Dubai: Rais Samia ashuhudia utiaji saini wa Mikataba ya Uwekezaji ya thamani ya Trilioni 17

Dubai: Rais Samia ashuhudia utiaji saini wa Mikataba ya Uwekezaji ya thamani ya Trilioni 17

Stress ndizo zilizoifanya Urusi kuwa tishio Kwa usalama wa mabwanyenye Wanyonyaji wa nchi za magharibi.

Hujajua kinachoondelea katika ulimwengu wa kiroho.
Sisi wengine tunaipenda sana nchi yetu mana ndio maana tunawachukia sana waovu wanaotumia hila kuiba Mali za umma au kuwabeba waovu wenzao wasio na sifa. Unamhujumu na kumfunga na kuvuruga uchaguzi ili watu kama Mbowe , Heche, Wenje, Msigwa ,Lema na kumpiga Lisu risasi Kisha unatuletea bungeni wabunge wa hovyo wale Kodi yetu Kwa Kupiga makofi Kwa mambo ya hovyo halafu unategemea tushangilie TU Kwa sababu hatuna stress.
Vita inayokuja ni kati ya wema dhidi ya waovu.
Usijifariji kuwa inatumia CCM kukwapua Mali za umma siku zote. Utaaibika siku Moja kufumba na kufumbua utaumia sana kuliko wale uliowaumiza wakiwa na stress.
Kamuulize Sabaya atakuambia kuwa CCM ni Chama TU kama vyama vingine na sio Mungu.

Tulimuelewa Ndugai pamoja na madhaifu yake , nchi isiuzwe. Hatuwezi kuwaruhusu Wageni ngozi nyeupe kuja kuwekeza kwenye ardhi yetu kuja kulima mahindi na maharage na mpunga . Bora tuwaite ndugu zetu wa Kenya kuliko wa Asia na wazungu .
Subiri Iko siku utajua hujui.
Hakuna anayeweza kuiuza nchi huru kwa viwango vyote vya UN. Hizi ni inferiority complex zinasumbua akili ndogo tuliyonayo.

Nchi isipigwe mnada ikiwa chini ya JPM aliyekopa pesa nyingi kuliko marais wote wanne waliomtangulia kwa miaka sita ije iuzwe kwa pesa inayokopwa kwa mwaka mmoja tu wa SSH!.

Tupunguze kujiona wanyonge, ukijihisi mnyonge kila kukicha utakwenda kaburini na unyonge huo huo.
 
Fedha zikiingia nyingi ni jambo jema lakini itakua ni kosa kubwa sana kama atawaacha Mbuzi wale fedha za umma kulingana na kamba zao.
Binadamu hawezi kamwe kuridhika na kuwa mwadilifu bila ama kudhibitiwa au yeye Mwenyewe kujidhibiti kutokana na kumwogopa Mungu. Je, Mbuzi tulio nao wanamuogopa Mungu? Je, hawatafuti mapesa Kwa ajili ya zinaa ,ulevi, kujilimbikizia Mali, uhuni Mwingine , kujiandaa na rushwa za uchaguzi n.k. Sasa unawezaje kuwaachia Mbuzi wa aina hii kamba bila kuwadhibiti ikiwezekana kuwatia gerezani Kwa uhujumu uchumi?

Mama alikosea sana akipowapongeza wake wanaotumia vema urefu wa kamba zao kula. Hakupaswa azungumzie kauli Ile inayobariki vitendo vya ubadhirifu na rushwa ndani ya mifumo.
Alipaswa akemee TU vitendo vya rushwa na kuonyesha wazi kukerwa na kuvichukia kuliko kitu chochote. Hata kama ni ndugu wa kuzaliwa kama ni mla rushwa hafai kukalia kiti Cha umma.

January amesemwa sana kuwa sio msafi. Ridhiwani amezungumzwa . Hakuna haja ya kuwabeba kama kweli Wana historia mbaya.
Taifa la Tanzania litapata Heshima na baraka kama tutaonyesha Kwa vitendo kuchukia vitendo viovu kama vile rushwa ,Ushoga, matumizi mabaya ya madaraka,uonevu, uhalifu dhidi ya binadamu, kukwepa Kodi ,madawa ya kulevia, mauaji , ulevi wa kupindukia hasa Kwa viongozi,uzinzi wa kulaghai na ubakaji hasa Kwa viongozi wa umma n.k.

Hatuwezi kujenga Taifa bala kudhibiti Wala rushwa na wanaotumia vibaya Mali za umma na ofisi za umma.Hii nchi haijaumbwa na mtu anayekufa Bali imeumba na Mungu wa milele. Kauli za kula Kwa urefu wa kamba Kwa nchi zenye watu wema wanaohitambia haifai kabisa na inaweza kutumika kujinyonga kisiasa badala ya kuzunguka kula Mali za umma.

Kwa Nini wale Kwa urefu wa kamba wakati Wana mishahara na stahiki zao za kisheria .Hivi kula Kwa urefu wa kamba Kwa Waziri wa maliasili,madini, fedha n.k kinaweza kuwa sawa na Mawaziri kama wa habari na michezo.? Bila shaka mambo hayo ndiyo yanayosababishwa watu wanakwapua Kwa kushindana na kutafuta fursa za kuiba Mali za umma. Ardhi atakulaje kama sio kuuza viwanja viwili viwili au kupima viwanja Kwa viwango vidogo na kuficha idadi sahihi huku viwanja vikikosa maeneo ya wazi na ya michezo Kwa Wakazi. !!


Sijafurahishwa na kauli Ile. Watu wote kuanzia wanye dini za Kumtaja Mungu mwenye haki na mtawala wa vyote tunapaswa kumuomba Mungu atutendee haki Kwa kuwaondoa watawala waovu kwenye nchi aliyoiumba.
Mali za umma zikiliwa basi wanaoweza kusoma albadiri wasome waliozila wavimbe matumbo wapasuke kama mayai viza. Na wasikubalike katika jamii. Wapotee na kumbukumbu zao zisisimuliwe Kwa mema Bali laana na ubaya uwe juu ya vizazi vyao.
Tusikubali kuwaombea wezi na walafi eti Mungu awabariki ,; hapana !! Hawataacha na hawataona ubaya wa kutafuna Mali za umma kwenye nchi maskini kama hii.
Dunia Sasa ni kati ya wema dhidi ya ubaya.
Wakijaribu kula Mali za umma basi watakutana na mkono wa Mungu . Ndio kazi hasa ya albadiri na Sala nyingine za kuwalaani waovu

Wawekezaji waje kufanya biashara ila wasifanye nchi yetu kuwa ni Shamba lao la bibi. Tungewekeza baada ya kukopa hatungepata shida ya kuwakaribisha watu kuja kuwekeza kwenye kilimo wakati wapo Watu wanaiba fedha za umma na kwenda kujenga manyumba makuuuubwa ya kulala tuu watu Wawili mana hata watoto hawana. Tungebana majizi tukawatumia Wafungwa, JKT, vyama vya ushirika vya kisasa vinavyoundwa na wasomi sio wanasiasa waliovalishwa vikofia na kufanya vyama vya ushirika Kwa lengo la kampeni wakati wa uchaguzi. No. Tuunde vyama vywa ushirika Kwa Vijana wanaomaliza mafunzo ya JKT Kwa kuwapa mashamba waliyotaanzisha wakati wa mafunzo Kwa ajili ya kilimo ,mifugo n.k. sio kwenda kukimbia kwenye matope bila faida ya kiuchumi. Wafungwa wanawekwa magerezani mijini wanalala na kula na kufanya mambo ya kijinga na kufundishana ujinga zaidi na uhalifu zaidi badala ya kupelekwa kwenye maeneo yenye mashamba na ujenzi wajenge barabara za mitaa,walime ,wachimbe mitaro ,wafanye usafi kwenye bustani za Mahospitali na maofisi ya umma.

Afrika Bado hatuoni kuwa tunaweza kujiendeleza bila kuwategemea wakoloni wetu wanaodhani kuwa waliletwa Duniani kuja kututawala na kutunyonya. Hapana. Tunaweza kujitegemea Kwa kuwabana majizi na wahuni wa ndani na kuzalisha Kwa kiwango kikubwa. Hakuna haja ya Kununua juisi na asali Toka Dubai . Eti tunaagiza biscuit Toka China. Ni laana kabisa. Kuna wakati Unaona Bora Putin aamue Moja tu ili tumsubiri Masihi aje aunusuru ulimwengu uliojaa viongozi waovu wanaobebana kutokana na urefu wa kamba zao.

Mbowe sio gaidi ni mfungwa aliyefungwa ili Mbuzi wapate nafasi kubwa zaidi ya kula na hata kukata kamba wale bila kuzuiwa.
Kuandika nadharia ndefu ndefu huwa tunaweza sana. Tatizo ni pale tunapopewa nafasi ya kutekeleza yale tunayoyaongea majukwaani.
 
Jamani amkeni amkeni

Huko Dubai mambo ni moto balaa! Leo hii Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba zaidi ya 30 ya uwekezaji Tanzania yenye thamani ya fedha za Tanzania zaidi ya Trilioni 17 na itakayotoa ajira kwa Watanzania za moja kwa moja zaidi ya laki 2.

Mikataba iyo inahusu maeneo ya Kilimo, Madini, Biashara, Utalii na Uzalishaji wa Viwanda

Hongera sana Mhe. Rais kwa jitihada hizi. Mungu akubariki kwa kweli. Haya ndo maendeleo tunayotaka Watanzania

Kutoka Nyasa, ziwani
Lord denning
Mkuu Lord denning hawajakuita chawa mpaka dakika hii?. Watu wana chuki za kijinga sana Tanzania ya leo.
 
Mikataba ya gesi ilikuwa hivyo hivyo kwani tumesahau tulipoambiwa kwamba kutumia miss na kuni itakuwa historia Tu na Mtwara kuwa kama Dubai?

Mimi nitafurahi pale nitakapoona uwekezaji umeenda sambamba na kubadilisha uchumi wa nchi siyo uchumi wa Kati wa makaratasi.

ASANTE WENGI WALIKUMBILIA KUWEKEZA MTWARA WANEPATA HASARA KUBWA SANA KWA KUISIKILIZA SERIKALI
 
Hii mikataba ilishawahi kupitiwa na wataalamu wetu hapa nchini?
Au imepitiwa juu kwa juu kama ile ya akina Sultani Mang'ung'o?
Iwekwe wazi ndio tuweze kutoa maoni bila hivyo hapana!
 
Hayo ni makaratasi tu sio hard cash.

Mziki upo kubadili hayo makaratasi kuwa hard cash na kwa faida iliyokusudiwa.
 
Back
Top Bottom