Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Hakuna ku balance, uzi ni mpini wa CCM ambao ni ACT. Mandelezo ya uzi ni kauli chafu na hatarishi dhidi ya taifa na utaifa.

Tueleweshe kwanza, kauli za Zitto zilikuwa sahihi kwa kuangalia ukweli wa takwimu na hoja?

Ni kweli kuwa Kilimanjaro na Arusha ndio chanzo cha matatizo ya Mwanza na Shinyanga?

Tunachopigania hapa ni kuondoa kizazi cha wanasiasa matapeli. Hawa akina supreme ni matapeli wanaochipukia.

Hatuwezi kukaa kimya tukiwaona wanakomaa katika utapeli.

Miaka 50 ya matapeli inatosha, sasa ni muda wa kusema, mh supreme leader siasa zako za kulitumbukiza taifa katika xenophobia unaziacha nyumbani kwako. Tanzania ni yetu sote, kuchonganisha mikoa ni jambo la hatari sana.

Ni hatari anayotengeneza supreme lazima ipingwe, ikemewe.

Hatutaweka kalamu chini hadi pale taifa na umma utakapokuwa salama!
 
Unaona sasa jinsi unavyochapia parazo ukuta, kuna mahala gani Zitto kasema Arusha na Kilimanjaro ndio chanzo cha matatizo Mikoa ya Mwanza na Shinyanga? Alichokisema Zitto anaelewa mwenyewe kama alivyosema Mbowe na mimi siwezi kuwasimamia kama niko vichwani mwao. Wewe ulotafsiri hivyo ndivyo nilivyoelewa ya Mbowe kwa mfano wako lakini mimi siona tatizo.

Pengine ungenambia zile ruzuku tunazolipwa toka migodi ya Bulyanhulu na Kahama huenda mfuko gani TRA ili tufuatilie mchango wao kwa Taifa. Unataka kuondoa kizazi cha matapeli, hivi kweli huwaoni matapeli au ndio ukishapenda huoni chongo! UKAWA ndio matapeli tena wa kutupa maana wameivuruga Chadema hadi kinaonekana chama cha kawaida kabisa na CCM wanafurahia UKAWA maana hakuna chama cha Upinzani..
 


Mchambuzi:

In one post I have asked you to provide the charactericts of Mzalendo au Uzalendo. So far you haven't done that. How do you say Zitto isn't mzalendo when there's no benchmark for that? Are you mzalendo? Is Mbowe mzalendo?
 
Zakumi sijui kama nitafanikiwa lakini naomba nijaribukueleza uzalendo kwa udogo wa akili yetu, niwieradhi endapo sitaidhi haja na makusudio.

Uzalendo ni hali, na mzalendo ni mtu anayetimiza yale yauzalendo.

Uzalendo ni unyenyekevu, kujitolea, kupigania, utii, mapenzi nauaminifu kwa nchi na taifa kwa ujumla.
Ni mtu aliye tayari kujitolea na kujitoa akipigania haki za nchi na wananchi wake


Huko nyuma tumeeleza makundi haya

1 Kundi linaloamini katika supreme leader, hili linaamini ni mzalendo kweli kweli.
Halina sababu nyingine bali kuamini tu na kwamba kumuondolea sifa hiyo ni kosa la jinai


2. Kundi hili haliamini kabisa katika supreme. Halimwamini hata kama ataahidi kuwapeleka peponi.
Linamuona supreme kama msaliti mkubwa na mlaghai. Haliamini katika uzalendo wa supreme


3. Kundi hili lina mashaka. Linaangalia definition ya uzalendo hapo juu na kujikuta lipo njia panda.
Linaangalia baadhi ya mambo ya nyuma na kumuona supreme katika ' kioo' cha uzalendo.

Linaposikia historiayake, linaposoma matendo yake na linapomsikia linajikuta njia panda na shaka kubwa sana


Kitendo cha kuchochea wananchi wafarakane ni kukosa uaminifuna utii kwa nchi.

Tendo la kufatakanisha jamii ni kukosa nia ya kulipigania umojawa taifa.


Tendo la kuzunguka washirika katika kundi, ni kukosa unyenyekevu.

Tendo la kudanganya umma ni kuwanyima haki wananchi.


Tendo la kugawa taifa nikukosa mapenzi na nchi


Ikiwa mtu ha-fit def na kwamba anaangaliwa na makundi 1-3 kwa jicho la tofauti, na ikiwa ana matendo yaliyoorodheshwa hapo juu, mtu huyo si mzalendo

Hata hivyo, kukosa hayo hapo juu hakumzuii mtu kujiita mzalendo. Mzalendo ni neno tu linaloweza kutumiwa na yoyote.
 


Mimi nilikuwa nina masuala kidogo.

1. Kwanini Chadema wanapambana au wanaona adui yao mkubwa ni Zitto?
2. Sote tunaamini kuwa wanasiasa wote ni waongo na walaghai wakubwa hususan wanapokuja kuomba ridhaa za wananchi ili wapewe uongozi. Sasa kwanini mnazijadili kauli za Zitto pekee yake wakti uongo na ulaghai huo unafanywa na kila mmoja including Dr Slaa, Salum Mwl, Mnyika na hata Mate wangu Prof Lipumba. Kwanini Zitto tu?

Mimi naamini kuwa mti wenye matunda ndio unaotupiwa mawe.

Keep it up Zitto.
 

Swali la kwanini Chadema wanapambana na Zitto, hilo siwezi kulijibu maana mie si msemaji wa Chadema.. Bali ni mpenda mageuzi na ni mwanachama wa kawaida kabisa.. Ila nafikiri viongozi wa chadema wanafanya makosa na kujibizana na Zitto maana yeye ndicho anachopenda.. Na ukiangalia si chadema "wanaochokonolewa na ZIttotu, bali hata NCCR rejea kauli yake za KIgoma na Mkosamali alivyomtolea uvivu, Cuf imechokonolewa ila wao walimu-ignore, njoo Ukawa hapa alipambana na Mtatiro kule facebook. Kwa hiyo utaona Zitto ndo mpenda chokochoko sasa inategemea na mtu na mtu kuna atayemjibu na kujaribu kuonyesha kuwa huko siko na kuna wale wanaomdharau....

Mimi kama mimi sipendi siasa za ulaghai, maana siasa za ulaghai ndo zimetufikisha hapa tulipo, zile siasa za Kigoma kuwa Dubai, au Meli katika ziwa Victoria zikome..

Na tunazikomesha kwa kuwambia wanasiasa ukweli, kuwambia kwa sasa tumechoka na siasa za kilaghai, hatuwezi kupiga hatua kama tukiwaacha wanasiasa wakaongopa mchana kweupe huku tukishangilia kwa kibwagizo cha "mbona hata Pro.Lipumba au Dr. Slaa nao ni walaghai" Ulaghai wa Slaa haumfanyi Zitto naye kuongopa, kutomwambia Slaa kuwa hapa umesema uongo hakumfanyi Zitto kutohojiwa.

Tujifunze kuhoji, tuwakosoe wanasiasa maana wao si malaika, tujenga kizazi chenye kuhoji, tuwe wajasili pale unapoona kosa tulikemea kwa nguvu zote sio kuanza na "mbona fulana.." Tukifanya hivi tutapumguza ulaghai wa kisiasa, wanasiasa hawatajiona ni miungu watu, tatawajengea watoto wetu,wajukuu zetu ujasiri ili wasiwe watawaliwa katika nchi yao kama sisi bali wapate viongozi wa kuwaongoza..

Pia Zitto ni msomi kuliko "vilaza wa Chadema" sasa huyu msomi kwanini afanye siasa kama za vilaza? nini tofauti ya msomi na kilaza Mbowe?? Tunataka kuona siasa za kisomi si siasa za kilaghai.

Kwanini tunajadili kauli za Zitto? nafikri ungerejea "kichwa cha habari" basi usingeuliza ili swali bali ungetupa pongezi pamoja na kufika pg. no.29 tumebaki kwenye hoja ya msingi ambayo ni ..
 

Nasikitika pamoja na maelezo yako marefu na mazuri lakini hakunijibu maswali yangu.. Nimeulza hivi huu unafiki na ulaghai kwa faida ya nani? na ili iweje? na ni kwanini hiki chama kinajengwa katika misingi ya ulaghai na unafiki? kweli kuna matumaini ya kuleta ukombozi kwa chama kinachojengwa kwa misingi hii?

Mambo ya Ukawa sijui hawaongelei kuhusu Uchumi ni lini na wapi ulihudhuria mkutano wa Ukawa? na katika mkutano huo walizungumzia nini?
 
Mchambuzi:

In one post I have asked you to provide the charactericts of Mzalendo au Uzalendo. So far you haven't done that. How do you say Zitto isn't mzalendo when there's no benchmark for that? Are you mzalendo? Is Mbowe mzalendo?

Zakumi, kama ni kukwepa maswali, wewe na wenzako mmekwepa mengi tu.

Kuhusu uzalendo, Nguruvi3 kajadili vyema sana. Mimi narudi pale pale katika Zitto na Ujamaa. Kwa kauli zake, mzalendo ni mwananchi ambae anaitetea nchi yake ya Tanzania kwa misingi ya ujamaa, kwani kwa mujibu wa zitto, hiyo ndio njia pekee ya kuwatetea wanyonge na rasilimali zao kama taifa, bila unafiki, bila kuyumba, bila ulaghai. Nahoji tena:

Upo wapi ujamaa wa zitto?
 
Unafiki na ulaghai wa nani maana miye wanasiasa wote ni wanafiki na walaghai kwa sababu ni wasaka tonge tu. Mishahara mikubwa kama millioni 11 kwa kila mbunge, ruzuku za chama na guarantee ya maisha bora na Uheshimiwa ndio unaotuponza sisi sote maana huwezi linganisa mishahara yao na kazi walizofanya. Iwe kuandika sheria, Kuisimamia serikali au kupitisha bajeti yaani wapo wapo tu kubishana basi inapita kama ulivyo andikwa muswada. Mfumo mzima wa kisiasa nchini ni CHUKUA CHAKO MAPEMA haijalishi wewe CCM au Chadema ni mfumo mbovu unaotokana na marekebisho ya sheria ya katiba 1993 yalojenga kundi la WAHESHIMIWA.

Sasa basi niwaulize wana Chadema kwa nini wanamwita Zitto mnafiki, ilihali ishara za mnafiki ni mtu Muongo kamwe hasemi ukweli, ni mtu asiyeaminika kigeugeu, akiahidi kitu hatimizi.. Na haya yote tunayaona katika wanasiasa sio Zitto peke yake bali WOTE maana mfumo wenyewe wa utawala ni wa Kinafiki. Huwezi kunambia Mbunge ndiye hupeleka Maendeleo kwa wananchi lakini utawasikia wakiahidi hayo, wakati wanajua fika hawawezi. Mnyika yule pale hadi kesho anaomba wananchi wa Ubungo wapelekewe maji na hawajapata kwa sababu ya muundo wa Winner takes all na mpini kaushika CCM sio Chadema.

Na kipimo cha Uzalendo kwangu mimi nilikipata pale Katiba Mpya haikupatikana, aidha kwa walotoka nje au CCM wote hawa wametumia UCHAMA na sio uzalendo wao kuandika ama kugomea Katiba. Haiwezekani leo vyama vijiandae kugombea Uongozi ndani ya katiba ile ile tuloikataa toka mwaka 2005 leo wajiite Wazalendo kwa Uzalendo gani ikiwa wananchi hawakupewa Katiba yao halafu wanakimbilia Uchaguzi kutaka katiba ifanyiwe marekebisho katika mambo yanayowahusu wao tu ili uchaguzi huu uwe Huru kwao.

Just Imagine how shallow hawa jamaa walivyo, yaani toka katiba pendekezwa imetoka ni miezi 4, wasigombanie kubadilisha japo moja la wananchi isipokuwa jambo linalowahusu wao ili uchaguzi huu uwape japo mwanya wa kushinda. Wananchi wanataka Wabunge wasiwe Mawaziri, Mbunge lazima awe mkazi wa sehemu anayogombea, RC na DC wachaguliwe na wananchi kwa sababu hawa ndio kiini cha fedha za serikali ktk maendeleo ya mikoa na wilaya. Yote haya tutapuyanga nayo kwa miaka mingine mitano kwa sababu hayawahusu wao leo wala kesho.

wao wanataka nini? NEC iwe huru, TISS iwe huru, sijui sheria na vipengele vinavyowanyima haki wao ya kufanya mikutano na maandamano huku leo hii serikali imeweka saini kuweka sheria kali ya Cybercrime dhidi ya wananchi, sijamsikia mwanasiasa yeyote kati yao akipinga kuhalalishwa kwa sheria hiyo japo ilipitishwa na kundi dogo sana la wabunge (Akidi haikutimia). Haya ndio mambo ya wananchi lakini wameshindwa kuona umuhimu wake, Wananchi kwa ujumla hawaitaki sheria hii na walitaka irudishwe bungeni lakini hao UKAWA wako wapi?...hatuwaoni kwa sababu wapo katika harakati za kutafuta millioni 11 kwa mwezi..
 
Mchambuzi,

  • mzalendo ni mwananchi ambae anaitetea nchi yake ya Tanzania kwa misingi ya ujamaa, kwani kwa mujibu wa zitto, hiyo ndio njia pekee ya kuwatetea wanyonge na rasilimali zao kama taifa​



Mkuu labda tufahamishe wewe Zitto ana mapungufu gani katika sifa hizo maana mimi sioni mwenye kuitetea NCHI zaidi yake wengi wanatetea vyama vyao wala sio sera zinazojenga Itikadi yao.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu labda tufahamishe wewe Zitto ana mapungufu gani katika sifa hizo maana mimi sioni mwenye kuitetea NCHI zaidi yake wengi wanatetea vyama vyao wala sio sera zinazojenga Itikadi yao.
Niliwahi kukuuliza haya yafuatayo, hukuwa na jibu. Mkandara ukweli kuwa huwezi kusimama na kutetea hoja zinazomkabili Zitto bila kutaja watu wengine unaeleza wazi kiwango cha juu cha unafiki na ulaghai wa supreme leader. Kwamba hata wewe huwezi kusimama bila nguzo katika kumtetea

Tunafahamu viongozi wengi wanafiki, kinachotutisha ni kuhusu unafiki wa Zitto ambao sasa unaelekea kulivuruga taifa.
Miaka mingi ameachwa na sasa anafikia kiwango cha siasa za hatari sana nchini

Tumekuuliza ilikuwa sahihi kwa Zitto kusema Shinyanga/Mwanza wanapata kidogo wanachangia sana na Kilimanjaro/Arusha wanachangia kidogo wanakomba sana? Majibu unayotupa ni kuwa Mbowe kasema abcd!!!

Hata wewe na nafasi yako unaelewa wazi Zitto amefikia mahali pabaya sana.

Anapoanza siasa za kuchonganisha wananchi wa kanda moja dhidi ya nyingine, ni siasa muflisi za hatari na mtu huyo ni wa kuangalia. Zitto alipaswa kujua madhara ya kuchonganisha watu kuliko mtu mwingine. Si katoka Kigoma? Kwani hakuyaona na hadi sasa haoni madhara yake. Leo anaelekeza sumu hiyo kwenye mikoa mnataka tukae kimya! ebo

Mkuu Jenga hoja, tetea hoja, hapa hakuna cha UKAWA au nini, kilichopo mbele yetu ni ACT na jinsi ilivyo mpini wa kumaliza upinzani na sasa hivi kuvuruga nchi. Mwenye kauli ni Zitto na ndiye anawajibishwa kwa kauli zake.


Muda wa ulaghai na unafiki sasa basi. Hatuwezi kuwa na walaghai miaka 50 tukaendelea kulea makinda!
 
Mkuu wewe ndiye unazunguka zunguka huku na kule ukirudia maswali yale yale hata kama nimesha kupa jibu kwa sababu unataka jibu unalolipenda wewe. na nimekwambia sii mara moja wala mbili ya kwamba huwezi kumuuliza mtu swali wakati wewe ukiwa na majibu yako. Hii sio 2+2=4, ni hoja zako juu ya jambo/kitendo wala sii mtu fulani na chukua jibu la jambo/kitendo sio mtu fulani. Hukuridhika litoe makosa pale umeona hakuna ukweli maana pengine wewe unajua zaidi kiichopo kichwani mwa Zitto.

Mimi siwezi kumjibia maswali ya kwa nini Zitto alitoka nje wakati najua Zitto ana akili zake, najua alifukuzwa Chadema, yeye akisema bado yupo Chadema na Chadema nasema hakuwa mjumbe wao. Hapa kuna majibu matatu tofauti na kila moja linatoka akilini mwa mhusika. Kilichokuwa kichwani mwake siwezi kukielewa wala wewe huwezi ndio maana unauliza maswali kama vile mimi ndiye Zitto na unataka majibu kama unavyofikiria wewe uliye kuwa kichwani mwa Zitto. Nachoweza tu kusema ni kile nachokiona toka nje kama mshiriki wa mjadala huu na sio Zitto au alichokuwa akifikiria.

Na ndio maana nikasema chochote atakachofanya Zitto hakiwezi kupokelewa vizuri kwa sababu yeye ni adui wa Chadema toka afukuzwe. Japo UKAWA imeunda baada ya kutoka nje ya bunge na kupanga safu ya viongozi wake hivyo walipokuwa bungeni kila mtu alitakiwa kuchagia kama mtu Binafsi lakini haikuwa na haikutakiwa hivyo na vyama. Leo UKAWA imekuwa ni wajumbe wa bunge la katiba upande usokubaliana na CCM kama vile UKAWA ilikuwa mshirika wa bunge la katiba na sio baada ya kutoka nje. Ni maajabu makubwa haya mnavyoweza kutunga ulaghai..

Zitto alotoka nje wakati wa kuapishwa Kikwete alliitwa Mnafiki kwa kubakia ndani akieleza msimamo wake na Zitto alotoka nje na wengine kaitwa tena Mnafiki kwa sababu katoka nje kufuatia agizo la viongozi wake walitaka Upinzani wote watoke nje. Kutokubaliana tu na wazo hilo anaitwa tena Mnafiki. Wale walobakia wakaitwa wanafiki na huyu alotoka mnafiki pia.
Inakuja swali Ma Supreme ni kina nani hapa!
 
Mkandara unaposema jambo inabidi uwe na uhakika nalo au ushahidi nalo. Ukimtetea supreme kwa kauli yake ya umasikini wa kanda fulani, basi tueleze utetezi huo unaegemea wapi? Hatutaki utupe majibu tunayotaka, tunataka ufafanue utetezi wako unasimamia wapi

Sisi wengine tunasema, alichosema si sahihi, ni makosa makubwa, uchonganishi na ulaghai.

Tunasimama hapo kwa takwimu na hoja. Zimewekwa takwimu za kuonyesha ni mlaghai, hakuna takwimu za kuonyesha alisema maneno hayo kwa data zipi. Kama zipo takwimu za supreme kuonyesha jinsi uporaji unavyofanywa na kanda moja dhidi ya nyingine basi uwekwe hapa

Pili, tuweke rekodi clear

1. Msimamo wa upinzani ulikuwa kupinga kuvurugwa kwa uchaguzi mkuu.

Zitto akaamua kukaa ndani na mwisho wa siku akapewa 'trip' Sudan na Mzee kama sehemu ya ku appreciate uwepo wake bungeni. That's ok

2. Katika bunge la katiba, supreme alipotoka hakukuwa na maneno.
Na angebaki kusingekuwa na maneno kama ilivyo kwa Mrema, Cheyo na Kuga

Tatizo linaanzia hapa
a. Yeye alikuwa muumini wa mfumo uliopingwa na CCM wa S3. Angebaki ndani angakuwa anatetea nini?

b. Alipotoka na kusema Ukawa wamefanya makosa kutoka, nini kilimtoa na makosa gani aliyaona na kwanini hakuyasema

c. Alipotoka na kusema UKAWA ni wasaka tonge, kumbe basi alitoka na wasaka tonge ili iweje

d. Alipotoka na kusema anataka kuungana na UKAWA, alaa! iweje aungane na wasaka tonge?

Ukiangalia mambo hayo hapo juu, utaona jinsi asivyoeleweka, alivyo kigeuge, mnafiki na mlaghai
 
Mkuu nimeandika mara ngapi juu ya hilo ili uelewe nnilichokielewa mimi.

1. Haya umeruka na kuja ta trip na Uchaguzi mkuu mbona kuna wabunge wengi wa Chadema kasafiri nao JK katika misafara yake. Kwa nini wewe mna m single out Zitto? Au unataka tuanze kuwataja walosafiri na JK nchi za nje katika misafara yake na tujenge sababu.

2. Kama unadai hakukuwa na maneno sasa hya unayoyasema wewe yametoka wapi? nimekwambia sababu katoka kwa sababu viongozi wake walitaka atoke japo yeye hakuafiki. Kilichomponza kni ile haki yake ya kusema mtazamo wake. Nadhani unakumbuka mimi nilisema mapema kabla yake kuwa Upinzani wamefanya kosa kubwa sana kwa sababu CCM walitaka watoke ili wasipate ushindani katika maswala muhimu ya wananchi. Utafikiri alinisoma na kusema kweli lilikuwa kosa kususia uandikaji wa Katiba Mpya.

a-b) Sawa unavyofikiri wewe lakini mimi nimekupa mtazamo wangu ya kwamba alifuata wengine kujenga umoja wa walosusia maana hakukubaliana na serikali 2 wala 3 za Jumuiya. Na elewa kuna wajumbe mle walobakia walotaka serikali 3 za Warioba hawakupata sauti. Je, hawa walotoka walijua hawataweza kushinda ktk upigaji kura ndio maana wakatoka? tazama matokeo ya Ushindi CCM walifikia exactly akidi ina maana Upinzani wangekuwepo pamoja na wale walopiga kura against CCM na ushawishi zaidi wangefikia ushindi.

c-d) Hili la wasaka Tonge, labda nikupe mfano unaokuhusu, Unaweza wewe kutokubali kuoana na mwanamke Mkatoliki kwa sababu ya UKATOLIKI lakini ukamwambia kama kweli unaitaka ndoa basi badilisha shehebu uwe Lutheri kwa maana ya kwamba unaimani na Ulutheri tu. sasa iwe wewe kusimamia Ulutheri ni U Supreme wakati unashindwa kumtazama mke ambaye anadai pia uende kanisa la Kikatoliki naye ni Supreme nitashindwa kukujibu. maana wewe unatazama upande mmoja wa kichwa cha shilingi, penye picha ya mheshimiwa na kutaja jina lake, hali mimi natazama pande zote kukupa thamani ya shilingi.

Kwa maana hiyo basi ndio nikasema Zitto ni MJAMAA na Chadema ni WAHAFIDHINA inakuwa vigumu watu hawa kuelewana kisiasa watakuwa na migongano mara kwa mara bora Zitto kajitoa na kuunda chama chake kwa imani yake kuliko kuendelea na mahusiano na watu ambao hawana itikadi ya pamoja. Ndivyo nilivyolitazama swala hili.

Na nakushangaa kila mara unapenda nijibu maswala ya ACT wakati mimi sio kiongozi wala mwanachama isipokuwa nimesema mimi ni MJAMAA na ningependa sana UJAMAA urudi kwa sababu Ubepari katika nchi Tajiri na watu maskini huleta vurugu za kupigania mali kama sinia la Pilau katika maulidi. Bado Watanzania hatujafikia ustaarabu wa kula kwa kisu na uma kutokana na umaskini wetu na ndio maana kila mtu anataka kutoka kwanza. hapa sizungumzii Chadema wala ACT bali mtazamo wangu wa kiitikadi unaweza jenga haki na hata kuwaletea maendeleo kwa wananchi.

Wewe fikiria huko vijijini, waanzie kula kwa kisu na uma utawatesa tu, watavitupilia mbali na kuanza kula kwa mkono wakinyang'anyana nyama na pilau na sii kwa sababu nyingine isipokuwa kila mtu anataka kushiba haraka hata kama chakula kipo kingi cha kuwatosha wote, matokeo yake wapo watakao ondoka na njaa. na ndivyo navyoitazama tanzania nzima kwa Umaskini wetu huwezi kutumia Ubepari ambao una ustaarabu wake nasi hatuna mila wala desturi za ustaarabu huo. Tutakuwa tunaiga tu Ubepari wakati njaa zinatumaliza.
 

Nashukuru kwa kukiri ya kuwa Zitto ni mnafiki na mlaghai...

kuhusu hayo mengine uliyoyaandika kuna ukweli ndani mwake ingawaje sielewi ni vipi vyama vya upinzani vinaweza kubadilisha sheria bungeni.. Hapa nanihitaji shule lakini si katika uzi huu maana tunaweza kuvuruga uzi wa Nguruvi3.

Kuhusu Cybercrime naona kama unapenda kuwaonea tu wapinzani..Kwa kumbukumbu zangu Lissu na Mdee walipigia kelele saaaaaaaaaaaana mbunge na Dr. Slaa alishalizungumzia tena sana tu ila kama unavyojua hawa watu hawawezi kufanya zaidi ya hicho walichofanya na sababu unazifahamu. (ila wakati wingine Mkuu Mkandara huwa unaandika vitu kama huko katika dunia yako tu, yaani unawatupia lawama wabunge wa upinzani as if hujui sheria zetu ni kuwa wengi wape)

Kuhusu Uzalendo ndo maana wengine tunahoji iweje mtu ajiite mzalendo na hatuimize watu tuwe wazelando wakati yeye kila mwisho wa mwezi anapokea mil 11, anakataa elf 80 za posho lakini anapokea mil.200 za mkopo(kama hii mikopo unarudishwa mimi na wewe hatujui), miaka 5 ya ubunge kiinua mgogo ni mil.200,mil.90 za nini sijui, vikao vya PAC alikuwa anapokea kati ya laki 5 na 1mil.ana mahekta ya mashamba hali kuna wakulima hawana maeneo ya kulima, ana vitalu vya Gas wakati wananchi wa Mtwara wananyanyasika na Gas, mtoto wake huyu International school wakati wakwangu yuko St. Kayumba hatuna hata chaki achilia mbali walimu, anaendesha Hammer wakati hakuna hata gari la kubebea wagonjwa hospitalini tena katika jimbo lake.

Huyu mtu anatuhimiza tena kwa nguvu zake zote, akili zake zote na kwa uchungu kabisa tuwe wazalendo. Swali kwako hivi kweli kuna uzalendo hapo?

Naelewa uzalendo si umasikini lakini kipato chako kiendane na watu unaowahimiza kuwa wazalendo..
 
Kwanza tukubaliane kuwa Bunge ndilo hutunga sheria, hawa viongozi wa UKAWA wote walikuwa wapi?.. na wakati muswada huu unapelekwa IKULU kusainiwa iwe sheria walikaa pembeni wakitazama picha inavyokwenda tena basi tunaambiwa walopitisha muswada huo bungeni hawakufika hata 60 ina maana Adiki haikutimia na wabunge wengi hawakushiri. Hata kama muswada ulipelekwa kama swala la tahadhari na haraka UKAWA walitakiwa kwenda baada ya kujua ni mambo gani na yatakuwa na athari gani kwa wananchi. wamewaachia kina Maria sarungi ndio wamebeba mzigo wa kazi ya wabunge mitandaoni..Kama UKAWA sio Wanafiki kuna lipi ziada.

Swala la Uzalendo halitokani na mtu kukataa hata mshahara, Mishahara yao hupangwa na hupitishwa na wabunge wote hata kama yeye hakubaliani. Dr.Slaa alikuwa mtu wa kwanza kupinga mshahara mkubwa wa wabunge lakini mbona alipokea wakati akiwa bungeni. Kinachohesabika bungeni ni msimamo wako katika kila hoja na muswada hata kama umeshindwa kwa kura na wakashinda wengine. Hivyo record itaonyesha wazi kwamba Chadema akiwemo Zitto walipinga mishahara mikubwa lakini wakashindwa katika kura, kina Shibuda wa CDM kuunga mkono upande wa pili.

Hivyo kwa kila jambo ambalo Zitto amelipinga bungeni linampa record yeye na wale wote walopiga kura against na nakumbuka swala la Posho Chadema pia walipinga lakini wakashindwa katika kura. Hivyo CDM wanachukua kwa sababu ya utaratibu uliopo Bungeni - Wa wengi wape, hivyo unalazimika kukubali ya wengi na sio kususia. Ukisusia ni utovu wa taratibu za bunge na una gharama zake. Zitto kasusia Posho kama ilivyo mbinu ya UKAWA na kususia Katiba Mpya ila uwe tayari kukubali madhara yake. Zitto amekubali kuikosa Posho na UKAWA lazima wakubali kuikosa Katiba Mpya.

Swala la Mikopo, kusema kweli hapa unakwenda nje kabisa maaa katika nchi za Kibepari Mikopo ndio chanzo cha fedha za ujenzi wa maisha ya kila mtu. katika nchi ya Kibepari kila mtu hukopeshwa iwe rais au Billgates maana usidhani Bill gates anatumia frdha yake laa anakopeshwa kwa kila anachowekeza na kulipa Interest lakini maadam anazalisha zaidi hulipa dei lake kirahisi sana na billioni alizowekeza zinaua interest kubwa kwa kupewa interest yeye.

Swala la vitalu, nadhani nilimsoma mahala akizungumzia hilo kama ameunda shirika la Maendeleo jimboni kwake kukuza kilimo na hivyo unachosoma magazetini ni kuwa hilo shirika ni mali ya Zitto kwa sababu ametumia mtaji wake kuunda shirika hilo ambalo linawawezesha wananchi kulima, kuvuna na kuuza mazao yao. Hata mimi hapa nikifungua Biashara Bongo itasomeka ya Mkandara lakini wanaofaidika na bishara hiyo ni ndugu zangu na ifahamike tu kwamba Biashara inakuwa na jina lake hivyo inakuwa inajisimamia kama Legal Entity. Mwanzilishi hana sauti zaidi ya Board iliyopo na kwa Zitto hiyo board ya shirika la Maendeleo ndio wenye maamuzi nadhani hata Makamba anayo yake Bumbuli.
 
 

What are the characteristics of Ujamaa or Mjamaa? And what disqualifies Zitto from being one? If he isn't mjamaa, what is he? Kupe? Bepari?

The way I see it is since the guy left CDM, some people have engaged in the character assassination. They think that the only way the opposition will stay stronger is by discrediting him. And they aren’t afraid to use any tactics in the book to undermine him. What is this? Is the country sliding back to the authoritarian regime of the single party system?

Voters have shorter memories. But it seems to me that CDM and its supporters want to be remembered for what they did 5 years ago. They want to show up with the same team and them same configuration and expect results. This has become a narrative and it upsets them when one within their ranks wants to alter it. The truth of the matter is the 2015 general election will constitute new dynamics that weren’t factored in 2010.
 
 
Mkuu Mkandara 'jeuri na ujasiri' wa kukacha posho ndicho chanzo cha neno unafiki

1. Alikwenda mahakamani kulinda Ubunge wa BMLK. Kuna jeuri gani hapo?
Walipotoka nje akasema wamefanya kosa, kumbe kosa ni kwenda kinyume na lengo la kubaki BMLK. Mkuu huoni unafiki hapo?

Siku za mwanzo za BMLK alichukua tu kama wabunge wengine kwa kukaa. Ndani ya Bunge la JMT anasema hawezi kulipwa kwa kukaa. Mkuu mbona kuna doubel std? Au tunaona vitu tofauti

2. Kuna yale ya TANAPA, hakuna ufafanuzi hadi sasa. Kuna jeuri gani hapo

3. Kuna yale ya kukodi ndege, hayajafafanuliwa hadi sasa, kuna jeuri gani hapo

4. Je,aliwahi kukataa posho za PAC? Tunajua kazi za PAC ni sehemu ya kazi za bunge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…