Mabingwa wa Soka Tanzania Bara na Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika wamepangwa kuvaana na timu ya Rivers United kutoka Nigeria katika hatua ya Robo fainali ya michuano hiyo.
Endapo Yanga itafuzu kwenda Nusu Fainali itakutana na mshindi wa mechi kati ya Pyramids ya Misri Vs Marumo Gallants ya Afrika Kusini