Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Wanajamvi
Huu ni mwendelezo wa uzi wa https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/308989-duru-za-siasa-matukio-20.html
Tutaangalia matukio mbali mbali yanayotokea nchini na dunia kwa nyakati tofauti.
Tutaendelea na nyuzi nyingine mahususi kama zilivyo sasa.
MTAFARUKU WA IRAQ NA SOMO KWA VIONGOZI WA TANZANIA
Sehemu ya I
Katika siku za karibuni kumetokea uasi nchini Iraq unaoelekea kuangusha utawala wa waziri Mkuu Nuur Maliki.
Maliki ni kiongozi anaytokana na sehemu ya tawi la Waislam la Shia. Waasi wa serikali wanatoka katika tawi la sunni
Kwa faida tu ya wasomaji na kwa ufupi wa habari, matawi hayo yana matawi mengine madogo mengi.
Kwa mfano, sunni wana matawi (madehebu) ambao yanatokana na mitazamo na tafsiri kutoka kwa wasomi waliobobea(scholars).
Matawi madogo ndani ya tawi moja hayana tofauti kubwa kimtazamo.
Tofauti kubwa ipo katika matawi makubwa kama Shia, Sunni, Sufi na Ahamdiyya.
Kundi kubwa ni la Sunni likifuatiwa na Shia na mengine yote yakiwa yameenea katika sehemu za dunia, kutokana na kuenea kwake. Mathalan, nchini Saudia, sehemu kubwa ni Sunni tofauti na eneo kama Iran ambako ni Shia Islam.
Kwa nchi kama Iraq, matawi Makuu ya Waislam yamegawanyika kutokana na jiografia ya eneo.
Nchi ya Iraq inapakana na nchi za Iran na Saudia na hivyo kuwa na influenced na waislam wa pande zote.
MAREKANI ILVYOLIKOROGA NA SASA IPO NJIA PANDA
Utawala wa Saadam Hussein ulitumia mkono wa chuma kiutawala.
Kwa upande mmoja ilionekana Sunni walikuwa wanatawala,upande mwingine Saadam aliweza kuyaunganisha makundi hayo katika utaifa mmoja.
Baada ya kuvamia Iraq, Marekani ilifanya kosa moja la kihistoria linaloiandama nchi hiyo hadi tunavyoandika.
Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuungwa mkono na wananchi wa Iraq kwa kutumia siasa na dini.
Marekani ndiyo iliyoanzisha kauli mbinu ya Saadam aliwaonea Shia na kuendelea kujenga hali hiyo vichwani mwa watu.Matokeo yake yalikuwa kuungwa mkono na viongozi kama Murtada el Saada wa kundi la Shia.
Hali hiyo iliigawa nchi kwa Sunni kuhisi kuwa kuondolewa kwa Saadam kulikuwa na siri zaidi ya ile iliyosemwa. Tukaanza kuona makundi ya upinzani wa kidini yakizuka kati ya Sunni na Shia.
Wakati huo huo, Shia walikuwa wanaungwa mkono na Iran ambaye ni hasimu Mkubwa Marekani kwa sasa.
Ghafla tukaona akina Mortada el Sada wakiungwa mkono na Iran na kuleta upinzani kwa Marekani
Kwa uchache, aliyechochea mgawanyiko wa makundi katika nchi ya Iran ni uvamizi wa Marekani kwa kutumia siasa maeneo yenye watu wenye mitazamo tofauti ya kiimani.
Kabla hatujaangali jinsi ugumu ulivyo kwa Marekani nchini Iraq, tuangalie kwa uchache siasa za mashariki ya kati.
Siasa za mashariki ya kati ni za kuchanganya sana(complicated).
Unaweza kutafuta suluhu ya tatizo moja, wakati huo huo ukazua tatizo jingine kubwa zaidi.
Kwa mfano, wakati Hezbollah chini ya Imam Hussein Nasrallah wanapigana na Israel, misaada yao ilitoka Iran kwenye Shia wengi na kuwafikia kupitia baadhi ya sehemu za Syria yenye Sunni.
Wakati huo huo, Hamas hawakuwa katika maelewano na Hezbollah na walipata misaada yao kutoka Saudia na Syria.
Marekani ingependelea kumsaidia Israel, na ili kufanikiwa ni lazima isaidie kundi moja.
Endapo itamsaidia Hezbollah basi ni wazi itaungana na Iran ambaye ni tishio kubwa kwa Israel.
Endapo wataunga Mkono Hamas, watakuwa wanawatosa Waisrael.
Na hayo yakiendelea ni ima Marekani itaudhi Saudia au Israel achilia mbali Iran.
Na ugumu huo upo Syria kwa sasa. Marekani inashindwa kuingilia mzozo huo kwasababu wanaopigana Syria ni Sunni.
Sunni wanafanya takriban asilimia zaidi ya 60 ya watu wa Syria.
Wapinzani wa Al Asaad wanatokana na tawi la Sunni linaloojulikana kama Wahab au Wahabia.
Wahabia ni kundi la harakati (movement) ambalo linatengeneza makundi mengine yenye misimamo mikali zaidi na yanayopigana dhidi ya Marekani.
''Inasemekana'' makundi yote kama Alshabab na Alqaida yanaundwa na watu wenye msimamo au wanaofuata mafunzo ya Wahabia (Shool of thought).
Hivyo Marekani kuunga mkono kwa uwazi ni jambo la hatari kwa kutokujua nini hatima ya makundi hayo yatakapochukua nchi ya Syria.
Wakati huo huo kuna shinikizo la chini kwa chini kutoka Saudia likiitaka Marekani iunge mkono wapinzani.
Tunaona Marekani ikifanya hivyo kwa tahadhari kubwa bila kuingilia mapambano.
Ndivyo siasa za mashariki ya kati zilivyo na utata. Ni ngumu kuwa na balanced equation kutoka na jiografia na historia ya eneo hilo kwa ujumla wake
Inaendelea....
Huu ni mwendelezo wa uzi wa https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/308989-duru-za-siasa-matukio-20.html
Tutaangalia matukio mbali mbali yanayotokea nchini na dunia kwa nyakati tofauti.
Tutaendelea na nyuzi nyingine mahususi kama zilivyo sasa.
MTAFARUKU WA IRAQ NA SOMO KWA VIONGOZI WA TANZANIA
Sehemu ya I
Katika siku za karibuni kumetokea uasi nchini Iraq unaoelekea kuangusha utawala wa waziri Mkuu Nuur Maliki.
Maliki ni kiongozi anaytokana na sehemu ya tawi la Waislam la Shia. Waasi wa serikali wanatoka katika tawi la sunni
Kwa faida tu ya wasomaji na kwa ufupi wa habari, matawi hayo yana matawi mengine madogo mengi.
Kwa mfano, sunni wana matawi (madehebu) ambao yanatokana na mitazamo na tafsiri kutoka kwa wasomi waliobobea(scholars).
Matawi madogo ndani ya tawi moja hayana tofauti kubwa kimtazamo.
Tofauti kubwa ipo katika matawi makubwa kama Shia, Sunni, Sufi na Ahamdiyya.
Kundi kubwa ni la Sunni likifuatiwa na Shia na mengine yote yakiwa yameenea katika sehemu za dunia, kutokana na kuenea kwake. Mathalan, nchini Saudia, sehemu kubwa ni Sunni tofauti na eneo kama Iran ambako ni Shia Islam.
Kwa nchi kama Iraq, matawi Makuu ya Waislam yamegawanyika kutokana na jiografia ya eneo.
Nchi ya Iraq inapakana na nchi za Iran na Saudia na hivyo kuwa na influenced na waislam wa pande zote.
MAREKANI ILVYOLIKOROGA NA SASA IPO NJIA PANDA
Utawala wa Saadam Hussein ulitumia mkono wa chuma kiutawala.
Kwa upande mmoja ilionekana Sunni walikuwa wanatawala,upande mwingine Saadam aliweza kuyaunganisha makundi hayo katika utaifa mmoja.
Baada ya kuvamia Iraq, Marekani ilifanya kosa moja la kihistoria linaloiandama nchi hiyo hadi tunavyoandika.
Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuungwa mkono na wananchi wa Iraq kwa kutumia siasa na dini.
Marekani ndiyo iliyoanzisha kauli mbinu ya Saadam aliwaonea Shia na kuendelea kujenga hali hiyo vichwani mwa watu.Matokeo yake yalikuwa kuungwa mkono na viongozi kama Murtada el Saada wa kundi la Shia.
Hali hiyo iliigawa nchi kwa Sunni kuhisi kuwa kuondolewa kwa Saadam kulikuwa na siri zaidi ya ile iliyosemwa. Tukaanza kuona makundi ya upinzani wa kidini yakizuka kati ya Sunni na Shia.
Wakati huo huo, Shia walikuwa wanaungwa mkono na Iran ambaye ni hasimu Mkubwa Marekani kwa sasa.
Ghafla tukaona akina Mortada el Sada wakiungwa mkono na Iran na kuleta upinzani kwa Marekani
Kwa uchache, aliyechochea mgawanyiko wa makundi katika nchi ya Iran ni uvamizi wa Marekani kwa kutumia siasa maeneo yenye watu wenye mitazamo tofauti ya kiimani.
Kabla hatujaangali jinsi ugumu ulivyo kwa Marekani nchini Iraq, tuangalie kwa uchache siasa za mashariki ya kati.
Siasa za mashariki ya kati ni za kuchanganya sana(complicated).
Unaweza kutafuta suluhu ya tatizo moja, wakati huo huo ukazua tatizo jingine kubwa zaidi.
Kwa mfano, wakati Hezbollah chini ya Imam Hussein Nasrallah wanapigana na Israel, misaada yao ilitoka Iran kwenye Shia wengi na kuwafikia kupitia baadhi ya sehemu za Syria yenye Sunni.
Wakati huo huo, Hamas hawakuwa katika maelewano na Hezbollah na walipata misaada yao kutoka Saudia na Syria.
Marekani ingependelea kumsaidia Israel, na ili kufanikiwa ni lazima isaidie kundi moja.
Endapo itamsaidia Hezbollah basi ni wazi itaungana na Iran ambaye ni tishio kubwa kwa Israel.
Endapo wataunga Mkono Hamas, watakuwa wanawatosa Waisrael.
Na hayo yakiendelea ni ima Marekani itaudhi Saudia au Israel achilia mbali Iran.
Na ugumu huo upo Syria kwa sasa. Marekani inashindwa kuingilia mzozo huo kwasababu wanaopigana Syria ni Sunni.
Sunni wanafanya takriban asilimia zaidi ya 60 ya watu wa Syria.
Wapinzani wa Al Asaad wanatokana na tawi la Sunni linaloojulikana kama Wahab au Wahabia.
Wahabia ni kundi la harakati (movement) ambalo linatengeneza makundi mengine yenye misimamo mikali zaidi na yanayopigana dhidi ya Marekani.
''Inasemekana'' makundi yote kama Alshabab na Alqaida yanaundwa na watu wenye msimamo au wanaofuata mafunzo ya Wahabia (Shool of thought).
Hivyo Marekani kuunga mkono kwa uwazi ni jambo la hatari kwa kutokujua nini hatima ya makundi hayo yatakapochukua nchi ya Syria.
Wakati huo huo kuna shinikizo la chini kwa chini kutoka Saudia likiitaka Marekani iunge mkono wapinzani.
Tunaona Marekani ikifanya hivyo kwa tahadhari kubwa bila kuingilia mapambano.
Ndivyo siasa za mashariki ya kati zilivyo na utata. Ni ngumu kuwa na balanced equation kutoka na jiografia na historia ya eneo hilo kwa ujumla wake
Inaendelea....