Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Hutuitaji kutafsiri "Wakati watu wa Kigoma wanapigwa mabomu kwa kutaka mageuzi watu wa ARusha, Singida, Iringa walikuwa wanakumbatia watawala.. hapa hakuna lugha ya picha bali ni ujumbe wa moja kwa moja kwenda kwa watu wa Iringa na nk.. "Laiti kama angesema baadhi ya watu" "bila kutaja mikoa" hapo walau tungeweza kusema anawalenga wabaya wake ambao ni viongozi wa Chadema. Kitu ambacho ni kawaida kwa siasa zetu za maji taka.
Lakini unapotaja watu wa sehemu fulani wako hivi au vile huwezi kusema hii ni lugha ya picha iwe umeitaja kwa mbaya au kwa mazuri.

Pia bado sijaona uhusihano wa speech ya Obama na speech za Zitto , Obama ametumia msemo na huu msemo ameutumia kwa kumlenga mtu mmoja ambaye kila mtu ni anamfahamu kuwa ni Bi.Hilaly. Hebu niambie kama huu msemo angeutumia kwa kumaanisha wakazi wa Mississipi au Carifornia hali ingekuwaje? Na hapo ndo point yangu ilipo kuwa iwe ni lugha ya picha kama unavyotafsiri yaani uongo au laa swali langu liko pale pale ni kweli watu wa Iringa, Arusha na Singida wanamidomo mrefu au ( waongo) (lugha ya picha)?

Niliishatoa maelezo marefu sana juu ya hili,dunia haisimami,tuangalie mengine.

wale watu waliokuwa na hisia kuwa "wachaga wanakwapua fedha za mikoa fulani na kuzipeleka makwao na ndo maana wanakuwa na maendeleo zaidi ya maeneo mengine, SI KWELI BALI WATU WA ARUSHA/KILIMANJARO MAENDELEO YAO YAMELETWA NA JUHUDI ZAO

"wachaga" , Wamedhalilishwa, kuna watu walienda mbali zaidi na kusema kuwa wanakwapua pesa za maendeleo ya mikoa mingine wanapeleka kwao, kuwa wachaga wamejazana TRA na nk.

Kama u mkweli utakubaliana nami kuwa Zitto hajasema popote kuwa kuna mkoa wowote unaounyonya mkoa mwingine,hajataja kabisa kanda yoyote, alitoa takwimu za nchi nzima,akitoa mifano ya baadhi ya mikoa,alitaja mikoa ya pande zote za nchi, huwezi kurasimisha kwenye KANDA MOJA,unless una lako jambo.

Kama u mkweli wa nafsi yako utakubaliana na mimi Zitto hajaongea neno/maneno yoyote ya kuwabagua watu wengine (juu ya mapato), wewe mwenyewe unasema hapa kuwa ni tafsiri za baadhi ya watu ndio zilikwenda huko, na mbaya zaidi ata ma-great thinker hapa wakazitafsiri kwa tafsiri zao hizohizo zilizosukumwa na chuki za kisiasa na kuzipa jina la "ZItto kasema".Hili ni kosa. Mjadala wote huu umejikita kwenye msingi huu mbovu.

Na jambo la kusikitisha wewe niliyekuona katika huo mjadala ukikemea ubaguzi wa wazi ulionyeshwa bali ulikaa na kunywa Chai, au soda au bia huku huku ikushangilia kuona watanzania wenzako wakidhalilishwa kutokana na kauli za fitina na chuki za Zitto.

Hapa kweli siwezi kushangaa kuhusu tafsiri za hayo ya Zitto maana napata picha hapa jinsi ulivyo na uwezo wa kudhania, mpaka kwenye keyboard yako ukaweza "kuniona nikishangilia"!!hisia hisia hisia

kwa makusudi Zitto aliona reaction ya watu juu ya kauli yake Lakini hakujitokeza kusema "jamani sikumaanisha hivyo au sikujua kuwa watu wangechukulia hivi bali nimaanisha hivi na vile.. Zitto alikaa kimya akifurahi watu wakibaguana na kudhalilishana.

Na Zitto nae katu hakuwezi kujificha, kupitia keyboard yako uliweza kumuona jinsi anavyokuwa akifurahia watu wakibaguana!!hisia hisia hisia.

Yaan tupo page ya 66 lakini msingi wa hoja yenyewe upo kwenye hisia, tunahisi "alimaanisha hivi", "tunahisi anauchukia na mkoa wa nyumbani kwetu", "tunahisi analichukia kabila letu","tunahisi hatupendi sisi watu wa huku", "tunahisi anaona sisi tunapendelewa", "tunahisi kuwa alimaanisha kuwa mchango wa mapato wa mkoa ndio KIGEZO PEKEE cha maendeleo", msisitioz "KIGEZO PEKEE".

Hoja kubwa kama hii haiwezi ikasimama kwenye jukwaa la great thinkers kwa muda wote huu na msingi wake TUNAHISI TU.

Sasa kama wewe ambaye akina Nguruvi ndio wanakufanya msahafu wa kutoa habari za "ndani" za Zitto(refer Udini/Ubaguzi) na hapa unahisi tu sasa vip wao?maana wewe ndio reference ati.

Ila tatizo lako ni baada ya Nguvuri3 kuona hizo sitofahamu na kuamua kutumia muda wake ambao labda angeutumia kufanya shughuli zake za kujiongeza kipato na kuleta hoja hapa ya kupingana na Zitto juu ya fitina zake na uongo.

Nikukumbushe aliyeleta kauli ya Arusha Kili vs Shinyanga si Alinda wa Nguruvi3 ni Zitto Kabwe...

Zitto kaleta pambano la Arusha Vs Shinyanga? ajabu hii, unarudia kumaanisha kuwa Zitto hakupaswa kutaja jina la Kilimanjaro kwenye mfano wake lakini angetaja Lindi sio kosa, maana hakuna mtu kalalamika kutajwa kwa Lindi na hatujaona watu wa Lindi wakilalamika kutajwa mkoa wao, vip Kilimanjaro?kuna nini mpaka ilete maneno yote hayo kwa kutajwa tu Kilimanjaro?hii ndio inaleta picha ya tatizo mahsusi.

Tatizo sio mfano huo bali tatizo ni kuutaja mkoa wa Kilimanjaro, kuwa mwanasiasa asiyetoka Kilimanjro haruhusiwi kutoa mfano wa mkoa wa Kilimanjaro?hizi hisia zenu za uzalendo kwa mkoa badala ya taifa mnapaswa ni ishara ya upungufu wa Utanzania na ndio maana mnaspin kila kitu ili kutafuta excuse ya kujenga hisia kupitia mgongo wa mtu mwingine, kwenye hii thread Zitto, ili kuepuka kuonyesha sura zenu halisi.

Muda huu ungetumika vizuri zaidi kujenga utaifa badala ya kujenga Ukaskazini kulikoshamiri kwenye thread hii, muda huu ungetumika vizuri sana kuitambua mipaka ya nchi ya Tanzania, tanzania moja, isiyo na mipaka ndani yake, thread hii imeonyesha "uzalendo wa dhati" wa baadhi ya watu kwenye maeneo wanayotokea, miaka 54 baada ya Uhuru bado watu hawajaweza kujitambua kwa taifa lao bali wapo sensitive zaidi na kutajwa tu kwa eneo lao na kitu kitu kiwe ata cha kisera wanakitafsiri kwanza kwa mkoa wao.

Hii ni aibu, tutoke huko.
 
Nategemea upofu wa Nguruvi3 na Alinda maana wao mkosaji ni Zitto tu,kama kauli ya mbowe aikua tishio,itawezaje ya Nassari, mpango wao kwa Zitto wanajua wao moyoni kwao

Nguruvi3,

Kwani ni dhambi Kaskazini kuwa na Taifa lao na kwenda huko watu wa maeneo mengine mpaka tuwe na Visa daah!!!.

Soma hapa chini kiduchu mwambie na Alinda.

Huyu Nassari hakuchukuliwa hatua yeyote na chama chake inaoneka huu ni mpango maalum wa Chadema Nassari hakusema haya maneno kwa bahati mbaya alikuwa anajua anachokisema kauli kama hizi za kuwagawa Watanzania Nguruvi3 na Alinda hata siku moja hamuwezi kuzikemea na mnaweza kujenga hoja kuitetea.

Chadema wanataka taifa lao la kaskazini bado tunawachekea hawa watu wanataka kutupeleka wapi wanataka Tanzania tuigawane vipande vipande.

Audio: https://www.youtube.com/watch?v=1fPJYAeUy-4

Sina uhakika kama huu Ukaskazini unaojengwa kwenye thread hii unahusiana na huu wa Nassari.

Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe alikuwepo pia kwenye mkutano huo.
 
Audio: https://www.youtube.com/watch?v=1fPJYAeUy-4

Sina uhakika kama huu Ukaskazini unaojengwa kwenye thread hii unahusiana na huu wa Nassari.

Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe alikuwepo pia kwenye mkutano huo.
Kapwela

Hoja zako hazijibu hoja zilizo mbele yetu

Kukaa kimya ni kuruhusu uhuni wakisiasa wa viongozi, wengine wakuu, kuhalalishwa kwa hoja zisizo na mashiko.

Kama utakumbuka hoja za Nassari zilikuwepo katika jukwaa la siasa.
Sijui kama unakumbu kumbu ninikiliongelewa. Hebu pitia makabrasha kwanza upate uelewa
.

Umeshauriwa sana , kwanza upate uelewa ili uje kwampangilio.
Unadandia hoja za spinning zilizopuuzwa na kuonekana upo
nje ya mstari.


Hoja za Zitto hazijibiwi na hoja za mtu mwingine.
Kwamba,yupo aliyesema abcd na hivyo inajibu hoja za kiongozi mkuu ni udhaifu wa kushindwa kumtetea


Maswali yameulizwa, je kiongozi mkuu anaposema alitaka uenyekiti kwasababu si ''dhambi kwa Mkigoma kuwa mwenyekiti'' ilikuwa muafaka''

Je, uenyekiti wa chama chake cha zamani ndio sababu yamgogoro ?
Je, aliwaeleza wananchi waraka ulikusudia nini na ushiriki wake katika vurugu za chama chake?

Wakati kauli zinatolewa, kiongozi mkuu alikuwa ndani yachama, je, aliwahi kukemea

Wakati ukitafakari hayo, mnawajibu wa kuelewa, maneno yakiongozi mkuu wa chama hayajibiwi na hoja za mtu mwingine.

Kwamba, Nassari akiongea fyongo basi inajaenga uhalali wa mtu mwenye miaka 20 ya kisiasa kuvurunda, inasikitisha

Manchotakiwa ni kujibu hoja zinazomkabili. Hoja zinazotokana na kauli zake za kutaka kulibomoa taifa.

Kiongozi mkuu hachaguliwi kwasababu ''si dhambi mkigoma kuwa mwnyekiti au supreme wa ACT''
 
Audio: https://www.youtube.com/watch?v=1fPJYAeUy-4

Sina uhakika kama huu Ukaskazini unaojengwa kwenye thread hii unahusiana na huu wa Nassari.

Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe alikuwepo pia kwenye mkutano huo.
Mkuu Kapwela msikilize kwa makini Joshua Nassari anasema kwa uchungu sana anasema Kaskazini wataishi kama Ulaya.

Anaenda mbali zaidi anataja na Baraza la Mawaziri la nchi ya Kaskazini akimteua Lema kama waziri mkuu wa taifa la kaskazini.

Anasema wana kila kitu daah!!!wana mbuga za wanyama wana mlima Kilimanjaro nk... mkuu wangu Kapwela kwenye ili kina Nguruvi3 wanapita mbali umesoma utetezi wake eti hoja zake ziliongelewa jukwaa la siasa kwa hiyo watu wakae kimya mtu anatangaza taifa la kaskazini anawawabagua watanzania Nguruvi3 anaita fyongo eboo!!! Uasi huu unaita fyongo.

Hawa hata siku moja hawawezi kunyanyua vidole vyao kupinga ili maana wao ni wamoja wamo kwenye huu mpango wa taifa la kaskazini.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kapwela msikilize kwa makini Joshua Nassari anasema kwa uchungu sana anasema Kaskazini wataishi kama Ulaya.

Anaenda mbali zaidi anataja na Baraza la Mawaziri la nchi ya Kaskazini akimteua Lema kama waziri mkuu wa taifa la kaskazini.

Anasema wana kila kitu daah!!!wana mbuga za wanyama wana mlima Kilimanjaro nk... mkuu wangu Kapwela kwenye ili kina Nguruvi3 wanapita mbali umesoma utetezi wake eti hoja zake ziliongelewa jukwaa la siasa kwa hiyo watu wakae kimya mtu anatangaza taifa la kaskazini anawawabagua watanzania Nguruvi3 anaita fyongo eboo!!! Uasi huu unaita fyongo.

Hawa hata siku moja hawawezi kunyanyua vidole vyao kupinga ili maana wao ni wamoja wamo kwenye huu mpango wa taifa la kaskazini.

Kuna tatizo kubwa sana hapa.

Nimeuona kwenye thread hii uzalendo wa dhati wa watu hawa kwenye hiyo nchi ya kufikirika ya "Kaskazini" wakijificha kwenye "Zitto kasema".
 
Last edited by a moderator:
Kapwela

Hoja zako hazijibu hoja zilizo mbele yetu

Kukaa kimya ni kuruhusu uhuni wakisiasa wa viongozi, wengine wakuu, kuhalalishwa kwa hoja zisizo na mashiko.

Kama utakumbuka hoja za Nassari zilikuwepo katika jukwaa la siasa.
Sijui kama unakumbu kumbu ninikiliongelewa. Hebu pitia makabrasha kwanza upate uelewa
.

Umeshauriwa sana , kwanza upate uelewa ili uje kwampangilio.
Unadandia hoja za spinning zilizopuuzwa na kuonekana upo
nje ya mstari.


Hoja za Zitto hazijibiwi na hoja za mtu mwingine.
Kwamba,yupo aliyesema abcd na hivyo inajibu hoja za kiongozi mkuu ni udhaifu wa kushindwa kumtetea


Maswali yameulizwa, je kiongozi mkuu anaposema alitaka uenyekiti kwasababu si ''dhambi kwa Mkigoma kuwa mwenyekiti'' ilikuwa muafaka''

Je, uenyekiti wa chama chake cha zamani ndio sababu yamgogoro ?
Je, aliwaeleza wananchi waraka ulikusudia nini na ushiriki wake katika vurugu za chama chake?

Wakati kauli zinatolewa, kiongozi mkuu alikuwa ndani yachama, je, aliwahi kukemea

Wakati ukitafakari hayo, mnawajibu wa kuelewa, maneno yakiongozi mkuu wa chama hayajibiwi na hoja za mtu mwingine.

Kwamba, Nassari akiongea fyongo basi inajaenga uhalali wa mtu mwenye miaka 20 ya kisiasa kuvurunda, inasikitisha

Manchotakiwa ni kujibu hoja zinazomkabili. Hoja zinazotokana na kauli zake za kutaka kulibomoa taifa.

Kiongozi mkuu hachaguliwi kwasababu ''si dhambi mkigoma kuwa mwnyekiti au supreme wa ACT''

Wala usijifiche kwenye kasome, kasome, kasome, hakuna ambacho sikijui kwenye hii thread.

Niliishasema huko nyuma, hayo mambo ya ndani ya Chadema kama haupo kwenye inner-cycle kama nilivyo mie huwezi kuconclude confidently kuwa yapo/hayapo/ukweli au uongo.

Mzee Mtei alipoulizwa juu ya Zitto kugombea Uenyekiti aliwahi kusema wazi na vyombo vya habari vilimnukuu kuwa "hatuwezi kumpa Uenyekiti mtu from nowhere".

Hiyo from nowhere haipo kwenye sifa kikatiba za kuwa Mwenyekiti, sasa sijui from nowhere ni wapi au ni nini, je inaendana na anachosema Zitto hapo?sitaki kuwa mbashiri.

Ila nijuacho ni kuwa mambo ya ndani ya taasisi yoyote, unahitaji kuwa chumba cha ndani huko kuyajua, akina Zitto na Mbowe wanaijua vizuri Chadema kuliko akina sie.

Kujaribu conclude hapa kuwa huko ndani kupoje na ukweli wake ni nin ni kutaka kujifanya wanajimu ambapo bahati mbaya tutaishia tu kwenye hisia zetu ambazo sio lazima ziwe ukweli.
 
Niliishatoa maelezo marefu sana juu ya hili,dunia haisimami,tuangalie mengine.



Kama u mkweli utakubaliana nami kuwa Zitto hajasema popote kuwa kuna mkoa wowote unaounyonya mkoa mwingine,hajataja kabisa kanda yoyote, alitoa takwimu za nchi nzima,akitoa mifano ya baadhi ya mikoa,alitaja mikoa ya pande zote za nchi, huwezi kurasimisha kwenye KANDA MOJA,unless una lako jambo.

Kama u mkweli wa nafsi yako utakubaliana na mimi Zitto hajaongea neno/maneno yoyote ya kuwabagua watu wengine (juu ya mapato), wewe mwenyewe unasema hapa kuwa ni tafsiri za baadhi ya watu ndio zilikwenda huko, na mbaya zaidi ata ma-great thinker hapa wakazitafsiri kwa tafsiri zao hizohizo zilizosukumwa na chuki za kisiasa na kuzipa jina la "ZItto kasema".Hili ni kosa. Mjadala wote huu umejikita kwenye msingi huu mbovu.



Hapa kweli siwezi kushangaa kuhusu tafsiri za hayo ya Zitto maana napata picha hapa jinsi ulivyo na uwezo wa kudhania, mpaka kwenye keyboard yako ukaweza "kuniona nikishangilia"!!hisia hisia hisia



Na Zitto nae katu hakuwezi kujificha, kupitia keyboard yako uliweza kumuona jinsi anavyokuwa akifurahia watu wakibaguana!!hisia hisia hisia.

Yaan tupo page ya 66 lakini msingi wa hoja yenyewe upo kwenye hisia, tunahisi "alimaanisha hivi", "tunahisi anauchukia na mkoa wa nyumbani kwetu", "tunahisi analichukia kabila letu","tunahisi hatupendi sisi watu wa huku", "tunahisi anaona sisi tunapendelewa", "tunahisi kuwa alimaanisha kuwa mchango wa mapato wa mkoa ndio KIGEZO PEKEE cha maendeleo", msisitioz "KIGEZO PEKEE".

Hoja kubwa kama hii haiwezi ikasimama kwenye jukwaa la great thinkers kwa muda wote huu na msingi wake TUNAHISI TU.

Sasa kama wewe ambaye akina Nguruvi ndio wanakufanya msahafu wa kutoa habari za "ndani" za Zitto(refer Udini/Ubaguzi) na hapa unahisi tu sasa vip wao?maana wewe ndio reference ati.



Zitto kaleta pambano la Arusha Vs Shinyanga? ajabu hii, unarudia kumaanisha kuwa Zitto hakupaswa kutaja jina la Kilimanjaro kwenye mfano wake lakini angetaja Lindi sio kosa, maana hakuna mtu kalalamika kutajwa kwa Lindi na hatujaona watu wa Lindi wakilalamika kutajwa mkoa wao, vip Kilimanjaro?kuna nini mpaka ilete maneno yote hayo kwa kutajwa tu Kilimanjaro?hii ndio inaleta picha ya tatizo mahsusi.

Tatizo sio mfano huo bali tatizo ni kuutaja mkoa wa Kilimanjaro, kuwa mwanasiasa asiyetoka Kilimanjro haruhusiwi kutoa mfano wa mkoa wa Kilimanjaro?hizi hisia zenu za uzalendo kwa mkoa badala ya taifa mnapaswa ni ishara ya upungufu wa Utanzania na ndio maana mnaspin kila kitu ili kutafuta excuse ya kujenga hisia kupitia mgongo wa mtu mwingine, kwenye hii thread Zitto, ili kuepuka kuonyesha sura zenu halisi.

Muda huu ungetumika vizuri zaidi kujenga utaifa badala ya kujenga Ukaskazini kulikoshamiri kwenye thread hii, muda huu ungetumika vizuri sana kuitambua mipaka ya nchi ya Tanzania, tanzania moja, isiyo na mipaka ndani yake, thread hii imeonyesha "uzalendo wa dhati" wa baadhi ya watu kwenye maeneo wanayotokea, miaka 54 baada ya Uhuru bado watu hawajaweza kujitambua kwa taifa lao bali wapo sensitive zaidi na kutajwa tu kwa eneo lao na kitu kitu kiwe ata cha kisera wanakitafsiri kwanza kwa mkoa wao.

Hii ni aibu, tutoke huko.

Hayo yote uliyoandika hakuna kitu kipya. Yote tumeisha yasoma katika thread hii. Labda tu kuna maswali ambayo hajajibiwa hivyo naomba ufafanuzi ili tupate mwanga zaidi.

Je uchangiaji wa pato la taifa, kunahusikaje na maendeleo ya sehemu husika??

Video ambao mpaka sasa sijapata majibu ya kujitosheleza: Je ni kweli kuwa wakati watu wa Kigoma wanapigwa mabomu, watu wa Iringa, Singida na Arusha walikuwa anakumbatia watawala?


NB:
Kuna audio nimeisikiliza leo na kwa bahati mbaya sana Invisible wamefuata huo uzi. Nimesikliza sehemu moja 1 na kabla ya kuitolea comment ningependa kusiliza sehemu ya 1 na ya 2..Kwa mwenye nayo naomba atuwekee hapa au anitumie kwenye email yangu.
 
Last edited by a moderator:
Nategemea upofu wa Nguruvi3 na Alinda maana wao mkosaji ni Zitto tu,kama kauli ya mbowe aikua tishio,itawezaje ya Nassari, mpango wao kwa Zitto wanajua wao moyoni kwao
Adharusi Unachotaka kusema ni nini? Kwamba Zitto, Mbowe na Nassari ni wakosaji (wabaguzi) ila tatizo lako ni kwamba hatujamkea Mbowe na Nassari? Na tukiwakemea Mbowe na Nassari basi utakubaliana na sisi kuwa Zitto ni mbaguzi?

Kwani kukemea mpaka akemee Alinda na Nguvuri3 tu? wewe huwezi? Hebu anzisha uzi jenga hoja zako juu wa ubaguzi wa Nassary au Mbowe au Slaa tutakuja tu kuchangia na kukemea.
 
Last edited by a moderator:
Adharusi Unachotaka kusema ni nini? Kwamba Zitto, Mbowe na Nassari ni wakosaji (wabaguzi) ila tatizo lako ni kwamba hatujamkea Mbowe na Nassari? Na tukiwakemea Mbowe na Nassari basi utakubaliana na sisi kuwa Zitto ni mbaguzi?

Kwani kukemea mpaka akemee Alinda na Nguvuri3 tu? wewe huwezi? Hebu anzisha uzi jenga hoja zako juu wa ubaguzi wa Nassary au Mbowe au Slaa tutakuja tu kuchangia na kukemea.

Ishu sio kukemea,napata hofu pale mnapojificha KATIKA Utaifa,kumkosoa Zitto,kitu ambacho sikioni,naona kuna kitu kimejificha ndani ya mioyo yenu kutokana na ushawishi wa Nguruvi3 binafsi Naamini hakuna uzalendo unapiganiwa kutoka kwenu juu ya matamshi,na siasa za Zitto,mnachotamani Zitto astaafu siasa,au asisikike(Mtazamo wangu binafsi), Tunaona wewe na Nguruvi3 mkitafuta minakasha ya zamani ya Zitto,ila kina Ritz wakifanya hivyo Nguruvi3 utasikia tulishajadili,mbona ishu ya Zitto imejadiliwa,jukwaa la siasa,lakini nguruvi3 hakutosheka akaileta huku GT..
NB sikuwai kuwa mshabiki wa Zitto,nilikua mtu ninae mkosoa sana,upepo ulibadilika pale LEMA alipoleta uzi kumkashifu Zitto nikaona CDM viongozi waandamizi wamekaa kimya,kumbuka Zitto alikua kiongozi,LEMA alikua chini ya Zitto kimadaraka kama NKM,nikafuatilia mjadala ule,na LEMA akaleta thread kibao kumchafua Zitto,SLAA,MBOWE,MTEI,wakawa kimya..binafsi niliona CDM hakuna siasa, ni genge tu la wahuni tu.mfano utasikia Eti Zitto alikua anatoa siri za CHAMA,najiuliza hizo siri zimeathiri vp CDM, na ni Siri gani hizo,kuna baadhi mpaka wasomi nao wanahubiri ili,uwa najiuliza vyama vya siasa vina siri gani,maana kampeni zinafanyika viwanjani,labda km wanataka kufanya mapinduzi
 
Last edited by a moderator:
Mkandara nilikuuliza swali rahisi kabisa kuwa





Kwanza napenda kusahihi hapo kwenye blue si mijitu ni watu.. Ili ni jukwaa la great thinker ni wajibu wetu mimi, wewe na yule kulipa hadhi inalostahili. Haipendizi kuona mtu kama wewe uliyetumia nguvu na mali zako kujenga hadhi ya JF leo hii wewe ndo unakuwa wa kwanza kubomoa ulichojenga kwa mikono yako. Jifunze kutawala "hasira" zako si Hasira zikutawale wewe.


Baada ya hapo tuendelee na mjadala wetu:

Lakini jibu lako haliendani na swali langu, Ila nitakuuliza tena swali lile lile.. Je ni lini Kigoma iliacha kuichagua CCM, na ni lini mikoa mingine ilianza kuchagua vyama vya upinzani?

Kinachobishaniwa si kuwa Kigoma si wana mageuzi, ninachopinga kwa nguvu zangu zote ni ile kauli ya kuwa "Wakati Kigoma wakipigwa mabomu, mikoa mingine walikuwa wanakumbatia watawala" Hii si kweli maana tumeona kuwa uchaguzi wa mwaka 1994 (uchaguzi mdogo) Dr. Amani alishindwa. Mwaka 1995 baada ya Mrema kuleta chachu katika vyama vya upinzani ndo Kigoma waliweza kupata Mbunge na si kigoma pekee bali hata Iringa, Rolya,Vunjo, Arusha, Karatu,Ubungo (kama sikosei) na maeneo mengine.. Hivyo si kweli kuwa mikoa ya Arusha, Singinda na Iringa walikuwa anakumbatia CCM.

Swali la pili Tanzania nzima tunafahamu hakuna mkoa ambao wananchi wake wamedhalilishwa na dola kama Arusha, kuanzia kupigwa viongozi, kufunguliwa kesi za kubambikizwa, kuuawa na nk. Hivi leo hii mbunge wa Arusha anaweza kusimama na kusema wakati watu wa Arusha wanapigwa mabomu watu wa Mwanza, Mbeya, Kagera walikuwa walikuwa wanakumbatia watawala kwa vile tu hii mikoa haikupigwa mabomu?


Kuhusu CCM kuchakakachua kura, hilo ni kweli ninakubaliana nalo ila CCM hawachakachui Kigoma tu bali wanachakachua maeneo yote pale wapinzani wanapolala /au wanapokosa umakini maana CCM wamebobea kwenye wizi.

Kwa hiyo ili si tatizo la wanakigoma peke yao bali ni tatizo la mikoa yote...

Ni kweli chama kimekua na wote tunakubalina kuwa Zitto ana mchango wake mkubwa ndani ya Chadema hilo halina ubishi.. Lakini hiyo si sababu yeye kukiuka utaratibu waliojiwekea (nafahamu hapa utakaja na maelezo marefu khs Mbowe na Zitto
:smile-big🙂

Na kuwa mkongwe kwenye chama si sababu ya wewe kuwasimanga watu waliojinga leo au jana. La sivyo una haja ya kutafuta wanachama wapya maana kwako wewe hawana maana. Kila mwanachama au uwe umejiunga leo kutoka ccm au umejiunga na miaka 16 wote mna haki sawa. Ukikosea utawajibishwa kama wanachama yeyote yule.
Sikia kama unataka kujadili hoja ningependelea uwe unazungumzia mawazio yako wewe na sio kuniongoza mimi niseme nini? Mmi sii mtoto mdogo najua nilichokiandika na kwa maana yake. Mbona nyie mnamwita Zitto Ayatola, mnamuita Zitto Msaliti hili neno msaliti mnalichukulia dogo kwa upande wenu, na hata sisi kutupa majina na makundi lakini hamtaki kutiwa doa lolote.

Hizi fikra za kufikiria unaweza kuwaongoza watu na kuwachagulia waseme nini, kunichukulia mimi kama mwanao ama mtoto mdogo wa kuongozwa ndizo zinazotushinda sisi wengine!. JF ni uwanja huru na kila mwenye mawazo anayaweka wazi, hoja hujibiwa kwa hoja, kosa ni kumtukana mtu. Neno MIJITU ina maana ya watu walokosa UTU katika maamuzi yao ama matendo yao haina maana zaidi ya hiyo na hatupo darasani kiasi kwamba unapomsoma mtu unatafuta makosa yake katika maandishi ili kumfundiusha kuandika vizuri huu ni mjadala pokea hoja na jibu hoja ya mtu, kazi nyingine waachie moderators.. Sorry kama nimekukwaza but please usitake kuniongoza niandike nini humu., sote watu wazima hapa..
 
Sikia kama unataka kujadili hoja ningependelea uwe unazungumzia mawazio yako wewe na sio kuniongoza mimi niseme nini? Mmi sii mtoto mdogo najua nilichokiandika na kwa maana yake. Mbona nyie mnamwita Zitto Ayatola, mnamuita Zitto Msaliti hili neno msaliti mnalichukulia dogo kwa upande wenu, na hata sisi kutupa majina na makundi lakini hamtaki kutiwa doa lolote.

Hizi fikra za kufikiria unaweza kuwaongoza watu na kuwachagulia waseme nini, kunichukulia mimi kama mwanao ama mtoto mdogo wa kuongozwa ndizo zinazotushinda sisi wengine!. JF ni uwanja huru na kila mwenye mawazo anayaweka wazi, hoja hujibiwa kwa hoja, kosa ni kumtukana mtu. Neno MIJITU ina maana ya watu walokosa UTU katika maamuzi yao ama matendo yao haina maana zaidi ya hiyo na hatupo darasani kiasi kwamba unapomsoma mtu unatafuta makosa yake katika maandishi ili kumfundiusha kuandika vizuri huu ni mjadala pokea hoja na jibu hoja ya mtu, kazi nyingine waachie moderators.. Sorry kama nimekukwaza but please usitake kuniongoza niandike nini humu., sote watu wazima hapa..


:A S wink::A S wink::smile-big::smile-big::smile-big: Naona umeamua kunipata za uso!!! Hivi keyboard yako bado nzima?? ooooohh ngoja nisepe maana ukirudi hapa unaweza kunivunjwa taya...
 
Ishu sio kukemea,napata hofu pale mnapojificha KATIKA Utaifa,kumkosoa Zitto,kitu ambacho sikioni,naona kuna kitu kimejificha ndani ya mioyo yenu kutokana na ushawishi wa Nguruvi3 binafsi Naamini hakuna

Kwa hiyo unataka tumpige Zitto kwa kitu ambacho unakiona wewe? Hivi si unafahamu binadamu ni tofauti, unachokiona wewe sicho ninachokiona mimi na hizi tofauti zetu ndo zinafanya dunia iwepo la sivyo maisha yangekuwa boring!!

Kitu cha kujificha ndani ya mioyo yetu hizo ni hisia zako tu, Na hiyo ni haki yako ya msingi kufikiria kile ambacho unapenda kufiria.!!


uzalendo unapiganiwa kutoka kwenu juu ya matamshi,na siasa za Zitto,mnachotamani Zitto astaafu siasa,au asisikike(Mtazamo wangu binafsi), Tunaona wewe na Nguruvi3 mkitafuta minakasha ya zamani ya Zitto,ila kina Ritz wakifanya hivyo Nguruvi3 utasikia tulishajadili,mbona ishu ya Zitto imejadiliwa,jukwaa la siasa,lakini nguruvi3 hakutosheka akaileta huku GT..

Hayo pia ni mawazo wako, hupo huru kufikiria chochote juu yetu..Ila unashindwa kuelewa uwezo wa kuzuia Zitto asifanye mambo yake hatuna, nia ya kumzuia Zitto hasifanye siasa zake hatuna na lengo la kumzuia Zitto hasifanye siasa zake hatuna. Tunachafanya ni kuchambua kauli zake zenye utata na hilo hakuna mtu anaweza kutuzuia kufanya hivyo. Cha muhimu ni kuvumiliana na kama umeona kuna kosa, kosoa kwa hoja na ndo maana ya mjadala. (mdajala lazima uwe na pande mbili zinazopingana)


NB sikuwai kuwa mshabiki wa Zitto,nilikua mtu ninae mkosoa sana,upepo ulibadilika pale LEMA alipoleta uzi kumkashifu Zitto nikaona CDM viongozi waandamizi wamekaa kimya,kumbuka Zitto alikua kiongozi,LEMA alikua chini ya Zitto kimadaraka kama NKM,nikafuatilia mjadala ule,na LEMA akaleta thread kibao kumchafua Zitto,SLAA,MBOWE,MTEI,wakawa kimya..binafsi niliona CDM hakuna siasa, ni genge tu la wahuni tu.mfano utasikia Eti Zitto alikua anatoa siri za CHAMA,najiuliza hizo siri zimeathiri vp CDM, na ni Siri gani hizo,kuna baadhi mpaka wasomi nao wanahubiri ili,uwa najiuliza vyama vya siasa vina siri gani,maana kampeni zinafanyika viwanjani,labda km wanataka kufanya mapinduzi

Kwa hiyo wakati unamkosoa Zitto ulikuwa na lengo la kumfanye astaafu siasa/hasisisike? Kama lengo lako halikuwa hili unapata wapi ujasiri wa kutusema sisi kuwa tunataka astaafu siasa wakati na wewe ulikuwa unamkosoa kama tufanyavyo?

Na je baada ya Lema kuandika upuuzi wake, je yale uliyokuwa unamkosoa Zitto yalibadilika yakawa mazuri?

Kuhusu siri za chama, Hapa duniani hata wewe una siri zako ambazo hupendi mtu afahamu, sembuse chama cha siasa? Yaani wewe siri za chama ni kupindua nchi tu? Muuliza hata Zitto na ACT yake wana siri zao au unafahamu kila kitu kuhusu ACT?
 
Kwa hiyo unataka tumpige Zitto kwa kitu ambacho unakiona wewe? Hivi si unafahamu binadamu ni tofauti, unachokiona wewe sicho ninachokiona mimi na hizi tofauti zetu ndo zinafanya dunia iwepo la sivyo maisha yangekuwa boring!!

Kitu cha kujificha ndani ya mioyo yetu hizo ni hisia zako tu, Na hiyo ni haki yako ya msingi kufikiria kile ambacho unapenda kufiria.!!




Hayo pia ni mawazo wako, hupo huru kufikiria chochote juu yetu..Ila unashindwa kuelewa uwezo wa kuzuia Zitto asifanye mambo yake hatuna, nia ya kumzuia Zitto hasifanye siasa zake hatuna na lengo la kumzuia Zitto hasifanye siasa zake hatuna. Tunachafanya ni kuchambua kauli zake zenye utata na hilo hakuna mtu anaweza kutuzuia kufanya hivyo. Cha muhimu ni kuvumiliana na kama umeona kuna kosa, kosoa kwa hoja na ndo maana ya mjadala. (mdajala lazima uwe na pande mbili zinazopingana)




Kwa hiyo wakati unamkosoa Zitto ulikuwa na lengo la kumfanye astaafu siasa/hasisisike? Kama lengo lako halikuwa hili unapata wapi ujasiri wa kutusema sisi kuwa tunataka astaafu siasa wakati na wewe ulikuwa unamkosoa kama tufanyavyo?

Na je baada ya Lema kuandika upuuzi wake, je yale uliyokuwa unamkosoa Zitto yalibadilika yakawa mazuri?

Kuhusu siri za chama, Hapa duniani hata wewe una siri zako ambazo hupendi mtu afahamu, sembuse chama cha siasa? Yaani wewe siri za chama ni kupindua nchi tu? Muuliza hata Zitto na ACT yake wana siri zao au unafahamu kila kitu kuhusu ACT?

Maisha binafsi najua yana siri,ila kuniambia CDM kuna siri ilo nakataa,sioni siri yoyote KATIKA vyama vya siasa,ila kuna mikutano ya ndani,ambayo sio siri,labda unieleze siri gani Zitto kazitoa,maana kama zilitolewa basi sio siri,nidokeze nibaini
Namkosoa Zitto anapokesea,sio km nyie kila alipo mpo,mpaka anachofikiria nyie tayali,kumlisha maneno n.k
 
Lol.. Yangu mpaka dakika hii hiko poa tu.. Ila tatizo ni shemeji yako ameanza kuwa na kawifi na keyboard..:teeth::teeth::teeth:

Lol;

Mjadala huko personal. Kwa maoni yangu binafsi hicho sio kitu kibaya. Ni kitu kinachoonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya watu tofauti and tofauti plays an important roles in political discourses, even though we don't want to admit. Maswali nayojiuliza

Je kama Zitto angekuwa mtu wa Kaskazini, maendeleo yake ya kisiasa yangekuwaje? Je Dr. Slaa angekiwa mzaliwa wa Mpindimbi, juhudi zake zingemfikisha alipo?

Hili kuzifanya tofauti zetu kuwa ni nguvu ya maendeleo na sio vikwazo, je ni juhudi gani zifanyike?
 
Zakumi

Jibu la swali lako ni kuwa tunahitaji
Watanzania kama wananchi wa nchi mmoja
Tunahitaji wana siasa na elected officials to stand up for the common good


Jambo zuri lililojengwa toka mwanzo wa taifa hili ni wananchi kuishi popote bila kubaguliwa.
Kuwa na haki ya kuongoza au kuongozwa bila kujali nani katoka wapi


Temeke iliwahi kuwa na mbunge Mh Mrema. Korogwe ina mgoni na Mh Zitto ana nia ya ubunge Ubungo, kahama n.k

Huko kote viongozi hawachaguliwii kwasababu ‘kwani kuna dhambi Mkigoma akiwa kiongozi''


Maendeleo ya Mtwara ni yako , yangu na yule. Hakuna aliyezuiwa kuishi Mtwara.
Hakuna aliyezuiwa kuishi Muheza. Hivyo, maendeleo ya Lushoto au Uvinza ni yetu sote


Ni kwa muktadha huo, wanaoingiza mbegu za u-mkoa au ukanda , wanataka kutugawa na kutuvuruga.
Ndio maana tunasimama hapa kusema,daraja la malagarasi lijengwe si kwasababu ni la Wakigoma, bali letu sote

Tulipojenga daraja la Rufiji,sote tunafaidika. Hatuna sababu ya kuwasikiliza wapuuzi wanaotaka kutuaminisha, matatizo ya Mtwara ni ya Mtwara na matatizo ya Shinyanga yanasababishwa na watu wa Arusha au Kilimanjaro.

Hatuhitaji watuw anaotueleza ‘Kilimanjaro ina maendeleo' bila kufafanua wana maana gani,maendeleo gani na kwasababu gani ukilinganisha na kwingine

Hatuhitaji watu wa kusema mkoa fulani unachangia kuliko mwingine na unahitaji maendeleo. Sote kapu letu ni moja.

Tatizo letu si wananchi wa kanda, mkoa au wilaya fulani.Tatizo letu ni umasikini, ujinga na maradhi.

Tuliowapa dhamana ndio hao wanaitana Dodoma
na kugawana pesa za ‘katiba mpya'
Mabilioni yamepotea tukiomba balozi wa Japan atupe msaada wa kujenga vyoo vya shule.


Hayo ndiyo matatizo yetu,tuangalie tunafumua vipi mfumo.
Si kushambulia mikoa bila sababu kwa kutumia takwimu kujenga chuki.
 
Wanjamvi hebu pitieni hapa
Kwa hisani ya gazeti la Nipashe na MwandishiG.Mushi (tunashukuru
)

Wanakijiji Nronga wajifunga kuweka lami barabara yao

Na Godfrey Mushi
17th December 2014

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe.

Wakazi wa Kijiji cha Nronga kilichopo Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro wamechanga zaidi ya Sh. milioni 170 kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kalali-Nronga, yenye urefu wa kilomita 6.6

Barabara hiyo inayojengwa na Kampuni ya Elerai Civil Engineering & Constructions ya Arusha, itakapokamilika, itakuwa kichocheo kikubwa cha kufunguka kwa fursa za kiuchumi zitakazowanufaisha wakazi Nronga na vijiji jirani vya Wari na Foo, wilayani hapa.

Diwani wa Kata ya Machame Magharibi (Chadema), Elibariki Lema alisema jana kuwa, kwa sasa ujenzi huo upo katika hatua za uumbaji wa barabara pamoja na uwekaji wa makalavati ili kupisha uwekaji wa lami nyepesi kwenye eneo la mradi.

"Zaidi ya kilomita nne za barabara hii ni eneo korofi lisilopitika kwa urahisi wakati wa nyakati za mvua. Kutokana na adha hiyo, wananchi wa Kijiji cha Nronga waliamua wenyewe waanze kutafuta namna ya kukabiliana na hali hiyo; ndipo ikaamuliwa na vikao vya serikali ya Kijiji kwamba tuwashirikishe na wazawa waliopo nje ya mkoa wa Kilimanjaro ambao waliitikia wito huo na kutufikisha hatua hizo za ujenzi,"alisema Lema.

Kwa mujibu wa Lema, usanifu wa mradi huo, ulianza mwaka 2012 chini ya usimamizi wa Samweli S. Lema ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya Elerai, inayojishughulisha na kazi za ujenzi wa barabara na ukadiriaji wa majenzi.

Aidha, alisema Halmashauri ya Wilaya ya Hai imewaunga mkono wananchi hao kwa kuwapa makalavati na kuwaondolea kodi ya malighafi ya ujenzi kwenye barabara hiyo.

Kuhusu mkakati wa kuiimarisha pia barabara ya Foo-Nronga kwa kiwango cha changarawe, Diwani huyo alisema Mbunge wa jimbo la Hai na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe, amewaahidi kuwapatia greda kwa ajili ya kuisafisha na kuimarisha miundombinu yake ili iweze kupitika kwa urahisi nyakati zote.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Boniface Kwayu, aliiambia NIPASHE kwamba mradi huo utakapokamilika utavinufaisha kiuchumi vitongoji vya Nrwaa, Nkwamakya, Nkwamandaa, Maasen, Nkwelengya, Nkwakishu na Naluti ambavyo wakazi wake walio wengi ni wakulima na wafanyabiashara.

"Tumefika katika hatua nzuri ya ujenzi ambapo mkandarasi yupo kwenye eneo la mradi, akiwa tayari ameshamwaga vifusi vya changarawe kwa ajili ya kushindilia baada ya kuweka makalavati na kuiumba barabara.

Hayo yanayofanyika kwa sasa ni maandalizi ya kupisha uwekaji wa lami baadae tutakapopata fedha za kutosha,"alisisitiza Kwayu.

Alisema moja ya mambo atakayotekeleza kwa kipindi kifupi tangu kuchaguliwa kwake kukiongoza kijiji hicho ni kuunda kamati itakayokuwa na mammlaka ya kuratibu shughuli zote za kiuchumi ikiwamo kufungua akaunti maalumu ili kuiwezesha barabara hiyo kuwa mradi endelevu.

"Rai yangu kwa wadau wa maendeleo, serikali na wafanyabiashara wenye moyo wa kutuunga mkono, wasisite kufanya hivyo kwa kuwa nchi hii, tunaamini itajengwa na wenye moyo. Tunahitaji sapoti ya hali na mali kwa sababu kaya 713 za kijiji cha Nronga chenye wakazi zaidi ya 2,500 hawawezi peke yao,"alisema Kwayu.

Awali, Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho (VEO), Valerian Lema, alisema wakazi wake bila ya kujali itikadi za vyama vyao, kwa kauli moja wameridhia kila kaya kuchangia kiasi cha Sh. 10,000 kwa mwezi ambao hadi kufikia sasa wamekusanya zaidi ya Sh. 3,000,000 katika awamu ya kwanza ya mradi huo.

"Kila kaya inalazimika kuchangia kiwango hicho kama nguvu za wananchi, lakini pia wazawa wa Nronga ambao wanaishi nje ya mkoa wa Kilimanjaro, wanashiriki moja kwa moja kwenye kuuwezesha mradi huu kufanikiwa.

Wananchi hawa wamejitoa kwa moyo mkunjufu kukikwamua kijiji chao kiuchumi kwa kuanza ujenzi wa barabara…Huu ni mwanzao mzuri wa kukumbuka walipotoka,"aliongeza Valerian.



CHANZO: NIPASHE
 
Maisha binafsi najua yana siri,ila kuniambia CDM kuna siri ilo nakataa,sioni siri yoyote KATIKA vyama vya siasa,ila kuna mikutano ya ndani,ambayo sio siri,labda unieleze siri gani Zitto kazitoa,maana kama zilitolewa basi sio siri,nidokeze nibaini
Namkosoa Zitto anapokesea,sio km nyie kila alipo mpo,mpaka anachofikiria nyie tayali,kumlisha maneno n.k

Nimekwambia hivi siri ni hulka ya binadamu, na ndo maana siri inaanza kwa mtu moja, unapo kuwa na mke/mme basi kuna siri za bibi na bwana, unapolkuwa na watoto kuna siri za familia, na kuendelea mpaka kufika katika taifa. Siri hazimaanishi ni kupigindua nchini. Sasa basi kama binadamu yule yule mwenye siri kuanzia katika familia yake kwenda kwenye ukoo wake, mpaka taifa kinachobadilika ni nini akiwa ndani ya chama fulani? jibu unalo.

Swala la Chadema na Zitto kuhusu siri za chama, Hilo siwezi kukujibu maana sijui kama Zitto alitoa siri za chama au la, Na hakuna sehemu yeyote katika mjadala huu nilipoongelea mambo ya Zitto na siri za chama.
 
Lol;

Mjadala huko personal. Kwa maoni yangu binafsi hicho sio kitu kibaya. Ni kitu kinachoonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya watu tofauti and tofauti plays an important roles in political discourses, even though we don't want to admit. Maswali nayojiuliza

Je kama Zitto angekuwa mtu wa Kaskazini, maendeleo yake ya kisiasa yangekuwaje? Je Dr. Slaa angekiwa mzaliwa wa Mpindimbi, juhudi zake zingemfikisha alipo?

Hili kuzifanya tofauti zetu kuwa ni nguvu ya maendeleo na sio vikwazo, je ni juhudi gani zifanyike?

Nafikiri hajalishi mtu umezaliwa wapi maana uzuri wa siasa ziko kila sehemu na kwa kuanzia ngazi za chini kabisa. Hivyo hata kama Zitto angezaliwa Ikwiriri bado angekuwa mwanasiasa hivyo hivyo hata Dr. Slaa. Ila kufika sehemu walizopo sasa nikifiri hii linaitaji mtu akuone na akupe nafasi ya kutumia kipaji chako. Na kwa hili la kuona kipaji cha mtu na kumpa nafasi, kusema ukweli Chadema wako vizuri.

Kuhusu maendeleo Nafikiri Nguvuri3 amelielezea vizuri sana, tujiangalie kama watanzania si kama wana Mwanza ua Mara. Matatizo ya mtu wa Songea na ni matatizo yetu sote, maendeleo ya mtu wa Mbeya yawe maendeleo ya kila mtanzania. Tutembee vifua mbele kama watanzania si kama wana Kagera au mwana Lindi.
Matumbo ya mama wa kitanzania yasizae manamba.. Si matumbo ya mama wa Kigoma au Lindi.

Tujiepushe na kauli za uchochezi, kauli za kutengana, kauli za kikanda, udini na nk. Maana hivi vitu havitatusaidia kutuletea maendeleo bali vitazidi kuturudisha nyuma. Ni muhimu tufahamu kuwa maendeleo yanaanzia majumbani kwetu.

Wanasiasa waache siasa za fitina, siasa za utengano, bali siasa za utaifa.
 
Hivi Wazo la Jamhuri ya Watu wa Kaskazini iliishia wapi?
Taifa la Kaskazini lipo kwenye mpango wa Chadema walikuwa wanafanya siri siyo tena siri.

Mkuu Gamba la Nyoka msikilize kwa makini Joshua Nassari anajiapiza kuwa haki ya Mungu Kikwete hatofika Kaskazini.

Anaenda mbali zaidi anasema karibia wanajitangazia Taifa la Kaskazini kama vile Sudan Kusini walivyofanya.

Kapanga kabisa na serikali ya Taifa la Kaskazini, Nassari ni rais na Lema waziri mkuu wizara zingine watazitangaza.

Kuna sehemu anasema Taifa la Kaskazini wataishi kama Ulaya...daah!!!

Hawa Chadema badala kujiangalia kama Watanzania lakini wao wanajiangalia kama Wakaskazini hii ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa letu, watu kama hawa wakipewa uongozi wataligawa taifa letu.

Wanasiasa waache siasa za fitina, siasa za utengano, bali siasa za utaifa.

Tujiepushe na kauli za uchochezi, kauli za kutengana, kauli za kikanda, udini na nk. Maana hivi vitu havitatusaidia kutuletea maendeleo bali vitazidi kuturudisha nyuma. Ni muhimu tufahamu kuwa maendeleo yanaanzia majumbani kwetu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom