.Mkuu Sifongo, tukubali tukatae, NECTA, wamekaza uzi, kama ni geme ya football, wamekaba mpaka kona!, kama ni mkanda, wamekaza na kubana mpaka tundu la mwisho!. The motive behind ni kuwabania "wakina fulani" ili kuwakomoa!, na kiukweli, wamekomoleka!. Nimeuliza jee mnaijui long term impact ya ukomoaji huu?!. Watu hamuoni mbali, ukifika muda wa kutokea ya kutokea ndipo mtawatafuta CIA, FBI na Scortland Yard, kuja kutafuta chanzo!. Jee wewe unawajua wengi waliozungusha ni kutoka kundi gani?!. Pasco.Mkuu Pasco nadhani hapa umeenda pembeni ya mstari, sidhani kama NECTA walifanya hicho ulichoandika, na unavyosema hivyo ni unawakosea hao unaodhani ni wajinga mpaka NECTA wawe na uhakika kuwa kwa mtihani huu wakina fulani watashinda na kina fulani watashindwa.
Kabla sijachangia mkuu pasco naomba jibu, nakiri sijui wanatoka kundi lipi. Tafadhali funguka.Mkuu Sifongo, tukubali tukatae, NECTA, wamekaza uzi, kama ni geme ya football, wamekaba mpaka kona!, kama ni mkanda, wamekaza na kubana mpaka tundu la mwisho!. The motive behind ni kuwabania "wakina fulani" ili kuwakomoa!, na kiukweli, wamekomoleka!. Nimeuliza jee mnaijui long term impact ya ukomoaji huu?!. Watu hamuoni mbali, ukifika muda wa kutokea ya kutokea ndipo mtawatafuta CIA, FBI na Scortland Yard, kuja kutafuta chanzo!. Jee wewe unawajua wengi waliozungusha ni kutoka kundi gani?!. Pasco.
Na masters yako bwana mushi..mawazo yako bado ni butu! kisaikolojia mwalimu toka moyoni anauwezo mkubwa wakumwezesha mwanafunzi yeyote..kitaalamu!!
We unamfahamu sana hadi uone si Pasco aliyeandika? si ndio huyu huyu huwa anaona kuwa ccm ni watawala wazuri? kawambwa ndio!
Wanabodi,
Kwa maoni yangu, kitendo cha NECTA kutunga mtihani ambao siyo ili kuwakomoa "watu fulani " kulikopelekea wanafunzi kufeli vibaya ili kujustify hao kina "fulani" ni wajinga!, na kuyapeleka makaratasi halisi ya mtihani kuuanika uthibitisho wa jinsi hao kina fulani walivyo jibu utumbo yakiwemo matusi ili kupata public sympathy kujustify tatizo sio NECTA, sio mitihani wall sio usahihishaji bail ni wanafunzi ndio wajinga na vibonde, hakipaswi kuachwa bila kupingwa!.
Wengi waliangalia hili kwa jicho la juu juu juu tuu bila kujiuliza wajinga halisi ni kina nani na long impact ya ukomoaji huu wa NECTA utalifikisha wapi taifa letu in a long run baada ya matokeo hayo kujenga matabaka ya wenye nacho na wasionacho!.
Kwa sio jua Wengi wa waliofaulu ni watoto wa wenye nacho ambao wana uwezo wa kuwalipia watoto wao shule bora, na wengi wa waliofeli ni watoto wa wa wasionacho hivyo Mama Ndalichako kupitia NECTA anawanyanganya hata hicho kidogo walichonacho, unategemea mini after a long time ?!.
I think it's time up for Mama, Dr. Joyce Ndalichako to go!, not withstanding madhaifu mengine yote wenye mfumo wetu wa elimu.
Pasco.
Wanabodi,
Kwa maoni yangu, kitendo cha NECTA kutunga mtihani ambao siyo ili kuwakomoa "watu fulani " kulikopelekea wanafunzi kufeli vibaya ili kujustify hao kina "fulani" ni wajinga!, na kuyapeleka makaratasi halisi ya mtihani kuuanika uthibitisho wa jinsi hao kina fulani walivyo jibu utumbo yakiwemo matusi ili kupata public sympathy kujustify tatizo sio NECTA, sio mitihani wall sio usahihishaji bail ni wanafunzi ndio wajinga na vibonde, hakipaswi kuachwa bila kupingwa!.
Wengi waliangalia hili kwa jicho la juu juu juu tuu bila kujiuliza wajinga halisi ni kina nani na long impact ya ukomoaji huu wa NECTA utalifikisha wapi taifa letu in a long run baada ya matokeo hayo kujenga matabaka ya wenye nacho na wasionacho!.
Kwa sio jua Wengi wa waliofaulu ni watoto wa wenye nacho ambao wana uwezo wa kuwalipia watoto wao shule bora, na wengi wa waliofeli ni watoto wa wa wasionacho hivyo Mama Ndalichako kupitia NECTA anawanyanganya hata hicho kidogo walichonacho, unategemea mini after a long time ?!.
I think it's time up for Mama, Dr. Joyce Ndalichako to go!, not withstanding madhaifu mengine yote wenye mfumo wetu wa elimu.
Pasco.
Mkuu Nguruvi3, hili nililijibu katika uzi wangu mwingine Opinion: Matokeo Mabaya ya Form IV, Jee?, Is It "Real?F" or there ...Kabla sijachangia mkuu pasco naomba jibu, nakiri sijui wanatoka kundi lipi. Tafadhali funguka
Wanabodi,
Naomba kuanza kwa kudeclare interest, mimi ni mhanga wa matokeo haya mabaya ya Form IV, nilikuwa na vijana wangu wawili, ambao walichaguliwa kujiunga na shule za kata, wife akashauri tuwahamishie shule za maana, kwa vile mimi ni mtu wa Nyerere type, nikamgomea, kwa hoja kuwa maadam watoto wa wananchi wa kawaida, wanasoma shule hizo za kata kwa sababu hawana jinsi, lets watoto wetu wasome shule hizo hizo za kawaida, "if they are bright, they are bright no matter wanasoma wapi!". Kiukweli kwa hili, tuligombana!.
Baada ya kufanya mitihani, wote wawili walituhakikishia Div 1 zisizo na mawaa!, wakasema kwa jinsi walivyoiona mitihani hiyo na jinsi walivyoifanya, "there is no way, watakosa first class!, matokeo yametoka, "No first class!", na kwa shule zao, first class ni nil!, yaani hakuna!.
Nazungumza haya kwa uchungu sana, kwa sababu nimeguswa!.
wanabodi,
kwa maoni yangu, kitendo cha necta kutunga mtihani ambao siyo ili kuwakomoa "watu fulani " kulikopelekea wanafunzi kufeli vibaya ili kujustify hao kina "fulani" ni wajinga!, na kuyapeleka makaratasi halisi ya mtihani kuuanika uthibitisho wa jinsi hao kina fulani walivyo jibu utumbo yakiwemo matusi ili kupata public sympathy kujustify tatizo sio necta, sio mitihani wall sio usahihishaji bail ni wanafunzi ndio wajinga na vibonde, hakipaswi kuachwa bila kupingwa!.
Wengi waliangalia hili kwa jicho la juu juu juu tuu bila kujiuliza wajinga halisi ni kina nani na long impact ya ukomoaji huu wa necta utalifikisha wapi taifa letu in a long run baada ya matokeo hayo kujenga matabaka ya wenye nacho na wasionacho!.
Kwa sio jua wengi wa waliofaulu ni watoto wa wenye nacho ambao wana uwezo wa kuwalipia watoto wao shule bora, na wengi wa waliofeli ni watoto wa wa wasionacho hivyo mama ndalichako kupitia necta anawanyanganya hata hicho kidogo walichonacho, unategemea mini after a long time ?!.
I think it's time up for mama, dr. Joyce ndalichako to go!, not withstanding madhaifu mengine yote wenye mfumo wetu wa elimu.
Pasco.
Unajua watz tumezoea kulalamika tu. Hivi mtoto akifaulu si unatamba mitaani? Je, unampelekea kitenge Ndalichako au kreti ya soda Dr Shukuru Kawamba? Si unatamba kuwa mtoto wangu kipanga? Akifeli unatafuta mchawi. Je, Ndalichako kasema wachore mazombi? Inauzi baadala ya kuudhi. Kwa mtindo huu wa kutaka watu wajiuzulu, basi na wazazi watoto wao waliofeli wajiuzulu.Thanks Bamukunda kwa appreciation.
WAKATI mjadala wa matokeo mabaya ya kidato cha nne ukiendelea kulitikisa taifa, kashfa mpya ya matokeo hayo imeibuliwa.
Kashfa hiyo mpya imeibuliwa na Mkurugenzi wa Shule ya Green Acres, Julian Bujugo, kwamba matokeo ya baadhi ya shule nchini ikiwamo yake yamechakachuliwa.
Akizungumza na gazeti hili jana, Bujugo alisema kuwa baadhi ya wanafunzi kwenye shule yake hawakufanya mitihani ya kidato cha nne, lakini matokeo yanaonesha wamefaulu kwa kupata alama za juu.
Alitaja mfano wa mwanafunzi, Humphrey Sanga, mwenye namba 01197/148, ambaye hakufanya mitihani hiyo lakini matokeo yanaonesha amefaulu kwa kupata alama nzuri.
Huyu mwanafunzi tulimsimamisha na hakufanya mitihani, lakini matokeo yake yanaonekana amepata hivi; Civics D, Historia D, Jiografia C, Kiswahili D, English C, Physics D, Chemistry C, Biology C, Basic Mathematics D, ambapo amepata daraja la tatu pointi 24, alisema Bujugo.
Alimtaja mwanafunzi mwingine, Martin Rushaigwa, namba 01197/0173, ambaye alifanya masomo ya Arts.
Alisema matokeo ya mwanafunzi huyo yanaonesha kuwa ameongezewa alama za masomo ya biashara ya Bookeeping na Commerce, ambayo hakuyafanya kabisa.
Alimtaja mwanafunzi mwingine aliyefanya mtihani huo lakini matokeo yake yanaonesha amewekewa absent na mwanafunzi mwingine, Mbazi Volta, hakufanya mitihani lakini amepewa alama za ufaulu.
Matokeo hayo yananipa wasiwasi kwamba yanaweza kuwa yamechakachuliwa, alisema Bujugo.
Mkurugenzi huyo anaiomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kurudia kusahihisha mitihani hiyo ili kuondoa ukungu ulioligubika taifa kwa sasa kuhusu matokeo ya kidato cha nne.
Naomba usahihishaji urudiwe, maana huu ni ubabaishaji mkubwa matokeo hayo yamewaathiri watoto kisaikolojia na sijui watakwenda wapi?, alihoji.
Alisisitiza kuwa usahihishaji urudiwe kwani katika shule hiyo wanafunzi wenye uwezo mkubwa tangu walipoanza kidato cha kwanza ndio waliofanya vibaya wakati waliokuwa wakifanya vibaya, wameibuka na alama za juu.
Mkurugenzi huyo alisema wazazi wa watoto hao wanatarajiwa kukutana mwishoni mwa wiki hii kujadiliana kuhusu matokeo hayo na hatua za kuchukua.
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Msemaji wa Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), John Nchimbi, alisema si kweli kuwa matokeo hayo yamechakachuliwa bali ni matokeo halisi ya shule hiyo.
Alisema iwapo mkurugenzi wa shule hiyo ana shaka na matokeo hayo, alitakiwa kufika katika ofisi za baraza hilo ili apatiwe taarifa sahihi kabla ya kutoa taarifa katika vyombo vya habari.
Mi nimeangalia hayo majina, naona yapo sawa na hata huyo mwanafunzi ambaye anasemekana hakufanya mitihani na akapewa alama napenda kusema kuwa alama alizopewa si zake na hata katika orodha yetu anaonekana kuwa hakufanya mitihani, alisema.
Katika hatua nyingine, Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa na wenzake, wamekuwa bubu kueleza endapo wako tayari kujiuzulu au la.
Tanzania Daima ilifika wizarani hapo jana kutaka kuonana na Waziri Kawambwa ili atoe msimamo wake, mwandishi alijibiwa kuwa waziri huyo alikuwa kikaoni na asingeweza kutoka.
Hata waziri alipopigiwa simu pamoja na kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno, hakupokea wala kujibu ujumbe huo.
Kwa upande wake, katibu mkuu wa wizara hiyo naye hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa alikuwa kikaoni.
Naye Naibu Waziri, Philipo Mulugo, alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi kueleza msimamo wake, simu yake iliita bila kupokewa na hata hakuwa tayari kujibu meseji ya ujumbe mfupi.
[TD="bgcolor: #FFFFFF"]
[/TD]
Matokeo kidato cha nne feki
Mkurugenzi Green Acres afichua siri nzito
na Betty Kangonga
Tanzania Daima
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"][/TD]
Baadhi ya Wahandishi wa Habari epukeni kufikiria kwa kutumia masaburi!