Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Dah.. aliyesema siasa ni mchezo mbaya hakukosea... Siasa inaweza kukujengea heshima katika jamii na pia siasa inaweza kukufanya uonekane kituko katika jamii hiyo hiyo.. Sikutegemea kama ndugu yangu Mwigamba ndani ya mwaka mmoja angekuja kuonekana kituko...
 
Dah.. aliyesema siasa ni mchezo mbaya hakukosea... Siasa inaweza kukujengea heshima katika jamii na pia siasa inaweza kukufanya uonekane kituko katika jamii hiyo hiyo.. Sikutegemea kama ndugu yangu Mwigamba ndani ya mwaka mmoja angekuja kuonekana kituko...
Na zaidi ya hapo, Mwigamba kabeba watu wasioweza kufikiriwa na jamii kuwa wa aina yake. Yaani wapo waliounga tela leo hata nyuso zao sijui wanaziweka wapi.
 
Wanaduru

Kufuatilia hukumu ya kesi ya Zitto Vs Chadema tutajadili ;
- Mchezo wa kisiasa wa Zitto
-Mahakama ilivyotumika katika mchezo wa kisiasa
-Chadema walivyomsaidia kucheza mchezo huo
-Yale yaliyosemwa kuhusu Zitto/Bunge la katiba na hatima yake kisiasa
-Maadili ya kiroho na udanganyifu wa wanasiasa, kuwalilia wananchi kumbe wanalilia matumbo, Je, Zitto ni tofauti?

Usikose na mengine katika uzi huu kuanzia leo
 
MADAI YA ZITTO DHIDI YA CHAMA CHAKE(CHADEMA)

MWENENDO HADI HUKUMU YA MWISHO

MCHEZO WA KISIASA WA WANASIASA WA ZAMA HIZI

Sehemu ya I

Tuangalie mwenendo wa wanasiasa na matumizi ya chombo cha mahakama.
Hili litatuwezesha kuona undani wa mchezo wa wanasiasa unaoshika kasi na kuwa sehemu ya demokrasia ya nchi yetu

Mahakama: Ni chombo cha kusimamia sheria, tafsiri ya sheria,kusuluhisha na kutoa haki kwa mtu, watu au jamii husika.
Kutoa haki hufanyika katika msingi wa hukumu, na hivyo pande husika hupata haki stahiki kulingana na sheria husika.

Na katika kuona haki ikitendeka, mahakama ina uwezo wa kuzuia, kusimamisha mwendelezo wa jambo hadi suluhu au hukumu itakapopatikana.

Hii ni kusidia pande husika kufikia muafaka ndani au nje ya mahakama bila upande mmoja kuchukua sheria mikononi, au kutumia mbinu na njia zinazoweza kuathiri upande mwingine. Ndio msingi wa pingamizi la mahakama au zuio la mahakama


Ni kwa bahati mbaya, hakuna sheria inayoweza kusimama kama nzuri au mbaya, bali hutegemea upande husika unanufaika vipi.

Hivyo, haki ya zuio au pingamizi la mahakama haiwezi kuelezwa kama kitu kizuri au kibaya kwasababu uwepo wake ni kwa ajili ya kusimamia haki.

Ni kwa bahati mbaya, katika ukuaji wa demokrasia nchi, na hata utawala, watu wametumia baadhi ya haki za mahakama kinyume na ilivyokusidiwa. Kwa mfano, agahalabu wafanyabiashara wakikimbilia mahakamani ili suala husika lisizungumzwe katika kiwango cha kuathiri shughuli zao.

Ndivyo ilivyo katika utawala, tunapoona watu wakikimbilia mahakamani ili kuzuia hoja zinazoonekana kuwaweka katika hali mbaya.
Mfano wa kesi ya maadili vs escrow ni mmoja kati ya mingi


Hali hiyo haijaacha eneo la siasa. Imekuwa ni utaratibu wa viongozi wa kisiasa kukimbilia mahakamani kuweka mazuio katika yanayohusu vyama, au taasisi za kisias.

Bunge la JMT limejaa wabunge wengi ambao uwepo wao ni wa nguvu za mahakama baada ya migogoro katika vyama vyao.

Wabunge walioweka mapingamizi, hijanasibu kutafuta haki wakiwa na haki zao kama wabunge.

Nyuma ya pazia, wabunge wametumia fursa kwa masilahi yao na si ya vyama au maeneo wanayowakilisha. Hili limekuwa donda ndugu.

Wabunge hao wa mahakama, hukosa nguvu za uwakilishi ikizingatiwa kuwa uwepo wao ni 'hisani' tu na muda wowote hisani husika inaweza kuondolewa kwa kuharakaisha masuala yao mahakamani.

Na hapa tutoe mfano hai. Yupo mbunge wa upinzania aliyewahi kuwa katibu mkuu na makamu mwenyeitiki wa chama, mtu mashuhuri wa siasa za Zanzibar. Mbunge huyo baada ya kutimuliwa ndani ya chama chake, kama walivyo wengine akakimbilia mahakamani.

Ni mwaka wa 3 kesi inaunguruma naye akimaliza muda wake.
Wakati kesi ipo mahakamani, mbunge huyo ni mwanachama wa 'siri' na kiongozi wa chama kipya cha upinzani.

Mbunge anayezugumziwa, kwa kutambua uwepo wake ni hisani ya 'serikali' amekuwa mshirika mkubwa wa CCM, chama alichotumia muda mwingi kukiponda. Mbunge huyo ndiye aliyehusika kuvuruga mchakato, kutafuta wabunge feki na kupigia debe katiba ya Chenge.

Amesahau yeye ni mwanzilishi wa madai ya mfumo wa muungano na aliyeulaani huu anaoupigia debe sasa kama mbunge wa mahakama


Mfano, huo ni katika kuonyesha kuwa, mapingamizi ya wabunge hayatokani na kudai haki. Mazuio huwa na malengo mawili
1. Kuvuta muda na kujipanga kisiasa
2. Kutumikia matumbo yao kwa kuchelea kuacha mafao, masurufu na marupu rupu ya nafasi zao

Ili kufaniskisha zama hiyo, mapingamizi na mazuio ya mahakama sasa ni 'fashion'

CHADEMA NA ZITTO

Mgogoro wa ZZK na CDM ulihitimishwa kwa kutimuliwa ndani ya Chama chao.

Ushahidi dhidi ya Zitto na wenzake ulijitosheleza kiasi cha wao kukiri ndani ya vikao vya chama.

Taratibu za kuwatimua zilifuatwa na kama mahakama ilivyoonyesha hakukuwa na ukiukwaji kama ilivyoainishwa leo

Zitto akimbilia mhakamani

Inaendelea
 
Sehemu ya II

ZITTO ATIMKIA MAHAKAMANI, WASHIRIKA WAHAMIA ACT

Zitto alikimbilia mahakamani kudai kutotendewa haki.

Washirika wake hawakuelekea mahakamani ingawa walihukumiwa na cha Chadema katika kikao kimoja.

Hilo tu linaonyesha wasi wasi wa haki aliyokuwa anaidai mh Zitto.


ZZK akilimbilia mahakamani kukiwa na bunge maalumu la katiba, na muda mwingi kabla ya bunge la JMT halijamaliza muda wake.

Akiwa mahakamani, washirika wake walijiunga na chama kipya cha kisiasa na kutelekeza haki ZZK aliyoiona imeminywa Chadema


Katika uzi huu tuliwahi kujadili kwa undani kuwa ZZK hakukimbilia mahakamani kudai haki ya kisiasa.

Alichokifanya ni kwenda kudai haki ya kulinda masilahi yake ya kisiasa na wala si uwakilishi wa wananchi wake.

Alitambua, kufukuzwa kungekatisha ubunge mapema na kumletea usumbufu wa masilahi,zaidi ya haki aliyotambua hanayo.

Uwezekano wa ZZK kuchaguliwa kama mbunge wa chama kingine ulikuwepo sana.

Kilichomkwamisha ZZK ni bunge maalumu la katiba ambalo alitegemea kujijenga kisiasa zaidi wakati akununua muda wa kuelekea kwingine. Ushahidi wa hili ni pale aliposema, ilikuwa ni makosa kwa wapinzani kutoka BMLK.


Kwa mtazamo wa ZZK, UKAWA kususia BMLK hakukutimiza malengo yake.

Lengo la kwanza lilikuwa ni kuweka pingamizi ili aendelee kuwemo bungeni, na lengo la pili, kujijenga kisiasa.
Kuondoka kwa UKAWA kulivuruga mipango yote hiyo.

Fursa ya bunge la JMT ameitumia vema kwa kuwa mwiba mkali kwa masuala ya escrow na kamati ya PAC kwa ujumla
Inafahamika hoja ya escrow chanzo chake na mhusika, lakini ni karata muhimu kisiasa ZZK akaamua kuitumia vema kujijenga kisiasa.

Inaweza kuwa sahihi kwa yale aliyofanya, lakini nia na dhamira ni ya kutiliwa shaka kwa kuzingatia mazingira ya kisiasa yanayomkabili na mustakabali wake kisiasa

Laiti angelitambua BMLK litavunjika, ZZK asingekwenda mahakamani.
Angetimka na wenzake kwenda kujenga chama kipya.

Kuvunjika kwa bunge la katiba, kulivuruga malengo yake ya kisiasa na kimasilahi kwa kiasi kikubwa sana.

WASHIRIKA WAMWANDALIA ZITTO MAKAO MAPYA

Washirika waliojiunga na cha ACT walianza harakati za kuhakikisha kuwa wanamwandalia makao mapya mapema iwezekanavyo.

Msingi wa jambo hilo ni ukweli wa shinikizo la kutaka ACT iwe na uchaguzi si zaidi ya Mwezi May mwaka huu.

Tunafahamu timbwili lililozuka baada ya hapo. Washirika waliololamika kutotendewa haki, wakiwa wahubiri wakuu wa kulaani siasa za kutimuana, ghafla wakaacha falsa hiyo iliyompleka ZZK mahakamani, na kukumbatia timua timua walioilaani kule walikotoka

Mwezi May umewekwa mahususi kwa kutambua muda wa kuelekea October katika uchaguzi mkuu ulikuwa ni mchache.

Hivyo, safu ya uongozi wa ACT ilitakiwa ipangwe haraka kwa kuzingatia machafuko yaliyosababishwa na UKAWA kuondoka bungeni.

ZITTO AONEKANA MIKUTANO YA CUF

Katika hali ya kuendelea kuuchanganya umma na hasa wafuasi wake, Zitto alionekana katika mikutano ya CUF

Lengo lilikuwa ni kutumia majukwaa ya kiasiasa ili kutopotea katika ulingo wa kisiasa

Na pia kuondoa minong'ono inayomhusu kuhusu kuhamia ACT ili kupunguza joto la kisiasa ndani ya ACT kwavile anaonekana kama yeye ndiye chanzo akiwa mwandaliwa kuchukua hatamu za uongozi

Kama mtakumbuka, akiwa Chadema, ZZK alitamgaza kuachana na siasa na kuwa mwalimu. Nyuma ya pazia alikuwa na mpango wa mapinduzi kwa kile tunachokijua sasa kama Waraka.

Na huko nyuma, ZZK alitumia vijana hadi kuwapeleka maeneo ya tabibu za asili ili walimwe chale za makalioni katika kujiweka sawa kisiasa na hususwan kufanilisha jaribio la mapinduzi ambalo Ben Saanane wa Chadema alikinusuru chama chake kwa kujitoa mhanga.

Hivyo uwepo wa ZZK eno lolote, au kauli zake si jambo la kutilia maanani hasa kwa kuangalia historia yake inayoonyesha kukosa kile kinachosemwa kama ''sense of morality'

HUKUMU YATOKA
CHADEMA WAFANYA KOSA LA KISIASA

Inaendelea sehemu ya II
 
Sehemu ya II

MAANDALIZI YA KUELEKEA ACT

Mwezi huu, ZZK alisikika akisema ataweka wazi mustakabali wake kisiasa kabla ya mwisho wa mwezi.

Kauli ile ilitolewa kwa kufahamu kuwa kule mahakamani kesi itasikilizwa na yeye na wakili wake hawana haja ya kushinda

Hivyo alifahamu matokeo ya kesi wiki nzima kwa kujua kuwa anakwenda kushindwa, si kwa hoja bali kwa kupenda

Muda alionunua kisiasa unatosha, na muda uliobaki hauwezi kuwa na masilahi zaidi.

Japo anaweza kukosa bunge la bajeti, lakini hiyo ni fursa ya kujijenga kuelekea uchaguzi ikifahamika takuwa ni miezi 5 tu

CHADEMA walitambua kuondolea kwa ZZK na wenzake kulizingatia hatua zote za kisheria, kanuni na taratibu za chama

Hivyo kwenda mahakamani ilikuwa ni sehemu tu ya wajibu na wala siyo kutetea msimamo wao.

Jana, kumeletwa habari za hukumu huku mamia ya washabiki wa CDM wakishangilia kwa ushindi

Katika mazingira ya kawaida, CDM hawakupaswa kuzungumzia hukumu ya ZZK.

Kilichotakiwa ni kumuandikia barua, na kumpa ZZK mzigo wa kueleza hukumu yeye mwenyewe

Chadema wametenda kosa la kisiasa. Kitendo cha wao kueleza kwa furaha kilimaanisha maamuzi waliyotafanya yalikuwa na shaka, na kwamba mahakama imeondoa shaka hiyo.

Hili halikuwa jambo sahihi kama lilivyoletwa na wana CDM

Pili, katika mazingira yaliyopo, hukumu inampa ZZK publicity bila sababu

Ikizingatiwa kuwa tayari alishasema ataweka msimamo, sasa macho na masikio ya watu yataelekezwa katika msimamo wa wapi anaeleka badala ya yeye kueleza hukumu imesemaje na kwanini.

Kwa maneno mengine Chadema wamemuondolea ZZK mzigo wa kueleza ilikuwaje na kwanini.

Hatima ya ZZK kisiasa ipo kwake kama mtu binafsi anayekubalika na sehemu ya jamii. ZZK anabahati ya kuwa na wafuasi wasiotazama pembeni, kulia au kushoto.

Kwa bahati mbaya hali tata ya kisiasa anaisababisha mwenyewe na ni yeye wa kujilaumu.

Kama taasisi, hatima ya ZZK ina mashaka makubwa. Uwezekanao wa ZZK kuhamia chama cha ACT ni mkubwa kuliko mwingine.

Tatizo linalomkabili mbele ya safari ni kundi linaloambatana naye kisiasa.

Washirika wanaonekana wasaliti mbele ya umma. ZZK atakuwa na kazi ya kuondoa sintofahamu hiyo, na kisha ujenzi wa chama

Ujenzi wa chama utakabiliwa na matatizo ambayo yameanza kabla ya kufika kwake.

Picha iliyopo ni kuwa ACT ni mahususi kwa kundi la wahamiaji ambao historia inawaweka katika wakati mgumu kuaminika kisiasa.

Wamepoteza kile kinachosemwa kama ushawishi wa kisiasa.

KUHAMIA CUF

Hili lina utata sana. Kwa makubaliaano ya UKAWA, ujio wa ZZK unaweza kuleta mpasuko mkubwa.

Haitakuwa rahisi kwa mahasimu kukaa meza moja(Chadema Vs CUF-Zitto).

Kutoamaniana kwa Zitto na CDM hakutoi nafasi ya mipango endelevu ya UKAWA. Pengine anaweza kuwa chanzo cha kuvunjika.

Tatizo si kuaminiana kati ya ZZK na CDM, bali Zitto amepoteza sehemu kubwa sana ya imani waliyokuwa nayo wananchi juu yake.

Hili la kwenda mahakamani kwa kununua muda linazidi kummaliza kisiasa.

NINI HATIMA YA ZZK NA MAJAALIWA YA SIKU ZA USONI?

Inaendelea kesho....
 
Nguruvi3,

Kama ulivyobainisha ni Kazi za Mahakama: Ni chombo cha kusimamia sheria, tafsiri ya sheria,kusuluhisha na kutoa haki kwa mtu, watu au jamii husika. Kutoa haki hufanyika katika msingi wa hukumu, na hivyo pande husika hupata haki stahiki kulingana na sheria husika. na vile vile mahakama ni chombo huru kabisa kisichoweza kuingiliwa utendaji wake wa kazi na chombo chochote cha mamlaka ya nchi.

Sasa unapomuona mtu si tu kiongozi bali mtu yoyote anapoona hajatendewa haki ana haki kamili na hata sharia za Tz zinamrukhusu kwenda mahakamani KUDAI haki yake.

Na ukija katika Mfumo wa mahakama za huko Tz utaona zinabainisha wazi kuwa unapoona haki yako imefinywa au ukuridhika na hukumu yoyote ya mahakama unakwenda kwenye mahakama ya juu kudai haki yako.

Nikirudi katika Suala la ZZK , kama ulisikiliza hukumu iliyotolewa basi inampa nafasi yeye kuweza kukata Rufaa kwenye mahakama ya juu au hata kufungua shauri hilo katika mahakama za chini kama Zito ataona hakutendewa haki na mahakama kuu. Hiyo ni haki yake kikatiba.

Mimi nafikiri badala ya kupoteza muda mwingi kujadili suala la kesi ya ZZK ni vizuri muangalie mambo mengine yenye maslahi katika uchumi na ustawi wa nchi yenu na kumuacha Zito na wanasharia wake wakiangalia hukumu hiyo kama wameridhika na kukubaliana nayo bila chembe ya mashaka au hawajaridhika nayo na hivyo kukata Rufaa katika mahakama za juu.

Hakika hiyo ndio Demokrasia inayofuatwa na Tz nchi inayofuata Utawala wa sharia.

Hayo ni maoni yangu na mtazamo wangu kwako katika mwelekeo wa uzi wako.
 
....
Mimi nafikiri badala ya kupoteza muda mwingi kujadili suala la kesi ya ZZK ni vizuri muangalie mambo mengine yenye maslahi katika uchumi na ustawi wa nchi yenu na kumuacha Zito na wanasharia wake wakiangalia hukumu hiyo kama wameridhika na kukubaliana nayo bila chembe ya mashaka au hawajaridhika nayo na hivyo kukata Rufaa katika mahakama za juu.
.......
Hayo ni maoni yangu .....

Ni kweli ni maoni yako. Ila bahati mbaya sana sikubaliani nayo.

Kichwa cha uzi huu kinasema" Duru za Siasa: Chama cha ACT-Mpini wa CCM kumaliza Upinzani". Kichwa cha uzi huu kinatoa uhalali wa mada hii kumjadili Zitto Buyagwa Kabwe (Sijajua kwa nini siku hizi hapendelei jina la Zuberi litumike kwenye utambulisho wake). Nitaeleza.

Buyagwa ni mwanasiasia anayetuhumiwa kushirikiana na CCM kukiangamiza Chadema (rejea post mbalimbali hapa JF zinazomuhusu Buyagwa/Zitto). Buyagwa ni mwanasiasa ambaye ametimuliwa na wenzake (Mwigamba; Mkumbo) amabao walikuwa wote CHadema ila sasa wao wameamia ACT wakati yeye bado hajasema mstakabali wake kisiasa baada ya jana kufutwa rasmi uanachama wa Chadema. Kumbuka kilichosababishwa kutimuliwa watatu hao (Buyagwa,Mkumbo, na Mwigamba) ni kuandaa mkakati wa kuuangusha uongozi wa sasa wa Chadema ili 'Akili Kubwa' iweze kuendesha chama yaani Buyagwa awe Mwenyekiti wa Chadema. Kumbuka pia Chadema ni chama cha Upinzani.

'Bahati' haikuwa yao mpango haukufanikiwa wakaamia (Mwigamba,Mkumbo) chama cha siasa kiitwacho ACT. Minong'ono kutoka ACT ikabainisha wahamiaji kutoka Chadema (Mwiga na Mku) wanataka kupindua uongozi wa ACT uliopo ili wampe Buyagwa uongozi huo. Hili liliingia akilini maana mkakati uliowafanya watimliwe Chadema ni huo. Songombingo za ACT kwa sasa karibu kila mfuatiliaji wa habari za siasa nchi anazijua.

Mkuu mpaka hapo unaweza kuona ilivyo ngumu kukwepa kumjadili Buyangwa (a.k.a Zitto) na umahakama na usiasa wake kwenye uzi huu. Ukiunganisha nukta vizuri utagundua kuwa Nguruvi3 yuko sahihi kuendeleza mjadala huu akimuhusisha Buyagwa na 'timbwili timbwili' zake za kisiasa.

Pia na mimi haya ni maoni yangu, unaweza kuyakubali ama kuyakataa.


........
Na ukija katika Mfumo wa mahakama za huko Tz utaona zinabainisha wazi kuwa unapoona haki yako imefinywa au ukuridhika na hukumu yoyote ya mahakama unakwenda kwenye mahakama ya juu kudai haki yako......


Sawa, na wewe Wasalaamu huko '
nchini Zanzibar'.

Wabilah Tawfiq !

 
Inaendelea...

Awali ya yote tuwashukuru waliochangia mawazo hapo juu. I

kumbukwe kuwa Zitto ni mwanasiasa , mwakilishi na ni kiongozi wa umma kutoka pande zote za utawala, uwalkilishi na kichama hata kama alivuliwa hadhi nyingine.

Kanuni zisizo rasmi za uongozi zinasema, awaye kiongozi huyatoa maisha yake kwa jamii' public figure'' na kuzungumzwa kuhusu yeye bila shaka. Ndivyo ilivyo duniani kote.

Mfano, watu hukosea kama wanadamu, Wasira alipofunga vifungo vya koti kwa kupishana hiyo ikawa ni habari.
Public figure ni habari kabla ya yeye kuleta habari

Wazungu husema, with great power comes great responsibility, wakimaanisha, kwa mamlaka au uwezo mkubwa basi majukumu makubwa yanajitokeza.

Zitto ana nguvu kutokana na nafasi yake kijamii, hakuna namna anaweza kukwepa kuwajibika ikiwa ni pamoja na kujadiliwa kwa hadhi ile ile anayoitumia kuwasiliana na jamii.

Ni ujinga kudhani maendeleo yanakuja katika mafurushi au makontena.

Maendeleo ya mtu au watu hutegemea mipango thabiti yenye maono.

Katika nchi yetu jukumu hilo kwa umma kwa ujumla wake wanalo viongozi.

Endapo tutadhani kuwa uwepo wa viongozi wabovu hautuhusu, basi hatutafanikiwa.

Hawa viongozi ndio wanaopanga mipango inayotuhusu kama wananchi na watu binafasi.

Kwasababu tunadhani jukumu letu ni kuchagua viongozi na si kuwawajibisha, nchi imezama katika lindi la wizi, ufujaji, ufisadi na kila aina ya uovu.

Wengine wanadhani ni muhimu kujadili mambo ya manufaa kwa nchi na si jukumu letu kuwawajibisha wanaotukwamisha.

Hivyo, hatuwezi kutenga uongozi, viongozi, majukumu, wajibu na mambo yenye manufaa kwa taifa letu kama vitu tofauti na visivyotegemeana. Kufanya hivyo ni kosa kama tulilofanya miaka 50 iliyopita.

Utamaduni huo lazima ufike mwisho. Viongozi watambue kuwa wananchi wa zama hizi ni tofauti. Kama wanavyoheshimiwa na jamii, nao wanawajibu wa kuiheshimu jamii, kujadiliwa, kukoselewa, kupongezwa n.k.

NINI HATMA YA ZITO NA MAJAALIWA YA SIKU ZA USONI

Ni wazi, ZZK atatafuta chama cha kisiasa ili kuendelea kuwepo.

Chama itakuwa ni jukwaa la yeye kuwasiliana na jamii. Katika kipindi cha mpito tokea alipotimuliwa hadi hukumu ya jana, Zitto amekosa jukwaa la kisiasa na hivyo kuathiri taswira yake kisiasa. Hilo ndilo lililomsukuma kwenda kwenye mikutano ya CUF

ZZK ana ushawishi mkubwa kisiasa, na kwamba ataendelea kuwa kiongozi,ni suala la muda.

Tatizo linalomkabili kwa sasa,ni kushindwa uongozi. Kashfa zilizojitokeza akiwa Chadema ambazo nyingi zina ushahidi usio na mashaka, zinakuwa ni kipimo kizuri cha kushindwa kwake

Kwa ushawishi alio nao katika jamii na chama chake, haikutegemewa Zitto aongeze harakati kama za masalia, na waraka badala ya kuongoza mabadiliko kwa hekima, busara na mantiki.

Hata baada ya kupewa nafasi za kujirekebisha na kukua kimawazo na busara, Zitto hakuonekana kujifunza.

Alitumia umaarufu wake kuendeleza matatizo alliyosababisha kwa njia tofauti.

Huko ni kushindwa kuongoza. Kiongozi hujifunza kutokana na makosa, na wala kukiri kosa hakumfanyi kiongozi kuwa dhaifu bali kuwa mwenye hekma na busara

Zitto alipotakiwa kupatanishwa na wenzake, alichokifanya ni kutoa masharti na si kutafuta suluhu kati na kati.
Kutoa masharti kumejengwa na hali ya majivuno 'narcissism' akiamini ni mtu muhimu kuliko wengine.

Endapo alikiri ndani a kikao kushiriki waraka, alishindwa vipi kuzungumza na wenzake ili ya kale yaishe wafungue ukurasa mpya?Majivuno, kukosa hekma na busara si sifa za kiongozi mzuri, kama si kushindwa uongozi.

Inaendelea...
 
Inaendelea

Kikubwa zaidi kinachoathiri mustakabali wa kisiasa kwa siku za usoni ni kupungua 'public trust'' miongoni mwa jamii iliyomtazama kama kiongozi wa siku za usoni.

Kashfa nzito za kipuuzi zinazomwandama zinamweka ZZK 'on the spot'

Kwanza, haaminiki tena miongoni mwa viongozi wenzake
Pili, haaminiwi na jamii na kama anaaminiwa ni kwa jicho la hadhari

Hivyo, ZZK aliyekuwa na 100 public trust na kujijengea immunity ya wananchi sasa anasimama akiwa na makundi matatu

Kwanza, kundi linalomwamini kwasababu linamwamini na halitakia kusikia jambo jingine (Zealot)

Pili, kundi llilopoteza imani naye kwa kila anachofanya

Tatu, kundi lisiloweza kumweka ZZK katika upande wowote lakini lina shaka njema na mbaya(Linajiuliza kuhusu ZZK)

Kundi la kwanza na la pili hayawezi kumsumbua Zitto. Ni makundi yenye misimamo yao na hayawezi kubadilika

Kundi la tatu ni baya sana kwasababu linamweka ZZK on the spot. Hili ndilo litaamua safari yake kisiasa.

Kwa mfano, kundi hilo linapohisi ZZK alikwenda mahakamani kununua muda na si haki, linakwazika

Likisikia habari za escrow(iwe ukweli au uongo) na ushiriki wa ZZK linakuwa na mashaka yasiyo ya lazima kwa ZZK

Na kwa vile ZZK keshapoteza public trust, 'maadui' hutumia fursa hiyo kumweka mahali pagumu.

Mathalan, sakata la escrow ametajwa kula mlungula . Hawa wanajua wakitumbukiza kitu kidogo tu, lipo kundi la tatu linaloweza kuachana na ZZK kabisa. Na maadui wanaitumia fursa hiyo vema

Zitto ajilaumu kwa kujenga mazingira hayo na wala si mtu au chama.

ZZK atakuwa na wakati mgumu kisiasa kama hataachana na washirika wake wanaompoteza.
Washirika wake wanaamini ZZK ni chama akiwa mwenyewe, Nyerere hakuwahi kuamini hivyo pamoja na umaarufu wake!!

Kwa sasa washirika wametangaza vita na Chadema kupitia chama cha ACT
Je, hilo linamsaidia Zitto?

Ikumbukwe umma umechoshwa na CCM, vita nyingine ni sawa na kumsaidia adui.

Wapo watakaosema rafiki ya adui yako ni adui. Je, huko anakotarajia kwenda ataweza kufanikiwa katika mazingira hayo?
 
Sehemu ya miwsho

Matatizo ya wananchi na nchi yetu si rasilimali au watu. Ni kukosekana kwa uongozi na viongozi waadilifu, wenye maono, wakweli na wanaotetea haki kwa dhati ya mioyo yao wakiweka wananchi mbele

CCM imetufikisha hapa miaka 50 kwasababu ya kukosa maadili, kutosimamia sheria na kuogopana.

CCM imejenga utamaduni wa kuvumiliana na wala si kusimamiana.

CCM imegeuka kuwa taasisi ya watu na si chama kwasababu tu wananchama wanaamini CCM ni watu na si taasisi.

CCM imeshindwa majukumu ya nchi ya ya chama chao kutokana na kukosekana kwa nidhamu.

Nidhamu hainunuliwi, wala utamaduni hauibuki kama uyoga.

Ni vitu vinavyojengwa ka gharama kubwa. Siku tutakapokuwa na taasisi za kisiasa zenye nidhamu, tutakuwa na serikali yenye nidhamu na kupiga hatua.

Hatua walizochukua Chadema si maarufu( popular ) kwa umma, lakini ni muhimu(necessary) kwa demkorasia ya nchi.

Utamaduni wa vyama kuwa mali za watu sasa ukome. Wananchi wamelipa gharama kubwa kule NCCR. CUF n.k.

Chadema wameotoa funzo moja kubwa kwa mara ya pili. Taasisi inaundwa na watu, na hakuna mtu ambaye ni taasisi akiwa peke yake. Walifanya kwa madiwani Arusha, na sasa kwa mtu anayeaminiwa ni nguzo ndani ya CDM.

CDM ina hoja, kwamba inaweza kuchukua maamuzi magumu

Na kwamba, inasimama kama taasisi na si mtu au watu.

Katika siku za usoni, CDM itajenga nidhamu kubwa miongoni mwa wanachama na wananchi.

Kama watamudu kuvuka mawimbi yanayovuma salama, CDM kitakuwa taasisi imara siku za baadaye.

Ukishaanza kujenga utamaduni wa nidhamu, kuwajibika na kuwajibishana bila kujali majina au hadhi, tayari unajenga taasisi imara.

Pamoja na hayo, timbwili la ZZK limetoa funzo kwa CDM.

Kwamba, kuchukua hatua mapema ni bora kuliko kufanya ukarabati uharibifu ukishatokea.

CDM bado wana tatizo kubwa la mawasilano na jamii na mkakati. Haitoshi tu kuchukua hatua, ni lazima hatua zieleweke, upotoshaji udhibiwe na kuepuka yasiyo ya lazima.

Hili si tatizo la ZZK ni tatizo la CDM kwa muda mrefu. Wasipokuwa wangalifu ipo siku watalipa gharama kwa uzembe huo
Hivi kuna sababu gani za kushangilia ushindi wa mahakamani kama walishatoa uamuzi sahihi katika vikao vyao

Hivi kuna sababu gani taasisi ibishane na mtu binafsi na kumpa publicity kwa kutegewa? Kuna tatizo mahali

Hatuwezi kuwa na serikali imara tukiwa na vyama vya wahuni, vinavyoongozwa na wahuni kwa ubinafsi

Jukumu letu ni kusimama na kusema 'hili yes, hili hapana' bila kujali vyama, mtu au watu.

Tusipoweza kujenga nidhamu kwa kizazi kijacho, nasi tutakuwa tunawaanda mafisadi wakiwa na majoho na kanzu zao tukidhani ni mashemasi na maustadhi.

Hili la ZZK halina utetezi, je haiwezekani kuwa mfano 'template' kwa maeneo mengine?

ZZK upo ma utakuwepo kisiasa tena ukivuma, lakini Zitto wa miaka 10 iliyopita si Zitto wa leo!

Tusemezane
 
Zitto, Kitila na Mwigamba walifukuzwa Chadema Kwa tuhuma Za kuandaa kushiriki Njama za kuhujumu Chadema hasa kuandaa mikakati haramu Ya kubadilisha uongozi wa juu wa chama. Hilo halina mjadala.

Katika Chama kipya cha ACT, watatu wale wale wanatuhumiwa kwa makosa yale Yale - yani kutaka kuleta mapinduzi ndani Ya Chama cha ACT ili Zitto Ambae Njama za kumfanya mwenyekiti Chadema kwa njia haramu zilikwama, sasa aweze kuwa mwenyekiti wa ACT Taifa, Sio kwa mujibu wa kanuni, katiba, Utaratibu au njia Ya demokrasia, bali kwa njia zile Zile haramu zilizowafukuzisha uanachama Chadema. Ni kutokana na uharamia ule ule wakiwa Chadema, mwenyekiti halali wa Sasa wa Chama cha ACT, Kadawi Limbu anataka mahakama itoe Amri Ya kumzuia mwigamba na wenzake wasijihusishe na Chama cha ACT, pia wasikiongelee Chama cha ACT popote mbele Ya umma, Kwenye vyombo vya habari au kutoa maelekezo kwa wanachama na Viongozi wa ACT. Wameondolewa Chama chao cha zamani kutokana na vitendo haramu, wakaenda Chama kipya, kwenda kufanya makosa yale Yale. Katika hati Ya kiapo iliyowasilishwa mahakamani na mwenyekiti halali wa ACT Taifa - Limbu, Naibu Katibu Mkuu Bara - Mahona, katibu mwenezi na mwenyekiti wa Vijana taifa - Nyakarungu, mwenyekiti wa wanawake taifa - Dotto Wangwe, makamo mwenyekiti Zanzibar - Suleiman, Madai yao Ya msingi ni kwamba - watu hawa wamefanya mapinduzi ndani Ya Chama kinyume cha katiba Ya ACT. Ni Yale Yale, hivyo hoja juu Ya wivu au uonevu dhidi Ya Zitto ni hoja za kipunguani tu.

Tuhuma zilizopo ni kwamba Akina Kitila wameanzisha kadi Mpya za Chama, bendera mpya, katiba Mpya, nembo Mpya Ya Chama, na vyote hivi ni tofauti na vile vinavyotambuliwa Rasmi na Ofisi Ya msajili wa vyama vya Siasa.

Mwigamba alitangaza mkutano mkuu wa ACT kwamba ni Machi 28, na inasemekana Zitto ndio angetangazwa Rasmi kuwa mwenyekiti wa ACT taifa, kinyume na demokrasia ambayo alikuwa anaililia Chadema.

Zitto anastahili kuyapata yakiyomkuta, hana wa kumlaumu bali yeye mwenyewe. Mbaya zaidi ni kwamba anaonyesha Aidha alidhania yeye ni mkubwa kuliko Chama au hakuwa na uelewa nini katiba Ya Chama chake "cha zamani" Chadema inasema nini, kwa mfano, ipo kanuni Ya kusimamia shughuli, mwenendo, na maadili Ya wabunge wa Chadema (2006) ambayo Zittto na wenzake walishiriki kuziweka. Zinasomeka hivi:

"Chadema itashughulikia matatizo Ya Viongozi na wanachama kwa Kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa katiba ya Chama, wala hata siku moja haitashughulikia mambo hayo mahakamani. Mwanachama atakayeshindwa Kufuata utaratibu wa Ngazi za Chama hatavumiliwa na atafukuzwa uanachama."

Kipengele hiki hakikuwekwa ili Kuja kumshughulikia Zitto bali kiliwekwa kwa maslahi Ya Chama, miaka mingi tu Kabla hata Akina Zitto hawajaja na waraka wa mapinduzi.

Jaji Utamwa amekubaliana na hoja zilizowasilishwa na mawakili wa Chadema ambao waliomba mahakama ifute kesi Hiyo kwa kuwa inakiuka katiba ya Chama cha Chadema.

Katiba ya Chadema haijamlinda Zitto katika Suala husika bali imemshughulikia kwa uwazi kabisa. Katiba Ya Jamhuri Ya muungano wa Tanzania haimlindi Zitto Bali haimtambui Rasmi kama Mbunge kwani moja Ya masharti Ya mtu kuwa Mbunge kwa mujibu wa katiba ya Nchi ni kwamba ni lazima awe mwanachama wa Chama cha Siasa. Mahakama ambayo ni chombo cha kusimamia haki nayo imeshindwa kumlinda Zitto - rejea hukumu Ya Jaji Utamwa. Katika hali Hiyo Nani atamlinda Zitto? Spika wa bunge? Kwa misingi ipi? Wanachama wa Chadema? Kwa misingi ipi? Wananchi? Kwa misingi ipi?

Zitto was good only when he lasted.
 
Mchambuzi
Ahsante kwa hoja zako. Nichangie kidogo tu kuhusu uliyosema.
Kitila Mkumbo alikuwa mshauri wa Chadema mwelekezaji, Zitto akiwa naibu katibu mkuu na Mwigamba akiwa makao makuu.

Wote walishiriki kupitisha kifungu cha katiba ya CDM ulichokijadili kuhusu mahakama.

Tunakumbuka, Kitila aliaminiwa sana hata kuja na formula ya kupata wabungewa viti maalumu.

Kumbu kumbu zipo hapa tukihoji kuhusu formula iliyotumika.

Leo wale wale waliopitisha sheria za chama hawafahamu zinafanyaje kazi.

Tunaweza kusema wanafahamu bali waliamua makusudi kutozifuata kwasababu maalumu.
Kwamba, ilikuwa ni lazima Zitto aende mahakamani ili kununu muda wa kubaki kama mbunge na kushiriki bunge la katiba.

Walifahamu, katiba ya Chadema walioiandika, na kuiridhia haitoi nafasi kwa Zitto mahakamani.

Walitambua kuwa hata mahakama ingeamua kwa kutoa hukumu dhidi ya Chadema, bado Zitto asingeweza kurudi katika Chadema.

Ukweli wa hilo unaonekana katika historia ya vyama vya siasa nchini.
Hakuna mgogoro uliokwenda mahakamani na wahusika kubaki salama. Si NCCR, CUF, TLP, UDP n.k.

Hivyo, mahakama ilitumika katika kuficha ubinafsi na si kutafuta haki.
Hilo halina mjadala, na ndio msingi wa kusema kuwa, kwenda mahakamani kunammaliza Zitto.

Hoja si kuwa hakuwa na haki, la hasha! haki ya kikatiba kwenda mahakamani alikuwa nayo na anayo sana.
Ukweli wa mazingira, kurudi Chdema ilikuwa haiwezekani.

Lakini pia baada ya kupoteza trust, Zitto angekaa mezani gani na wanachadema wenzake?

Na zaidi ya hapo, Zitto angefanyaje kazi washirika wake 'mentors' wakiwa wameshatafuta ACT?

Kitendo cha washirika kukimbilia ACT kilikuwa na siri moja, walitambua mwendo wa mahakamani ulikuwa ni kudanganya

Huko ACT yanayoendelea yanajulikana. Wamewafukuza waanzilishi wa chama kwa mwendo ule ule wanaoulaani kule walikotoka

Washirika na Zitto ni waumini wa kukaa mezani kwa majadiliano. Huko ACT uumini huo umewashinda.

Na dambi ile iliyowaondoa Chadema inajidhihiri. Washirika hukoaACT wameifanya Chadema adui namnba moja.

Wamechukua mistari ya CCM ya ukanda, ukanda ule ule ulioandikiwa formula na Kitila akiwa mshauri wa Chadema

Wasichokiona ni ACT kubeba mzigo wa ukanda siku za mbeleni.
Nani asiyejua ACT ipo Kigoma? Je, dhambi hiyo itakapowarudi watakuwa wameonewa?

Chuki dhidi ya chama chao inajidhihirisha kutokana na mwenendo wa ACT kuona Chadema kama ndilo tatizo lao na kufumbia macho tatizo halisi. Mbele ya safari itawagharimu sana.

Huko waliko, washirika na wapambe wanasema Zitto ameonewa wakitaja sababu za ukanda n.k.

Wasichokionyesha kwa uwazi ni wapi Zitto ameonewa?

Wasichokijadili ni matatizo yaliyotokana na Zitto na wao ndani ya Chadema.
Hakuna mgogoro wa Chadema uliotokea bila mkono wao, hakuna!

Hilo halisemwi, kinachosema ni kuonewa bila kuonyesha ni wapi.

Na kama walionewa Chadema, je mahakamani nako wameonewa na nani?

Ni wakati wa kulea viongozi wa taifa hili wawe na hekma, busara, maono na uadilifu.

Siasa za kubabaisha umma ndizo zimetufikisha hapa kama nchi masikini duniani.

Kukaa kimya bila kusema ukweli ni kudhulumu nafsi zetu, kuonea kizazi cha sasa na kurithisha matatizo kizazi kijacho.

Hapana! ni wakati wa kusimama kuhesabiwa katika ukweli.
 
Ni kweli ni maoni yako. Ila bahati mbaya sana sikubaliani nayo.

Kichwa cha uzi huu kinasema" Duru za Siasa: Chama cha ACT-Mpini wa CCM kumaliza Upinzani". Kichwa cha uzi huu kinatoa uhalali wa mada hii kumjadili Zitto Buyagwa Kabwe (Sijajua kwa nini siku hizi hapendelei jina la Zuberi litumike kwenye utambulisho wake). Nitaeleza.

Buyagwa ni mwanasiasia anayetuhumiwa kushirikiana na CCM kukiangamiza Chadema (rejea post mbalimbali hapa JF zinazomuhusu Buyagwa/Zitto). Buyagwa ni mwanasiasa ambaye ametimuliwa na wenzake (Mwigamba; Mkumbo) amabao walikuwa wote CHadema ila sasa wao wameamia ACT wakati yeye bado hajasema mstakabali wake kisiasa baada ya jana kufutwa rasmi uanachama wa Chadema. Kumbuka kilichosababishwa kutimuliwa watatu hao (Buyagwa,Mkumbo, na Mwigamba) ni kuandaa mkakati wa kuuangusha uongozi wa sasa wa Chadema ili 'Akili Kubwa' iweze kuendesha chama yaani Buyagwa awe Mwenyekiti wa Chadema. Kumbuka pia Chadema ni chama cha Upinzani.

'Bahati' haikuwa yao mpango haukufanikiwa wakaamia (Mwigamba,Mkumbo) chama cha siasa kiitwacho ACT. Minong'ono kutoka ACT ikabainisha wahamiaji kutoka Chadema (Mwiga na Mku) wanataka kupindua uongozi wa ACT uliopo ili wampe Buyagwa uongozi huo. Hili liliingia akilini maana mkakati uliowafanya watimliwe Chadema ni huo. Songombingo za ACT kwa sasa karibu kila mfuatiliaji wa habari za siasa nchi anazijua.

Mkuu mpaka hapo unaweza kuona ilivyo ngumu kukwepa kumjadili Buyangwa (a.k.a Zitto) na umahakama na usiasa wake kwenye uzi huu. Ukiunganisha nukta vizuri utagundua kuwa Nguruvi3 yuko sahihi kuendeleza mjadala huu akimuhusisha Buyagwa na 'timbwili timbwili' zake za kisiasa.

Pia na mimi haya ni maoni yangu, unaweza kuyakubali ama kuyakataa.



Sawa, na wewe Wasalaamu huko '
nchini Zanzibar'.

Wabilah Tawfiq !


TUJITEGEMEE.

Nafikiri hata CHADEMA wenyewe unawatumia katika kujenga khoja zako kwenye magazeti ya LEO huko Tz wameweka bayana HAWANA MUDA WA KUMJADILI ZZK kwani wana mambo mengi.

Lakin nilitaka nikupe angalizo moja,Katiba ya Tz ya 1977 imebainisha wazi kuwa Katiba yoyote au sharia yoyote ya Chama chochote au kikundi chochote cha kijamii inayomzuia mtu yoyote kwenda mahakamani kudai haki yake kwa kuona imekiukwa au inaelekea kukiukwa, katiba au Sharia hiyo inakuwa batili tangu mwanzo wake (Null and Void ab initio)

Na hakuna sharia ya Tz iwe ya chama cha kisiasa au kijamii au inayotungwa na Bunge inayoweza kuwa juu ya Katiba mama ya TZ.

Binafsi nilikuwa sawa kabisa na mtazamo wa CHADEMA kuwa si wakt wa malumbano na ZZK bali ni wakti wa kuangalia mambo mengine makubwa ya kiuchumi na kijamii na hata kujipanga na uchaguzi mkuu kwa kuimarisha safu zao za kiuongozi na ulinzi na hata kusaidiana na Serikali yenu kupambana na kuzuia mauaji ya Albino.

Na vile vile nafikiri umesikia Principal Justice (Jaji Kiongozi ) wa JMTz ameliitisha jalada la Kesi ya ZZK na kutaka kufanya Review. Sasa lolote linaweza tokea.

Kifupi mpe nafasi ZZK atafakari na wanasharia wake waangalie nini cha kufanya. Sisi tujadili mengine ikiwemo hili la aibu na fedhweha kwa Tz la mauaji ya Albino huko kanda ya Ziwa.

Pole sana.

 
SAKATA LA ZITTO

YAMETIMIA YALIYOANDIKWA DURU


Kwa wafuatiliaji,sakata la Zitto na washirika wake limeongelewa katika nyuzi hii na nyingine kwa kina na nukta
Yote yaliyozungumzwa yametimia, hatimaye Zitto amejiunga na ACT kama mkakati ulivyokuwa, amefanikiwa kununua muda wa ubunge akijua matokeo yake, na sasa anaendeleza jitihada za kisiasa kwa mitazamo tofauti

Tulisema, mgogoro wa ACT ulitengenezwa na washirika wa Zitto kumuandalia nafasi walioitaka kuanzia walipokuwa CDM
Tulifafanua kuwa, haraka za mkutano wa ACT ziliambatana na muda wa Zitto kujiunga na maandalizi ya uchaguzi mkuu
Hakuna kilichokwenda tofauti na tuliyoongea. Haukuwa utabiri ni jambo lililojulikana ingawa linadhaniwa liliandaliwa kifundi

Katika wiki mbili na ushee, Zitto amekuwa katika mitandao na vyombo vya habari akieleza hatma yake
Kilichoitwa hotuba ya kuaga wabunge ilikuwa ni sehemu ya mbinu za kuendeleza siasa na pengine kuponya majeraha

Kwa uapnde mwingine, ilikuwa maandalizi ya wapenzi wake kumfuata huko aliko(rejea makundi katika bandiko #154 lililozungumzia kundi la kwanza)

'Hotuba yake bungeni' ilizungumzia kwa ufundi sana namna alivyoishi na wenzake na yale aliyoyafanya. Ikagusia kuhusu kufukuzwa, na wakati huo huo ikimwelezea kama aliyeng'atuka. Hotuba hiyo haikuzungumzia matatizo yake na chama chake, bali kumjenga kama mtu aliyeonewa, na hivyo kutafuta 'sympathy'

Zitto anatambua kuwa kuisema CDM kutaamsha majeraha aliyojisababishia kisiasa kwa majibu asiyopenda yarudiwe midomoni mwa watu. Hata hivyo, wapambe wake wanazidi kumweka katika wakati mgumu pale wanapoituhumu chadema

Ni wakati mgumu kwasababu Zitto asingependa mgogoro uliomfikisha hapo uzungumzwe mara nyingi kwa kutambua unatonesha vidonda vya kisiasa.

Kwa upande mwingine, huo ni mkakati maalum ili asionekane kama mhujumu wa kambi ya upinzani. Iwavyo iwe, Zitto na wapambe wake wanatakiwa wachukue muda kuitathmini kwa kutoa muda wa majeraha kupona

ZITTO ACHUKUA KADI

Zitto amechukua kadi ya ACT katika tawi la Tegeta kama mwanachama mwingine. Huu ni mkakati wa kisiasa uliolenga kupunguza joto la kisiasa na mogoro unaovuma katika chama chake.

Isingekuwa busara kama angechukua kadi hiyo makao makuu, hilo lingewewapa ACT original nafasi ya kuendeleza mgogoro kwa kusema, ACT wahamiaji wamekuja na mtu wao

Na wala isingekuwa busara kuchukua kadi kutoka Kigoma, kwani kufanya hivyo kuendeleza ile hali ya ACT kuwa chama cha Kigoma, jambo ambalo linegkinzana na hoja za Ukanda walizolalamikia miaka mingi.

MKUTANO WA HABARI
Kama ilivyoandikwa na kama haitabadilika, Zitto atakuwa na mkutano na wana habari Serena Hotel
Wengi wanataraji Zitto kuanza kuiandama Chadema.
Wanaofikiri hivyo wamepotoka

Kinachotarajiwa ni Zitto kujitambulisha kama mwanachama,kutimiza ahadi ya kueleza hatma yake kama livyowahisema

Pia atatumia nafasi hiyo kujieleza kama mwanachama anayejiunga kama mwingine ili kuondoa wingu la ujio wake kama linavyojulikana 'uenyekiti''

MKUTANO WA ACT

Mkutano mkuu kama unavyotarajiwa utafanyika siku za karibuni wakati Zitto akiwa mwanachama.
Hizo ndizo hesabu zilizofanyika kuanzia mwanzo na kuleta mtafaruku mkubwa ndani ya ACT.
ACT Wahamiaji walijua ujio wa Zitto, na ACT original walijua ujio wake ni wa uenyekiti

Isitegemewe kuwa Zitto atapewa nafsi yoyote ya uongozi. Pengine hata ujumbe wa kamati muhimu hatapewa

Yote yanafanyika kuondoa hisia,ujio wake ulikusudiwa na kwamba mgogoro ni uenyekiti

Asijedhani awaye kuwa Zitto atachukua uongozi wa chama cha ACT

Pamoja na yote hayo, Zitto atabaki kuwa mtu mwenye nguvu ndani ya ACT bila wadhifa unaojulikana.

Inaeleweka ni muda mfupi kuelekea uchaguzi mkuu na hakuna matumaini ya Zitto kugombe nafasi ya Urasi.
Lengo ni Zitto kuwa mwenyekiti siku za usoni na hesabu hizo zinafanywa kiufundi sana.

Nafasi anayotajiwa kugombea ni ubunge. Haijulikani ni eneo gani, lakini yatosha kusema harakati na haraka zote ni kutengeneza mazingira ya kurejea bungeni na kumuandaa kwa uenyekiti siku za usoni. Kundi la ACT wahamiaji lina mtazamo huo kuanzia CDM

ACT wahamiaji ni sehemu ya kundi la kwanza(rejea bandiko 154) wakiamini kuwa Zitto alizaliwa kuwa mwenyekiti wa vyama vya siasa. Kundi hilo halina sababu za msingi bali mapenzi ya dhati kwa Zitto. Ni kundi lisiloweza kubadilisha msimamo wala kubadilishwa, linaamini katika Zitto na hakuna namna nyingine kwao isipokuwa Zitto

Nini kinafuata miezi miwili ijayo?
Nani ataathirika na hali ya mambo kama ilivyo

Itaendelea...
 
tunashukuru wachambuzi wetu ..mnatutendea haki na natamani watanzania wengi wangekuwa wanapata wasaa wakupata vitu adimu kama hivi.. kuna upotoshaji mkubwa sana unaendelea na hii kwa sababu ya watanzania tuliowengi hatupendi kabisa kujishughulisha na mambo ya msingi ya taifa letu...
 
Zitto ni mwanasiasa na siasa zetu ni za vyama,kama amefukuzwa CDM je hasijiunge na chama cha Siasa Zitto alishatambua kuna wachache wanatamani hasichomoze tena kisiasa. ndomana na yeye anaishi kwa kujipanga tena yenye akili ..mda mwingine ishu ya Zitto nafafanisha na watu wanaomchukia diamond kwa sababu mafanikio yake,wasiompenda wamejikuta kazi yao kutafuta mabaya yake ,kana kwamba hakuna zuri wamefanya,na ukiona wanatoa ushauri,Mara nyingi ni ule wa kumtaka awe mnyonge
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,nakushukuru sana kwa uzi wako huu wewe na wadau wote kama akina Mchambuzi, Jitegemee na wengineo kuanzia kipindi cha mgogoro mpaka sasa, mekua kama watabiri juu ya hitimisho la waraka wa usaliti kwenye chama kikuu cha upinzani CDM.

Ni kweli ile project ya akina Kitila na Mwigamba Zitto ni muhusika mkuu kama mlivyochambua na mipango yake yote, sasa ni kweli yametimia na wale walio kuwa wanamtetea Zitto na genge lake wameona dstination yao na mipango yao.

Nina mambo mawili ya kuchangia, moja kupongeza na moja kukosoa,
kwanza niwapongeze CDM kwa maamuzi magumu waliyoyafanya na kuonyesha always taasisi ni kubwa kuliko mtu, niseme tu kwa chochote kitakachowapata hata kama ni kupoteza baadhi ya wafuasi wao, stil wasete standard kwamba taasisi na misingi yake iheshimiwe na sio kumwabudu mtu kwamba atau chama, haya yaliwaponza sana NCCR na hata TLP, hata kama ni nani awajibishwe kwa misingi ya chama.

Lakini pia niwakosoe CDM kwa namna walivyo handle isu ya Zitto hasa hapa mwishoni, walikua tu emotional na kupanick kusiko na maana, Zitto issue was closed since last year alipoenda mahakamani,mhawakua na haja ya kuitisha mi pres comference za mbwembwe kama walikua wanashindana nae, kiukweli wameishia kumpa publicity ya bure na isiyokua na sababu,
nadhani kwa mtazamo wangu Tundu Lissu aangaliwe saidi, asipewe majukumu yanohusu Siasa kudili nayo kama hili la zitto, hakutakiwa kuwa too emotional kwenye suala linalijieleza kamanlile.

Narudia tena kukushukuru Nguruvi3 na wadau wote wa Duru kwa michango yenu very productive.
 
Hivi niulize, Zitto alipofukuzwa Chadema walitegemea atafanya nini? arudi Kigoma kuwa mkulima au akatafuta kazi za maofisini? jamani mwanasiasa yeyote ambaye anataka kufanya mageuzi ya kijamii lazima kwanza ajiunge na chama cha siasa na kikubwa zaidi vision yake iwe ktk mrengo anao uafiki kwa ndio njia pekee ya kuwaletea wananchi mendeleo.

Zitto lazima angejiunga na chama cha siasa sasa chama gani hilo ndio wengi walikuwa wakisubiria japo ilijulikana wazi kwamba baada ya kufukuzwa walianzisha chama chao ili kuendelea Fikra na ndoto zao ktk kumkomboa Mtanzania na sio kuivuruga Chadema. Chadema itajivuruga yenyewe maana kuondoka kwa Zitto sii mwisho wa Chadema na sio tu waliamini hivyo bali walijiandaa kwa hilo.

sasa nashangaa sana kuwasoma watu mkisema ACT na Zitto ni Mpini wa CCM ilihali Mapinduzi waotaka kuyafanya ndani ya Chadema na sio kuiweka Chadema chini ya CCM. Mapinduzi walotaka kuyafanya yalihusu utawala wa chama ambao kulingana na katiba na kanuni za Chadema sii lazima wawe viongozi wa Kitaifa. Mwenyekiti sii lazima awe mgombea Urais. Tumeona ya Dr.Slaa na tulitegemea pia mwaka huu atachaguliwa mgombea na sio lazima atoke kati ya wajumbe wa kamati kuu.

I mean mimi nashindwa kabisa kuwaelewa Watanzania maana mliwafukuza mkijua watajiunga na chama kingine hawatakomea hapo maana hawa ni wanasiasa na maisha yao yamejengeka ktk siasa, halafu leo wameamua kutojiunga na chama kingine chochote, bali waendeleze azma yao wenyewe kwa kuunda chama chao imekuwa shida kwenu, kwani hamkujua kwamba hawa watu wataendelea kuwepo ktk SIASA? Yaani kufukuzwa Chadema ndio mlitaka wafikwe na mabaya na uwe mwisho wao!. Kwa nini sisi watu maskini wa roho na mali siku zote ni kuombeana mabaya tu, hakuna mtu anafikiria kumtakia mema mwenzake!.
\- Hizi ndizo huitwa akili ndogo..
 
Back
Top Bottom