Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Mkandara;

Mimi ni Neutral kwanini nipoteze muda wangu kusoma waraka? Nadhani hiyo ni kazi yenu wanaCDM. Jinsi waraka ulivyopatikana kwa kutumia njia za kijasusi inaonyesha hata bila waraka mambo yalikuwa sio swari.

Hili kukipa maendeleo chama, sio lazima Zitto na Mbowe wapendane. Na sio lazima viongozi wote wawe na sauti moja. Wanachotakiwa ni kuwa profressional katika majukumu yao. Kinachoonyesha ni kuwa viongozi wa CDM sio professional.
Zakumi, mimi ni mwanachama tu ambaye niliweka matumaini na nguvu zangu kwa CDM kuiangusha CCM. Kama Mtanzania mwenye kuipenda nchi yangu niliona umuhimu wa mchango wangu kadri ya uwezo wangu kuiangusha CCM ambayo imetugharimu sana kimaendeleo, hivyo kujiunga na CDM ilitokana na tumaini langu kwamba tukishirikiana sote kuibwaga CCM inawezekana..

Viongozi wa chama hawawezi kuongoza Chama ikiwa hawapendani ama kutoelewana. Neno professional linaweza tu kufanya kazi ikiwa kuna ushirikiano ambao mara zote kwa watu wasiopendana hutumia kigezo hiki cha kutoshirikiana kutoonyesha mapenzi yao. Kushirikiana ktk jambo ndio mapenzi yenyewe, ndio urafiki, ndio umoja laa sivyo pasipo mapenzi utaona ushirikiano nao ukitoweka.
 
Mkuu Zakumi , kumbuka jambo lililopelekea Zitto kuchukuliwa hatua si moja, yapo 11 kwa mujibu wa Mnyika.
Ni mmapema mno kusema alichukuliwa hatua kwa waraka tu.

Pili,zito hajavunja sheria yoyote ya nchi. Katika chama Zitto amekiuka miiko ya uongozi ambayo ni uwajibikaji wa pamoja
Zitto aliingia katika vikao vyote vya chama lakini amejitoa katika maamuzi aliyokuwa mshirika kama waraka ulivyogusia.

Zitto akiwa mtendaji mkuu msaidizi ameshindwa kuisaidia CDM na badala yake ametumia mwanya huo si kuweka ukweli bali kama silaha ya kukishambulia chama ambacho yeye ni kiongozi.

Waraka umeonyesha kuwa kombora la matumizi ya fedha litawamaliza CDM na yeye alifanya hivyo.
Kwa umma hilo ni sahihi ingawa pia motive behind ni mbaya kwasababu halikudhaniria kuusadia umma bali yeye.
Kichama ni kujiondoa katika uwajibikaji, kutumia nafasi hiyo pengine kukihujumu chama katika mambo aliyoweza kusaidia

Zitto hajatumia uhuru wa katiba ya nchi au ya CDM kueleza alichikusudia.
1. Hakuna kumbu kumbu kwamba aliwahi kuleta madai kama hayo.
Zipo kumbu kumbu za kutosha kuhusu madai yake yakiwa katika mitandao kwa kupitia watu wengine.

2. Alipaswa kutumia uhuru wake kujiuzulu ili aweze kuongea kama mwanachama asiyeridhishwa na maendeleo.
Zitto hakufanya hivyo.

3. Kwa kushindwa kutumia uhuru wake kama 1 na 2 hapo juu, Zitto ameshiriki kikamilifu katika kuandaa makundi yaliyotishia uhai wa CDM.
i) Ametajwa katika sakata la Masalia 7 tena na ID yake. Kwanini asitumie uhuru wake hadi ajifiche katika ID
2) Ametajwa katika mzozo wa Kafulila kikamilifu
3)Ameshiriki katika mzozo wa waraka, kikamilifu

Hayo ni baadhi tu ya yale aliyoyasababisha akiwa kiongozi mwenye dhamana ya CDM.
Sijui kwa hayo kunahitajika nini kubaini kuwa alichokifanya ni utovu wa nidhamu.

Hebu tuangalie kwa uchache sana sana, watu wanavyotumia uhuru wao kikatiba
- Seneta Liebaman alimuunga mkono John Mcain na kuamua kuwa mgombea binafsi nje ya chama cha Democrat
- Seneta Mcain amepinga uwepo wa tea party kwasababu Republican wanahitaji kuwa moderate kwa maoni yake
- Secretary Collin Powell alijiuzulu kwasababu hakukubaliana na sera mbaya za vita za akina Dickey Chen
-Collin Powell alimuunga mkono Obama hadharani akiwa Republican.
- John Major alimpinga Thatcher hadharani na akafanya kampeni ya kumuondoa hadharani
- Linda Choker alimpinga Blair ndani ya house of common hadharani na kujiuzulu
- Godon Brown alimpinga Blair na kuendesha kampeni ya kumuondoa kupitia chama chake
- Malema alipinga sera za ANC hadharani kuhusu wafanyakazi, kilichomuondoa ni mtamshi ya ubaguzi.
-Zitto Kabwe alipinga msimamo wa wabunge wa CDM kuhusu JK bungeni. Hakuchukuliwa hatu kwa uamuzi huru
- Kigwangalla amempinga spika wa CCM hadharani , hajachukuliwa hatua. Pengine amewekwa kiporo! sina uhakika
-Kitila alipinga Juliana Shonzo kufukuzwa. hakuchukuliwa hatua kwasababu yalikuwa maoni huru
- Sumaye anaipinga CCM hadharani na anaendelea, hajachukuliwa hatua kwa maoni yake

Ni mifano rahisi michache sana, orodha inaweza kufika kurasa 99.75

Ukiangalia, uhuru unatumika hadharani, kuchochea vurugu si uhuru. Uhuru wa kusema haukupi uhuru wa kwenda kupiga gita mwaisela au Sewahaji. Uhuru una limitations, una ethics na una boundaries.

Kama Zitto anaona hana uhuru kwanini asitafute eneo atakalokuwa huru?
Kwani ni lazima apate uhuru kule anakoamini hakuna uhuru. Kufanya hivyo ni kujinyima uhuru kabla hajanyimwa uhuru.

Nguruv3;
Kwa kusoma maelezo yako, kuna uwezekano mkubwa kuwa Zitto is ahead of time. Hapa nimeifungua katiba ya CDM. Naomba unionyeshe kipengele alichovunja?
Ngoja nikubali kuwa kuna mambo 11. Haya mambo ameyafanya kwa mara moja au ni mkusanyiko wa kipindi kirefu? Kama ni mkusanyiko wa kipindi kirefu kwanini hatua hazikuchukuliwa mapema?
Au CDM ilimvumilia kwa sababu alikuwa mpiga debe?
 
Zakumi, mimi ni mwanachama tu ambaye niliweka matumaini na nguvu zangu kwa CDM kuiangusha CCM. Kama Mtanzania mwenye kuipenda nchi yangu niliona umuhimu wa mchango wangu kadri ya uwezo wangu kuiangusha CCM ambayo imetugharimu sana kimaendeleo, hivyo kujiunga na CDM ilitokana na tumaini langu kwamba tukishirikiana sote kuibwaga CCM inawezekana..

Viongozi wa chama hawawezi kuongoza Chama ikiwa hawapendani ama kutoelewana. Neno professional linaweza tu kufanya kazi ikiwa kuna ushirikiano ambao mara zote kwa watu wasiopendana hutumia kigezo hiki cha kutoshirikiana kutoonyesha mapenzi yao. Kushirikiana ktk jambo ndio mapenzi yenyewe, ndio urafiki, ndio umoja laa sivyo pasipo mapenzi utaona ushirikiano nao ukitoweka.
Mkandara;

Uliyosema hapa ni muhimu sana. Ningekuwa Tanzania, na mimi ningei-support CDM hili CCM ibadilike au itoke madarakani. Sina mapenzi yoyote na CDM, Zitto au Mbowe. Mapenzi yangu na CDM ni adui wa adui yako ni rafiki yako.

Tatizo linalokuja ni kuwa baadhi ya viongozi wa CDM wanafikiri they are doing Tanzanians a favor kwa wao kuwa wapinzani wa CCM.
 
Mkuu Mchambuzi
Katika bandiko #32 umejasdili scenario 3 ambazo kamati kuu inazo kwa sasa.
Sijaona scenario inayoweza kutumika bila kuacha matatizo.

CDM wamepalilia hali hiyo kwasababu zifuatazo.
1. Double standard:
a)Wamekuwa na double standard kufikia maamuzi. Waliwaacha akina Kafulila wakaondoka wenyewe hata pale walipotakiwa kuwafukuza ili wasiondoke na heshima kama walivyowagomea Kitila na Zitto.

b)Walishindwa kuwafukuza akina Juliana na Mwampamba kupitia kamati kuu.
Walitumia BAVICHA ili kutoa nafasi ya kamati kuu kuwa neutral.
Ukweli ni kuwa waliogopa kuwaudhi akina Zitto na Kitila ambao walishatoa ushauri 'waachwe wabalehe'.

c)Chadema ikawafukuza madiwani wa Arusha kupitia kamati kuu na kamati za mikoa

d)Chadema ikasita kuchukua hatua dhidi ya Shibuda na kumwacha aendelee bila kuwa na mchango wowote.

e)CDM hawakuwahi kumchukulia hatua Zitto za kinidhamu japo onyo alipotajwa bila kuwa kinara wa makundi 3 sasa

Swali linakuja, ni standard gani CDM wataitumia ili kuhakikisha kuwa maamuzi yao hayakinzani na baadhi ya maamuzi ya siku za nyuma?

2.
CDM wamejichanganya kwa kuchukua kesi hii bila kujua ramifications wakiwa washtaki, waendesha mashtaka na mahakimu. Kulikuwa na nafasi ya kutumia chombo 'neutral'

Endapo wangefanya hivyo kazi ya kusimamia mamuzi ingekuwa rahisi, na wangeweza kuepuka lawama zisizo na ulazima ambazo zinaweza kupandikizwa kukidhi haja.

3
kamati kuu haikuwa na muda wa kutafakari tatizo zima kwa ujumla na upana wake.
Kitendo cha kuondoa mtu na kumweka mwingine ni hukumu tayari.
Sijui katika siku 14 ni kukata rufaa au ni kujitetea! Maamuzi ya hasira yanawaweka mahali pagumu kwa sasa.

Wafanye nini?
Wakusanye ushahidi usio na shaka, wasikilize upande wa utetezi kwa umakini na hukumu izingatie facts na si hisia.
Kitengo cha elimu na utafiti ulichosema kinaweza kabisa kusawazisha hali kama kitakuwa na watu makini.
Madiwani walifukuzwa Arusha, na CDM wakshinda viti vile vile walivyokubali kuviachia.

Maana yake ni wananchi wanaelewa wakielezwa, wanakereka na mambo kama ya waraka na wapo tayari kubadilika. Ikibidi kumfukuza mtu kwa vigezo sahihi na vyenye ushahidi let it be.

Kuendelea kulea personality kama walivyofanya huko nyuma hakutatoa matokeo tofauti na haya.Ni kuahirisha tatizo.

NCCR iliwahi kuondokewa na Mrema na kundi zima. Wale waliobaki wameendeleza NCCR na sasa ni bora kuliko TLP. Kwanini CDM waendelee ku entertain personality iliyowatesa, inayowatesa na itakayowatesa?

Sisi wananchi wa kawaida tunauliza, endapo CDM hawawezi kujenga nidhamu ndani ya chama, hawawezi kusimamia haki kwa makundi kwa standard moja na wanaogopa persnality kwasababu ya kura itakuwaje wakipewa nchi?
Je, wataweza kukabiliana na wezi wakiletewa taarifa ya CAG, Uswiss, visiwa vya Jersy au ufisadi wa bandari?

Mkuu Nguruvi3,

Kutokana na hoja yako ya maamuzi yenye double standard,
Je nitakuwa sahihi kusema moja ya tafsiri ni kwamba uamuzi wa kamati kuu kuwasimamisha wahusika uongozi ulilenga kulinda uongozi kwa kutumia "katiba ya chadema" na uamuzi wa kutowachukulia hatua zaidi wahusika utalenga kulinda kura 2015 kwa mujibu wa "ratiba ya chadema"?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Kutokana na hoja yako ya maamuzi yenye double standard,
Je nitakuwa sahihi kusema moja ya tafsiri ni kwamba uamuzi wa kamati kuu kuwasimamisha wahusika uongozi ulilenga kulinda uongozi kwa kutumia "katiba ya chadema" na uamuzi wa kutowachukulia hatua zaidi wahusika utalenga kulinda kura 2015 kwa mujibu wa "ratiba ya chadema"?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mkuu naomba uedit post yako, hakuna aliyesimamishwa uongozi bali wamevuliwa/fukuzwa nyadhifa zao.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu sijui huu waraka umeandikwa lini lakini kulingana na events zilizoorodheshwa hapo juu inaonekana kuwa waraka huu umeandikwa sii muda mrefu sana laa sivyo hoja ya uchaguzi mdogo za wawakilishi kwenye Halmashauri ya June 2013 isingekuwepo..

Ukweli utabakia tu kwamba swala langu la namba TANO (5) ndilo wengi wetu wameshindwa kulipa uzito ama kuliona maana kama kweli kuna kundi hili ndani ya CDM sioni sababu kwa nini Zitto analaumiwa kuunda makundi wakati tayari kuna kundi hili ambalo kiutawala Zitto alitakiwa kuwa moja wao. Hawa watu watatu ni kina nani na wameaniwa kiasi gani kuwatenga kina Zitto na imeanza lini huku kutoaminiana ndani ya chama.

Je, kuna ukweli wowote kuhusu tuhuma hizi?...Tumeyasikia malalamiko kama ya waraka huu toka enzi za marehemu Chacha Wangwe, na tumeyasoma humu humu JF - haiwezekani iwe kila siku Makao makuu inasingiziwa na jambo lisilokuwepo.
Mkuu Mkandara huo waraka umeandikwa muda sasa na kinachofanyika ni uekelezaji wake ambao Zitto anaufanyia kazi ikiwa ushahidi kuwa alishakubali jukumu kama waraka ulivyosema. Hakuondolewa katika hao watatu bali alijiondoa, soma maneno haya
Mwaka huu viongozi wetu wamekuja na ugatuaji madaraka kutoka makao makuu ya taasisi na kupeleka madaraka kwenye kanda mbalimbali.
Zitto hawezi kusema viongozi wetu yeye akiwemo! Kama hakushirikisha hiyo ilikuwa fursa ya kueleza na si kutumia mitandao.

Hao watu watatu wametajwa katika waraka kuwa ni Mbowe, Dr Slaa na mtunza fedha. Hakuna sababu za kufikiri kuna wengine zaidi

Kuhusu watu kulalamika sehemu kama hapa JF nakubalina nawe kuwa wameanza muda mrefu kidogo.
Tena malalamiko yako yanafanana sana na malalamiko yaliyopo katika waraka.

Mathalan, kuna mwana CCM lakini kwa kusukumwa na utashi wa demokrasia nchi nzima ameamua kuwaasa wana CDM. Ushauri wake umefanyiwa kazi na waandika waraka kwasababu yeye aliandika muda mrefu kabla ya waraka.

Nadhani tuangalie malalmiko haya na ya waraka tuone kama yanatupa jingine zaidi ya kuuona waraka kama ulivyo ili
Waraka:Mpinzani wetu (Mbowe)ni mtu aliyezaliwa kwenye utajiri na anadhani pesa ni kila kitu
HAMY-D(July 2013): Mbowe ni mtoto wa kishua, unadhani atakuwa na huruma na watanzania?Mbowe kama hajawahi kuonja suruba ya umaskini, uchungu kwa watu maskini ataupata wapi?
Waraka:Simtu wa kujipenda nafsi na katika kupambana umaskini wa watu badala ya umaskiniwake

HAMY-D :
sisi tunataka maskini wenzetu ndio watutoe hapa tulipo na kutupeleka mbele. Birds of the same feathers, flock together!!
Waraka: Matukiomawili yanamwacha uchi katika hili pale alipolitangazia taifa kwambawawakilishi wetu wote hawatachukua posho za vikao halafu yeye na wengine wotewanazichukua hadi leo na kumwacha mtendaji msaidizi peke yake. Na la pililinalofanana na hilo ni pale alipotangaza kutotumia gari la serikali ambalo nila kifahari kisha akalirudia kimya kimya

HAMY-D: Pia, kama Mbowe ana stahili kuliendesha hilo gari, huoni ndio maana serikali ilimpa hili awe nalo? sasa kwanini yeye alirudishe? haafu sasa hizo sababu zake utasikia mara uzalendo, mara nawaulumia wananchi kwani serikali ina matumizi makubwa. Sasa kwanini alichukue wakati tayari alitoasababu za kulikataa? Nikisema Mbowe hana msimamo nitakuwa nimekosea?Last edited by HAMY-D; 12th July 2013 at 11:26.
Waraka:Nikubadilisha uongozi wa taasisi haraka iwezekanavyo

HAMY-D: Fanyeni uchaguzi haraka wa ndani ya CDM mumtoe huyu Mbowe, mauaji aliyofanya kwa vijana wetu chini ya uongozi wake yanatosha.
Waraka: Tutahakikisha tuko busy kupost mambo mema na mazuri yatakayokuwa yakifanywa na MM kila wakati na kuzidi kusambaza sifa zake njema kila inapotokea nafasi. Atakayefanya kazi hiyo ni sisi wengine wala si yeye! Pia tutahakikisha kila post ya kumchafua inapatiwa majibu bila kutumia ID yake inayojulikana.

HAMY-D WanaJF, hivi ni kwanini Mbowe asiige siasa za Zitto?
Sikuwahi kumuona Zitto kwenye maandamano yaliyo husisha mauaji au uvunjifu wa amani wa aina yoyote!
Waraka: Uongozi wa sasa wa taasisi yetu umefanya tuonekana kwamba taasisi yetu ipo kwa ajili ya kuvuruga amani ya nchi, Yote hii ni kwa sababu tumekuwa hatuna mbinu mpya za mapambano zinabadilikabadilika zaidi ya maandamano ya kila mara.

Hamy-D:
Utajadili maendeleo wakati amani na utulivu vipo hatarini?
Hatuwezi kuijenga nchi wakati kuna kundi la watu linaibomoa nchi kwa kasi.
Amani ni tunu ya taifa letu, ikipotea kuirudisha si jambo dogo.
Ni bora tubaki na dhiki na ufukara wetu ila amani idumishwe. Jambo ambalo MBOWE na Dr Slaa hawaoni kama ni muhimu.
 
Mkuu Mkandara
Katika bandiko lako hapo nyuma umeonyesha wazi madai ya waraka yana uhalali
Mimi sijasema hayana uhalali au vinginevyo.
Ninachosema yamekosa nguzo muhimu ya uhalali kama alivosema Mchambuzi.
Waraka una makosa katika maudhui, uandishi na hoja. Hapo ndipo tatizo lilipo.

Umesema pia watu wasisusie suala la kutajwa watu watatu.
Huko nyuma nimewahi kuandika kuhusu udhaifu wa Mbowe, udhaifu wa Slaa, udhaifu wa Zitto na upotoshaji wa Kitila.

Nilionya sana kuhusu tatizo la masali na Kafulila. Nilisema uongozi wa CDM unalea personality na kushindwa kuchukua hatua. Hata pale unapochukua hatua kuna double standard.
Nilikumbusha mgogoro utalipuka ndani ya miezi 18 nikiandika June 2012.

Kuna mapungufu kama taasisi hilo, lazima walikiri.
Hata hivyo ni wazi mapungufu ni kutokana na kutoaminiana au kuhujumiana.

Sidhani kama ni vema tukijisahaulisha ya nyuma ili tutee waraka au tusiseme wahusika au kutoa excuse kwa Zitto. Waraka ni mwendelezo wa tatizo la muda mrefu. Tatizo lililopo ni njia zilizotumika kufikisha ujumbe kwa taasisi.

Ni kwa msingi huo Zitto ambaye ni kiini cha mgogoro ataangaliwa kwa ukubwa na mapana yake.
Hakuna asiyejua kuwa public ilianza kupoteza imani naye siku nyingi aliposhiriki sakata la Kafulila, Masalia na Juliana.

Katika waraka huu ametekeleza mambo muhimu yaliyosemwa kama kulipua bomu la ukaguzi wa fedha ambalo waraka umetamka wazi litawamaliza viongozi wa sasa.

Nia haikuwa kutetea fedha za umma, ilikuwa kutumia nyadhifa na ofisi za umma kuungamiza uongozi ambao yeye ni mshiriki. Hivi kitendo hicho kinatofauti gani na usaliti wa umma na chama chake.
Anausaliti umma kwa kujivika ngozi ya ushujaa, anasaliti chama chake kama katibu mkuu kwa kutumia umma.

Tunaelewa Kitila alikimbilia kusema Zitto hakushiriki ili kumokoa. Alichosema ni Zitto kutoshiriki kuandika, lakini ukweli usio na chembe ya shaka Zitto ameshiriki kuutekeleza waraka katika hatua za awali.
1. Ameshiriki katika kulipua bomu la ukagauzi lililoandikwa vema katika waraka.
2. Ameanza kushiriki kampeni za chama baada ya kususia miaka mingi kama ilivyoandikwa katika waraka
3. Alianza kujenga mtandao ambao leo utasikia matamko ya kulaani tu kufukuzwa si upuuzi wa waraka kama ilivyoandikwa katika waraka.

Pamoja na hayo, Zitto amendelea kuughilibu umma. Leo alikuwa na Fina Mango ambaye ukisoma interview ni kama pre prepared lakini tunaipa benefit of doubt.

Zitto ameeleza jinsi gani ameshiriki mambo ya kitaifa na kimataifa, akitaka kuundoa umma katika hoja za msingi kabisa za jinsi anavyowasumbua CDM kwa makundi, kiu ya madaraka na usaliti na ushiriki katika waraka ambao Kitila amekiri ni makosa na Zitto mshiriki na mtekelezaji anajiondoa.

Mkakati huu wa kueleza mazuri na si kuomba radhi kwa uchafu waliowahi kuufanya ni ishara njema ya kukosa hekima na uaminifu kwa Zitto.

Ni Zitto huyu anayezungumzia ufisadi wakati tunafahamu wazi kuwa aliisema sana Barrick na kisha kwenda Kigoma kupokea milioni 10 kwa mlango wa halamshauri.

Baada ya hapo ni Kimya hadi leo.
Ufisadi gani atauongelea huyu kijana na kughilibu umma wote. Yes, anaweza lakini ni kwa baadhi.

Hatuhitaji kusikia Zitto alishirikiana na kiongozi gani wa nje, tunamtaka ajibu tuhuma zinazo mkabili ikiwa ni pamoja na usaliti wa wenzake mara nyingi sana akipewa benefit of doubt.

Mkuu Mkandara, kuna tatizo ndani ya CDM. Wakati watu wanaliona leo sisi tumeliongelea miezi 14 iliyopita na wewe ulikuwa sehemu ya mjadala.

Tuliwasaidia CDM kuwashauri kwa nia njema kabisa wakaamua ku entertain personality.
Mimi nipo katika rekodi ya kusema Juliana alikuwa anatumiwa na watu wakubwa sana, nikamtaja Kitila Mkumbo hasa kwa kauli yake ya 'waachwe wabalehe'.

Niliwaambia CDM, Juliana kwa umri wake, kielimu, kisiasa na kijamii hawezi kuleta timbwili kama lile kulikuwa na vigogo. Leo waraka umefumua kila jambo.

Sidhani kama taifa hili lina upungufu wa viongozi iwe CCM au CDM.
Wapo watu wazuri na vichwa vya maana kutoka kila chama.

Taifa hili haliwezi kuendelea kama tutakemea ulaghai wa CCM na kuficha ulaghai wa CDM.
Sioni tofauti ya mhalifu wa CCM na mhalifu wa CDM ndio maana tunasema wazi tukiwa huru.

CDM kama wanachama hawana tatizo to be honest with you.
Matatizo yaliyopo ni ya kitaasisi tena inayokua hivyo kuna nafasi ya kujirekebisha.

Tatizo la CDM ni hizi personality zinazodhani kuwa zenyewe ndio CDM hasa viongozi.
Hizi ndizo zitaitafuna CDM hadi mwisho. Nilidhani Zitto angechukua ushauri wa kukaa kimya ili japo aonekane amejifunza.

Ukosefu wake wa busara unazidi kutamalaki kwa kudhani kuwa anaweza kufanya spinning dunia yote ikaingia katika ghiliba zake kama alivyozoea na kama waraka ulivyotaja kuwa ni moja ya strength zake.

Kwa mwendo wa Zitto wa sasa na ukosefu wa uaminifu, busara, hekima na uwezo wa kupima nadhani CDM wanacheza na kaa la moto.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Kutokana na hoja yako ya maamuzi yenye double standard,
Je nitakuwa sahihi kusema moja ya tafsiri ni kwamba uamuzi wa kamati kuu kuwasimamisha wahusika uongozi ulilenga kulinda uongozi kwa kutumia "katiba ya chadema" na uamuzi wa kutowachukulia hatua zaidi wahusika utalenga kulinda kura 2015 kwa mujibu wa "ratiba ya chadema"?Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mkuu ndio maana halisi. Kwamba kuna personality zinapokea special treatment. Hili si tu kuwa limekuwepo bali litaendelea ku set bad precedent katika siku zijazo.

CCM waliwahi kuchukua maamuzi mazito na wakabaki kama chama imara. Mrema aliondoka na kundi kubwa la wanachama. Miaka ya karibuni CCM wakaanza ubabaishaji wa kuogopa personality, angalia jinsi wanavyowatesa sasa hivi.
Watu watadhani CCM ni shwari, ukweli hali ni mbaya sana kwasababu wao tofauti na CDM wana vigogo wanaoamini ndio Chama. CDM wana tuvigogo tu.

Ninaamini katika ujenzi wa taasisi imara zaidi za vyama vyote. Hata kama ni kupoteza kura ni heri kuwa na chama chenye watu committed na effective kuliko lundo linalochanganya umma.
 
Nguruv3;
Kwa kusoma maelezo yako, kuna uwezekano mkubwa kuwa Zitto is ahead of time. Hapa nimeifungua katiba ya CDM. Naomba unionyeshe kipengele alichovunja?
Ngoja nikubali kuwa kuna mambo 11. Haya mambo ameyafanya kwa mara moja au ni mkusanyiko wa kipindi kirefu? Kama ni mkusanyiko wa kipindi kirefu kwanini hatua hazikuchukuliwa mapema?
Au CDM ilimvumilia kwa sababu alikuwa mpiga debe?
Katiba ya Chadema toleo la 2006. Katika Kanuni za Uendeshaji Kazi za Chama. Sura ya 10, Ibara ya ix, imeandikwa: "Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya Uongozi wa Chama au Wanachama wake."

Na katika Katiba hiyo hiyo Sura ya 7 kuhusu kazi za Kamati Kuu, Ibara ya 7, Ibara ndogo t, imeandikwa: "Kufanya uamuzi juu ya mapendekezo ya kufukuza Mwanachama." Na Ibara ndogo v, imeandikwa: "Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume na Katiba, Kanuni na Maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake."
 
Katiba ya Chadema toleo la 2006. Katika Kanuni za Uendeshaji Kazi za Chama. Sura ya 10, Ibara ya ix, imeandikwa: "Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya Uongozi wa Chama au Wanachama wake."

Na katika Katiba hiyo hiyo Sura ya 7 kuhusu kazi za Kamati Kuu, Ibara ya 7, Ibara ndogo t, imeandikwa: "Kufanya uamuzi juu ya mapendekezo ya kufukuza Mwanachama." Na Ibara ndogo v, imeandikwa: "Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume na Katiba, Kanuni na Maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake."

Mwanaukweli:

Ndio maana niliomba hicho kipengele. Kwenye jumuia yoyote, hata jumuia ya watu wawili, ni lazima migogoro ijitokeze. Na migogoro mingine inajitokeza bila watu kujifahamu. Hivyo kipengele hicho hakina nafasi katika katiba ya nchi, chama au ya nyumbani.

Kwa kutumia kipengele hicho kiongozi asiyefuata utaratibu au katiba ya chama anaweza kuwahukumu wapinzani wa vitendo vyake kuwa ni wachochezi wa migogoro. Na wapinzani wake wanamuona kiongozi asiyefuata utararibu ni chanzo cha migogoro. Hivyo migogoro is a relative term.

Kwa kutumia mtaji huu ni nani atoe hukumu kuwa viongozi fulani wanaanzisha vikundi? Kwanini hukumu ya Zitto itolewe na watu ambao anaona kwa kiasi fulani wanaboronga?

Kuna vitu CDM ni lazima kijifunze kuishi navyo kama chama kinataka kuwa na nafasi katika jamii. Kwanza ni lazima kijifunze kuishi na makundi na migogoro. Pili migogoro na vikundi ndivyo vinavyokuza demokrasia ndani ya nchi na vilevile ndani ya chama. Tatu uchu wa madaraka ni chanzo cha migogoro lakini chanzo kikubwa ni uongozi mbovu au usiojiamini. Kwa mfano Mbowe hana ubunifu wa kifikra na wenye ubunifu wa kifikra pose serious threats to his leadership.
 
Mwanaukweli:

Ndio maana niliomba hicho kipengele. Kwenye jumuia yoyote, hata jumuia ya watu wawili, ni lazima migogoro ijitokeze. Na migogoro mingine inajitokeza bila watu kujifahamu. Hivyo kipengele hicho hakina nafasi katika katiba ya nchi, chama au ya nyumbani.

Kwa kutumia kipengele hicho kiongozi asiyefuata utaratibu au katiba ya chama anaweza kuwahukumu wapinzani wa vitendo vyake kuwa ni wachochezi wa migogoro. Na wapinzani wake wanamuona kiongozi asiyefuata utararibu ni chanzo cha migogoro. Hivyo migogoro is a relative term.

Kwa kutumia mtaji huu ni nani atoe hukumu kuwa viongozi fulani wanaanzisha vikundi? Kwanini hukumu ya Zitto itolewe na watu ambao anaona kwa kiasi fulani wanaboronga?

Kuna vitu CDM ni lazima kijifunze kuishi navyo kama chama kinataka kuwa na nafasi katika jamii. Kwanza ni lazima kijifunze kuishi na makundi na migogoro. Pili migogoro na vikundi ndivyo vinavyokuza demokrasia ndani ya nchi na vilevile ndani ya chama. Tatu uchu wa madaraka ni chanzo cha migogoro lakini chanzo kikubwa ni uongozi mbovu au usiojiamini. Kwa mfano Mbowe hana ubunifu wa kifikra na wenye ubunifu wa kifikra pose serious threats to his leadership.
Mkuu Zakumi kuna element za kutaka ku justify uovu kwasababu tu ya kumkinga Zitto.

Mwandishi wa waraka Kitila Mkumbo amekiri ilikuwa ni makosa. Wote waliandika barua za kujiuzulu hata kabla ya kunyooshewa kidole. Watu hawajiulizi endapo Zitto hakuhusika na kuandika waraka kwanini alitaka kujiuzulu?

Malalamiko ya Zitto na Kitila hayakuwahi kuwa tishio kwasababu hawakautoa hadharani.
Hakuna rekodi ya kikao au mkutano ambao wamesema hayo,ushahidi kuwa hawakujiamini na walikuwa na ni ovu sana.

Alichokifanya Zitto ni kutumia nyaraka za chama na ofisi ya serikali kutaka kupanda ngazi kwa njia za kitoto na zisizo na element za usomi.

Huwezi kutupa komkbora kwenye nyumba ya glasi unayoishi mwenyewe.
Huwezi kutoboa mtumbwi unaosafiri nao. Walichotaka wasaliti hawa ni kuporomosha CDM ili kuwaondoa wasiowataka tena kwa jia zisizofuata demoktasia wakiwa chama cha kidemokrasia.

Endapo kuna tatizo la uongozi hilo lisemwe hadharani siyo kwenda kuwachochea akina Juliana Shonzo kuleta mitafaraku.
Leo kampeni zote za kueneza CDM zimekufa kwasababu ya Zitto. Tuwaambie ukweli

Walitakiwa wasimame kidete katika kuhakikisha chaguzi zinakuwa za wazi na kampeni zinakuwepo.
Uwepo wa vikundi hauepukiki lakini vikundi vya maana si hivi vya akina Kitila Mkumbo, Juliana Shonzo ili kumweka Zitto madarakanii. Huyu ndiye amekuwa kinara wa matatizo ndani ya CDM, let me be honest

Wanachama waachwe waamue nani anaongoza chama chao.
Huyo Zitto unayesema ni tishio na mbunifu nakuhakikishia ni mnafiki mkubwa.
Kahongwa na Barrick huo ndio ubunifu!!!

Pengine mada haijaeleweka. Mada ni kujadili waraka uliopo hapo juu.
Na kwabahati nzuri utetezi wao umewekwa.

Kinachoshangaza ni kuona watu hawawezi kabisa kumtetea Zitto na Kitila kwa waraka bali mapenzi tu.
Ndio maana tunaona hoja za mapenzi zaidi kuliko ukweli unaonekana.

Nimeuliza kwanini watu hawachambui waraka uliopo na kuonyesha mikakati ya hawa jamaa?
Mimi nimeonyesha wapi kuna tatizo mstari mmoja hadi mwingine, wenzangu mnaotetea onyesheni nia njema ya waraka mstari hadi mwingine. Hata kama ni 'Mbowe' hana akili onyesheni tutaelewa.

Wao wenyewe wametaka kujiuzulu, maana yake ni kuwa hilo halikuwa sahihi kufuatana na vifungu vilivyowekwa na wanavyovifahamu. Lakini basi kama wangekuwa wakweli wasingeanza kuchafua watu mitandaoni.
Hebu soma kwa undani bandiko#92 hapo juu uone jinsi waraka ulivyokuwa unafanyiwa kazi si hadharani bali mafichoni.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi kuna element za kutaka ku justify uovu kwasababu tu ya kumkinga Zitto.

Mwandishi wa waraka Kitila Mkumbo amekiri ilikuwa ni makosa. Wote waliandika barua za kujiuzulu hata kabla ya kunyooshewa kidole. Watu hawajiulizi endapo Zitto hakuhusika na kuandika waraka kwanini alitaka kujiuzulu?

Malalamiko ya Zitto na Kitila hayakuwahi kuwa tishio kwasababu hawakautoa hadharani.
Hakuna rekodi ya kikao au mkutano ambao wamesema hayo,ushahidi kuwa hawakujiamini na walikuwa na ni ovu sana.

Alichokifanya Zitto ni kutumia nyaraka za chama na ofisi ya serikali kutaka kupanda ngazi kwa njia za kitoto na zisizo na element za usomi.

Huwezi kutupa komkbora kwenye nyumba ya glasi unayoishi mwenyewe.
Huwezi kutoboa mtumbwi unaosafiri nao. Walichotaka wasaliti hawa ni kuporomosha CDM ili kuwaondoa wasiowataka tena kwa jia zisizofuata demoktasia wakiwa chama cha kidemokrasia.

Endapo kuna tatizo la uongozi hilo lisemwe hadharani siyo kwenda kuwachochea akina Juliana Shonzo kuleta mitafaraku.
Leo kampeni zote za kueneza CDM zimekufa kwasababu ya Zitto. Tuwaambie ukweli

Walitakiwa wasimame kidete katika kuhakikisha chaguzi zinakuwa za wazi na kampeni zinakuwepo.
Uwepo wa vikundi hauepukiki lakini vikundi vya maana si hivi vya akina Kitila Mkumbo, Juliana Shonzo ili kumweka Zitto madarakanii. Huyu ndiye amekuwa kinara wa matatizo ndani ya CDM, let me be honest

Wanachama waachwe waamue nani anaongoza chama chao.
Huyo Zitto unayesema ni tishio na mbunifu nakuhakikishia ni mnafiki mkubwa.
Kahongwa na Barrick huo ndio ubunifu!!!

Pengine mada haijaeleweka. Mada ni kujadili waraka uliopo hapo juu.
Na kwabahati nzuri utetezi wao umewekwa.

Kinachoshangaza ni kuona watu hawawezi kabisa kumtetea Zitto na Kitila kwa waraka bali mapenzi tu.
Ndio maana tunaona hoja za mapenzi zaidi kuliko ukweli unaonekana.

Nimeuliza kwanini watu hawachambui waraka uliopo na kuonyesha mikakati ya hawa jamaa?
Mimi nimeonyesha wapi kuna tatizo mstari mmoja hadi mwingine, wenzangu mnaotetea onyesheni nia njema ya waraka mstari hadi mwingine. Hata kama ni 'Mbowe' hana akili onyesheni tutaelewa.

Wao wenyewe wametaka kujiuzulu, maana yake ni kuwa hilo halikuwa sahihi kufuatana na vifungu vilivyowekwa na wanavyovifahamu. Lakini basi kama wangekuwa wakweli wasingeanza kuchafua watu mitandaoni.
Hebu soma kwa undani bandiko#92 hapo juu uone jinsi waraka ulivyokuwa unafanyiwa kazi si hadharani bali mafichoni.

Nguruv3;

I am a libertarian. Hivyo ninaamini kuwa watu wana haki ya kufikiri na kuandika mawazo yao. Kama inavyoonyesha, waraka huu ulikuwa bado katika private domain. Hivyo si haki ya viongozi kutumia mbinu za kijasusi kupata waraka huu.

Je kwenye waraka waandishi wanataka kuwaondoa viongozi wa CDM kwa kutumia nguvu au kimabavu? Je hao viongozi waliopo madarakani wanatumia njia za kidemokrasia kukaa madarakani? Je wanatumia njia za kidemokrasia kuendesha chama?

Demokrasia haishii pale kiongozi anapochaguliwa kwa kura nyingi?
 
Mkuu Zakumi:

Taifa letu bado linaugua makovu yaliyotokana na siasa za minyukano, fitina, upandikizaji wa chuki, makundi majungu, na mengine mengi ambayo yalihujumu demokrasia katika mchakato wa kupata mgombea urais ccm 2015. Mkakati kwa mujibu wa waraka husika hauna tofauti kubwa na kilichotokea 2005 ndani ya ccm; Kwa ccm, matokeo yake ikawa kwa mtandao kupasuka vipande vipande na kuingiza nchi katika mgogoro mkubwa unaoendelea hadi leo, kutoweka kwa dhana ya kuheshimu demokrasia kwani ilishahujumiwa (rejea matukio katika uchaguzi uliofuatia - 2010),n.k;

Kwa mwanachama yoyote wa chadema mwenye nia ya dhati ya kuona chama chake kinafika 2015 kikiwa intact, united and stronger, hapakuwa na sababu ya kufanya haya, hasa ikizingatiwa kwamba chadema ilikuwa inakata mbuga kwa kasi ya ajabu kuliko kipindi chochote katika historia ya chama hiki; Kwa mtazamo wako, je:

*Kulikuwa na haja kweli ya wahusika kuvuruga kasi hii katika kipindi ambacho taifa lilikuwa linashukuru ujio wa upinzani wa kweli kwa CCM ambapo CCM ilianza kujirudi na kuanza kujali tena hali duni za wananchi japo kwa mwendo wa konokono?

Ni dhahiri kwamba uongozi wa sasa wa chadema (taifa) una mapungufu mengi kama ilivyo kwa ccm na kwingine. Lakini, viongozi waliopo madarakani chadema leo (taifa) wanahusika moja kwa moja na mafanikio ambayo chadema na wanachama wake wanajivunia leo; Kwa mfano, viti bungeni vimeongezeka, wabunge wamekomaa zaidi kisiasa na kuipa serikali ya ccm changamoto zinazostahili kuletwa na upinzani, lakini muhimu ni kwamba chini ya uongozi huo, leo hii chaguzi za ubunge sehemu yoyote bara odds za ushindi ni karibia 50/50 na CCM; mkuu Zakumi, shukrani kwa haya ndio iwe "a coup" kwa hoja kwamba uochama chao (chadema) kinaelekea in the wrong direction na kwamba kipo in the wrong hands?what's a better direction for chadema leo kuliko direction ya sasa? Na kama tatizo ni leadership, je kuna kipindi chochote ambacho chadema wauonaweza kujisifia kwa mafanikio ya kiuongozi kuliko kipindi cha sasa?

Mkuu Zakumi, waraka husika una mapungufu sana, sio tu on context and intent, bali hata substance/content, kwani kulikuwa na njia mbadala za kufanikisha malengo husika ambayo isingejumuisha ujenzi wa makundi, chuki, fitina, uchochezi, na mengine mengi yanayohujumu demokrasia. Binafsi sioni cha maana mle zaidi ya mambo makuu matatu:

*Elitism ambapo kuna kila dalili kwamba wahusika wanataka kuweka chama mikononi mwa wasomi, not necessarily mikononi mwa wananchi, hasa vijana ambao ndio mtaji mkuu wa chama;
*Chauvism - wahusika kutaka anzisha utamadumi wa prejudiced belief kwamba wao ndio wana superiority in terms of knowledge, intellect etc;
*Nepotism - kwa kuja na mikakati ya wazi ya kuweka relatives or close friends in power;

Katika yote haya, hakuna lenye manufaa kwa demokrasia na maendeleo ya chama wala taifa, badala yake ni hujuma kwa the aforementioned. Mkuu Zakumi, katika hili, sioni any relevance na wewe kuwa "a libertarian" kama unavyodai, badala yake naona you are "a fanatic" - kwani its clear that you are motivated by irrational enthusiasm;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi:

Taifa letu bado linaugua makovu yaliyotokana na siasa za minyukano, fitina, upandikizaji wa chuki, makundi majungu, na mengine mengi ambayo yalihujumu demokrasia katika mchakato wa kupata mgombea urais ccm 2015. Mkakati kwa mujibu wa waraka husika hauna tofauti kubwa na kilichotokea 2005 ndani ya ccm; Kwa ccm, matokeo yake ikawa kwa mtandao kupasuka vipande vipande na kuingiza nchi katika mgogoro mkubwa unaoendelea hadi leo, kutoweka kwa dhana ya kuheshimu demokrasia kwani ilishahujumiwa (rejea matukio katika uchaguzi uliofuatia - 2010),n.k;

Kwa mwanachama yoyote wa chadema mwenye nia ya dhati ya kuona chama chake kinafika 2015 kikiwa intact, united and stronger, hapakuwa na sababu ya kufanya haya, hasa ikizingatiwa kwamba chadema ilikuwa inakata mbuga kwa kasi ya ajabu kuliko kipindi chochote katika historia ya chama hiki; Kwa mtazamo wako, je:

*Kulikuwa na haja kweli ya wahusika kuvuruga kasi hii katika kipindi ambacho taifa lilikuwa linashukuru ujio wa upinzani wa kweli kwa CCM ambapo CCM ilianza kujirudi na kuanza kujali tena hali duni za wananchi japo kwa mwendo wa konokono?

Ni dhahiri kwamba uongozi wa sasa wa chadema (taifa) una mapungufu mengi kama ilivyo kwa ccm na kwingine. Lakini, viongozi waliopo madarakani chadema leo (taifa) wanahusika moja kwa moja na mafanikio ambayo chadema na wanachama wake wanajivunia leo; Kwa mfano, viti bungeni vimeongezeka, wabunge wamekomaa zaidi kisiasa na kuipa serikali ya ccm changamoto zinazostahili kuletwa na upinzani, lakini muhimu ni kwamba chini ya uongozi huo, leo hii chaguzi za ubunge sehemu yoyote bara odds za ushindi ni karibia 50/50 na CCM; mkuu Zakumi, shukrani kwa haya ndio iwe "a coup" kwa hoja kwamba uochama chao (chadema) kinaelekea in the wrong direction na kwamba kipo in the wrong hands?what's a better direction for chadema leo kuliko direction ya sasa? Na kama tatizo ni leadership, je kuna kipindi chochote ambacho chadema wauonaweza kujisifia kwa mafanikio ya kiuongozi kuliko kipindi cha sasa?

Mkuu Zakumi, waraka husika una mapungufu sana, sio tu on context and intent, bali hata substance/content, kwani kulikuwa na njia mbadala za kufanikisha malengo husika ambayo isingejumuisha ujenzi wa makundi, chuki, fitina, uchochezi, na mengine mengi yanayohujumu demokrasia. Binafsi sioni cha maana mle zaidi ya mambo makuu matatu:

*Elitism ambapo kuna kila dalili kwamba wahusika wanataka kuweka chama mikononi mwa wasomi, not necessarily mikononi mwa wananchi, hasa vijana ambao ndio mtaji mkuu wa chama;
*Chauvism - wahusika kutaka anzisha utamadumi wa prejudiced belief kwamba wao ndio wana superiority in terms of knowledge, intellect etc;
*Nepotism - kwa kuja na mikakati ya wazi ya kuweka relatives or close friends in power;

Katika yote haya, hakuna lenye manufaa kwa demokrasia na maendeleo ya chama wala taifa, badala yake ni hujuma kwa the aforementioned. Mkuu Zakumi, katika hili, sioni any relevance na wewe kuwa "a libertarian" kama unavyodai, badala yake naona you are "a fanatic" - kwani its clear that you are motivated by irrational enthusiasm;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi;

Tatizo lako unataka chama cha upinzani kilicho-strong ambacho kitaifanya CCM kiwe chama cha kuwajibika. Una ndoto za mfumo wa vyama viwili kama ule wa Marekani. Na unaona kuwa CDM na CCM zina nafasi ya kufanya hivyo.

Ukweli wa mambo kuwa na vyama vya kisiasa sio msingi wa demokrasia. Ni misingi mizuri ya demokrasia ndio inayofanya vyama vya kisiasa viwepo na vifanikiwe. Swali je Tanzania ina misingi mizuri ya demokrasia? Jibu hapana.

Matatizo yote ya CCM na CDM, chanzo chake ni katiba ya nchi. Na suala la watu kujiunga na CDM kwa wingi ni ukosefu wa alternative ya ku-vent. Katiba inawanyima haki hiyo. Hivyo wanaingia CDM kwa sababu CCM imeshindwa kuwasaidia.

Vilevile unapotaka kuwa agents of change, ni lazima wewe mwenyewe uwe umebadilika. CDM wanamatatizo yao. Kwanza wajisafishe. Migogoro, fitna ni sehemu ya maisha ya jumuia.

Kuhusiana na mimi kuwa a libertarian, hiyo ni kweli. Na kwa imani yangu sitakiwi kumpeleleza mtu au kutumia vyanzo vya kijasusi kama facts. Hivyo ningekuwa kama kiongozi wa CDM, nisingekubali kupokea waraka na kuutumia kama facts. Kupokea na kusikiliza maneno ya pembeni hata kama yako kwenye waraka ni chanzo kikubwa cha fitna.
 
Mkuu Zakumi nadhani umemsoma Mchambuzi vema hapo juu.

Huu waraka ulikuwa nje ya private domain ulipokamatwa. Mkakati ulishaanza, mtamamko ya mkoa mmoja mara 3 na watu tofauti ni dalili wapo waLiokereka mpango kufyatuka, wapo wasiojua na wapo walioko upande mwingine.

Wakati waraka unakamatwa Mwigamba alikuwa ndani ya kikao akiwasiliana na watu wake.
Kitendo cha Lema kuingia na kwenda kumnyang'anya lap top ni ushahidi kuwa ujasusi ulikuwa unaendelea kwa upande wa Mwigamba. Sasa sijui hapa mpaka wa private domain na confidential info za chama upo wapi.
Kasome bandikio #92 kwa umakini na tafakari mantiki ya bandiko lile.

Mtu anapojifanya mwana CCM huku akiwa ni CDM kiongozi na kuleta habari za uchochezi huo si ujasusi ni uhuni, uharibifu na upuuzi. Nyuzi zinazoshabihiana na waraka zipo nyingi sana sasa sijui private domain ipo wapi.

Waraka ulilenga kuwaondoa viongozi kwa nguvu. Waraka ulikuwa na malengo mawili.
1. Kushawishi wajumbe waanze harakati za kumtayarisha mtu wanayemtaka ambaye ni Zitto.
Njia hizo ni kutoka mtandao wa kanda na mikoa mara jaribio litakapokamilika.

Walifahamu tatizo la Zitto na haiba yake kupungua kwa umaarufu kutokana na weakness ambazo waraka umezionyesha, itakuwa vngumu kuweza kuchaguliwa haraka mapinduzi yakikamilika.

2. Jaribio lilipangwa kwa njia hizi
a) Zitto arushe kombora la fedha kwa kutumia kofia ya PAC ili CAG na Msajili waingilie kati.
Alifahamu wazo litaungwa mkono na CCM kwavile litakuwa linaimaliza CDM na CCM walifanya ushabiki.

Wakati wa crisis wazo la viongozi kujiuzulu lingetolewa na baada ya hapo mrithi kutafutwa.
Ndipo hoja namba 1 itakapokuwa na nguvu.

Jaribio hilo linafuatia kushindwa kwa jaribio la Kafulila ambalo lilikuwa vijana kupata nafasi zaidi likimlenga Zitto.
Jaribio lilibeba hoja ya ukanda na lililenga kuleta mtafaruku ili Zitto awe mmoja wa viongozi wa juu.
Ni jaribio hilo limemwezesha Zitto kuwa naibu katibu mkuu hata pale anapofanya maasi.

Jaribio la Kafulila limeacha makovu ndani ya CDM. Leo kanda ya mwanza na kila mahali wanadai ukanda umetwala baaada ya hoja ya uchaga kuoenekana haina mashiko. Hizi ni mbegu alizopanda Zitto na sasa zinachanua vema.

Jaribio la Juliana Shonzo na Masalia liliungwa mkono na Zitto na Kitila likilenga kumuondoa mwenyekiti BAVICHA ili Juliana aliepenyezwa katika nafasi ya umakamu wachukue ukanda kwa masilahi mapana ya Zitto na Kitila.
Nalo lilishindwa baada ya watu 'kujitoa mhanga'

Jaribio kwa mujibu wa waraka lilikuwa liwe na makada 30 kama ilivyokuwa huko nyuma.
Waraka ukasema safari hii iwe siri kubwa na watafutwe watu waaminifu katika mikoa.
Mmoja wa watu hao ni Mwigamba na ni ukweli wapo wengi wanaoandika matamko na wengine wameshajiuzulu

Demokrasia
Ni kweli demokrasia haishii kuwa na viongozi ni zaidi ya hapo. Ukisoma waraka hakuna mahali wameeleza wapi demokrasia imeminywa.

Walichosema ni mbowe kung'ng'ania madaraka kwa vipindi viwili hata kama katiba inasema hivyo.
Wanachotaka ni utashi wa Makani na Mtei uwe guideline na si katiba ili tu kufikia ndoto zao.

Demokrasia wanayolalamika ni kuhusu elimu magumashi ya Mbowe na akili ndogo ya Mbowe.
Akili ndogo iliyofanya recruitment na kuwalea akina Zitto.

Akili ndogo ndio imefanya chama kutoka wabunge watatu na kuwa chama rasmi cha upinzani.
Sijui demokrasia gani wanataka maana kama ni akili ndogo hilo halina uhusiano na demokrasia.

Ukisoma utetezi wao hakuna mahali wanaongelea demokrasia na kuminywa kwake, wanachoongelea ni spinning na ghilaba tu.

Nani asiyejua kuwa waraka ulimshauri Zitto alipue bomu kama mwenyekiti wa PAC ili alete mapinduzi ndania ya chama chake na si ukombozi wa mtanzania na kodi yake.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi kuna element za kutaka ku justify uovu kwasababu tu ya kumkinga Zitto.

Mwandishi wa waraka Kitila Mkumbo amekiri ilikuwa ni makosa. Wote waliandika barua za kujiuzulu hata kabla ya kunyooshewa kidole. Watu hawajiulizi endapo Zitto hakuhusika na kuandika waraka kwanini alitaka kujiuzulu?

Malalamiko ya Zitto na Kitila hayakuwahi kuwa tishio kwasababu hawakautoa hadharani.
Hakuna rekodi ya kikao au mkutano ambao wamesema hayo,ushahidi kuwa hawakujiamini na walikuwa na ni ovu sana.

Alichokifanya Zitto ni kutumia nyaraka za chama na ofisi ya serikali kutaka kupanda ngazi kwa njia za kitoto na zisizo na element za usomi.

Huwezi kutupa komkbora kwenye nyumba ya glasi unayoishi mwenyewe.
Huwezi kutoboa mtumbwi unaosafiri nao. Walichotaka wasaliti hawa ni kuporomosha CDM ili kuwaondoa wasiowataka tena kwa jia zisizofuata demoktasia wakiwa chama cha kidemokrasia.

Endapo kuna tatizo la uongozi hilo lisemwe hadharani siyo kwenda kuwachochea akina Juliana Shonzo kuleta mitafaraku.
Leo kampeni zote za kueneza CDM zimekufa kwasababu ya Zitto. Tuwaambie ukweli

Walitakiwa wasimame kidete katika kuhakikisha chaguzi zinakuwa za wazi na kampeni zinakuwepo.
Uwepo wa vikundi hauepukiki lakini vikundi vya maana si hivi vya akina Kitila Mkumbo, Juliana Shonzo ili kumweka Zitto madarakanii. Huyu ndiye amekuwa kinara wa matatizo ndani ya CDM, let me be honest

Wanachama waachwe waamue nani anaongoza chama chao.
Huyo Zitto unayesema ni tishio na mbunifu nakuhakikishia ni mnafiki mkubwa.
Kahongwa na Barrick huo ndio ubunifu!!!

Pengine mada haijaeleweka. Mada ni kujadili waraka uliopo hapo juu.
Na kwabahati nzuri utetezi wao umewekwa.

Kinachoshangaza ni kuona watu hawawezi kabisa kumtetea Zitto na Kitila kwa waraka bali mapenzi tu.
Ndio maana tunaona hoja za mapenzi zaidi kuliko ukweli unaonekana.

Nimeuliza kwanini watu hawachambui waraka uliopo na kuonyesha mikakati ya hawa jamaa?
Mimi nimeonyesha wapi kuna tatizo mstari mmoja hadi mwingine, wenzangu mnaotetea onyesheni nia njema ya waraka mstari hadi mwingine. Hata kama ni 'Mbowe' hana akili onyesheni tutaelewa.

Wao wenyewe wametaka kujiuzulu, maana yake ni kuwa hilo halikuwa sahihi kufuatana na vifungu vilivyowekwa na wanavyovifahamu. Lakini basi kama wangekuwa wakweli wasingeanza kuchafua watu mitandaoni.
Hebu soma kwa undani bandiko#92 hapo juu uone jinsi waraka ulivyokuwa unafanyiwa kazi si hadharani bali mafichoni.

Nguruvi3

Kwa mujibu wa Tundu Lissu pamoja na John Mnyinka, waraka uliosababisha kuvuliwa vyeo vya siyo huo unaouzungumzia wewe huo ni fake wala Chadema hawautambui.

Waraka ambao wanasema ndiyo walioutumia kama ushahidi bado hawajautoa kwenye vyombo vya habari wamesema ikibidi kuutoa watautoa.

Wala hayo hizo tuhuma 11 zinazowakabili kina Zitto na Kitila hakuna anayezijua kama yupo atutajie tuzifahamu.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3

Kwa mujibu wa Tundu Lissu pamoja na John Mnyinka, waraka uliosababisha kuvuliwa vyeo vya siyo huo unaouzungumzia wewe huo ni fake wala Chadema hawautambui.

Waraka ambao wanasema ndiyo walioutumia kama ushahidi bado hawajautoa kwenye vyombo vya habari wamesema ikibidi kuutoa watautoa.

Wala hayo hizo tuhuma 11 zinazowakabili kina Zitto na Kitila hakuna anayezijua kama yupo atutajie tuzifahamu.
Lissu na Zitto katika taarifa zao hawakukanusha kuhusu waraka huu ambao ulisambazwa kabla ya taarifa yao kwa jina la CDM na wao.
Pili, tumewatahadharisha CDM kuwa waraka huo umesambazwa kwa jina lao from the very beginning.
Tunaendelea
 
Kwa mtazamo wangu naona ni udhaifu wa kihoja kudhani watu fulani ni bora sana kwakuwa eti wameifikisha CDM hapa ilipo leo na hawakustahili kuandaliwa waraka kama ule
Hoja kama Mbowe amemlea Zitto, amefanikisha idadi ya wabunge kuongezeka, na kuifanya CDM chama kikuu cha upinzani nk nk hakumaanishi chochote iwapo kuna viti haviendi sawa
Mimi ninaweza kona ilitakiwa CDM wawe wamechuka nchi kitambo lakini wana wabunge kidogo sana, Mbowe alitakiwa kuwa amela akina Zitto kama 1000 hivi lakini yupo mmoja nk nk

Sehemu yoyote kwenye demokrasia upinzani ni swala la zima, makundi ya watu wenye mtazamo mmoja ni lazima, pengine kinacho tushinda sisi ni namna tu ya kufanya kazi pamoja kama chama baada ya chaguzi

Tunaweza kuona madhambi mengi sana ya Zitto kama mkuu Nguruvi3 na Mchambuzi wanavyojaribu kuyadadafua ambayo kimsingi inaonekana ni kama CDM walishindwa kuyathibitisha miaka nenda rudi lakini sasa kwa waraka ule wakaona sasa hapa hapa tummalize

Pamoja na tuhuma za Zitto lakini wakosoaji wa Zitto hawataki kufikiri zaidi kiasi kwamba pia hawataki kuamini CDM kuna ombwe la uongozi
CDM hawataki demokrasia ndani ya chama kwa kisingizio cha "kugawa" chama........Ni ajabu sana
Leo hii hata ukitangaza nitagombea cheo fulani ndani ya chama utaambiwa unakiherere, unaharaka nk nk
Uoga umewajaa viongozi wa CDM kumbuka nguvu kubwa iliyotumika kumlazimisha Zitto atoe jina wakati ule

Binafsi sitaki kuamini waraka ule it worth kuwavua uongozi Zitto na Kitila uongozi, Kitila alipoomba kujiuzulu alijua wenzake hawawezi kuwa na imani naye tena lakini hakusema ilikuwa ni kosa
 
Last edited by a moderator:
.....
CDM hawataki demokrasia ndani ya chama kwa kisingizio cha "kugawa" chama........Ni ajabu sana
Leo hii hata ukitangaza nitagombea cheo fulani ndani ya chama utaambiwa unakiherere, unaharaka nk nk

Uoga umewajaa viongozi wa CDM kumbuka nguvu kubwa iliyotumika kumlazimisha Zitto atoe jina wakati ule

Binafsi sitaki kuamini waraka ule it worth kuwavua uongozi Zitto na Kitila uongozi, Kitila alipoomba kujiuzulu alijua wenzake hawawezi kuwa na imani naye tena lakini hakusema ilikuwa ni kosa

Jamani Paul S.S...mbona na wewe unapotosha umma wa watanzania wanaofuatilia suala hili....!? Ebu soma hapa chini nukuu ya alichokisema Lissu (Mbunge) amabaye ni mwanasheria mkuu wa Chadema. Ninachotaka usome ni hicho nilichokoleza rangi nyeusi.

...........

Alisema mashtaka ya makosa 11, ambayo Zitto na Dk. Kitila wanatuhumiwa kuyatenda hawawezi kuyaweka hadharani, bali watawakabidhi wahusika na kwamba, kama wao wataamua kufanya hivyo hilo litakuwa juu yao.

Hata hivyo, alisema wanaweza kuyaweka hadharani baada ya CC kupokea utetezi kutoka kwa watuhumiwa.

Alisema mwaka 2012, Chadema ilitengeneza mwongozo unaomtaka mwanachama kutangaza kusudio la namna ya kugombea uongozi katika chama na kwamba, walifanya hivyo ili kuzima chokochoko zilizokuwa zimekithiri kuelekea kwenye uchaguzi katika siku za nyuma.

Kwa mujibu wa Lissu, mwongozo huo unataka mwanachama atangaze wazi kusudio lake hilo kwa kupeleka barua kwa Katibu Mkuu na siyo kwa kujificha na kuchafua wengine.

"Kama wangekuwa wanataka mtu wao (awe mwenyekiti wa Chadema) wangetangaza. Maamuzi ya Kamati Kuu ni uthibitisho kwamba hakuna tunayemuogopa,"
alisema Lissu.

Alisema ni kweli suala la PAC lilijadiliwa katika vikao vya CC, lakini halikuwa hoja ya kuwashtaki wahusika.

CHANZO: NIPASHE

=============
 
Back
Top Bottom