Duru za siasa: Matukio nchini na duniani kwa ujumla

Duru za siasa: Matukio nchini na duniani kwa ujumla

Nilipita tu kufyonza ilmu hapa.

Mimi msisitizo wangu upo pale pale SKULI NI MUHIMU SANA. NA ILMU NI BORA SANA KAMA UTAIPATA SEHEMU SAHIHI na sio hizo za propaganda.

Siasa za Middle east ni ngumu na pana sana NA KILA MTU ANAWEKA PROPAGANDA ZAKE kwa maslahi ale lakin ukweli upo kweupeeeeeee.

Nikinafasika nitawawekea mambo kadhwa hapa na website mpitie muone.

Aksantum kwa darsa
 
Sehemu ya I

WANANCHI WAMESHINDWA NA MAFISADI

KAtika sakata la Escrow, wananchi wameshindwa vita dhidi ya ufisadi. Kushindwa kwao kunaelezeka kwa namna tofauti.

  1. Kwamba, hawajaweza kuzuia madhara ya mafisadi kutokana na kujirudia
  2. Mategemeo ya kuwa na suluhu ya kudumu (durable solution) dhidi ya ufisadi yamekwisha
  3. Wameendelea kuamini vyombo vya umma vilivyowajifisha walipo sasa
  4. Wanaendelea kuumia kwa gharama za ufisadi na mafisadi
  5. Wameendelea kudanganywa na wanasiasa wakitumiwa kama ngazi za kufikia malengo ya kisiasa
  6. Hali zao zinazidi kudumaa, huku wakimenyeka kulipa kodi wasizostahili
  7. Wanasalitiliwa na wale waliowaamini kwa mjaina ya viongozi

Kuhsindwa kwa wananchi kunatokana na mambo kadha wa kadha

  1. Wananchi kutojitambua na kutotambua haki zao wakidhani kutendewa ubaya ni haki yao na kutendewa wema ni fadhila.
  2. Woga uliojengwa na wahuni , kwamba, kudai haki zao ni kuvunja amani na utulivu. Kwamba amani na utulivu ni zao la wao kukaa kimya hata wakiumia.
  3. Kuamini serikali licha ya kudanganywa miaka nenda rudi
  4. Kutokuwa na ari ya kuwajibisha waliowaweka madarakani
  5. Kuamini wanasiasa badala ya kuamini hoja za nguvu zao wenyewe

KUTOJITAMBUA
Hili ni tatizo zito sana. Kwa miaka zaidi ya 7 na mingine ya nyuma, wananchi wameshuhudia mafisadi wakipora rasilimali zao huku wakiaminishwa serikali inachukua hatua dhidi ya rushwa na ufisadi.

Hadi leo hakuna jibu la kashfa yoyote kubwa iliyowahi kutokea. Kila wanapouliza, jibu ni serikali kuendelea na uchunguzi.
Haiwezekani serikali yenye vyombo vyote ikashindwa uchunguzi kwa miaka 7.

Haiwezekani wananchi wasijue nani aliingia hazina akachota pesa za rada, pesa zimerudi kwa nani na zinafanya kazi gani.

Muhimu zaidi ni kuwa hata wanapofunguliwa vichwa , bado hawaamini wanachokiona.
Tumeona jinsi pesa zilivyoandaliwa na Ikulu kuhonga wana habari na wasomi ili katiba ambayo basically ni ya wananchi ipite.
Hii ndiyo ofisi inayomiliki vyombo vyote, sasa kama inatoa rushwa, ni lini na kwa vipi inawza kushughulikia rushwa?

AMANI NA UTULIVU
Kauli hiyo uinatumiwa kuwatisha wananchi wasidai haki zao au kuwawajibisha wahusika.
Kwa mfano, mwezi mzima hospitali hazina dawa, watu wanalala sjkafuni mahospitalini wakisubiri hatima za maisha yao.

Wananchi hawajitambui kwa kujiuliza, kama hakuna pesa, zile walizojipangia wabunge na maafisa wa serikali kwenda kutibiwa nje zinatoka wapi?

Wanachoambiwa ni kuwa kuzungumzia haki zao ni kuvunja amani na utulivu.

Labda wajiulize, wakati kuna mtu hawezi kununua dozi ya malaria, inakuwaje kiongozi wa serikali apewe milioni 40 bila sababu?
Ili kuzuia kuhojia, wananchi wanaambiwa kuuliza ni kuvuruga amani na utulivu.
Kwamba, amani ipo wkiteseka kimya, wakidai haki zao ni kuvuruga amani.

KUAMINI SERIKALI NA VYOMBO VYAKE
Wananchi hawajitambui, kwamba haiwezekani wezi wakatumia njia zile zile kila siku kuiba na serikali isiwe na jibu. Hakuna kesi au tatizo lolote ambalo wananchi wanaweza kusimama na kusema serikali imelipatia ufumbuzi.
Lakini, bado wanaamini kuwa ipo siku serikali itakuja na majibu ya jumla ya matatizo yote. Miaka inasonga mbele….

KUAMINI WANASIASA
Hili nalo ni tatizo. Katika sakata la Escrow, wengi tulisema hoja si pesa za umma kurudishwa.
Hoja ni kupata majibu ya kudumu ya kukomesha hali iliyojitokeza.
Escrow si suala la watu wachache, ni tatizo la mfumo mzima.

Wanasisasa hawakueleza wananchi ubovu huo, walitumia hoja dhiafu za uzalendo, upigananaji na kutaja majina ya wapiganaji hata kama ilikuwa wazi hiyo ilikuwa ni kujijenga kisiasa ''political stunt'

Ndio maana tumeona suala la Escrow likiwa limelenga zaidi watu badala ya mfumo.
Likiongelewa kama hoja za viongozi ABCD badala ya hoja ya wananchi.
Likalenga baadhi ya watu na kuacha sehemu kubwa sana ya tatizo kama tunatakvyoeleza.

Kwasasababu lengo la wanansiasa ni kujenga majina yao, maazimio yaliyofikiwa na bunge hayana msingi wowote wa kumaliza tatizo, wala hayakuleta matarajio yaliyokusudiwa na wananchi.

Wananchi wajiulize, inawewzakanje kukawa na maazimio ya maridhiano katika ya wezi na waliobiwa?
Kitu gani kinaridhiwa? Kwamba kuna majadiliano ya wahalifu na uhalifu.

Baada ya aazimio ya wezi na walioibiwa, wanasiasa sasa wanatoka na kuaminisha umma tatizo limepatiwa jawabu! Wanajifaragua kwa majina yao kutajwa kama vinara na wapiganaji. Kipi walichokipagania hadi wakaja na maridhiano na wezi?

Inaendelea……
 
TATIZO LA ESROW SI NANI AMEIBA, BALI NINI KIMESABABISHA WIZI

Tunakumbuka tatizo la madni lililoanza kwa hoja zile za Buzwagi.
Mwisho wa siku kamati iliundwa na hadi leo tatizo lipo pale pale huku serikali iliyosema inashughulikia ikiwa imekalia taarifa hizo makabatini. Wanasiasa wakapanda chati, wananchi wakapoteza!

Ndivyo ilivyokuwa kwa EPA, Richmond n.k. Haiwezekani eti wananchi waambiwe pesa zilitoka hazina bilioni 28 na hakuna anayewajibika au aliyebainika kuzitoa.

Hakuna jibu la mfumo uliotumika na udhaifu wa mfumo kudhbiti tatizo hilo.
Wanasiasa walipanda chati kwa kelele, wananchi wakapoteza kwasababu hawana jjibu.

Tatizo la Escrow si tofauti. Wananchi wasichokitambua ni kuwa huu ni wizi unaofanywa na genge la watu wenye elimu, watu wanaoweza kuiba na kusimama mbele kusema hawakuiba bila kuchukuliwa hatua.

MFUMO MZIMA WA WIZI

Ukitazama kwa undani, suala la Escrow si uzembe wa watu wawili. Ni mfumo mzima uliokufa.
Ndizo sababu za taasisi mbali mbali za kijamii, asasa na watu binafasi kuwa sehemu ya uhalifu huo

Tunasema uhalifu kwa uhakika kwasababu bunge limekubali upo uhalaifu ndio maana limeagiza uchunguzi na hatua za kuchukuliwa. Hivyo, si suala la kusema kuna uhalaifu, bali uhalifu upo tena wa kiwango cha juu sana.

Tumeona mzozo mkali kati ya watu watatu au wane, hasa waziri nishati, katibu mkuu nishati, waziri mkuu na waziri mmoja aliyetuhumiwa kwa uoenvu mama Anna Tibaijuka.

Tuna sababu za kusema Tibajuka katuhumiwa bila sababu za msingi.
Na hapa tufafanue kabla hatujaendelea na ubovu wa mfumo mzima.
Ukisoma orodha ya wahusika na taarifa, hakuna mahali jina la Tibaijuka limejitokeza katika Escrow.

Jina lake limetokea katika wale waliofadika na mgao wa pesa hizo ambaozo bunge limeridhia ni haramu kwa kusema Stanbic inatakatisha.

Orodha iliyotolewa ni ya account moja. Hakuna orodha iliyo wazi ya account zingine na hivyo hatujui wangapi wamefadika na mgao Tibaijuka kapokea kama msaada, hata kama alikuwa na dhamana ya kutulia shaka, na kwamba, ni kiongozi alitakiwa kuwa makini, swali ni kuwa viongozi wangapi wamepokea mgao huo na majina yao hayakutajwa tena pengine moja kwa moja kuliko ''msaada''?

Kwanini ionekana mama Anna Tibaijuka peke yake na wala si mlololongo mzima uliochukua pesa hizo haramu?
Nani anajua majina yaliyotajwa yalikuwa na uhusiano na viongozi wengine?

Mfano, lingetajwa jina la kachabuseta kupata milioni 600, je tunatakiwa tukae kimya tu kwasababu mtajwa si waziri?
Vipi kama mtu huyo ametumika kama conduit(njia tu) ya kupatishia pesa za wazee?

Mfano mwingine. Ukisoma orodha ya wafaidika utaona watuhumiwa wakubwa kama waziri na katibu au wale wa ofisi nyingine kama BoT na Ikulu hawapo. Kwanini waziri au katibu mkuu apiganie jambo ambalo mgao wake haupo?

Je, tuamini tu kuwa makosa yao ni kufanikisha dili bila ya malipo ya aina yoyote?
Kama walipata mgao, wapi majina yao yaliyopo?

Kwanini Anna aliyepata aoenkane peke yake?
Huko BRELA na BoT hakuna waliosadia kusukuma cheki za pesa za mbele?

Wameyajwa majaji katika mgao na viwango vyao.
Kwanini hakuna anayeona kama kuna ukiukwaji wa maadili, lakini watu wadhani Tibaijuka ndiye pekee aliyekiuka maadili?

Turudi katika mfumo
Ukitazama ripoti, kila sehemu ya serikali, bunge na mahakama ambayo ni mihimili mikuu ya nchi.

Escrow si suala la kisiasa ni la Kiuchumi. Kuzagaa kwa pesa kunaweza kuwa na athari katika mzunguko wa pesa, na anayepokea athari ni mwananchi anayeishi kwa dola 1 si ‘mwenye nchi aliyepata dola 10,000 au zaidi''

Katika nchi yetu tuliko la kampuni hewa liliwahi kujitokeza kwa Richmond.
Ubalozi wetu ukatusaidia kubaini kampuni hiyo hewa.
Tulidhani hilo lilitakiwa liwe funzo kwamba balozi zetu zina nafasi katika usalama wa nchi kiulinzi na kicuhumi.

Inashangaza tatizo limejirudia kwa kuwa na kampuni hewa kutoka Malaysia iliyoingia katika Escrow.
Hatukutumia balozi zetu, tumetuma mtu kwenda kuchunguza badala ya vyombo vya kidiplomasia.

Leo tumetengenezewa umeme na kampuni hewa. Tunaambiwa bora umeme umekuwepo.

Tujiulize katika hali hii, hivi si kweli kuwa ipo siku makundi kama Alshababab yanaweza kuja kuwekeza nchi katika sekta nyeti, yakisoma siri za nchi napengine kuleta hujuma kubwa kwa taifa?

Hivi taasisi ya BRELA kazi yake ni kuorodhesha majina ya kampuni au ni zaidi ya hapo.
Kwanini taarifa hakuonyesha ima kuzembea au kuhongwa kwa viongozi wa BRELA? Hili si tatizo la mfumo kweli!

Usalama wa taifa

Huu kazi zake ni zaidi ya kulinda viongozi. Inapotokea tapeli anaweza kuja na kampuni hewa, akawekeza, akavuna pesa tena akinunua viongozi waliokula kiapo cha umma, hapa hakuna hujuma kutoka taasisi hii muhimu katika uchumi na ulinzi wa taifa kweli!
Mbona hatukuona ushiriki au kutoshiriki au jitihada za taasisi hizi katika suala zima.

Inaendelea mfumo……..
 
Last edited by a moderator:
''''Wananchi kutojitambua na kutotambua haki zao wakidhani kutendewa ubaya ni haki yao na kutendewa wema ni fadhila'''-nguruvi3
mkuu hali hii imeshakua kama ugonjwa,ndo mana leo ata ukienda taasisi yote ukipewa huduma mzuri,unashukuru na kutoa ahsante,ndomana akitokea kiongozi akawa na mambo mazuri machache, anaonekana mtu mzuri,wakati ametimiza wajibu wake,ni sawa na kusifia serikali kwa kujenga shule,au barabara
tatizo tuna NAKISI YA UADILIFU,tumekuwa kama taifa lilishikwa MATEKA,ukiachiwa HURU unatoa AHSANTE KWA JAMBAZI NA KUMUONA MWEMA
 
Shemu ya III

Mfumo

Tunaendeleakuangalia mfumo unaozaa ufisadi. Eneo jingine ni BoT, chombo huru, (Gavana) akiwa mteule wa Rais kama Mwanasheria mkuu,mkuu wa taasisi ya usalama au awaye.

Hoja ya PAC: BoT ilisita kuidhinisha malipo. Utetezi ni hafifu kwasababu PAC inasema, baadaye BoT ikabidi itoe pesa kwa shinikizo la mwanasheria mkuu.

Haiwezekani AG akamshinikiza Gavana wa benki kuu. Ilikuwepo nafasi ya Gavana kuonana na waziri mkuu au mkuu wanchi kueleza wasi wasi kwa kuzingatia kiasi cha pesa na athari zake katika uchumi kwa mzunguko


Inajulikana katibu wa Rais naye alishinikiza. Bado Gavana kama mteule mwingine alikuwa na nafasi ya kuonana na mh Rais kueleza wasi wasi.

Aidha,kulikuwa na nafasi ya kutaarifu vyombo vya usalama.
PAC haukueleza jitihada zaBoT ziliishia wapi. Wanachosema, BoT walijaribu sana kuzuia.
Well, hawakujaribu kwasababu wizi umetendeka on their watch.


Wizara yafedha
Nayo inahusika na mambo ya fedha kwa kuhusiana na benki kuu na mabenki mengine.
Haionekani kama wizara ilikuwa na ushiriki au la, tunachojua PAC haikueleza kwa kina upande huo.
Ni kwanini, linabaki kuwa swali la kujiuliza


TANESCO
Zimekuwepo tuhuma kuwa mwenyekiti wa bodi alikuwa anashirikiana na wafanyabiashara kutengeneza mgao ili kuagiza mafuta. Tuhuma hizi na mikataba ya haraka harak ailipaswa kutiliwa shaka kuanzia mwanzo.
Leo tunafahamu Tanesco imeshiriki vema katika wizi kwa namna nyingi, kuanzi mikataba n.k.


Mwenyekiti au mkurugenzi mtendaji walikuwa na nafasi ya kuonana na uongozi wa nchi ilikueleza wasi wasi kuhusu malipo, au capacity charges zisizolingana na mkataba, kiashirio kizuri sana cha hujuma.

Ofisi yawaziri mkuu
PAC imeelezawaziri mkuu alikuwa na taarifa za kinachoendelea.
PAC haikuenda mbali kutafuta endapo PM alikuwa na mawasiliano na bosi wake ambaye ni Rais.

Hatuelewi kwanini PAC haikuenda mbali Zaidi kutafuta ukweli na kuishia katika hoja yaofisi ya waziri mkuu kushiriki.

Ofisi ya PMhaikutumia vyombo vyake kubaini ukweli. Walichofanya ni kutoa kauli za uongokuhusu pesa.
Ofisi ya PM ilikuwa na kila sababu za kushtuka tukizingatia uzembe wa vyombo vingine tulivyoeleza.

Ukifikiria kuwa katibu wa Rais alishinikiza, inakuwaje ofisi ya waziri mkuu na oifisi ya Rais visiwe na mawasiliano ingawa wantu mmoja mmoja wana mawasiliano? Nini kilitokea hapo haijaelezwa.

Inaendelea...
 
sehemu ya IV

BUNGENI
Ni eneo lilionyesha udhaifu mkubwa wakati wa kujadili suala la Escrow
Bunge lilikuwa tayari kuuza nafasi yake kwa kutumia mhimili wa sheria ili kulinda watuhumiwa.

Watoa hoja walipata nafasi ya kuungwa mkono na wenzao wa UKAWA
Pengine hilo lingeanza mapema , kutokana na migogoro wote wakaunganishwa na Escrow

Wapinzania waliungwa mkono na mkundi ya CCM yenye masilahi tofauti yaliyotaka kuona ‘mahasimu wao'' wakianguka tukielewa safari ya kuelekea 2015 inachezwa rafu.

Hata wale CCM waaminifu, ilikuwa ni dhahiri hawakutaka kuhusishwa na sakata hilo.
Ndio maana CCM ikawatuma watu vituko kwenda kutetea serikali.

Ule utamaduni wa CCM kuwafunga midomo wabunge wako nao ulitumika.
Ndio hasa msingi wa manung'uniko ya chini kwa chini.

Wabunge wa CCM walikuwa na hofu iliyosababishwa na

  1. Ugomvi unaoweza kukigawa chama, hata katika masuala yanayohitaji umoja wao kama yale ya katiba ya CCM wanaotaka kusikumiza kwa wananchi
  2. Chuki kuendelea na kudhoofisha nafasi za watarajiwa, kukiweka chama katika wakati mgumu
  3. CCM kuchafuka na huenda ikawa ndio mwanzo wa anguko kwa hasira za wananchi

Ni kwa mtazamo huo, upinzani ulikuwa na nguvu kubwa kuliko ilivyowahi kutokea huko nyuma.

Ni kwa bahati mbaya, wapinzani si watu wa kusoma kutokana na makosa ya nyuma.

UDHAIFU WA WAPINZANI
Hakukuwa na shaka kuwa CCM ilitambua uwepo wa hujuma.
Kutokana na watu mbali mbali kukingia kifua Escrow isijadiliwe bungeni, wapinzani walitakiwa kuelewa na tuliwahi kuwaambia wasiruhusu jambo hilo likarudi serikali.

Nia ya serikali ni kuficha escrow na kutumia mjadiliano ya bunge kama muafaka kabla ya kwenda kwa wafadhili.

Inajulina PCCB, DPP, Police na sasa mahakama ni vyombo vya serikali.
Haiwezekani serikali ikatumia vyombo hivyo kujikaanga.

Wapinzania walitakiwa kuelewa taarifa ya CAG na PCCB ilikuwa ni mwanzo mzuri wa uchunguzi na mashtaka kwa wahusika bila kuanza mlolongo wa urasimu utakaohusisha serikali.

Hadi leo hakuna kashfa hata moja iliyotanzuliwa.
Kila mara serikali inasema uchunguzi unaendelea, wapinzani wanaamini ni muafaka kurudi serikalini.

NJIA ZILIZOTUMIWA
Kwamba, waliotuhumiwa ni wateule na hivyo bunge halina njia ya kuwawajibisha isipokuwa kumshauri rais atengeue uteuzi wao. Ukisangalia majadiliano, hilo ndilo lililokuwa kubwa sana kwa CCM na serikali

Wapinzani wamesahau huko nyuma waliwahi kutoa mapenedekezo kama hayo na hayakufanyiwa kazi. Watuhumiwa wa rushwa kama katibu mkuu Jairo wakapewa nafasi ya kustaafu.
Bunge likapoteza, wananchi wakapoteza.

MBOWE
Wapinzani walipotaka kuondoka bungeni, kiongozi wa upinzania aliwazuia.
Hili lilikuwa kosa kubwa. Lini CCM imekubali majadiliano na wapinzani?

Mbowe amesahau miswada imepitishwa kwa nguvu huko nyuma tena kukiwa na wabunge 100 wa CCM.

Mbowe amaesaahu Bunge la katiba CCM haikutaka kujadiliana kama alivyosema Makinda
Mbowe alipaswa kuwaacha wapinzani watoke, ili CCM wabaki wenyewe.

Kitendo cha CCM kumuomba Mbowe wabaki ilikuwa ni dalili ya kutafuta mahala pa kutokea.
Kwamba mazimio ni ya bunge na wala si ya CCM.


Inaendelea …..
 
Inaendelea...


WABUNGE
Mbowe alipaswa kujiuliza, Makinda anawataka wajadiliane kitu gani zaidi ya taarifa ya PAC

CCM walijua kuondoka kwa wapinzani kungekuwa na ugumu wa kuandika mapendekezo ya bunge kwa wabunge wao. Wasingalikuwa tayari kukanga watu wao.

Ni lini CCM wamekaa na kujadiliana na wapinzani?
Mbowe alitakiwa kujua ulaghai uliowahi kufanyika huko nyuma si kwa timu ya CCM bali mwenyekiti wao.

Wamejadiliana na mwenyekiti wa CCM kusitisha BMLK, kinyume chake amewageuka. Dharau, matusi na kujeli kwa wapinzani ikawa ndiyo majadiliano yenyewe.

Hilo Mbowe na viongozi wa UKAWA hawajajifunza hata siku moja.
Wamekuwa wahanga wa udanganyifu. Mbowe na viongozi wenzake wakiwemo ‘wapiganaji' walifanya makosa kuendelea kujadiliana na wezi.

MARIDHIANO
Ikaundwa kamati ya maridhiano wakiwemo akina Mbowe na Zitto kwa upande mmoja, upande mwingine ukiongozwa na akina Chenge.

Hivi Chenge anawezaje kutoa hukumu kwa jambo linalomhusu?

Kibaya zaidi, lini kumekuwepo na mjadiliano kati ya wezi na walioibiwa?

Kazi ya bunge ni kusimamia serikali itekeleze majukumu yake na wala si maridhiano. Tunarudi nyuma na kujiuliza, lini CCM wamekubali maridhiano katika masuala ya kitaifa. Ni kwanini hili la Escrow wamekuwa mstari wa mbele kwenye maridhiano!

Kamati ya PAC, Mbowe, Zitto na wapinzani, walitenda kosa kuundwa kamati ya maridhiano. Kwa maneno mengine walikubali kukaa meza moja na wezi ili kujadiliana namna ya kumaliza tatizo.

Ndivyo ilivyokuwa kwa EPA,kamati ya maridhiano iliyoundwa haijatoa matokeo. Tunakumbuka kamati ya mwanasheria mkuu, IGP na katibu kiongozi.

Ni wapi duniani wahalifu wanapewa fursa ya kuridhiana na waliohalifiwa!!!

WALICHOPASWA KUFANYA

CCM ilishindwakuwashinikiza watu wake wawajibike ili kuvuja siri na orodha ya waliopata mgao .Mwanasheria mkuu, waziri, naibu waziri na wengine wakadinda, CCM haina la kuwafanya

Wenyeviti wa kamati za bunge ni wajumbe wa NEC na CC ya CCM.
Nani anaweza kusimama na kwenda kinyume na matakwa yao.

Wapinzania hawakupaswa kuhangaika na kikundi kidogo eti kiwajibishwe.
Hoja kubwa ilikuwa ;
Kutafuta chanzo cha mfumo mzima uliosababisha yote kutokea

Pili, kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu ili kulazimisha serikali kuvunjwa

Hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu ilikuwa kudanganya umma na bunge pesa si za umma. Pili, mawaziri wa serikali walisimama bungeni wakitetea kuficha ukweli.
Na tatu, hoja ya PAC kuwa waziri mkuu alikuwa na taarifa kuhusu uhalifu.

Waziri mkuu yupo katika mamlaka yao, na kura ya kutokuwa na imani ingelazimisha serikali kuanguka kwa namna yoyote. Hata kama ingeshindwa, kulikuwa na sababu za Rais kuwaondoa wahusika kwa vile bunge halina imani na serikali

Hoja ya PAC kuhusu Maswi, Mhongo, Masele, Werema kujiuzulu haikuwa na mantiki hata kidogo. PAC walijenga hoja kwa sababu zao. Hoja kubwa ilikuwa serikali nzima kuwajibika. Aliyetakiwa kubeba mzigo ni kiongozi wa serikali bungeni ambaye bunge linaweza kutokuwa na imani naye.

Lakini pia PAC ilitakiwa iangalie mfumomzima uliohusika katika uhalifu.

Hapa ndipo tunajiuliza kama kamati ya PAC iliangalia suala zima kwa mtazamo mpana au kwa jicho la watu wane.

N apengine hilo linaeleza kushindwa kwa hoja na kushindwa kwa wananchi.
Ni kushindwa kwasababu hakuna matokeo yoyote ya maana yaliyopatikana.

Ni mwendelezo way ale ya Buzwagi, ambapo Zitto alikuwa mwanakamati wa tume ya Bomani. Hadi leo taarifa po makabatini! Yale ya tume ya rais ya EPA, hadi leo hakuna jibu. Yale ya Pesa za uswiss hadi leo ni kitendawili, n.k.

Je hoja ya Escrow imeleta lolote la maana kwa wananchi? Je, haiwezi kuwa na siasa ndani yake katika kutafuta umaarufu kwa wabunge ‘wapiganaji''

Inaendelea……
 
MAAZIMIOYA BUNGE
Kutokana na hali ya kutotambua mazingira yaliyojengwa na CCM napengine kuogopa serikali kuanguka kama alivyowahi kusema Zitto, maazimio waliyoyapendekeza yana udhaifu mkubwa

1Hakukuwana jitohada za kumwajisha waziri mkuu kwa kura ya kutokuwa na Imani, serikali kuvunjwa na kuondolewa wahusika wengine
2Taarifaya PAC imegusa watu si mfumo, na kuacha mwanya kwa watuhumiwa wengine. Taarifa imejikita kwa watu 4 badala ya taasisi n.k
3.Kukubali kile walichonyimwa siku za nyuma ‘maridhiano'' na kushindwa kutumia nafasi iliyopatikana kuweka misingi imara ya uwajibikaji.

MAAZIMIONA UDHAIFU WAKE

1HarbinderSing wa PAP na wengine wachukuliwe hatua baada ya uchunguzi kukamilika
Hoja zetu: Sheileshi Vithilan aliondoka nchini hadi leo hajapatikana.
Walioiba pesa na uziweka Uswiss hakuna aiyechukuliwa hatua.
Watu waliohusika naEscrow hakuna ushahidi wa kuwashtaki.



Uchunguzi utafanywa na Polisi ambacho ni chombo cha serikali ile ileiliyokataa Escrow kujadiliwa
kwahoja za kilaghai na njia kama za barua ya mahakama


2. Serikaiichukue mitambo ya IPTL
Hoja:Kwani tatizo ni mashine au ni watu wanaotumia mashine hizo kuiba?
Mitambo yaumeme haina tatizo, tendo la kuitafisha ni kutisha wawekezaji.
Uzembe waserikali si tatizo la wawekezaji bali mfumo unaoruhusu uhalifu.

3.Bungelinaazimia kupitia mikataba ya umeme
Hoja:Zitto alikuwa jumbe wa tume iliyoshughulikia mikataba ya madini. Hadi leomadini na mikataba ni kitendawili.
Ni kipi serikali inaweza kufanya tofauti namikataba mingine au sekta nyingine zenye matatizo kama ya nishati?

Mikataba sitatizo, tatizo ni watu wanaotumia nafasi zao kujifaidisha kwa mikataba. Mkataba wa IPTL ulitiwa sahihi na viongozi waliopo na wakati huo JK alikuwa waziri wanishati. Ni kipi kipya tuitegemee ikiwa waliyoingia mikataba hiyo hawaelewi tatizo hadi leo.

4.Kuanzishwataasisi mahususi ya kushghulikia rushwa kubwa
Hoja zetu:Kuna Polisi,Usalama wa taifa na Takukuru. Vyombo hivyo vimeshindwa kuzuia madudu ya sasa.
Hiyo taasisi nyingine itakuja na kitu gani tofauti Zaidi yahivi vilivyopo?
Hapa ni kuunda takukuru nyingine badala ya ukomesha mfumo wawizi.
Kwamba suluhu ni kukimbia wizi kwa kujficha katika Takukuru namba 2. Niupuuzi tu

5.
Raisaunde tume kujadili majaji waliokiuka maadili
Hoja zetu:Kuna ushahidi gani wa kutosha kuhusu majaji husika?
Mahakama imetumika katikasakata zima, kuna uhakika gani itatekeleza majukumu iliyopewa na bunge ikiwa yenyewe ni sehemu ya ‘dili'

6.
Mawazirina katibu mkuu pamoja na wajumbe wa bodi ya Tanesco wawajibishwe kwa utenguziwa nyadhifa
Hoja zetu:Tatizo si watu ni mfumo. Hao wanaotajwa wakiwajibishwa ni kitu gani kitatokea.
Je, watashtakiwa au kufilisiwa? Je, mtandao mzima una husu watu hao wane?
kule Stanbic nani anajua majina yao. Hizi ni solution za knee jerk, hazitafutiufumbuzi na chanzo cha tatizo

7.
Chenge,Ngeleja na Mwambalaswa kuvuliwa nyadhifa katika kamati zao
Hoja zetu: Kuwavua nyadhifa hakujaondoa tatizo. Bado watakuwa wajumbe wa kamati husika.
Kama bunge haliwezi kuchukua hatua kali dhidi ya wabunge, wapi linapata nguvu za kuisimamia serikali?
Kwani hao watatu ndio tatizo pekee! Vipi wale waliochukuarushwa ili kutetea hao watatu, nao wanachukuliwa hatua gani
?

Inaendelea.....








 
Inaendelea....

Sehemu ya VI
TUNAJIFUNZA NINI KUTOKANA NA MAMBO KAMAHAYA!

Watanzaniani watu wagumu kujifunza.
Mfumo nimbovu wala si watu wane. Wizi wa kiwango unajirudia, hatuna majibu.

Escrow nikushindwa kwa wananchi, wanasiasa wakitumia kujipatia umaarufu.
Tuhuma zawizi zipo, wizi umefanyika na wahusika wamejulikana baadhi yao.

Walioibuahoja hawakuwa na mkakati, na waliozungumzia hawakujua mbinu.

Kwanza,ilitakiwa tume huru ya bunge ifanye uchunguzi
Pili,taarifa za CAG na PCCB zifikishwe bungeni(sharia hairuhusu hivyo kwa PCCB)
Tatu, bungelitumie rungu la kumwajibisha mkuu wa shughuli za serikali bungeni PM
Nne, bungelichunguze ofisi kuu ya nchi (Ikulu) ima kwa kuzembea au kuhusika
Tano, mfumowote uliohusika uwekwe hadharani,na mbele ya sharia

PAChaikwenda mbali katika taarifa, ikiacha mfumo mzima na kushambulia watuwachache. Hao wachache ni sehemu ya ''syndicate'' kubwa sana.

Kwa mfano,PAC haikusema waziri mkuu alijua kwa kiasi gani na kama alimjulisha mkuu wa nchi.Hili linabaki kuwa open question

Taarifa yaPAC imeacha swali . Katika maazimio, inasemwa STANBIC ielezwe kama Bankinayotakatisha pesa haramu.

Hatujuimajina ya waliotakatisha pesa hizo, leo inawezakanaje Bank hiyo ikaitwa yakutakatisha?

Kuna Bank yaMkombozi ambayo wengi wa mgao wa Ruge wampitishia pesa zao huko. Haielewekitofauti ya Mkombozi na Stanbic katika timbwili hili ni ipi.

Tena Mkomboziwameonyesha orodha, Stanbic tusiojua orodh, inawezaje kutakatisha pesa?

Taarifa yaPAC imeacha wananchi wakiwa na hasara bila majibu.

Kilichopatakinani umaarufu wa wanasiasa bila matokeo chanya.


WANANCHI
Mfumo mbayaunagusa sehemu zote. Wananchi wamekaa pembeni wakisubiri wanasiasa wazungumzekuhusu masilahi yao.

Wizi kama waEscrow ulipaswa kuwa na shinikizo la wananchi, ili ukweli ujulikane, wahusikawatajwe na wafikishwe katika sharia

Wananchiwanategemea katiba ya mwaka 1977 iliyolundika madaraka kwa Rais, inaweza kujana matokeo tofauti na yake ya siku za nyuma.

Ni ukweli katibaya 1977 inafunga mikono wananchi unless kama wataamua kutumia maguvu. Katiba inalinyima bunge uwezo, inaleta migongano yamihimili na inaipa nguvu serikali juu ya mihimili mingine miwili.

Kwa kutambua‘uzuri'' wa katiba ya 1977, Ikulu na Serikali vimejitahidi suala hili lirudiserikalini. Maana kubwa umiliki wa vyombo vyote,hivyo kuweza kudhibiti aukubabaisha

Na kwakutojua, wabunge wamekubali hilo. Sasa ni suala la Rais kuamua kama anachukuahatua au la.

Hakunasehemu inayomlazimisha kufuata maagizo ya bunge.
Ndivyoalivyowahi kufanya huko nyuma.

Hataakifuata maagizo bado ana uwezo wa kutoa ‘msamaha ' kwa wahusika. Kuwaondoaukatibu mkuu au uwaziri si adhabu ni nafuu .


Hiyo piainatoa nafasi kwa mfumo wa wizi kuendelea.
Si raisatakuwa amefanyia kazi yale ya bunge? Sasa kuna sababu gani za kuchukua hatuaza kisheria tena. Imetokea huko nyuma.


 
Inaendelea

Shemu ya VII
KATIBA MPYA

Ukisoma rasimu ya Warioba, mambo yote yalitafutiwa dawa.
Kwanza, kumuondolea Rais madaraka makubwa yanayompa haki ya kuyatumia vibaya''abuse''

Pili, kuunda taasisi na mamlaka huru yatakayotoa majibu ya matatizo bila kusubiri uamuzi wa mtu mmoja.

Tatu, rasimu iliweka maadili ya viongozi na miiko yake.
Ikaondoa mamlaka na kuyaweka katika taasisi nyingine.
Mfano,ni kuthibitishwa kwa mwanasheria mkuu na bunge, wakuu wa vyombo kama PCCB,DPP kutowajibika kwa rais n.k.

Nne, njia za kuwajibisha viongozi wenye dhamana zilirahishwa na hivyo kila mmoja angejua amekalia kuti kavu

Tano, wananchi kuwawajibisha wabunge kama wale wa CCM waliochangia kwa aibu na fedheha kubwa kwa CCM, majimbo yao na nchi kwa ujumla

Ukisoma rasimu ya Warioba, matatizo kama ya Escrow yalishatafutiwa majibu

RASIMU YA CCM (CHENGE NA SITTA)
Kwa kutambua kuwa kuna mikataba kama ya IPTL yenye miaka 20, haikuwa jambo jema kuwa na katiba kama ya Warioba.

Pesa zikatumika kuhakikisha inaandikwa katiba itakayofanana na ya mwaka 1977 ambayo mafisadi watakuwa na uwezo wa kumchagua kiongozi na kumwelekeza nini afanye.

Ndivyo walivyofanikiwa hadi sasa kwani viongozi wa CCM wameufaya, tunawaskia wakiongelea pembeni kama wasemaji wa serikali.

Katiba yote ya Chenge/Sitta ni photocopy ya ile ya mwaka 1977 kwa makusudi tu ya kuhakikisha inalinda masilahi ya watu wachache na si ya umma.

Huo ndio msingi mkubwa wa kutumia nguvu, ulaghai, rushwa kuipiga vita rasimu ya Warioba.

Wabunge wa BMKL wa CCM hawakujua pesa zinazowanunua ndio hizi ‘Escrow''.
Fikiria, watu wawili wamepata3.2 Bilioni.

Kiasi hicho kinaweza kuhonga wabunge wenye njaa kwa milioni 10 katika idadi ya wabunge 160.

WABUNGE WA CCMHAWAJUI MADHARA

Wabunge wa CCMwa BMK waliohongwa, hawakujua katiba ni mwongozo unaogusa maisha yao. Leo tumeona Dodoma jinsi mihimili mitatu inavyosigishana kutokana na katiba ya 1977. Tumeshuhudia mhimili mmoja ukijaribu kununua mhimili mwingine.

Wabunge wa CCM hawakujua tatizo wanalonunua, na hili limejitokeza hata kabla ya katiba ya CCM haijajadiliwa.

Hii maana yake ni kuwa katiba ya Chenge ambayo ameiandika inatengeneza matatizo makubwa kuliko tunavyodhani.

Katika kiwango cha rushwa tulichoona Mkombozi na kile tusichokijua huko Stanbic, na ambacho kimehusu CCM ,hivi kweli wananchi wanaamini mawaziri , makada wa CCM na serikali yao waliochotewa mabilioni wanaweza kuandika katiba yenye masilahi kwa wananchi na si masilahi yao?

Ukiangalia kamati za bunge la katiba la CCM, wamo akina Werema, Tibaijuka, Muhongo, Chenge, Ngeleja, Mwambalaswa n.k.

Hivi kweli hawa wanaweza kuandika katiba ikakinzana na tunayoyajua sasa hivi kuhusu matumbo yao?

HONGO ZA KATIBA
Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu amekiri waraka wa kununua waandishi wa habari na wasomi ili katiba mpya ya CCM ipite.

Wananchi lazima wajiulize. Endapo katiba ni nyaraka ya umma ni kwanini zitolewe bilioni 2.5 kwa ajili ya kuhonga waandishi na wasomi ili kuitetea?

Wapi pesa hizo zinapatikana katika bajeti ya mwaka 2013/2014?

Je haiwezekani ni hizi zilizozagaa sasa zinatumika kununua haki za wananchi?
Ikiwa watu wawili wamepata bilioni 3.6 ni kipi kinashindikana kupata bilioni 2.5 za kuhonga?

Ukiangalia mgao wa escrow, ni kipi inashindikana hata kununua bunge zima la CCM ili kuhakikisha masilahi ya kundi dogo yanalindwa?

Kulindwa masilahi ni kuhakikisha kuna udhibiti wa system kama ilivyo sasa ili mikataba kama ya IPTL yenye miaka 20 iendelee kuwepo.

Watakuwepo na watarithisha watoto wao mikataba na mafao yatokanayo.

Njia rahisi ni kuhakikisha ile katiba ya wananchi kupitia tume ya Warioba inapigwa chini.
Katiba ya 1977 inayotoa fursa za wizi ipakwe rangi na kuwa katiba mpya ya CCM.
Ndio maana wahusika walioandika katiba ya CCM ndio wale wale walioko katika orodha ya mgao.

Hoja ni kuhakikisha masilahi ya kundi yanalindwa yale ya wananchi yanatupwa.

HITIMISHO

Homa si ugonjwa bali dalili ya ugonjwa. Ili kuonda homa ni lazima kutibu ugonjwa. Escrow na watuhumiwa 4 ni sawa na homa.

Ni dalili ya ugonjwa wa mfumo mbaya.
Haiwezekani kuondoa watu 4 kukatoa jibu. Jibu linapatikana kwa kurekebisha mfumo.

Mfumo ungerekebishwa kwa katiba ya wananchi. Hii inayoandaliwa ni ya kundi la watu.
Ukiwaona wanapiga debe katika TV na Radio, hao ndio wale waliopewa mgao wa kurugenzi ya mawasiliano Ikulu.

Hawana cha kupoteza, ni sehemu ya mgao wa escrow kwa njia ya uani ili kulinda mfumo unaonufaisha wachache kwa gharama ya wengi.

Hakuna namna jinamizi hili litaondoka kama tutabaki na katiba ya 1977 iliyopakwa rangi na Sitta/Chenge kwa jina la katiba mpya

Ni wakati sasa wananchi wachukue hatua
Kwanza waache kuzngumzia katiba ya CCM kwasababu si yao ni ya kundi la watu wachache kama orodha ilivyoonyesha

Wanakila sababu ya kudai rasimu ya Warioba irudi na ijadiliwe na makundi ya jamii si CCM. Chama cha Mapinduzi kimeshindwa kuwachukuliwa hatua watu 4, haiwezekani kikawa na uhalali wa kuandika nyaraka ya watu milioni 45.


Kutojadili hata kura ya maoni, bali wadai katiba ya wananchi na si ya CCM

Mwenyezi mungu anawapenda sana Watanzania. Hizi dalili za migongano ya mihimili,

wizi, na kushindwa kupata majibu ni ujumbe mzuri kuwa kuna tatizo kubwa nchini.

Ukubwa wa tatizo hilo hautapatiwa ufumbuzi kwa kufanya yale ya katiba ya 1977 inayopakwa rangi sasa.
Majibu ni kukataa kwa nguvu zote katiba ya CCM na kudai katiba ya wananchi kupitia rasimu ya Warioba.

Kinyume chake wananchi wajiandae kwa maumivu kila uchao kwa miaka mingine 50 au 100.

Wananchi wana hiari ya kushtuka na kuchukua hatua au kuendelea kupiga debe katiba iliyotokana na hongo na kukabiliana na maumivu huku wenye CCM wakipeta kwa raha zao.

Tusemezane
 
katika ishu ya KATIBA kiukweli kutoka moyoni sikupenda wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano na baraza la wawakilishi wae WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA,sikatai wanasiasa kushirikili ila wangekuwepo kupitia vyama vyao,alafu kisheria ikoje wabunge waliapa kuilinda katiba(1977),alafu nashangaa nao wamekua sehemu ya kuibomoa
ALAMSIKI
 
ESCROW: SERIKALI YA PUMUA
PAC WATWANGA MAJI KWENYE KINU

MBOWE, KURUDIA MAKOSA SI SIFA YA UONGOZI
ZITTO: KUACHA VIPORO SI UTAMADUNI MZURI

Mabandikoyaliyopita tulisema wazi, serikali haikupenda Escrow ijadiliwe bungeni.
Njia zakutumia barua za mahakama, hoja za kuingilia mihimili na'ugumu' wakuwawajibisha wahusika ni janja tu ya kulirudisha suala hilo serikakini.

Mantiki nirahisi , rudisha suala serikalini waliko na uwezo wa kutumia vyombo husikakuficha uvundo na kulinda wahalifu.

Katibu mkuukiongozi ametoa kauli, suala la escrow linafikiriwa na Rais na uchunguzi wakina unahitajika kabla ya hatua.
Kauli hiyoni dharau kwa Bunge, kwamba halikuwa na taarifa za kina.

Hata kamabunge halikuwa na taarifa za kina, maswali yanabaki, serikali inafanyauchunguzi kwa kutumia vyombo gani nje ya PCCB na CAG?

Polisiimebaki kuwa chombo cha kukamata wezi wa kuku, wagoni n.k. na si kushughulikiamambo mazito kama Escrow.Sijui ni chombo gani kingine kitakachotumika

Uchunguzi utafanyikavipi ikiwa wahusika bado wapo madarakani?
Nani anawezakumsogelea wateule wa Rais katika taifa hili?

Nani anawezakuisogelea account ya Stanbic inayohusisha mapapa tusiowajua?
Nani anawezakumchunguza katibu wa Rais aliyeandika barua kushinikiza malipo?

Kinachoendeleani usanii tu kama ilibyowahi kutokea.
Muda si mrefu tutasikia Rais kavunja baraza lamawaziri, kaondoa ABCD kaweka EFG.

Escrow itakuwaimefikiamwisho na matanga.
Ndivyotulivyoruhusu kuchezewa akili zetu kama watoto wadogo.

MBOWE NAZITTO
Ni wabungewasiojifunza. Tendo la kukubali kuwa sehemu ya maazimio mfu ya bunge lilikuwabaya.

Mbowealiwazuia wapinzani wasitoke. Hiyo ilikuwa karata muhimu sana kwasababu leo CCMingekuwa imetoa majibu yao. Hata kama ni majibu yao, bado dunia isingekubaliananao.

Kinyumechake, linatumika kwa ujumla kwamaazimio yasiyo na maana.
Hayana maanakwasababu maoni ya wabunge yanasubiri fadhila za mtu mmoja.
Na tunajuaujanja ujanja tu unaotumika.

Zitto na PACnao pia wabebe lawama. Kitendo cha kutotoa taarifa kamili na kuficha wahusika Zaidihaikukuwa sahihi.

Inavyoonekanaakina Zitto walikuwa against kundi fulani na si mfumo uliosababisha hasara.Kisiasa wanaweza kutumia kukwea ngazi, kimatiki hasa kwa wenye fikra,walichokifanya ni failure kubwa.

Huwezikusimamia uzalendo nusu nusu.
Leowanaongolea suala la Sukari kana kwamba ile hoja ya Escrow ina majibu.

Tuliwahikuonya kuwa baadhi ya wanasiasa kwa uadilifu na si sifa zao, si watu wakutiliwa maanani.

Mtuanaposimamia jambo likaishia njiani na kisha kupewa ‘nishani' ya ushujaa, hilolinatia shaka. Je, si kweli kuwa escrow ilitumika kama political stunt?

Kama jibusiyo, basi tuelezwe mwisho wa escrow ni upi?
Na unatafoautigani nay ale ya pesa za Uswiss, Buzwagi, Richmond,meremeta n.k.

Tusemezane



 
YAMETIMIA, NYANI APEWA KAZI YA KUMCHUNGUZA TUMBILI

JK AJIBU KAZI YA KAMATI YA BUNGE.

TIBAIJUKA MBUZI WA KAFARA, WENGINE WAPATA SITRI YA MH RAIS

RAIS ADAI 'HANA MAMLAKA YA MAASKOFU AU MASHEIKH WALA RUSHWA'' HILO SI JUKUMU LAKE

Kwa wanajmavi mtakumbuka jinsi tulivyoliongelea suala la Escrow katika uzi huu.
Moja ya madhaifu yake ilikuwa kutoa nafasi kwa serikali kupumua(bandiko 52)
Makosa yalifanywa na akina Zitto na Mbowe kwa kukubali 'maridhiano'' ambayo leo Rais ameyatumia kama ksingizio.

Rais amesema, suala la Escrow ni la kitaifa na angeshangaa kama kuna ambao wangelipinga.
Hatujui kama mh Rais anakumbu kumbu makamu wa Rais na wabunge CCM waliweka vikao vya kujinasua katika timbwili kama chama.

Rais anasema, wapo waliotafuta sifa kiurahisi. Inashangaza kusikia katika hotuba hiyo hiyo akilisifu bunge kwa kazi nzuri.
Sasa kama kuna kazi nzuir imefanyika, suala la sifa linatoka wapi?

Hapa aliwalenga akina Zitto, Kafulila, Filikunjombe na wabunge wengine.
Ni mfano mzuri na ujumbe kwa mh Zitto kuwa JK hubadilika kila uchao.
Ule uswahiba umeisha, hata hivyo unaweza kurudi kutegemeana na mazingira.

Rais anasema yapo masuala yanayoshughulikiwa na kitengo cha intelejensia.
Hivi kweli Intelejensia iliyoshindwa kujua wizi wa miaka zaidi ya 7, inawezaje kufanya uchunguzi mafasili yakiwa yamefichwa na wahusika wamejiuzulu?

Rais kasema, ameonge ana Anna Tibaijuka na kumuuliza ilikuwaje pesa ziingie katika account yake na si shule.
Mama Tiabaijuka kasema hilo lilikuwa ni sharti la mtoaji.

Kuna eneo ambalo Tibaijuka alipaswa kuiona kabla ya kukubali.
Katika mazingira ya kawaida kulikuwa na conflict of interest na hasa baada ya shinikizo la account yake.

Mama Tibaijuka aelewe kuwa pesa zingetolewa na shirika la SIDA au Jica kwa sharti la kuingia katika account yake, hilo jambo lisingekuwa sahihi na anafahamu hivyo.

Hata hivyo, katika hali ya kushangaza, Rais kamfukuza kazi mama Tibaijuka hadharani.

Rais hakueleza, je ilikuwaje wajumbe wa kamati kuu, na wengine wenyeviti wa kamati za bunge wapewe mgao huo bila kuwa na conflcit of interest. Je, Rais hakuona tatizo hapo? Na wale waliohusika mbona hakuzungumza wamechukuliwa hatua gani

Lakini pia anasema, uchunguzi kuhusu waziri Muhongo unaendelea.
Kama aliweza kumwita Tibaijuka na kupata ukweli papo kwa papo, Rais alishindwa nini kutumia vyombo vyake vya Intelejensia kupata jibu la Muhongo ndani ya wiki mbili?

Kinachoonekana hapa ni kutafuta njia za kumnusuru Mhongo.

Ukisoma hotuba yake, ni kama Rais anasema suala la Escrow halikuwa na tatizo.
Halafu anasema ni bahati mbaya kuna pesa ziliposwa kuchukuliwa na serikali haikufanya hivyo.

Hapo hapo anadai suala hili limezungumzwa vema bungeni ni jambo jema.
Ukimsikiliza, ilikuwa ni mchanganyiko tu na wala hakukuwa na jibu la tatizo.

Kibaya zaidi ni pale anaposema yeye hana mamlaka na mashiekh au maaskofu waliopata mgao.
Ni kweli, lakini kama kiongozi wa nchi suala la maadili halichagui. Ataongoza vita ya rushwa kama anachagua makundi?

Kitendo cha kuwaacha viongozi wa dini kwa ksiingizio cha kutokuwa na mamlaka nao ni kukwepa wajibu wake.

Hakupaswa kuwachukuliwa hatua, lakini uchunguzi ulipaswa ufanywe ili kuona kama kuna uhalifu

Hapa ni sawa na kusema, wizi ukifanywa kupitia viongozi hao, yeye kama Rais hana wajibu wowote hata kama ni mali za taifa hili. Rais anafungua milango ya dini kutumika katika madili.

Jambo la hatari zaidi ni pale anapoingiza makundi mengine yasiyohusika. Hakuna mahali tumeona Sheikh akitajwa.
Hili lilikuwa suala la maaskofu waliotajwa na wachungaji. Rais hawezi kufanya balance kwa ksuingizia watu.

Rais anaogopa kusema ukweli, anatumia majumuisho. Huu ndio udhaifu wa kiongozi wetu.
Hakukuwa na sababu za kupendeza watu, alitakiwa asimame kwenye ukweli. Hakusima, alipiga dana dana tu

Na Rais anakwepa wajibu wake pale anaposema suala la majaji anamwachia jaji mkuu.

Well, ni wiki mbili zimepita, leo wananachi walitaraji alete majibu na si kutupiana mpira na viongozi wengine

Mkuatano wake ulikuwa kuonyesha anavyofanya kazi na si majibu ya tatizo la taifa.

Tutaendelea kuingalia hotuba yake ziaidi
 
Mkuu Nguruvi nitarejea baadae kuchangia zaidi, ila nimepigwa na butwaa mkuu wetu kaweza vipi kumfukuza direct Tibaijuka huku akisema anaendelea kuchunguzwa, na ajabu sana eti anamuacha Muhongo kiporo why??? Kwa nn kwa Tiba kafanikiwa kwa Muhongo kigugumizi,

Kama umefuatilia hivi karibuni vyombo vya habari hasa TBC, Habari Leo na uhuru walikua kama na mass Compaign ya kumsafisha Muhongo na pia kuonyesha kalifanyia makubwa taifa hili, sasa hapo ukiunganisha na yaliyotokea leo kwa uamuzi wake u can connect dots and get some ans.
 
MUHONGO AWEKWA ''KIPORO''

KAGASHEKI ALIONDOLEWA FASTA BILA KUWEKWA KIPORO
TIBAIJUKA ATOLEWA KAFARA ILI MAJAMBAZI YASALIMIKE
Mkuu Nguruvi nitarejea baadae kuchangia zaidi, ila nimepigwa na butwaa mkuu wetu kaweza vipi kumfukuza direct Tibaijuka huku akisema anaendelea kuchunguzwa, na ajabu sana eti anamuacha Muhongo kiporo why??? Kwa nn kwa Tiba kafanikiwa kwa Muhongo kigugumizi,

Kama umefuatilia hivi karibuni vyombo vya habari hasa TBC, Habari Leo na uhuru walikua kama na mass Compaign ya kumsafisha Muhongo na pia kuonyesha kalifanyia makubwa taifa hili, sasa hapo ukiunganisha na yaliyotokea leo kwa uamuzi wake u can connect dots and get some ans.
Mkuu hili ;a vyombo vya habari tumeliongelea juzi katika uzi mwingine

http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/33411-mzozo-escrow-kumalizwa-j3

Kwamba, Muhongo anasambaza umeme anafanya kazi nzuri n.k.
Ni kampeni ya kumlinda na JK sasa kavaa koti rasmi la kumlinda.

Kinachoshangaza ni pale Rais wa nchi anapokimbia majukumu yake.
1. Yeye ndiye mteuzi wa makatibu wakuu. Tunakumbuka suala la Jairo ni yeye alizuia na kumwachia astaafu.
Leo Rais anamwachia katibu mkuu kiongozi jukumu lake, ili tu asionekane mbaya.
Ina maana Rais hakujua katibu mkuu amechukua hatua gani kwa wiki 2.

Tangu aliporejea aliyempa habari za nchi ni katibu mkuu.
Ina maana katibu mkuu kiongozi hajui majukumu yake kiasi cha kusubiri Rais amwelekeze mambo yaliyopo katika mamlaka yake.
Lini na katiba ipi inampa uwezo katibu mkuu kama anavyodai Rais

Katika kukimbia majukumu, anasema suala la majaji anamwachia Jaji mkuu.
Hivi kweli jamani wiki 2 ina maana hajaonana na Jaji mkuu.
Na inachukua muda gani kufanya uchunguzi ikiwa taarifa za CAG na PCCB zipo wazi.

2. Rais anasema Muhongo yupo Kiporo. Masikini Kagasheki hakuwekwa kiporo.
Ni kipi cha maana cha Muhongo anachotilia shaka ikiwa alisimama na kusema pesa si za umma.
Ina maana taarifa ya CAG ni uongo!

Waliofanya makosa ni Zitto na Mbowe.
Kitendo cha kukubali maridhiano ndicho kimerudisha suala hili kwa JK.
Tulisema huo ndio mwisho wa Escrow, na imetokea
Akina Zitto na Mbowe walitakiwa kufanya mambo 2
a) Kushinikiza kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Hapa JK angevunja baraza
b) Kususia bunge ili maridhiano yafanywa kati ya JK na CCM. Leo angeudanganya umma kwa njia zipi.

3. Mimi sikubaliani na wanaoshangilia Tibaijuka kuondoka.
Kwanza JK kamdhalilisha kwasababu hakufanya hivyo kwa wote.

Kamchukua mtu mmoja tena asiye na uhusiano wa moja kwa moja na kashfa, kamtoa kafara ili apate pa kusema.
Wezi wenyewe wameachwa wastaafu tena akiwapongeza akina Werema.


Lakini tujiulize huyu Rais ana kila chombo cha uchunguzi na dola. Hivi anahitaji miaka mingapi kuja na majibu.
Ina maana wiki 2 zilizopita alikuwa hana habari za nini kinaendelea.

Watanzania lazima waone tatizo.
Tibaijuka si tatizo, tatizo ni CCM na Rais iliyoamua kuigeza nchi kama eneo la uhalifu.

Wananchi lazima waone kwa macho yao. Mungu anawaletea kila aina ya ishara, Watanzania hawaamki.

Yaani hotuba nzima, Rais anakwepa majukumu yake na wala haonyeshi kukasirishwa na rushwa.
 
HABARI YA MJINI NI MAMA ANNA TIBAIJUKA KAMA NDIYE ESCROW

Hotuba ya Rais aliyosema amemuomba mama Tibaijuka ampe nafasi ya kuteua mwingine imegeuza mweleko wa habari.

Kwa tafsiri iliyopo, mama Tibaijuka amewajibishwa kuhusiana na suala la Escrow.
Ingawa Rais alisema wamemuuliza kwanini pesa ziingie katika account yake na si ya shule, bado Rais amemfanya Tibaijuka kuwa gumzo la Escrow badala ya Escrow

Ukweli ni kuwa mama Anna Tibaijuka alipokea pesa katika account yake.
Amekiri mwenyewe.

Kwa nafasi yake kama waziri na hadhi yake kama profesa, ilibidi aangalie mambo mengi kuhusiana na bilioni 1.6 alizopewa


  1. Kwanini mtoaji alimshinikiza pesa ziingie katika account yake na si ya shule
  2. Je, ailikuwa ni sahihi kupokea pesa nje ya mfumo wa uwazi?
  3. Je, kama waziri hakukuwepo ukinzani wa maadili ''conflict of interest''
  4. Kama kiongozi wa umma, maadili yalimruhusu kuchukua pesa hizo?
  5. Je, alijiridhisha uhalali na chanzo cha pesa kabla ya kuchukua hata kama zinatoka kwa mfanyabiashara?

Ukiangalia hayo hapo juu ni wazi mama Tibaijuka alipotoka.
Hivyo, tatizo la mama si kuchukua pesa za Escrow, tatizo ni maadili ya uongozi, hadhi yake katika jamii na nafasi yake kama kiongozi.

Kinachotokea kwa Anna Tibaijuka ni kitu kinaitwa poor judgement and violation of work ethics kwa maana maamuzi yasiyo na busara pamoja na kukiuka maadili ya kazi

Hayo hayaelezi kuwa Tibaijuka kuhusika na Escrow kwa nafasi yake, na wala hayakusemwa na taarifa yoyote tunayoijua.

Hivyo Anna Tibaijuka si mshiriki wa Escrow kwa wakati huu na tunavyojua, bali ni beneficiary wa Escrow iwe kihalali au kiharamu.

Tunachoshuhudia ni kitu cha kusikitisha sana.

Rais amemfanya makusudi mama Anna Tibaijuka kama Escrow.

Pengine alichokusidia ni kutaka kubadili mwelekeo wa habari nzima.
Tunaweza kusema amefanikiwa

Watanzania wamesahau kila jambo lililo na mashaka ambalo Rais hakulitolea ufafanuzi.

Sasa hivi hoja ni Tibaijuka kana kwamba yeye ndiye tatizo.

Watu wamesahau kuwa orodha ya waliofadika wengine ni wajumbe wa kamati kuu ya CCM na NEC.

Wengine ni wenyeviti wa kamati za bunge.

Hao wote Rais hakuwauliza kwanini nao walipokea mgao na kama hakukuwa na kukinzana kwa masilahi. Aliyemuona na kumwandama ni Tibaijukua.

Watanzania wamesahu kuwa waziri Kagasheki alijiuzulu tu kwa kuwa kulitokea makosa ndani ya operesheni.

Pamoja na hujuma zilizofanywa kwa Kagasheki na makatibu wakuu na wakurugenzi, bado Rais hakumpa nafasi ya kuchunguzwa kama akina Mhongo

Hapa kuna maswali mengi sana na haijulikani dhamira ya Rais kwa akina Anna Tibaijuka na Kagasheki kwanini iwe tofauti na genge lingine la wahalifu

Tunachosema ni kuwa Watanzania, hoja ya mama Anna ni ya kuwaondoa katika mada halisi Escrow.

Anna hahusiki kama mshiriki, vipi leo washiriki wanafichwa na kuhifadhiwa huku mkitutupiwa makapi nanyi kushangilia mkidhani ni keki keki?

Je, mna majibu ya escrow?
Mnajua nani alipata kutoka stanbic?
Mnajua majina yote ya waliopata mgao na mahusiano yao na watu wengine?
Manajua account za viongozi huko ughaibuni?
Mumeelewa nini kuhusu pesa za umma? Mumemuelewa Rais kwa kiwango gani?

Tusemezane
 



UKAWA WAZINDUKA ‘TOO LATE'
TULISEMA, HAWAJIFUNZI KUTOKANA NA MAKOSA

Katika mabandiko 53,54 na 55 tumeeleza makosa yaliyofanywa na Zitto na Mbowe kukubali iundwe kamati ya maridhiano kuhusu Escrow
Tulitahadarisha hata kabla ya mjadala kuwa nia ya serikali haikuwa njema katika kulishughulikia tatizo. Walichotaka ni kulirudisha serikali ili waweze kulipa ‘uhalali'' katika uhalifu kwa kutumia vyombo vyake

Katika gazeti la mwananchi, UKAWA wamesema endapo serikali haitatekeleza maelekezo ya bunge, itaombwa kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu au serikali.

Hili ndilo walipaswa kufanya mapema. Walijua jitihada za kulirudisha serikalini ni kuficha uovu. Walitakiwa kulisimamia ili serikali iwajibike bila kupitia mtu mmoja.
Sasa wanakumbuka shuka ikiwa ni alfajiri.

Tulisema haya
……
Waliofanya makosa ni Zitto na Mbowe.
Kitendo cha kukubali maridhiano ndicho kimerudisha suala hili kwa JK.
Tulisema huo ndio mwisho wa Escrow, na imetokea
Akina Zitto na Mbowe walitakiwa kufanya mambo 2
a) Kushinikiza kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Hapa JK angevunjabaraza
b) Kususia bunge ili maridhiano yafanywa kati ya JK na CCM. Leo angeudanganyaumma kwa njia zipi.
ESCROW: SERIKALI YA PUMUA
PAC WATWANGA MAJI KWENYE KINU

MBOWE, KURUDIA MAKOSA SI SIFA YA UONGOZI
ZITTO: KUACHA VIPORO SI UTAMADUNI MZURI

Mabandikoyaliyopita tulisema wazi, serikalihaikupenda Escrow ijadiliwe bungeni.
Njia zakutumia barua za mahakama, hoja zakuingilia mihimili na'ugumu' wakuwawajibisha wahusika ni janja tu ya kulirudishasuala hilo serikakini.

Mantiki nirahisi , rudisha suala serikaliniwaliko na uwezo wa kutumia vyombo husikakuficha uvundo na kulinda wahalifu.

Katibu mkuukiongozi ametoa kauli, suala laescrow linafikiriwa na Rais na uchunguzi wakina unahitajika kabla ya hatua.
Kauli hiyoni dharau kwa Bunge, kwamba halikuwana taarifa za kina.

Hata kama bunge halikuwa na taarifa za kina,maswali yanabaki, serikali inafanya uchunguzi kwa kutumia vyombo gani nje yaPCCB na CAG?


Uchunguzi utafanyikavipi ikiwa wahusika badowapo madarakani?
Nani anawezakumsogelea wateule wa Rais katikataifa hili?

Nani anaweza kuisogelea account ya Stanbicinayohusisha mapapa tusiowajua?

Kinachoendeleani usanii tu kama ilivyowahikutokea.
Muda si mrefu tutasikia Rais kavunja barazalamawaziri, kaondoa ABCD kaweka EFG.

Escrow itakuwaimefikiamwisho na matanga.
Ndivyotulivyoruhusu kuchezewa akili zetu kamawatoto wadogo.

MBOWE NAZITTO
Ni wabunge wasiojifunza. Tendo la kukubali kuwasehemu ya maazimio mfu ya bunge lilikuwabaya.

Mbowealiwazuia wapinzani wasitoke. Hiyo ilikuwakarata muhimu sana kwasababu leo CCMingekuwa imetoa majibu yao. Hata kama nimajibu yao, bado dunia isingekubaliananao.

Kinyumechake, linatumika kwa ujumla kwamaazimioyasiyo na maana.
Hayana maanakwasababu maoni ya wabungeyanasubiri fadhila za mtu mmoja.
Na tunajuaujanja ujanja tu unaotumika.
Kwa hisani ya gazeti la mwananchi

[url]http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Ukawa-walitaka-Bunge-kuiwajibisha-Serikali/-/1597296/2568176/-/plhtao/-/index.html
[/URL]

Dar es Salaam.Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha serikaliikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwemokumng'oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Ukawa ProfesaIbrahim Lipumba akiwa na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na KatibuMkuu wa Chadema, Wilbrod Slaa, alisema Kikwete anasita kumuondoa Muhongo wakatiBunge lililishatoa maazimio ya kutaka aondolewe.
Profesa Lipumba alisema Bunge linalowakilishawananchi zaidi ya milioni 45 liliazimia uteuzi wa Muhongo utenguliwe lakinirais anasema bado anachunguza.
Profesa Lipumba alisema kama Rais Kikweteatashindwa kumwajibisha Muhongo atakuwa ameshindwa kutekeleza moja ya maazimioya Bunge na kwamba Ukawa litaliomba Bunge kuiwajibisha serikali.
Alisema moja ya njia ya kuiwajibisha serikali nipamoja na wabunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu.
Profesa Lipumba alisema " hivi rais anachunguza ninihaliamini bunge, kama anavyoteua mawaziri pia ana madaraka ya kutenguanafasi zao, sasa anasita nini wakati ni azimio la bunge limemwelekeza,ikumbukwe kuwa bunge kwa niaba ya wananchi ndilo lenye jukumu la kuisimamiaserikali," alisema Lipumba.
Alisema hotuba aliyoitoa Jumatatu wakatiakiwahutubia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, haijakidhi matarajio ya wengikwani kuna maazimio hayajatekelezwa.
Azimio ambalo halijatekelezwa na rais Kikwete nilile linalotaka kutaifishwa kwa mitambo ya IPTL na kutengua uteuzi waMuhongo.
Mwenyekiti huyo alisema rais amekataa kutekelezaazimio la kutaka mitambo ya IPTL itaifishwe na kutoa sababu ambazo hazinamaana.
"Tangu mitambo ya IPTL imefungwa taifalimepata hasara kubwa kwa sababu umeme unaouzwa na ni wa gharama kubwa kulikomitambo yoyote ya umeme inayotumika katika bara la Afrika taifa limeingiahasara kubwa, rais aitaifishe," alisema Profesa Lipumba.
Alisema katika hotuba hiyo rais alionyeshakuipendelea IPTL na kuikandamiza Tanesco wakati akielezea kuwa fedha za Escrowzilikuwa mali ya IPTL.
Hatua za kuchukua
Lipumba alisema kama rais atashindwa kutekelezabaadhi ya maazimio, Ukawa wataitisha maandamano nchi nzima ili kulaani ufisadiwa Tegeta Escrow na kushinikiza utekelezaji wa maazimio ambayo yatakuwahayajatekelezwa.
Alisema hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wotewaliohusika na ufisadi wa akaunti ya Tegeta Escrow na wengine walionufaikanazo.
Sheria ya maadili itungwe upya ili iweke uwazi wamtu yoyote kuona taarifa ya mali za viongozi.
Vyamavya siasa vya Ukawa kwa kushirikiana na wabunge vitaendelea kuelimishaumma kuhusu ufisadi wa Akaunti ya Tegeta Escrow
 
HOTUBA YARAISNA ESCROW
RAIS ALISIFU BUNGE BAADA YA KUDHALILISHA


Mabandikoyaliyotangulia tulieleza kuwa, hotuba ya Rais kwa ''wazee'' wa Dar ililengamambo 3.
Kwanza, kampeni ya tezi dume, Escrow na mwisho kura ya maoni.

Kilichofanywa ni kutenga, ile ya tezi dume ikafanyika Ikulu, nay a escrow ukumbini DiamondJubilee

Kura ya maoni iliyondolewa baada ya kubainika escrow ingefunika ujumbe wa katiba ya Chenge na CCM.
Ndio hasa msingi wa kuhamisha hadi mwisho wa mwezi


Taehem 31 Rais akatoa hotuba ya mwaka mpya iliyofunikwa zaidi na kura ya maoni ya CCM.
Rais alizungumzia umuhimu wa watu kujiandiskisha katika daftari la kupiga kura iliwaweze kushiriki kura ya maoni ya katiba ya CCM/Chenge na uchaguzi mkuu


Pamoja na ugumu wa kuandikisha ulioonyeshwa na tume ya uchaguzi, bado Rais anaamini kazi hiyo itafanyika ikifika mwezi Aapril 30.Hakukuwa na haraka kwasababu uchaguzi mkuu ni mwezi wa 10.

Haraka zinazoonekana ni kutaka kupitisha katiba ya Chenge kwa nguvu ili JK astaafu akiwana legacy ya imprimatur hata kama anajua hilo ni impromptu

Unadikishajiwa daftari la kupiga kura kwa kutumia teknolojia ya Bimetric una mtego ndani yake.
Kwanza, ni kuwachanganya wananchi waamini kuwa wanajiandikisha kwa ajiliya kura ya maoni ya katiba ya Chenge, na pili, kuna ukweli kama hawatajiandikisha basi wanaweza wasipige kura mwezi wa 10


Hoja kubwaya wapinzani na wananchi wanaoitakia nchi hii mema, ni kwanza kujiandisha iliwaweze kupiga kura uchaguzi mkuu. Pili, kuhakikisha hawajadili katiba ya Chenge ili kutoipa uhalali.
Ni haramu sasa kwanini watu wajadili mzoga kama unasehemuinayofaa.


Hayo yanafanyika makusudi ili kulazimisha katiba ya Chenge.
Hatari iliyopo mbeleni ni uchaguzi kutofanyika kwani nchi inaweza kuselelea katika machafuko.
Hatujui kwanini Rais halioni hilo


Kwa kutambua kuwa wananchi wamekasirika na serikali ya JK kwa kashfa kama Escrow, na kwa kujua kuwa wananchi hawajaridhika na majibu yake, na pia kutambua kuwa bunge limedharauliwa, JK amelisifu bunge kwa kusimamia serikali vema

Si kwamba amelisifu bunge kwa nia njema, ni kwa kutambua kuwa wabunge hasa wa CCM wamechukizwa na jinsi alivyolidhalilisha bunge na jinsi anavyolinda wahalifu.

Hofu aliyonayo JK ni kwa serikali kwanza kuwajibishwa hasa waziri mkuu, na pili miswada kukosa kuungwa mkono na wabunge, na muhimu zaidi ni wabunge kumsusia na kura yake ya maoni.

Huo ndio msingi wa kuonyesha ''anawapenda' wabunge kwa njia za undumila kuwili.

Jinsi JK alivyosimamia mchakato ambao si tu umeudhi wananchi bali pia wana CCM wengi, na jinsi alivyoshughulikia suala kama la escrow, safari ya katiba ya Chenge ningumu.

Ugumu nikuwa wananchi wametambua kwanini akina Chenge waliteka mchakato, na wamebaini kwanini akina Chenge wameandika katiba yao ya mafichoni na sasa wanailazimisha.
Uhusiano wa Escrow na katiba ya Chenge ni pacha


Safari hiyoinaweza kutokamilika kwa amani, na mwisho wa siku mwenye dhamana ya yote atakuwa JK

Tusemezane
 
IKULU YAKANAKUDHALILISHA BUNGE

NI KIWEWE CHAKUSUSIWA SHUGHULI ZA SERIKALI

Ikulu imejibutuhuma za bunge kudhalilishwa na Rais. Taarifa ya gazeti moja ilinukuu viongoziwa upinzani wakimtuhumu Rais kumwacha waziri Mhongo ateuwe wajumbe wa bodi yaTanesco

Pendekezo labunge lilimtaka Rais amuondoe Mhongo katika nafasi yake.
Rais katika hotuba akadia amemweka kipora akisubiri uchunguzi Zaidi.

Hakuna shakalilikuwa ni change la macho. Kwanza, Rais alikuwa waziri wa nishati na waziriwa fedha wa serikali ziliopita.

Akiwa waziriwa nishati, IPTL ilikuja nchini. Hivyo, suala la IPTL, Escrow na mengine, Raisana nafasi nzuri sana ya kuyafahamu kuliko Watanzania wengi

Pili, PCCBna CAG ni vyombo vya serikali. Waziri mkuu aliagiza uchunguzi ufanywe wa Escrowna vyombo hivyo. Kauli ya waziri mkuu ni ya serikali ndani ya Bunge.

Tatu, Rais ana vyombo vingine vya usalama kama usalama wa taifa na Polisi.
Vyombo hivyo hufanya kazi ya kumu-update Rais.

Hakukuwa nasababu zozote za kumweka Mhongo kiporo kwa uchunguzi wa jambo analojua Rais,tena likiwa limefanyiwa uchunguzi na vyombo vyake.

Swali nikuwa, uchunguzi alioagiza Rais ni upi tena na unafanywa na nani?
Kilichotakiwa kufanyika ni ima Rais amwache Mhongo bila makosa, au amtimue

Hila zakumweka kiporo ni danganya toto. Rais hawezi kumuondoa mtu aliyemteua kamambunge.
Kutengua uwaziri hakutatengue ubunge wake.


Ni danganyakama hiyo wapinzani wamekumbana nayo mara nyingi.
Kilichotokeasafari hii ni hofu inayotokana na malalamiko ya wabunge hasa wa CCM kuwa Raisamewadhalilisha.

Na hakika amewadhalilisha sana. Ukisikiliza majibu ya hotuba ya wazee wa CCM Dar, ni kana kwamba Rais alikuwa ana question uwezo, umakini na uadilifu wa bunge.

Tena kafanya hivyo akiwasifia huku nyuma akiwapiga kwa dharau, vijembe na kashfa

Kauli kwambahakudhalilisha bunge inatokana na hofu aliyo nayo kwa wabunge.

Kazi yakunadi katiba ya CCM na Chenge haijaanza, na wauzaji ndio hao wamedhalilishwa.

Pili, badoRais atakumbana na upinzani mkali ndani ya chama chake kilicho majeruhi wasiasa za leo.

Hilo nallinamtia hofu kwa kuwepo mtafaraku mkali ndani ya chama.
Na mwisho,hofu kubwa ni kuungwa mkono kwa wapinzani kama matokeo ya chaguzi za siku zakaribuni yanavyojieleza.

Rais amepata ujumbe mwanana kuwa wananchi hawaridhiki na kwa bahati mbaya au nzuri siasa zanchi zimebadilika, mitazamo imebadilika na mbadala wa CCM upo, ni suala lamuda.

Hayo ndiyo yanayomplekea Rais kuwaonyesha wabunge anawapenda sana, huku matendo yake yakiwa yakuwadhalilisha na kuwang'onga kama alivyo wang'onga wabunge wa CCM waliopigia chapuo kifo cha suala la escrow

Tusemezane
 
RAIS ALIPOWANG'ONGA WABUNGE

KABADILIMSIMAMO WA SERIKALI YAKE KUIPINGA ESCROW

WABUNGE WALIOTETEA SERIKALI WANAONEKANA HAYAWANI NA MAZUZU, RAIS WALIYEMTETEA ANAWASHNGAA

Tunasema anawang'onga wabunge kwasababu Rais anawashangaa wabunge wanaopinga escrokujadiliwa.
Hapa kunasura mbili.

Kwanza, Rais aliagiza serikali yake izuie suala la escrow lisiendebungeni hata kufikia mahali pa kuishinikiza mahakama iandike barua juu yazuio


Je, kunaudhati wa Rais kusema amefurahia suala hilo kujadiliwa?Anafurahi vipi ikiwa hakutaka lijadiliwe bungeni?

Kama Rais alitaka suala hilo lijadiliwe na aliridhika lijadiliwe, ilikuwaje Job Ndugaialiyekuwa anakaimu kiti cha spika apelekwe nje ya nchi naserikali ile ile inayosema imefurahishwa na suala escrow bungeni?

Pili, Raisanasema anashangaa wabunge wa CCM waliopinga suala la escrow lisijadiliwe.
Hawani mawaziri kama Lukuvi na wasira, wabunge akina AsumtaMshama, Luisnde na wengine.



Maana yakauli ya Rais ni kuwafanya waliotetea serikali waonekane mazuzu namazumbuku, na ndivyo
Tatu, Raisanapohoji umakini wa wabunge kuhusu azimio lao ka kutaifisha mitambo ya IPTL,hilo ni tusi.

Bunge lina wasomi walioangalia athari za kufanya hivyo.
Lakinipia, kuwafukuza wahuni ni jambo linalolalamikiwa na wafadhili wa serikali yake.


Hili lilikuwa ni tusi kwa wabunge na bunge kwa ujumla.
Somo kubwawanalopaswa kulipata wabunge na viongozi wengine ni kuwa kauli za Rais huwazina ncha mbili na wala haijulikani ni lini atachukua upande wancha

Wapinzaniwameonja joto la jiwe mara nyingi. Kundi lisiloona ni la wana CCM ambao hatawanapodhalilishwa bado wanabaki kuwa waadilifu. Ni wakati wabunge wajiulize, hivi watatumika kama karatasi za maliwato hadi lini?

Je, wabungehawaoni jinsi wanavyodhalilishwa?

Tusemezane
 
Back
Top Bottom