Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

kaburu ni nani huyu?
Huyo kijana alishawahi kuniuliza kama kuna ushaidi wa wananchi kuchukia uchonganishi uliotendwa, ukaburu unaohubiriwa
Tulimweleza hatuna ushahidi ! Wakati ukifika wananchi watasema, tutajua ukweli! sijui kama wakati umefika au la!

Utetezi wao ni kuwa mbona fulani kasema ABCD!

Tunasimama kupinga uchochezi uliofanywa kwa kutumia takwimu. Tumeonyesha wananchi wanavyojiletea maendeleo, habari hiyo hawataki kuigusa. Suala la maendeleo ni pana si kontena la ubuyu tunaloambiwa ligawanywe

Wengine akina Mknadara wanamuunga mkono kwa kusema mikoa kama Kilimanjaro/Arusha imewezeshwa.
Tumewaonyesha mfano wa mikoa hiyo hawana majibu. Tumewauliza imewezeshaje, jibu ni kuwa kuna maji.
Hivi nani asiyejua maji yanatoka ardhini na kwamba ni suala la kijiografia

Hawa wote ni watu elite bado wanamshangilia mtu aliyelenga kuvuruga taifa hili

Huwezi kutukana mikoa inayojileta maendeleo bila sababu wananchi wakakuelewa


Uchochezi ulaaniwe, hii ni nchi yetu. Ubaguzi wa '' kwani ni dhambi mtu wa abcd kuwa mwenyekiti"" ni kauli za kitoto
Hivi tunachagua viongozi kwa maeneo au makabila

Hawa wenzetu wanaona kauli hiyo murua kabisa. Hawaoni madhara yake kitaifa. Hawaoni kabisa!
 
Ritz , Gamba la Nyoka Mkandara....baada ya Mh. Joshua kutoa kauli hiyo mara moja mwenyekiti wa Chadema alipinga kauli hiyo na kusisitiza huo siyo msimamo wa chama cha chadema. Na haya yamo kwenye uzi wako (Ritz) uliobandika JF 2012. Mchangiaji mmojawapo kwenye uzi huo aliandika hivi.



Mwingine katika uzi mwingine aliandika hivi



Hii ni kwa uchache kuonyesha kauli za kuvunja umoja wa taifa hazichekewi na viongozi wakuu wa Chadema, wanachama wa chadema na sisi watanzania wengine kwa ujumla wetu bila kujali ni nani anatoa kauli hizo. Mbowe kama mwenyekiti wa chama cha Chadema aliwajibika kukanusha kauli ile pale pale...! Nassari naye alilazimika kutoa ufafanuzi wa kauli yake.

Kwa hiyo muda mwingine mtakapo kuwa mnaelezea suala la Nassari wekeni na maelezo jinsi viongozi wa chadema na wanachama wake na watanzania kwa ujumla jinsi walivyoshughulikia suala hilo.

Baada ya maelezo hayo sasa turudi kwenye mada iliyoko mezani.

1.chama-cha-ACT-mpini-wa-CCM-kumaliza-upinzani
2.
'Kauli' ya Zitto inahataraisha umoja wa kitaifa. Na kauli hizi Zitto (S.L) hajazitolea ufafanuzi.
Joshua Nassari katoa siri ya chama wewe unategemea Mwenyekiti wa Chadema Mbowe atasema nini?

Umeshajiuliza kwa nini Dr.Slaa, Lema aliyeambiwa atakuwa waziri mkuu wa Taifa la Kaskazini wote walikaa kimya bila kulaani kauli ya Nassari?

Wameishajiuliza kwa nini Baraza Kuu la Chadema walikaa kimya bila kutoa tamko h
Kuhusu kauli ya Nassari kuwa Chadema wataanzisha Taifa lao la Kaskazini kama Sudan Kusini.

Unakumbuka kauli ya Mtei kuhusu wajumbe wa katiba Mbowe alisema nini?

Msidhani watanzania wa sasa ni wajinga wanapima mambo kwa kina.
 
Last edited by a moderator:
Ritz , Gamba la Nyoka Mkandara....baada ya Mh. Joshua kutoa kauli hiyo mara moja mwenyekiti wa Chadema alipinga kauli hiyo na kusisitiza huo siyo msimamo wa chama cha chadema. Na haya yamo kwenye uzi wako (Ritz) uliobandika JF 2012. Mchangiaji mmojawapo kwenye uzi huo aliandika hivi.



Mwingine katika uzi mwingine aliandika hivi



Hii ni kwa uchache kuonyesha kauli za kuvunja umoja wa taifa hazichekewi na viongozi wakuu wa Chadema, wanachama wa chadema na sisi watanzania wengine kwa ujumla wetu bila kujali ni nani anatoa kauli hizo. Mbowe kama mwenyekiti wa chama cha Chadema aliwajibika kukanusha kauli ile pale pale...! Nassari naye alilazimika kutoa ufafanuzi wa kauli yake.

Kwa hiyo muda mwingine mtakapo kuwa mnaelezea suala la Nassari wekeni na maelezo jinsi viongozi wa chadema na wanachama wake na watanzania kwa ujumla jinsi walivyoshughulikia suala hilo.

Baada ya maelezo hayo sasa turudi kwenye mada iliyoko mezani.

1.chama-cha-ACT-mpini-wa-CCM-kumaliza-upinzani
2.
'Kauli' ya Zitto inahataraisha umoja wa kitaifa. Na kauli hizi Zitto (S.L) hajazitolea ufafanuzi.
Mkuu kama haya sio msimamo wa chama kwa nini bado huyo Nasari ni mgombea wa chama hicho kutoka majimbo hayo hayo? hii Nidhamu inayoongelewa ni kwa watu gani haswa ikiwa mtu amediriki kusema ama kusimamia mambo ambayo sii mwongozo wa chama?.. Tuamini lipi na tusiamini lipi maana kukana kauli hata CCM wanakana wao sio Mafisadi lakini kuwatenga wenye kashfa za Ufisadi wameshindwa wamebebwa hadi leo na kuwapa nafasi ya kugombea Urais. Kuna tofauti gani baina yenu?
 
1. Joshua Nassari katoa siri ya chama wewe unategemea Mwenyekiti wa Chadema Mbowe atasema nini?

2.Umeshajiuliza kwa nini Dr.Slaa, Lema aliyeambiwa atakuwa waziri mkuu wa Taifa la Kaskazini wote walikaa kimya bila kulaani kauli ya Nassari?

3.Wameishajiuliza kwa nini Baraza Kuu la Chadema walikaa kimya bila kutoa tamko h
Kuhusu kauli ya Nassari kuwa Chadema wataanzisha Taifa lao la Kaskazini kama Sudan Kusini.

4.Unakumbuka kauli ya Mtei kuhusu wajumbe wa katiba Mbowe alisema nini?

5.Msidhani watanzania wa sasa ni wajinga wanapima mambo kwa kina.

1. Hili linahitaji ulithibitishe kwa ushahidi usiotiliwa shaka. Na kwa usahihi, ushahidi huo nadhani unatakiwa uufungulie uzi mpya juu ya hilo. Maana hapa hapatakuwa mahala pazuri kuuweka kwani ushahidi huo hauwezi kujibu hoja ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania.

2. Kwa mujibu wa Itifaki kwa Viongozi Wakuu wa Chama (rejea - Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema | Itifaki ) ni kuwa Wenyeviti
Watakuwa wasemaji wakuu wa chama katika ngazi husika, wanaweza kutoa matamshi rasmi kuhusu chama. Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania.
3. Rejea namba 2 hapo juu.Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania..
4.Rejea namba 2 hapo juu.Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania..

5. Ni kweli si busara hata kidogo kudhani kuwa watanzania wa sasa ni wajinga, watanzania wa leo wanapima mambo kwa kina. Kwa msingi huo huo huna budi wewe (Ritz) ujipime kama kile unachokifanya hapa kwenye uzi huu; cha kuvuruga hoja iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania, kama kinakusaidia kuwafanya watanzania kuwa wajinga kiasi cha kushidwa kumtambua ni nani kwa makusudi ana vuruga ama anashabikia vurugu za kuua umoja wa taifa la Tanzania pia anahimiza ACT kuendelea kuwa mpini wa CCM kumaliza Upinzani. Watanzania siyo wajinga wanatutambua malengo yetu kutokana na nyendo zetu katika kuandika, kuongea, na kutenda. Lazima ulitambue hilo.


 
Mkuu kama haya sio msimamo wa chama kwa nini bado huyo Nasari ni mgombea wa chama hicho kutoka majimbo hayo hayo? hii Nidhamu inayoongelewa ni kwa watu gani haswa ikiwa mtu amediriki kusema ama kusimamia mambo ambayo sii mwongozo wa chama?.. Tuamini lipi na tusiamini lipi maana kukana kauli hata CCM wanakana wao sio Mafisadi lakini kuwatenga wenye kashfa za Ufisadi wameshindwa wamebebwa hadi leo na kuwapa nafasi ya kugombea Urais. Kuna tofauti gani baina yenu?
Kwa heshima kubwa kabisa rejea bandiko langu namba 1364 la uzi huu wakati nina mujibu Ritz.
 
Kwa heshima kubwa kabisa rejea bandiko langu namba 1364 la uzi huu wakati nina mujibu Ritz.
Alaa jamani kwa nini nyie mnataka kuchagulia watu maneno? mada inahusu ACT nanyi mnamshutumu Zitto sio chama kuwa ndiye Msaliti na mbaguzi sasa hivi vinahusianaje na ACT kuwa mpini wa CCM? Tukiwafuata katika hoja zenu mnabadilika na kutaka tufungue mada nyingine kwa nini isiwe nyie ndio muanzishe mada nyingine inayomhusu Zitto kama msaliti na Mbaguzi halafu tuzungumzie hayo..
 
Huyo kijana alishawahi kuniuliza kama kuna ushaidi wa wananchi kuchukia uchonganishi uliotendwa, ukaburu unaohubiriwa
Tulimweleza hatuna ushahidi ! Wakati ukifika wananchi watasema, tutajua ukweli! sijui kama wakati umefika au la!

Utetezi wao ni kuwa mbona fulani kasema ABCD!

Tunasimama kupinga uchochezi uliofanywa kwa kutumia takwimu. Tumeonyesha wananchi wanavyojiletea maendeleo, habari hiyo hawataki kuigusa. Suala la maendeleo ni pana si kontena la ubuyu tunaloambiwa ligawanywe

Wengine akina Mknadara wanamuunga mkono kwa kusema mikoa kama Kilimanjaro/Arusha imewezeshwa.
Tumewaonyesha mfano wa mikoa hiyo hawana majibu. Tumewauliza imewezeshaje, jibu ni kuwa kuna maji.
Hivi nani asiyejua maji yanatoka ardhini na kwamba ni suala la kijiografia

Hawa wote ni watu elite bado wanamshangilia mtu aliyelenga kuvuruga taifa hili

Huwezi kutukana mikoa inayojileta maendeleo bila sababu wananchi wakakuelewa


Uchochezi ulaaniwe, hii ni nchi yetu. Ubaguzi wa '' kwani ni dhambi mtu wa abcd kuwa mwenyekiti"" ni kauli za kitoto
Hivi tunachagua viongozi kwa maeneo au makabila

Hawa wenzetu wanaona kauli hiyo murua kabisa. Hawaoni madhara yake kitaifa. Hawaoni kabisa!

Mkuu wangu wote wameishakubali kuwa Zitto amekosea, wanaona kosa la Zitto na ndo maana wanasema basi tumkemee na Nassari.. Mtu mzina anapotoa kauli hii inadhihisha kuwa amekubali kuwa Zitto alikosea, ila si Zitto peke yake bali hata Nassari..

Hivyo ninaweze kutembea kifua mbele kuwa hawa watu waliokuwa namtetea sasa na wao wanaona kitu kile kile tunachoona mimi na wewe ila wanashindwa kumkemea kipenzi chao.

By the way kuna video moja ninaitafuta, nilisikiliza audio mara moja humu JF. Lakni nafikri kwa vile ilikuwa na maneno ya uchochezi sana Moderators waliondoa. (ni jambo jema tu maana ilikuwa haijengi bali inabomoa.)

Ni aibu kwa Kiongozi wa chama kutamka maneno kama yale sijui anapopanda jukwaani akili zake zinahama kwa muda?

Katika hiyo audio "Kuna sehemu ana sema hivi (km sijakosea) KWANI MATUMBO YA WANAWAKE WA KIGOMA HAYAWEZI KUZAA VIONGOZI WA VYAMA? KWANINI MATUMBO YA WANAWAKE WA KIGOMA YAZAE MANAMBA WA NCHI HII?

Yaani kijana anakatisha tamaa hata kwa wanaomtetea maana wakati bado hawajamaliza kutetea ili anakuja na lingine! Hakika anaitaji kuwa karibu na wazee wenye busara maana vijana wanaomzunguka ni design ya watu wanaomzunguka Lowassa. Wanachowaza ni kumlia pesa zake tu basi. Ni masikitiko kwa kijana mdogo kama huyu kuona anapoelekea. Na duniani unaweza kuwa na marafiki wengi lakini rafiki wa kweli akawa ni mmoja au hasiwepo kabisa. (mtanisamie kwenda in personal ila sina jinsi)

Mfn mzuri tu muone Lowassa baba wa watu anaumwa lakini kuna watu wanawimbia nyimbo ya kupamba hakuna anayejali afya yake wanawaza namna ya kupata pesa zake tu. Haki sisi binadamu ni wakatili kuzidi wanyama.
 
1. Hili linahitaji ulithibitishe kwa ushahidi usiotiliwa shaka. Na kwa usahihi, ushahidi huo nadhani unatakiwa uufungulie uzi mpya juu ya hilo. Maana hapa hapatakuwa mahala pazuri kuuweka kwani ushahidi huo hauwezi kujibu hoja ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania.

2. Kwa mujibu wa Itifaki kwa Viongozi Wakuu wa Chama (rejea - Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema | Itifaki ) ni kuwa Wenyeviti
Watakuwa wasemaji wakuu wa chama katika ngazi husika, wanaweza kutoa matamshi rasmi kuhusu chama. Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania.
3. Rejea namba 2 hapo juu.Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania..
4.Rejea namba 2 hapo juu.Hivyo acha tabia ya kututoa kwenye mada iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania..

5. Ni kweli si busara hata kidogo kudhani kuwa watanzania wa sasa ni wajinga, watanzania wa leo wanapima mambo kwa kina. Kwa msingi huo huo huna budi wewe (Ritz) ujipime kama kile unachokifanya hapa kwenye uzi huu; cha kuvuruga hoja iliyoko mezani ya ACT kuua upinzani na kauli za Zitto (S.L) kuhatarisha umoja wa taifa la Tanzania, kama kinakusaidia kuwafanya watanzania kuwa wajinga kiasi cha kushidwa kumtambua ni nani kwa makusudi ana vuruga ama anashabikia vurugu za kuua umoja wa taifa la Tanzania pia anahimiza ACT kuendelea kuwa mpini wa CCM kumaliza Upinzani. Watanzania siyo wajinga wanatutambua malengo yetu kutokana na nyendo zetu katika kuandika, kuongea, na kutenda. Lazima ulitambue hilo.


Mimi majibu yangu kwako ni haya kutoka kwa Mkuu Mkandara.

Alaa jamani kwa nini nyie mnataka kuchagulia watu maneno? mada inahusu ACT nanyi mnamshutumu Zitto sio chama kuwa ndiye Msaliti na mbaguzi sasa hivi vinahusianaje na ACT kuwa mpini wa CCM? Tukiwafuata katika hoja zenu mnabadilika na kutaka tufungue mada nyingine kwa nini isiwe nyie ndio muanzishe mada nyingine inayomhusu Zitto kama msaliti na Mbaguzi halafu tuzungumzie hayo..


Halafu nani kakupa mamlaka hapa JF kupangia watu vitu vya kuandika unataka wote tuwe mateka wa fikra za Nguruvi3 kama wewe nisipokubaliana na wewe basi naonekana Kuvuruga hoja hapana walionzisha hii forum wamesema wazi kuwa JF ni jukwaa huru kila mtu ana uhuru wa kuchangia chochote ili muradi tufuate sheria na kanuni za JF.

Mkui wangu sheria za JF zipo wazi kama navuruga mjadala niripoti kwa moderator wanichukulie hatua, kingine JF siyo mali ya Chadema naona unajisahu sana unadhani JF ni mali ya Chadema zikija fikra mpya unaona kama watu wanavuruga mjadala.

Mwisho kabisa nakushauri jifunze kusoma vitu usivyovipenda itakusaidia sana kuongeza ubora wa fikra.
 
Last edited by a moderator:
Mimi majibu yangu kwako ni haya kutoka kwa Mkuu Mkandara.

.......A. mada inahusu ACT nanyi mnamshutumu Zitto sio chama kuwa ndiye Msaliti na mbaguzi sasa hivi vinahusianaje na ACT kuwa mpini wa CCM? .....

.....B. walionzisha hii forum wamesema wazi kuwa JF ni jukwaa huru kila mtu ana uhuru wa kuchangia chochote ili muradi tufuate sheria na kanuni za JF. ..... sheria za JF zipo wazi kama navuruga mjadala niripoti kwa moderator wanichukulie hatua, ....

....C.Mwisho kabisa nakushauri jifunze kusoma vitu usivyovipenda itakusaidia sana kuongeza ubora wa fikra.

A. Mkandara , Katiba ya ACT iliyopitishwa na mkutano mkuu wa chama hicho 29/03/2015;

SURA YA NNE, fungu namba 29 : ACT Taifa, sehemu ya 25:Kazi na sifa za Kiongozi wa Chama , vipengele vya nane (ix) na tisa (ix) ukurasa wa 47 inaeleza hivi :

KATIBA YA ACT said:
viii. Atakuwa ndiye mtoa tamko rasmi kuhusu masuala ya sera na mtazamo wa Chama katika mambo ya kitaifa na kimataifa;

ix. Atakuwa mtoa habari mahususi kwenye Mkutano Mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu kuhusu hali ya kisiasa nchini na masuala mengine ya kitaifa na kimataifa"

Kiongozi mkuu (SL) wa sasa wa ACT ni Zitto, ambaye anatoa kauli za kutufarakanisha watanzania. Kauli hizi zimepigwa marufuku pia na KANUNI ZA MWENENDO NA MAADILI YA VIONGOZI WA ACT, chama anachokiongoza Zitto. kama zinavyosomeka:

Sehemu ya II Ibara ya 3: Kiongozi wa ACT:

1) Awe Mzalendo;
2) Asiidhalilishe nchi yake Tanzania na Watanzania; {sasa wengine anawaita wana midomo mirefu}
........
Sehemu ya III Ibara ya 4: Sheria na Kanuni ambazo kiongozi wa ACT anapaswa kuzitii
......
11) Awe mtetezi wa Umoja wa Taifa na Afrika; {anasema chama cha ACT ni cha watu wa Kigoma, kwa hiyo siyo cha
watanzania?! rejea clip aliyoleta Alinda}
..................................
12) Kupinga na kupigana dhidi ya ubaguzi wa aina zote;{ Alianzisha mada yenye mwelekeo wa 'kibaguzi' dhidi ya watanzania
wenzake wa mikoa ya kaskazini, mpaka sasa haja fanya juhudi zozote kutolea
ufafanuzi kauli hizo}

B. Sina hakika kama kweli unazielewa (Ritz) sheria za JF pale unapozisoma.
Mfano mmoja tu, sheria/kanuni namba sita (6) ya Kanuni na sheria za Jamiiforums inasomeka hivi


  • 6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.
    { Haujatoa ushahidi kudhibitisha kuwa Nassari alitoa siri ya Chama chake kutokana na kauli aliyotoa}



C.Kwa tabia yangu ya Udadisi hilo unalodhani unanishauri, ni sehemu ya utaratibu wangu wa kuhakikisha nina elewa dhana/dhima ama maudhui ya kile ninachokifuatilia.
======================================================================
Vipi, bado mnahitaji tena kupindisha mjadala ulioko mezani wa Chama cha ACT kuwa mpini wa CCM kumaliza upinzani na suala la kauli za Zitto kuhatarisha umoja wa Kitaifa ?
 
A. Mkandara , Katiba ya ACT iliyopitishwa na mkutano mkuu wa chama hicho 29/03/2015;

SURA YA NNE, fungu namba 29 : ACT Taifa, sehemu ya 25:Kazi na sifa za Kiongozi wa Chama , vipengele vya nane (ix) na tisa (ix) ukurasa wa 47 inaeleza hivi :



Kiongozi mkuu (SL) wa sasa wa ACT ni Zitto, ambaye anatoa kauli za kutufarakanisha watanzania. Kauli hizi zimepigwa marufuku pia na KANUNI ZA MWENENDO NA MAADILI YA VIONGOZI WA ACT, chama anachokiongoza Zitto. kama zinavyosomeka:

Sehemu ya II Ibara ya 3: Kiongozi wa ACT:

1) Awe Mzalendo;
2) Asiidhalilishe nchi yake Tanzania na Watanzania; {sasa wengine anawaita wana midomo mirefu}
........
Sehemu ya III Ibara ya 4: Sheria na Kanuni ambazo kiongozi wa ACT anapaswa kuzitii
......
11) Awe mtetezi wa Umoja wa Taifa na Afrika; {anasema chama cha ACT ni cha watu wa Kigoma, kwa hiyo siyo cha
watanzania?! rejea clip aliyoleta Alinda}
..................................
12) Kupinga na kupigana dhidi ya ubaguzi wa aina zote;{ Alianzisha mada yenye mwelekeo wa 'kibaguzi' dhidi ya watanzania
wenzake wa mikoa ya kaskazini, mpaka sasa haja fanya juhudi zozote kutolea
ufafanuzi kauli hizo}

B. Sina hakika kama kweli unazielewa (Ritz) sheria za JF pale unapozisoma.
Mfano mmoja tu, sheria/kanuni namba sita (6) ya Kanuni na sheria za Jamiiforums inasomeka hivi


  • 6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.
    { Haujatoa ushahidi kudhibitisha kuwa Nassari alitoa siri ya Chama chake kutokana na kauli aliyotoa}



C.Kwa tabia yangu ya Udadisi hilo unalodhani unanishauri, ni sehemu ya utaratibu wangu wa kuhakikisha nina elewa dhana/dhima ama maudhui ya kile ninachokifuatilia.
======================================================================
Vipi, bado mnahitaji tena kupindisha mjadala ulioko mezani wa Chama cha ACT kuwa mpini wa CCM kumaliza upinzani na suala la kauli za Zitto kuhatarisha umoja wa Kitaifa ?
Nakushauri hii sheria ya JF ulioileta ungewatumia Nguruvi3 na Alinda udadisi wako ungekamilika.

6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.

Zitto kusingiziwa hapa ukumbini hii sheria hamuhusu inamuhusu Nassari tu?

Wewe unasukumwa na ushabiki wa Chadema bora ungekaa kimya kila unavyozidi kuandika unazidi kuzama kwenye tope.

Nakushauri rudi jukwaa la siasa kwenye nyuzi zako za kumzomea Zitto.
 
Last edited by a moderator:
Ritz Unaikumbuka ile Kauli ya Muasisi wa Chadema, aliyehoji teuzi ya Raisi Kikwete kwa wajumbe wa Tume ya Katiba ya Warioba kwamba imesheheni " Waislamu" wengi?
Tunakumbuka ile nyuzi, hakika tulimteremkia mzee Mtei perfect and square.

Hapa tunajadili za kiongozi mkubwa na chama chake kinavyotumika kama mpini
Alinda kasema hapo nyuma, kimsingi manakubali kauli za ukakasi, kichefuchefu na kufilisika za Kiongozi mkuu
Mnachokifanya sasa hivi ni kutafuta uwiano. Kwa bahati mbaya uwiano haujibu hoja zinazomkabili

Atasimama ahesabiwe katika kauli zake, na mnaona zinavyomtesa
 
Last edited by a moderator:
kaburu ni nani huyu?

Humjui Dr Aman KABURU,aliewai kuwa mbunge wa kigoma mjini,kupitia CDM, na sasa ni mwenyekiti CCM mkoa,wa Kigoma,ametengeneza historia kua mbunge wa kwanza upinzani kuingia bungeni(1994),uchaguzi Mdogo.na akashinda tena 1995.naona ndugu yako Nguruvi3, tafsiri yake imeenda afrika kusini, sababu ya ubaguzi wake
 
Huyo kijana alishawahi kuniuliza kama kuna ushaidi wa wananchi kuchukia uchonganishi uliotendwa, ukaburu unaohubiriwa
Tulimweleza hatuna ushahidi ! Wakati ukifika wananchi watasema, tutajua ukweli! sijui kama wakati umefika au la!

Utetezi wao ni kuwa mbona fulani kasema ABCD!

Tunasimama kupinga uchochezi uliofanywa kwa kutumia takwimu. Tumeonyesha wananchi wanavyojiletea maendeleo, habari hiyo hawataki kuigusa. Suala la maendeleo ni pana si kontena la ubuyu tunaloambiwa ligawanywe

Wengine akina Mknadara wanamuunga mkono kwa kusema mikoa kama Kilimanjaro/Arusha imewezeshwa.
Tumewaonyesha mfano wa mikoa hiyo hawana majibu. Tumewauliza imewezeshaje, jibu ni kuwa kuna maji.
Hivi nani asiyejua maji yanatoka ardhini na kwamba ni suala la kijiografia

Hawa wote ni watu elite bado wanamshangilia mtu aliyelenga kuvuruga taifa hili

Huwezi kutukana mikoa inayojileta maendeleo bila sababu wananchi wakakuelewa


Uchochezi ulaaniwe, hii ni nchi yetu. Ubaguzi wa '' kwani ni dhambi mtu wa abcd kuwa mwenyekiti"" ni kauli za kitoto
Hivi tunachagua viongozi kwa maeneo au makabila

Hawa wenzetu wanaona kauli hiyo murua kabisa. Hawaoni madhara yake kitaifa. Hawaoni kabisa!

Mzee sijakuelewa unapomwambia Alinda kuwa ukabaru unahubiriwa,nilichosema Mimi kingene,nyie mnaleta tafsiri za ubaguzi
Humjui Dr Aman KABURU,aliewai kuwa mbunge wa kigoma mjini,kupitia CDM, na sasa ni mwenyekiti CCM mkoa,wa Kigoma,ametengeneza historia kua mbunge wa kwanza upinzani kuingia bungeni(1994),uchaguzi Mdogo.na akashinda tena 1995.naona ndugu yako Nguruvi3, tafsiri yake imeenda afrika kusini, sababu ya ubaguzi wak
 
Wanabodi,

Kwanza lazima kwanza tufahamu siasa ni kitu gani kisha ndio tujenge hoja zetu kwa maudhui (content) yanayolingana na siasa haswa tunapolijadili swala hili la Upinzani. Kwanza kabisa kuwepo kwa vyama vya Upinzani ni jambo jema sana maana sisi sote hatuwezi kufikiri sawa, hatuwezi kuwa na mahitaji sawa, mazingira tamaduni na kadhalika vyote hivi vinachangia katika tofauti zetu na vyote hivi huchangia utetea wa kisiasa katika kila tunachokiona kuwa ni haki na fursa ya wananchi katika ujenzi wa USAWA baina yao. Kwa hiyo kila mtu atautazama USAWA huo kutoka upande wake, kutoka kundi la kijamii yake wamepungukiwa nini ambacho wengine wanafaidika nacho ilihali wao ni jamii moja.

Chimbuko la kisiasa haswa limetokana na KUTETEA haki za watu wako kutokana na mfumo ama muundo wa kisheria unao wanyima haki na fursa zilizopo iwe ya kitamaduni, mila, desturi au mafao stahiki kutokana na mazingira wanayoishi kushiriki sawa na makundi mengine. Na imekuwa hivyo kwa miaka kiasi kwamba hata mbunge huwakilisha matakwa ya watu wake mbele ya mtazamo mpana wa Kitaifa. UTETEZI wa kundi la wanyonge kama mfano dhidi ya Udhalilishaji hata siku moja haiwezi kuwa ni Ubaguzi.

Na kutokana na tofauti hizi za kimazingira na tamaduni, rasilimali watu hujenga hisia za matabaka baina yao ambazo zinaweza kulijenga taifa ama kulibomoa ikiwa SIASA SAFI hazikutumika kuwa kigezo na mahala pa kufikiwa muafaka baina ya makundi haya ya kijamii ili kuunda UMOJA wa kudumu kwa kuzingatia yale yanayowaunganisha na sii yale yanayowatenganisha maana changamoto kubwa ya Utaifa ni USAWA baina ya wahusika katika mambo Yanayowaunganisha kwani hakuna Umoja wa kudumu unaoweza kupatikana kwa mambo yasowaunganisha maana hayana maslahi ya pamoja.

Sasa leo hii tukipuuza usawa tukajenga hoja ambazo zinapuuza ukweli wa kisiasa kwa sababu tu leo tunaishi kwa mazoea ambayo hayana USAWA, ali mradi kila mmoja kulinda fursa na haki walonazo kwa makusudi kabisa huu huitwa UJINGA kwa maana ya IGNORANCE. Wakoloni na Makaburu walikuwa na Ujinga (Ignorance) kwa sababu hawakutaka kujielimisha katika usawa walitetea fursa zao kwa hoja zinazopinga Usawa wa binadamu hautokani na haki ama fursa sawa kwa wote bali nani anastahili haki na fursa hizo ka vigezo vyao. Hata tawala wa Kiimla na kidikteta zilitumia UJINGA huo kutotazama USAWA wa binadamu kama kigezo kikubwa cha kujenga UMOJA wa KITAIFA.

Hivyo basi kutokana na Ujinga (ignorance) ndivyo harakati za fikra pevu za mageuzi hutokea, vyama vya UPINZANI (RESISTANCE) vikajitokea kutetea HAKI na FURSA hizo katka mazingira na nafasi zile zile zilizokandamizwa na UJINGA. Kwa hiyo vyama vya Upinzani asili yake ni kutokubaliana na hali iliyopo ya Utawala unaowanyima wananchi haki na fursa sawa kwa wote - As they say resistance is to refuse to comply with something..

Kwa karne za zamani, Upinzani waliingia msituni kwa sababu haikuwa HAKI wala halali kupingana na Utawala na matokeo yake upinzani ukawa wa siri na kujificha misituni. Upinzani ukazua vita na mauaji ya pande mbili zilizopingana kutetea kile kile walochukuwa wakiamini ni halali ya kila upande. Sasa Ujio wa vyama vya Upinzani kisasa ni ujenzi mpya wa vita baina ya jamii badala ya kuingia msituni na kupigana mapanga, ikawekwa sheria ya Upinzani kupitia mabaraza yetu na sheria zikatungwa kwa kuzingatia mazungumzo (dialogue) baina ya makundi yanayotofautiana kiitikadi (utetezi wa haki na fursa) kwa njia ya AMANI pasipo kupigana vita ama kujenga chuki baina yaa..

Kifupi nachotaka kusema hapa, Kila mwanasiasa ni lazima kwanza atetee watu wake, jamii yake kwa kusimamia haki na fursa zilizopo pale ambapo usawa umepotoshwa. Viongozi wote wa Kimataifa na wengine wameitwa mashujaa ni kwa sababu walianza na kutetea watu wao, kisha kupanua wigo zaidi kwa kadri na jinsi jamii hiyo inavyokubaliana. Hao Kina Abraham Lincorn, John MacDonald, Churchill, Mkwawa, Marealle, Nyerere, Nkrumah, Mandela hadi viongozi wa leo kina Harper, Cameron, Obama wanaweza tu kuitwa viongozi bora ikiwa wameweza kwanza kuwatetea USAWA wa haki na fursa kwa makundi yote yaloijenga JAMII hiyo kuwa Taifa moja.

Sasa huwezi sema leo ati kwa sababu Mandela alipingana na Utawala wa makaburu ambao dhahiri watu weupe walipendelewa basi ni mchonganishi kwa sababu ati aliwataja wazungu dhidi ya weusi akiwa yeye mweusi. Huwei sema Nyerere alikuwa mbaguzi kwa sababu alipingana na Wakoloni walotawala nchi za Afrika kwa sababu wazungu ama waarabu pia walizaliwa Afrika. hapa tutakuwa tunapotosha content kwa makusudi kwa sababu kinachogombaniwa ni mfumo ama muundo unaowakandamiza wengine kwa kutumia vigezo hivyo hivyo.

UJINGA ni pale hao Wakoloni, Makaburu na Waarabu walipokataa na kutetea nafasi zao ya kwamba kulikuwepo USAWA baina yao na weusi wakijenga hoja zinazowabagua wanyonge na kustahili haki na fursa walozopewa kwa sababu ya asili yao. Hata siku moja mtu anayelia kwa UNYONGE hawezi kuwa yeye mbaguzi bali mbaguzi ni yule mwenye nguvu na uwezo wa kushinikiza kuendelea kuwakandamizi ama kupinga matakwa ya wengine katika kuwapa nafasi sawa katika haki na fursa.

Hivyo napowasikia watu wa kaskazini wakiendelea kutetea Ubora wao na kwamba wao ni zaidi isipokuwa hawa kina Zitto wanaopigania fursa na haki sawa kwa mikoa mingine ndio wabaguzi inanishangaza sana na najitahidi sana kuwasoma hawa watu wanaojivunia na kutetea MIKOA yao, wakitumia jina la makabila yao kama wanatengwa kwa sababu wana mafanikio zaidi ili waendelee kufaidika na muundo wa kiutawala uliopo inanipa sura na picha wa wazungu wabaguzi naoishi nao kila siku hapa nilipo. Well anyway sitowalaumu sana maana siasa pia ni kutetea U Mangimeza!

Ebu msome huyu jamaa hapa:-

Wachagga wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa wa kufanya biashara na pia kilimo. Moshi ni maeneo ya mwanzo ambayo Wamisionari wa Ukristo walijenga makanisa na shule.Sababu hii imefanya Wachagga kuwa kabila lenye watu wengi zaidi walio na elimu ya kisasa na mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa idadi ya shule za sekondari nchini Tanzania. Kulingana na takwimu za elimu mkoa wa Kilimanjaro una shule za sekondari zaidi ya 320. Pia mkoa una shule za msingi zipatazo 950. Idadi hii ya shule ni kubwa zaidi ya idadi ya shule katika mikoa mingine Tanzania.
Shule nyingi za sekondari ziko katika mkoa huu kwa sababu zifuatazo: 1) Hali ya hewa na vivutio vya kitalii katika mkoa huu viliwavutia zaidi walowezi na wakoloni na kuweka makazi yao hapo. Hivyo wamisionari walijenga shule za kwanza wakifuatiliwa na serikali za wakoloni 2) Serikali ya Tanzania ilirithi shule zilizojengwa na wakoloni 3) Wachagga waliobahatika kupatafedha binafsi baadaye waliwekeza kwenye ujenzi wa shule binafsi kama kitega-uchumi, wakati wakazi wa mikoa mingine kadhaa walisubiri serikali iwajengee shule. 4) Ukichanganya sababu 1, 2 & 3 utagundua shule katika mkoa Kilimanjaro zimezidi sana idadi ya shule katika mikoa mingine yote.
Ni vema pia kusema kUwa shule hizo huvutia wanafunzi kutoka Tanzania nzima, haziwasomeshi Wachagga tu.
Inanishangaza..
 
Mkandara hebu tufafanulie , mikoa mingine imenyimwa haki gani? Fursa gani kiongozi mkuu anazopigania ambazo zinakandamizwa na watu wengine?
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,

Hata siku moja mtu anayelia kwa UNYONGE hawezi kuwa yeye mbaguzi bali mbaguzi ni yule mwenye nguvu na uwezo wa kushinikiza kuendelea kuwakandamizi ama kupinga matakwa ya wengine katika kuwapa nafasi sawa katika haki na fursa.

Hivyo napowasikia watu wa kaskazini wakiendelea kutetea Ubora wao na kwamba wao ni zaidi isipokuwa hawa kina Zitto wanaopigania fursa na haki sawa kwa mikoa mingine ndio wabaguzi inanishangaza sana na najitahidi sana kuwasoma hawa watu wanaojivunia na kutetea MIKOA yao, wakitumia jina la makabila yao kama wanatengwa kwa sababu wana wamfanikio zaidi ili waendelee kufaidika na muundo wa kiutawala uliopo.

Well anyway sitowalaumu sana maana siasa pia ni kutetea U Mangimeza!
Hayo umeyasema mkuu, tuendelee na mjadala.
 
Mkandara hebu tufafanulie , mikoa mingine imenyimwa haki gani? Fursa gani kiongozi mkuu anazopigania ambazo zinakandamizwa na watu wengine?
Mkuu siwezi kurudia kote kule tulikotoka. Itafute Hotuba mnayoikandya kwa utetezi wenu wenyewe maana unauliza swali wakati jibu lipo humu humu katika mada hiii hii..
 
Mkuu siwezi kurudia kote kule tulikotoka. Itafute Hotuba mnayoikandya kwa utetezi wenu wenyewe maana unauliza swali wakati jibu lipo humu humu katika mada hiii hii..
Mkuu wangu Mkandara sijui kwa nini hili jibu hawalitaki wakati limeeleza wazi.

Zitto,

Tanga ni ya 8 katika kuchangia Pato la Taifa. Pia ni mkoa wa 8 kwa kiwango cha maendeleo ya watu wake.Mikoa yenye Maendeleo zaidi ni Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam. Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7.Mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo nchini ni Kigoma, Singida, Dodoma, Kagera na Tabora. Hata hivyo Tabora ni mkoa wa 10 kwa kuchangia katika Pato la Taifa na Kagera ni mkoa wa 11 katika GDP.Mikoa yenye mchango mdogo zaidi kwenye Pato la Taifa ni Pwani (1.85%), Lindi (1.89%) na Singida (1.92%). Hata hivyo Lindi inashika nafasi ya 9 kwa Maendeleo, juu ya Shinyanga inayochangia 6% katika GDP.Dar inaongoza kwa kuchangia Pato la Taifa ambapo mchango wake kwenye pato la Taifa ni 16.9%. Inafuatiwa na Mwanza [kabla haijagawanywa] 9.2%, Mbeya 7.3%, Shinyanga 6% na Iringa 5.3%. Hata hivyo Shinyanga ni mmoja wa mikoa yenye umasikini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia Pato la Taifa.Ndio maana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi. Huwezi kuwa na mkoa unashika namba 5 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namba 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu. Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi. Shinyanga ina Ng'ombe na Pamba.Shinyanga tarehe 17 Aprili, tujadiliane jinsi ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi mkoani mwenu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu Mkandara sijui kwa nini hili jibu hawalitaki wakati limeeleza wazi.

Zitto,

Tanga ni ya 8 katika kuchangia Pato la Taifa. Pia ni mkoa wa 8 kwa kiwango cha maendeleo ya watu wake.Mikoa yenye Maendeleo zaidi ni Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam. Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7.Mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo nchini ni Kigoma, Singida, Dodoma, Kagera na Tabora. Hata hivyo Tabora ni mkoa wa 10 kwa kuchangia katika Pato la Taifa na Kagera ni mkoa wa 11 katika GDP.Mikoa yenye mchango mdogo zaidi kwenye Pato la Taifa ni Pwani (1.85%), Lindi (1.89%) na Singida (1.92%). Hata hivyo Lindi inashika nafasi ya 9 kwa Maendeleo, juu ya Shinyanga inayochangia 6% katika GDP.Dar inaongoza kwa kuchangia Pato la Taifa ambapo mchango wake kwenye pato la Taifa ni 16.9%. Inafuatiwa na Mwanza [kabla haijagawanywa] 9.2%, Mbeya 7.3%, Shinyanga 6% na Iringa 5.3%. Hata hivyo Shinyanga ni mmoja wa mikoa yenye umasikini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia Pato la Taifa.Ndio maana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi. Huwezi kuwa na mkoa unashika namba 5 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namba 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu. Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi. Shinyanga ina Ng'ombe na Pamba.Shinyanga tarehe 17 Aprili, tujadiliane jinsi ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi mkoani mwenu.
Hitimisho na point kubwa ya ujumbe wake wote ni kaitka maandishi hayo mekundu (Huwezi kuwa na nchi tajiri lakini watu wake Maskini!...) Mimi sio mtu wa Shinyanga wala Kigoma inakuwaje naona kuna matatizo ya Kimfumo hapa ktk kuwapa haki yao lkn hawa jamaa zangu wanaona tu Kilimanjaro na Arusha!
Halafu Ritz wao wenyewe wanamtuhumu Zitto kila kona lakini waulize inakujaje swala kama hili lihusiane na ACT kama mpini wa CCM kumaliza Upinzani?. wao watakuja na majibu yao! ukimzungumzia kiongozi wa CDM tu utaambia anzisha mada nyingine!...
 
Back
Top Bottom