TANZIA Dr. Sengondo Mvungi afariki Dunia

TANZIA Dr. Sengondo Mvungi afariki Dunia

R.I.P Dr. Mvungi na poleni sana wafiwa. Ila naomba niseme kwa sasa tuache usanii katika kuchezea roho za Watanzania wasomi ambao wapo kwa ajili ya ujenzi wa Taifa hili, tunaomba KOVA aache kuendelea na porojo na usanii kwa hili tunahitaji report iliyokamilifu na sio kuonyesha Kofia za CHADEMA kwenye TV huku taifa likiendelea kupoteza hazina muhimu. na kusipopatika taarifa yenye ufafanuzi wa kina juu ya hili tutaihusisha Serikali (CCM) na kifo hiki kutokana na kupinga Serikali Tatu
 
Kwa kuwa ni lazima tufe basi kila mtu ataondoka kwa namna yake, yaliyobaki tunamuachia mola kwa misingi ya wale wanaoamini kuwepo kwa muumba mbingu na inchi

Imani yangu inaniambia kuna vifo visivyopangwa na Mungu!
 
chadema ndio wanaotakiwa kujibu issue ya dr kupigwa mapanga sha,wao ndo watakuw wahusika wakuu wa hili tukio!huu ni mwendelezo wa ile muvi ya kuteka watu na kuwatesa kama walivyofnya ulimboka

Sina uhakika kama kweli wewe akiri zako ni timamu.....utaendelea kuwa mpuuzi ktk maisha yako yote yaliyobakia hapa duniani.....try to hv a reasoning ability even though common sense z not common to every one like u......mnayo serikali mbona hamjawakamata hao cdm?
 
Kitu ambacho siwezi kuafiki juu ya madhira yaliyomkumba Dr.Mvungi kuwa yote haya yalifanywa hili kukwapua simu na laptop au kopora fedha.Ni kitu ambacho kamwe sitokaa kuafiki,nadhani kuna motive kubwa zaidi ya vitu tajwa hapo juu,ukizingatia jukumu alilokabidhiwa lilikuwa ni muhimu na nyeti kwa mustakabali wa taifa letu.Kifupi waliotenda unyama huu walikusudia na inawezekana kuna mtu aliyesanifu na kufadhili unyama huu Kwa maslahi yake au taasisi aliyomo.RIP doctor.

Walikwapua na pisto pia.

Sasa sijui kwa nini hakuwatandika risasi na hiyo pisto. Au labda ilikuwa ni pisto maji....
 
Wote njia yetu ndio hiyohiyo, mbaya zaidi hayupo ajuae saa wala dakika na kuondoka kwake....

R.I.P. mh.
 
Kwa kweli vizuri havidum...! Mungu ni mwema/ lakini si kila kifo hupangwa na Mungu/hata shetani aweza kuua mwili ila hawezi kuua roho...tumshukuru Mungu kwa kila jambo.
 
Labda mimi nipingane na wewe kwa sababu nilishawahi kuwa muhanga wa yaliyomkuta mvungi ! Sema kwa kuwa wahanga wanakua ni watu wa kawaida polisi wanapiga kimya ,!! Nikiwa nyumbani kwangu kibamba nilivamimwa na majambazi wakatukata mapanga nyumba nzima, isingekuwa wazo la kuweka mikono kichwani basi ,probably nisingekuwa hapa kuandika posti hii hata hivyo nimepoteza vidole viwili mhimu mkono wa kulia .
Lakini kuna mazingira yanapromote sana aina hii ya ujambazi ,ikiwemo kujenga mbali na majirani au kujenga karibu na watu wanaomiliki maeneo makubwa bila kuyaendeleza,

dah maisha yana wafanya binadamu anakuwa mkati kiasi hichi, mkuu kwakweli inasikitisha sana, Pole sana wewe na Familia yako..very very sad indeed.
kinacho uma zaidi ni pale polisi wanapo chukulia poa na kule masihara kwa matukio ya kinyama na ya kikatili kama haya. Pole tena Mkuu
 
Umeondoka Taifa bado lakuhitaji Dk.. Elimu yako ilitusaidia sisi wengine tusio na elimu ya katiba..
 
Kitu ambacho siwezi kuafiki juu ya madhira yaliyomkumba Dr.Mvungi kuwa yote haya yalifanywa hili kukwapua simu na laptop au kopora fedha.Ni kitu ambacho kamwe sitokaa kuafiki,nadhani kuna motive kubwa zaidi ya vitu tajwa hapo juu,ukizingatia jukumu alilokabidhiwa lilikuwa ni muhimu na nyeti kwa mustakabali wa taifa letu.Kifupi waliotenda unyama huu walikusudia na inawezekana kuna mtu aliyesanifu na kufadhili unyama huu Kwa maslahi yake au taasisi aliyomo.RIP doctor.

Kwa nyongeza inawezekana kabisa hali yake haikuwa mbaya kivile ila kilichofanyika kilifanyika makusudi ili kufanikisha jukumu la kuondoa uhai wake. Kumbuka tukio la Marehemu Baba wa Taifa aliondoka akiwa mzima lakini alipogusa tu Hospitali hali yake ikawa mahututi pia Kifo cha Yasil Alafat na yeye hakina tofauti na kifo cha Baba wa Taifa.
 
Mungu awatie nguvu familia yake na kuwakumbusha kuwa hapa duniani hatuna mji udumuo. Safari ya Dr imekwisha. Sasa kilichobaki ni kwa yeye kusimama mbele ya Mungu siku ya kiama na kueleza jinsi alivyoishi alipokuwa hapa duniani. Tukumbuke hakuna cha sala wala nyimbo kutakachobadili. Kuingia mbinguni inataka maandalizi ukiwa hai na si vinginevyo. Bwana atusaidie kuzihesabu siku zetu.
 
kama laptop yake ilichukuliwa siku ya tukio basi, SIASA imechangia kuondoa Uhai wake.
 
Maneno yako yana ukweli ulitulia 100% mkuu, heri kule kuliko huku kwenye mateso mengi hasa majeraha ambayo yangemsababishia depression.
Tangulia baba wengi tupo nyuma yako twaja! Yamekwisha!!

Msiba Tume ya Katiba: Dk. Sengondo Mvungi afariki Duania Afrika ya Kusini

Kama ni wanangu, najua hawatakufa kwa kukosa chakula.
Wataishi, watakula na Watasoma...after all mke wangu yupo nao, atawatunza. Zaidi sana nina marafiki...hivi wanaweza kuninyanyapaa kisa nimehamia upande huu??, sidhani.

Nawaahidi kuwa Tanzania itapata Katiba nzuri tu, kuondoka kwangu kutalipia gharama ya katiba.

Jipeni moyo Watanzania.
Nawapenda sana.

Huku nilipo ni pazuri. Ni pazuri sana. Msinihofie mimi.
Angalieni zaidi mchakato wa Katiba.

Naamini siku isiyojulikana tutaunganishwa tena...sijui itakuwa katika umbo au hali gani, lakini ni ukweli dhahiri.

Ahsanteni.
 
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia. -

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid leo jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark. -

"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg-nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali. -

"Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumatano, Novemba 13, 2013)," ameongeza. -

Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013. -

Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.
R.I.P Sengondo Mvungi (PhD)
 
chadema ndio wanaotakiwa kujibu issue ya dr kupigwa mapanga sha,wao ndo watakuw wahusika wakuu wa hili tukio!huu ni mwendelezo wa ile muvi ya kuteka watu na kuwatesa kama walivyofnya ulimboka

unaandika na makamasi....kila kitu ni chadema, ata ukibakwa usiku utasema ni chadema. no sense!
 
Back
Top Bottom