TANZIA Dr. Sengondo Mvungi afariki Dunia

TANZIA Dr. Sengondo Mvungi afariki Dunia

Wakuu Dr Mvungi amefariki nchini afrika kusini alilokopelekwa kwa matibabu zaidi, baada ya kuvamiwa na majambazi.

Bwana ametoa bwana ametwaa

Source: ITV
 
Dah... So sad. Pole kwa familia, ndugu na jamaa
 
Pumzika kwa Amani Dr kwa waliousika hakuna cha kesi hapa ushaidi upo na wamekili kuhusika sheria itekelezwe tu iwe fundisho na kwa wengine wenye tabia kama hizo haramu katika jamii.
 
Wakuu Dr Mvungi amefariki nchini afrika kusini alilokopelekwa kwa matibabu zaidi, baada ya kuvamiwa na majambazi.

Bwana ametoa bwana ametwaa

Source: ITV

Na wewe unataka uonekane umepost
 
Ubongo wangu umesusa kukubali kama ule ni ujambazi.au sijui nimechanganyikiwa.tanzania kwa sasa inakuwa kama somalia.panapostahili doctor
 
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid leo jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.

"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg-nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali.

"Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumatano, Novemba 13, 2013)," ameongeza.

Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.

Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.

CHADEMA WATOA RAMBIRAMBI

Hivi watanzania hatuoni kuwa kwa sasa kumekuwa na matukio ya ujambazi usioeleweka wa kuwavamia, kuwaumiza, kuwateka na kuwatesa walio mstari wa mbele kupigania maslahi ya walio wengi, na kuwaua bila kuchukua chochote cha thamani na pale watesi wanapochukua kitu cha thamani kinaendana na maslahi ya walio wengi:

1. Dr. Ulimboka - wakabeba simu - haki ya madaktari
2. Kibanda - uandishi wa habari
3. Kubenea - kumwagiwa tindikali - uandishi wa habari
4. Prof. Mwakyusa/ Mwakusa - independent candidate
5. Dr. Mvungi - laptop yenye second draft ya katiba - mtaalamu wa katiba (na Agustino Ramadhani alisema ndio alikuwa tegemeo).

Jana kwenye magazeti Kova kaonesha mapanga yaliyotumika na kushindwa kuelezea laptop. kama dola haliwezi kutulinda na kusimamia haki zetu ni vyema kazi hiyo tukafanya wenyewe na mifano tayari tunayo kutoka kwenye Arab Spring.
 
RIP Dr Mvungi. Ila nawasiwasi na kifo chake. Kila mtu mwema anaetaka kuisaidia nchi hii huondolewa, leo hii tunaaminishwa ni majambazi je walichukua nini, laptop yake iko wapi. Yule aliesema mkenya ndio kampiga ulimboka antuambia eti mmoja wao amekiri kuhusika. Hili linchi linatia kinyaa.
 
RIP DK Mvungi. Wameua mwili lakini maarifa yako yataendelea kuwepo nasi. Naamini waliotekeleza mashambulizi dhidi yako wanajutia sasa na hata milele kwa kukupoteza. Upumzike kwa amani.
 
Back
Top Bottom