Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Kwa mtazamo wangu naona ni udhaifu wa kihoja kudhani watu fulani ni bora sana kwakuwa eti wameifikisha CDM hapa ilipo leo na hawakustahili kuandaliwa waraka kama ule

Hoja kama Mbowe amemlea Zitto, amefanikisha idadi ya wabunge kuongezeka, na kuifanya CDM chama kikuu cha upinzani nk nk hakumaanishi chochote iwapo kuna viti haviendi sawa
Mimi ninaweza kona ilitakiwa CDM wawe wamechuka nchi kitambo lakini wana wabunge kidogo sana, Mbowe alitakiwa kuwa amela akina Zitto kama 1000 hivi lakini yupo mmoja nk nk

Sehemu yoyote kwenye demokrasia upinzani ni swala la zima, makundi ya watu wenye mtazamo mmoja ni lazima, pengine kinacho tushinda sisi ni namna tu ya kufanya kazi pamoja kama chama baada ya chaguzi

Tunaweza kuona madhambi mengi sana ya Zitto kama mkuu Nguruvi3 na Mchambuzi wanavyojaribu kuyadadafua ambayo kimsingi inaonekana ni kama CDM walishindwa kuyathibitisha miaka nenda rudi lakini sasa kwa waraka ule wakaona sasa hapa hapa tummalize

Pamoja na tuhuma za Zitto lakini wakosoaji wa Zitto hawataki kufikiri zaidi kiasi kwamba pia hawataki kuamini CDM kuna ombwe la uongozi
CDM hawataki demokrasia ndani ya chama kwa kisingizio cha "kugawa" chama........Ni ajabu sana
Leo hii hata ukitangaza nitagombea cheo fulani ndani ya chama utaambiwa unakiherere, unaharaka nk nk
Uoga umewajaa viongozi wa CDM kumbuka nguvu kubwa iliyotumika kumlazimisha Zitto atoe jina wakati ule

Binafsi sitaki kuamini waraka ule it worth kuwavua uongozi Zitto na Kitila uongozi, Kitila alipoomba kujiuzulu alijua wenzake hawawezi kuwa na imani naye tena lakini hakusema ilikuwa ni kosa
Ndugu yangu umechukua maneno ukapandikiza ya kwako halafu ukahitimisha kuwa Nguruvi3 kasema.
Tafadhali simama katika ukweli utakuwa huru zaidi.

Waraka umesema uongozi wa sasa hauna lolote la maana ukisifia enzi za watangulizi Makani na Mtei kwa kuacha wabunge 3. Mimi nikasema waraka ungeeleza nani amefikisha CDM kuwa cha upinzani rasmi?
Takwimu zinasemaje kuhusu hilo.
Nilikusudia kuwa takwimu zisitumike nusu nusu, ima ni kamili au hakuna.

Waraka umesema mbowe ana akili ndogo sana na elimu yake ya magumashi.
Nimeuliza hivi huyu si ndiye alifanya recruitment ya Zitto na Kumlea hadi alipo? Akili ndogo imeweza kutoa 'shujaa' ambaye anatetewa hata kama ametenda ouvu.Nimeuliza tu akili ndogo haijafanya hivyo?

Hao vijana 1000 unaosema, pengine wapo zaidi, tatizo ni kuwa hawaoni kama wapo kwasababu wamefunikwa katika kivuli .

Ndio maana tunasema kama kuna kivuli kwanini kiweke giza chini ya mwamvuli tukijua kuna 1000 wanasubiri fursa hiyo?

Watu wanosema kuna ombwe la uongozi nakubaliana nao kwa hoja, lakini basi onyesheni wapi omwe lilipo. Hakuna ombwe la kujenga hoja za kumtetea mtu . Elezeni ombwe lipo wapi.

Nilishawahi kueleza tena kwa kina kuhusu ombwe bila kusukumwa na Zittoism, sasa ninyi mnaojenga ngao kwa Zitto onyesheni wapi ombwe lilipo na je namna ya kuziba ombwe ni njia haram, za kitoto za waraka.

Tulidhani Zitto angetangaza ili tuone hiyo demokrasia ya CDM inafanya kazi vipi.
Hakuwahi, alichokifanya ni kutumia mitandao na vijana kuchafua wenzake, je huko ndiko kutangaza nia?

Na mwisho hutaki kuamini waraka una makosa, au hutaki kuamini zitto kuvuliwa madaraka kufuatia waraka?




 
Ndugu yangu umechukua maneno ukapandikiza ya kwako halafu ukahitimisha kuwa Nguruvi3 kasema.
Tafadhali simama katika ukweli utakuwa huru zaidi.

Waraka umesema uongozi wa sasa hauna lolote la maana ukisifia enzi za watangulizi Makani na Mtei kwa kuacha wabunge 3. Mimi nikasema waraka ungeeleza nani amefikisha CDM kuwa cha upinzani rasmi?
Takwimu zinasemaje kuhusu hilo.
Nilikusudia kuwa takwimu zisitumike nusu nusu, ima ni kamili au hakuna.

Waraka umesema mbowe ana akili ndogo sana na elimu yake ya magumashi.
Nimeuliza hivi huyu si ndiye alifanya recruitment ya Zitto na Kumlea hadi alipo? Akili ndogo imeweza kutoa 'shujaa' ambaye anatetewa hata kama ametenda ouvu.Nimeuliza tu akili ndogo haijafanya hivyo?


Mkuu bandiko lako #92 ndilo nililo likusudia, sasa kama hukuwa unajaribu kuonyesha ubaya wa Zitto kama nilivyoeleza kwenye bandiko langu basi sijui ni kwa namna gani bandiko hilo lilikuwa linamsifia.

Swala la waraka na lugha iliotumika, hivi vitu havikuwa for public consumption jamani, NI HAKI YANGU KUGOMBEA HATA KAMA UONGOZI ULIOPO UNAFANYA VIZURI KIASI GANI.
Hata ujibu kwa umahiri gani neno kwa neno katika waraka ule hakumuondelei muhusika haki yake ya kujipanga kwa mapambano ya uchaguzi

Waraka ule ni waandaji waliamu kujaribu kuangalia udhaifu uliopo na ndio hapo niliposema hata awali kwamba wao kusema uongozi uliopo haujafanya lolote ni haki yao, inawezekana kwao wao CDM ilitakiwa iwe na wabunge zaidi ya mia wa kuchaguliwa lakini wapo wachache mmno

Tatizo lako wewe Nguruvi3 na wenzako wengi ni kuanza kuuchambua waraka as ulikusudiwa kwa watu wote kuusoma na kuujadili........kufanya hivyo utaishia kutoa hoja ambazo hazipo
Waraka ule ulikuwa kwa watu wa nne tu the rest ilikuwa ni utekelezaji
Hapa arguments zako zinatakiwa kuwa based na chama kitaathika vipi wakati wa utekelezaji wa mkakati huo? na si kuanza kujadili eti kwanini hawajafanyi hivi na vile wakati wao ni viongozi pia


Watu wanosema kuna ombwe la uongozi nakubaliana nao kwa hoja, lakini basi onyesheni wapi omwe lilipo. Hakuna ombwe la kujenga hoja za kumtetea mtu . Elezeni ombwe lipo wapi.

Nilishawahi kueleza tena kwa kina kuhusu ombwe bila kusukumwa na Zittoism, sasa ninyi mnaojenga ngao kwa Zitto onyesheni wapi ombwe lilipo na je namna ya kuziba ombwe ni njia haram, za kitoto za waraka.

Tulidhani Zitto angetangaza ili tuone hiyo demokrasia ya CDM inafanya kazi vipi.
Hakuwahi, alichokifanya ni kutumia mitandao na vijana kuchafua wenzake, je huko ndiko kutangaza nia?
Na mwisho hutaki kuamini waraka una makosa, au hutaki kuamini zitto kuvuliwa madaraka.
Natumia simu, nikitulia nitakuandia na kuquote ombwe la uongozi la CDM kwa ufasaha kabisa
Zitto mwaka huu sikumbuki lini alitangaza atagombea urais.........ilikuwa agenda ndani ya CDM hadi mzee Mtei akaunguruma toka Tengeru kumlaani Zitto achilia mbali Mbowe aliyesiliba kabisa kwamba kwa sasa hakuna kama Dr Slaa ikawa mwisho wa mjadala
Binadamu ana namna nyingi za kifikia malengo na makusudio yake, kuita njia ya waraka ni ya kitoto its ok ni mawazo yako mkuu lakini kama una weledi wa kutosha mikakati ni swala la lazima kwenye chaguzi, wengi wanaweza kujadili wasiandike popote wengine wana weza kuandika walichojadili..........sasa kama utoto ni kuandika mimi sijui

Kuhusu hilo la kuchafuana mitandaoni wala usiliseme kabisa mkuu, uongozi wa CDM umetumia pia njia haramu za kumchafua Zitto mitandaoni kwa kuwatumia akina Ben Saanane and the co
Tumeona akina Lema wakifunguka bila hiyana kwa kiongozi wake nk nk

Mwisho mkuu mimi sio kama siamini Zitto amevuliwa uongozi...hasha
Mimi siamini kama Waraka ndio sababu ya kumvua Zitto uongozi, sababu zipo na baadhi umezitaja mwenye kwenye bandiko lako #92
Ni upuuzi kwangu mimi eti Tundu lissu anasema kuna utaratibu ukitaka kugombea unaandika barua kwa KM kueleza kusudio lako............Hizi ndio demokrasia za woga na zilikuja baada ya kupata tabu kumshawishi Zitto atoe jina wakaona sasa piga pini
 
Last edited by a moderator:
Jamani Paul S.S...mbona na wewe unapotosha umma wa watanzania wanaofuatilia suala hili....!? Ebu soma hapa chini nukuu ya alichokisema Lissu (Mbunge) amabaye ni mwanasheria mkuu wa Chadema. Ninachotaka usome ni hicho nilichokoleza rangi nyeusi.

Mkuu hizo ndio hila zenyewe sasa. unategemea nini hapo?
Na sijui sasa hilo sharti ni kwa nafasi ya Uenyekiti wa CDM tu au la
 
Mkuu bandiko lako [URL=https://www.jamiiforums.com/usertag.php?do=list&action=hash&hash=92]#92 [/URL] ndilo nililo likusudia, sasa kama hukuwa unajaribu kuonyesha ubaya wa Zitto kama nilivyoeleza kwenye bandiko langu basi sijui ni kwa namna gani bandiko hilo lilikuwa linamsifia.

Swala la waraka na lugha iliotumika, hivi vitu havikuwa for public consumption jamani, NI HAKI YANGU KUGOMBEA HATA KAMA UONGOZI ULIOPO UNAFANYA VIZURI KIASI GANI.
Hata ujibu kwa umahiri gani neno kwa neno katika waraka ule hakumuondelei muhusika haki yake ya kujipanga kwa mapambano ya uchaguzi

Waraka ule ni waandaji waliamu kujaribu kuangalia udhaifu uliopo na ndio hapo niliposema hata awali kwamba wao kusema uongozi uliopo haujafanya lolote ni haki yao, inawezekana kwao wao CDM ilitakiwa iwe na wabunge zaidi ya mia wa kuchaguliwa lakini wapo wachache mmno

Tatizo lako wewe Nguruvi3 na wenzako wengi ni kuanza kuuchambua waraka as ulikusudiwa kwa watu wote kuusoma na kuujadili........kufanya hivyo utaishia kutoa hoja ambazo hazipo
Waraka ule ulikuwa kwa watu wa nne tu the rest ilikuwa ni utekelezaji
Hapa arguments zako zinatakiwa kuwa based na chama kitaathika vipi wakati wa utekelezaji wa mkakati huo? na si kuanza kujadili eti kwanini hawajafanyi hivi na vile wakati wao ni viongozi pia


Natumia simu, nikitulia nitakuandia na kuquote ombwe la uongozi la CDM kwa ufasaha kabisa
Zitto mwaka huu sikumbuki lini alitangaza atagombea urais.........ilikuwa agenda ndani ya CDM hadi mzee Mtei akaunguruma toka Tengeru kumlaani Zitto achilia mbali Mbowe aliyesiliba kabisa kwamba kwa sasa hakuna kama Dr Slaa ikawa mwisho wa mjadala

Binadamu ana namna nyingi za kifikia malengo na makusudio yake, kuita njia ya waraka ni ya kitoto its ok ni mawazo yako mkuu lakini kama una weledi wa kutosha mikakati ni swala la lazima kwenye chaguzi, wengi wanaweza kujadili wasiandike popote wengine wana weza kuandika walichojadili..........sasa kama utoto ni kuandika mimi sijui

Kuhusu hilo la kuchafuana mitandaoni wala usiliseme kabisa mkuu, uongozi wa CDM umetumia pia njia haramu za kumchafua Zitto mitandaoni kwa kuwatumia akina Ben Saanane and the co
Tumeona akina Lema wakifunguka bila hiyana kwa kiongozi wake nk nk

Mwisho mkuu mimi sio kama siamini Zitto amevuliwa uongozi...hasha
Mimi siamini kama Waraka ndio sababu ya kumvua Zitto uongozi, sababu zipo na baadhi umezitaja mwenye kwenye bandiko lako [URL=https://www.jamiiforums.com/usertag.php?do=list&action=hash&hash=92]#92 [/URL]
Ni upuuzi kwangu mimi eti Tundu lissu anasema kuna utaratibu ukitaka kugombea unaandika barua kwa KM kueleza kusudio lako............Hizi ndio demokrasia za woga na zilikuja baada ya kupata tabu kumshawishi Zitto atoe jina wakaona sasa piga pini
Ndugu yangu, tafadhali sana rudi katika bandiko #92 ulisome kwa utulivu sana halafu uone kilichokusudiwa.

FYI nimeweka bandiko lile kuonyesha yafuatayo

  1. Si kweli kuwa Zitto hajashiriki kutekeleza mkakati. Waraka umeonyesha njia zitakazotumika na ambazo zimetumika katika kuutekeleza. Nimeuliza swali waraka uliandikwa lini?
Kama hatujui basi rejea bandiko 92 uone maudhui ya waraka na yale ya mtandaoni. Utaona ya kuwa waraka huo
ulishaanza kufanyiwa kazi siku nyingi

2. Bandiko hilo linaonyesha kuwa kuna uchonganishi. Inakuwaje mtu wa CCM aandike mambo ya CDM neno kwa neno.
Mtu huyu ni CCM au ni CDM anayetumika au anayetumia jina la CCM kufikia malengo yake?

Kuhusu tuhuma dhidi ya uongozi, hilo sina tatizo nalo. Wanaweza kusema lolote likawa sawa kutokana na mtizamo wao. Nisichokubaliana nao ni kutoa data za upotoshaji hasa kwa baadhi yetu tusio na uelewa ili kufikia malengo.
Kiongozi haongozi kwa ghilba anaongoza kwa ukweli.

  1. Wamesema Mtei na Makani waliongoza kwa kipindi kimoja na Mbowe ana ng'ang'ania madaraka. Si kweli katiba inasema vipindi viwili. Kama yupo atakayetumia miezi 12 au 18 au 19 hiyo siyo standard ni utashi wake. Sasa wanapotosha ili umma uone kuna ubinyaji wa demokrasia wakati wao hawahubiri demokrasia bali wanachomeka idea zako ili kufikia malengo maovu
  2. Waraka unasema huko nyuma CDM ilifanya vizuri kwa kuongeza viongozi hadi kufikia wawakilishi watatu bungeni. Hawakuendelea kusema sasa wapo wangapi. Kipimo cha ubaya ni uzuri na kipimo cha uzuri ni ubaya. Je ni kwanini hawakusema sasa wapo wabunge wangapi chini ya uongozi huu.
Kama kulikuwa na uongozi 1,2 huu wa 3 kwanini hausomewi hukumu yake


Kuhusu waraka kuwa private, unataka kuhalalisha kuwa maudhui ya waraka ule yalikuwa sahihi.
Hawa ni viongozi wasiotakiwa kusema jambo moja jukwaani na kulirudia kwa namna nyingine nyuma ya pazia.

Mfano, akina Zitto wamekuwa wanatumia muda kueleza kuwa CDM si chama cha ukanda na udini.
Nyuma ya pazia(waraka)wameonyesha kutumia nyenzo hizo ili kufikia madaraka wanayotamani.

Ili kupata utetezi rahisi sana leo tunaambiwa waraka haukukusudia public hata kama tunajua ulikuwa kinyume na wanachosema, kinyume na maadili ya taifa na kinyume cha maadili ya uongozi.

Kutangaza na kuandika barua si jambo geni. Zitto akiwa katibu mkuu mtendaji aliridhia suala hilo kisheria. Kitila akiwa mshauri wa chama aliridhia suala hilo.
Wote walikuwa wanaingia katika vikao muhimu na hakuna rekodi kuwa waliwahi kulipinga.

Wanapolipinga uani ni kwenda kinyume cha maadili. Wanafanya maamuzi ambayo hawaridhiki nayo na kisha kurudi uani kutoa lawama kana kwamba walikuwa wageni na hawakujua chochote. Unafiki.

Waraka ni wa kitoto! Nasema ni wa kitoto sana. Huwezi kuandika mipango kwa njia za mipasho.
Hatuwezi kutofautisha maneno ya kwenye khanga za akina mama na baadhi ya maneno ya waraka.

Mfano, elimu yake ni magumashi, wana akili za kitoto, Zitto afanye mambo ya mapenzi kwa siri, uongozi unaonekana kama wahuni kwa kudhalilisha akina mama n.k.
Umepotosha kwa kusema Zitto mlengwa hana makundi wakati anachokifanya ni makundi wakati anaposema hivyo.

Hata hivyo historia inamhukumu Zitto kama mtu wa makundi kuliko kiongozi yoyote ndani ya CDM.
Amehusika sana na vurugu labda hilo nalo halikukusudiwa katika ‘public domain'

Umesema nifanye argument chama kitaathirika vipi kwa mkakati!
Nimeshasema huko nyuma lakini nirudie kwa kusema hakuna kinachoendelea CDM sasa hivi bali mtafaruku mkubwa.

Political base ipo confused and demoralized na kuna paralysis kubwa sana katika uendeshaji wa CDM
Sijui kama hilo hulioni ni tatizo. Na jiulize hao wanachama mamilioni wa CDM wanajisikiaje wakiona kikundi cha watu wawili watatu kinaleta mtafaruku huu

Jiulize hali ya kambi ya upinzani ambayo ni sehemu ya umma inayotambuliwa kisheria ipoje.
 
Mkuu Zakumi nadhani umemsoma Mchambuzi vema hapo juu.

Huu waraka ulikuwa nje ya private domain ulipokamatwa. Mkakati ulishaanza, mtamamko ya mkoa mmoja mara 3 na watu tofauti ni dalili wapo waLiokereka mpango kufyatuka, wapo wasiojua na wapo walioko upande mwingine.

Wakati waraka unakamatwa Mwigamba alikuwa ndani ya kikao akiwasiliana na watu wake.
Kitendo cha Lema kuingia na kwenda kumnyang'anya lap top ni ushahidi kuwa ujasusi ulikuwa unaendelea kwa upande wa Mwigamba. Sasa sijui hapa mpaka wa private domain na confidential info za chama upo wapi.
Kasome bandikio #92 kwa umakini na tafakari mantiki ya bandiko lile.

Mtu anapojifanya mwana CCM huku akiwa ni CDM kiongozi na kuleta habari za uchochezi huo si ujasusi ni uhuni, uharibifu na upuuzi. Nyuzi zinazoshabihiana na waraka zipo nyingi sana sasa sijui private domain ipo wapi.

Waraka ulilenga kuwaondoa viongozi kwa nguvu. Waraka ulikuwa na malengo mawili.
1. Kushawishi wajumbe waanze harakati za kumtayarisha mtu wanayemtaka ambaye ni Zitto.
Njia hizo ni kutoka mtandao wa kanda na mikoa mara jaribio litakapokamilika.

Walifahamu tatizo la Zitto na haiba yake kupungua kwa umaarufu kutokana na weakness ambazo waraka umezionyesha, itakuwa vngumu kuweza kuchaguliwa haraka mapinduzi yakikamilika.

2. Jaribio lilipangwa kwa njia hizi
a) Zitto arushe kombora la fedha kwa kutumia kofia ya PAC ili CAG na Msajili waingilie kati.
Alifahamu wazo litaungwa mkono na CCM kwavile litakuwa linaimaliza CDM na CCM walifanya ushabiki.

Wakati wa crisis wazo la viongozi kujiuzulu lingetolewa na baada ya hapo mrithi kutafutwa.
Ndipo hoja namba 1 itakapokuwa na nguvu.

Jaribio hilo linafuatia kushindwa kwa jaribio la Kafulila ambalo lilikuwa vijana kupata nafasi zaidi likimlenga Zitto.
Jaribio lilibeba hoja ya ukanda na lililenga kuleta mtafaruku ili Zitto awe mmoja wa viongozi wa juu.
Ni jaribio hilo limemwezesha Zitto kuwa naibu katibu mkuu hata pale anapofanya maasi.

Jaribio la Kafulila limeacha makovu ndani ya CDM. Leo kanda ya mwanza na kila mahali wanadai ukanda umetwala baaada ya hoja ya uchaga kuoenekana haina mashiko. Hizi ni mbegu alizopanda Zitto na sasa zinachanua vema.

Jaribio la Juliana Shonzo na Masalia liliungwa mkono na Zitto na Kitila likilenga kumuondoa mwenyekiti BAVICHA ili Juliana aliepenyezwa katika nafasi ya umakamu wachukue ukanda kwa masilahi mapana ya Zitto na Kitila.
Nalo lilishindwa baada ya watu 'kujitoa mhanga'

Jaribio kwa mujibu wa waraka lilikuwa liwe na makada 30 kama ilivyokuwa huko nyuma.
Waraka ukasema safari hii iwe siri kubwa na watafutwe watu waaminifu katika mikoa.
Mmoja wa watu hao ni Mwigamba na ni ukweli wapo wengi wanaoandika matamko na wengine wameshajiuzulu

Demokrasia
Ni kweli demokrasia haishii kuwa na viongozi ni zaidi ya hapo. Ukisoma waraka hakuna mahali wameeleza wapi demokrasia imeminywa.

Walichosema ni mbowe kung'ng'ania madaraka kwa vipindi viwili hata kama katiba inasema hivyo.
Wanachotaka ni utashi wa Makani na Mtei uwe guideline na si katiba ili tu kufikia ndoto zao.

Demokrasia wanayolalamika ni kuhusu elimu magumashi ya Mbowe na akili ndogo ya Mbowe.
Akili ndogo iliyofanya recruitment na kuwalea akina Zitto.

Akili ndogo ndio imefanya chama kutoka wabunge watatu na kuwa chama rasmi cha upinzani.
Sijui demokrasia gani wanataka maana kama ni akili ndogo hilo halina uhusiano na demokrasia.

Ukisoma utetezi wao hakuna mahali wanaongelea demokrasia na kuminywa kwake, wanachoongelea ni spinning na ghilaba tu.

Nani asiyejua kuwa waraka ulimshauri Zitto alipue bomu kama mwenyekiti wa PAC ili alete mapinduzi ndania ya chama chake na si ukombozi wa mtanzania na kodi yake.

Nguruv3;

Kwenye siasa mambo yote ni timing tu. Ongezeko la wabunge wa CDM haitokani na kazi za Mbowe. Inatokana na matatizo ya uongozi ndani ya CCM katika kipindi cha 2005-2010. Uchaguzi wa 2010 ilikuwa ni Taharir Square ya watanzania kutoridhishwa na uongozi wa CCM.

Hivyo kwa kiasi kikubwa ongezeko la wabunge uliofanya CDM kuwa chama cha upinzani rasmi hautokani na umahiri wa uongozi kama unavyotaka kusema. Kama ni umahiri kwanini hawakufanya vizuri toka 1992? NCCR ilipopoteza umaarufu kwanini watu wasiende CDM?

Kwanini vijana wengi waliopigia kura Kikwete 2005 walibadili nia zao 2010? Haya ni maswali ya kujiuliza. Chama kinaweza kupigiwa kura kwa wingi kwa sababu watu wamekosa imani na chama tawala.

Kuhusiana na waraka, inaonyesha kabisa kuna moto ndani ya CDM. Haiwezekani Lema na Zitto walumbane kuhusu posho za wabunge hapa JF na baada ya wiki au wiki mbili waraka ukamatwe. Haiwezekani mtu aonyeshe ushujaa wa kutoa picha za kulawiti na huyohuyo akamate laptop yenye waraka. Ukuwaji wa Chama na Demokrasia hazipatikani kwa public stunts.
 
MKuu Nguruvi3 umefafanua vizuri sana,

Waraka huu una sehemu mbili kuu;
i) Matatizo/Mapungufu ndani ya uongozi wa CDM
ii) Kukabiliana na mapungufu hayo

Hili la kwanza wote tunakubaliana kuwa kuna madhaifu kadhaa ya uongozi ndani ya chama. Lakini pia katika hili Zitto naye ni sehemu ya uongozi na hawezi kukwepa sehemu ya mzigo wa uwajibikaji katika madhaifu hayo. Kwa muda mrefu amekuwa akijitahidi kujipambanua kuwa tofauti na viongozi wenzake kimsimamo kwenye maeneo mbali mbali lakini mwisho wa siku yeye bado ni sehemu ya uongozi wa chama na historia haitaacha kumhukumu.

Suala la pili ndio la utata zaidi sababu waheshimiwa hawa hawajaweza kuonyesha ni kwa kiasi gani wametumia njia za kawaida kuwasilisha mawazo yao na hawakusililizwa. Wangeweza hata kujiuzulu nyadhifa zao kama alama ya kupinga mambo yanavyoendelea wangeweza kujijengea heshima zaidi. Matokeo yake wamechagua njia ambazo leo hii zinatafsiriwa kuwa sawa na uhaini...
 
Last edited by a moderator:
MKuu Nguruvi3 umefafanua vizuri sana,

Waraka huu una sehemu mbili kuu;
i) Matatizo/Mapungufu ndani ya uongozi wa CDM
ii) Kukabiliana na mapungufu hayo

Hili la kwanza wote tunakubaliana kuwa kuna madhaifu kadhaa ya uongozi ndani ya chama. Lakini pia katika hili Zitto naye ni sehemu ya uongozi na hawezi kukwepa sehemu ya mzigo wa uwajibikaji katika madhaifu hayo. Kwa muda mrefu amekuwa akijitahidi kujipambanua kuwa tofauti na viongozi wenzake kimsimamo kwenye maeneo mbali mbali lakini mwisho wa siku yeye bado ni sehemu ya uongozi wa chama na historia haitaacha kumhukumu.

Suala la pili ndio la utata zaidi sababu waheshimiwa hawa hawajaweza kuonyesha ni kwa kiasi gani wametumia njia za kawaida kuwasilisha mawazo yao na hawakusililizwa. Wangeweza hata kujiuzulu nyadhifa zao kama alama ya kupinga mambo yanavyoendelea wangeweza kujijengea heshima zaidi. Matokeo yake wamechagua njia ambazo leo hii zinatafsiriwa kuwa sawa na uhaini...

Mwalimu ahasante sana. Masuala yote mawili yanakwenda pamoja.
Endapo hawakuridhishwa na mwenendo walipaswa kujiuzulu nafasi zao ili wasiwe sehemu ya uongozi. Hilo lingewapa nafasi ya kusema kile ambacho hawakisemi hadharani.

Ni kweli hakuna rekodi yoyote ya jaribio la kusema hadharani. Walichokifanya ni kuwatumia akina Mwigamba ili kupata habari wakiwa viongozi wa uongozi ule ule wanaoulalamikia.

Walichokifanya ni kujificha katika mazulia ya uongozi uliopo wakikataa uchafu uliopo katika zulia walilolalia.
Aina hii ya viongozi hawafai, hawafai kuaminiwa leo,kesho na muda wote wa maisha yao kisiasa.
 
Last edited by a moderator:
Nguruv3;

Kwenye siasa mambo yote ni timing tu. Ongezeko la wabunge wa CDM haitokani na kazi za Mbowe. Inatokana na matatizo ya uongozi ndani ya CCM katika kipindi cha 2005-2010. Uchaguzi wa 2010 ilikuwa ni Taharir Square ya watanzania kutoridhishwa na uongozi wa CCM.

Hivyo kwa kiasi kikubwa ongezeko la wabunge uliofanya CDM kuwa chama cha upinzani rasmi hautokani na umahiri wa uongozi kama unavyotaka kusema. Kama ni umahiri kwanini hawakufanya vizuri toka 1992? NCCR ilipopoteza umaarufu kwanini watu wasiende CDM?

Kwanini vijana wengi waliopigia kura Kikwete 2005 walibadili nia zao 2010? Haya ni maswali ya kujiuliza. Chama kinaweza kupigiwa kura kwa wingi kwa sababu watu wamekosa imani na chama tawala.

Kuhusiana na waraka, inaonyesha kabisa kuna moto ndani ya CDM. Haiwezekani Lema na Zitto walumbane kuhusu posho za wabunge hapa JF na baada ya wiki au wiki mbili waraka ukamatwe. Haiwezekani mtu aonyeshe ushujaa wa kutoa picha za kulawiti na huyohuyo akamate laptop yenye waraka. Ukuwaji wa Chama na Demokrasia hazipatikani kwa public stunts.
Zakumi naomba watu waelewe hoja yangu. Mimi sijasema Mbowe amefanikisha upatikanaji wa wabunge wengi. Nilichosema ni kuwa waraka unatoa credit kwa Mtei na Makani kuitoa CDM point A to B halafu unaishia hapo.
Ninauliza Mbowe katoa point B-C mbona haionekani katika waraka? Je, hapo kuna anlysis kweli.
Kibaya zaidi waraka umeendelea kumsomea Mbowe hukumu ya madhaifu yake katika chaguzi ndogo. Narudi kusema inakuwaje waangalie chaguzi ndogo waache kubwa?

My point is, hakuna kuchagua data katika analysis. Kinachotakiwa zinawakilishwa kama zilivyo au haziwakilishwi kabisa.
Kinyume cha hivyo ni double standard na bias isiyo na kifani na inapelekea sisi tunaozungumza tukiwa huru tusema kwa uhakika kabisa huu ni utoto uliojengwa katika misingi ya Unafiki. Nafahamu Zittoism au Mbowelism hufumba macho mimi nimeshindwa kwasababu roho inanisumanga kama nitaidhalilisha akili ayngu kwa mahaba.
Mhaba yangu ni kwa demokrasia ya kweli na Tanzania imara.

Kuhusu Lema kwanza niseme rekodi ipo wazi mimi kukemea malumbano yasiyo na tija.
Unajua, kilichokuwa kinaendelea kilikuwa kinajulikana. Bandiko namba 92 nimeliweka makusudi naomba urudi na kuangalia nyuzi za nyuma. Dr Slaa amekuwa katika malumbano na huyo bwana kana kwamba ni watu wanafahamiana.

Mawasiliano ya team Zitto yalikuwa yanafahamika kilichokuwa kinasubiriwa ni timing ya kukamata ushahidi. Leo ungewezaje kusema Zitto ni mshiriki kama huna uthibitisho? Ndivyo alivyoruka viunzi vya Kafulila, na Juliana Shonzo.
Unakumbuka alimkana Ben Saanane kwamba hawajuani kabisa, na umma uliamini kwasababu hakuna ushahidi.
This time around amenasa pabaya ndipo wakamfyatua.

Alichokuwa anafanya Lema ilikuwa ni hasira kwa kukosa busara. Tena Mwigamba angekuwa makini asingewafikisha wenzake hapo walipo. Kulikuwa na kila dalili kuwa mawasiliano yao yalikuwa yananaswa.
Sasa swali la kuwa Lema alifanya vema kuhusu malumbano, absolutely no! Mwigamba alifanya vema kuhusu ujasusi wa kutoa habari 'live' kautoka kwenye vikao kwenda kwa masters yeye akiwa mtumwa, absolutely pathetic and immoral
 
Shida ninayoiona ndani ya CDM kwa muda mrefu ni kwa baadhi ya viongozi wake kutumia muda mwingi kujijenga wao zaidi kisiasa binafsi badala ya kufanya kazi pamoja kama team wakiwa na vision ya kuchukua nchi 2015. Mafanikio yaliofikiwa ni makubwa lakini bado the ultimate goal haijafikiwa hivyo wanapaswa kuimarisha team na sio kila mchezaji kutaka kucheza kivyake. Hii imekuwa na athari kubwa sana kwa chama kupoteza mwelekeo na wasipokuwa makini inaweza kuwagharimu zaidi huko mbele.
 
Kuhusu tuhuma dhidi ya uongozi, hilo sina tatizo nalo. Wanaweza kusema lolote likawa sawa kutokana na mtizamo wao. Nisichokubaliana nao ni kutoa data za upotoshaji hasa kwa baadhi yetu tusio na uelewa ili kufikia malengo.
Kiongozi haongozi kwa ghilba anaongoza kwa ukweli.

  1. Wamesema Mtei na Makani waliongoza kwa kipindi kimoja na Mbowe ana ng'ang'ania madaraka. Si kweli katiba inasema vipindi viwili. Kama yupo atakayetumia miezi 12 au 18 au 19 hiyo siyo standard ni utashi wake. Sasa wanapotosha ili umma uone kuna ubinyaji wa demokrasia wakati wao hawahubiri demokrasia bali wanachomeka idea zako ili kufikia malengo maovu
  2. Waraka unasema huko nyuma CDM ilifanya vizuri kwa kuongeza viongozi hadi kufikia wawakilishi watatu bungeni. Hawakuendelea kusema sasa wapo wangapi. Kipimo cha ubaya ni uzuri na kipimo cha uzuri ni ubaya. Je ni kwanini hawakusema sasa wapo wabunge wangapi chini ya uongozi huu.
Kama kulikuwa na uongozi 1,2 huu wa 3 kwanini hausomewi hukumu yake


Kuhusu waraka kuwa private, unataka kuhalalisha kuwa maudhui ya waraka ule yalikuwa sahihi.
Hawa ni viongozi wasiotakiwa kusema jambo moja jukwaani na kulirudia kwa namna nyingine nyuma ya pazia.

Mfano, akina Zitto wamekuwa wanatumia muda kueleza kuwa CDM si chama cha ukanda na udini.
Nyuma ya pazia(waraka)wameonyesha kutumia nyenzo hizo ili kufikia madaraka wanayotamani.

Ili kupata utetezi rahisi sana leo tunaambiwa waraka haukukusudia public hata kama tunajua ulikuwa kinyume na wanachosema, kinyume na maadili ya taifa na kinyume cha maadili ya uongozi.

Kutangaza na kuandika barua si jambo geni. Zitto akiwa katibu mkuu mtendaji aliridhia suala hilo kisheria. Kitila akiwa mshauri wa chama aliridhia suala hilo.
Wote walikuwa wanaingia katika vikao muhimu na hakuna rekodi kuwa waliwahi kulipinga.

Wanapolipinga uani ni kwenda kinyume cha maadili. Wanafanya maamuzi ambayo hawaridhiki nayo na kisha kurudi uani kutoa lawama kana kwamba walikuwa wageni na hawakujua chochote. Unafiki.

Waraka ni wa kitoto! Nasema ni wa kitoto sana. Huwezi kuandika mipango kwa njia za mipasho.
Hatuwezi kutofautisha maneno ya kwenye khanga za akina mama na baadhi ya maneno ya waraka.

Mfano, elimu yake ni magumashi, wana akili za kitoto, Zitto afanye mambo ya mapenzi kwa siri, uongozi unaonekana kama wahuni kwa kudhalilisha akina mama n.k.
Umepotosha kwa kusema Zitto mlengwa hana makundi wakati anachokifanya ni makundi wakati anaposema hivyo.

Hata hivyo historia inamhukumu Zitto kama mtu wa makundi kuliko kiongozi yoyote ndani ya CDM.
Amehusika sana na vurugu labda hilo nalo halikukusudiwa katika ‘public domain'

Umesema nifanye argument chama kitaathirika vipi kwa mkakati!
Nimeshasema huko nyuma lakini nirudie kwa kusema hakuna kinachoendelea CDM sasa hivi bali mtafaruku mkubwa.

Political base ipo confused and demoralized na kuna paralysis kubwa sana katika uendeshaji wa CDM
Sijui kama hilo hulioni ni tatizo. Na jiulize hao wanachama mamilioni wa CDM wanajisikiaje wakiona kikundi cha watu wawili watatu kinaleta mtafaruku huu

Jiulize hali ya kambi ya upinzani ambayo ni sehemu ya umma inayotambuliwa kisheria ipoje.

Mkuu hizo data za uongo wanakusudia kumpotosha nani? wakati umeambiwa waraka huu sio kwa public consumption?
Mbowe kungangania madaka inaweza kuwa kwa vipindi halali kikatiba lakini kwa njia za kulazimisha watu kondoa jina abaki peke yake
Habari ya watangulizi kufanya vizuri na huyu kufanya vibaya huo ni mtazamo wao mkuu kwanini unataka waamini unachoamini wewe, ni umma gani unaopotoshwa wakati waraka sio wa umma?
Narudia tena inawezekana hao walioanza walipata wabunge watatu kwa maono yao ikawa ni wengi kulingana na siasa za kipindi hicho lakini wakaona siasa za kipindi hiki CDM ilitakiwa iwe na wabunge 200........
UNAFANYA MAKOSA MAKUBWA KUDHAI WARAKA ULE UNAKUSUDIA KUPOTOSHA WATU.....NOPE........Waraka ule ni for only four person, the rest ilikuwa ni utekelezaji

Waswahili wanamsemo unasema SIRI YA KATA AIJUAE NI MTUNGI
Je ni mara ngapi Dr Slaa au Mbowe wanaulizwa kama kuna mgogoro CDM toka enzi ya akina Juliana na walikuwa wanasema hakuna lakini mwisho wasiku kila kitu kinakuwa hadharani
Je ni marangapi wameulizwa kama wana tatizo na Zitto? majibu yalikuwa Zitto hana tatizo na CDM na hayupo kwasababu A B C D lakini ukweli ni kwamba wanajua wanamatatizo
Nitakushangaa sana kama utatarajia eti kiongozi wa CDM aulizwe kuna ukanda ndani ya CDM na aseme ndio upo

Mnapokuwa kwenye taasisi linapokuja swala la maamuzi demokrasia lazima iheshimiwe, inawezekana kwenye majadilano hoja yako isipate nguvu na ikapita hoja ambazo wewe unadhani si sahihi, Huwezi kubisha na ndio maana waanda waraka wakaona viongozi wanapokea zaidi hoja mabazo kwao wao hazina msingi.....so cha kufanya ni kufuata misingi ya kidemokrasia kuhakikisha mtu wao anakuwa kwenye mazingira bora ya kushinda
Hoja ya kusema unakubali wakati unapinga haina mashiko..sababu waandaa waraka hawajapinga bali wameona ni vyema kutafuta njia mbadala

Kuhusu utoto wa waraka na lugha iliotumika bado nipo pale pale sijui lini utaondoa hii mentality ya kuuchukulia huu waraka kama uliandaliwa kwa watu wote ili kuuhadaa UMMA na kumdhalilisha mwenyekiti, maana kila sentensi lazima utarudia dhana hii
Labda nikusaidie kitu kimmoja mkuu unapoandaa mkakati wa mapambano yoyote yale unatakiwa kujua udhaifu na nafasi yako dhidi ya mpinzani wako, ukikosea hapa inakula kwako....lawama zote na kejeli ulizoziona kwenye waraka ndizo waanda waraka walizo ziona sasa kama wamekosea au wamepatia is none of your business
HUKUMU UTEKELEZAJI WA WARAKA ULE MKUU achana na lugha iliyotumika na maoni yao kwasababu wana uhuru wa kuwaza hivyo, ama kuwaza Mbowe malaya or whatever.....hayo ni mawazo yao na si kuja kuwatangazia umma

Kinachoendelea sasa hivi CDM hadi kufikia wana CDM wengi kuona kunamakundi yanasigana ni kutokuwa na uzoefu wa kutosha wa demokrasia ya ushindani ndani ya vyama vingi vya upinzani kuanzia CDM yenyewe CUF, NCCR, TLP.nk nk
Swala la makundi CDM hajalitengeneza Zitto bali ni uongozi wenyewe
Tuhuma hizo zinatumiwa sana kuhakikisha hakuna maamuzi yanayokwenda kinyume cha wenyechama
CDM ukiwa na mtazamo tofauti na wenye chama basi wewe ni mroho wa madaraka, unatumiwa na CCM, msaliti nk nk
 
Mkuu hizo data za uongo wanakusudia kumpotosha nani?
wakati umeambiwa waraka huu sio kwa public consumption?

Mbowe kungangania madaka inaweza kuwa kwa vipindi halali kikatiba lakini kwa njia za kulazimisha watu kondoa jina abaki peke yake. Habari ya watangulizi kufanya vizuri na huyu kufanya vibaya huo ni mtazamo wao mkuu kwanini unataka waamini unachoamini wewe, ni umma gani unaopotoshwa wakati waraka sio wa umma?

Narudia tena inawezekana hao walioanza walipata wabunge watatu kwa maono yao ikawa ni wengi kulingana na siasa za kipindi hicho lakini wakaona siasa za kipindi hiki CDM ilitakiwa iwe na wabunge 200........UNAFANYA MAKOSA MAKUBWA KUDHAI WARAKA ULE UNAKUSUDIA KUPOTOSHA WATU.....NOPE........Waraka ule ni for only four person, the rest ilikuwa ni utekelezaji

Waswahili wanamsemo unasema SIRI YA KATA AIJUAE NI MTUNGI
Je ni mara ngapi Dr Slaa au Mbowe wanaulizwa kama kuna mgogoro CDM toka enzi ya akina Juliana na walikuwa wanasema hakuna lakini mwisho wasiku kila kitu kinakuwa hadharani
Je ni marangapi wameulizwa kama wana tatizo na Zitto? majibu yalikuwa Zitto hana tatizo na CDM na hayupo kwasababu A B C D lakini ukweli ni kwamba wanajua wanamatatizo
Nitakushangaa sana kama utatarajia eti kiongozi wa CDM aulizwe kuna ukanda ndani ya CDM na aseme ndio upo

Mnapokuwa kwenye taasisi linapokuja swala la maamuzi demokrasia lazima iheshimiwe, inawezekana kwenye majadilano hoja yako isipate nguvu na ikapita hoja ambazo wewe unadhani si sahihi, Huwezi kubisha na ndio maana waanda waraka wakaona viongozi wanapokea zaidi hoja mabazo kwao wao hazina msingi.....so cha kufanya ni kufuata misingi ya kidemokrasia kuhakikisha mtu wao anakuwa kwenye mazingira bora ya kushinda
Hoja ya kusema unakubali wakati unapinga haina mashiko..sababu waandaa waraka hawajapinga bali wameona ni vyema kutafuta njia mbadala

Kuhusu utoto wa waraka na lugha iliotumika bado nipo pale pale sijui lini utaondoa hii mentality ya kuuchukulia huu waraka kama uliandaliwa kwa watu wote ili kuuhadaa UMMA na kumdhalilisha mwenyekiti, maana kila sentensi lazima utarudia dhana hii

Labda nikusaidie kitu kimmoja mkuu unapoandaa mkakati wa mapambano yoyote yale unatakiwa kujua udhaifu na nafasi yako dhidi ya mpinzani wako, ukikosea hapa inakula kwako....lawama zote na kejeli ulizoziona kwenye waraka ndizo waanda waraka walizo ziona sasa kama wamekosea au wamepatia is none of your business

HUKUMU UTEKELEZAJI WA WARAKA ULE MKUU achana na lugha iliyotumika na maoni yao kwasababu wana uhuru wa kuwaza hivyo, ama kuwaza Mbowe malaya or whatever.....hayo ni mawazo yao na si kuja kuwatangazia umma

Kinachoendelea sasa hivi CDM hadi kufikia wana CDM wengi kuona kunamakundi yanasigana ni kutokuwa na uzoefu wa kutosha wa demokrasia ya ushindani ndani ya vyama vingi vya upinzani kuanzia CDM yenyewe CUF, NCCR, TLP.nk nk

Swala la makundi CDM hajalitengeneza Zitto bali ni uongozi wenyewe
Tuhuma hizo zinatumiwa sana kuhakikisha hakuna maamuzi yanayokwenda kinyume cha wenyechama
CDM ukiwa na mtazamo tofauti na wenye chama basi wewe ni mroho wa madaraka, unatumiwa na CCM, msaliti nk nk
Nianze na hoja kuwa njia waliyotumia ni ya kidemokrasia. Nasema si kweli kwasababu demokrasia ina uhuru na mipaka yake. Nimeeleza jaribio la mapinduzi ambalo hukulikataa tena si moja. Walichokusudia ni mapinduzi kwa njia za mkato kuleta vurugu kwanza ili wapate upenyo.

Pili,walichotakiwa ni kujiuzulu nafasi zao kwanza ili wapate nafasi ya kuongelea walichokusudia au kutekeleza waliyokusudia. Kitendo cha kubaki na nyadhifa huku wakifanya mambo kinyume na makubaliano katika vikao vyao ni uhujumu mkubwa achilia mbali unafiki.

Tatu, ule waraka unajengewa uhalali kuwa ni private.
Kisichosemwa ule ndiyo msingi wa shughuli iliyotarajiwa kuwahusisha watu watatu waaminifu kwanza halafu makada 30 wa kanda ambao wangeenda katika mikoa na wilaya.

Kwa manenio mengine nyaraka ile ndiyo illikuwa road map ya kubadili mawazo ya watu.
Kama si road map ilikuwa template.

Kwa vile ilidhamiriwa kuwa road map au template hakuna shaka ndiyo imetumika kuwavutia baadhi. Ingalikuwa imesambaa(nadhani ilishasambaa) ingekuwa haipo katika watu watatu bali public.
Na kwavile ni public ilikusudia kuudanganya umma ambao si lazima uwe CDM hata walioko pembeni.

Haiwezekani watu watatu waandike waraka wa kujidanganya.
Wao walijua wameacha baadhi ya data lakini dhamira zao hazikuwa katika nafsi zao, zililenga public.

Pili, usichokielewa ni kuhusu waraka na data. Kama umetoa idadi ya chaguzi na mafanikio au mapungufu hilo halina kosa. Kama CDM walipaswa wawe na wabunge 200 kwa maono yao hilo halina tatizo.
Tatizo ni pale waraka unapowataja Makani na Mtei kwa ufanisi wao na kuacha uongozi uliopo kwa ufanisi kama wa Makani na Mtei na kurukia katika kusoma mashtaka, kuendesha kesi na hukumu hapo hapo.

Ni kwamba data zinatakiwa zijionyeshe zenyewe, siyo kuficha kwa ‘assumption'.
Unachoongelea wewe ni assumption, wanachoongelea wao ni upotoshaji, nianchoongelea mimi ni data analysis inavyopaswa kuwa.

Kuhusu kuwa na mtazamo tofauti unatuhumiwa, hilo ni la wanachama wa CDM na kama lina uthibitisho ndio wakati wa kueleza kwa vithibitisho na si hisia za mapenzi kwa mtu.

Kwa mfano, kama iliwahi kutokea hivyo kwanini akina Kitila na Zitto waliendelea kuwa viongozi? Walipaswa wajiuzulu ili waeleze kutoridhishwa kwao.

Kitendo cha kuwa viongozi na kwenda kinyume na maamuzi yao ni usaliti na ina fit def ya usaliti kabisa. Wanakaa katika vikao vya chama wakiondoka wana vikao vyao kupingana na maamuzi ya vikao, espionage ya hali ya juu na usaliti yakinifu.

Nakushangaa unaposema ukiwa na maamuzi unaonekana mroho wa madaraka, unatumiwa na CCM na kadhalika. Hebu nenda bandiko 92 halafu uniambie yule aliyeandika JF mambo yale akiwa nembo ya CCM alikuwa na nia gani?

Halafu elewa kuwa hii single inabadilka, leo mnasema uroho wa madaraka, waraka umesema ukanda.
Waraka ukachomeka udini, wakati waandika waraka wakipinga udini majukwani.
Huoni kama kuna utoto wa hali ya kuridhisha kabisa hapo.

Hata kama ni waraka wao leo tumejua kuwa kumbe jitihada si za kukisaidia chama chao bali kusemana kama akina mipasho ya mama katika khanga. Hawa ni wasomi walitakiwa wawe zaidi ya walivyoandika.
Matusi si njia ya msomi kujieleza.
 
Zakumi naomba watu waelewe hoja yangu. Mimi sijasema Mbowe amefanikisha upatikanaji wa wabunge wengi. Nilichosema ni kuwa waraka unatoa credit kwa Mtei na Makani kuitoa CDM point A to B halafu unaishia hapo.
Ninauliza Mbowe katoa point B-C mbona haionekani katika waraka? Je, hapo kuna anlysis kweli.
Kibaya zaidi waraka umeendelea kumsomea Mbowe hukumu ya madhaifu yake katika chaguzi ndogo. Narudi kusema inakuwaje waangalie chaguzi ndogo waache kubwa?

My point is, hakuna kuchagua data katika analysis. Kinachotakiwa zinawakilishwa kama zilivyo au haziwakilishwi kabisa.
Kinyume cha hivyo ni double standard na bias isiyo na kifani na inapelekea sisi tunaozungumza tukiwa huru tusema kwa uhakika kabisa huu ni utoto uliojengwa katika misingi ya Unafiki. Nafahamu Zittoism au Mbowelism hufumba macho mimi nimeshindwa kwasababu roho inanisumanga kama nitaidhalilisha akili ayngu kwa mahaba.
Mhaba yangu ni kwa demokrasia ya kweli na Tanzania imara.

Kuhusu Lema kwanza niseme rekodi ipo wazi mimi kukemea malumbano yasiyo na tija.
Unajua, kilichokuwa kinaendelea kilikuwa kinajulikana. Bandiko namba 92 nimeliweka makusudi naomba urudi na kuangalia nyuzi za nyuma. Dr Slaa amekuwa katika malumbano na huyo bwana kana kwamba ni watu wanafahamiana.

Mawasiliano ya team Zitto yalikuwa yanafahamika kilichokuwa kinasubiriwa ni timing ya kukamata ushahidi. Leo ungewezaje kusema Zitto ni mshiriki kama huna uthibitisho? Ndivyo alivyoruka viunzi vya Kafulila, na Juliana Shonzo.
Unakumbuka alimkana Ben Saanane kwamba hawajuani kabisa, na umma uliamini kwasababu hakuna ushahidi.
This time around amenasa pabaya ndipo wakamfyatua.

Alichokuwa anafanya Lema ilikuwa ni hasira kwa kukosa busara. Tena Mwigamba angekuwa makini asingewafikisha wenzake hapo walipo. Kulikuwa na kila dalili kuwa mawasiliano yao yalikuwa yananaswa.
Sasa swali la kuwa Lema alifanya vema kuhusu malumbano, absolutely no! Mwigamba alifanya vema kuhusu ujasusi wa kutoa habari 'live' kautoka kwenye vikao kwenda kwa masters yeye akiwa mtumwa, absolutely pathetic and immoral

Nguruv3;

Kwa hiyo tunakubaliana kuwa waraka ni matokeo tu ya vuguvugu zilizokuwepo kwa muda mrefu ambazo CDM walihamua kuzifumbia macho?

Vilevile tunakubaliana kuwa desperation yetu ya kutaka kuiondoa CCM ndio inayofanya baadhi ya watu kui-support CDM?

Vilevile unakubaliana kuwa pamoja na Zitto kuwa ni tatizo ndani ya chama, Mbowe naye ni tatizo vilevile?

Vilevile unakubaliana na mimi kuwa CDM ni chama cha mkusanyiko wa watu wenye matamanio tofauti tofauti kama vile CCM?

Vilevile unakubaliana na mimi kuwa migogoro ndani ya chama ni kitu kisichokwepeka?

Je unakubali kuwa katika kipindi cha sasa nguvu za CDM zielekezwe kwenye kubadili katiba na sio kuiondoa CCM madarakani?

Je unakubaliana na mimi kuwa kuvaa magwanda au uniform inawafanya watu wawe cocky kisaikolojia? Hivyo CDM waachie huo utamaduni CCM.

Je unakubaliana na mimi kuwa kuendesha magari makubwa (mashangingi) kunawafanya watu wawe cocky kisaikolojia? Hivyo CDM waachie huo utamaduni CCM.

Vilevile unakubali kuwa nchi kujiita Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo si lazima iwe ya kidemokrasia?

Je unakubaliana na mimi kuwa Mkandara bado hajarudisha kadi yake ya CCM?

Je unakubaliana na mimi kuwa katiba ya CDM ilitungwa na mtazamo wa kuwa na wabunge watatu bungeni na imeshindwa kuwa mwongozo kwa kipindi cha sasa chenye wanachama wengi na wabunge zaidi ya watatu?
 
Shida ninayoiona ndani ya CDM kwa muda mrefu ni kwa baadhi ya viongozi wake kutumia muda mwingi kujijenga wao zaidi kisiasa binafsi badala ya kufanya kazi pamoja kama team wakiwa na vision ya kuchukua nchi 2015. Mafanikio yaliofikiwa ni makubwa lakini bado the ultimate goal haijafikiwa hivyo wanapaswa kuimarisha team na sio kila mchezaji kutaka kucheza kivyake. Hii imekuwa na athari kubwa sana kwa chama kupoteza mwelekeo na wasipokuwa makini inaweza kuwagharimu zaidi huko mbele.

Nakubaliana na wewe. Lakini hilo Tatizo lipo kwa vyama vingine vya siasa pia. Na hii yote inatokana na mentality ya watanzania wengi kuchukulia siasa kama sehemu ya kunufaisha.

Ukweli wa mambo kujiingiza kwenye siasa kuwe na lengo la kutumikia umma.
 
Nguruv3;
1.Kwa hiyo tunakubaliana kuwa waraka ni matokeo tu ya vuguvugu zilizokuwepo kwa muda mrefu ambazo CDM walihamua kuzifumbia macho?

2.Vilevile tunakubaliana kuwa desperation yetu ya kutaka kuiondoa CCM ndio inayofanya baadhi ya watu kui-support CDM?

3.Vilevile unakubaliana kuwa pamoja na Zitto kuwa ni tatizo ndani ya chama, Mbowe naye ni tatizo vilevile?

4.Vilevile unakubaliana na mimi kuwa CDM ni chama cha mkusanyiko wa watu wenye matamanio tofauti tofauti kama vile CCM?

5.Vilevile unakubaliana na mimi kuwa migogoro ndani ya chama ni kitu kisichokwepeka?

6.Je unakubali kuwa katika kipindi cha sasa nguvu za CDM zielekezwe kwenye kubadili katiba na sio kuiondoa CCM madarakani?

7.Je unakubaliana na mimi kuwa kuvaa magwanda au uniform inawafanya watu wawe cocky kisaikolojia? Hivyo CDM waachie huo utamaduni CCM.

8.Je unakubaliana na mimi kuwa kuendesha magari makubwa (mashangingi) kunawafanya watu wawe cocky kisaikolojia? Hivyo CDM waachie huo utamaduni CCM.

9.Vilevile unakubali kuwa nchi kujiita Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo si lazima iwe ya kidemokrasia?

10.Je unakubaliana na mimi kuwa Mkandara bado hajarudisha kadi yake ya CCM?

11.Je unakubaliana na mimi kuwa katiba ya CDM ilitungwa na mtazamo wa kuwa na wabunge watatu bungeni na imeshindwa kuwa mwongozo kwa kipindi cha sasa chenye wanachama wengi na wabunge zaidi ya watatu?
Zakumi nayarejea maswali yako kama nitakavyojaaliwa.

Sikubaliani na hoja ya waraka kuwa vugu vugu lililokuwepo.
Nakubaliana na hoja vurugu zilizopo ni matokeo ya CDM kutoweka misingi ya nidhamu tangu awali.
Kulikuwa na kila kiashirio cha hujuma kuendelea kichini chini kwa bahati mbaya CDM wakaoneana haya.
Hayo ndio yamezaa kiburi cha waraka. Waraka haunavugu vugu bali vurugu.
Ni kwa msingi huo hadi sasa tupo page 100 hakuna anayeniambia kwa dhati substance(s) ya waraka ni ipi.

Desperation ya kuiondoa CCM
Kuna makundi yenye maono tofauti kuhusu hili.
1. Waliochoka na CCM kwasababu tu imeshindwa kukidhi haja na haionekani kama ina dhamira
2. Kundi dogo linaloamini katika sera za vyama na uwepo wa wapinzani kama mbadala ukiwakilisha mawazo yao
3.Kundi linaloona sasa ni zamu yao, hili ni la 'power mongers'

Nilishasema huko nyuma kuwa uongozi wa CDM ni tatizo.
Nilikuwa na sababu zifuatazo
1. Kushindwa kusimamia nidhamu kama timu
2. Kusimamisha chama kwa misingi ya personality na si wanachama
3.Kufanya mambo kwa template ya CCM
4. Kushindwa kusimamia sera zao na kutegemea udhaifu wa CCM.

Sikubaliani na hoja kuwa CDM au CCM ni mikusanyiko ya watu.
Wananachi wanajua thamani ya vyama kwa kuanzia na historia.
Hivi karibuni wameona thamani ya upinzani na chama tawala vikifanya kazi kwa pamoja hata kama ni kwa kutofautiana. Tunaona hamasa za wananchi iwe kwa CCM au CDM kwa kujitoa.
Tatizo la CCM na CDM ni viongozi waliolewa madaraka, wasiosikia na wenye matamanio tofauti na ya wananchi.
Vyama vyetu vimekosa akina Mahatma Gandhi, Mandela n.k wanaoamini katika utu na si kitu.

Migogoro katika vyama ni jambo jema 'balance and check'.
Lakini migogoro iwe katika policy, mission and vision.
Ningefarijika waandika waraka wangejitokeza na kukosoa sera za chama chao.
Hapana, hilo halipo, kilichotokea ni matusi, huyu hana akili, mapenzi kwa siri, takwimu fabricated,elimu ya magumashi na utoto mwingi kama huo. Hii si migogoro ya maana ndio maana tunasema spade ni spade siyo kijiko across the board.

Nguvu za CDM kwasasa si kubadili katiba, nguvu zielekezwe katika kuleta nidhamu, kurudisha chama kwa wanachama, kuondoa elements za personality, kuibua vipaji vingine na kujenga utamaduni mpya wa siasa za 2013.
Siasa zinazolenga katika uchumi utamaduni kwa faida ya jamii.
Katiba liwe jambo la mwisho kwasababu kutokana na ukosefu wa nidhamu, personality kuwa zaidi ya chama tunayoyaona sas. Katiba ni maandishi watu waliokubaliana yawaongeze, nidhamu ni utaratibu mzima wa kusimamia waliyokubaliana au waliyotofautiana katika maridhiano na maelewano.Nidhamu kwanza mengine yatafuata.

Kuvaa sare ni brand na wala si lazima yawe magwanda. Mara zote brand huwafanya watu wajisikie ni sehemu ya.
Sare huwa cocky wanachama na ni fursa nzuri kwa viongozi makini ku galvanize political base zao.
Sioni tatizo la brand kwa vyama vyote kwasababu ndio utambulisho tu.

Nadhani kuendesha magari siyo big deal, muhimu ni sera na kujitofautisha.
Ni kujisikia mwananchi na kumwelewa mwananchi wa kawaida.
Wanaweza kuacha kuendesha magari (mashangingi) lakini hilo linatosha?
Je dhamira zao zinawatuma kujisikia mwananchi anavyojisikia.
Kuna faida gani ya kuendesha Kibajaji ukiwa na account Uswiss.

Demokrasia ni neno na si lazima iwe nchi.
Ubaya ni pale demokrasia itakapotumika kama brand halafu ikachakachuliwa.
Huwezi kusema wewe ni chama cha demokrasia wakati umejificha uwanja wa fisi ukiandaa mapinduzi.
Huwezi kusema ni chama cha demokrasia ukichochoe maasi.
Huwezi kuwa chama cha demokrasia wakati hufuati misingi ya demokrasia.

Hilo la mkubwa Mkandara namwichia mwenyewe.
Ninachoweza kusema kurudisha au kutorudisha kadi hakuna maana yoyote.
It is just a symbolic gesture kuwa ima umejiunga au umeondoka.
Kadi inaweza kuwa souvenir tu.Na umiliki wa kadi hauwez ku hold ideology ya mtu au chama. Ni Piece of ID,that's it.

Sidhani kama maana ya uwepo wa katiba ni kwa ajili ya watu wachache.
Nadhani katiba ni muongozo wa jumuiya nzima.
Kwa vyama vichanga kisiasa kama CDM mabadiliko ya katiba ni jambo la kawaida kukidhi mahitaji ya wakati.
Hata CCM imekuwa inafanya mabadiliko licha ya ukongwe wake ili kukidhi haja ya wakati na mabadiliko.
Nakubaliana nawe kuwa yanapotokea matatizo hasa ya kikatiba ni vema kukaa na kuiangalia.

Sikubaliani kuwa wanapotokea wahuni kutoka embe kiburugwa wakataka kukidhi haja na matamanio yao ni vema kubadili katiba ili kutimiza malengo yao.
Vyama vya siasa si Simba na Yanga ambazo katiba hubadilishwa ili kumpata mwenyekiti anayetakiwa.
Vyama vya siasa vina dhamana kubwa zaidi ya hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Wana duru
Kuna jambo linalotokea kuhusu timbwili la CDM linanitatiza kidogo.

Mashabiki wengi wa CCM wanaona Zitto Kaonewa kuvuliwa madaraka.
Wengine wameanzisha hata nyuzi za kuonyesha hatari iliyopo ya kumeguka CDM wakimtimua.
Ina maana CCM wanampenda sana Zitto akiwa upinzani au ni uchungu walio nao kuhusu hatima ya upinzani?

Nilitaraji wangekuwa makini sana ili CDM imfukuze na kusambaratika, sivyo! wapo bize kumtetea kabisa. What's going on!

Katika mazingira ya kawaida nilitegemea CCM wawe wamekaa kimya ili wavue ‘papa' kama itabidi, la sivyo! wapo bize wakitetea nafasi ya Zitto tena wakishikiza utetezi
 
  1. Pasco;7982892]Wanabodi, Kikao cha Bunge kinaanza leo,pamoja na mambo mengine, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, KUB, itafanya Kikao chake kutekeleza maazimio ya yaliyofikiwa na Kamati Kuu Chadema, kumvua Zitto Zuberi Kabwe, (Mb.) al-maarufu kama ZZK ikiwemo Naibu Kiongozi wa KUB!.Pasco;7982892]
  2. Nafasi pekee ambapo Chadema hawawezi kumvua ZZK ni ile ya Mwenyekiti wa PAC, at least not for now, wakisubiria utekelezaji wa sheria, taratibu na kanuni za kumvua rasmi uanachama hivyo kupoteza ubunge na hivyo kupoteza Uenyekiti wa PAC outright, and be reduced to nobody!.
  3. Mimi kama raia mkeketwa wa demokrasia ya kweli ndani ya vyama na taifa kwa ujumla,nashauri yafuatayo:

  1. Uamuzi ule wa Kamati Kuu Chadema ni uamuzi batili ambao haukufuata the principles of the natural justice inayosema "nobody is condemned unheard!", yaani mtu yeyote hatahukumiwa bila kusikilizwa!. Kitendo cha Kamati Kuu ya Chadema kutoa hukumu ya kuwavua Zitto, Dr.Kitila na Mwigamba, nafasi zao zote za uongozi kabla ya kuwapelekea rasmi hati za mashitaka na kusikiliza utetezi wao ndipo watoe hukumu, huku ni to "put the cart before the horse!". The right way was kuwasimamisha kwanza nafasi zao zote za uongozi ndani ya chama kupisha uchunguzi na kuzingatia sheria, taratibu na kanuni kufuatwa, ndipo kuwapelekea mashitaka, kupokea utetezi wao, kuwaita kujieleza mbele ya kamati, kisha kupeleka mapendekezo yao Baraza Kuu ndilo pekee lenye mamlaka hayo ndani ya katiba ya sasa ya Chadema, not otherwise!, hivyo kitendo cha kuwavua kabla ya kuwasimamisha na kuwasikiliza kwanza ni kinyume cha sheria na wote wanaoutete uamuzi huo, wanatetea ujinga!, regardless ni kina nani na positions zao ni nani ndani ya chama, chonde chonde tafadhalini sana msituletee ujinga huu ndani ya bunge letu tukufu!.
  2. Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, inayo mamlaka yake huru ya kumbadili kiongozi yoyote wa KUB awe Kiongozi wa KUB, au Naibu Kiongozi wa KUB au mawaziri kivuli wowote, wakati wowote na kwa sababu zozote bila kuingiliwa na chombo chochote, au mamlaka yoyote!, basi nashauri kama umefika wakati wa kumbadili Naibu Kiongozi wa KUB, then mbadilini for a genuine reason and for the right course bila kuufuata ule ujinga wa Kamati Kuu ya Chadema!.
  3. Kwa vile KUB imehodhiwa na chama kimoja na ilipoundwa nilisema humu japo kikanuni its right, morally it's wrong ila kwa mazingira ya wakati ule kulikuwa hakuna any United front ya Wapinzani, lakini sasa tumeishuhudia ipo!, its high time now, Chadema kuacha rasmi kuihodhi KUB kwa kuwakaribisha na wengine kujiunga nayo na kuiunda upya Kambi hiyo Rasmi ya Upinzani Bungeni ambayo sasa itakuwa ni KUB ya ukweli kinyume cha hii iliyopo sasa ambayo ni KUB ya jina tuu, ila kiukweli ni kambi ya Chadema pekee inayolitumia jina la Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni!.
  4. Hili likifanyika, napendekeza Naibu Kiongozi wa KUB atoke nje ya Chadema just for the balance of power na kuongezeka busara zaidi!. Moja ya udhaifu mkubwa kabisa wa Chadema, ni kukosekana kwa busara, inayoipunguzia maarifa!, ikitokea siku moja Chadema ikaangamia!, itaangamia kwa kukosa maarifa!.
  5. KUB hii ilipoundwa Nilisema humu Chadema pekee yenu hamuwezi!. CCM ni lidudu likubwa lililo kubuhu kwa kila kitu aina ya wema na ubaya!. Wema kama kujenga mabarabara, kugawa fedha kwa mtindo wa "safety net", kuleta maendeleo japo kiduchu, ila pia limekubuhu kwa kila aina ya uovu na ubaya, ukiwemo rushwa, ufisadi, uwongo, fitna na majungu, hivyo bila ya a "united front" ya wapinzani wote wa kweli, then, hamuwezi kuliondoa hili lidude/lidudu kubwa CCM madarakani!. Pasco

  1. Mkuu Pasco nikushukuru kwa bandiko natumaini hutakwazika tukilitumia katika mjadala.
    Nia ni kuunganisha maudhui yake na mitazamo tofauti kila uchao.
    Pasco nakualika kwa kutumia ‘nguvu za psychic’ ujumbe utakufikia.
    Ulilosahau kueleza ni tuhuma zipi walipaswa kusikilizwa jambo linalokwepwa na wengi. Unasema CDM wame 'put the cart before the horse' nasema umetoa hukumu kabla mashtaka. Tuangalie hoja zako kwa uchache

    Hoja kuhusu mzozo
    Pasco Zitto na Kitila walifikisha barua za kujiuzulu kabla ya kikao cha kamati kuu.
    Walizuiliwa kujiuzulu kama mashujaa. Tayari walishakubali walichokifanya ni makosa.
    Hakukuwa na jambo la wao kusikilizwa tena kwasababu walishajisikiliza, wakajihukumu kujiuzulu kutoka na makosa wenyewe. Hivyo suala la kusikilizwa halina msingi katika hoja.

    Chenye msingi ni kuhusu CC ya CDM kuchukua uamuzi wa kuwavua badala ya kuwasimimisha wakati wakisubiri uamuzi wa bara kuu kama ndivyo katiba inavyosema.

    Nimeandika huko nyuma replacement ya haraka ya Zitto haina maana.
    Zitto hakushiriki shughuli zao na pengo lake lisingezorotesha lolote.

    Kitendo cha kumweka Msigwa ilikuwa ni jabza kwasababu tutaiuliza CC ya CDM, mbona hakuna replacement ya makamu wa mwenyekiti?

    1. At least KUB itakaa kumjadili mhusika,sidhani kama ni tatizo kwa taratibu.
    Ni kweli (KUB) ina mamlaka ya kufanya mabadiliko bila kuingiliwa.
    Unasahau wajumbe wa KUB ni wabunge wa vyama na misimamo yao ni ya vyama vyao.
    Mzozo wa kuunda KUB unatokana na vyama kuwa na misimamo tofati.

    Kiongozi wa serikali (PM) ambaye ni counterpart wa KUB anatoka chama tawala, ni mjumbe wa CC ya CCM na ndiye kiongozi wa wabunge wa CCM.
    Maazimio ya CCM hupitia kwake .

    Hili la CDM KUB kuchukua maamuzi ya CC CDM si jipya. Ni muundo wa bunge .
    Labda kama unataka KUB iwe huru ili kulinda masilahi ya Zitto.
    Hapo ni kupindisha taratibu kwasababu Bunge la CCM mbona halijawa huru kuingiliwa? 2. KUB wa mabunge ya commonwealth inaundwa na vyama vya upinzani chenye kwa kuongozwa na chenye wabunge wengi si suala la moral ni kanuni, taratibu na sheria.

    Kilichoplekea KUB kuhodhiwa na CDM ni uroho wa madaraka na kutoaminiana.
    Yapo maongezi ingawa sikujua yaliishia wapi ya kutengeneza upya KUB.
    Hadi itakapoundwa iliyopo ni halali na Zitto ni kiongozi na aliridhia.
    Sioni kwanini leo akikabiliwa na tifu sheria na taratibu zigeuge ghafla, haya ndio tusiyoyakubali wana demokrasia ingawa baadhi ya wanademokrasia mnayafumbia macho.

    3.Hilo la kuwa na naibu KUB ku-balance power ni suala la makubaliano lakini haliondo haki ya upinzani kuwa kambi rasmi.

    Mwisho, endapo Zitto atakuwa reduced to nobody hilo ni shauri lake na hana wa kumlaumu.
    Zitto is an author of his own chapter kutokana na arrogance, ignorance, grandiosity, Narcissism, and egoism. Pasco Zitto/Kitila kuendesha hujuma na mapinduzi si demokrasia unapaswa kukemea uhuni kwanza ili utonyeshe demokrasia
    Huwezi kutetea matokeo ya uhuni kwa mwamvuli wa demokrasia.
 
Navutiwa na mivutano yenu wanajamvi, nafurahi zaidi mnapojaribu kuipigania Demokrasia, mnaitetea vya kutosha, lakini bado inawatupa mkono! Ilishanenwa, HATUIWEZI! Wengine mnataka uwepo wa busara ndani ya Demokrasi, ama mantiki ya mambo ndani ya Demokrasia, mkisahau Demokrasia ni Kanuni. Ndio maana wapo wagombea bora wamekosa nafasi za uongozi na kupewa watu wa ovyoo! Hakuna nafasi ya Busara ndani ya Demokrasia! Na hakuna mwenye uhalali wa kuvunja kanuni zilizowekwa ndani ya demokrasia! Ukizingatia hilo sijui ni nani hastahili kufukuzwa ndani ya CCM na CDM. Kama mtakiuka kanuni na kutumia busara, basi isiwe bias.
Mkuu Nguruvi3, nastaajabishwa na hitimisho lako unaposema Zitto na Kitila kutaka kujiuzulu ni kuonesha wazi kuwa ni wakosaji! Ni kweli kila anayejiuzulu ni mkosaji? Sidhani kama dhana hii ni sahihi ya kutambua makosa ya Zitto!
 
Last edited by a moderator:
Katika bandiko#115 nimeuliza swali, kwanini wana CCM wanampigania sana Zitto katika sakata hili? Tulitarajia wawe na faraja CDM kumeguka au kuvua papa, lakini ni kinyume chake. Why?

Kuna nadharia kadhaa kuhusu hili.
Yapo makundi mawili makubwa
1. Kundi la wana 'CCM' ambao walianza kazi kama waraka ulivyoelekeza. Kundi hili linatambua kuwa Zitto nje ya CDM kitakuwa kifo cha kisiasa. Hata atakapokwenda anaweza kuishia kule waliko akina Kaborou na wenzao. Kundi linapigana kuhakikisha anabaki ndani ya CDM akiwa na wadhifa wake.

2. Kuna WanaCCM hasa ambao nao wana malengo yao.
a) Ima wanataka uwepo wa Zitto ndani ya CDM ili kuendeleza tension iliyopo na kuwagawa wanachama
b) Kuogopa nguvu ya uongozi ulipo na hivyo kuunga mkono jitihada zozote na za yeyote anayekabiliana na uongozi
c) Wanafahamu Zitto ni soft spot na hivyo ni easy target akiwa kiongozi
d) Wanamtumia kwa masilahi yao.

Kundi la wanaCCM hasa halina makosa kwasababu linafanya kazi iliyoandikwa na kukusudiwa. Kuua upinzani.
Kundi la 'WanaCCM' linafanya makosa sana kwasababu linaongeza curiosity juu ya Zitto ambaye yupo katika microscope

Jaribu kutafakari, kwanini hakukuwa na shauku na utetezi kama tunaouona wakati CCM inawafukuza akina Mansour Zanzibar? Kwanini hilo lionekane suala la chama na la Zitto(tena si Kitila, ni Zitto) liwe la kitaifa?

Makundi yote mawili yameshindwa kujibu tuhuma zinazomkabili hoja kwa hoja, yamebaki kusema kaonewa, chama kitasambaratika, ni mtu maarufu, amejitolea sana, ananyimwa fursa, anaonewa wivu n.k. bila kujibu hoja hasa zinazotokana na tuhuma zake.

Laiti makundi hayo yangejua tafsiri za kisiasa yasingeingia katika mjadala huu. Kinachoendelea sasa hivi ni kumweka Zitto katika mazingira magumu na hata waliokuwa na wasi wasi pengine unaanza kuwatoka.
Kwa Zitto hizi si habari njema kwasababu zinazidi kutoa image yako ambayo imepoteza public trust kwa kiasi kikubwa sana. Hii haina maana 'the end of politics' ina maana una wakati mgumu na muda mrefu to regain the the eroded and severely compromi
 
Navutiwa na mivutano yenu wanajamvi, nafurahi zaidi mnapojaribu kuipigania Demokrasia, mnaitetea vya kutosha, lakini bado inawatupa mkono! Ilishanenwa, HATUIWEZI! Wengine mnataka uwepo wa busara ndani ya Demokrasi, ama mantiki ya mambo ndani ya Demokrasia, mkisahau Demokrasia ni Kanuni. Ndio maana wapo wagombea bora wamekosa nafasi za uongozi na kupewa watu wa ovyoo! Hakuna nafasi ya Busara ndani ya Demokrasia! Na hakuna mwenye uhalali wa kuvunja kanuni zilizowekwa ndani ya demokrasia! Ukizingatia hilo sijui ni nani hastahili kufukuzwa ndani ya CCM na CDM. Kama mtakiuka kanuni na kutumia busara, basi isiwe bias.
Mkuu Nguruvi3, nastaajabishwa na hitimisho lako unaposema Zitto na Kitila kutaka kujiuzulu ni kuonesha wazi kuwa ni wakosaji! Ni kweli kila anayejiuzulu ni mkosaji? Sidhani kama dhana hii ni sahihi ya kutambua makosa ya Zitto!
Kwanza ahsante sana kwa hekima zako kuhusu demokrasia. Watu hawafahamu kuwa demokrasia si dude linaloelea bali kanuni zinazofuatwa na kuheshimiwa.

Pili, Zitto na Kitila walifikisha barua za kujiuzulu baada ya kubaini kuwa Mwigamba ameuza 'silaha'.
Kitila kakubali ilikuwa ni kosa kushiriki kuandika waraka. Hakuna shaka ilikuwa njia rahisi kujiuzulu ili kuepusha madhara zaidi. Hivyo kujiuzulu kwao ambako kuliambatana na waraka kwa mtazamo wangu ilikuwa ni makosa.

Ni makosa kwasababu waraka kabla haujatoka tulishasoma harakati zao dhidi ya chama chao mtandaoni.
Tafadhali rejea bandiko #92 unielewe ninaongelea nini.

Endapo wangekuwa na nia njema ya kujiuzulu wangeshafanya hivyo baada ya kubaini mambo sivyo kama wanavyodai. Hawakufanya hivyo bali kuingia katika vikao na kwenda kujificha kufanya counter attack ya maazimio yale yale waliyoyaunga mkono wakiwa viongozi.
Hawakujiuzulu bali kumtumia Mwigamba kutoa mambo ya vikao vikiendelea kama sehemu ya habari za mitandaoni.
Walifanya espionage badala ya kujiuzulu. Ni uhuni wa demokrasia na hawafai kupewa benefit of doubt kwa namna yoyote ile.

Na zaidi hawakufuata kanuni zinazojenga misingi ya demokrasia kama ulivyoonyesha katika andiko#117.
 
Katika bandiko#115 nimeuliza swali, kwanini wana CCM wanampigania sana Zitto katika sakata hili? Tulitarajia wawe na faraja CDM kumeguka au kuvua papa, lakini ni kinyume chake. Why?

Kuna nadharia kadhaa kuhusu hili.
Yapo makundi mawili makubwa
1. Kundi la wana 'CCM' ambao walianza kazi kama waraka ulivyoelekeza. Kundi hili linatambua kuwa Zitto nje ya CDM kitakuwa kifo cha kisiasa. Hata atakapokwenda anaweza kuishia kule waliko akina Kaborou na wenzao. Kundi linapigana kuhakikisha anabaki ndani ya CDM akiwa na wadhifa wake.

2. Kuna WanaCCM hasa ambao nao wana malengo yao.
a) Ima wanataka uwepo wa Zitto ndani ya CDM ili kuendeleza tension iliyopo na kuwagawa wanachama
b) Kuogopa nguvu ya uongozi ulipo na hivyo kuunga mkono jitihada zozote na za yeyote anayekabiliana na uongozi
c) Wanafahamu Zitto ni soft spot na hivyo ni easy target akiwa kiongozi
d) Wanamtumia kwa masilahi yao.

Kundi la wanaCCM hasa halina makosa kwasababu linafanya kazi iliyoandikwa na kukusudiwa. Kuua upinzani.
Kundi la 'WanaCCM' linafanya makosa sana kwasababu linaongeza curiosity juu ya Zitto ambaye yupo katika microscope

Jaribu kutafakari, kwanini hakukuwa na shauku na utetezi kama tunaouona wakati CCM inawafukuza akina Mansour Zanzibar? Kwanini hilo lionekane suala la chama na la Zitto(tena si Kitila, ni Zitto) liwe la kitaifa?

Makundi yote mawili yameshindwa kujibu tuhuma zinazomkabili hoja kwa hoja, yamebaki kusema kaonewa, chama kitasambaratika, ni mtu maarufu, amejitolea sana, ananyimwa fursa, anaonewa wivu n.k. bila kujibu hoja hasa zinazotokana na tuhuma zake.

Laiti makundi hayo yangejua tafsiri za kisiasa yasingeingia katika mjadala huu. Kinachoendelea sasa hivi ni kumweka Zitto katika mazingira magumu na hata waliokuwa na wasi wasi pengine unaanza kuwatoka.
Kwa Zitto hizi si habari njema kwasababu zinazidi kutoa image yako ambayo imepoteza public trust kwa kiasi kikubwa sana. Hii haina maana 'the end of politics' ina maana una wakati mgumu na muda mrefu to regain the the eroded and severely compromi

Mkuu nguruvi
CCM wamekuwa wakimpigia chapuo Zitto kuwa anafaa kuiongoza CDM na hata kugombea urais kwa muda mrefu sasa. Na hii ikachagizwa zaidi na kauli ya Rais kuwa angependa mrithi wake awe kijana...kauli ambayo ilitafsiriwa na baadhi ya watu kuwa alikuwa akimzungumzia Zitto. Sababu hasa ya kumuunga mkono ni fumbo kuu lakini inawezekana kabisa kuwa wanamchukulia kama easy target endapo atapeperusha bendera ya upinzani. Bahati mbaya sana chapuo hizo zimekuwa zikiambatana na propaganda za udini, ukabila na ukanda kutaka kuaminisha watu kuwa mheshimiwa huyu anabaguliwa kutokana na dini/kabila lake....
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom