Duru za siasa: Matukio nchini na duniani kwa ujumla

Duru za siasa: Matukio nchini na duniani kwa ujumla

Sehemu ya III

UKUBWA WA TAARIFA
Kutokana na ukubwa, unyeti na hisia za wananchi, ni jambo la kushangaza taarifa hiyo inaweza kujadiliwa katika siku moja. Lakini hili limefanyika makusudi.

1.Ili serikali ipate muda wa kuahirisha bunge kwa kisingizio cha kukosa muda. Maana yake jambo hili lijadiliwe kwa siku moja.

2.Serikali kupitia bunge inaanda mbinu za kuwapanga wasemaji watakaohakikisha wanababisha zaidi ya kujadili taarifa.

KITAKACHOFANYIKA
Baada ya mjadala mfupi, itatolewa rai kuwa limeagiza serikali ishughulikie suala hilo na wote waliohusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Hadi hapo mjadala utakuwa unaahirishwa kwasababu

  1. Serikali haina pesa za kikao kingine siku inayofuata
  2. Wazungumzaji wa kupangwa watakuwa wamechukua nafasi ya siku moja.

Mkuu huo mstari niliopigia mstari nakubari kabisa mafisadi wasivyo na haibu,wanaweza kutumia hiyo,ila wabunge ambao wameamua kutetea wananchi,mimi kama mtanzania,kama ANNE MAKINDA ateleta upuuzi wake,basi aingie katika historia kuliingiza taifa katika machafuko,WABUNGE WAUNGANE WAWATANGAZIE WANANCHI HIYO JUMATANO WAZUNGUKE BUNGE,ili kukitokea ulaghai wabunge wa upinzani na baadhi wazalendo{ccm} wasikubali kutoka ndani ya bunge,wakikomaa siku mbili au tatu historia mpya itaandikwa
 
MTAZAMOKUHUSU KINACHOJIRI DODOMA HASA ANGA ZAKISIASA


Wanaduru
Makundituliyosema yanawindana na hicho ndicho chanzo chasakata hili kushikiwa bango Zaidiya masakata mengine. Pengine tujaribukuangalia kuhusu hali ya wabunge wa CCMna sakata zima.

1.Mgombea mtarajiwa EL anaungwa mkono na kundilake linalopigana kuhakikishaanafikia ndoto aiyowahi kusema ni ya matumaini.Uwepo wa waziri mkuu mwinginealiyechufukakutasaidia kuondoa kikwazo cha EL katika king'anyiro kwa hoja kuwawotewamewajibika kama EL na wala siyo makosa

Kundi lake linataka Pinda ambaye ametangaza niakuenguliwa katika kinyang'anyiro.
Pinda anaonekana tishio hasa baada ya kutoa mwelekeo

Kashfa itawaondoa vijana kama Ngeleja ambao naoni sehemuya makundi
Kashfa itaondoa watu kama Anna Tibaijukawanaotajwa kama akina mama


Hivyokashfa ina manufaa kwa timu EL kuliko mgombeamwingine

2.Vijana
Kundi hili linaunga mkono sakata la Escrowkwasababu yakutaka kupunguza ushindani. Kwasasa, January ni mmoja wawatarajiwa. Kuondokakwa Ngeleja kutamsaidia abaki na vijana dhaifu

Kundi la vijana lingependa kashfa hii iondoke nawatu ilikujinasibu kuwa vijana wanaweza. Kundi linaunga mkono vijana wa upinzani ambaonao kama wenzao wa CCMwanataka kutumia kashfa kupanda ngazi au kujijenga tenakisiasa.

3.Waliovurunda

Hapa wapo akina Sitta, ambao kuondoka kwa baadhi yawatukunaweza kuwasaidia kutajwa Zaidi hasa baada ya kuchafuka kutokana nakuvurundakatika uendeshaji wa bunge la katiba

Katika kundi la kuvurunda yupo Membe. Huyuanawindwa kwa tuhuma za Radar ambazoamezificha bila kutaja wahusika. Naye piaana kashfa zinazotajwa tu kuhusiana napesa zinaoztoka nje. Hayo ni tuhuma. Nimmoja wa wagombea dhaifu, hata hivyouwepo wake unaonekana kupunguza nguvu yatimu EL


4.Kundi la wasaka nafasi za huruma: Hili halinanguvu sana, isipokuwalinategemea huruma na muda wa kujijenga. Linataka waliopowaondoke ili wawezekupata nafasi za kujitanua. Hapa wapo akina Mwandosya,Mwigulu.


Kundi la huruma lingependa waliopo waondoke ili waowapatenafasi, lakini halipendi serikali kuanguka au kashfa kuumiza Zaidi kwakuelewafadhila wanazotegemea kutoka katika serikali iliyopo kama kukwea ngazizakisiasa


5.Kundi la wazalendo: Hili linachukizwa namwenendo wamambo. Linapiga kelele ili kashfa zifike mwisho.
Kwa bahati mbayasana ni kundi dogo lisilo na ushawishi na linaloweza kutishwakirahisi.


6. Kundi la hohe hahe: Hili halikuwemo katikampango na wala halijui kama kunamipango ya mamilioni. Lipo lipo tu kwakutegemea masilahi ya ubunge.



KUNDIPINGAMIZA
Hili nikundi la waliofaidika na mgao wa Escrow.Linahusisha wazoefu wa ma-deal nalisingependa kashfa hii izungumzwe. Ni kundilenye nguvu sana ndani ya chama,linalopanga safu za viongozi kutoka naushawishi wa fedha ulio nazo.

Kundi hililinaunga mkono kundi namba1 na limefanikiwakuwaingiza katika mtego kundi namba2 na wale waliokuwa hawatarajiwi kama mamaAnna

Ikumbukwendilo kundi lililomuondoa Sitta na kumweka AnnaMakinda.
Hivyo,anachokifanya Makinda ni kutetea masilahi yawateule wake.
Kaziinayomkabili ni kuhakikisha kashfa inakufa auinafifia.

KUNDI MASILAHI
Hili ndilolimetibua kila kitu na kumwaga mtama. Kundi hililinaongozwa na mbungealiyenusurika kwa kutuhumu kulishwa sumu. Hili lilikuwalina mikataba minono nandilo linalosemwa limemwaga data zote.

Kundimasilahi lina vijana waliojipambanua kamawapambanaji ambao nao wana masilahiima ya moja kwa moja au ya kisiasayatakayotokana na ushindi dhidi ya kashfa.

Inaendeleana kundi la upinzani dhidi ya hoja ya escrow

MATATIZO NDANI YA CCM

Makundi yote yana masilahi yao na wala hayaunganishwi nakitu kimoja. Litakuwa jambo gumu sana kwa CCM kuyaweka pamoja siku za usoni. Ningumu kufariji kundi moja bila kuudhi jingine. Hapo ndipo pana tatizo.

Uwepo wa makundi tajwa hapo juu unaweka suala la katibaya CCM njia panda.

Kwa mfano, katiba pendekezwa ya CCM imeandaliwa na kundi‘'pingamizi la Escrow'' likiongozwa na mh Cheng.Makundi mengine hayatakubaliana na ushindi wakundi pingamiza ima katika escrow au katiba ya CCM.

Kundi pingamizi la Escrow ndilo limeandika katiba ya CCMinayopendekezwa, hasa kwa kuondoa vipengele korofi kama maadili ya viongozi.Utaona watajwa wa kundi hili ni wazoefu wa kupiga ma deal. Wapo katika kilakashfa.

Ni bahati mbaya, ule uungwaji mkono ulioonekana bunge lakatiba sasa umeingia nyongo.

Uhasama unaojengeka utakwenda mbali Zaidi kama maeneo yakatiba.

Ikitokea suala la katiba likajadiliwa tena bungeni, UKAWAitaungwa mkono kuliko ilivyokuwa hapo awali.



Itaendelea….
 


MATARAJIORIPOTI YA ESCROW NI MAKUBWA
JE,YATAFIKIWA KATIKA HARAKATI NA HUJUMA ZA CCM

WENYEMATUMAINI, WAJIULIZE, KWA MBINU ZINAZOENDELEA LIPO LA MAANA LITAKALOPATIKANA?

Sehemuya I

Kumekuwepo na harakati za nguvukuzima escrow isijadiliwe bungeni.
Waziri mkuu amekaririwa mara nyingiakitahadharisha kuhusu mjadala

Katibu mkuu kiongozi naye anatoakauli za kutatanisha kila kukicha
Sasa vyombo vya sharia navyovinahusishwa katika harakati

Bunge lilikataa kuundwa kwa kamati yabunge kuliangalia tatizo.
Kazi hiyo akapewa CAG na PCCB.Pengine katika Imani ya udhibiti wa vyombo hivyo k

Katika muda wote wa uchunguzi, hojailiyotawala vyommbo vya habari vilivyonunuliwa ilikuwa ni serikali kutohusikana malipo kwani fedha hazikuwa za umma.

Taarifa Ikatiliwa mkazo iende bungeni, ghafla mambo ya kisheriayakaanza.
Wananchi wakaaminisha suala la pesaambazo sio zao lilikuwa mahakamani. Imedhihirika hakuna suala hilo.

Zikawepo tetesi za mahakama kuandika barua yazuio, mwisho wa siku ikakanwa.
Leo tunasikia PAP wamekwendamahakamani kuzuia suala hilo lisizungumzwe kwa barua ya mahakama.

Yote yanatokea wakati tuliaminishwa pesa hazikuwaza umma.
Endapo ni hivyo, wenye pesa zao wanawasi wasi gani suala lisilohusu umma au serikali kuzungumzwa?

Orodha ya wafadika imeonekana. Hiyoni ya account ya Ruge ambako milioni zimegawanywa kwa viongozi waserikali,chama, dini na taasisi mbali mbali.

Endapo pesa zilikuwa si umma,kulikuwa na motive gani ya kuwapa viongozi wa serikali mgao wa pesa ''halali'baina ya makampuni?
Je, maadili ya kazi yanasemaje kwawaliopokea?

Jitihada za waziri mkuu tunawezakuzieleza katika namna mbili


1. Kwamba anatetea nafasi yake ili kuweza kuitumia kufikia malengo ya kisiasa
2. Kwamba, anaogopa orodha nyingine ya PAP inayosemwa imewashirikisha nyangumi na papa kuanikwa hadharani


Kati ya hayo mawili, moja ni jibu sahihi na ni suala la muda tu itabainika

Inaendelea...
 
Sehemu ya II
.

MBINUZA KUWAPUNZA WATANZANI ZILITUMIKA KATIKA KATIBA

Hivi karibuni mjadalamkubwa wa kitaifa ulihusu katiba.
Kwa bahati nzuri wapowanaojua, waliohusika au walioshiriki katika Escrow na kuachwa katika mzunguko.Haondio waliotoa habari

Baada ya kubainika hojainabeba uzito, wahusika wa Escrow wakatafuta njia za kupumbaza taifa.

Wakashiriki na kugawamafao hasa kwa wajumbe wa znz wakubaliane na hoja zao.

Mjadala wa Escrowukapoteza nguvu, na katiba ikapamba moto.

Mmoja wa walioshirikini mh Chenge ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya uandishi wa katiba.Lengolilikuwa kuendeleza mjadala wa katiba ili mjadala wa Escrow ufe daima

Kundi la Escrowlilitumia pesa nyingi kuhonga wajumbe wa bunge la katiba ilimradi tu mchakatouendele.

Ilifikiriwa kuwa baadaya katiba kupendekezwa, kinachofuata ni kura ya maoni halafu uchaguzi. Mambohayo yangesahulisha umma kuhusu Escrow.

Kwa bahati mbaya,wale waliovalianjuga jambo hili walilifahamu vema.
Ndio hasa msingi wahoja ya Escrow kubeba nguvu, na ndio sababu kubwa ya wahusika wa wizi wa escrowkushiriki katika katiba.

Lengo lilikuwa kuondoaattention ya umma kutoka escrow na kwenda kwenye katiba

KATIBA
Kutokana na mpango wakuzima hoja ya Escrow kwa kutumia katiba, ni wazi kila kilichoandikwa katikakatiba ya CCM kilifanywa kwa lengo maalum la kundi maalumu

1.Kupumbaza wananchi kwa kutumia escrow
2. Kujiinda kwa uhalifu

KULINDA UHALIFU
Wahusika walihakikishasuala la maadili ya viongozi linaondolewa, rais anabaki na madaraka makubwa namuundo hauruhusu ujio wa serikali ya Tanganyika ambayo huenda wasingekuwa naushawishi nayo(control)

Pesa za Escrowzilitumika sana katika mchakato wa kuandika katiba ya CCM.
Wengi walidhani akinaChenge na Sitta walisimamia masilahi ya taifa.

Leo wanashangaa Chengeanatajwa kupata bilioni 1.6 akiwa hana wadhifa.
Na ni huyo ndiyealiyeandika katiba inayosukumizwa vinywani mwa wananchi.

PESAZA KUHONGA ILI KATIBA IPITE
Mkurugenzi wamawasiliano Ikulu alikiri kuwepo kwa mpango wa matumizi ya bilioni 2 kununuawaandishi na wasomi, pamoja na vyombo vya habari katika kuhamasisha katiba.Pesa hizo hazijulikani zilitoka fungu gani.

Hivi, endapo watuwataamini kuwa mafisadi walitoa kiwango hicho ili kuendeleza kelele za katibana kuficha Escrow, nani anaweza kukanusha? Inakuwaje serikali haina bilioni 10za kununua dawa, wakati huo huo kuna sehemu ya serikali ina bilioni 2 zakuhonga waandishi na wasomi?

MASWALIYA KUJIULIZA
Iko wapi orodha yawaliopata mgao wa PAP?
Kwanini viambatanishovinafichwa hasa kwa wabunge wa CCM
Je, kamati ya PACitaweza kuweka wazi kila kitu ikiwemo yale ya mgao wa PAP
Je, bunge litawezakukwepa mitego ya kuvurugwa mjadala?

Endapo PAC itashindwakueleza kwa kina na utilifu kuhusu suala hili, basi yale mashaka waliyonayowengi kuhusu uadilifu wa wajumbe yatapata nguvu .
Kisiasa yatakuwa naimpact kubwa kwa washiriki wa kamati hasa wanaotaka nafasi za kisiasa.

MBINU MBADALA ZA CCM
Ikitokea hakuna njia yakuzuia mjadala, tunaweza kusikia tukio lolote nje au ndani ya bunge litakalokuwasababu ya kuahirisha mjadala.
Hili ni pamoja na malumbano na vurugu ndani yabunge.

Dalili za awali ni zileza kumuondoa Ndugai kwa madai ya kushindwa kudhibiti mjadala usiendelee.

Bunge litakapojadiliescrow, mama Anna Makinda ambaye ni beneficiary wa watuhumiwa kwa wadhifa wak,atawapanga wazungumzaji kutokana na maelekezo ya chama

Kuna uwezekano, mudamfupi tu wa mjadala serikali ikatoa tamko la kufanyia uchunguzi na waliohusikakuchukuliwa hatua.

Wapinzani na hasa walewenye uchungu upo uwezekano wasipewe nafasi.

KOSALA WAPINZANI
Mtego unaotegwa nikuhakikisha mjadala unavurugwa ima kwa hila au kwa mbinu kama ilivyokuwa wakatiwa bunge la katiba.

Itakuwa ni makosa kwawapinzani kuanza kutoka au kupinga kwa vurugu. Wanachotakiwa ni kujenga hoja zanguvu na si kutumia msuli.
Hilo ndilo limewekwakiporo ili wakikosea tu, basi bunge linaahirishwa.

Ingawa wananchi wanamatumaini na mjadala, kwa mbinu zinazosukwa, matumaini ni madogo.

Serikali inachotaka nikukwepa kuanika wahusika ambao wengine kwa nyadhifa zao ni aibu kubaini wamenunliwa na mhindi.

Tusemezane
 
mkuu kipengele cha maadili katika katiba pendekezwa mbona kipo ama kilvyokua katika rasim TOFAUTI NI SURA,KWA CHENGE NI SURA YA NNE NA WARIOBA NI YA TATU
SURA YA NNE
MAADILI NA MIIKO YA UONGOZI NA UTUMISHI WA UMMA
SEHEMU YA KWANZA
MAADILI YA UONGOZI NA UTUMISHI WA UMMA
Dhamana ya
uongozi wa
umma
27.-(1) Madaraka anayopewa kiongozi wa umma:
(a) ni dhamana na atatumia madaraka hayo na kutekeleza wajibu
wake kwa:
(i) kuzingatia masharti ya Katiba hii;
(ii) kuheshimu wananchi;
(iii) kukuza hadhi ya Taifa na kulinda heshima ya ofisi
anayoitumikia; na
(iv) kukuza heshima ya ofisi kwa wananchi;
(b) yanatoa wajibu kwa kiongozi kuwatumikia wananchi.
(2) Dhamana ya uongozi wa umma itazingatia mambo yafuatayo:
(a) anapokuwa anafanya uamuzi wa uteuzi atahakikisha kwamba
anafanya uteuzi bila ubaguzi ila kwa kuzingatia uwezo, sifa na
mwenendo unaofaa;
(b) anakapokuwa anafanya uamuzi wowote katika jambo lolote la
umma atahakikisha uamuzi wake hautokani na udugu, ukabila,
udini, rushwa au ubaguzi wa aina yoyote;
(c) utoaji wa huduma pasipo upendeleo na kwa kufuata maslahi ya
umma kwa kuonyesha:
(i) uwazi, ukweli na uaminifu katika utekelezaji wa kazi za
umma;
(ii) wajibu wa kutangaza maslahi binafsi ili kuepuka mgongano
wa maslahi;
(d) uwajibikaji kwa umma katika kufanya uamuzi na katika utendaji;
na
(e) uadilifu, nidhamu na kujituma katika kutoa huduma kwa umma.
Kanuni za uongozi
wa umma
28.-(1) Kiongozi wa umma, akiwa katika kazi za ofisi au kazi binafsi
au wakati amejumuika na watu wengine, atahakikisha kwamba
10
mwenendo wake:
(a) hauruhusu kutokea mgongano wa maslahi kati ya maslahi binafsi
na maslahi ya utumishi wa umma;
(b) haushushi hadhi ya ofisi anayofanyia kazi; au
(c) hauruhusu matumizi ya ofisi ya umma kwa maslahi binafsi.
(2) Kwa madhumuni ya Katiba hii, Bunge litatunga sheria
itakayoweka, pamoja na mambo mengine-
(a) tafsiri ya neno zawadi, aina, thamani, kiwango na uhifadhi wa
zawadi za Jamhuri ya Muungano;
(b) masharti ya kufungua akaunti za nje kwa kiongozi wa umma;
(c) masharti ya kumtaka kiongozi wa umma kutoa tamko la mali na
thamani yake, madeni yake pamoja na ya mwenza wake wa ndoa;
(d) masharti ya kuzuia kiongozi wa umma kutoshiriki kufanya
uamuzi wa jambo au shughuli yoyote ambayo ana maslahi nayo
yeye binafsi, mwenza wake wa ndoa, mtoto wake, jamaa au rafiki
yake au mtu yeyote wa karibu;
(e) masharti ya matumizi ya mali ya umma;
(f) utaratibu wa utwaaji wa mali za kiongozi wa umma
zinazopatikana kwa kukiuka sheria;
(g) utaratibu wa kumwajibisha kiongozi wa umma aliyekiuka maadili
na miiko ya uongozi wa umma;
(h) uanzishaji wa mitaala inayohusu Katiba, maadili na uraia, shuleni
na vyuoni; na
(i) mambo yasiyotakiwa kwa watumishi wa umma.
(3) Wadhifa wa "kiongozi wa umma" kama ulivyotumika katika
Sehemu hii utajumuisha kiongozi wa kuchaguliwa au kuteuliwa kama
itakavyoainishwa kwenye sheria za nchi.
SEHEMU YA PILI
MIIKO YA UONGOZI WA UMMA
Utii wa miiko ya
uongozi wa umma
29.-(1) Bila kuathiri masharti ya Katiba hii, kiongozi wa umma
ataheshimu na kutii maadili ya uongozi wa umma na miiko ya uongozi.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoainisha:
(a) miiko inayopaswa kuzingatiwa na viongozi wa umma;
(b) utaratibu wa kumuondoa kazini kiongozi wa umma kutokana na
kuvunja miiko na kukiuka maadili ya uongozi wa umma;
(c) vitendo ambavyo Kiongozi wa umma hapaswi kuvitenda; na
(d) ngazi au orodha ya viongozi wa umma wanaofungwa na Ibara hii.
Marufuku
baadhi ya
vitendo
30.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu
hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine yoyote ya kudumu yenye malipo
ya mshahara.
(2) Mtumishi wa umma haruhusiwi kugombea au kuteuliwa kushika
nafasi ya madaraka katika chama cha siasa au nafasi ya madaraka ya kisiasa ya
aina yoyote chini ya Katiba hii.
11
(3) Endapo mtumishi wa umma ataamua kugombea au kuteuliwa
kushika:
(a) nafasi ya madaraka ya kisiasa ya aina yoyote chini ya Katiba hii; au
(b) uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa,
mtumishi huyo atachukuliwa kuwa utumishi wake umekoma tangu siku ya
kuteuliwa kuwa mgombea au kuteuliwa kushika nafasi ya madaraka ya kisiasa
au uongozi katika chama cha siasaTATU
 
SAKATA LA ESCROW
HOJA ZINAZOTATIZA


RASIMU YA WARIOBA IMENG'ARA

Uwasilishwaji wa taarifa ya PACA umekamilika licha ya mizengwe mikubwa.
Taarifa imeonyesha kwa namba na kujibu hoja zilizokuwa zinatatiza

Kwamba, zipo pesa za umma, hilo si mjadala tena.
Ukweli umeonekana zipo iwe moja kwa moja au kwa namna nyingine

Bado duru inapitia taarifa kwa kina, hata hivyo yapo machache ya kujadili

Kamati imeibana wizara ya nishati na madini, na mwanasheria mkuu kama wahusika
Pia ofisi ya waziri mkuu imetakiwa kuwajibika kwa matatizo yaliyojitokeza ikijua yapo

Ukiisoma taarifa, kulikuwa na systemic failure katika suala zima.
Si vyombo vya usalama vya taifa, taasisi kama BRELA au nyingine.
Pia kulikuwepo na ukiukwaji mkubwa wa maadili ya uongozi uliochagizwa na utoaji wa rushwa.

Kamati haikuleza ni kwa vipi kampuni ilisajiliwa kama kampuni kutoka nje ikiwa haipo kiuhalisia.
Je,msajili wa makampuni aliwezaje kufanya usajili bila kujiridhisha na kama hakukuwa na rushwa
Je, balozi zetu azinazofuata siasa za uchumi zilikuwa na mchango gani kufanikisha au kuzuia tatizo?

Kamati imetaja baadhi ya watu waliopata mgao wa fedha.
Hao walikuwa wanasiasa wachache. Kuna orodha iliyotaja wanasiasa hao ikiwa na majaji waliopata mgao.
Je, majaji hawakupewa mgao? Na kwanini hawakutajwa?

Ipo taarifa kuhusu ugawaji wa fedha kutoka katika account ya Rugemalira.
Je, kampuni zingine kama PAP, Piperlink au IPTL zilizokuwa katikati ya sakata hazikuwa na 'wafaidika' wa mgao?
Je, mgao ulikuwa kwa account moja tu au ni zaidi ya hapo?Akina nani walipata nje ya mgao wa Ruge?

Taarifa imemtaja waziri mkuu kama mtu aliyefahamu taarifa zote.
Je, kamati imejiridhisha kuwa waziri mkuu alifikisha/hakufikisha taarifa kwa bosi wake?
Mbona taarifa haikueleza na imesishia kumtaka ajiuzulu.

Je, waziri mkuu anatakiwa ajiuzulu kwa kutetea kutokuwepo kwa fedha za umma, au kwa kukalia taarifa bila kumjulisha bosi wake?

Na kama bosi wa Pinda hakujua, kwanini katibu mkuu kiongozi amejihusisha sana na suala hili ambalo ''inaonekana Ikulu haikutaarifiwa na Pinda''

Mengi yapo, tuanze na haya machache.


RASIMU YA WARIOBA

Rasimu ilipendekeza rais apunguziwe madaraka ikiwemo uteuzi wa wenyeviti wa bodi za mashirika.
Hili lililenga kumpa uwezo wa kushughulikia matatizo bila kukinzana na matakwa yake binafsi au ya kiofisi.

Taarifa ya PAC inaonyesha bodi ya TANESCO inahusika au inatiliwa shaka sana katika sakata la Escrow.
Mwenyekiti wa bodi ni mkuu mstaafu wa majeshi.
Je, ikidhihirika kuwa zipo hujuma na wahusika ni pamoja na mwenyekiti wa bodi, Rais kwa ataweza kuamuru DPP amkamate?

Lakini pia utaona wahusika wengi wa Escrow ni wateuliwa wa Rais.
Je, hilo linamweka Rais katika nafasi ipi?

Na mwisho, PAC imeshauri wahusika wajiuzulu nafasi zao.
Wengi ni wabunge ambao wamechaguliwa. Hakuna namna wanaweza kujiuzulu wenyewe au kulazimishwa kujiuzulu.
Kuna njia moja tu ambayo ni kuwanynag'anya uanacha ili wapoteze ubunge.

Njia hii imeshindwa, na ndio maana wapo watuhumiwa waliotajwa kila kashfa na majina yao yanaendelea kung'ara katika medani ya wizi. Maana yake chama hakiwezi kuwawajibisha.

Rasimu ya Warioba ilipendekeza wabunge wawajibishwe na wapiga kura wao.
Je, leo hatuoini ukweli huo?

Tusemezane
 
RAIS wa TANZANIA ana tofauti kubwa na RAIS wa UJERUMANI,Rais wetu ni mtendaji,kwanini kila siku wawajibike wa chini yake,ni tatizo kubwa,bora RAIS wetu anyang'anywe madaraka awe kama wa UJERUMAN
 
ESCROW: KUJIUZULU HAKUKWEPEKI
SERIKALI HAIAMINI VYOMBO VYAKE

RAIS ATABEBA LAWAMA ZITOKANAZO

Utetezi dhidi ya taarifa ya PAC unaendelea. Katika nchi za wenzetu, uwajibika ni sehemu ya maadili ya uongozi. Kutajwa tu katika kashfa inatosha kabisa kwa kiongozi kujiuzulu.

Kujiuzulu kuna maana nyingi kisiasa

  1. Kukubali kuchukua wajibu kwa kosa
  2. Kutoa nafasi ya kuchunguzwa ili ukweli ujulikane
  3. Kuepusha madhara kwa serikali/taasisi au shirika husika
  4. Kusaidia chombo teuzi kuondokana na lawama
n.k.
Taarifa ya PAC iliyowasilishwa, imenukuu uchunguzi uliofanywa na ofisi ya CAG na PCCB ambavyo ni vyombo vya serikali.

Kila lililosemwa si kutokana na utashi wa watu au mtu bali taarifa ya kitaalamu kutoka katika mamlaka husika

Serikali iliekeza vyombo hivyo vifanye uchunguzi na kuja na taarifa.
Taarifa imeonyesha kuhusika kwa kundi kubwa la watu kutoka kila eneo la jamii, kuanzia mawaziri, wabunge, raia, viongozi wa dini na taasisi kama TANESCO, BRELA n.k.

Kitendo cha mawaziri kuhusishwa na kashfa ni tukio baya hata kabla ya kuangalia ubaya wake.

Kwasasa, serikali ipo mateka kutokana na watu wachache ima kuvurunda au kufanya uhalifu.

Vyovyote iwavyo, hakuna jinsi ya kuisaidia serikali iliyopo madarakani kama si wahusika kujiuzulu nafasi zao.

Hilo sit u litarudisha imani ya wananchi kwa serikali yao, bali pia litaonyesha utawala wa sheria na demokrasia

Katika taratibu za kiutawala, wateuliwa wa Rais wanawajibika kwake.
Makosa yao ni makosa ya mteuzi ambaye ni Rais. Katika hali iliyopo, watuhumiwa wakigoma, watakuwa wanamweka Rais katika wakati mgumu sana.

  1. Kwamba, alazimike kuwawajibisha ili kuondokana na lawama
  2. Aendelee kuwa nao, wananchi wapoteze imani na serikali yao

Taarifa ya PAC iliyonukuu CGA na PCCB imeonyesha wazi uwepo wa uzembe ambao ulitetewa kwa uongo ndani ya bunge.

Pia imeonyesha kukiukwa kwa baadhi ya taratibu za utendaji.
Na kibaya zaidi, kuna shaka juu ya maadili ya kiroho ''moral authority'' ya viongozi husika.

Hayo tu yanatosha kabisa kueleza kwanini viongozi husika wanatakiwa kujiuzulu.

Endapo hawakubaliani na hilo, suala na mzigo mzito wa tuhuma utamwangukia Rais wan chi. Hatuwezi kuwa na serikali isyoamini uchunguzi wa vyombo vyake vyenyewe.

Hapo kuna tatizo kubwa sana.

Tusemezane
 
ESCROW: HISIA ZITAZOJENGEKA
KUWAJIBIKA NDILO JIBU LILILO MEZANI

PAC KUNA HOJA ZAIDI KUHUSU TAARIFA ZENU

WARIOBA BADO ANANG'ARA BILA MSAADA WA MTU

Kadri suala la Escrow linavyozidi kukingiwa kifua hata ukweli unapokuwa wazi, zipo hisia zisizo na picha nzuri zinazoanza kujengeka.

Kwanza, Serikali haina imani na vyombo vyake na hivyo taarifa za CAG na alau PCCB haziaminiki tena. Sasa, serikali inafanyaje kazi ikiwa haiamini vyombo vyake.

Pili, kwamba, watu wanaanza kuchimba chimbuko la mkataba wa IPTL.
Mkataba huo ulipingwa ndani na nje ya nchi, na sasa madhara yake yanaonekana

IPTL ilianza wakati mh Rais akiwa waziri wa nishati.
Na kIsha mikataba ikaendelea akiwa waziri wa fedha

Hii maana yake, Rais anafahamu mambo yote yalivyoanza na anajua chimbuko la tatizo. kwa mantiki hiyo, watendaji walioteuliwa na Rais wanapokataa kuwajibika, kuna hisia za serikali kushiriki au ushiriki wa mgao huo kuwa mpana kuanzia enzi hizo hadi sasa.
Hisia hizo ni zinapata ''halali'' kutokana na mazingira yanayojengwa

Nne, chama tawala kimejiondoa katika suala hili.
Haiwezekani CCM imudu kuwafunga midomo wabunge 400 wa bunge la katiba, isiweze kuwawajibisha watu wasiozidi 30 waliovurunda katika sakata hili

Hapa kuna hisia kuwa yale yaliyofichwa pengine ni mapana zaidi ya yanayoonekana.
Kwa mfano, watu wataweza kuhoji account za Piper link na PAP kama hazikuwa na mgao na akina nani walihusika hata kama ni fedha binafsi.

PAC
Katika mabandiko yaliyotangulia tumehoji baadhi ya mambo yanayohitaji ufafanuzi.
Leo mbunge Lissu ameongeza idadi ya yale yanayohitaji kufafanuliwa

Mathalan, hivi nini ushiriki wa wizara ya fedha ambayo sehemu kubwa ya transaction imehusu? Je, hakukuwa na kushtuka kwa namna yoyote

BoT kama chombo huru, kwanini kilishinikizwa na AG kuhusu malipo.
Je, huko BoT hakuna wataalam wa sheria au kodi ambao wangebaini tatizo kabla?

PAC imesema waziri mkuu alifahamu jambo hili.
Je, walitafuta zaidi kuona kama alikuwa na mawasiliano na ofisi nyingine za juu?

Je, kile kipengele cha taarifa ya CAG kuwa katibu wa rais alishiriki katika mawasiliano kwa nyakati fulani, kilikuwa kweli, na je ushiriki wa katibu wa rais ulikuwa katika kiwango gani?

RASIMU YA WARIOBA
Leo wabunge wanalumbana, wakitetea na wengine wakipinga kuwajibishwa kwa viongozi husika.

Tumeeleza ugumu uliopo TNAESCO kwa kuzingatia uteuzi unatoka ofisi ya Rais, na kwamba mwenyekiti wa bodi ni Jenerali mstaafu, jambo linaloleta ugumu katika kuwajibishana hasa nchi changa kama yetu.

Kwa upande wa bunge, tume ya Warioba ilishauri mawaziri wasitokane na wabunge.
Leo mawaziri wasingekuwa wabunge, pengine ilikuwa rahisi kuwaambia bunge halina imani nao na wasiingie huko.

Hilo lingemsaidia Rais kuchukua hatua tukizingatia udhaifu uliopo wa kuwajibishana.

Bunge lilishauriwa lithibitishe uteuzi wa mwanasheria mkuu.
Hilo nalo lingekuwa na meno kama ingekubalika.

Leo Werema asingeweza kusimama na kusema, bunge si mamlaka inayoweza kutengua wadhifa wake.

Hili pia linaonyesha mgongano uliopo, kati ya mihimili.
Tumeona suala la mahakama na bunge na sasa mhimili wa tatu serikali(Werema) na mawaziri.

WABUNGE
Wabunge wa CCM waliopitisha katiba yao kwa nguvu ili ijekuwa ya wananchi, lazima wajitahmini na kuona mtatizo kama haya yanapoanza mapema, siku za usoni itakuwaje.

Ule umoja ambao tunajua ulikuwa wa ''pesa'' ndio unaonyesha matunda yake hata kabla ya katiba ya Chenge haijasukumizwa kwa wananchi.

Kuna tatizo kubwa sana linainyemelea nchi hii.

Kama hatutakaa chini na kuweka utaratibu kwa kukubaliana na kuacha wingi, basi tujiandae kwa maafa siku moja mbele ya safari.

Hizi ni salamu tu tunazopewa kuhusu matatizo ya katiba.
Warioba aliweka wingi na uchama pembeni, Je haonekani kama alikuwa na majibu ya muda mrefu ujao?

Tusemezane
 
Hayati Shaaban Robert aliielezea siasa ifuatavyo "Kwa mzoea ndoto na mpenda kujipoteza katika mawazo huona siasa ina wingi wa mambo ya kufikiri na kutenda. Macho yake huvutwa juu na chini,nje na ndani,mbele na nyuma,na kulia na kushoto ya nchi, uraia na serikali. Kwa muhtasari na kutaradhia,katika kupima na kuhidi na katika kadha na kadhalika."
 
MTAZAMOKUHUSU KINACHOJIRI DODOMA HASA ANGA ZAKISIASA Wanaduru Makundituliyosema yanawindana na hicho ndicho chanzo chasakata hili kushikiwa bango Zaidiya masakata mengine. Pengine tujaribukuangalia kuhusu hali ya wabunge wa CCMna sakata zima. 1.Mgombea mtarajiwa EL anaungwa mkono na kundilake linalopigana kuhakikishaanafikia ndoto aiyowahi kusema ni ya matumaini.Uwepo wa waziri mkuu mwinginealiyechufukakutasaidia kuondoa kikwazo cha EL katika king'anyiro kwa hoja kuwawotewamewajibika kama EL na wala siyo makosa Kundi lake linataka Pinda ambaye ametangaza niakuenguliwa katika kinyang'anyiro. Pinda anaonekana tishio hasa baada ya kutoa mwelekeo Kashfa itawaondoa vijana kama Ngeleja ambao naoni sehemuya makundi Kashfa itaondoa watu kama Anna Tibaijukawanaotajwa kama akina mama Hivyokashfa ina manufaa kwa timu EL kuliko mgombeamwingine 2.Vijana Kundi hili linaunga mkono sakata la Escrowkwasababu yakutaka kupunguza ushindani. Kwasasa, January ni mmoja wawatarajiwa. Kuondokakwa Ngeleja kutamsaidia abaki na vijana dhaifu Kundi la vijana lingependa kashfa hii iondoke nawatu ilikujinasibu kuwa vijana wanaweza. Kundi linaunga mkono vijana wa upinzani ambaonao kama wenzao wa CCMwanataka kutumia kashfa kupanda ngazi au kujijenga tenakisiasa. 3.Waliovurunda Hapa wapo akina Sitta, ambao kuondoka kwa baadhi yawatukunaweza kuwasaidia kutajwa Zaidi hasa baada ya kuchafuka kutokana nakuvurundakatika uendeshaji wa bunge la katiba Katika kundi la kuvurunda yupo Membe. Huyuanawindwa kwa tuhuma za Radar ambazoamezificha bila kutaja wahusika. Naye piaana kashfa zinazotajwa tu kuhusiana napesa zinaoztoka nje. Hayo ni tuhuma. Nimmoja wa wagombea dhaifu, hata hivyouwepo wake unaonekana kupunguza nguvu yatimu EL 4.Kundi la wasaka nafasi za huruma: Hili halinanguvu sana, isipokuwalinategemea huruma na muda wa kujijenga. Linataka waliopowaondoke ili wawezekupata nafasi za kujitanua. Hapa wapo akina Mwandosya,Mwigulu. Kundi la huruma lingependa waliopo waondoke ili waowapatenafasi, lakini halipendi serikali kuanguka au kashfa kuumiza Zaidi kwakuelewafadhila wanazotegemea kutoka katika serikali iliyopo kama kukwea ngazizakisiasa 5.Kundi la wazalendo: Hili linachukizwa namwenendo wamambo. Linapiga kelele ili kashfa zifike mwisho. Kwa bahati mbayasana ni kundi dogo lisilo na ushawishi na linaloweza kutishwakirahisi. 6. Kundi la hohe hahe: Hili halikuwemo katikampango na wala halijui kama kunamipango ya mamilioni. Lipo lipo tu kwakutegemea masilahi ya ubunge. KUNDIPINGAMIZA Hili nikundi la waliofaidika na mgao wa Escrow.Linahusisha wazoefu wa ma-deal nalisingependa kashfa hii izungumzwe. Ni kundilenye nguvu sana ndani ya chama,linalopanga safu za viongozi kutoka naushawishi wa fedha ulio nazo. Kundi hililinaunga mkono kundi namba1 na limefanikiwakuwaingiza katika mtego kundi namba2 na wale waliokuwa hawatarajiwi kama mamaAnna Ikumbukwendilo kundi lililomuondoa Sitta na kumweka AnnaMakinda. Hivyo,anachokifanya Makinda ni kutetea masilahi yawateule wake. Kaziinayomkabili ni kuhakikisha kashfa inakufa auinafifia. KUNDI MASILAHI Hili ndilolimetibua kila kitu na kumwaga mtama. Kundi hililinaongozwa na mbungealiyenusurika kwa kutuhumu kulishwa sumu. Hili lilikuwalina mikataba minono nandilo linalosemwa limemwaga data zote. Kundimasilahi lina vijana waliojipambanua kamawapambanaji ambao nao wana masilahiima ya moja kwa moja au ya kisiasayatakayotokana na ushindi dhidi ya kashfa. Inaendeleana kundi la upinzani dhidi ya hoja ya escrow MATATIZO NDANI YA CCM Makundi yote yana masilahi yao na wala hayaunganishwi nakitu kimoja. Litakuwa jambo gumu sana kwa CCM kuyaweka pamoja siku za usoni. Ningumu kufariji kundi moja bila kuudhi jingine. Hapo ndipo pana tatizo. Uwepo wa makundi tajwa hapo juu unaweka suala la katibaya CCM njia panda. Kwa mfano, katiba pendekezwa ya CCM imeandaliwa na kundi‘'pingamizi la Escrow'' likiongozwa na mh Cheng.Makundi mengine hayatakubaliana na ushindi wakundi pingamiza ima katika escrow au katiba ya CCM. Kundi pingamizi la Escrow ndilo limeandika katiba ya CCMinayopendekezwa, hasa kwa kuondoa vipengele korofi kama maadili ya viongozi.Utaona watajwa wa kundi hili ni wazoefu wa kupiga ma deal. Wapo katika kilakashfa. Ni bahati mbaya, ule uungwaji mkono ulioonekana bunge lakatiba sasa umeingia nyongo. Uhasama unaojengeka utakwenda mbali Zaidi kama maeneo yakatiba. Ikitokea suala la katiba likajadiliwa tena bungeni, UKAWAitaungwa mkono kuliko ilivyokuwa hapo awali. Itaendelea….
naona LUSINDE alishindwa kutoa credit kwa nguruvi3,kwamba kuhusu makundi amecopy JF
 
Hayati Shaaban Robert aliielezea siasa ifuatavyo "Kwa mzoea ndoto na mpenda kujipoteza katika mawazo huona siasa ina wingi wa mambo ya kufikiri na kutenda. Macho yake huvutwa juu na chini,nje na ndani,mbele na nyuma,na kulia na kushoto ya nchi, uraia na serikali. Kwa muhtasari na kutaradhia,katika kupima na kuhidi na katika kadha na kadhalika."
Mkuu, hapa umeniacha porini kidogo. Unajua Shaaban Robert kila mstari wa maandiko yake ni mtihani. Hebu tunyumbulie kidogo katika lugha laini maana hapo uliopo ni parefu
 
SERIKALI YAWEKWA ‘MATEKA' NA WATUHUMIWA
MBINU TULIZOSEMA SASA ZINATUMIKA

MTUHUMIWA APEWA NAFASI YA KUPENDEKEZAADHABU YAKE

Bungelimeahirishwa baada ya kukosekana muafaka wa hatua za kuchuliwa dhidi yawatuhumiwa. Jambo moja lililowazi, maazimio 7 bunge limeyakubali. Hii maanayake ni kuwa bunge limekubali uwepo wa uhalifu na wahalifu.

Hoja ya pesakutokuwa za umma imekufa. Maazimio yanaondoa utetezi wowote kuhusu pesa. Tatizolililopo ni hatua za kuwachulia wahalifu.

Mtakumbuka,mabandiko ya nyuma tumeeleza nia yaserikali kuliondoa jambo hili katika macho ya watu ili serikali ifanye mbinu zakuficha na kulindana kwa kutumia mbinu za uchunguzi unaendelea n.k.

Mbinu hizozimeanzishwa na Ikulu kupitia katibu mkuu kiongozi kabla ya kushindikana.
Mbinu zakuzuia kwa kutumia Mahakama nazo zimekwama.

UTETEZI HAFIFU
Utetezi wakushindwa kuwachulia hatua wahusika kwa maana ya kuwawajibisha kisiasa,zimewekewa kikwazo cha kuingilia mhimili mwingine.
Kwamba,mamlaka za uteuzi ndizo zitawawajibisha.

Serikaliilipotafuta mbinu za kuzuia mjadala ilikuwa kuingilia mamlaka nyingine.
Mahakamailipotumiwa kupeleka barua ilikuwa kuingilia mamlaka nyingine.

YALIYOPITA
Mbinuiliyotumika kuficha uhalafi wa Rada, Meremeta, Tangold , EPA na Richmondhazitoa majibu hadi leo. Kesi za kubabaisha zipo na hakuna matokeo ya maana.
Weziwaliohusika na kashfa kama za Richmond sasa wanahusika na Escrow.

Tunajuaofisi ya mwendesha mashataka si huru, ofisi za uchunguzi kama Polisi si huru.Vyombo kama PCCB si huru. Hivyo kurudisha suala hilo kufanyiwa uchunguzi nikutaka kulinda wahalifu kwa kuwafanya Watanzania wapuuzi.

Endapohatujui pesa za Rada ziliztokaje, au za EPA, ni vipi watu waamini wahusika waEscrow ambao wengine wamehusika huko nyuma watachululiwa hatua

Jambo lakushangaza ni kauli ya kufanya uchunguzi.
Vyombovilivyochunguza ni vya umma, kipi tena kinahitajika ili uchunguzi ukamilike?

Bunge hililinaloendelea liliwahi kutoa mapendekezo katibu mkuu nishati awajibishwe kwakutoa rushwa bungeni. Rais alikataa na kumpa nafasi ya kustaafu.

Leowanaambiwa Rais ana uwezo wa kuhangaika na mapapa ya kifasadi. Kama huo siudanganyifu hatujui ni kitu gani.

MAKINDAATUMIWA
SpikaMkainda wamerudi kuchukua nafasi yake baada ya Job Ndugai kupelekwa likizo kwa kile kilichosemwa kushindwa kuzuiamjadala.
TunakumbukaMakinda alichaguliwa chini ya usimamizi wa mafisadi

Kazi kubwa ni kulinda mafisadi. Jana, katika hali yakushangaza na kuchekesha, Anna Makinda alimpa nafasi Andrew Chenge ya kutoaushauri wa adhabu ya watuhumiwa!!!

AndrewChenge ni mutuhumiwa mzoefu, na hili la Escrow amepokea Bilioni 1.6.
Kamamtuhumiwa, Chenge ana nafasi ya kujitetea lakini Chenge hana nafasi ya kutoaushauri watuhumiwa wachukuliwe hatua gani ikiwa yeye mwenyewe ni mtuhumiwa.

MBINU INAYOTAKIWA KUTEKELEZWA
Nikulirdisha suala hili kwa serikali. Rais afanye mbadiliko ya baraza la mawazirina nafasi nyingine akiondoa watuhumiwa. Ndivyo alivyomuokoa Jairo na Luhanjo

Watakamatwadagaa ili kesi iwe mahakamani na kuzuia mjadala usiendelee popote kamailivyokuwa kwa Richmond na EPA

Bungelitaendelea kutokuwa na haki ya kuhoji kwa msingi kuwa suala lipo kwenye vyombovya serikali kwa uchunguzi na suala lipo mahakamani. Ndiko Makindaanapowaelekeza wabunge leo hii

Kesizitaendelea hadi uchaguzi ujao. Kesi hizo zitamalizika kwa kutokuwa na ushahidiwa kutosha. Watuhumiwa watakuwa wamelindwa, na serikali itakuwa imelindwa.

Mzunguko wawizi wa kodi utaendelea kwa kasi, wananchi watamenyeka vilivyo na watarudi tenabungeni kutaka wezi wajiuzulu. Imetokea miaka 7 iliyopita na ndiko wanakoelekea

Wafadhiliwataaminishwa suala limeshajadiliwa bungeni na vyombo vya dola vinashughulikia.

Hadi hapowatuhumiwa watakuwa huru wakinufaika na uhalifu, wananchi wakiendelea kulipagharama zinazotokana na uzembe wa watu watakaokuwa wanaia kivulini

Inaendelea…….
 
HII MAANAYAKE NINI
Ni kuwa
Chenge kamakiongozi wa mtandao wa ufisadi ameiteka serikali.
Kwa sasaanaamuru serikali ifanye nini.

Umiliki waserikali haushii hapo. Mtuhumiwa huyo na wenzake wamepewa nafasi ya kuandikakatiba, seuse kushauri wahalifu wachukuliwe hatua zipi!

MTANDAO NIMPANA NA UNATISHA
Waziri mkuualiwahi kusema mtandao wa mafisadi ni mpana na unatisha.
Leo tunajuaukweli wa kauli hii. Ni mafisadi wanaoamua nani awe kiongozi nani ajiuzulu.Wapo bize wakimtetea waziri mkuu kama alivyowahi kusema ni hatari.

Mafisadiwamefikia hatua ya kuamuru serikali na chama kifanye nini.
Serikalihaina nguvu mbele ya mafisadi na CCM imeshasalim amri.

MAKOSA YAWANANCHI
Wananchi wanadhanikurudishwa kwa pesa au kujiuzulu kwa viongozi ni njia muafaka.
Viongozi waserikali wana uwezo wa kushughulikia tatizo.

Tatizo linajirudia,na zinatakiwa hatua madhubuti ili kudhibiti uhalifu huo.
Njia mojakubwa ni wananchi kuchukua ownership ya maamuzi ya nchi.
Si kazi yawananchi kukimbizana na mawaziri, makatibu wakuu n.k

Wananchiwana njia rahisi, nayo ni kutaka waliomwajiri awajibike.
Mwajiriwa huyo si mwingine bali Rais wa Jamhuriya muungano.
Wananchi waTanzania, mlinzi wa watu na mali zao ni Rais, si katibu mkuu.

Wananchiwana dhima ya kumwajibisha mwajiriwa wao ambaye ni Rais na wala si waziri mkuu,waziri au katibu mkuu

Njia ya pilini kuwapa ujumbe wabunge wanaotetea wizi kuwa hatima yao imefika.
Tatu nikukiadhibu chama tawala kwa kushindwa kuendesha dola na badala yake kuwa matekawa mafisadi, katika sanduku la kura

Wananchi ndiowaathirika kule Muhimbili na Kariakoo sokoni, ni wajibu wao kuelewa kuwa CCM nadola sasa vipo chini ya uangalizi wa wahalifu. Ni sababu hizo ndizo zinapelekeamateso wanayoyapata

Hoja yakumwajibisha rais ipo katika ukweli kuwa kwa miaka 7 aliyokaa madarakani,kashfa za wizi zimepamba moto na wala haionekani kuwa na dawa.

Hilo linaeleza kushindwa kwa Rais kusimamiamali na watu, na kushindwa kuongoza.

Kibaya Zaidi,Raisaliyepewa vyombo vyote muhimu vya dola anaposhindwa kuwawajibisha wateule wakekwa hofu ya ukubwa wa mtandao, inatisha sana.

Kwa manenomengine, usalama wa wananchi wa Tanzani haupo mikononi mwa Rais, bali mafisadi.

Tusemezane

 
Hii ni hatari na tutaendelea kunyanyaswa sana.
 
LA ESCROW LIMEZIKWA LEO
WANANCHI WATANZANIA WAMESHINDWA VITA NA MAFISADI

WANASIASA WAMEFANIKIWA KUPANDISHA CHART ZAO

Mabandiko yahapo juu tumeeleza mbinu zilizopangwa ili kuliondoa suala la Escrow bungeni nakulirudisha serikalini.
Huko serikali inafahamika ‘nchi ipo mateka'' Mafisadi wataamua namna ya kumaliza mjadala


Eti imesemwa vyombo vya dola vitashughulikia. Ikiwa bunge halikuweza kumshughulikia mawazirina makatibu wakuu, ni kituko kama koplo wa Polisi ataweza

Tunakumbukumbu za Rada, Richmond,Dowans, n.k. yaliyokabidhiwa serikali.
Hadi leouchunguzi unaendelea, wezi wanavumbua mbinu, nchi inavunwa kwa gharama kubwa yawananchi masikini wanaoishi kwa dola 1 kwa siku


Kama unataka kujua kifo cha Escrow, ni pale mbunge Ole Sendeka alipotaka pawepo nakufuatiliwa bungeni kwa maazimio. Spika Makinda akakataa na kusema ‘tuaminiane''Yaani mtu kama Muhongo aaminiwe kufanya uchunguzi !!!

Maazimio yaliyotolewani kichekesho pia. Kwa upande wa CCM na serikali waliolenga kuficha ukweli,kulinda watu na familia zao kwa kuzingatia unyeti wa suala lenyewe, hakika wamefanikiwa. Wao wana Polisi, usalama wa taifa, na kila chombo

Watatumiavyombo vyao kulindana. Utamaduni uliokomaa.
Hiki ndicho wanasiasa waliaminisha watu kuna tatizo na wanapigania masilahi ya umma.

Hakuna ambacho umma umepata. Umma umeshindwa na mafisadi walioteka serikali.
Wananchi wamepata kipigo na leo mafisadi wanashangilia kwa champagne ushindi mnono uliopatikana kwa msaada wa PAC,Zitto, Mbowe na Upinzani.

Ni kituko kwa wezi na walioibiwa kukaa meza moja wakitafuta maridhiano.
Lini wezi wa kuku walikaa meza moja na polisi kukubaliana wapi wafanyie kazi na wapipaachwe.

Wakati wananchi wakiwa wameshindwa mpambano, wanasiasa sasa wanajipanga kutangazamajina yao.
Wanatumia kipigo walichotoa mafisadi kama ngazi za kukwea kisiasa.Ndivyo ilivyokuwa kwa scandal nyingine


Kuanzia leo tutakuwa na mbandiko mfululizo tukieleza nini kimetokea na kwanini.
Tutachambua madhaifu yote yaliyojitokeza ikiwemo ulaghai wa wanasiasa

Tutawaelezawananchi nani wa kuamini nani wa kutililiwa shaka.
Katika kufanya hivyo,hatonewa mtu wala hataonewa huruma awaye.


Tutaangaliakwa undani kisiasa na kijamii nini hasa kimetokea, na malengo yake ni yapi.

Ingawa tuliyoeleza yote yametokea, haitakuwa vibaya tukiyaweka katika uhalisiana matokeo ya leo kwa kuoanisha hoja moja hadi nyingine.


Ni mfululuzowa mabandiko 7 kuanzia kesho, jumapili.

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3, wakati uko mapumzikoni, naomba nikupe zawadi hii;

ESCROW.jpg

AG Werema, Ex-AG Chenge na Mkono.
Soma hizo body language!
 
Last edited by a moderator:
Mag3, mwenye macho haambiwi tazama. Baada ya madole nasikia walimkosa kosa London
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom