Duh! Rais Samia amkataa mama mnyonge aliyetaka kumlilia kama Magufuli. Nenda kakae…

Duh! Rais Samia amkataa mama mnyonge aliyetaka kumlilia kama Magufuli. Nenda kakae…

Majukumu ya rais sio hayo yakuokoteza shida za wananchi mmoja mmoja.ndo maana nchi ina vyombo na wizara mbali mbali.kama mtu anashida na haitatuliwi ngazi ya chini xiko taratibu zakupeleka malalamiko yake ngazi ya juu.acheni kujitoa ufahamu kwa mambo madogo kama hayo kisa kuna limbukeni mmoja alikua anasikiliza matatizo ya watu kienyeji bila kuhimarisha taasisi zakutatua kero za wananchi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app


Raisi ni Baba/ Mama/Mfariji Mkuu wa Taifa ndio Kimbilio la kila mtu kama baba na Mama nyumbani

Huwezi kumwambia mtoto wako husiniambie mambo ya home work nimeweka house girls kwa ajili yenu ongea na dada 😥😥😥😥😥
 
Maigizo yote haya yaliletwa na Magufuli kwa kutaka cheap popularity na kujifanya eti anapenda Saana wanyonge.

Upumbavu mtupu

Marehemu Kwanini unawatesa walio Hai. Kama mtu alikuwa dikteta Kwanini hatafute cheap popularity?
 

😂 mama kaamua Kama mbwai iwe mbwai
Wanyonge wamezoea papaa alikuwa anatembea na manoti kibao anamwaga tu kwa wanyonge 😃😃😃😃 mama hataki mambo ya kishamba kapambane huko
 
Kanuni ya mawasiliano HANA au HAJUI.
Ukitaka kuzungumza na mtoto shuka katika kimo chake.
She is standing tall all over the time

Madaraka yanalewesha kuliko hata Spirytus Rektyfikowany (96% Alcohol)![emoji28]
 


==========

Mama mmoja amesikika akimuomba Msheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassani kuwa anaomba atendewe haki, mama huyo amerudia mara 3 kusema anaomba atendewe haki, Lakini Rais Samia alimjibu kuwa hawa hapa wapo umeshatuandikia litanifikia nenda kakae. Rais Samia Aliendelea kusema kuwa ona yanajitokeza hata hapa. Hivyo kusisitiza mahakama zitende haki kwa kuangalia utu wa mtu.

Hapa tulipigwa
 
Raisi ni Baba/ Mama/Mfariji Mkuu wa Taifa ndio Kimbilio la kila mtu kama baba na Mama nyumbani

Huwezi kumwambia mtoto wako husiniambie mambo ya home work nimeweka house girls kwa ajili yenu ongea na dada [emoji26][emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]

Rais hajui kuwa hata kuomba kuonana na mkuu wa wilaya tu ni kama kuomba kuonana na Mungu!
 
Kuna kipindi flani kama nilimsikia anasema akiwa kwenye ziara zake ataki kuona mabango yamalalamiko, aliagiza wateule wake wafanye kazi.

Sasa sijui alikuwa na maana kwamba akiona bango atawawajibisha wahusika wanao zembea kufanya kazi.
Ama alikuwa na maana hatakitu kuona mabango kwa sababu zingine.
 
Haifai Rais kuchukua nafasi ya Hakimu au Jaji kugawa haki, huna uhakika suala la huyo bibi yako lilikwisha kwa sababu haki ilikuwa upande wake au watu walitimiza tu matakwa ya Rais bila kuangalia haki iko wapi.

Huo Mfumo wa Kangaroo courts ni dalili ya mhimili dhaifu sana wa mahakama.
Wewe acha hizo Rais hatoi uamuzi, ujasoma mambo ya uongozi nini? Kinachofanyika ni Rais kusaidia huyo mama kusikilizwa kwa haki. Yaani humu kuna mtu anaweza andika jambo mpaka unajiuliza hivi watu wanaufahamu kweli? Au wamekalia ushabiki? Asilimia kubwa ya Jamiiforums watu wamekaa kichawa. Hawachanganui mambo kwa hoja na kuangalia dunia inavyokwenda.

Pengine wengi hawajui mifumo ya utendaji kazi katika kiserikali. Na pia kama wanajua wapo kiushabiki au kichawa zaidi. Kwa taarifa yako, wananchi wengi wanaonewa. Na wengi wanapoteza haki zao. Nimeshuhudia haya. Na siongoi tu najua.

Mfano mfupi, kuna mzee mmoja ni kipofu au asiyeona. Alizurumiwa nyumba yake iliyokuwa eneo zuri sana na tajiri mmoja mkubwa. Huyu mzee alikuwa anaumwa wakajua atakufa. Hakuwa na watoto. Majirani ndo walimsaidia. Hivyo akasainishwa mkataba kwa kuweka dole gumba wakati akiwa mahututi.

Kaja kuzinduka baada ya miezi, anaambia alilidhia nyumba kuuzwa. na bei ya nyumba ati imeuzwa kwa millioni 5 tu. Akashangaa! Kesi kwenda mbele yule mzee alishindwa huyu tajiri alikuwa anaonga fedha nyingi. Eneo ni nzuri la beach. Hakimu alikuwa anakula rushwa saana. Akidai hawezi ingiliwa. Suala lile lilikatiwa rufaa.

Huyu tajiri alozurumu akapiga simu akitaka kutoa milioni mia moja hili anaefuatilia hili suala na kumsaidia huyu mzee aache.
Bahati mbaya huyu mbwana alikwenda masomoni.
Kilichotokea huko nyuma mzee alibambikwa kesi, akaenda jela, huyu jamaa akachukua nyumba akavunja na kujenga mjumba wa kifahari. Na maeneo hayo kuna Port ndogo. kesi ikamalizwa ki namna.

Ni mengi tu. Katika moja ya utafiti wangu wakati nafanya shahada ya uzamili nilipendekeza serikali kuanzisha chombo maalum cha kusikiliza malalamiko. Kenya walianzisha nadhani miaka michache ilopita.
Tanzania hii watu wananyang'anywa maeneo, wanateswa, wanaingizwa ktk chumba inachomwa pilipili, wanateswa, maeneo yao na mifugo vinachukuliwa. Na huu ni mtandao mkubwa. Kuna viongozi wakubwa wanahusika. Basi tu mtu kama huko mjini unadhani mambo ni mazuri.
 
Hii kwa Zanzibar itawezekana ila sio bara, Zanzibar ni kama wilaya moja huku bara

Watu milioni 60 wakutumie kero zao kupitia app?[emoji23][emoji23]

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app


Zanzibar ni Wilaya?! Hata hao watu milioni 60 bara sio wote wenye uwezo na ujuzi wa kutumia app

Tatizo sio idadi ya watu au kuusu hiyo app nimeleta kuwaonesha wale waliokua wanapotosha kua Raisi sio kazi yake kusikiliza Kero za kila mtu hizo Mwinyi anasikiliza kwa kutumia app ni matatizo ya wanyama au majini au dr. Hussein ni katibu kata sio Raisi😢😢😢😢😢
 
Zanzibar ni Wilaya?! Hata hao watu milioni 60 bara sio wote wenye uwezo na ujuzi wa kutumia app

Tatizo sio idadi ya watu au kuusu hiyo app nimeleta kuwaonesha wale waliokua wanapotosha kua Raisi sio kazi yake kusikiliza Kero za kila mtu hizo Mwinyi anasikiliza kwa kutumia app ni matatizo ya wanyama au majini au dr. Hussein ni katibu kata sio Raisi[emoji22][emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]
Mwinyi sio model ya kufuatwa na marais wote mkuu

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Nimependa Sana hii, haya maigizo ya kijinga ifike muda tuyapuuze yanaleta unafiki na utwana kwa viongozi wetu
Endeleeeni kushabikia upuuz wenu huo..siku yakikukutaa ndo utataman na ww kwenda kwa mwenye mamlaka ya ju..ushezi wa ushabik unamaliza wengi..kama nyie wapuuzi puuzi wa humu jf
 
Hii kwa Zanzibar itawezekana ila sio bara, Zanzibar ni kama wilaya moja huku bara

Watu milioni 60 wakutumie kero zao kupitia app?[emoji23][emoji23]

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app

Hapa umeongea kwa kutia chumvi, ndugu yangu. Kwani kila mtu ana kero binafsi anayohitaji kuifikisha kwa Rais?

Kitu muhimu ni yeye Rais kupeleka ujumbe kwamba she’s accessible to the ordinary people. Trust me, hakuna mteule ambaye yuko tayari kuonekana kwa Rais kwamba ameshindwa kutatua kero ambayo iko ndani ya uwezo wake. Kitendo chake cha kuonesha kwamba she isn’t accessible to the ordinary people kinapeleka wrong message kwa wateule wa Rais, ambao siku zote hawana utamaduni wa kuwajibika kwa wananchi!
 
Back
Top Bottom