Tetesi: Dr. Ramadhani Dau apigwa marufuku uzinduzi wa Daraja la Kigamboni

Tetesi: Dr. Ramadhani Dau apigwa marufuku uzinduzi wa Daraja la Kigamboni

Status
Not open for further replies.

George Smiley

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2011
Posts
471
Reaction score
266
CgMY_7bXIAAh3vy.jpg

Kuna habari zimeenea kwenye mitandao ya kijamii toka juzi kuwa Waziri wa Kazi na ajira Jenista Mhagama na Katibu Mkuu wa hiyo wizara Eric Shitindi wametoa agizo kwa shirika la NSSF wasimwalike aliyekuwa DG wa shirika hilo Dr Ramadhani Dau kwenye sherehe za ufunguzi wa Daraja hilo wiki Ijayo.

Ikumbukwe kuwa Dr Ramadhani Dau amepigania hili daraja lijengwe kwa miaka yote aliyokuwepo kwenye hilo shirika mpaka aliopoondolewa wiki chache zilizopita.Sitaki kuingilia ugomvi na vita vinavyoendelea kati ya akina Magori, Eunice Chieume, Jenista Mgahama na Eric Shitindi lakini kama ni kweli bas sidhani kama Dr Dau alistahili kudhalilishwa kiasi cha kupigwa marufuku kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa hili Daraja. Pia sidhani kama Mheshimiwa Rais Magufuli atafurahia uamuzi huu wa uongozi mpya wa NSSF na Wizara.

====================

====================
Update;

Habari hii si Kweli kwani Dr Ramadhani Dau amehudhuria. Soma=>Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani kwake
 
Dr Dau si ameishaondoka hapo na nafasi yake kachukua mtu mwingine sasa aende kwenye uzinduzi kama nani? Ingawa kama atakuwa free siku hiyo anaweza kwenda kama raia wa kawaida au kwa nafasi aliyonayo sasa kama inahusiana na madaraja....

Ikumbukwe kuwa muda wote ambao Dr Dau alikuwa pale NSSF alikuwa analipwa mshahara na kila alichokifanya hakufanya kwa hisani bali kutimiza wajibu. Jina la Dr Dau litakumbukwa kwa mchango wake kufanikisha ujenzi wa daraja miaka mingi ijayo lakini sherehe za ufunguzi ni siku moja tu
 
CgMY_7bXIAAh3vy.jpg

Kuna habari zimeenea kwenye mitandao ya kijamii toka juzi kuwa Waziri wa Kazi na ajira Jenista Mhagama na Katibu Mkuu wa hiyo wizara Eric Shitindi wametoa agizo kwa shirika la NSSF wasimwalike aliyekuwa DG wa shirika hilo Dr Ramadhani Dau kwenye sherehe za ufunguzi wa Daraja hilo wiki Ijayo.

Ikumbukwe kuwa Dr Ramadhani Dau amepigania hili daraja lijengwe kwa miaka yote aliyokuwepo kwenye hilo shirika mpaka aliopoondolewa wiki chache zilizopita.Sitaki kuingilia ugomvi na vita vinavyoendelea kati ya akina Magori, Eunice Chieume, Jenista Mgahama na Eric Shitindi lakini kama ni kweli bas sidhani kama Dr Dau alistahili kudhalilishwa kiasi cha kupigwa marufuku kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa hili Daraja. Pia sidhani kama Mheshimiwa Rais Magufuli atafurahia uamuzi huu wa uongozi mpya wa NSSF na Wizara.



Acha majungu wewe!!! .....mtu akisoma btn the lines, umembwelambwela tu na ulichotaka kusema, hujakisema!!!!
 
~~>Watanzania ni Mabingwa wa kuzalisha Majungu na Fitna.....


~~~>Hili bandiko lako limekaa Kichonganishi.
 
Kuna chuki kali sana dhidi ya Dr Dau, hilo liko wazi.
Hata wasipomualika, ukizungumzia ujenzi wa daraja la Kigamboni, JK, JPM na Dr Dau majina yao yataandikwa kwenye kurasa za dhahabu
 
Wamuue, wamfunge, walibomoe Daraja bado historia yake Itabaki pale pale!
 
Duu, huyu mtoa maada amulikwe, anaweza kuwa shahidi mzuri sana. Who is Dau anyway?? A THIEF!! Mtu utatumiaje hela za watu at an inflated rates na kufanyia vikao vya bodi DUBAI, halafu unataka ukumbukwe,, KWA LIPI? UBADHIRIFU.?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom