Hukuna lolote, ni kutojiamini kwa wasanii tu, Sugu alimgusa kidogo tu akaishia kuomba suluhu kupitia Waziri Nchimbi na akina Tundu Lissu, kama alikuwa anaweza lile battle kilichomfanya akimbilie kuomba poo ni nini? Jide tu hapo wamemshindwa!!
Ukiangalia vizur utagundua ni kutojiamini tu kwa Wasanii wetu, kwa mfano huyo Ruby wanaosema kuwa walimbeba, mim nilisikia wimbo wake kupitia radio nyingine tofauti kabisa na nikamkubali, hali kadhalika hawa akina Raymond, Billnas na wengine waliochipukia majuzi, wote nilisikia nyimbo zao kupitia media nyingine na nikawaelewa.
Kitu ambacho wasanii wetu hawajaelewa ni kuwa, Wimbo mzuri ndio utambeba, promo ina nafasi yake ila kama unafanya nyimbo nzuri utatoboa bila hata hao watu!! Kuna nyimbo kibao kutoka mataifa mbali mbali zinapendwa sana hapa Tz, je hao mawingu ndio wanawabeba hao wasanii wa Kimataifa? Jibu ni hapana, Ubora wa Nyimbo zao ndio zinawabeba!! So kuwekeza tu kwny mziki wako ndio utakubeba na sio media fulani!! Kujitambua ni hazina kubwa sana!!