Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Mkandara nitakuja kukujibu baada.. Ila niweke mambo sawa..

Nasisitiza Mimi na nguvuri3 hatufahamiani kabisa ni kama wewe na mimi...yaani tunakutana hapa JF. Ingawaje nigefurahi kama ningewafahamu nje wa JF..

Mimi sio kiongozi wa Chama, Ingawaje ninapenda mageuzi na sera za Chadema zinanivutia hasa swala la Elimu.

Swala la Urais ndo na wewe ushangae.. Lakini zaidi ya hapo siwezi kwenda deep. Nitaishia hapo kwenye urais...

.
Hapana sijasema mnafahamiana ila mnaonyesha kuyajua yya Chadema kama watu wa ndani maana mnasema kwa uhakika exactly what where and how it started, ilihali mtu wa nje hawezi kuyajua haya isipokuwa kwa tulosimuliwa na kuunganisha dots. Mimi kila nachoandika ni kuwasoma, kuwasikia viongozi wa Chadema lakini siwezi kusema kilichotokea ndani ya Chadema mawati sikuwepo..
 
Hapana sijasema mnafahamiana ila mnaonyesha kuyajua yya Chadema kama watu wa ndani maana mnasema kwa uhakika exactly what started, ilihali mtu wa nje hawezi kuyajua haya isipkkuwa tulisomuliwa. Mimi kila nachoandika ni kuwasoma, kuwasikia viongozi wa Chadema lakini siwezi kusema kilichotokea ndani ya Chadema mawati sikuwepo..

Hebu nipe mfano nilichoongea kama wanandani..Sio kwa nia mbaya inawezekani ulinielewa vibaya au nilishindwa kujieleza.
Swala la urais hilo ni 100% ndicho kilichotoka mdomoni mwa Zitto..
 
Alinda , siku zote hoja zinapomuelemea mkuu Mkandara, kunanjia tatu anazotumia.

Moja, atachomeka hisia za udini, pili atahamisha mada (ref jitegemee) na mwisho atafanya character assassination


Bandiko lake anasema sisi wengne ni Chadema tunajua kwa undani na tunatumika.

Kwawasomaji wa duru wataelewa udhaifu wa hoja hii kwani hoja za duru zipo wazi na zinalikana.

Hakuna aliyeachwa au kusamehewa. Kinachojadiliwa ni hoja kwa mustakabali wa nchi na taifa

Pengine angesema sisi ni ACTtungemwelewa maana tumeeleza ‘movie' nzima ya Zitto ikiwa studio, sasa hivi watu wapo theatre wanaangalia na kubaini script yetu ilikuwa sahihi 100.


Tumechambua kuanzia siasa za ndani, nje na popote.
Ningemuomba apitie nyuzi za duru aone tunavyosimama katika issue na si watu au gengela wahuni


Kama ulivyosema, hatufahamiani wengi tu,ingawa pia ningefurahi kama tungekutana.

Mkandara atakumbuka mabandiko tunayokubaliana ninasemahivyo, tunayopishana ninasimama na anasimama kwa
anachokiamini.


Mawazo mbadala tunayapenda na kuyakaribisha sana.

Tusichokipenda ni spinning, maana akina Kitila na Zitto wanapofanya hivyo,halafu tukubali JF itufanyie hivyo, hatujitendei haki.

Tutaita spade kama spadena si kijiko kikubwa.


Nawaomba nirudi kwenye mada hasa kupitia hoja zawachangiaji, na kisha kuzama katika siasa mpya za ACT za kuligawa taifa.
Siasa za ukanda ambazo walizipiga vita na sasa ndio vinara
Tutaeleza kwa kina kwanini Zitto ameamua kwenda kwenyeUkanda na hoja dhaifu
Tuteleza kwa kuangalia anachopotosha na ukweli wa mambo
Inaendelea…

JokaKuu
 
Last edited by a moderator:
Mwanzo tulihubiriwa kuwa Chadema ni chama cha Wachaga ni chama wa wakristo ni chama cha kibaguzi haya yalisemwa na CCM, watu tulipinga na kuwaionya CCM kuwa huu ubaguzi mnauleta hautaishia kwa Chadema tu utakwenda mbali zaidi..

Kuna kipindi niliwahai kuongea na Mh. Zitto"Zitto alikiri mwenyewe kuwa ni kweli Chadema ni wabaguzi na ni wadini, alienda mbali zaidi na kusema Mbowe na Slaa

Nilimuuliza je kama ni wadini na wanakuonea wifu je ilikuwaje uwe kiongozi mkubwa hali utoki Kaskazini na pia sio mkristo?
Sikupata jibu ila alisema wewe huwafahamu hawa watu...

Kwa hiyo utaona swala la udini na ukabila lilikuzwa na Zitto na yeye ndo alilipeleka CCM..

Hakuna mtu mnafiki kama Zitto nafikiri kama Mkandara atakuwa mkweli (maana Zitto ni rafiki zako) utakiri hilo..

Sasa rangi za Zitto zinazidi kuonekana wazi, alianza kuhubiri ukabila na udini kwa usiri (hapa kwa wafuasi wake) sasa ameamua kuhubiri ukabila kujenga chuki miongoni mwa watanzani na wachaga akiwa majukwaani..

Leo tunashuhudia wasemaje wa ACT hapa mtandaoni wakijipata kuwa kuna watu hawatompigia kura Slaa (padre) kwa vile ni mkatoliki na hao watawapigia ACT.. Na ukisoma hiki kitu na ukarejea ule waraka wa akina Kitila unaona huyu msemaji wa ACT ambaye ni Kapwela anawakilisha mawazo ya kwenye waraka.

Hivi kwenye karne hii na chama cha wasomi kama ACT bado wanaendekeza siasa hizi za udini na ukabila?

hivi hatuoni majirani yetu huko Rwanda na Burundi jinsi ukabila unavyowatesa mpaka leo?

tena kwa bahati nzuri Zitto ana vinasaba vya hizo nchi au na yeye anataka tuanze kupinga kama wenzetu?

Wanasiasa fanyeni siasa zenu lakini tuacheni Tanzania yetu ikiwa na amani
Ahsante sana
 

Katika Gazeti la Raia Mwema la April 8, 2015 toleo namba 500, Prof. Kitila Mkumbo anajadili dhana ya "Kiongozi Mkuu wa Chama", ndani ya ACT. Hii ni kwa sababu, umma umebakia kuduwaa kufuatia Chama chao cha ACT kuja na muundo mpya ambapo ACT itakuwa na "Kiongozi mkuu wa chama" sambamba na "mwenyekiti wa chama Taifa". Kwa mujibu wa
, maamuzi hayo yamelenga "kuepuka kutengeneza chama dola". Kitila anaendelea kujadili kwamba nchi nyingi barani Africa zimekuwa na vyama dola, suala ambalo limeathiri demokrasia. Anaenda mbali zaidi na kuja na mifano ya nchi kama Uingereza na Afrika ya kusini. Kwa mfano, anasema , namnukuu "Nchini Uingereza, chama cha Conservatives kina kiongozi mkuu wa sasa, David Cameroon, huku wenyeviti wake wakiwa ni Grant Shapps na Lord Feldman". Vile vile, Kiongozi wa chama cha Liberal Democrats ni Nick Clegg, na Mwenyekiti wake ambaye pia anaitwa Rais ni Sal Brinton. Nchini Afrika ya Kusini, Kiongozi wa chama cha ANC ni Jacob Zuma, huku Mwenyekiti wake akiwa ni Bi. Baleka Mbete, ambae pia ni Spika wa Bunge la Afrika ya Kusini.

Kitila anaendelea kujadili kwamba Chama Tawala Tanzania (CCM)ni mfano wa chama dola,kwani muundo uliopo ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) ni muundo ambao umeshindwa kutenganisha mwenyekiti wake na kiongozi wa serikali, hivyo kufanya CCM kuwa ni chama dola. Hivyo basi, kwa mujibu wa Kitila, muundo mpya wa ACT unalenga kuondoa dhana ya udola katika chama chao cha ACT.

Tujaidili hoja hii ya Prof Mkumbo:

Kwanza: Udola wa chama ni suala la mfumo ambao unatambulika kwa mujibu wa katiba Ya chama husika cha siasa. Inaonekana kana kwamba Kitila hajafanya utafiti vizuri kufahamu ili kuwa chama dola, sio lazima chama husika kiwe kimekamata madaraka ya nchi. Kinaweza kuwa ni chama ambacho hakijawahi kuongoza serikali, lakini pia kinaweza kuwa ni chama kipya kabisa katika anga za kisiasa ndani ya taifa husika, lakini mfumo wake ukakifanya kuwa ni "chama dola", kwa mujibu wa katiba ya chama.

Pili, muundo wa chama dola ni muundo ambao uliasisiwa na chama cha mapinduzi nchini Tanzania. Ni muundo huu ndio chama cha ACT aidha kwa kujua au kutojua, kimeamua kuiga. Tukiangalia Katiba za vyama vya CCM na ACT, katiba zote zinataja ‘uchama dola'. Kwa mfano, kwenye katiba ya CCM, mwenyekiti wa chama taifa ndiye huyo huyo Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mwenyekiti huyu mwenye kofia ya urais wa nchi ndiye anayeongoza vikao vyote vizito ndani ya chama kwa maana ya vikao vya CC, NEC na Mkutano mkuu wa taifa. Mwenyekiti huyu wa chama ambae pia ni Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua viongozi wakuu wa chama ngazi ya taifa kuanzia Katibu mkuu wa chama, manaibu na viongozi wa idara mbalimbali ndani ya chama. Pia ana mamlaka ya kuteua watu anaopenda wawepo katika kamati kuu ya chama (CC)Nguvu hii ni karibia sawa na nguvu ya kifalme kwani nafasi aliyonayo ya uenyekiti kamwe haishindanishwi na kupatikana kwa njia ya demokrasia. Kinachotokea ni kwa wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura ya ndiyo au hapana, basi.

Ukiangalia kwa undani, udola uliopo CCM hauna tofauti yoyote ya msingi na nafasi ya kiongozi mkuu wa chama cha ACT,
Zitto. Kama ilivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ambae pia ni rais wa wa nchi, Kiongozi mkuu wa ACT Taifa, Zitto ndio kila kitu ndani ya chama na hakuna nguvu wala mamlaka yoyote ile ambayo inaweza kushindana nae. Kama ilivyokuwa kwa CCM, kwa ACT pia, Madaraka na mamlaka yote yamelundikwa mikononi mwa kiongozi mkuu wa Chama Taifa. Hivyo basin i muhimu Kitila akaacha kuadaa umma kwani ACT ni chama dola kwani kama tulivyojadili awali, udola wa chama hautokani na chama hicho kuwa madarakani, Udola wa chama ni suala la kimfumo zaidi kwa mujibu wa katiba ya chama.

Tukija kwenye hoja ya Kitila ambayo inafananisha ACT na vyama vya nchi za wenzetu, pengine Kitila hana taarifa kwamba vyama vya conservatives na liberal democrats kwa upande wa Uingereza na chama cha ANC kwa upande wa Afrika ya kusini, vyama hivi havina title ya uongozi inayoitwa "Kiongozi Mkuu Wa Chama", badala yake, vyama hivi vina cheo kinachoitwa "Kiongozi wa Chama". Tofauti na wenzetu hawa wa nje, ndani ya katiba ya ACT, hakuna kipengele kinachoeleza jinsi gani nguvu za Kiongozi Mkuu wa chama zinaweza kudhibitiwa. Mamlaka ya aina hiyo haipo ndani ya Katiba ya ACT. Kwa maana hii, mkakati wa akina Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na wenzake uliilenga kumtengenezea Zitto ufalme ndani ya ACT. Mfumo huu uliandaliwa kwa ajili ya mtu mmoja tu, Zitto Kabwe. Chama cha aina hii ni cha kuogopa kama ukoma kwani kinajenga udola hata kikiwa bado hakijapewa ridhaa na wananchi kuongoza nchi.

Wengi bado tunakumbuka vyema jinsi gani Mkumbo, Mwigamba na wenzao walivyokuja na waraka ambao uliwatuhumu viongozi wa chadema kitaifa kwamba ni madikteta. Ukweli unabakia wazi kwamba hadi leo, hakuna kiongozi ndani ya Chadema ambae amewahi kujiundia genge kama la akina Zitto na wenzake. Isitoshe, Katibaya chadema haielekezi kwamba Mwenyekiti au Kiongozi Mkuu wa Chama ndiye atakayegombea urais. Tumeshuhudia kwamba nafasi ya urais inaweza kwenda kwa mwanachama yoyote mwenye sifa. Kwa mfano, Dr. Slaa hajawahi kuwa mwenyekiti au kiongozi mkuu wa Chadema lakini badi ni Kiongozi ambae hadi sasa ndiye anayeaminiwa zaidi katika mbio za urais kwa tiketi ya chadema.

Kwa hiyo anachofanya kitila mkumbo ni upotoshaji wa makusudi kabisa kwani hakuna ukweli wowote kwamba kutenganisha uenyekiti wa chama taifa na nafasi ya kiongozi mkuu wa chama ni kuondoa udola wa chama. Wanachofanya akina kitila ni kupandikiza mbegu ya udikteta. Hatudanganyiki.
Umeeleza vema sana mkuu. Kitila anadhani watu hawaoni alichokifanya.

Kwanza, kitendo cha kuvuta uchaguzi mwezi march ili kumu accommodatemtu mmoja ni udikteta.

Chama ni watu si mtu, ile dhana ya Waraka badoinafanya kazi nje ya ‘adui' yao. Dhana ya kuamini hakuna siasa bila Zitto


Katiba ya ACT inasema, ‘kiongozi mkuu ndiye atakayegombea nafasi ya Urais'

Kwa maana nyingine mgombea wa ACT kwasasa ni Zitto.
Nafasi hiyo imeundwa masaa 24 kabla ya mkutano mkuu.

Kwa maana nyingine wajumbe hawakujua katiba inabadilishwaje na kwasababu zipi.

Kitila na Mwigamba ndio taasisi na taasisi ndio wao


Ule udikteta waliokukimbia CDM, wanautekeleza .Wana supreme leader kwa sababu za Zitto na si mahitaji ya taasisi.
Anachokifanya Kitila ni kudanganya umma.

Umma unafahamu nafasi ya supreme imeundwa kimagumashi ilikumu accommodate Zitto.

Haikuwa nafasi iliyo rasmi hata wajumbe wa kamat ikuu achilia mbali wanachama hawaelewi maana ya supreme.

Wanachoelewa ni kuwa wamepigwa pini kwa nafasi ya Urais kama itakuwepo


Siyo CCM , NCCR, TLP wala CDM yenye katiba inayosema, ‘supreme'wao ndio wana nafasi ya kugombea.

Hoja za Kitila ndio msingi wa sisi wengine kusimama hapa.

Tunajua anachokitaka ni kutumia weledi finyu wa wananchi kuwalaghai.


Wamekula wanatapika sasa wanameza matapishi yao, wakiwalaghai wananchi ni uji wa mchanganyiko.

Coming up!
Siasa chafu za Zittoya kuligawa na kuparaganyisha taifa
Achukua mfumo wa ukbila jiranina nyumbani kwao

Zitto atangaza vita namikoa ya kaskazini. Hasira dhidi ya watu 2, sasa ni mikoa

Apotosha umma kuhusupato na mgawanyo. Abeba sera za CCM kulifarakanisha taifa
Stay tuned
 
mkuu Nguruvi3, nina sikitika sana a suprime leader wa ACT ZZk anapotosha sana wananchi na kuhubiri chuki za ukanda na ukabila kama propoganda za Chama tawala na mawakala wao,

leo hapa Mwanza karudia mambo haya kwa kuwaambia wananchi kwamba mkoa wa Mwanza unachangia sana pato la taifa ila miko y Arusha na Moshi ipo juuu, na pia matamshi yake mengi si ya kujenga cham ial kujijenga binafsi na kuboa upinzani, " walisema mimi na wenzangu si lolote sasa wanaogopa nn kwamba nitagawa kura za upinzani" mara nimefanya mengi bungeni kuzidi wao, this is not politics za kujenga bali kufanya fitna na kujijenga binafsi.

mm binafsi nilikua sipati shida na kuanzishwa kwa cham hiki, il loooh movements zao sasa zinaanza kunip mashak kama vile wako strategically kuvuruga nguvu ya upinzani na kugawa kura haswaa, na kwa hilo sijui CCM mtaisimisha vipi kama kun wapinzani wa wapinzani.
Mkuu sasa hivi si suala la kura, wameanza ''vita vya ukabila''

Zitto kaanza mkakati wa kupambana na mikoa na si mahasimu wake wa kisiasa

Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro sasa ni ‘vita' tu. Mkakati huu ni mzuri sana maana Zitto atakuwa ametangaza ‘vita' na mikoa inayojiletea maendeleo. Sijui akienda Kagera na Mbeya atawaeleza nini

Tutafafanua kwa kina upotofu wa hoja za Zitto.

Kinachotia hofu ni mbegu ya chuki anayoipanda.

Tulitegemea Mwalimu Kitila mkumbo aone hatari hii, kama ndiye anayemshauri basi lipo tatizo kubwa sana nchini


Baada ya Waraka sasa wanashambulia makabila. Wamechukua sera za CCM rasmi

CCM wapo pembeni, mpini unafanya kazi. CCM wanateswa na ukabila na udini walioanzisha, sasa wamekabidhi mafaili wao wanaendelea na ziara za chama
 
Mkuu sasa hivi si suala la kura, wameanza ''vita vya ukabila''

Zitto kaanza mkakati wa kupambana na mikoa na si mahasimu wake wa kisiasa

Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro sasa ni ‘vita' tu. Mkakati huu ni mzuri sana maana Zitto atakuwa ametangaza ‘vita' na mikoa inayojiletea maendeleo. Sijui akienda Kagera na Mbeya atawaeleza nini

Tutafafanua kwa kina upotofu wa hoja za Zitto.

Kinachotia hofu ni mbegu ya chuki anayoipanda.

Tulitegemea Mwalimu Kitila mkumbo aone hatari hii, kama ndiye anayemshauri basi lipo tatizo kubwa sana nchini


Baada ya Waraka sasa wanashambulia makabila. Wamechukua sera za CCM rasmi

CCM wapo pembeni, mpini unafanya kazi. CCM wanateswa na ukabila na udini walioanzisha, sasa wamekabidhi mafaili wao wanaendelea na ziara za chama

Wapi Zitto kataja MAKABILA
 
Last edited by a moderator:
Anachokifanya Nguruvi3 na wenzake kujifanya mtabiri(ablakadabla) wa maisha ya kisiasa ya Zitto.ni sawa mimi niwe naandika kuhusu CDM na UKAWA,
Nianze hivi,huu Muungano wa ukawa naamini hauna maisha,najua kabla au baada ya uchaguzi lazima watagombana,hawateelawana,pia swala la uchaguzi wa Rais na wabunge ukawa linateletta mtifuano,alafu likitokea nije kusema mnaona script yangu imetimia tulisema haya...(ablakadabla)
 
Hebu nipe mfano nilichoongea kama wanandani..Sio kwa nia mbaya inawezekani ulinielewa vibaya au nilishindwa kujieleza.
Swala la urais hilo ni 100% ndicho kilichotoka mdomoni mwa Zitto..

  • Hapa sijui unataka kusemaje? kwamba tunatunga sheria lakini wakati wa kuzitumia basi tuangalie huyu mtu anayetaka kushurutiwa ana cheo gani? na ushawishi gani katika chama na nchi kwa ujumla? yaani kwa maana nyingine sheria zetu ni kwa ajili ya wanyonge tu? Kweli? Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kuwalaumu CCM kuwa wanashindwa kushughulikia mafisadi papa, wauza uga na nk.. wanadeal na vidagaa visivyo na ushawishi wowote katika jamii... au nielewa vingine.



 

  • Hapa sijui unataka kusemaje? kwamba tunatunga sheria lakini wakati wa kuzitumia basi tuangalie huyu mtu anayetaka kushurutiwa ana cheo gani? na ushawishi gani katika chama na nchi kwa ujumla? yaani kwa maana nyingine sheria zetu ni kwa ajili ya wanyonge tu? Kweli? Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kuwalaumu CCM kuwa wanashindwa kushughulikia mafisadi papa, wauza uga na nk.. wanadeal na vidagaa visivyo na ushawishi wowote katika jamii... au nielewa vingine.

  • Ooh nafikiri ni kushindwa tu kujieleza lakni nilikuwa ninamaanisha in general (yaani mawazo yangu hayakuwa katika vyama nilikwenda zaidi katika serikali... Sorry kwa kunielewa vibaya....
 

  • Hapa sijui unataka kusemaje? kwamba tunatunga sheria lakini wakati wa kuzitumia basi tuangalie huyu mtu anayetaka kushurutiwa ana cheo gani? na ushawishi gani katika chama na nchi kwa ujumla? yaani kwa maana nyingine sheria zetu ni kwa ajili ya wanyonge tu? Kweli? Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kuwalaumu CCM kuwa wanashindwa kushughulikia mafisadi papa, wauza uga na nk.. wanadeal na vidagaa visivyo na ushawishi wowote katika jamii... au nielewa vingine.

  • Ooh nafikiri ni kushindwa tu kujieleza lakni nilikuwa ninamaanisha in general (yaani mawazo yangu hayakuwa katika vyama nilikwenda zaidi katika serikali... Sorry kwa kunielewa vibaya....
Haina taabu maana tulikuwa tunazungumzia vyama ndio nikasema kumbe najadili na watunga sheria ndio maana basi hatutaelewana..kama J Makamba na Cyberbill..
 
Tutaangalia kuhusu kauli za supreme leader aliposhambulia mikoa ya kaskazini

Kauli ya kuchangia pato na maendeleo ya sehemu ni ya hatari na ina hitaji mjadala

Tutakuwa na mfulululizo wa mabandiko tukiangalia kauli za supreme na lengo lake katika taifa hili

Inafuata usiku huu
 
Juzi CCM wamemtimua mkongwe Mzee Nassor Moyo kwa sababu eti anashirikiana na CUF... Timua timua hii ingetokea CHADEMA watu wangepiga kelele za "UDIKTETA" ila kwa kuwa imetokea Lumumba hakuna shida!

Ndio mnapokosea hapo wadau wa mabadiliko(demokrasia),jambo likiwa baya ata kama linafanywa na CCM halitoi uhalali wa kuwa jambo jema....sababu ya watu kuunga mkono mabadiliko ni kuichoka CCM( chama changu).na kuhitaji mabadiliko,hatuwezi kuitoa CCM alafu tukaweka mbadala wa hovyo ilo haliwezekani,mmi nipo tayali kwa mabadiliko lakini si ya kuingiza CDM madarakani,chama kinachosigina kanuni na taratibu zake zilizojiwekea,chama kinapata hati yenye mashaka kutoka kwa CAG,kama CCM,ni kujidanganya kuwa wakishika dora kwa bahati mbaya watabadilika ni uongo..nimegundua kitu waliounda vyama vingi vya upinzani walikua CCM ndio mana wanaviendesha Kkama CCM,bora ACT KIMEANZISHWA NA VIJANA,NAZANI HIKI KITAKUA NA MABADILIKO MAKUBWA naweza kujiunga nacho siku moja kama kitafuata mabadiliko ya kweli na demokrasia
Samahani kutoka nje ya mada nilibidi nimjibu huyu kijana
 
Ndio mnapokosea hapo wadau wa mabadiliko(demokrasia),jambo likiwa baya ata kama linafanywa na CCM halitoi uhalali wa kuwa jambo jema....sababu ya watu kuunga mkono mabadiliko ni kuichoka CCM( chama changu).na kuhitaji mabadiliko,hatuwezi kuitoa CCM alafu tukaweka mbadala wa hovyo ilo haliwezekani,mmi nipo tayali kwa mabadiliko lakini si ya kuingiza CDM madarakani,chama kinachosigina kanuni na taratibu zake zilizojiwekea,chama kinapata hati yenye mashaka kutoka kwa CAG,kama CCM,ni kujidanganya kuwa wakishika dora kwa bahati mbaya watabadilika ni uongo..nimegundua kitu waliounda vyama vingi vya upinzani walikua CCM ndio mana wanaviendesha Kkama CCM,bora ACT KIMEANZISHWA NA VIJANA,NAZANI HIKI KITAKUA NA MABADILIKO MAKUBWA naweza kujiunga nacho siku moja kama kitafuata mabadiliko ya kweli na demokrasia
Samahani kutoka nje ya mada nilibidi nimjibu huyu kijana

ACT pia imefanya timua timua kwa kina Limbu so nao ni wale wale tu... shida yangu kubwa ni kwamba huku kwingine zikifanyika hakuna makelele yanayopigwa isipokuwa kwa CHADEMA tu!
 
Ndio mnapokosea hapo wadau wa mabadiliko(demokrasia),jambo likiwa baya ata kama linafanywa na CCM halitoi uhalali wa kuwa jambo jema....sababu ya watu kuunga mkono mabadiliko ni kuichoka CCM( chama changu).na kuhitaji mabadiliko,hatuwezi kuitoa CCM alafu tukaweka mbadala wa hovyo ilo haliwezekani,mmi nipo tayali kwa mabadiliko lakini si ya kuingiza CDM madarakani,chama kinachosigina kanuni na taratibu zake zilizojiwekea,chama kinapata hati yenye mashaka kutoka kwa CAG,kama CCM,ni kujidanganya kuwa wakishika dora kwa bahati mbaya watabadilika ni uongo..nimegundua kitu waliounda vyama vingi vya upinzani walikua CCM ndio mana wanaviendesha Kkama CCM,bora ACT KIMEANZISHWA NA VIJANA,NAZANI HIKI KITAKUA NA MABADILIKO MAKUBWA naweza kujiunga nacho siku moja kama kitafuata mabadiliko ya kweli na demokrasia
Samahani kutoka nje ya mada nilibidi nimjibu huyu kijana
Ndugu yangu, umeshindwa kuelewa hoja ya wadau

Mkandara alisema kuwa mambo ya chama yanamalizwa katika vikao kama CCM wanavyofanya.
Wadau wanauliza, kama ndivyo hivyo, je Mansour na Naossoro Moyo mbona hayakumalizwa katika vikao?

Mkandara anasema, ACT-Waraka hawakutenda kosa linalopaswa kufukuzwa.
Wadau wanauliza, je kusema serikali tatu ni tatizo kubwa kuliko Waraka wa Zitto na kundi lake waliokwenda mbali na kuporomosha matusi kwa mwenyekiti wao?

Washabikii wa ACT wanasema waraka ni mkakati wa ushindi ndio maana ulikuwa siri na hilo si kosa
Je, Manosur na Nassoro moyo wanayoyasema hadharani bila makundi wana makosa gani?

Hoja si kuiga mfumo wa CCM, bali kuonyesha kuwa hoja za utetezi wa ACT kwa kutumia CCM ni muflisi.

Nadhani utakuwa umeelewa
 
Ndugu yangu, umeshindwa kuelewa hoja ya wadau

Mkandara alisema kuwa mambo ya chama yanamalizwa katika vikao kama CCM wanavyofanya.
Wadau wanauliza, kama ndivyo hivyo, je Mansour na Naossoro Moyo mbona hayakumalizwa katika vikao?

Mkandara anasema, ACT-Waraka hawakutenda kosa linalopaswa kufukuzwa.
Wadau wanauliza, je kusem serikali tatu ni tatizo kubwa kuliko Waraka wa Zitto na kundi lake waliokwenda mbali na kuporomosha matusi kwa mwenyekiti wao?

Wahsabiki wa ACT wanasema waraka ni mkakati wa ushindi ndio maana ulikuwa siri na hilo si kosa
Je, Manosur na Nassoro moyo wanayoyasema hadharani bila makundi wana makosa gani?

Hoja si kuiga mfumo wa CCM, bali kuonyesha kuwa hoja za utetezi wa ACT kwa kutumia CCM ni muflisi.

Nadhani utakuwa umeelewa
Mkuu wambo ya chama humalizwa ndani ya Chama kwa maana kwamba Mansour na Moyo wamewafukuza ndio tukatangaziwa. Chadema swala la Zitto na Kitila lilikuwa mitandaoni wakihukumiwa hata kabla ya vikao vya chama. hapakuwa na sababu ya kufanya hivyo inaonyesha utoto na kutojua siasa.
 
Mkuu wambo ya chama humalizwa ndani ya Chama kwa maana kwamba Mansour na Moyo wamewafukuza ndio tukatangaziwa. Chadema swala la Zitto na Kitila lilikuwa mitandaoni wakihukumiwa hata kabla ya vikao vya chama. hapakuwa na sababu ya kufanya hivyo inaonyesha utoto na kutojua siasa.
Nadhania tu sina uhakika. Chadema walituhumiwa siku nyingi kumhujumu Zitto kwa ukanda na hata ukabila. Ikaelezwa, na wewe ni mmojawapo kuwa kutangaza nia ya kugombea uenyekiti ndicho chanzo cha mgogoro

Tuhuma hizo ziliaminika kwa wengi, sisi tupo katika rekodi hapa jamii forum tukisema 'kutangaza nia halikuwa tatizo, tatizo ni busara na muda'

Tukaongeza kusema haiwezekani CDM wawe na mgombea wa Urais halafu Zitto anatangaza nia wakati huo huo.
Hii ilikuwa kumfanya mgombea wao 'useless''

Madai hayo ya uenyekiti na Urais ndiyo yaliovuma na kutumika kama hoja ya kumkweza na kumtetea Zitto
Chadema wakaona hakukuwepo njia nyingine isipokuwa kuelewesha umma yaliyotokea

Mwigamba(Mkulima masikini) akiwa ndani ya kikao alikuwa anaandika na tunasoma hapa JF live.

Mwigamba hakutumia kikao kueleza hisia au asichoridhishwa nacho.

Wala waandika waraka hawakutumia vikao kumaliza matatizo yao.

Hakukuwepo njia nyingine ya kuaminisha umma kuwa zipo hujuma dhidi ya CDM ispokuwa kuweka waraka hadharani.

Leo tunajua kumbe ACT si chama kichanga, ni chama kilichoanza ndani ya Chama. Waraka unatuleza bila kificho
Nadhani ilikuwa ni muhimu kufanya hivyo, vinginevyo CDM ingeshaporomoka siku nyingi kwa mbinu za ACT-WARAKA

Unakumbuka mambo ya vikao waliyafanya sana. Tuliwatahadharisha kuwa Zitto ataleta tatizo. Hiyo ilikuwa 2011, leo yanatokea.

Kuna wakati radical intevention inahitajika. Si katika siasa tu hata maisha ya mwanadamu

Daktari anapotumia dawa bila matokeo mazuri, kuna nyakati hutumia kisu kufanya operation.

Hiyo ndiyo inaitwa radical intervention.
 
Back
Top Bottom