Kuweka kumbukumbu sawa NCCR Mageuzi hawakupata viti hivyo 19.
Uchaguzi wa kwanza katika mfumo wa vyama vingi 1995, Chama tawala cha CCM kilipata viti 186, CUF viti 24, NCCR MAGEUZI viti 16, CHADEMA viti 3, UDP viti 3 na TLP kiti 1.
Hata hueleweki, sijui una haraka gani. Kabla hujabonyeza "submit button" soma uliyoandika, fanya marekebisho kama kuna sehemu umekosea ndipo submit. Mnatupa taabu kwa kuandika kama vile mnakimbizwa!Huko sahihi Mbunge wa kwanza kukaa upande wa upinzani baada ya vyama vingi kuruhusiwa ni Kaburu, mwaka 1994 Alinda amelisishwa ubishi na wenzake,maana ukisoma maelezo yake,anataja wabunge wa upinzani wa Arusha,Kilimanjaro,ila kwa kigoma hajataka kujishughulisha,wakati hizo amegoogle,kwanini hasigoogle na kigoma,nilichogundua,baada ya kutuvutiwa na Zitto,sasa hivi wanaichukia hata na historia ya upinzani kutoa mbunge wa upinzani kutoka kigoma,wanatamani angetoka mikoani kwao huko,huzi ulishapotea njia huu,tokea Zitto alipo amia ACT
Hivi mtu asimame na kusema mikoa fulani ina maendeleo, hata hivyo mikoa inayochangia abcd inapata zaidi. Hakuna ushahidi, tumeomba hapa jamvini hakuna aliyeleta
Takwimu zote zinakataa, hesababu za darasani, kijiograifia n.k. zinakataa
Leo utuambie kauli hiyo ni 'lip stick...''
Tatu, hivi unataka tukae kimya huyu kijana akilimega taifa eti tu move on! nani atakemea!
Nne, kauli zinatoka kwa nani, sisi au yeye? Kwani hukumbuki mshauri wake Kitila alisema nini na mlezi wake Baregu alisema nini.
Tano, huyu mtu anayetaka uongozi wa taifa huku nyuma akimega mega taifa anatufaa kwa mtazamo wako?
Kapwela uchaguzi wa kwanza kabisa kufanyika baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi na upinzani kushinda ulikuwa ni wa serikali za mitaa mwaka 1994. Aliyeshinda uchaguzi huo na kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa kijiji kupitia chama cha Chadema aliitwa Simon Kibola aliyeshinda na kuwa Mwenyekiti wa Kijiji kinachoitwa Gongali huko Karatu.
Chama cha Mapinduzi hakikuamini kwamba kingeweza kushindwa na hivyo uchaguzi kurudiwa mara nne chini ya usimamizi wa defenda za polisi kutoka Arusha. Ilibidi uchaguzi wa wazi ufanyike baada ya wana Karatu kukomaa na kumkataa kabisa mgombea wa CCM.
Kwa kumbukumbu Dr. Slaa mwaka 1995 alichaguliwa kuwa mbunge pia kupitia Chadema alikohamia baada ya chama chake cha CCM kumletea mizengwe. Katika uchaguzi huo wabunge machachari Masumbuko Lamwai na Mabere Marando walichaguliwa kupitia chama cha NCCR Mageuzi.
Sijui hii ya Kabourou kuchaguliwa mwaka 1994 unaipata wapi lakini ni wazi watu wa Karatu ndio wanaweza kupewa sifa kwa kuvunja mwiko wa CCM kushindwa kwenye uchaguzi wowote ule. Sasa na wewe naomba uje hapa na facts jinsi wana Kigoma walivyopigwa virungu kwa kuunga mkono mageuzi.
Katika wabunge waliochaguliwa mwaka 1995 kutoka Upinzani, wengi kwa ulafi walirudi CCM isipokuwa wanamageuzi wa kweli ambao walikataa vishawishi vya CCM na hadi leo tunao wakiongoza Upinzani katika nyadhifa mbali mbali.
Katika wabunge waliochaguliwa mwaka 1995 kutoka Upinzani, wengi kwa ulafi walirudi CCM isipokuwa wanamageuzi wa kweli ambao walikataa vishawishi vya CCM na hadi leo tunao wakiongoza Upinzani katika nyadhifa mbali mbali.
Na mwaka 1993 wakati Zitto anajiunga na Chadema alikuwa kidato cha tatu Dr.Slaa alikuwa anawakumbatia watawala "CCM" Tundu Lissu huko Singida sijui alikuwa wapi.
Na mwaka 1993 wakati Zitto anajiunga na Chadema alikuwa kidato cha tatu Dr.Slaa alikuwa anawakumbatia watawala "CCM" Tundu Lissu huko Singida sijui alikuwa wapi.
Mkuu Kapwela , maendeleo si robota la mitumba unaloweza kugawa nchi nzima baloi ni matokeo ya vitu vingi ikiwemo fursa na jitihada.Hilo la mgawanyo wa mapato sina cha ziada maana mshakuwa na mjadala mrefu sana hapa, sina lolote la tofauti.
Ila langu ni dogo tu, tunaweza kuwa na mawazo tofauti lakini sote tuna lengo moja mahsusi, kujenga taifa moja,la watu wamoja, taifa la Watanzania, lenye maendeleo kwenye pande zote za nchi hii.Sina shaka ata kidogo na Zitto juu ya hili, alichosema ni haja ya kusukuma maendeleo PIA kwenye maeneo yaliyo nyuma.
Tatizo ni kuwa baadhi yetu wamekuwa sensitive zaidi na eneo lao/kabila lao, hii ni ishara ya wazi kuwa kuna wengi wetu ambao tu wa eneo letu zaidi kuliko tulivyo Watanzania, kama tungelikuwa ni Watanzania Kwanza basi Tabora ni kwetu kama kulivyo Arusha na kama kulivyo Mtwara, hivyo tatizo la Mtwara linanihusu sana kama linavyonihusu sana la Kagera. Kushindwa kujitafsiri hivyo ndipo lilipo tatizo letu.NI sisi wenye tatizo.Tutoke hapa!!
Kwa kuwa nchi yetu ina central government iliyo na nguvu, ndio yenye almost kila kitu, kwa mfumo huu lazima tuwe na namna ya kusambaza maendeleo pande zote.Jinsi gani?lazima tutatofautiana hapa na pale, lakini tuheshimu mawazo ya wenzetu na kama unaona una wazo bora zaidi unaweza shauri lakini sio kubatizana ubaguzi sehemu ambayo haupo, bila kujijua ni sie tunaochochea hizo hisia na matokeo yake tunasambaza ubaguzi huo.Tuache!!
Nimepotosha nini?Acha kupotosha wewe,
Nimepotosha nini?
Hata hueleweki, sijui una haraka gani. Kabla hujabonyeza "submit button" soma uliyoandika, fanya marekebisho kama kuna sehemu umekosea ndipo submit. Mnatupa taabu kwa kuandika kama vile mnakimbizwa!
SAMAHANI kwa uandishi,wewe na wote,mlioshindwa kuelewa,maana yangu ni kuwa KABURU alishinda uchaguzi Mdogo mwaka 1994,kumbuka uchaguzi MKUU ulikua mwaka 1995,Sasa inawezekanaje historia ianzie 1995 wakati kuna mbunge kashinda uchaguzi Mdogo 1994 na kuingia bungeni kama mbunge wa upinzani kupitia upinzani(CDM),Naamini huyu angetokea KATIKA mikoa mnayoipenda msingebishia,sababu anatokea mkoa anaotoka Zitto imekua tatizo
Wewe kazi yako kufuata mkumbo tu msikilize Zitto mwenyewe kwenye hiyo video aliyoleta Alinda.
Mkuu Kapwela , maendeleo si robota la mitumba unaloweza kugawa nchi nzima baloi ni matokeo ya vitu vingi ikiwemo fursa na jitihada.
Maendeleo hayapelekwi,yana hamasishwa.
Pili, sehemu zenye maendeleo si kwasababu zilipewa. Ni kutokana na mazingira mbali mbali, tumejadili .
Mazingira yametengeneza fursa,iliyokutana na jitihada. Unaunga mkono hoja ya maeneo fulani kupewa zaidi, na kwamba ni wakati wa kugawa sawa kama anavyosema Zitto.
Hiyo ndiyo inaamsha hisia,. Huwezi kuwalaumu wananchi wa Kilimanajaro au Arusha kwa mafanikio yao.
Hilo hatukubaliani, halina mantiki,ukweli , akili au mashiko. Ni cheap politics, tunazilaani
Kama unakubali central gov ina nguvu, wapi hoja ya kusambaza maendeleo sehemu zote inatoka? Unachosema, central gov imegawanya kiupande upande.
Endapo ni hivyo, nani wa kulaumiwa? Kwanini wananchi wakaskazini wabebeshwe zigo lisilowahusu?
Kwani wananchi wa kaskazini ndiyo central gov?
Haya ndiyomawazo yanayopigwa vita hapa, hatari Zitto aliyofanikiwa kupanda vichwani mwa watu.
Hatutetei ukabila tunalaani wale wanaotumia umaarufu wao kuchochea ukabila na ukanda.
Zitto hakwepi mkono kwa hili.
Tumkemee sote kwa kujenga Tanzania yetu, si Ujiji au Isevya,Kadewele au Kicheba.
Ni Tanzania yetu sote
Tusemezane
Sipo hapo kukulizamisha wewe kuamini ninachoandika nipo hapa kuwafahamisha wale wote wanaofuatilia huu mnakasha.Siwezi kununua uongo wake, kama wewe unaamini maneno yake amini hivyo, nitamsoma kiduchu, nitamsikiliza kiduchu ila siwezi kukubali maneno yake bila kuhoji
Chadema ndicho chama cha kwanza kuwahi kumwingiza Mwenyekiti wa Kijiji wa Kwanza mwaka 1994 katika kijiji kimoja huko Karatu kinaitwa Gongali na Mwenyekiti mwenyewe anaitwa Simon Kibola.
Uchaguzi wa huyu mwenyekiti ulirudiwa kwa zaidi ya mara nne chini ya usimamizi wa defender za polisi kutoka Arusha Mjini lakini mwishowe kura za wazi ndizo zilizomfanya ashinde.
Sijui mnachopinga nini mnaleta mfano wa Mwenyekiti wa Kijiji wakati Kigoma walitoa mbunge wa kwanza wa Chadema 1994 kwenye Bunge ili kwenu siyo kubwa, kubwa ni la Mwenyekiti wa kijiji kuchaguliwa.Chadema ndicho chama cha kwanza kuwahi kumwingiza Mwenyekiti wa Kijiji wa Kwanza mwaka 1994 katika kijiji kimoja huko Karatu kinaitwa Gongali na Mwenyekiti mwenyewe anaitwa Simon Kibola.
Uchaguzi wa huyu mwenyekiti ulirudiwa kwa zaidi ya mara nne chini ya usimamizi wa defender za polisi kutoka Arusha Mjini lakini mwishowe kura za wazi ndizo zilizomfanya ashinde.
Nishakujibu huko mwanzo, juu ya "midomo mirefu", sitaki kuamini kama bado lugha ya picha hiyo haieleweki.
Pili, nimeishasema hapo juu, mikoa mingi hasa hasa Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mara na Kigoma kulikuwa na upinzani mkali kwenye uchaguzi wa mwaka 1995.Hakuna mtu atakataa hili.
Hivi umeisikiliza hiyo video? na je umesoma na kuelewa kwanini tunasema ni uogo? Kama hukuisikiliza ni hivi Zitto anasema Wakati wana Kigoma wako katika harakati ya mageuzi watu wa Arusha walikuwa wanakumbatia watawala.. Hiki ndicho ninachobishania kuwa Si kweli kuwa Arusha, Singida na Iringa walikuwa wamelala. NA KWA JIBU LAKO HAPO JUU TUKO PAMOJA.
.Hoja hapa sio uchaguzi wa 1995, hoja iliyotolewa hapa ni kuwa "wakati kigoma upinzani umekomaa kwingine CCM ilikuwa imetamalaki", sasa la kujiuliza ni je hii ni kweli?jibu ni NDIYO, kabla ya mwezi wa 4 mwaka 1995 hakukuwa na upinzani wowote wa kuitisha CCM mikoa mingine.Ni kuanzia April 1995 ndipo takribani nchi nzima ilifufuka ghafla na kimbunga cha Mrema
Je ni kweli wakati Kigoma upinzani umekomaa Arusha, Singida na Iringa walikuwa wanashangilia watawala?
Jibu ni hapana ila ni kweli kuwa kuna baadhi ya mikoa mpaka leo wao ni CCM damu damu.
Na kwa ili sitegemea kiongozi msomi kama Zitto kuwakashfu watu kwa vile tumetofautiana kimtazamo na pia si haki pale watu wanapoona umuhimu wa vyama vya upinzani na kujiunga havyo , wauulizwe/wasimangwe/wakweke daraja la pili kwa vile tu majiunga le hawakujiunga miaka 20 iliopita. Vyama havijengwi kwa kutazama ni lini umejiunga bali kwa kutazama unakitumikiaje chama.Na hizi ndo argument za kijinga kutoka kwa Zitto. (kwamba mie nimejiunga nikiwa na miaka 16 na nyie umejiunga jana.. au sie tulipigwa mabomu wakati nyie mnashangilia watawala) .
Nakubaliana na wewe kuhusu kimbuga cha Mrema lakini Mrema alikuta mageuzi yapo ila alipojiunga na upinzani ni kama alileta chachu za mabadiliko na hizi chachu za mabadiliko zilienea Tanzania nzima ikiwemo na Kigoma. Hivyo basi huwezi kusema kuwa Kigoma hawakufaidika na Mrema maana wao walishapiga hatua kwenda mbele kuliko mikoa yote.
LAKINI Kigoma tayari kuliishakuwa na upinzani mkali sana toka mapema baada ya 1992, masuala ya kupigwa mabomu na watu kufungwa yaliishaanza Kigoma kabla ya mkoa mwingine wowote. Mwaka 1994 mbunge wa kwanza wa upinzani Tanganyika alichaguliwa Kigoma Mjini..Hii ni fact. Kukataa hili ni kuikataa historia.Weka kumbukumbu zako sawa.Katika uchaguzi wa mwaka 1995 Kigoma ilipata atleast wabunge watatu wa upinzani(sina kumbukumbu nzuri hapa)
Ila ni kuwa baada kifo cha aliyekuwa mbunge wa wakati huo, ulifanyika uchanguzi wa mbuge wa CCM alishinda ila matokeo yalitenguliwa na mahakama. Hii ndo fact.,
Otherwise, ninaelewa ilivyo ngumu kuelewa kitu kama tayari umeishatanguliza "jibu" unalolitaka.ndilo tatizo lililoko hapa.