi wa jengo umoja wa vijana ccm mnazimoja jinsi alivyotaka kulipiga juu kwa juu.

Ni hatari japo vijana wa tanzania hawataki kuelezwa jinsi mtu huyu alivyohatari kwa mustakabali mwema wa nchi yetu. Tuwaache naamini baada ya miaka 5 kama atapewa nchi watabaki wakilia.




Tunamtaka huyo huyo fisadi hatari. CCM kwaheri
 
Toa sababu ya kumchagua Lowassa., mimi natoa za kumchagua Magufuli.

Sababu za kumchagua MAGUFULI.
1. Magufuli ni mchapa kazi nadhani wizara ya ujenzi unaiona jinsi ilivyo kuwa mbele"

A: Ni kweli barabara zote alizojenga ziko chini ya kiwango na nyingi zilibomoka hata kabla ya kuzinduliwa na ameliingiza taifa hasara ya takribani billioni 900 ambazo ni riba au faini kwa kushindwa kuwalipa wakandarasi kwa wakati. saafi sana


2. ni mtu asie na kundi lolote na huwa anasimama yeye kama yeye katika kila linalo muhusu"

B: Binadamu is a social being, katika maisha yetu ya kawaida ni lazima tuchanganyike na kushirikiana, usiri na ubinafsi wa Magufuli ni tabia ya watu wahalifu wasiopenda watu wengine waujue undani wao; wanajipa social distance kupunguza uwezekano wa mtu kuhoji hili na lile! utamuanzaje hamuzoeani?! magufuli huyoo!

3. kielimu huwezi fananisha Magufuli na Lowassa sababu Magufuli ni mkemia lakini lowassa ni msanii maana degree yake ni ya sanaa''

C: Uliwahi kusikia wapi shahada ya kuwa Rais; a president is a manager, managers use brains not misuli na jazba! managers are born and groomed, unlike Nyaparas; kutumia Nguvu nyingi kuliko akili, matokeo yake ni kuliiingiza taifa kwenye hasara kama vile meli ya samaki wa Magufuli!

4. Anaposimama jukwaani anaeleza kitu kwa mifano hai na kwa kusisitiza na huwezi fananisha sera zake na mgombea wa ukawa ambae hawezi hata kueleza back ground ya maisha yake ndani ya siasa.

D: Political novices kama magufuli ambaye hajawahi hata kuwa mwenyekiti wa tawi la CCM popote; hata shina! ndio wanahitaji kujieleza na kujipigia tarumbeta kila mara na kila mahali; sio a political GIANT kama EL ambaye track record yake inajieleza yenyewe loud and clear; amejijengea "political constituency" yake kwa miaka mingi sana; haitaji kujipigia tarumbeta; No wonder EL is a man "political novices" love to hate!

5. Chama chake Magufuli alichotoka bado hakijafarakana hivyo ni jambo jepesi hata kuunda baraza la serikali mpya na haiwezi fananishwa na ukawa ambapo wanaotegemewa wamekikimbia chama na kubakiza watu wasio waelewa maana hata nyumba kumi hawawezi kuongoza hivyo utajikuta baraza linajazwa na akina mnyika wasio na kauli wala nidhamu hata wawapo bungeni.Hii inatukumbusha kuwa tukiwapa utawala ukawa basi serikali itapambwa na mafisadi waliokimbia ccm.

E: Hujui unachoandika, ni wa kudharau tu wewe! kumbe hukusikia kauli hizi:

"CCM tunapambana na CCM maslahi upande mmoja na UKAWA kwa upande mwingine"! Samia Suluhu mgombea mwenza Urais 2015 na Muuaji Mwenza wa katiba ya wananchi BMK 2014.

"Najua kuna watu wananiunga mkono mchana kwenye kampeni zangu lakini usiku wanapigia kampeni UKAWA" John Magufuli; mgombea wa CCM urais 2015 akiwa mkoani Kagera

"Nimeachana na Siasa na sitarajii kupanda tena jukwaani kumuunga mkono John Magufuli". Makongoro Nyerere; Msasani kwa Mwalimu September 2015

Nawewe toa sababu ya kumchagua Lowassa.

Jawabu umeshalipata kama una akili!!
 
Wewe acha ujinga usione aibu kusema au kukubali ukweli. Jenga hoja kamanda maana maelezo yako hayawezi hata mshawishi mtu akabadili mawazo.
Kila kukicha viongozi wa chadema wanajitoa wanarudi ccm hivi hayo huoni. Kila kikucha wanachama wanapungua wewe unasema eti tumeshaamua. Unaishi dunia gani? Labda wewe na famikia yako usiwasemee wengine. Tafakari msitujazie simu zetu kwa idea na kijinga.
Tafuta mbinu mbadala za kurudisha imani kwa wananchi
We bakia na hoja kisha ongeza vioja juu yake, CCM TUSHAWACHOKAAAAAAAAAAAA.

CCM IKISHINDA NACHANA KADI YANGU YA KURA, NA KUWA NDO MWISHO WA KUJIHUSISHA NA KUSHABIKIA MAMBO YA POLITIK
 
mwisho wa siku naona watu mmefunguka macho.. hongereni sana....

Saana tu mkuu, tjmeng'amua tumegundua mamvi anazitamani mali za nchi yetu ili ziwe mikononi mwake na sie hatumpi hata kama asingekuwa mgonjwa ..ni bora tuishi hivi hivi na umaskini kuliko kuleta minyoo yake na makupe yake
 
Watanzania sisi ni malofa tena sana tu. Serikali iliyoshindwa kila kitu, imeshindwa kumanage rasilimali zetu,imeshindwa kumanage kodi zetu ili kuleta maendeleo..na kubwa zaidi imelea rushwa katika kiwango ambacho rushwa inaonekana ni sehemu ya kawaida ya maisha..Eti bado tunaipigania kwa nguvu zote iendelee kututawala. Kwa kweli hatusaidiki
 
Watanzania sisi ni malofa tena sana tu. Serikali iliyoshindwa kila kitu, imeshindwa kumanage rasilimali zetu,imeshindwa kumanage kodi zetu ili kuleta maendeleo..na kubwa zaidi imelea rushwa katika kiwango ambacho rushwa inaonekana ni sehemu ya kawaida ya maisha..Eti bado tunaipigania kwa nguvu zote iendelee kututawala. Kwa kweli hatusaidiki

Hao unaowashabikia leo kama hujui ndo walikuwa kila leo wanazunguka na kumharibia JK, JK aliwasoma na kwasababu alikuwa hana jinsi ya kuwafanya kwasababu ndo waliomweka madarakani akaamua kuwatafutia dawa ya Magufuri alafu wao watupwe mbali nje ya fensi, sasa leo wanawaambia eti serikali imeshindwa, kama si wao waliokuwa wanahujumu wasimame wakane ..wanasambaza unafiki sahivi, tumewashtukia na itakula kwao maxima, wasubiri waone ama sivyo wahame nchi
 
Pole sana mkuu. Ila kwa sasa kila mtu ameshajua anamchagua nani. Wala hakuna mtu atakayebadilika tena. Hayo uliyoandika hayana maana tena, yaani yameshapitwa na wakati. Kwa muda uliobaki wa lowassa watabaki kwa lowassa hata lolote limfike.

kwel mkut huyo hana hoja zenye maxhko kwanza maguful elim yake ni ya kuunga unga maana mwanzo alikua na diploma ya ualim kaunga unga mpaka kafikia hapo lakin lowaxa kapita moja kwa moja
 
kila kona ya ccm utasikia; "....tanzania yangu....tanzania ya magufuli.."

ndio kusema amejimilikisha laslimali zetu?
au ni gaidi?
maana hata mabango yake hayaoneshi kuichagua ccm. inamaana yy ni gaidi au anataka kujenga hostel magogoni(ikulu)?
huyu si wa kuamini....
 
Kwa maoni yangu mimi binafsi Magufuli hafai hata kidogo. Ni bora na Mama Samia kuliko huyu bwana. HAFAI.
 
Back
Top Bottom