Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Mag3,

Kwa kukufahamisha zaidi tofauti zinakuja pale unapokuwa na MAMBO SII YA PAMOJA hii inaleta Ujumuiya, kama nakumbuka vizuri wamesema wanataka hata Mafuta na Gas yasiwe ya pamoja. Na ukiisoma rasimu kwa makini wamezungumzia mambo yasokuwa na muungano wala sio mwenye mamlaka ya kusimamia shughuli hizo.

Halafu kuna mamlaka ya kusimamia shughuli ni ya nani hii huwa katika Shrikisho pamoja na utunzi wa sheria. Kwa hiyo rasimu imeeleza mamlaka wakati huo huo ikitofautisha Mambo yaliyopo ktk muungano. Hiki chako/changu na hiki sii chetu.

Kwa hiyo utaona kama hapa Canada kama sikosei jambo pekee ambalo sio la Muungano ni ELIMU na hii inatokana na Quebec ambao wao elimu inafundishwa kwa Kifaransa na wana mitaala yao (am I right na kiswahili hiki?) tofauti na upande mwingine. lakini kila Province as state ina mamlaka ya kushughulikia mambo yake japo ni ya Kitaifa. Wamegawana kazi..
 
Mkandara narudia, unayo matatizo. Naomba nikuulize ulitaka Muungano wetu wa Shrikisho ufanane na wa nchi gani ndiyo uukubali? Ujerumani, Marekani, Canada, Uingereza au nchi gani na kwa nini ufanane na nchi hizo? Ni wewe huyo huyo unatetea Muungano wetu wa sasa wa serikali mbili, je huu uliwahi kuuona wapi? Tunapoukosoa ni nyie hao hao mnasema si lazima ufanane na Muungano mwingine, kwamba ni ubunifu wetu; sasa unapodai kwamba Uliopendekezwa na tume haufanani na wa huko unakokaa, does all this make any sense to you?
 
Last edited by a moderator:
Mkandara narudia, unayo matatizo. Naomba nikuulize ulitaka Muungano wetu wa Shrikisho ufanane na wa nchi gani ndiyo uukubali? Ujerumani, Marekani, Canada, Uingereza au nchi gani na kwa nini ufanane na nchi hizo? Ni wewe huyo huyo unatetea Muungano wetu wa sasa wa serikali mbili, je huu uliwahi kuuona wapi? Tunapoukosoa ni nyie hao hao mnasema si lazima ufanane na Muungano mwingine, kwamba ni ubunifu wetu; sasa unapodai kwamba Uliopendekezwa na tume haufanani na wa huko unakokaa, does all this make any sense to you?
Duh mkuu unataka mimi niseme miye weee...Nimeshasema wazi kabisa kwamba sipendi swala la Muungano lijadiliwe, kama kweli wanataka maoni yangu basi ni SERIKALI MOJA ifuate baada ya serikali MBILI. lakini maadam hilo haliwezekani basi hakuna sababu kabisa ya kuongelea Muungano kwa sasa kukidhi matakwa ya wanasiasa.

Na maadam wananchi walitaka serikali 3 za Shrikisho basi wengi wapewe, lakini kuisoma rasimu nakuta sivyo ndipo nikapingana na rasimu hiyo. Na nikaendelea kupingana na Chadema kufikia maamuzi ya kuungana na CUF kwa sababu wanapotosha zaidi wananchi na msimamo wao juu ya swala hili aidha hawakujua nao au ndivyo wanavyotaka.

Kwa hiyo mawazo yangu na fikra zangu ni mimi zichukue kama navyo chukua zenu na kuzitolea hoja na makosa yake. Sikuona faida ya kujadili Muungano na serikali 2/3 wakati sheria kuu hairuhusu.. maamuzi ya kutaka kubadilisha Muungano ni makosa sawa na yale ya kamati kuu ya Chadema kuwahukumu kina Zitto. Muungano hubadilishwa kwa referendum pale wananchi wanapewa fursa ya kupiga kura ya NDIO au HAPANA juu ya muungano uliopo, sio maoni ya watu wachache juu ya katiba. Ni mtazamo wangu kufuata sheria za nchi na ndio Uzalendo.
 
Mkandara;12482071]Mag3,

Kwa kukufahamisha zaidi tofauti zinakuja pale unapokuwa na MAMBO SII YA PAMOJA hii inaleta Ujumuiya, kama nakumbuka vizuri wamesema wanataka hata Mafuta na Gas yasiwe ya pamoja.
Ngoja tuweke mambo sawa kwa kuchomoka chomoka kidogo nje ya mada

Mkuu kwa kauli hii ndiyo maana Mag3 hakuelewi. Rasimu ya Warioba iliondoa mafuta na gesi kama kilio cha wazanziibar

Katiba ya Chenge yenye muundo wa S2 imeondoa mafuta na gesi

Tupe muundo mwingine, maana yote miwili imeliona tatizo.
 
Last edited by a moderator:
Mag3;12482209]Mkandara narudia, unayo matatizo. Naomba nikuulize ulitaka Muungano wetu wa Shrikisho ufanane na wa nchi gani ndiyo uukubali? Ujerumani, Marekani, Canada, Uingereza au nchi gani na kwa nini ufanane na nchi hizo?
Sijui kama swali hili litajibiwa, atakayejibu swali hilo atazua mengine,wanajua. Wataliacha lipite
Ni wewe huyo huyo unatetea Muungano wetu wa sasa wa serikali mbili, je huu uliwahi kuuona wapi?
Tunapoukosoa ni nyie hao hao mnasema si lazima ufanane na Muungano mwingine, kwamba ni ubunifu wetu; sasa unapodai kwamba Uliopendekezwa na tume haufanani na wa huko unakokaa, does all this make any sense to you?
Katika kuficha ukweli , muungano huu wanauita wa 'kipekee''

Likibuniwa shirikisho la 'kipekee' inakuwa dhambi kubwa maana hakuna kitu hicho duniani.

Neno 'kipekee' ni mali ya CCM, kibali kinahitajika kabla ya kulitumia

Hapa ndipo tusema , ni ngumu sana kumuelewa mkuu Mkandara anasimamia wapi
 
Mkandara;12482271]Duh mkuu unataka mimi niseme miye weee...Nimeshasema wazi kabisa kwamba sipendi swala la Muungano lijadiliwe, kama kweli wanataka maoni yangu basi ni SERIKALI MOJA ifuate baada ya serikali MBILI. lakini maadam hilo haliwezekani basi hakuna sababu kabisa ya kuongelea Muungano kwa sasa kukidhi matakwa ya wanasiasa.
Mkuu Mkandara anasema, hali ibaki kama ilivyo akimaanisha S2 za kipekee. Kutojadili muungano ni kosa kubwa, Kikwete alijaribu akakumbana na hasira za umma, likarudishwa katika rasimu
Na amejaribu katika BMLK unaona aibu aliyokutana nayo. Huwezi kuficha uvundo uvunguni kwa kupulizia utuli
Sikuona faida ya kujadili Muungano na serikali 2/3 wakati sheria kuu hairuhusu.. maamuzi ya kutaka kubadilisha Muungano ni makosa sawa na yale ya kamati kuu ya Chadema kuwahukumu kina Zitto. Muungano hubadilishwa kwa referendum pale wananchi wanapewa fursa ya kupiga kura ya NDIO au HAPANA juu ya muungano uliopo, sio maoni ya watu wachache juu ya katiba. Ni mtazamo wangu kufuata sheria za nchi na ndio Uzalendo
Sheri gani inayouzia kujadili muungano?

Wananchi wapi na referendum ipi ilipigwa wakati wa kuungana?
Kama maoni ya Warioba ni ya wachache, yapi ya wengi yaliyotengeneza muungano huu unaoutetea kwa sheria?

Ni wapi maoni ya wengi yalizingatiwa kwa kutumia katiba ya Chenge?

Sheria gani unayotaka ifuatwe?

Kufanya referendum kumeainishwa katika katiba sehemu gani na nani mwenye mamlaka na eneo hilo?

Na referendum ni universal law au !
 
ngurivi3,

Samahani nilitoka kidogo nimerudi. Ni wapi mimi nimesema katiba ya Chenge ni nzuri kuliko ya Warioba? Nizungumze mara ngapi ya kwamba tulichovuna ni matokeo ya nyie kutaka kuzungumzia Muungano, hatukutakiwa kuzungumzia kabisa Muungano acha ulivyo wanasiasa ndio wamesababisha haya na maamuzi yametokana na wanasiasa.

Narudia kusema hivi wananchi walitaka serikali ya Shirikisho, sii jambo baya ni zuri, lakini bado nakubaliana na mwalimu Nyerere kwamba sisi bado maskini, hatuna uwezo huo kutokana na mapungufu yetu wenyewe ni mengi..Na hii inatokana na mageuzi ya mwaka 1984 na 1993 tumekuwa na mipango mibaya ya ukusanyaji kodi na mgawanyo wa mapato hata ndani ya Tanganyika tu bado mikoa inategemeana sana.

Hivyo, kilichotakiwa kwangu mimi ni kurekebisha tu maadhi ya sheria ambazo ziliwakwaza wananchi katika jamii na taasisi zao, vyama vya siasa na ushirika, mashirika ya Umma na uwekezaji, Miswala ya Utawala katika uadilifu na uwajinikaji. haya ndiyo chimbuko la matatizo yetu na wakatafuta mchawi kama kawaida akawa Muungano, hivyo tunauadhibu muungano kwa makosa ya kimfumo.

Pili, Refendum ya Muungano haiwezi kuwa katika Katibamkuu wangu inatangulia uandishi wa katiba. Muungano ndiyo nchi nyenyewe na katiba inaandikwa kutokana na kile ulichonacho. Kwa mfano Muungano ni ramani ya kiwanja na katiba ni archtectural plan ya nyumba, hivyo huwezi kuandaa plan ya nyumba pasipo kuwa na hati ya kiwanja, wala ramani ya nyumba haiwezi kuwa sababu ya upataji wa kiwanja. Umenielewa!

Kwa nini mnazunguka tuu nikitoka huku mnaingia mlango huu, tumezungumza ya Shirikisho na Jumuiya mmeingia ya katiba ya Chenge nani aloipitisha au alosababisha ikawepokakma sio nyie mpolotaka muungano wa Jumuiya. Hao Wazanzibar wachache wala mimi hawanipi homa wala kunikosesha usingizi kwa sababu najua endapo watapewa referendum ya kuchagua NDIO au HAPANA wengi watasema HAPANA kwa sababu wanajua haya yanayotokea leo South yatakuja Bara na itakuwa hamna tena usalama wala undugu..
 
Mkandara;12484077]ngurivi3,

Samahani nilitoka kidogo nimerudi. Ni wapi mimi nimesema katiba ya Chenge ni nzuri kuliko ya Warioba?
Unaposema ni afadhali tubaki kama tulivyo tusizungumzie muungano maana yake umeridhika na S2 na muundo wa sasa. Unaona mkuu unavyohamisha magoli wengine tunapochukua mpira!
Nizungumze mara ngapi ya kwamba tulichovuna ni matokeo ya nyie kutaka kuzungumzia Muungano, hatukutakiwa kuzungumzia kabisa Muungano acha ulivyo wanasiasa ndio wamesababisha haya na maamuzi yametokana na wanasiasa.

Narudia kusema hivi wananchi walitaka serikali ya Shirikisho, sii jambo baya ni zuri, lakini bado nakubaliana na mwalimu Nyerere kwamba sisi bado maskini, hatuna uwezo huo kutokana na mapungufu yetu wenyewe ni mengi..Na hii inatokana na mageuzi ya mwaka 1984 na 1993 tumekuwa na mipango mibaya ya ukusanyaji kodi na mgawanyo wa mapato hata ndani ya Tanganyika tu bado mikoa inategemeana sana.
Dah mkuu yaani watanzania wote na hasa wazanzibar hawaelewi isipokuwa wewe peke yako! Kwani vurugu zimeanzia wapi?
Hivyo, kilichotakiwa kwangu mimi ni kurekebisha tu maadhi ya sheria ambazo ziliwakwaza wananchi katika jamii na taasisi zao, vyama vya siasa na ushirika, mashirika ya Umma na uwekezaji, Miswala ya Utawala katika uadilifu na uwajinikaji. haya ndiyo chimbuko la matatizo yetu na wakatafuta mchawi kama kawaida akawa Muungano, hivyo tunauadhibu muungano kwa makosa ya kimfumo.
Halafu unakana kuwa hupendi katiba ya Chenge. Sasa tutabaki vipi kama si S2 za Chenge? Mkuu mbona unakata rivasi bila indiketa. Unaposema tubaki kama tulivyo, maana yako ni S2 na kwa maana kubwa tukubali katiba ya Chenge ya S2.
Mag3 anaposema ni ngumu sana kukuelewa, nadhani unaweza kutazama katika kioo na kuona wapi watu hawakuelewi
Pili, Refendum ya Muungano haiwezi kuwa katika Katibamkuu wangu inatangulia uandishi wa katiba. Muungano ndiyo nchi nyenyewe na katiba inaandikwa kutokana na kile ulichonacho. Kwa mfano Muungano ni ramani ya kiwanja na katiba ni archtectural plan ya nyumba, hivyo huwezi kuandaa plan ya nyumba pasipo kuwa na hati ya kiwanja, wala ramani ya nyumba haiwezi kuwa sababu ya upataji wa kiwanja. Umenielewa!
Mkuu hatuandiki katiba kutoka mwanzo. Ipo ya 1977 iliyounda sheria ya mchakato. Sheria ya mchakato haikusema uwepo wa referendum. Sasa unaposema unasimama katika sheria za nchi kama mzalendo, sheria gani unayosimamia isiyokuwepo. Kwangu mimi ningesema, kabla ya kujadili katiba lazima tungekuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu mambo kadha wa kadha muungano ukiwemo. Kisha tunachagua nini kianze, kwa vipi na sababu zipi. Ni lazima tuweke dira. Hili linaeleweka zaidi mkuu
Kwa nini mnazunguka tuu nikitoka huku mnaingia mlango huu, tumezungumza ya Shirikisho na Jumuiya mmeingia ya katiba ya Chenge nani aloipitisha au alosababisha ikawepokakma sio nyie mpolotaka muungano wa Jumuiya. Hao Wazanzibar wachache wala mimi hawanipi homa wala kunikosesha usingizi kwa sababu najua endapo watapewa referendum ya kuchagua NDIO au HAPANA wengi watasema HAPANA kwa sababu wanajua haya yanayotokea leo South yatakuja Bara na itakuwa hamna tena usalama wala undugu..
Mkuu umetuondoa katika mada ya ACT, sasa unashtumu.

Hiki ni kionjo tu cha uzi huu katika kupunguza kasi ya kuwaangalia walaghai. Turudi kwenye nyuzi za muungano, waungwana wapo

Mengine tuwaachie wznz kwasababu hata sasa hivi sioni future nzuri kwao. Wanataka nchi yao wapewe!


Kwa taarifa yako.

Zitto alipotoka katika BMLK alisema UKAWA wamekosea, walitakiwa wabaki ndani.
Kinachoshangaza yeye aliungana na waliokosea kutoka, halafu anawasota vidole

Leo ACT wanasema moja ya sera zao ni kurudi katika rasimu ya Warioba

Nadhani taratibu utatuelewa tuna maana gani!
 
Nguruvi3,
Wewe una matatizo ya kumsoma mtu ukamuelewa. Hilo nalijua wala sio limeanza leo hii.
Nimesema swala la Muungano ni la referendum halihusiki kabisa na maoni ya wananchi wala Katiba Mpya, na nikakupa mfano wa Kiwanja cha nyumba. Ili watu mgawane Kiwanja kilichopo tayari, hamtatazama matakwa ya ramani za nyumba ya kila mmoja wenu kujadili kiwanja hicho, bali mmekubaliana nini kuhusu makazi yenu yatakuwa vipi, Je, kugawana kiwanja kimoja ktk nyumba mbili tofauti, au hiyo hiyo moja lakini msingi ubomolewe na kujenga mkubwa zaidi na kikubwa zaidi ujirani wenu utakuwa vipi. Mazungumzo haya hupitia maafikiano ya kusema tugawane ama tujenge nyumba moja kwa wote - Artical of Union sio Constitution.

Kwa hiyo, Kama tulitaka kuzungumzia Muungano hapakuwa na sababu wala haja ya kuandika katiba ya Muungano ilihali tunataka kugawanyika. Tungeichukua Artical of Union ijadiliwe, tukafanya referendum yake pekee kisha majibu yakipatikana tunaunda hizo nchi na serikali zake. halafu ndio itafuatia uandikaji wa katiba za nchi ama katika Mpya ya JMT ilokubaliwa, aidha kwa serikali 1, hizi hizi 2, serikali 3 ya Shirikisho au Jumuiya kutokana na maamuzi ya wananchi.

Kilichofanyika,tulianza kuchora ramani ya nyumba na kugawana hadi kiwanja wakati kisheria kiwanja kina jina moja tu. Ina maana tulitaka kujenga nyumba mbili ambazo hazina Title wala hati miliki..

Vurugu zipi? Wazanzibar ni kina nani haswa kwako ni hao CUF? maana kulikuwepo wajumbe wa Zanzibar walopinga serikali 3 na ndio walofanya akidi itimie. Wewe umewezaje kuchagua kuwasikiliza Wazanzibar wa CUF na isiwe wa CCM..Hawa CUF walowaacha mataani uchaguzi wa 2010 wakaungana na CCM dhidi yenu?.

Huelewi na Hutaelewa juu ya Muungano na serikali zake nitakuacha ulivyo maana nilichosema ni kwamba hatukutakiwa kuzungumzia Muungano wakati tunaandika Katiba. katiba haizai Muungano ila Muungano ndio huzaa katiba. Wewe umezaliwa kutokana na wazazi wawili haiwezekani ukawepo wewe kwanza ili kuwazaa wazazi wako wawili.

Katiba haijengi sheria za Muungano, muungano hutanguliwa na makubaliano yake Artical of Union ambayo huelezea kitu kilichopo ni kama hati ya kumiliki kiwanja. Hivyo huwezi kunambia unapochora ramani ya nyumba itaonyesha hadi masharti ya kiwanja hicho badala ya mipaka yake tu.

Hapana mada ya ACT ipo pale pale ni maswali mlotaka nyie uniuliza na sikuchoka kuwajibu. Na naendelea kusema ACT ni zao la Chadema kama nilivyosema Katiba ya Chenge ni za la UKAWA. If only, wangetumia kidogo hekima na busara matokeo yake yasingekuwa haya tulonayo.
 
Katika Gazeti la Raia Mwema la April 8, 2015 toleo namba 500, Prof. Kitila Mkumbo anajadili dhana ya “Kiongozi Mkuu wa Chama”, ndani ya ACT. Hii ni kwa sababu, umma umebakia kuduwaa kufuatia Chama chao cha ACT kuja na muundo mpya ambapo ACT itakuwa na “Kiongozi mkuu wa chama” sambamba na “mwenyekiti wa chama Taifa”. Kwa mujibu wa Kitila Mkumbo, maamuzi hayo yamelenga “kuepuka kutengeneza chama dola”. Kitila anaendelea kujadili kwamba nchi nyingi barani Africa zimekuwa na vyama dola, suala ambalo limeathiri demokrasia. Anaenda mbali zaidi na kuja na mifano ya nchi kama Uingereza na Afrika ya kusini. Kwa mfano, anasema , namnukuu “Nchini Uingereza, chama cha Conservatives kina kiongozi mkuu wa sasa, David Cameroon, huku wenyeviti wake wakiwa ni Grant Shapps na Lord Feldman”. Vile vile, Kiongozi wa chama cha Liberal Democrats ni Nick Clegg, na Mwenyekiti wake ambaye pia anaitwa Rais ni Sal Brinton. Nchini Afrika ya Kusini, Kiongozi wa chama cha ANC ni Jacob Zuma, huku Mwenyekiti wake akiwa ni Bi. Baleka Mbete, ambae pia ni Spika wa Bunge la Afrika ya Kusini.

Kitila anaendelea kujadili kwamba Chama Tawala Tanzania (CCM)ni mfano wa chama dola,kwani muundo uliopo ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) ni muundo ambao umeshindwa kutenganisha mwenyekiti wake na kiongozi wa serikali, hivyo kufanya CCM kuwa ni chama dola. Hivyo basi, kwa mujibu wa Kitila, muundo mpya wa ACT unalenga kuondoa dhana ya udola katika chama chao cha ACT.

Tujaidili hoja hii ya Prof Mkumbo:

Kwanza: Udola wa chama ni suala la mfumo ambao unatambulika kwa mujibu wa katiba Ya chama husika cha siasa. Inaonekana kana kwamba Kitila hajafanya utafiti vizuri kufahamu ili kuwa chama dola, sio lazima chama husika kiwe kimekamata madaraka ya nchi. Kinaweza kuwa ni chama ambacho hakijawahi kuongoza serikali, lakini pia kinaweza kuwa ni chama kipya kabisa katika anga za kisiasa ndani ya taifa husika, lakini mfumo wake ukakifanya kuwa ni “chama dola”, kwa mujibu wa katiba ya chama.

Pili, muundo wa chama dola ni muundo ambao uliasisiwa na chama cha mapinduzi nchini Tanzania. Ni muundo huu ndio chama cha ACT aidha kwa kujua au kutojua, kimeamua kuiga. Tukiangalia Katiba za vyama vya CCM na ACT, katiba zote zinataja ‘uchama dola’. Kwa mfano, kwenye katiba ya CCM, mwenyekiti wa chama taifa ndiye huyo huyo Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mwenyekiti huyu mwenye kofia ya urais wa nchi ndiye anayeongoza vikao vyote vizito ndani ya chama kwa maana ya vikao vya CC, NEC na Mkutano mkuu wa taifa. Mwenyekiti huyu wa chama ambae pia ni Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua viongozi wakuu wa chama ngazi ya taifa kuanzia Katibu mkuu wa chama, manaibu na viongozi wa idara mbalimbali ndani ya chama. Pia ana mamlaka ya kuteua watu anaopenda wawepo katika kamati kuu ya chama (CC)Nguvu hii ni karibia sawa na nguvu ya kifalme kwani nafasi aliyonayo ya uenyekiti kamwe haishindanishwi na kupatikana kwa njia ya demokrasia. Kinachotokea ni kwa wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura ya ndiyo au hapana, basi.

Ukiangalia kwa undani, udola uliopo CCM hauna tofauti yoyote ya msingi na nafasi ya kiongozi mkuu wa chama cha ACT, Zitto. Kama ilivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ambae pia ni rais wa wa nchi, Kiongozi mkuu wa ACT Taifa, Zitto ndio kila kitu ndani ya chama na hakuna nguvu wala mamlaka yoyote ile ambayo inaweza kushindana nae. Kama ilivyokuwa kwa CCM, kwa ACT pia, Madaraka na mamlaka yote yamelundikwa mikononi mwa kiongozi mkuu wa Chama Taifa. Hivyo basin i muhimu Kitila akaacha kuadaa umma kwani ACT ni chama dola kwani kama tulivyojadili awali, udola wa chama hautokani na chama hicho kuwa madarakani, Udola wa chama ni suala la kimfumo zaidi kwa mujibu wa katiba ya chama.

Tukija kwenye hoja ya Kitila ambayo inafananisha ACT na vyama vya nchi za wenzetu, pengine Kitila hana taarifa kwamba vyama vya conservatives na liberal democrats kwa upande wa Uingereza na chama cha ANC kwa upande wa Afrika ya kusini, vyama hivi havina title ya uongozi inayoitwa “Kiongozi Mkuu Wa Chama”, badala yake, vyama hivi vina cheo kinachoitwa “Kiongozi wa Chama”. Tofauti na wenzetu hawa wa nje, ndani ya katiba ya ACT, hakuna kipengele kinachoeleza jinsi gani nguvu za Kiongozi Mkuu wa chama zinaweza kudhibitiwa. Mamlaka ya aina hiyo haipo ndani ya Katiba ya ACT. Kwa maana hii, mkakati wa akina Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na wenzake uliilenga kumtengenezea Zitto ufalme ndani ya ACT. Mfumo huu uliandaliwa kwa ajili ya mtu mmoja tu, Zitto Kabwe. Chama cha aina hii ni cha kuogopa kama ukoma kwani kinajenga udola hata kikiwa bado hakijapewa ridhaa na wananchi kuongoza nchi.

Wengi bado tunakumbuka vyema jinsi gani Mkumbo, Mwigamba na wenzao walivyokuja na waraka ambao uliwatuhumu viongozi wa chadema kitaifa kwamba ni madikteta. Ukweli unabakia wazi kwamba hadi leo, hakuna kiongozi ndani ya Chadema ambae amewahi kujiundia genge kama la akina Zitto na wenzake. Isitoshe, Katibaya chadema haielekezi kwamba Mwenyekiti au Kiongozi Mkuu wa Chama ndiye atakayegombea urais. Tumeshuhudia kwamba nafasi ya urais inaweza kwenda kwa mwanachama yoyote mwenye sifa. Kwa mfano, Dr. Slaa hajawahi kuwa mwenyekiti au kiongozi mkuu wa Chadema lakini badi ni Kiongozi ambae hadi sasa ndiye anayeaminiwa zaidi katika mbio za urais kwa tiketi ya chadema.

Kwa hiyo anachofanya kitila mkumbo ni upotoshaji wa makusudi kabisa kwani hakuna ukweli wowote kwamba kutenganisha uenyekiti wa chama taifa na nafasi ya kiongozi mkuu wa chama ni kuondoa udola wa chama. Wanachofanya akina kitila ni kupandikiza mbegu ya udikteta. Hatudanganyiki.
 
Last edited by a moderator:
....
Kwa nini mnazunguka tuu nikitoka huku mnaingia mlango huu, tumezungumza ya Shirikisho na Jumuiya mmeingia ya katiba ya Chenge nani aloipitisha au alosababisha ikawepokakma sio nyie mpolotaka muungano wa Jumuiya......
Mpaka hapa nawashukuru sana kwa michango yenu juu ya mada iliyoko mezani. Haikuwa nia yangu kujadili mtu, lakini utaratibu huu wa michango ya Mkandara na lazimika 'kumsema kidogo'. Mkandara nadhani hana nia ya dhati ya kujadili mada muhimu katika jukwaa hili. Hii nikutokana na tabia yake ya kuzungusha maneno ya mjadala mmoja kwenda kwa mjadala mwingine. Mkiwa kwenye mada ya muungano atafanya kila njia kuwaingizia habari za Supreme leader na ACT yake, mkienda huko anawarudisha kwenye mada ya muungano....basi kazi yake ni kuzungukazunguka tu ili apunguze uzito wa hoja iliyoko mezani.

Nashauri tuendelea kupinga upotoshaji wa malengo ya mada husika unaofanywa na Mkandara, ambaye anazungushazungusha maneno. Wamejitahidi sana Mchambuzi, Mag3, Nguruvi3 kwa muda mrefu na wengineo kupinga upotoshaji huu. Na wahasa tusikubali kuingia kwenye mitego ya Mkandara ya kuvuruga mada.
=============================================================
Mpaka sasa tunaweza kuwa sahihi kwa kubadili kichwa cha mada hii na kusomeka " Zitto na wenzake mpini wa CCM kuhujumu upizani/ushindani wa kisiasa Tanzania". Sababu za kubadili kichwa cha mada hii zipo post namba 216, 224,227,231, 233 kwa uchache.
 

Mpaka hapa nawashukuru sana kwa michango yenu juu ya mada iliyoko mezani. Haikuwa nia yangu kujadili mtu, lakini utaratibu huu wa michango ya Mkandara na lazimika 'kumsema kidogo'. Mkandara nadhani hana nia ya dhati ya kujadili mada muhimu katika jukwaa hili. Hii nikutokana na tabia yake ya kuzungusha maneno ya mjadala mmoja kwenda kwa mjadala mwingine. Mkiwa kwenye mada ya muungano atafanya kila njia kuwaingizia habari za Supreme leader na ACT yake, mkienda huko anawarudisha kwenye mada ya muungano....basi kazi yake ni kuzungukazunguka tu ili apunguze uzito wa hoja iliyoko mezani.

Nashauri tuendelea kupinga upotoshaji wa malengo ya mada husika unaofanywa na Mkandara, ambaye anazungushazungusha maneno. Wamejitahidi sana Mchambuzi, Mag3, Nguruvi3 kwa muda mrefu na wengineo kupinga upotoshaji huu. Na wahasa tusikubali kuingia kwenye mitego ya Mkandara ya kuvuruga mada.
=============================================================
Mpaka sasa tunaweza kuwa sahihi kwa kubadili kichwa cha mada hii na kusomeka " Zitto na wenzake mpini wa CCM kuhujumu upizani/ushindani wa kisiasa Tanzania". Sababu za kubadili kichwa cha mada hii zipo post namba 216, 224,227,231, 233 kwa uchache.
hivi ndivyo unavyoamini wewe pasipo kunisoma isipokuwa kutazama mjadala umekwenda wapi. Kinachotokea mimi naulizwa maswali yanayotutoa ktk mada husika na kosa langu pengine useme ni kuyajibu badala ya kuendelea kudai majibu.

Lakini kama kweli unatafuta ukweli rudi nyuma ukurasa wa 11 hoja yangu ya 217 kisha tazama imejibiwa vipi na tumeendelea vipi toka hapo au rudi mnyuma labisa hoja yangu ya 19. je, mimi nilipatiwa majibu ama nilirudishiwa maswali mengine yalotutoa nje..
 

Mpaka hapa nawashukuru sana kwa michango yenu juu ya mada iliyoko mezani. Haikuwa nia yangu kujadili mtu, lakini utaratibu huu wa michango ya Mkandara na lazimika 'kumsema kidogo'. Mkandara nadhani hana nia ya dhati ya kujadili mada muhimu katika jukwaa hili. Hii nikutokana na tabia yake ya kuzungusha maneno ya mjadala mmoja kwenda kwa mjadala mwingine. Mkiwa kwenye mada ya muungano atafanya kila njia kuwaingizia habari za Supreme leader na ACT yake, mkienda huko anawarudisha kwenye mada ya muungano....basi kazi yake ni kuzungukazunguka tu ili apunguze uzito wa hoja iliyoko mezani.

Nashauri tuendelea kupinga upotoshaji wa malengo ya mada husika unaofanywa na Mkandara, ambaye anazungushazungusha maneno. Wamejitahidi sana Mchambuzi, Mag3, Nguruvi3 kwa muda mrefu na wengineo kupinga upotoshaji huu. Na wahasa tusikubali kuingia kwenye mitego ya Mkandara ya kuvuruga mada.
=============================================================
Mpaka sasa tunaweza kuwa sahihi kwa kubadili kichwa cha mada hii na kusomeka " Zitto na wenzake mpini wa CCM kuhujumu upizani/ushindani wa kisiasa Tanzania". Sababu za kubadili kichwa cha mada hii zipo post namba 216, 224,227,231, 233 kwa uchache.
Mkuu nashukuru sana sana umeliona hilo, ndio njia yake inayotuika kupoteza mada.
Nia ya mkuu ni kupunguza uzito wa mada.

Anachotaka nikuondoka katika mada akijua yapo mengi hayajafumuliwa kuhusu ACT na kiongozi mkuu

Turudi kwenye mada na tuendelee
 
Mkuu nashukuru sana sana umeliona hilo, ndio njia yake inayotuika kupoteza mada.
Nia ya mkuu ni kupunguza uzito wa mada.

Anachotaka nikuondoka katika mada akijua yapo mengi hayajafumuliwa kuhusu ACT na kiongozi mkuu

Turudi kwenye mada na tuendelee
Ok nipeni basi majibu yenu ya hoja zangu toka #19 au rukia #217 usilete majibu ama hoja inayotutoa ktk mada hii wala msizungumzie Mkandara quote my name only..maana ndio kawaida yenu hoja ya ACT au Zitto hugeuka kuwa Mkandara..
 
Ngoja tuzirejee hoja zako za bandiko 217
[Mkandara;12470233]MchambuziUnajua mnasiitisha sana nikiwasoma maana kama vile hamjui siasa?
Inawezakana hatujui siasa, na inawezakana hujui siasa. Jambola muhimu tuache wasomaji waamue pumba na mchele. Kumbuka ‘the beauty is on the eye beholder
iweje ACT ije kuuwa upinzani ikiwa itikadi na sera zao zinatofautiana? Je, Ushindani wa vyama ni kuvunjana au mlitaka mfumo wa chama kimoja maana siwaelewi kabisa.
ACT inakuja kutimiza malengo yaliyoshindikana walikotoka(Mag3).

Focus ya wananchi ni kuunga mkono upinzani ili kuondoa donda ndugu la miaka 50 linalowatafuta.

Jana Zitto anawaambia wananchi wa Shinyanga,mikoa ya Kilimanjaro na Arusha inachangia pato dogo lakini ipo katika kumi la kwanza la maeneo yaliyopiga hatua


Hakutumia busara kwasabau hoja yake haiungwi mkono na historia, jitihada na jiografia kwa uchache wa kusema.

Alitoa hoja ilikuwaaminisha wananchi wa Shinyanga kuwa yeye ni mtu wa eneo lao na hivyo wakatae watu wa ‘maeneo' tajwa.

Lengo lilikuwa kuwazuia wananchi kuunga mkono upinzani kwa kutumbukiza hoja chafu, dhaifu na kipuuzi ya kuwagawa


Hoja aliyotumia ni ile ya CCM wanayotumia kuhusu vyama vyakikanda na kikabila.

Hapa Zitto akiwa ‘mpinzani' kabeba mpini wa shoka la CCM kuondoa focus ya wananchi kuhusu CCM na kubomoa upinzani. Umeelewa ?
Na mnaposema Upinzani mna maana gani maana kuna vyama 22, hiyo UKAWA yenyewe vyama vitatu sijui vinne waloungana, Je wao hawakuvunja Upinzani? Ni kipimo gani mnachotumia kuusema Upinzani ni huu maana vyama vyote 21 kasoro CCM ni Upinzani, iweje mchague vyama vitatu tu na kuuita Upinzani mkaviacha vyama vingine 17 vilivyokuwepo hata kabla ya ACT? vile vyama walivyoviacha nje ya UKAWA havikuwa Upinzani isipokuwa wabunge wa Chadema, CUF na NCCR..Na Mrema kwa nini walimwaga UKAWA? sababu gani na kupitia sheria zipi..Je, Hivi vyama vilivyoachwa nje wakiamua kuungana na kuunda umoja wao watakuwa wamekuja kuvunja Upinzani pia sio? ama wao itakuwa tofauti..nani alowapa ridhaa UKAWA kuwa na mamlaka ya kusema nani awe nao nani asiwe nao ikiwa wote lengo lao ni kuindoa CCM madarakani..
UKAWA imeundwa katika bunge la katiba. Wabunge hao waliona haja ya kuwa na umoja wa wabunge wa bunge la JMT.

Vyama ulivyosema vinauwakilishi. Hivyo Ukawa haikuanzishwa kwa sharia na haina kizuizi kwa vyamavingine vilivyobaki


Vyama vilivyo nje ya UKAWA tayari vina umoja wao. Nadhani upo nyuma ya wakati

Umoja wao si wa distraction inayoletwa na ACT kama hoja ya ukanda inayohubiriwa na Zitto.

Kwamba, siasa imemuelemea sasa anagawa wananchi.

Vyama 17 havijawahi kuja na agenda ya kibubusa kama ya Zitto


Mrema hajazuiliwa au kupigwa marufuku UKAWA. Amejiuzia kwa kushirikiana na CCM.

Huyu mtu anayesema CCM haishikiki akiwa na mgombea Uraiswake katika kampeni ni mpinzani kweli?

Tofauti ya Mrema na Zitto ipo wapi kwamwendo uliopo sasa hivi?
Nitasema moja tu ya kwamba ACT isingekuwepo kama Chadema wasingewafukuza Kitila, Mwigamba na Zitto. Hivyo maadam Chadema waliona umuhimu wa kuwafukuza wakijua fika kwamba hawa watu ni wanasiasa, kuondoka kwao wataunda chama chao lakini haitakuwa tishio kwao, basi hakuna sababu ya kulalamika leo maana Chadema walijua na walitegemea haya kutokea. Tulionya mkasema Chadema haiwategemei wao waende wanakotaka Chadema Imara, sasa uimara huo unaogopa mpini tu pasipo hata shoka lenyewe....Alaa kumbe Upinzani ni gogo la mti lilosubiri kupasuliwa bahati mbaya tawi lake limejengwa kuwa mpini!..
ACT ilikuwepo siku zote.

Waandika waraka ndio vinara wa ACT.

Kilichobadilika ni kuwa katibua wa Waraka sasa ni katibu wa ACT.

Mshauri wawaraka sasa ni mshauri wa ACT.

Mhusika mkuu aliyetajwa katika Waraka sasa ni supreme leader
Unapomtalakia mkeo, tarajia ya kwamba ipo siku atakuja olewa na mume mwingine. Na haolewi ili akuvunje nguvu wewe bali amefanya maamuzi hayo kwa kutazama maisha yake mwenyewe, yeye kasonga mbele nawe songa mbele usitazame sana maisha ya mtalaka wako. Yote mnayomsema humu Zitto hayana ubaya isipokuwa yeye anaposema ndio mnachukulia -Unaona kasema hivi na vile lakini ya kina Mbowe, Mnyika na Lissu ni maneno matamu
Kama mtalaka huyo anayekujua atashirikiana na majambazi,nawe ukarudi kulala raha mstarehe utakuwa ni mpuuzi wa haja. Utakuwa mjinga kami

Zitto kaanza kuhubiri sera za kuwagawa wananchi kwa kitumbua chake,unataka tuseme maneno hayo kaya sema Mrema, Mnyika au Kuga Mziray? Ebo!

Supreme leader anaposimama na kuhubiri sera za kuwagawawananchi unataka tukae kimya.

Supreme leader anatakiwa awe role model ya umojana mshikamano.

Siasa zina muelemea sasa anarudi kwenye siasa za CCM zaudini, ukanda na ukabila.
Alichokisema hakina ukweli, hakina busara wala hekima.

Tukaekimya siasa majitaka zikilielemea taifa! Maiaka 50 tume kaa kimya, unataka tukae kimya tena!

Tutamwambia supreme , no way! Hapa umebofoa, chukua likizo utulize akili.

Siasa za kugawa wananchi ni muflisi, dhaifu chafu na hazikubaliki

Hapa ni JF 'Duru' hapendwi mtu inapendwa hoja



 
Wanasiasa wa Tanzania ni umiza kichwa, Mwanzo tulihubiriwa kuwa Chadema ni chama cha Wachaga ni chama wa wakristo ni chama cha kibaguzi haya yalisemwa na CCM, watu tulipinga na kuwaionya CCM kuwa huu ubaguzi mnauleta hautaishia kwa Chadema tu utakwenda mbali zaidi..

Kuna kipindi niliwahai kuongea na Mh. Zitto kuhusu swala la Ukabila na udini nikataka maoni yake yeye kama kiongozi wa chama Kweli majibu yake nilibaki nimepigwa na butwaa "Zitto alikiri mwenyewe kuwa ni kweli Chadema ni wabaguzi na ni wadini, alienda mbali zaidi na kusema Mbowe na Slaa unamuonea wivu maana yeye atakuwa rais (kumbuka hapo ilikuwa ni mwaka 2008) Nilimuuliza je kama ni wadini na wanakuonea wifu je ilikuwaje uwe kiongozi mkubwa hali utoki Kaskazini na pia sio mkristo? Sikupata jibu ila alisema wewe huwafahamu hawa watu...

Kwa hiyo utaona swala la udini na ukabila lilikuzwa na Zitto na yeye ndo alilipeleka CCM.. Hakuna mtu mnafiki kama Zitto nafikiri kama Mkandara atakuwa mkweli (maana Zitto ni rafiki zako) utakiri hilo..

Sasa rangi za Zitto zinazidi kuonekana wazi, alianza kuhubiri ukabila na udini kwa usiri (hapa kwa wafuasi wake) sasa ameamua kuhubiri ukabila kujenga chuki miongoni mwa watanzani na wachaga akiwa majukwaani..

Leo tunashuhudia wasemaje wa ACT hapa mtandaoni wakijipata kuwa kuna watu hawatompigia kura Slaa (padre) kwa vile ni mkatoliki na hao watawapigia ACT.. Na ukisoma hiki kitu na ukarejea ule waraka wa akina Kitila unaona huyu msemaji wa ACT ambaye ni Kapwela anawakilisha mawazo ya kwenye waraka.

Hivi kwenye karne hii na chama cha wasomi kama ACT bado wanaendekeza siasa hizi za udini na ukabila? hivi hatuoni majirani yetu huko Rwanda na Burundi jinsi ukabila unavyowatesa mpaka leo? tena kwa bahati nzuri Zitto ana vinasaba vya hizo nchi au na yeye anataka tuanze kupinga kama wenzetu? Wanasiasa fanyeni siasa zenu lakini tuacheni Tanzania yetu ikiwa na amani.


"""Zanzibar kumbuka kura mnazozitafuta ni laki 2 tu, sio kiasi kikubwa kama unavyodhani.Pia fahamu kuwa wapiga kura wengi wa CUF hasa bara watawakimbia hasa mgombea akiwa Dr Slaa(Padre), hivyo kura pekee za CUF ambazo Chadema ina uhakika nazo ni za Zanzibar sababu ya serikali tatu.

NCCR haina wapiga kura.

Narudia, ni mapema mno saizi, subiri baada ya bunge kuvunjwa na vyama vipate wagombea ndio tutakuwa na position ya kuongea lolote."""

Hii ndo kauli ya ndugu Kapwela ambaye ni mpiga debe wa ACT..
 
Nguruvi3 na Alinda,

Pengine hamnielewi mimi msimamo wangu katika jambo hili la Uanachama. Sikubaliani na fukuza fukuza ya wanachama iwe kwa chama chochote, ni maamuzi ambayo binafsi nayaacha kwa mwanachama mwenyewe. Hivyo vyama vinapoendesha siasa za fukuza fukuza haina maana kwamba wako sawa kwa mtazamo wangu, wako sawa kwa mtazamo wao.

Nimeweka hiyo katiba kukuonyesha kuwa hata ACT wanakipengele cha kufukza fukuza, hivyo basi nilitegemea hii nguvu unayotumia kupinga hicho kipengele kwa Chadema basi ungetumia hata robo yake kuwashawishi hao viongozi wa ACT walioathariwa na kipengele cha fukuza fukuza wasikiweke katika katiba yao. Ukizingatia kuwa katiba yao umefanyiwa marekebisho hivi karibuni.

Hivyo inaweza kuwa sawa kwao lakini basi wafuate taratibu na sheria zao zinavyosema. Swala la kina Kitila limeanza katika uongozi kuondolewa kinyume cha taratibu walizoweka Chadema, halafu sababu za kufukuzwa pia hazijitoshelezi kutokana na hizo hizo kanuni zao. Ndio maana napingana nano kwa sheria zao wenyewe na kusherehesha na maoni yangu juu ya kufukuzana.

Kama waliondolewa kama unavyodai walikuwa na wajibu wa kufuata taratibu za kukaa rufaa katika chama chao.

Halafu kuhusu Masour Himid tunazungumzia wanachama ngazi ya uongozi ndani ya chama. Umuhimu wa Himid katika uongozi wa chama CCM hata iwe Zanzibar ndio nilitaka kujua maana anayefukuzwa ni mwanachama na jinsi gani anahitajika na chama na ndio maana yeye kafukuzwa lakini mtu kama Lowassa ameachwa huru hadi kesho. Na sidhani kama Himid na Lowassa unaweza pima nguvu zao. Hili pia sina maana CCM wamefanya inavyotakiwa ila wajanja ndani ya sheria zao wenyewe. Wametazama maslahi ya chama mbele, kuondolewa kwake kunaweza sababisha mgawanyiko.

Hapa sijui unataka kusemaje? kwamba tunatunga sheria lakini wakati wa kuzitumia basi tuangalie huyu mtu anayetaka kushurutiwa ana cheo gani? na ushawishi gani katika chama na nchi kwa ujumla? yaani kwa maana nyingine sheria zetu ni kwa ajili ya wanyonge tu? Kweli? Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kuwalaumu CCM kuwa wanashindwa kushughulikia mafisadi papa, wauza uga na nk.. wanadeal na vidagaa visivyo na ushawishi wowote katika jamii... au nielewa vingine.

Niaminivyo mimi mwanachama yeyote akinyimwa fursa za kushiriki katika mambo yote ya chama basi tayari kisha malizwa kisiasa, maana hata mikutano ya chama hatashirikishwa. Atabakia mwanachama wa kadi tu na kama atapenda kuendelea kushika ganda hilo ni juu yake. Mimi nawaona watu kibao wakijiita Chadema au CCM wakati hawashirikishwi ktk maandalizi ya jambo lolote yaani wana kadi tu. Wakati ninavyoamini mimi kuhusu mfumo wa chama, mtu yeyote anapojiandikisha uanachama ina maana yupo tayari ku volunteer katika jambo lolote atakapo hitajika na chama. Kuchaguliwa kuongoza ama kusaidia chama katika maandalizi ya jambo lolote. sasa huu mpango wa kuwa na wanachama millini 2 ukategemea ati wao ndio watakupigieni kura ni makosa kabisa na nayaona Tanzania tu.

Wazo lako ni vizuri lakini kuna mantiki yeyote kuwa na wanachama ambaye anakihujumu chama? Mfano hashiriki katika shughuli zozote za chama, ana nadi chama kingine, unatoa siri za chama na nk.Hivi ukiamua kufanya sensa ya wanachama huyu unamhesabu kuwa naye ni wanachama wako ingawaje kadi nayo? Tukumbuke kila chama au jumuia ina sheria zake, kabla ya kujiunga unakubaliana na hizo sheria zao, sasa iweje ukiuke hizo sheria na utake kubaki chamani? hataka kanisani usipofuata sheria zao watakutenga na nadhani hata kwa waislam ni hivyo hivyo..(ingawaje sina uhakika).

Huku kwenye demokrasia ya ukweli, inapofikia wakati wa kupiga kura kila mwananchi ana ruksa ya kumchagua mtu yeyote na toka chama chochote na asipoteze uanachama wake. Wakati wa kura kila mtu ni free of choice na kama sikosei uchaguzi wa 2008 (awamu ya kwanza ya Obama), Colin Powell a Republican alisema wazi tena mbele ya vyombo vya habari kwamba kura yake atampa Obama (Democratic), na hatukuona akifukuzwa uanachama. Kwa hiyo sina maana ACT ndio wako sawa Kikatiba ila siwezi pindua maamuzi yao na itakuwa vema wafuate masharti waloyaweka. Wakienda nje ya kanuni zao nitawapata vile vile.

Ukisoma kipengele cha katiba ya ACT wao inatosha kabisa wewe Mkandara wana ACT unaposema "Alinda mwana Chadema ni jembe" huna uwanachama tena.. Je hilo ni sawa na kama sio sawa unashauri nini kifanyike kwa hawa ACT, maana siasa sio ugomvi na si dhani kama wanaccm wote wanapigia wagombea wa ccm au chadema na nk.
 
Mkuu nashukuru sana sana umeliona hilo, ndio njia yake inayotuika kupoteza mada.
Nia ya mkuu ni kupunguza uzito wa mada.

Anachotaka nikuondoka katika mada akijua yapo mengi hayajafumuliwa kuhusu ACT na kiongozi mkuu

Turudi kwenye mada na tuendelee

mkuu Nguruvi3, nina sikitika sana a suprime leader wa ACT ZZk anapotosha sana wananchi na kuhubiri chuki za ukanda na ukabila kama propoganda za Chama tawala na mawakala wao,

leo hapa Mwanza karudia mambo haya kwa kuwaambia wananchi kwamba mkoa wa Mwanza unachangia sana pato la taifa ila miko y Arusha na Moshi ipo juuu, na pia matamshi yake mengi si ya kujenga cham ial kujijenga binafsi na kuboa upinzani, " walisema mimi na wenzangu si lolote sasa wanaogopa nn kwamba nitagawa kura za upinzani" mara nimefanya mengi bungeni kuzidi wao, this is not politics za kujenga bali kufanya fitna na kujijenga binafsi.

mm binafsi nilikua sipati shida na kuanzishwa kwa cham hiki, il loooh movements zao sasa zinaanza kunip mashak kama vile wako strategically kuvuruga nguvu ya upinzani na kugawa kura haswaa, na kwa hilo sijui CCM mtaisimisha vipi kama kun wapinzani wa wapinzani.
 
nguruvi3 na Alinda,

Nawasoma vizuri tu lakini inaonyesha kama kwamba hapa tunabishana watu wa makundi ya Chadema na ACT, badala ya mawazo binafsi na mkamuelewa mtu kama mawazo yake against institutions hizi. Na kibaya zaidi juu ya mada hizi ni kwamba mnataka watu wote tufikirie sawa, na yeyote anayepingana na hoja zenu basi yeye huwa hafai isipokuwa mawazo yenu ndio yanayotakiwa. sasa kweli kuna haja ya kuwa na mjadala ikiwa mawazo ya wengine hupewa majina na kuwa wewe mfulani uko hivi na vile badala ya mada na hoja yenyewe. Ni fikra za kimfumo kama hizi ndizo zinatuponza wakati wote aidha ni mila na desturi yetu ama ni kuamini ushindani wa fikra ni dharau fulani.

Mimi nishasema sina maamuzi ya ujenzi wa ACT na kanuni zao ila nategemea watazitumia ipaswavyo kama walivyoandika, japo sikubaliani na fukuza fukuza ya wanachama maana chama hakipati usajili pasipo kuwa na wanachama. Na wakisha pata Usajili tu, ndio hizi habari za wenye chama unaanza ni makosa! Without them, chama kisingepata usajili hata kama mngekuwa wasomi 100. Ni mawazo yangu Huru ambayo hata ACT wanakaribishwa tulonge sina mshirika katika ninayo amini kuwa ndio ukweli.

Mimi siwafahamu na nimeyasoma maelezo yenu ni kama vile nyie ni watu wa ndani wa Chadema mnaokitumikia chama kwa njia moja ama nyinginezo. Majibu yenu ni ya uhakika na chanzo na kilichotokea wakati mimi ni mtazama sinema ilokwisha tolewa. Ni mawazo yangu binafsi hayatokani na Zitto wala ACT isipokuwa picha yenyewe. na kila napowasoma huona mahusisho mengi baina yangu na Zitto au ACT, jamani Mnajua fika kwamba I was Nobody Chadema, na nilikuwa nazungumzia mazuri yake kila siku humu JF na wala sikuwa na Ukaribu wa kisiasa na kiongozi yeyote isipokuwa mawazo yangu binafsi iweje leo iwe Mkandara na ACT au Zitto.

Back to the topic, Sasa kama kweli mlijua toka zamani kwamba Zitto alianzisha chama ndani ya chama ili awe sijui rais? ingewezekana vipi wakati Zitto mwaka 2008 alikuwa hana Umri wa kugombea Urais iwe kwa mwaka 2010 au 2015? Je, kuna kosa lolote mimi kupingana na ushahidi wenu juu ya Motive yake, maana crime yoyote huanza na motive! Ila nachokiona hapa ni Zitto kutaka kugombea MWENYEKITI ndilo lingetumiwa ningekubali. Hizi habari za kuunda chama ndani ya chama ili awe rais wa chama au wa serikali ya JMT... maana sielewi mnachokisema na wala sijawasoma Chadema mahala popote wakisema Zittto alitaka kubadilisha mfumo wa uongozi wa Chadema ili awe rais wa Chadema kama alivyo ACT.

Zitto asingeweza kuanzisha chama ndani ya chama halafu akataka kugombea Uenyekit wa chama anachokivuruga. Hii haingii akilini.. Aliutaka uenyekiti wa nini na kwa nini iwe kosa na haramu kugombea kiasi kwamba hadi aitwe na wazee wa chama. Nilipoongea naye Zitto kwa bahati mwaka 2009 kama sikosei alisema yeye alipendekezwa na watu kugombea na akaletewa fomu akiwa uwanja wa ndege kugombea. Kwa hiyo kilichofuata kabla hazijaza akatangaza nia yake.. Ikawa kosa kubwa na utovu wa nidhamu.. Hakuelewa why? do I blame him no.

Huu ndio ukweli naoufahamu mimi na nilipofanya utafiti wangu niajulishwa kwamba maamuzi yalikwisha pitishwa nafasi ya Uenyekiti Mbowe aendelee na Muhula wa pili. Sijui na kina nani lakini ndivyo ilivyokuwa na Zitto pamoja nambaadhi ya watu hawakujulishwa. Hivyo utaona tayari kulikuwa na kutoelewana ndani ya chama maana siwezi amini Zitto aliunda chama ndani ya chama wakati huo huo akigombea uenyekiti wa chama anachotaka kukivuruga. Mkinambia Zitto had a dream one day atakuwa rais wa nchi hii na aliwaambia watu hayo naweza kubali lakini haya ya kupindua chama 2008 na motive iwe apate kugombea Urais - Hapana..

Mimi Mbowe mshikaji wangu, na amekuwa na ambition ya Urais Urais toka zamani nikimjua na sikuona ubaya maana kila binadamu ana ndoto zake. Na kufanikisha ndoto hiyo ni swala la kutokata kamaa wala kukubali maneno ya watu kwamba huwezi. Binafsi nilisema hawezi kuwa rais wa Tanzania maana sikutegemea Mbowe nimjuaye angeweza kuwa mwanasiasa na kipaji cha kuongea na ushawishi vile hivyo ilikuwa shock kwangu. Na nadhani yeye akiwa hapa JF kwa jina bandia kama sikosei, alinambia yule Mbowe umjuaye wewe sio huyu tafuta muda umjue vizuri..

Nachokumbuka mimi kabla ya uchaguzi wa 2010, Chadema ilibadilisha Mrengo kuwa kulia kati sielewi sababu lakini sisi wengine wapiga debe tulisema tupo na Chadema kwa lengo ya kuionda CCM madarakani, hivyo haikujalisha ni itikadi kwa muda huo. Hizi siasa za Udini na Ukabila ndani ya vichwa vya wanaChadema zipo japo sio kikatiba wala kanuni. Mkumbuke tena mimi husema Chama ni WANACHAMA wenye uuamini wa itikadi sio Club wala NGO. Pamoja na kuwepo Katiba, Wanachama ndio hu define chama, wakienda nje ya imani yao ndivyo chama kitatambulika na sio Katiba yao wala kanuni yao. Tunawaona CCM leo na katiba yao havifanani kabisa kwa sababu CCM ni jina tu, Wanachama wake ndio sura kamili ya chama hicho.

Na niseme pia ni Ujinga kuamini kwamba Tanzania hakuna Udini, udini upo na Ukabila unaanza kujitokeza japo sheria zetu mama zinakataza lakini on the ground viashirio vya Ukabila vipo. Na ndio maana tunazo sheria kama nchi haina Ukabila ama Udini hamuwezi kuweka sheria maana havipo ila sheria hutungwa kwa kuzuia vile vilivyopo ili wakosa wapewe adhabu kali. Kwa hiyo kama Zitto alisema kuna Udini na Ukabila ingetakiwa viongozi wa Chadema wajitazame upya na wanachama wake. Mimi nawasoma humu JF mawazo ya watu wakifungamana na Chadema katika siasa za Udini. na kibaya zaidi hata napojaribu kuelezea hoja inayohusu haki za Waislaam hutupiwa majibu mazito na wengine tayari wanaamini nimemfuata Zitto kwa sababu za kidini. Tungekuwa kabila moja oooh ndio ungekolea zaidi.

My Findings, ACT ni mazao ya kile Chadema ilichopata yenyewe na kile walichovuna. Nimesoma habari nyingi zsana juu ya Zitto nyingine zikiandikwa na viongozi na kila siku kuna tuhuma tofauti. In fact waraka ni sababu ndogo sana imetumiwa na viongozi ambao baadhi yao walisema hata huo waraka sio sababu. Kuna utata katika ukweli kwamba Zitto aliarifiwa mashataka yake maana ilisemekakan Zitto, Kitila na Mwigamba walikuwepo siku ya kuhiojiwa, kumbe sio kweli alokuwepo ni Kitila peke yake.

Hakuna ukweli kwamba Zitto aliwahi kuepelekewa mashataka kwa maandishi akajieleza, yupo kiongozi alosema hapakuwa na sababu maana aliitwa ktk kikao hakutokea. yaani kuna uongo uong mwingi katika sakata la kina Kitila. hujui umuamini nani. Sasa Chama kuwa WAZI wakatueleza exactly what happened na mashtaka hayo kufikishwa baraza kuu kulikuwa na shida gani? No one knows.

Yes, ACT inaweza kuwa mpini wa CCM lakini ulochongwa na Chadema kuibomoa Chademana sio UPinzani maana UKAWA sio Upinzani ila ni kundi la watu wanaotaka kugawana majimbo. hawana nia thabiti ya kuchukua IKULU na kama wangekuwa nayo wangeisha ungana na kuunda UMOJA unaotambulika. Huu ndio mtazamo wangu na haya ndio mawazo yangu mimi..
 
Mkandara nitakuja kukujibu baada.. Ila niweke mambo sawa..

Nasisitiza Mimi na nguvuri3 hatufahamiani kabisa ni kama wewe na mimi...yaani tunakutana hapa JF. Ingawaje nigefurahi kama ningewafahamu nje wa JF..

Mimi sio kiongozi wa Chama, Ingawaje ninapenda mageuzi na sera za Chadema zinanivutia hasa swala la Elimu.

Swala la Urais ndo na wewe ushangae.. Lakini zaidi ya hapo siwezi kwenda deep. Nitaishia hapo kwenye urais...

.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom