Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

ha ha ha ....umeuliza maswali mazuri

ugomvi wa kaburu na chacha, Nguruvi hawezi kueleza maana ukimgusa chacha unagusa kila kasoro na baya la chadema ambalo limekuwa likilalamikiwa na kila mpenda mabadiliko

Ni hivi, Nguruvi pamoja na kuandika post ndefu ambazo huwa hakuna akili inayotumika kuandika bali mahaba yake kwa Mbowe, huwezi hata kidogo ukamuweka kwenye kundi la GT
Waberoya huo mgogoro wa Chacha na Kaborou siyo ‘taboo'unajadilika.

Ni vema mngeujadili nasi tutachangia kama mnavyofanya nyie


Pili, loh nikushukuru maana wafuasi wa kiongozi yoyote yule ni nadra kukubaliana nasi.
Huwa siangalii makunyanzi naangalia hoja, maono ,mitazamo na uadilifu


Sina uhakika kama wapenzi wa Mbowe wataridhika au kufurahiakauli yako!

Tatu, kuhusu mabandiko marefu yasiyo na akili, hilo nawaachiawasomaji. Ninaandika binafsi.

Nilichokiona, unayosoma sana kiasi cha kujua hayana akili, lakini bado unayasoma.
Ni kweli unaweza kusoma ujinga kila siku ukiamini ni ujinga?


Nne, kuhusu GT, ni wewe umeniambia hilo. Sijaomba kuwa GT na wala si nia ya mabandiko haya kutufikisha huko.

Nia ni majadiliano na kupanua fikra. Katika kufikia lengo hilo, hatuna mapenzi na mtu bali na hoja


Ningeshangaa kama ungezungumza jema kutuhusu.
Mtu akitaka maadui kiurahisi njia nyepesi ni kusema ukweli. Tunakumbatia ukweli kwasababu Unatuwe kahuru


Katika ‘mabandiko yasiyo na akili' hakuna tulichosema ambacho Zitto hajafanya.

Kinachotokea sasa hivi ni ‘movie ikiwa theatre' sisi tulikuwa studio tukiwaletea wanajamvi kila kinachojiri. Ndivyo ilivyo !

Bandiko moja nyuma, tumesema, Zitto ni mwanasiasa mwenye charisma(kismati).
Kwa bahati mbaya hana vichocheo vya Charisma kimoja kikiwani busara.

Tulieza kuwa charisma ya Zitto ina makundi haya


1 Wanaomwamini tu bila sababu bali wanamwamini. Hawa watasimama kidete kumtetea Z akiwa na kinyesi.
Watasema siyo uchafu wa mwanadamu ni mbolea ya mboji.

Kundi hili likimuona Zitto bila mavazi haliwezi kusema kuna tatizo, litasema anadumisha utamaduni wa mwafrika.

Kundi hilo wenyewe wanasema lipo mesmerized and hypnotized.Waberoya ni mfano mzuri wa wamiliki wa kundi hili

2 Kundi lisolomwamini Zitto. Hili halimwamini kwasababu limeshaondoa Imani naye.

Lilianza kama kundi lenye chuki tu(haters), kadri siku zinavyosonga mbele, kundi limebadilika na halionekani kama haters.
Linakumbatia ukweli unaojitokeza.Kundi linapata nguvu kila siku na sasa ni mwiba kwa Zitto.

3. Kundi la tatu ni lile lenye mashaka. Halina uhakika kamaZ ni mtu wa ina gani.

Nalo linazidi kumegeka na kuondoa mashaka yaliyokuwepo.Lina hama kwenda kundi la pili.

Kadri Z anavyozungumza, kundi la tatu ambalo nikubwa linazidi kumegeka.
Limebaki kidogo lenye shaka shaka, kama ni kweli au sikweli.


Zitto anapoteza public trust. Na sasa ana makundi mawili, lakwanza na la pili.
La tatu linamtoka, maaana mashaka juu ya z yanazidi kuondoka kila uchao.


Umeelewa mkuu?
 
Nguruvi, zitto amekuathiri kisaikolojia

fanya kazi mkuu, ndio siasa zilivyo

ukimsema na kumuwaza mtu kila siku kila saa maana yake anakutawala

that is the facts
 
Nguruvi, zitto amekuathiri kisaikolojia

fanya kazi mkuu, ndio siasa zilivyo

ukimsema na kumuwaza mtu kila siku kila saa maana yake anakutawala

that is the facts
Hapana !!! nipo 'sober' ndiyo maana ninakuwa mbele ya kila anachokifanya kila mara.

Tuliandika hapa kuwa Zitto hakwenda mahakamani kudai haki, alikwenda kupigania tumbo lake.

Mwenye kathibitisha kuwa ni mwanzilishi wa ACT. Yaani wakati anapigania haki ya kubaki CDM wakati huo huo anatekeleza mradi wa ACT. Ndiyo yale yale ya kada wa CDM akiwa na waraka mkononi

Tulisemwa tuna chuki kwasababu haki inapatikana mahakamani.
Watu wakaimba na kuserebuka. Leo wanageukia mabandiko haya na kuona haya. Zitto kawaacha njia panda

Tunachofanya ni kuutanabahisha umma kuhusu utapeli.

Hatutegemei kundi la kwanza (mesmerized and hyptonized) wanaweza kutuelewa.

Hatutegemei kundi la pili kubadili msimamo wao kwasababu kila siku msimamo wao unapata ushahidi na nguvu mpya.

Tunategemea kundi la tatu lenye mashaka linaweza kupata kitu.
Linaweza kuondoa mshaka juu ya zitto iwe kwa njia hasi au chanya.

Tunalaani uhuni wa kisiasa, tunataka kizazi kipaya chenye fikra mpya, uadilifu na ukweli.

Tunapoteza maadili ya kiroho tukiendelea kuwasumanga CCM ni wahalifu wakati matapeli wapo katika viunga vya nyumba zetu

Tunaita mafisadi wa CCM wezi na majambazi, halafu mafisadi wa kisiasa tunawaita wazalendo.
Tunawaita CCM majambazi, wengine tunawaita wajasirilia mali

Hapana, tutasimama kuusaidia umma kuelewa mbivu na mbichi. Katika hali hiyo, tunategemea maadui wengi.

Maadui ni wengi, hata hivyo si wengi kuliko umma unaotutia moyo.

Kama kuna mwananchi mwadilifu mmoja tu ataelewa tunadhamiria nini katika mabandiko, huyo ni bora kuliko wapiga debe 10 wanaotegemea mkate wa bwana kwa kulaghai umma

Tukijiunga na wanaosema Zitto ni msaliti, tukaweka kalamu chini bila kuonyesha ubora na udhaifu wake,tutakuwa wasaliti wa mageuzi nchini kuliko yeye.


coming up, flip flop za Zitto katika wiki mbili tu kama kiongozi mkuu (supreme leader)
 
Mimi nataka kuuliza swali moja tu kwa ndugu zangu wana UKAWA maana tunapozungumzia jambo lazima tulipime na kuelewa mnachopigania. Na huu uwe mtihani kwenu kujiuliza pangine mnayo majibu tayari naomba mnipe nami nifumbue macho pale napokataa kuamini..

Katiba ya JMT ya mwaka 1977 -Sura ya Pili sehemu ya kwanza, Ibara ya 41 inasema hivi:-

(6) Mgombea yeyote wa kiti cha Rais atatangazwa kuwaamechaguliwa kuwa Rais iwapo tu amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote.
(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka yakuchunguza kuchaguliwa kwake.

Sasa tuseme, hypoathetical matokeo ya Urais yakiwa hivi kwa asilimia:- Mgombea wa CCM 45, Chadema 35, CUF 10, NCCR 5, TLP 3, na vyama vinginevyo 2.

1. Hapa japo CCM imeshindwa na umoja wa Upinzani UKAWA kwa asilimia kubwa tu, lakini mnadhani nani ataunda serikali kulingana na Katiba iliyopo?

2. Imetokea tofauti Chadema wamepata asilimia 45, CCM 35, CUF 10, NCCR 5, TLP 3 na vinginevyo 2.. Je, ni sheria gani inayoilazimu Chadema kuunda serikali ya mseto na vyama vilivyoshindwa wakawaacha CCM waloshika nafasi ya pili?

3. Je makubalino yoyote baina ya vyama vya mseto huu yanapewa kinga gani Kikatiba (sheria) maana nijuavyo rais anayechaguliwa na kupata ushindi huchukua mamlaka yote The Winner take all. Sasa atalazimika kuunda vipi baraza la Mawaziri kutoka vyama vilivyoshindwa, ikiwa hakuna sheria yoyote inayoruhusu wala kulazimisha serikali ya mseto kutokana na matokeo ama makubalino ya vyama kuunda serikali pasipo kuungana.

4. Kuna tofauti gani kati ya kuunda umoja huu na Uchaguzi ulopita 2010 ikiwa kila chama kitasimamiasha kitahesabiwa kwa kura za mgombea wake na sio mjumuiko wao? UKAWA haikusajiliwa kama umoja wa vyama kugombea uongozi..

5. Ni kiasi gani cha asilimia ya kura ambazo kikatiba au sheria, chama kimetakiwa au kulazimika kuunda serikali ya Mseto?..

Naomba kuwakilisha na tafadhali msije na matusi ila hoja ili tuelimishane.
 
Tuliandika hapa kuwa Zitto hakwenda mahakamani kudai haki, alikwenda kupigania tumbo lake.
Mkuu Nguruvi3, tarehe 7/1 2015, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kesi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe ambapo ilimpa kinga ya muda kutojadiliwa uanachama wake na Kamati Kuu ya Chadema! Swali ambalo wengi tulikuwa tunajiuliza ni hili, je huyu Zitto ana ajenda gani anapoomba mahakama iizuie Chadema isimjadili? Kwa nini wenzake aliopanga nao pamoja njama za kuanzisha chama ndani ya chama waliridhika haraka haraka na hatua iliyochukuliwa na Chadema dhidi yao lakini Kiongozi wao ang'ang'anie kubaki Chadema? Kumbe...! Wale walikuwa ni watengeneza njia. Zitto alishafanya uamuzi kitambo wa kuondoka Chadema ila alitaka aondoke kwa mbwembwe ili aweze kuisababishia Chadema alichoamini ni madhara makubwa kisaikolojia. Kwake maamuzi yoyote yale ya mahakama hayangebadilisha kitu; alikuwa tayari kajipanga kuyakabili ila bahati mbaya hakujiandaa kwa hatua ambayo ingechukuliwa na Chadema.
Mwenye kathibitisha kuwa ni mwanzilishi wa ACT. Yaani wakati anapigania haki ya kubaki CDM wakati huo huo anatekeleza mradi wa ACT. Ndiyo yale yale ya kada wa CDM akiwa na waraka mkononi
Kama ilivyokuja kuthibitika Zitto ni ACT na ACT ni Zitto, yeye sio tu ni Kiongozi Mkuu wa ACT; yeye ni nuru wa ACT, bila yeye hakuna mwanga, watu hawaonani. Alitanguliza watengeneza njia kuhakikisha kazi hiyo wanaifanikisha kabla ya hukumu ya Mahakama kama ilivyopangwa...kusafisha njia kwa kung'oa visiki vyote ambavyo vingekuwa vikwazo katika kutawazwa kwake kuwa Kiongozi Mkuu. Baada ya hukumu kutolewa lillopangwa kufuata ni kuitishwa kwa waandishi wa habari huku akiwa amezungukwa na wajumbe watiifu, kutangaza kujitoa Chadema na kuvikwa taji. Fikiria magazeti ya kirafiki na redio, habari kubwa ambayo ingetawala...Mh. Zitto aiacha Chadema kwenye mataa!
Tulisemwa tuna chuki kwasababu haki inapatikana mahakamani. Watu wakaimba na kuserebuka. Leo wanageukia mabandiko haya na kuona haya. Zitto kawaacha njia panda
Huu mchezo ulipangwa kitambo sana lakini wakasahau kitu kimoja; palipo na watu wanaoongozwa na mahaba, lazima pia kuwe na watu wa kuhoji kulikoni? Wenye mahaba waliwaona watu wanaohoji kama wenye chuki ingawa ukweli ambao hawataki kuuona acha kuuhoji ni hili; Zitto alikuwa na sababu gani za kuing'ang'ania Chadema? Alipoona hawezi kutimiza ndoto yake kupitia Chadema kwa nini hakubwaga tu manyanga kama Freddy Mpendazoe alipoamua kusamehe Ubunge kupitia CCM? Hapana Zitto alikuwa na ajenda kubwa zaidi na chama chake cha zamani na kama si intelijensia ya Chadema yenye vichwa kama Lissu, Mnyika, Marando n.k. utabiri wa Wassira ungetimia kupitia kwa Zitto Kabwe. Kumbe ujanja si kuwahi, ni kupata.
Tukijiunga na wanaosema Zitto ni msaliti, tukaweka kalamu chini bila kuonyesha ubora na udhaifu wake,tutakuwa wasaliti wa mageuzi nchini kuliko yeye.
Hapana, katu hatunyamazi. Wengine tumenyamaza toka kuanzishwa kwa vyama vingi, tukiweka matumaini yetu mikononi mwa walafi, wafitini na wasaliti na sasa imetosha. Hii ni JF where a spade is called by its name, a spade! Chama cha ACT hakingezinduliwa bila Zitto na hizi harakati za chama cha ACT hazingefanyika bila Zitto...Zitto ndiye nuru, Zitto ndiye mwanga na Zitto ndiye njia. Cha kujiuliza ni hizo nguvu anazipata wapi? Huo uwezo anaupata wapi? Tumeshuhudia Nape na Kinana, kwa mwaka mzima wanazurura kila pembe ya nchi hadi wamesahau makwao, ndugu zao na rafiki zao kwa sababu CCM ni kila kitu; ni bunge, ni mahakama, ni vyombo vya usalama, ni serikali na ni imani. Je ACT ni nani? Kung'oa visiki na kusafisha njia hakukuwa taabu, kupanga, kugharamia na kuratibu mikutano hakukuwa na taabu...yote ilishapata baraka kitambo. Usaliti? Ushahidi gani unatakiwa ili usaliti usijifiche ndani ya kipande cha kanga?
 
Adharusi Mkuu Mchambuzialipokujibu sikuchangia tena, majibu yamstari wa kwanza yalijitosheleza

Pili, hatujadili nani kaleta mzozo gani. Hatujui nani kafanyanini, tuna kumbu kumbu za nani kafanya nini.

Bandiko linahusu
ACT ya Zitto,kiongozi mkuu na mwanzilishi akiwa chanzo cha mgogoro kambi ya upinzani


Hatuna kumbu kumbu kama Kaborou alikuwa na mtafaruku na CDM
.

Tunakumbu kumbu alirudi CCM akiwa katibu mkuu wa CDM bila mawaa, kuzawadia nafasin.k.

Jambo la maana alilofanya Amani ni kukaa kimya akitimiza haja zake

Chacha Wangwe, hakuna ushahidi wa wahusika. Kutaja watu kwatukio zito bila ushahidi ni kutowatendea haki wahusika.

Lakini pia hatujui nani alikuwa nyuma ya pazia.

Hatukujua nani anachochea mitafaruku hadi pale, masalia walipojitokeza, Ben Saanane,Mwigamba,Kitila na waraka.

Kama unakumbu kumbu mgogoro wa Wangwe walitajwa watu nyumaya pazia, Unawakumbuka?

Swali utakalouliza , je hii migogoro iliyomhusisha ZZK inaushahidi gani ?

Jibu ni rahisi, ndiyo zipo kumbu kumbu. Waraka, Bavicha,masalia n.k.

Sijui kama unapenda tueleze ushiriki wake kama ulivyotolewaau tuishie hapa

Mwisho, kama unajua migogoro waliosababisha akina Mbowe naSlaa, weka hapa, fanyaia uchambuzi.

Hilo ndilo lengo la majadiliano.

baada ya maelezo hayo nimejua lengo ni Zitto si kinginine,maana mtindo unautumia kumchambua Zitto ulipenda ikiwezakana hasishiliki siasa za Tanzania kabisa,ili mseme si unaona tulisema akitoka CDM anakufa kisiasa.Mda mwingine mpaka mnajichanganya(kuchamba kwingi),Mara ooh angebaki ili kuleta mabadiliko,hasingeondoka,maana anataka kugawa kura,wakati mbowe hamtaki,nanyie mda mrefu mlisema hafukuzwe,eti Zitto anawapa siri usalama wa taifa na CCM, tujaribu kuwaza vizuri,hivi CHADEMA kuna siri gani,ishu ya uchaguzi haina siri maana kura zinaombwa hadharani, zinapigwa katika shule za serikali,ningeomba Mbowe atuambie hizo siri ambazo Zitto alikua anawapa usalama,tuzijue maana Mimi sioni siri katika vyama siasa,labda iwe mipango haramu.Mbowe alisema anamkanda wa Bomu la Arusha mpaka Leo hajautoa.
Nitarudi
 
Last edited by a moderator:
baada ya maelezo hayo nimejua lengo ni Zitto si kinginine,maana mtindo unautumia kumchambua Zitto ulipenda ikiwezakana hasishiliki siasa za Tanzania kabisa,ili mseme si unaona tulisema akitoka CDM anakufa kisiasa.

Mda mwingine mpaka mnajichanganya(kuchamba kwingi),Mara ooh angebaki ili kuleta mabadiliko,hasingeondoka,maana anataka kugawa kura,wakati mbowe hamtaki,nanyie mda mrefu mlisema hafukuzwe,eti Zitto anawapa siri usalama wa taifa na CCM, tujaribu kuwaza vizuri,hivi CHADEMA kuna siri gani,ishu ya uchaguzi haina siri maana kura zinaombwa hadharani, zinapigwa katika shule za serikali,ningeomba Mbowe atuambie hizo siri ambazo Zitto alikua anawapa usalama,tuzijue maana Mimi sioni siri katika vyama siasa,labda iwe mipango haramu.Mbowe alisema anamkanda wa Bomu la Arusha mpaka Leo hajautoa.
Nitarudi
Adharusi
Ningependa uwe mkweli katika yale unayoandika. Kwanza, kamatungependa Zitto asishiriki siasa, na hatuna uwezo huo, tusingemshauri mara nyingi kuhusu siasa zake.

Ni mabandiko machache tu ya nyuma tumemueleza Zittokama mtu aliyekosa busara.


Pili, kumbu kumbu zipo zikionyesha tulivyounga mkono hojazake na si yeye kama mtu.
Hilo haituzuii kusema madhaifu ya hoja zake na si yeye.

Uchambuzi hauishii katika nyimbo, ngonjera na mashairi na sebene.


Tatu, hatukuiwahi kusema akitoka CDM atakufa kisiasa. Hayo umetengeneza.

Tulichosema ni kuwa kashfa na mazonge zonge yake yanammaliza kisiasa.
Tambua kuwa kifo cha kisiasa si sudden death bali hutokea kutokana na muda

Jiulize, Zitto yule wa miaka 10 ni wa leo? Miaka 10 hakutiliwashaka, Z wa leo anachokifanya ni kuondoa mashaka makubwa yanayomkabili.

Pengineni kuvia kisiasa, je kuvia huko kutakoma au kutafikia hatua nyingine kama sikwisha kisiasa?


Nne, kwamba Z angebaki kuleta mabadiliko, hilo ni lakounless uonyeshe wapi tumesema.
Tulichokisema kuanzia mwaka 2011 katika mabandiko ni kuwa Z alikuwa tatizo na CDM walipaswa kuchukua hatua. Hawakuchukuahatua yaliyotokea ni historia


Tano, kwamba anataka kugawa kura, hatujasema hilo.
Hata hivyo wiki hii amesema ACT inachukua mkoa mzima wa Kigoma. Mbunge mmoja waKigoma kaja juu.


Kama hakuweza kuuchukua mkoa akiwa CDM, anachoweza ni kugawana kura na akina NCCR na kuwaacha CCM wakitanua.

Hilo linahitaji maono mapana, sijui kama utaelewa katika mzingo wa ‘mahaba'
Ukisimama huru katika ukweli unaweza


Sita, kwavile umeomba Mbowe aeleze siri za chama, hilo tuliache maana halituhusu hata wewe umetambua.

Adharusi, tatizo lipo wapi ikiwa akina EL, CCM , Mremaa nawengine wanajadiliwa kila uchao?

Unadhanin kuna mahali anaonewa na labda watu wapaangalie! anayetoa kauli ni nani kama si yeye mwenyewe.

Tutaonyesha kaulizake, utuonyeshe ubaya wa kuzijadili.

Coming up flip flop ya Zitto
 
Mag3;12453966]Mkuu Nguruvi3, tarehe 7/1 2015, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,kinga ya muda kutojadiliwa uanachama wake na Kamati Kuu ya Chadema! Swali ambalo wengi tulikuwa tunajiuliza ni hili, je huyu Zitto ana ajenda gani anapoomba mahakama iizuie Chadema isimjadili?

Kwa nini wenzake aliopanga nao pamoja njama za kuanzisha chama ndani ya chama waliridhika haraka haraka na hatua iliyochukuliwa na Chadema dhidi yao lakini Kiongozi wao ang'ang'anie kubaki Chadema? Kumbe...! Wale walikuwa ni watengeneza njia. Zitto alishafanya uamuzi kitambo wa kuondoka Chadema ila alitaka aondoke kwa mbwembwe ili aweze kuisababishia Chadema alichoamini ni madhara makubwa kisaikolojia. Kwake maamuzi yoyote yale ya mahakama hayangebadilisha kitu;
Mkuu Unakumbuka wakati Zitto anasema anatembea na barua ya kujiuzulu!
Baada ya muda akwa MM (mhusika mkuu), Kitila na wenzake wanaanzisha ACT wakiwa ndani ya CCM
Huu mchezo ulipangwa kitambo sana lakini wakasahau kitu kimoja; palipo na watu wanaoongozwa na mahaba, lazima pia kuwe na watu wa kuhoji kulikoni? Wenye mahaba waliwaona watu wanaohoji kama wenye chuki ingawa ukweli ambao hawataki kuuona acha kuuhoji ni hili; Zitto alikuwa na sababu gani za kuing'ang'ania Chadema? Alipoona hawezi kutimiza ndoto yake kupitia Chadema kwa nini hakubwaga tu manyanga kama Freddy Mpendazoe alipoamua kusamehe Ubunge kupitia CCM? Hapana Zitto alikuwa na ajenda kubwa zaidi na chama chake cha zamani na kama si intelijensia ya Chadema yenye vichwa kama Lissu, Mnyika, Marando n.k. utabiri wa Wassira ungetimia kupitia kwa Zitto Kabwe. Kumbe ujanja si kuwahi, ni kupata.
Mkuu, kama kawaida, wenye mahaba hawataki kusikia au kuelezwa ukweli. Wanasema sisi ni watabiri, wanajimu, vigagula.

Tulifahamu jitihada zilikuwa kutukatisha tamaa tuweke kalamu chini, waendelee na ulaghai.
Tumekataa hilo tumesimama kidete. Hakuna jambo hata moja tulilowahi kuzungumza ambalo halikutokea, halijatokea au halitatokea.

Tulikuwa mbele yao, na hiyo kazi tutaifanya.

Miaka 50 ya ulagahi inatosha, hatuwezi kwenda kustaafu na CCM tukaachia vijana matapeli wengine.
Matapeli wanaosema Marekani yao ni vijiji vya Tanzania, wanahutubia wakiwa juu ya Hummer !
Hapana, katu hatunyamazi. Wengine tumenyamaza toka kuanzishwa kwa vyama vingi, tukiweka matumaini yetu mikononi mwa walafi, wafitini na wasaliti na sasa imetosha. Hii ni JF where a spade is called by its name, a spade! Chama cha ACT hakingezinduliwa bila Zitto na hizi harakati za chama cha ACT hazingefanyika bila Zitto...Zitto ndiye nuru, Zitto ndiye mwanga na Zitto ndiye njia. Cha kujiuliza ni hizo nguvu anazipata wapi? Huo uwezo anaupata wapi? Tumeshuhudia Nape na Kinana, kwa mwaka mzima wanazurura kila pembe ya nchi hadi wamesahau makwao, ndugu zao na rafiki zao kwa sababu CCM ni kila kitu; ni bunge, ni mahakama, ni vyombo vya usalama, ni serikali na ni imani. Je ACT ni nani? Kung'oa visiki na kusafisha njia hakukuwa taabu, kupanga, kugharamia na kuratibu mikutano hakukuwa na taabu...yote ilishapata baraka kitambo. Usaliti? Ushahidi gani unatakiwa ili usaliti usijifiche ndani ya kipande cha kanga
Mkuu unakumbuka wanachama wawili maarufu hapa jamvini. Tuntemek na Hammy..
Leo mmoja wao aliyejinasibu kama CCM ndiye msemaji wa genge.

Hatuwezi kuendelea na siasa za kihuni!

Miaka 50 ya utapeli wa CCM eti tukae kimya tena tukiona machipukizi ya wahuni , walaghai yakichanua na kustawi!
Hapana tutasimama kidete kusema wahuni hawafai, magenge ya wahalifu sasa basi.

Hatuwezi kulaani mbwa mwitu, au Janjawidi kama makundi ya wahalifu, halafu wahalifu wengine tukawaita wazalendo.

Hatutaomba radhi, tutasimama katika ukweli.
 
FLIP FLOP ZA SUPREME LEADER (''KUJIKANGANYA'')-ACT

Takribani wiki mbili sasa kiongozi mkuu amekuwa ziarani na chama chake kueneza na kukitangaza

Wiki moja iliyopita zilikuwepo habari za kutoelewana kati ya mwenyekiti wa chama na kiongozi mkuu (supreme leader)
Habari hizo hazijakanushwa, muhimu zaidi, kuna habari zinazothibitisha hilo kuwa kweli. Itafafanunuliwa

Wiki zilizopita kiongozi mkuu Zitto ametuma ujumbe kwa wananchi akitaka yaliyopita si ndwele siasa ziendelee mbele
Ujumbe huo uliwakusudia hasa Chadema

Kiongozi mkuu akatoa tamko la kuwa ACT inaunga mkono jitihada za umoja wa wapinzani(UKAWA)

Habari zilizofuata ni zile za majibizano yasiyo rasmi kati ya kauli za kiongozi mkuu kuhusu mkoa wa Kigoma na wabunge

Kauli ilijibiwa na mbunge wa NCCR kwa ukali akitahadharisha kuhusu 'timbwili' linalofukuta kati ya ACT na NCCR

Siku chache zilizopita, mwenyekiti wa ACT akakaririwa na magazeti akitoa onyo kwa wanachama wa ACT kushabikia UKAWA, na kwamba atakayefanya kinyume chake atafukuzwa

Ghafla kiongozi mkuu akaja na kauli ya kubabaisha kuwa ACT inaunga mkono UKAWA kwa falsafa na si kugawana uongozi.
Supreme haukueleza kama mwenyekiti alikosea, bali alitumia lugha iliyoonyesha hakubaliani na kauli za mwenyekiti wake

Huko nyuma kiongozi mkuu aliwahi kutoa kauli kama hiyo akiwa bado mwanachama wa CDM akisubiri kesi.
Alichosema kilikuwa 'ACT ni muungano wa kugawana uongozi...''

Kauli ya kiongozi mkuu si ngeni, bali marudio ya kauli zake zinazogeuka kuwa kauli za ACT

HOJA ZETU
1. Endapo kiongozi mkuu ana uwezo wa kuuchukua mkoa wa Kigoma, vipi hilo lilishindikana akiwa CDM?

Na je, kwa kauli hiyo anawatendea ''haki' viongozi na wanachama wa NCCR mkoa wa Kigoma ambako ni sehemu muhimu ya uwakilishi walio nao bungeni? Je, ile hoja ya act kuunga mkono UKAWA ina mashiko?

2. Pili, kwa kauli ya kugeuza mkoa mzima wa Kigoma(kama ni kweli au itatokea) je hilo halifanani na Uchagga na ukanda ule ule walioupiga vita huko CDM? Je, halielezi kitu kuhusu ukanda au umkoa au vinginevyo?

3. Mwenyekiti alipotoa taarifa, alitoa maazimio ya chama. Kiongozi mkuu anapokuja kukanusha haieleweki ni kipi wanasimamia. Kibaya zaidi, mwenyekiti amesema watakaoshabikia UKAWA watafukuzwa.

Kushabikia tu bila kufanya jambo jingine mtu anapoteza uanachama.

Je, wale waliondika nyaraka (Waraka) wakiwa CDM walipaswa kuchukuliwa hatua gani, ikiwa kushabikia tu unapoteza uanachama? Kipi lilikataliwa na kipi ni halali sasa baada ya kukikataa walikotoka?

4. Je, ile kauli ya mwenyekiti haikinzani na ya kiongozi mkuu?

Ikiwa kiongozi mkuu anasema wanaunga mkono UKAWA kwa falsafa, mwenyekiti akisisitiza kutimuliwa kwa washabiki, hapa kuna uwiano gani wa kauli hizi mbili.

Endapo ACT itakubaliana na falsafa ya UKAWA, mwenyekiti hatawafukuza washabiki wa falsafa hiyo!

Ukiangalia kwa umakini, mkanganyiko wa kauli za mbele nyuma ni matokeo ya mambo mengi.

Kauli walizolaani za kibabe, kikanda, kikabila n.k. zinaonekana kuwa sehemu ya misimamo ya ACT
Kauli za mtu mmoja kuwa kauli za chama ni yale yale waliyosema ubabe na udikteta

Kuvurugana kati ya mwenyekiti na kiongozi mkuu ni matokeo ya haraka haraka ya kutenegeneza nafasi bila kuwa na mpangilio. Tunafahamu kiongozi mkuu ni nafasi iliyoundwa kwa dharura kutokana na sababu nje ya uongozi

Ni nafasi iliyoundwa si kwa kufuata kanuni, bali masharti ya nafasi kwa kiongozi anyetakiwa

Kwa mtazamo huo, hakuna shaka jahazi linakwenda kila mmoja akiwa ameshika upogo.

Timbwili halionekani kuwa 'nyumbani' sasa linavuka na imekuwa 'vita' kati ya wapinzani kwa ujumla
Mwanzoni katibu mkuu aliwaandamana CUF, Kiongozi mkuu akawaandama NCCR, huku hasimu mkubwa akiwa CDM

Kauli za mbele nyuma kwa muda mfupi hazionyeshi ACT kuwa kiungo cha mabadiliko wala kujipanga, pengine ni nyundo

CCM wapo pembeni wakitembelea wananchi wakihubiri amani na utulivu

Tusemezane
 
Nguruvi3 anatamani Act uzalendo wagawane mbao kitu ambacho naona kama dua ya Kuku kwa mwewe.
Nianze na ishu mgogoro wa ACT ulioletwa JF,nilisoma ule Uzi lengo la mleta uzi ilikua kuleta uchonganishi,ili kina Zitto wawe bize kukanusha,maana tokea kuzinduliwa ACT watu wamekua wakihoji kwamba mwenyekiti yupo geresha,pamoja na watu wengi kutoa ufafanuzi kwamba hii style ata ANC,chama cha Malema,pia Kenya ....lakini mmekuwa wahafidhina,hamtaki hii style ya kiongozi mkuu mnashindwa kuandika tu...kisa Zitto...!binafsi nilijua ule Uzi ni wa uchonganishi, eti mnahisi ni kweli sababu haujakanushwa,wakati ata akikanusha hamkubali,nani aje kujibu kila utoto unaondikwa JF
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3 anatamani @ACT uzalendo wagawane mbao kitu ambacho naona kama dua ya Kuku kwa mwewe.
Nianze na ishu mgogoro wa ACT ulioletwa JF,nilisoma ule Uzi lengo la mleta uzi ilikua kuleta uchonganishi,ili kina Zitto wawe bize kukanusha,maana tokea kuzinduliwa ACT watu wamekua wakihoji kwamba mwenyekiti yupo geresha,pamoja na watu wengi kutoa ufafanuzi kwamba hii style ata ANC,chama cha Malema,pia Kenya ....lakini mmekuwa wahafidhina,hamtaki hii style ya kiongozi mkuu mnashindwa kuandika tu...kisa Zitto...!binafsi nilijua ule Uzi ni wa uchonganishi, eti mnahisi ni kweli sababu haujakanushwa,wakati ata akikanusha hamkubali,nani aje kujibu kila utoto unaondikwa JF
Habari ya mwenyekiti kutaka wanachama wafukuzwe nayo ni uchonganishi?

Pia naomba urudi na kusoma vema bandiko letu hasa aya ya kwanza, kwa utulivu utaelewa

Hatuna sababu za kutaka chama kife, na hatuwezi kufanya hilo litokee.

Nadhani ningeandika ACT ni wazuri na wema usingeweza kuja na kauli ya 'tunataka chama kistawi''

Maneno wanaongea wenyewe, sisi tunafanyia uchambuzi. Katika wiki hii nani kaongea mwingine?

Kuna bandiko linalohusu marufuku ya kuongelea katiba kwa makundi ya dini. Hivi unataka tukae kimya tukipiga makofi tu bila tafakuri!
 
Sina maana ya kupigia makofi,ingeletwa sauti aliyosema wasishabikie Ukawa,
 
Sina maana ya kupigia makofi,ingeletwa sauti aliyosema wasishabikie Ukawa,
Ulisoma magazeti ya jana na juzi likiwemo Mwananchi? Kama tutahitaji video kwa kila jambo, mhh

Alichosema supreme ni kuwa ACT itaungana na UKAWA kwenye falsafa si nafasi za uongozi
Kabla ya hapo, mwenyekiti alisema 'ukionekana unashabikia Ukawa, unapoteza uanachama''

Hapa ndipo tunawahoji wale wanaosema suala la Waraka lilikuwa dogo la kuzumgumzika. Iweje kushangilia tu iwe kosa kubwa kuliko kuandika waraka wa matusi na mipango kem kem isiyo ya kidemokrasia?

Hoja za watetezi wa waraka ni kuwa , jambo lile lilikuwa dogo sana. Mbona tunaona madogo zaidi huku walalamikaji waking'aka na kuwa moto! real, kwamba mtu anapoteza uanachama kwa kusema Ukawa!

Una maoni gani kwa hilo suala mkuu




Coming up, supreme leader awaweka wabunge njia panda. Hawaelewi wamfuate au wabaki walipo. Hawajui adhabu ya mahakama ya wananchi itaandikwaje. Hofu imewatanda, wengi watunduwaa!!
 
Mwenyekiti asema sasa ni wakati wa
kukijenga chama kwa kusimamisha
wagombea wake wa nafasi mbalimbali
Dar es Salaam
Chama cha ACT-Wazalendo kimesema
kila mwanachama anapaswa kuwaunga
mkono wagombea watakaopitishwa na
chama hicho katika nafasi mbalimbali
katika Uchaguzi Mkuu ujao, kwani
kinyume chake ni kukisaliti na
adhabu yake ni kufukuzwa.
Mwenyekiti wa chama hicho, Anna
Mghwira alisema mwishoni mwa juma
kuwa katika kipindi hiki cha
kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, chama
hicho kinahitaji nguvu za pamoja.
“Sisi bado hatujajiunga na Ukawa,
hivyo wanachama wetu wanapaswa
kulitambua hilo na kuepuka kushiriki
kwenye ushawishi wa kufanya kampeni
za wagombea wa vyama vingine. Hata
kwenye katiba yetu tunasema sasa
tunalenga zaidi katika kujiimarisha
ili kutoa ushindani mzuri wa kisiasa
katika uchaguzi huu,” alisema.
Katiba ya ACT, imeeleza wazi kuwa
pamoja na sababu nyingine na kwa
mujibu wa kanuni zitakazotungwa na
Halmashauri Kuu, mwanachama yeyote
ambaye atasaidia kushawishi,
kujiunga, kutoa tamko la kuunga
mkono chama kingine au mgombea
wakati chama kimeweka mgombea wake
kwa mujibu wa sheria za nchi,
atakuwa amepoteza uanachama wake.!!!!!
Msome vizuri,nilichoelewa amesema sasa hatujaungana na ukawa,hivyo hawana budi kuunga mkono Act, maana ya sasa ni wakati uliopo,hivyo baadae inaweza kutokea wakaungana kwa mujibu wa ilo gazeti,nimecopy JF..na mda mrefu ili lipo kama chama hakina makubaliano maalum,sijaona kikimuunga mkono Mgombea wa chama kingine wakati wao wamesimamisha Mgombea
###############msome zitto Msimamo wa ACT Wazalendo kuhusu
Ushirikiano wa vyama
Kumekuwa na shauku ya wananchi kwa sisi
kushirikiana na vyama vingine vya siasa ili
kufanikisha malengo yetu ya kuleta mapinduzi
ya kiuchumi kwa kuubomoa mfumo ...wa
uchumi unaonyonya wananchi. Msimamo wetu
upo wazi na tumeueleza mara kadhaa
1 tunaunga mkono juhudi zozote za kushirikiana
kwa vyama na hili linathibitishwa na jina letu
ALLIANCE na Msimamo wetu kuhusu mabadiliko
ya Katiba.
2 tunataka ushirikiano utakaonufaisha wananchi
na sio ushirikiano wa kugawana nafasi za
uongozi.
3 hatuna shida na Tupo tayari kushirikiana na
chama chochote kilicho tayari kushirikiana na
sisi ikiwemo UKAWA ili kuunganisha nguvu
kuitoa CCM kwa malengo ya kujenga uchumi
shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora,
wenye mfumo wa hifadhi ya jamii kwa wananchi
wote na wenye kutokomeza umasikini.
ACT Wazalendo haijatoa kauli yeyote dhidi ya
UKAWA kama inavyoaminishwa na baadhi ya
watu. Bali tumeweka wazi kuwa lazima misingi
ya kiitikadi na kifalsafa izingatiwe katika
ushirikiano. Tupo tayari kwa UMOJA. UMOJA ni
moja ya misingi mikuu 10 ya chama Chetu na
Umoja ni nguvu.
Tupo tayari
*****************"***
Angalizo:
magazeti hayaandikii habari kwa usawa Mara nyingi inategemea umemlipa nini,yanaandika kwa kumfurahisha anaekulipa..tumeona Mara nyingi habari moja maelezo tofauti
 
Angalizo:
magazeti hayaandikii habari kwa usawa Mara nyingi inategemea umemlipa nini,yanaandika kwa kumfurahisha anaekulipa..tumeona Mara nyingi habari moja maelezo tofauti
Adharusi sasa ulichokataani kipi? Bado unahitaji video
Kwaheshima kabisa, napenda kukueleza kuwa hujatenda haki kwa wasomaji

Hapa inashambuliwa hoja hasambuliwi mtu.

Na hoja hujibiwa kwahoja. Utetezi wa ACT si kuzungumza tu bali kuzungumza kwa hoja na mantiki
 
Maudhui ya uzi huu ni kwamba Zitto na Chama Chake Cha ACT hawana nia ya dhati ya kuletea wananchi mabadiliko au mageuzi katika maisha yao kisiasa, kiuchumi na kijamii. Badala yake, Zitto na genge lake la ACT ni chama cha watibuaji wa harakati hizo. Zitto na genge lake la ACT kazi yao kubwa ni moja tu, nayo ni kukisaidia CCM kibaki madarakani. Ushahidi juu ya hili upo na umeujadiliwa kwa muda mrefu humu jamvini – kwa mfano, kauli za wenzake Zitto huko nyuma (Kitila Mkumbo na Mwigamba) kwamba lengo la ACT ni kuwa chama kikuu cha upinzani nchini (na sio kuwa chama tawala), huku wakielezea kwa ufasaha kabisa kwamba adui namba moja wa ACT ni Chadema. Hata kauli za viongozi wa sasa wa ngazi ya juu wa ACT – Mwenyekiti wa ACT taifa, Anna Mugirwa na Zitto Kabwe ambae Nguruvi3 amejitahidi kutuelezea jinsi gani kwa nafasi hii, Zitto amejitwalia madaraka ya kuwa a “Supreme Leader” wa chama cha siasa, viongozi wote hawa wawili wameonyesha wazi na kwa dhati kabisa kwamba adui yao namba moja ni upinzani uliopo sasa na sio chama tawala.

Tuanze na Zitto, hasa jinsi gani asivyokuwa mpenda mageuzi kwa dhati, jinsi gani alivyo mvurugaji na vile vile jinsi gani anatumika kama mpini wa CCM kumaliza upinzani uliopo sasa nchini. Katika mahojiano yake hivi karibuni na kituo cha televisheni cha EATV, Zitto alinukuliwa akijadili kwamba “Chama changu kitapigania kufa na kupona majimbo matatu ya uchaguzi jijini Dar-es-salaam”. ZItto akaenda mbali na kuyataja majimbo hayo kwamba ni Kawe, Ubungo na Segerea. Mpenda mabadiliko au mageuzi yeyote atakubaliana nasi kwamba moja ya kazi kubwa inayokabili vyama vya upinzani nchini ni kunyakua majimbo ya uchaguzi yaliyopo DSM na pia kwamba kufanikiwa katika hilo ni hatua muhimu sana katika kuleta mabadiliko ya kweli nchini.

Sote tunajua pia kwamba Dar-es-salaam ina majimbo mengine mengi nje ya matatu anayotaja zitto. Zitto anataja Kawe, Ubungo na Segerea lakini hasemi kwamba yapo mengine ambayo ni Ilala, Kigamboni, Temeke Kinondoni na Ukonga. Hakuna mjadala kwamba majimbo haya bado ni ngome ya Chama cha Mapinduzi, ngome ambayo upinzani unatakiwa kuivunja. Lakini muhimu zaidi ni kwamba – ni jambo lisilo na mjadala kwamba majimbo matatu anayolenga Zitto kuweka wagombea wake kutoka chama cha ACT, yani (Kawe, Kinondoni, Ubungo), hizi ni ngome za Chadema ambazo zilipiganiwa kwa juhudi kubwa na chadema pamoja na watafuta mabadiliko. Lakimi cha ajabu ni kwamba, Zitto ananukuliwa akisema kwamba “Chama changu kitafia au kitaimarika kusimamisha wagombea katika majimbo haya kwa gharama zote”.

Maswali ya kujiuliza:

1. Je, kama kweli ACT sio Mpini wa Kumaliza upinzani nchini, kwanini Zitto mchana kweupe ataje majimbo ya Kawe, Ubungo na Segerea ambayo ni ngome za Chadema lakini hasemi kwamba ACT inasimamisha wagombea kwenye majimbo mengine ya DSM ambayo ni ngome za CCM kwa maana ya Kinondoni, Temeke, Ilala, Ukonga na Kigamboni?

2. Je, kuna haja gani ya kuondoa wabunge waliopo katika Majimbo ya Ubungo, Kawe na Segerea hivi sasa?
Ubungo ni jimbo linaloshikiliwa na John Mnyika, Kawe ni Jimbo linaloshikiliwa na Halima Mdee, na Segerea ni Jimbo ambalo Chadema ilishinda uchaguzi wa 2010 lakini matokeo yakachukuliwa. Segerea ni jimbo ambalo wapiga kura wake wanasubiri kulikabidhi kwa Chadema na ushahidi juu ya hili upo wazi.

Suala lingine muhimu kujadili ni lile la Zitto na UKAWA. Ikumbukwe kwamba Zitto alitamka wazi kwamba UKAWA ni genge la wasaka madaraka na kwamba hawezi kujihusisha nalo. Tafsiri rahisi hapa ni kwamba kwa Zitto, UKAWA ilikuwa ni tishio na sio fursa. Je ni kwanini wakati katika hali ya kawaida, mtafuta mabadiliko yoyote kwake yeye UKAWA ni fursa? Inavyoelekea, upeo wa Zitto juu ya agenda ya UKAWA ilikuwa ni kwamba, UKAWA ulilenga kugawana madaraka ya kisiasa. Kwa maana hii basi, Zitto hakuwa tayari kugawana madaraka na wana UKAWA kwani ‘wangempunja alichokuwa anakitaka’. Kama tupo sahihi hadi hapa, basi nadhani tutakubaliana kwamba mtu wa aina hiyo moja kwa moja ni ‘mroho wa madaraka’. Isitoshe, ndio maana tayari tumeshaona jinsi gani Zitto alivyoamua kujitwalia madaraka ndani ya ACT kinyume na utaratibu na pia kinyume na utamaduni wa siasa za vyama, suala ambalo Nguruvi3 kalijadili kwa ufasaha. Wakati wana UKAWA wanaunganishwa na viongozi ambao ni wenyeviti wa vyama vyao, Zitto na ACT yake anakuja na upinzani mpya ambao unaongozwa na “Supreme Leader”. Hili ni doa kubwa sana kwa demokrasia yetu changa kwani katika uongozi wa kisiasa, dunia imepata uzoefu wa kutosha na ‘supreme leaders’ wa aina ya Hitler, Musolini, Stalin, North Korea, n.k. Zitto anaelekea kujiunga na orodha hiyo.

Mwisho ni muhimu tukajikumbusha kwamba huko nyuma zitto alinukuliwa mchaka kweupe akisema kwamba:
“Siwezi Kujiunga na UKAWA kwa kuwa baadhi ya viongozi wake hawataki muungano. Wamejificha nyuma ya pazia la muundo wa serikali tatu”.

Zitto akaendelea kujadili kwamba:

“Msimamo wangu siyo kuwa na marais watatu kwa sababu najua msimamo wa marais watatu utavunja nchi. Msimamo wangu ni Rais mmoja wa jamhuri ya muungano, Mkuu wa serikali ya Zanzibar na mkuu wa serikali ya Bara”
.
Ni wazi kwamba msimamo wa Zitto wa kukataa serikali tatu ni msimamo ambao unapingana na maoni ya wananchi walio wengi waliyoyatoa mbele ya tume ya jaji warioba. Msimamo wa Zitto wa kukataa Serikali tatu ndio msimamo wa CCM ambao umekwamisha mchakato wa Katiba Mpya. Msimamo wa Zitto ambao ndio ule ule wa CCM ulienda sambamba na vitisho kwamba umma ukiridhia mfumo wa serikali tatu, jeshi litapindua serikali.

Kwa kuhitimisha, mtu yeyote ambae ana nia ya dhati ya kuiondoa CCM madarakani atafanya kila linalowezekana kuzuia hujuma dhidi ya Upinzani ulipo sasa (Ukawa). Mtu wa aina hiyo atakaa mbali kabisa na majimbo ambayo yanan’gara kutokana na uwepo wa wabunge (wa upinzani), wabunge wachapa kazi na waliokuwa mstari wa mbele katika kutetea maslahi ya taifa letu linalozidi kuteketea. Mtu wa aina hii atakaa mbali kabisa na hujuma dhidi ya UKAWA kuelekea uchaguzi mkuu kwani kitendo cha Zitto na ACT kupinga UKAWA kinalenga kuleta mnyukano baina ya ACT na UKAWA ili iwe rahisi kwa CCM kupenya katikati ya vumbi hilo na kurudi madarakani baada ya uchaguzi mkuu.

Kuna kila sababu ya wananchi waelewa kumkataa zitto na genge lake.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,

Unajua mnasiitisha sana nikiwasoma maana kama vile hamjui siasa? sasa ACT imekuja kuvuruga Upinzani kivipi, chama ni wanachama na hunadi itikadi na sera zake ili wapewe nafasi ya kuongoza nchi. Ushindi unatokana na wananchi kuwakubali kwa kile mnachosimamia, iweje ACT ije kuuwa upinzani ikiwa itikadi na sera zao zinatofautiana? Je, Ushindani wa vyama ni kuvunjana au mlitaka mfumo wa chama kimoja maana siwaelewi kabisa.

Na mnaposema Upinzani mna maana gani maana kuna vyama 22, hiyo UKAWA yenyewe vyama vitatu sijui vinne waloungana, Je wao hawakuvunja Upinzani? Ni kipimo gani mnachotumia kuusema Upinzani ni huu maana vyama vyote 21 kasoro CCM ni Upinzani, iweje mchague vyama vitatu tu na kuuita Upinzani mkaviacha vyama vingine 17 vilivyokuwepo hata kabla ya ACT? vile vyama walivyoviacha nje ya UKAWA havikuwa Upinzani isipokuwa wabunge wa Chadema, CUF na NCCR..Na Mrema kwa nini walimwaga UKAWA? sababu gani na kupitia sheria zipi..Je, Hivi vyama vilivyoachwa nje wakiamua kuungana na kuunda umoja wao watakuwa wamekuja kuvunja Upinzani pia sio? ama wao itakuwa tofauti..nani alowapa ridhaa UKAWA kuwa na mamlaka ya kusema nani awe nao nani asiwe nao ikiwa wote lengo lao ni kuindoa CCM madarakani..

Nitasema moja tu ya kwamba ACT isingekuwepo kama Chadema wasingewafukuza Kitila, Mwigamba na Zitto. Hivyo maadam Chadema waliona umuhimu wa kuwafukuza wakijua fika kwamba hawa watu ni wanasiasa, kuondoka kwao wataunda chama chao lakini haitakuwa tishio kwao, basi hakuna sababu ya kulalamika leo maana Chadema walijua na walitegemea haya kutokea. Tulionya mkasema Chadema haiwategemei wao waende wanakotaka Chadema Imara, sasa uimara huo unaogopa mpini tu pasipo hata shoka lenyewe....Alaa kumbe Upinzani ni gogo la mti lilosubiri kupasuliwa bahati mbaya tawi lake limejengwa kuwa mpini!..

Unapomtalakia mkeo, tarajia ya kwamba ipo siku atakuja olewa na mume mwingine. Na haolewi ili akuvunje nguvu wewe bali amefanya maamuzi hayo kwa kutazama maisha yake mwenyewe, yeye kasonga mbele nawe songa mbele usitazame sana maisha ya mtalaka wako. Yote mnayomsema humu Zitto hayana ubaya isipokuwa yeye anaposema ndio mnachukulia -Unaona kasema hivi na vile lakini ya kina Mbowe, Mnyika na Lissu ni maneno matamu sana..
 
Nitasema moja tu ya kwamba ACT isingekuwepo kama Chadema wasingewafukuza Kitila, Mwigamba na Zitto.

ACT ilikuwepo/ilianzishwa na kina Kitila, Mwigamba & Zitto kabla hawajaondoka chadema. Kuna tofauti kubwa kati ya mke anayeachwa halafu baadaye apate mume mwingine wa kumuoa na mke anayeazisha mahusiano na mchepuko akiwa ndani ya ndoa halafu anapoachwa anaenda moja kwa moja kwa mchepuko wake kuhalalisha mahusiano yao...
 
ACT ilikuwepo/ilianzishwa na kina Kitila, Mwigamba & Zitto kabla hawajaondoka chadema. Kuna tofauti kubwa kati ya mke anayeachwa halafu baadaye apate mume mwingine wa kumuoa na mke anayeazisha mahusiano na mchepuko akiwa ndani ya ndoa halafu anapoachwa anaenda moja kwa moja kwa mchepuko wake kuhalalisha mahusiano yao...
Mwalimu huyo Mkandara ni habari nyingine. Mimi kwa kuwa sina uvumilivu na watu wa aina yake, wanafiki, nimeamua kuacha kabisa kujibu hoja zake. Mifano yake ni hiyo hiyo, kila kitu kwake ni kama ndoa, kila kitu ni mahusiano kati ya mke na mme, kila siku ni mikwaruzano ndani ya ndoa...badala ya Mkandala kujibu hoja anakimbilia mifano ya mtu na mkewe! Kwenye mjadala wa katiba alikimbilia mifano ya mke na mume, kwenye mjadala wa katiba alikimbilia mfano wa mume na wake wawili! Naanza kuamini kwamba ni kweli huyu bwana aliwahi kuwa mwanachama wa Saigon, Kariakoo! Mfano wa wazi ni huo ulioutoa; mume unagundua mkeo anaanza mahusiano na jamaa mwingine akiwa ndani ya ndoa, kwamba uvumilie tu kwani ukimfukuza ataenda kwa huyo jamaa...!

Hayo tuyaache kwa sasa...Zitto aliandaliwa, akapikwa na akapikika, na CCM ilijua na kuamini kabisa kuwa iko siku itamtumia...siku ambayo kutatokea chama kitakachohatarisha maslahi ya mafisadi waliokiteka. Mwanzoni alikuwa anauma na kupuliza na iliichukua Chadema muda mrefu kumshtukia na kuweza kujua huyu kinyonga rangi yake halisi ni ipi? Maswali aliyoyatoa Mchambuzi ni maswali ya msingi yakihusisha vyama vya upinzani jinsi pamoja na changamoto kutoka chama tawala zimejitahidi zikaipokonya CCM majimbo ndani ya Dar es Salaam City, makao makuu ya serikali. Halafu kinaanzishwa chama chenye malengo si ya kuipokonya chama tawala majimbo yaliyobaki bali kuuupokonya upinzani majimbo walioipokonya CCM.

Samahani wakuu nina muda mfupi, kama itawezekana nitarudi...
 
Last edited by a moderator:
ACT ilikuwepo/ilianzishwa na kina Kitila, Mwigamba & Zitto kabla hawajaondoka chadema. Kuna tofauti kubwa kati ya mke anayeachwa halafu baadaye apate mume mwingine wa kumuoa na mke anayeazisha mahusiano na mchepuko akiwa ndani ya ndoa halafu anapoachwa anaenda moja kwa moja kwa mchepuko wake kuhalalisha mahusiano yao...
Ningependa sanakuamini haya lakini naomba ushahid japo mdogo kuwa ACT ilianzishwa hata kabla ya hawa kutoka Chadema. Kwa sababu nachokijua na nilichokisoma mimi hawa watu walitaka mabadiliko ya Uongozi Chadema na pengine walichokifanya ACT ndicho walikitaka. Sasa Je, kweli kingewezekana! Na hata kama Zitto alitakiwa awe KIONGOZI wa Chadema kweli hilo jambo lingewezekana?. Mimi siamini katika hayo na siamini tena kwamba Zitto, Kitila, Mwigamba pamoja na kundi lao walikuwa na ushawishi wa kutosha ama wangeweza kubadilisha mfumo uliopo kwa sababu wanachama hawaufahamu na hawautaki. Leo tunashuhudia kile haswa walichokusudia na wanachama wanaipiga vita, hiyo support wangeitoa wapi?.

Mag3,
Mkuu wangu kwanza pole sana kama huwa nakukwaza na habari ya ndoa. Mimi hutumia ndoa kama mfano kwa sababu ya maamuzi yetu tu pale tunapojifikiria nafsi zetu pasipo kujua kuna roho mbili zenye uhuru na haki sawa. Ni mifano ilokaribu na maisha ya kila mtu hivyo usinielewe vibaya kabisa pengine wewe nipe neno la kutumia nitakwenda huko huko...

Isitoshe basi mambo alozungumzia Mchambuzi ni yake yeye, mimi pia nina uhuru wa kutoa mawazo yangu maana maswali yake ni ya mtazamo wake yaani anayo majibu yeye tayari kama vile mtu anakwambia 2+2 = 22. Maswali yake sikukubaliana nayo kwa kujua Upinzani kwake ni UKAWA. Ndipo nauliza huo UPINZANI ni hivi vyama vitatu peke yake kweli? ikiwa tuna vyama 21 vya Upinzani iweje leo muwape legitimacy vyama hivi tu kuwa ndio Upinzani lakini sio vinginevyo. Ukiondoa ACT vile vyama 16 vilivyobaki sio mpini wa CCM pia au ACT peke yake maana sielewi sababu ya wao kuachwa nje au nao CCM... Nani mwenye kupitisha Umoja huu kuwa ndio Upinzani wengineo sio. Kuna tatizo gani kufahamishwa hapo ili tujenge hoja za mbeleni.

Tukiweza kuelewana hapo nitakubaliana na wewe au nyie. Na swala la Katiba Mpya yale ni mawazo yangu. Usifikirie sana hiyo ndoa kama ndio inakutoa steam ni mfano tu mkuu wangu, wewe fikiria nachokisimamia na tujadiliane kwa fikra na hoja zangu dhidi ya zako na sii utake mimi nikubali kila linaloamuliwa na Chadema au UKAWA. They have chosen to take a highway, I stick with the basic, sikuingia Chadema kwa sababu ya Mbowe wala Slaa isipokuwa kile CHAMA kilichokuwa kikisimamia toka mwanzo. Kwenye serikali 3 nakubaliana na Zitto kulitaka SHIRIKISHO badala ya JUMUIYA. Siii kweli kabisa kwamba kura za maoni wananchi waliitaka JUMUIYA ukweli ni kwamba walitaka muungano wa SHIRIKISHO..
 
Back
Top Bottom