Dullah Planet(EARADIO/EATV) weka wazi WCB wamekukosea nini?

Dullah sio wa kulaumiwa sana, inawezekana ni maswala ya mikataba, kati ya WCB na EATV/EARADIO.

Tutaziangalia nyimbo zao kwa kuzi-download Wasafi.com

Nadhani hili ndilo lengo kubwa la WCB.
 
Hicho ni chombo cha biashara na sio cha msaada, unakosea sana kumu attack mtu, dullah ni presenter tu sio mkuu wa vipindi, hana mamlaka hayo, usifikiri kwamba watangazaji wanaamua tu kupiga nyimbo au kutopiga, kila nyimbo inayoenda hewani na imeenda mara ngapi per day inakuwa counted, media zote kubwa huwa zina watu wanaondaa playlist, Dulah anaongea kile tu alichoambiwa aongee, sijui kama unafahami jinsi media zinavofanya kazi.

Anyway, Clouds wana karibia miaka mitano tangu waache kupiga nyimbo za lady jaydee, ni uhamuzi wao lakini media zingine zinapiga, mbona hulalamiki redio imani hawapigi nyimbo ya msanii yoyote? Hayo ni maamuzi ya media husika na sio lazima......kumbuka pia maneno ya diamond aliyoyasema kuhusu eatv na earedio, aliongea shit kwa vile ye ni msanii mkubwa na akajiona ni mkubwa kuliko hiyo media, so ulitaka eatv wafanyeje? Wakampigie magoti au wakamuombe awape nyimbo zake wapige?
 
Umekiri kuwa Vituo ni vingi vinavyoweza cheza nyimbo za hao WCB.


Sasa povu la nini kwa wao kutocheza nyimbo hizo?


Wanayo haki ya kuamua wapige au wasipige nyimbo hizo endapo wanasababu zao za msingi kwao.
 
ujumbe umefika. mzee mengi ataingilia kati hili
 
Lakini ilikuwa si hoja kumchukia msanii wakati tunzo ilikuwa si lazima.
Mwisho wa kunukuu.
Kwani kupiga nyimbo ya msanii n lazima hapo ea radio???

2. Wcb bado Zita hit kwani n ukweli ulio wazi EA RADIO kwa sasa haina nguvu kuzidi clouds na E fm radio pamoja ina frequency mbili.
Sasa Kama haina nguvu kwa nini unalazimisha wapige hizo nyimbo??


Nadhani mleta mada ulivyoleta mada yako ulikuja na upande wako direct kwa hao wcb. Umetumia hisia Sana pasipo akili kuwasilisha mada yako hii japo una lengo Zuri la aman kwa upande wa music.
 
Umemaliza mkuu
 

Weka huo uchochezi

Kwanza wcb ndio nini??
 
Nimefanya utafiti na nimegundua kuwa Dullaha ndio chanzo kikuu kwa nyimbo za WCB kutopigwa kwenye vituo vyao..
 
Mwambie diamond aachane name mambo ya kisiasa, wakati viombo vya habari vilimsusa bashite,wakati bashite anawanyanyasa wanamziki yeye diamond kwanza ndio alikuwa akimpa Promo bashite.
 
Mwambie diamond aachane name mambo ya kisiasa, wakati viombo vya habari vilimsusa bashite,wakati bashite anawanyanyasa wanamziki yeye diamond kwanza ndio alikuwa akimpa Promo bashite.
unakula na anaekula na wewe..kwani hujui bashite ndo mlezi wa wcb au umejitoa ufahamu
 
Radio/TV yao kodi wanalipa wao, mishahara wanalipa wao, nyimbo za kucheza wanachagua wao msiwapangie cha kufanya. Waambieni uhuru fm, radio tanzania, tbc wacheze nyimbo za wcb
 
Hatupangiwi kazi,Kodi yulipe sisi,kuajiri tuajiri sisi,Alafu utupangie nyimbo upendazo? Rudi kwenu matombo kachague nyimbo kwenye ile redio jamii!

Eti za Diamond na WCB!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…