Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

[/LIST]
[/COLOR][/COLOR]
  1. Mkuu Pasco nikushukuru kwa bandiko natumaini hutakwazika tukilitumia katika mjadala.
    Nia ni kuunganisha maudhui yake na mitazamo tofauti kila uchao.
    Pasco nakualika kwa kutumia ‘nguvu za psychic' ujumbe utakufikia.



  1. Pasco Zitto/Kitila kuendesha hujuma na mapinduzi si demokrasia unapaswa kukemea uhuni kwanza ili utonyeshe demokrasia
    Huwezi kutetea matokeo ya uhuni kwa mwamvuli wa demokrasia.
Mkuu Nguruvu3, kwanza asante, wewe kutumia bandiko langu ni heshima kubwa kwangu.
Mwaliko wako wa PSI niliupata jana ulipomwaga tuu thanks kwenye bandiko langu, ila pia kwenye zile powers from within, Mkuu Nguruvi3, you are very powerful!, you have the powers to make things happen kwenye political atmosphare, nakuomba sana make you wish now!, ili 2015 mambo ya change!, play more active role kwa kusema tuu kunatosha!, sio lazima mpaka uingie kwenye ngoma kuicheza!, vivyo hivyo Mzee Mwanakujiji a very powerful man inside, keeps playing "hide and seek", saidieni!, jahazi ndio hili linakwenda marama!. 2015 tutakuja tuu kutoa pole na kusema tuliwaambia!.

Nakutafutia muda nikujibu rasmi posti yako, ila kuna jambo nimeanza kulinote, nikilithibitisha, nitakuambia!, in short kuna ma great thinkers wako blindfolded na mapenzi ya Chadema!, wametake sides! ukiwemo wewe Mkuu Nguruvi3!.

Nilimwambia Mzee Mwanakijiji mahali, kuwa "mchelea mwana kulia, hulia yeye!", Mkuu Nguruvi, 2015 mtalia..!.

Kwa vile huu uzi uko page zaidi ya 100, mambo ya "powers" yalinitinga nikapoteza a bit of my political focus, nitakurudia tangu mwanzo, nitakueleza ya kwangu!.

Tangu alipoanza Tumtemeke, wakaja kina Shonza, waraka wa Mngamba, waraka wa Kitila, nyaraka zote hizo zina hoja za msingi sana ambazo kamwe hazijibiwi!, inachofanya Chadema ni kuwatimua watoa nyaraka, kisha kufunika kombe mwanaharamu apite!, wanachofanya ndio ile ile ya mbuni kujificha ndani ya mchanga kwa kufunika kichwa!.
Nitakujibu!.

Pasco.
 
Wana duru
Kuna jambo linalotokea kuhusu timbwili la CDM linanitatiza kidogo.

Mashabiki wengi wa CCM wanaona Zitto Kaonewa kuvuliwa madaraka.
Wengine wameanzisha hata nyuzi za kuonyesha hatari iliyopo ya kumeguka CDM wakimtimua.
Ina maana CCM wanampenda sana Zitto akiwa upinzani au ni uchungu walio nao kuhusu hatima ya upinzani?

Nilitaraji wangekuwa makini sana ili CDM imfukuze na kusambaratika, sivyo! wapo bize kumtetea kabisa. What’s going on!

Katika mazingira ya kawaida nilitegemea CCM wawe wamekaa kimya ili wavue ‘papa’ kama itabidi, la sivyo! wapo bize wakitetea nafasi ya Zitto tena wakishikiza utetezi

Nguruv3;

Unapofanya uchambuzi na wewe ukiwa mshabiki wa upande fulani unaweza kupoteza mwelekeo. Unaonyesha bado una upendeleo fulani na CDM. Lakini kumbuka kuwa wanachofanya CCM kuhusu Zitto kinafanywa sana wanaCDM pale migogoro inapozuka ndani ya CCM.

Kama sitakosea kuna kipindi CDM ilikuwa inasubiri atakayenyimwa tiketi ya kugombea urais CCM apitishwe na CDM kugombea urais. Kama CCM isingempa JK nafasi ya kugombe urais mwaka 2005, CDM walikuwa tayari kumpokea. Na kwenye mitandao watu walikuwa wanajadili possibility hiyo. Na vilevile walikuwa wanajadili nani awe mgombea urais ndani ya CCM.

Hivyo CCM wanachofanya sasa sio kitu kipya na tena hawakuanza wao. Hata hapa Marekani Republicans wanazungumza Democrats and vice versa.

Vilevile CDM, CCM, CUF na vyama vingine vya upinzani vinaishi kwa kutumia ruzuku za serikali. Hivyo ni haki ya kila mtanzania kuvijadili. Kama CDM hawataki kujadiliwa kuna mawili. Waache siasa kabisa au wapunguze migogoro.
 
Nguruv3;

Unapofanya uchambuzi na wewe ukiwa mshabiki wa upande fulani unaweza kupoteza mwelekeo. Unaonyesha bado una upendeleo fulani na CDM. Lakini kumbuka kuwa wanachofanya CCM kuhusu Zitto kinafanywa sana wanaCDM pale migogoro inapozuka ndani ya CCM.

Kama sitakosea kuna kipindi CDM ilikuwa inasubiri atakayenyimwa tiketi ya kugombea urais CCM apitishwe na CDM kugombea urais. Kama CCM isingempa JK nafasi ya kugombe urais mwaka 2005, CDM walikuwa tayari kumpokea. Na kwenye mitandao watu walikuwa wanajadili possibility hiyo. Na vilevile walikuwa wanajadili nani awe mgombea urais ndani ya CCM.

Hivyo CCM wanachofanya sasa sio kitu kipya na tena hawakuanza wao. Hata hapa Marekani Republicans wanazungumza Democrats and vice versa.

Vilevile CDM, CCM, CUF na vyama vingine vya upinzani vinaishi kwa kutumia ruzuku za serikali. Hivyo ni haki ya kila mtanzania kuvijadili. Kama CDM hawataki kujadiliwa kuna mawili. Waache siasa kabisa au wapunguze migogoro.
Niliuliza tu kwasababu wakati CCM wanamfukuza Mansour hilo lilikuwa jambo la chama, lakini naona wao wana uchungu sana na upinzani hasa Zitto. It was just a heads up. Hakuna ubaya wowote ila ni pale unapomuona tembo akiwa juu ya mti utajiuliza ilikuwaje. Unapoona Simba anamtetea swala asiliwe na chui utajiuliza mapenzi hayo simba kaanza lini.
 
Mkuu nguruvi
CCM wamekuwa wakimpigia chapuo Zitto kuwa anafaa kuiongoza CDM na hata kugombea urais kwa muda mrefu sasa. Na hii ikachagizwa zaidi na kauli ya Rais kuwa angependa mrithi wake awe kijana...kauli ambayo ilitafsiriwa na baadhi ya watu kuwa alikuwa akimzungumzia Zitto. Sababu hasa ya kumuunga mkono ni fumbo kuu lakini inawezekana kabisa kuwa wanamchukulia kama easy target endapo atapeperusha bendera ya upinzani. Bahati mbaya sana chapuo hizo zimekuwa zikiambatana na propaganda za udini, ukabila na ukanda kutaka kuaminisha watu kuwa mheshimiwa huyu anabaguliwa kutokana na dini/kabila lake....

Mwalimu:

Wenzetu waliosoma kama Mchambuzi, Mkandara, Nguruv3 wanaangalia siasa kutokana na sera za vyama. Sisi walalahoi tunaangalia siasa kwa kuangalia personalities za wanasiasa. Pamoja na kuwa ni mleta migogoro ndani ya CDM, Zitto ana personality inayokubalika na watu wengi nje ya CDM.

Na kuna viongozi wa juu ndani ya CDM ambao wanakubalika ndani ya CDM lakini personalities zao haziivi nje ya CDM.
 
PUPA ZA CHADEMA ! NANI ANAWASHAURI?

Tifu la vurugu linaendelea huku kukiwa na taharuki kubwa. Inavyoonekana kuna loss of control kwa upande wa uongozi.
Pasco amesema kuna nyakati busara inatakiwa itawale. Ingawa busara anayoongelea ni kuhusu ZZK, nakubaliana naye kuwa kuna ukosefu wa busara katika baadhi ya mambo.

Kitendo cha kuwavua madaraka watuhumiwa na kuweka replacement haraka hakikuwa cha busara. Hakuna sababu za nafasi zao kujazwa haraka tukifahamu hawakuwa wanashiriki shughuli za chama na ombwe lao lisingeweza kuathiri utendaji kwa namna yoyote. Pili, kuna swali linajitokeza kwanini hakukuwa na kuziba pengo la makamu mwenyekiti aliyejiuzulu ambaye nafasi yake kichama ni nyeti na muhimu.
Hata baada ya kujiuzulu hakuna guideline nani anakaimu nafasi hiyo endapo mwenyekiti atakuwa incapacitated kutimiza majuku ya CDM katika wakati wa dharura au vinginevyo
Busara ilikuwa kuchukua hatua kwa taratibu badala ya jazba hata kama wajumbe walikuwa na jazba.

Tembo yupo anasubiri kuingia kibandani. Mawimbi ni mazito yanayohitaji udharura wa kuyashughulikia.
Katibu mkuu Dr Slaa anataka kufanya ziara kwenye maeneo yanayoonyesha kutoridhishwa na maamuzi kama Kigoma.

Huo ni ukosefu wa busara wa kiwango kikubwa. Tatizo lipo makao makuu si mikoani,. Mikoani ni mwangi tu.
Katibu mkuu hana sababu za kufanya ziara kwa sasa hivi alipaswa atulie CDM ipate ‘ccoling effect'

Tifu ni fursa nzuri kuacha wanachama waamue kutokana na mitazamo yao. Endapo wanaacha CDM na kujiunga kwingine hiyo ni hiari yao.
Mzozo ungetumika kama chujio la kufahamu wanachama wanaosimamia sera na wale waliopo kwa ajili ya watu au mtu, kwa ajili ya masilahi n.k.

Mfano, kujiuzulu mwenyekiti wa mkoa wa Singida si jambo baya hasa ukizingatia kuwa kwa miaka 20 ameshindwa kujenga ofisi ya chama licha ya ukongwe wake.
Wananchi wa Kilolo wamejenga ofisi yao wenyewe, sijui kwanini mwenyekiti wa singida aonekane muhimu kiasia cha watu kuhamaki wakifahamu mchango wake duni.
Busara ilikuwa Dr Slaa kutulia na kuacha chama kijichuje na wala si kukimbilia Kigoma kusigishana na watu wa mitaani.

Matokeo ya mbio hizo ni resistance ambayo itasambaa zaidi na kuzidi kumfedhehesha.
Busara zimekosekana. Huu si wakati wa kupambana na watu wa mitaani ni wakati wa kushughulikia tatizo ndani ya makao makuu.

Tumeshuhudia habari ya kusifia jinsi CDM ilivyo kimataifa kwa uwazi.
Habari imeletwa makusudi kupunguza nguvu ya timbwili lililopo.
Kwa bahati mbaya ni mbinu hafifu sana na imefanyika kwa njia hafifu sana.

Huwezi kuundoa umma katika masuala yanayogusa CDM kwa kuleta habari za nje ya nchi.
Hilo si tatizo au mafanikio ya CDM kwa sasa.
Tatizo ni mgogoro wa uongozi na mafanikio ni jinsi gani watautatua.

Kuna umuhimu wa kutumia busara katika kufanya mambo. Uongozi wa CDM taifa usikwepe ukweli kuwa tatizo ni kubwa.
Uongozi unapaswa kukabiliana na tatizo na si kufukia au kutafuta dawa za kuonguza maumivu.

Ndio maana tunauliza, nani anawashauri kufanya mambo kwa pupa namna hiyo? Je hiyo ndio njia nzuri ya kumaliza tatizo.
Msifanye mambo kwa template au ujanja wa CCM, hoja za kifasadi zinazimwa kwa ulaghai wa hoja nyingine. Badilikeni mjitofautishe, vinginevyo tofauti yenu na CCM ni ipi?

Nguruvi3
 
Niliuliza tu kwasababu wakati CCM wanamfukuza Mansour hilo lilikuwa jambo la chama, lakini naona wao wana uchungu sana na upinzani hasa Zitto. It was just a heads up. Hakuna ubaya wowote ila ni pale unapomuona tembo akiwa juu ya mti utajiuliza ilikuwaje. Unapoona Simba anamtetea swala asiliwe na chui utajiuliza mapenzi hayo simba kaanza lini.

Nadhani inabidi tutofautishe vitu viwili: Political Pundit and politician. Mtu mmoja anaweza kuvaa kofia zote mbili. Katika kipindi cha sasa political pundits wengine wakiwa CCM politicians watatoa analysis zao kuhusu migogoro ndani ya CDM. Hizi ni analysis tu na sio lazima iwe mikakati ya CCM kuhusu CDM. Kuna watakao mpe support ZZK na watakao mkataa.

Hivyo kama watu wanaanza kutilia wasiwasi analysis au kufanya political punditry kwanini basi wanajiunga kwenye siasa? Analysis sio ziwe za kisomi au zenye manufaa kwa jamii.

Kuhusiana na Mansour, kwanza alikuwa sio heavy weight ndani ya CCM. Pili sio jukumu la CCM kuwaambia political pundits kumfanyia analysis Mansour. Kama kulikuwa na umuhimu, watu wangemzungumza.
 
Nadhani inabidi tutofautishe vitu viwili: Political Pundit and politician. Mtu mmoja anaweza kuvaa kofia zote mbili. Katika kipindi cha sasa political pundits wengine wakiwa CCM politicians watatoa analysis zao kuhusu migogoro ndani ya CDM. Hizi ni analysis tu na sio lazima iwe mikakati ya CCM kuhusu CDM. Kuna watakao mpe support ZZK na watakao mkataa.

Hivyo kama watu wanaanza kutilia wasiwasi analysis au kufanya political punditry kwanini basi wanajiunga kwenye siasa? Analysis sio ziwe za kisomi au zenye manufaa kwa jamii.

Kuhusiana na Mansour, kwanza alikuwa sio heavy weight ndani ya CCM. Pili sio jukumu la CCM kuwaambia political pundits kumfanyia analysis Mansour. Kama kulikuwa na umuhimu, watu wangemzungumza.
Si kweli, Mnasour alikuwa heavy weight upande wa visiwani.
Utakumbuka ndiye aliyekuwa sterling wa kuondoa suala la mafuta na gesi

Siasa zote za visiwani zilitawaliwa na jina lake kwa kuzingatia ni mwana CCM.


Alipoondolewa kutokana na mawazo yake ambayo yalikuwa huru kabisa na wazi lilionekana jambo la kidemokrasia.


Nilisimama kuhoji kuondolewa kwake na kusema hakutendewa haki.

Uhuru wa mawazo ndani ya vyama lazima uwepo.


Ni uhuru huo huo niliwahi kuandika kuwa japo sikubaliani na hoja ya Zitto kuhusu serikali 3 alivyoijenga nakubaliana naye kuwa muwazi kabisa na kueleza mawazo yake hadharani.


Hili la sasa hakuwa muwazi, alijificha nyuma ya akina Kitila wakakaa ‘Buguruni kwa malapa' wakaandika waraka, wakatumia watu kuuchomeka katika public domain kabla haujakamatwa.


Wakamtumia Mwigamba kuwa kama conduit ya mawazo yao katika public, Mwigamba akauza ghala la silaha. Hapo hakuna uwazi au demokrasia, ni uhuni na utoto tu uliotamalaki kwa kiwango chema sana.


Kinachoshangaza ni hao pundits na politicians kugoma kabisa kumchukua Zitto bali wanataka abaki kule kule wasikokutaka.

Nimeweka makundi mawili hapo juu na kwanini nadhani yanafanya hivyo.


Simba anapolalamika swala kukamatwa na chui kuna maswali mengi sana, nature haisemi hivyo. Huruma hiyo kaipata wapi Simba tunayemjua.


Kazi za pundits zinaonekana kuumiza zaidi ZZK kuliko kumsaidia ndio maana nimeshauri wafanye tofauti kwasababu sasa hivi wanazidi kumwanika katika scrutiny, microscope and kuna curiosity ya juu sana juu yake.


Historia ya ZZK haitoa nafasi kwa scrutiny kwasababu si nzuri.



 
Nguruv3;

Unapofanya uchambuzi na wewe ukiwa mshabiki wa upande fulani unaweza kupoteza mwelekeo. Unaonyesha bado una upendeleo fulani na CDM. Lakini kumbuka kuwa wanachofanya CCM kuhusu Zitto kinafanywa sana wanaCDM pale migogoro inapozuka ndani ya CCM.

Kama sitakosea kuna kipindi CDM ilikuwa inasubiri atakayenyimwa tiketi ya kugombea urais CCM apitishwe na CDM kugombea urais. Kama CCM isingempa JK nafasi ya kugombe urais mwaka 2005, CDM walikuwa tayari kumpokea. Na kwenye mitandao watu walikuwa wanajadili possibility hiyo. Na vilevile walikuwa wanajadili nani awe mgombea urais ndani ya CCM.

Hivyo CCM wanachofanya sasa sio kitu kipya na tena hawakuanza wao. Hata hapa Marekani Republicans wanazungumza Democrats and vice versa.

Vilevile CDM, CCM, CUF na vyama vingine vya upinzani vinaishi kwa kutumia ruzuku za serikali. Hivyo ni haki ya kila mtanzania kuvijadili. Kama CDM hawataki kujadiliwa kuna mawili. Waache siasa kabisa au wapunguze migogoro.
Zakumi aliyekuwa anasubiriwa ni JK au Sitta? Taarifa za mitaani ni JK, taarifa za ndani ni Sitta aliyechomoa dakika za mwisho.
 
Last edited by a moderator:
Zakumi aliyekuwa anasubiriwa ni JK au Sitta? Taarifa za mitaani ni JK, taarifa za ndani ni Sitta aliyechomoa dakika za mwisho.

Ni JK ,Sitta hakuwa na uzito huo kipindi hiko,JK ndo alikua anauzika sokoni kikwazo kikawa ndani ya chama,narudi katika mada,salamu zenu wakuu,kuna nimekuwa nikisoma huu Mnakasha mda mrefu,kuna vitu naona watu wameamua kuwa kihisia si kisheria au kiukweli,nakuona kabisa wanamsurubu Zitto kwa kosa asilofanya,lazima tuweke Mizania sawasawa
 
Last edited by a moderator:
Ni JK ,Sitta hakuwa na uzito huo kipindi hiko,JK ndo alikua anauzika sokoni kikwazo kikawa ndani ya chama,narudi katika mada,salamu zenu wakuu,kuna nimekuwa nikisoma huu Mnakasha mda mrefu,kuna vitu naona watu wameamua kuwa kihisia si kisheria au kiukweli,nakuona kabisa wanamsurubu Zitto kwa kosa asilofanya,lazima tuweke Mizania sawasawa
Karibu sana tuweke mizani sawa sawa. Kwakweli hilo ni jambo jema kabisa.
 
Mkuu Nguruvu3, kwanza asante, wewe kutumia bandiko langu ni heshima kubwa kwangu.
Mwaliko wako wa PSI niliupata jana ulipomwaga tuu thanks kwenye bandiko langu, ila pia kwenye zile powers from within, Mkuu Nguruvi3, you are very powerful!, you have the powers to make things happen kwenye political atmosphare, nakuomba sana make you wish now!, ili 2015 mambo ya change!, play more active role kwa kusema tuu kunatosha!, sio lazima mpaka uingie kwenye ngoma kuicheza!, vivyo hivyo Mzee Mwanakujiji a very powerful man inside, keeps playing "hide and seek", saidieni!, jahazi ndio hili linakwenda marama!. 2015 tutakuja tuu kutoa pole na kusema tuliwaambia!.

Nakutafutia muda nikujibu rasmi posti yako, ila kuna jambo nimeanza kulinote, nikilithibitisha, nitakuambia!, in short kuna ma great thinkers wako blindfolded na mapenzi ya Chadema!, wametake sides! ukiwemo wewe Mkuu Nguruvi3!.

Nilimwambia Mzee Mwanakijiji mahali, kuwa "mchelea mwana kulia, hulia yeye!", Mkuu Nguruvi, 2015 mtalia..!.

Kwa vile huu uzi uko page zaidi ya 100, mambo ya "powers" yalinitinga nikapoteza a bit of my political focus, nitakurudia tangu mwanzo, nitakueleza ya kwangu!.

Tangu alipoanza Tumtemeke, wakaja kina Shonza, waraka wa Mngamba, waraka wa Kitila, nyaraka zote hizo zina hoja za msingi sana ambazo kamwe hazijibiwi!, inachofanya Chadema ni kuwatimua watoa nyaraka, kisha kufunika kombe mwanaharamu apite!, wanachofanya ndio ile ile ya mbuni kujificha ndani ya mchanga kwa kufunika kichwa!.
Nitakujibu!.Pasco
.
Mkuu Pasco wakati tunasubiri udurusu kurasa ili uje na yako, ningependa nizungumzie kidogo kuhusu aya ya mwisho.

Awali ya yote nieleze kuwa ukiwa huru utaongea bila hofu. Nia kubwa ya baadhi yetu si ushabiki bali kuona tunafikia demokrasia ya wenzetu ambayo si uchama bali kanuni, misingi, taratibu na nidhamu.

Tony Blair aliondolewa na Labour baada ya kubaini anakipeleka chama kusiko.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Margareth Thatcher na wengine.
India imeweza kubaki bila waziri mkuu kwa miezi 3 na nchi haikuathirika.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Uingereza baada ya GB kutoweza kuundwa seikali ya minority kwa wiki tatu.
Yote yametokea na nchi zimeendelea kuwepo. Ndipo wenzetu walipo katika demokrasia.

Tunainyooshea kidole CCM kwa kushindwa kuchukua hatua au kuwawajibisha viongozi wake.
Inapofika waziri mhusika anakutwa na majnga 2 ya vifo vya raia bila hatia kwa mabomu na bado yupo ofisini inatupaswa tisikitike.CCM ni 'old dog you can't teach new tricks'.

Hivi vyama vingine vinavyowania madaraka lazima vijifunze taratibu, nidhamu na sheria.
Tutake tusitake inaweza kutokea siku vikachukua dola. Je, tuendelee kuishi katika mazingira tuliyo nayo sasa hadi lini?

Kama umeusoma waraka na mjadala hatukatai uwepo wa matatizo. Tunachojadiliana ni jinsi gani watu wanashughulikia matatizo hayo. Njia zilizotumika katika waraka hazionyeshi political maturity ya aina yoyote.
Njia za kuwa kiongozi na kuchukua siri ili kuzifanyia kazi embe kiburugwa ni za kizamani, kishamba na kihuni zisizopaswa kufumbiwa macho

Tumeeleza Kitila na Zitto walipaswa wajiuzulu nafasi zao kama hatua ya kwanza ya kupinga mambo yalivyo ndani ya chama chao. Hatua ya kwanza ilikuwa kuongea katika vikao na kama hawakupewa nafasi katika agenda wangeweka katika OAB. Hawakufanya chochote zaidi ya espionage na kwenda embe kiburugwa.

Hao akina Kafulila, Juliana Shonzo, Masalia ni sehemu ya mtandano wa watu hawa.
Soma bandiko la nyuma nimeeleza kwa undani ilianza vipi kwa Kafulila, ikahamia kwa akina Juliana.

Sakata la Juliana halikuwa kuhusu uongozi bali kauli ya Heche kwa Shibuda.
Ilikuwa timing ili kumuondoa Heche na Juliana ambaye ni 'mtu wao' achukue nafasi katika kujenga mtandao.
Sakata la Masalia lilikuwa na lengo la kumweka Zitto kama lilivyokuwa la Kafulila.

Masakata yote Zitto ametajwa. Huu mtandao wa waraka ilikuwa ni hatua nyingine ya kudhibiti habari kuvuja.
Ukisoma utaona wanasema 'watu waaminifu' wachache. Ni kwa bahati mbaya Mwigamba kauza silaha.

Hakuna kupuuza malalamiko yao lakini basi yaelezwe kwa lugha ya kidplomasia, yawe na maono na mipango,nidhamu, hekima,taratibu na si matusi na kejeli kama unavyousoma waraka.

Ni kutokana na kukosa mashiko wenyewe wameshindwa kuutetea waraka na kukimbilia kujiuzulu.
Soma waraka na utetezi wao uone kama kuna hoja.

Ndugu yangu Pasco, unafahamu kuanzia duru ilipoanza na ukweli upi nasimamia.
Wakati namkaanga Mbowe kuhusu Togwa na chaguzi ndogo, au Dr Slaa na msimamo wa Rwanda pamoja na ulege ulege nilionekana mwema, leo nasema ukweli kuhusu waraka nashutumiwa.
Uhuru unaniweka huru sana na nafurahia hilo.

Labda tukusikilize uje na habari nyingine mpya kwasababu tuhuma, shutuma na lawama tumezieleza vema tu.
Tumeuangalia waraka upside down na tunaendelea kuuangalia nukta hadi nyingine.

Mkuu Pasco kwani mwenzetu una lipi jipya utuhabarishe wanajamvi wenzako kuhusu timbwili hili? Karibu uwanjani
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3 Mchambuzi

Nakubaliana na uchambuzi wenu katika vipengele vyote kuhusiana na mapungufu kwenye huo waraka. Pia nakubaliana na nyie kwenye maeneo ambayo waraka umegusia ambapo kusingekuwa na nia mbaya, huenda hayo mapungufu yaliyoainishwa yangeweza kukisaidia zaidi chama katika kukijenga na kuonekana kwamba kinafaa kuongoza nchi.

Mimi binafsi ningependa kujikita katika maeneo mawili; Nini kitafuata baada ya siku 14 za akina Zitto kujieleza; na pili CDM ifanye nini katika kurudisha imani ya wananchi kama mbadala wa chama tawala.

Siku 14 za Zitto zikiisha
Mengi yameshasemwa na mengi yanategemewa kutoka kwenye pande zote mbili za huu mgogoro. Kama ambavyo Nguruvi3 alivyotanabahisha kwenye bandiko lake, ingawa busara haikutumika wakati wa kufanya maamuzi haya ya pupa na hasira ya kuwasimamisha uongozi, ni mategemeo yetu busara itatumika zaidi wakati wa kufanya maamuzi ya aidha kumbakishia au kumfukuza uanachama Zitto na wenzake.

Kwa maoni yangu, nafikiri namna pekee ya ku-handle hii situation kwa chama ni kumalizia walichokwisha kianza. Ni vyema kwa chama kuainisha makosa ya Zitto na wenzake, kuyaweka katika lugha nzuri inayoeleweka katika jamii, na kufuata taratibu za kikatiba na kikanuni kumvua uanachama. Nafahamu kutakuwa na wengi sana ambao watachukizwa na hayo maamuzi hasa hasa wale ambao ni wafuasi wa 'personalities' badala ya wafuasi wa chama lakini hiyo itakuwa ni namna pekee ya kulimaliza na kulizika kabisa hili tatizo. Kama itabidi chama kupoteza baadhi ya hao wafuasi, basi na iwe hivyo.
Kwa hili, litakifanya chama kuonekana kuwa na msimamo dhabiti katika kusimamia nidhamu katika chama na mimi binafsi nitakiamini kwamba kinaelekea kuonyesha kwamba kiko tayari kuongoza kitaasisi bila kuwa na woga na baadhi ya personalities.

Chama kifanye nini katika kurudisha imani ya wapenzi wake hasa hasa watakaokuwa wameumizwa na hayo maamuzi
Kwanza kabisa, chama kinatakiwa kijipange katika kujibu tuhuma zote zilizoelekezwa kwake kutoka kwenye huo waraka pamoja na hoja mbalimbali zilizojitokeza katika kipindi hiki. Naelewa mengi kati ya hayo mambo yaliyotamkwa kwenye waraka yanaweza kuhusishwa na propaganda za kuchafuana ili kugombea nafasi hiyo ya juu kwenye chama, lakini hizo hoja tayari zimeshaweka doa kwenye usafi wa chama. Wengi wa wapenzi wake wameanza kukiangalia chama kwa jicho la wasiwasi na hivyo basi, ni muhimu chama kuangalia namna ya kuzijibu hoja zote tena katika lugha inayoeleweka ikiambatanishwa na vielelzo mbalimbali ku-justify hoja zao.

Chama lazima kipitie muda wa kukaa kimya na kujitafakari. Matamko mbalimbali yakomeshwe na hata hiyo ziara ya katibu mkuu isimamishwe kwa muda. Pia iwape nafasi wapenzi na washabiki wake wajitafakari. Chama kinaweza kutumia kipindi hicho kujichunguza na kujiangalia kama kipo tayari katika kinyang’anyiro cha urais 2015. Wakati mwingine ni vyema kujikubali kwamba hauko tayari ili basi aina ya vita unayopigana uweze kuibadili. Chama kinaweza kubadili strategy ya badala ya kukimbilia ku-focus katika Urais, basi ijikite zaidi katika kuongeza viti vya madiwani na wabunge.

Chama lazima kijipange na namna ya kutoka upya na kusimama katika medani za kisiasa. Katika bandiko moja la Mchambuzi aligusia suala la kuhusisha vyama vingine vya upinzani katika umoja ambao ulionyesha mafanikio makubwa katika suala la katiba. CDM wanaweza hata kufikiria kuwahushisha baadhi ya wabunge wa vyama vingine vya upinzani katika kutengeneza baraza jipya la kivuli bungeni. Hilo la kujiunga na wengine linaweza kuipa tena presa ya kutosha CCM ambayo mpaka sasa pamoja na kelele zote inazopiga kuhusiana na hili Zitto, bado haijajielewa ni kwa namna gani linaweza kuwa na manufaa au likawa tatizo katika siasa zake.

Kuna mambo mengi sana ambayo yamegusiwa kwenye huo waraka ambayo yakifanyiwa kazi yanaweza kuwa na manufaa na kubadili aina ya siasa za chama. Chama kianze kutumia wasomi ili wakishauri namna nzuri zaidi ya kukoga nyoyo za watanzania katika siasa. Watanzania wanaonekana ni wapenzi wa siasa za matukio lakini tatizo ya siasa za namna hiyo huwa zinachuja mapema sana. Inabidi chama kiangalie ni aina gani za siasa ambazo zinaweza kukaaa kwenye mioyo wa watanzania kwa muda mrefu ni zikawasaidia katika kuchukua nchi. Mfano mzuri kabisa ni falsafa ya majimbo ambazo binafsi naona kwamba kama ikiweza kufikishwa vizuri kwa wananchi inaweza kuwa turufu nzuri sana katika uchaguzi. Inatakiwa iandaliwe katika lugha inayoeleweka na utaratibu ufanyike wa namna inavyoweza kunadiwa kwa wananchi ili na wenyewe waweze kuielewa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco wakati tunasubiri udurusu kurasa ili uje na yako, ningependa nizungumzie kidogo kuhusu aya ya mwisho.

kwani mwenzetu una lipi jipya utuhabarishe wanajamvi wenzako kuhusu timbwili hili? Karibu uwanjani
Mkuu Nguruvi3, kiukweli sina jipya ila nitakapokuja na maoni yangu, nitajikita zaidi kwenye contents na the motive behind watu kujificha uvunguni na kutaka kuhamisha kitanda huku mwenye kitanda chake akiwa kitandani kwa kudhani amelala, kumbe amejiegesha!.

Cha kwanza kabisa ambacho mimi nalia nacho na nimelia nacho tangu wale madiwani wa Arusha kutimuliwa, nikakumbushia kina Shonza walipotimuliwa, na nimetoa angalizo kabla Zito hajatimuliwa!.

Nchini kwetu tuna siasa na tuna katiba!. Siasa ni uwongo mwingi including just feelings, katiba ni sheria, taratibu na kanuni!.

Kosa kubwa la CCM ni kuingiza siasa kwenye katiba!.

Katiba iliweka wazi mipaka ya utumishi wa siasa na utumishi wa umma. Iliweka huru kila raia ana haki ya kushiriki uongozi tangu wa serikali za mitaa hadi serikali kuu!. Serikali ya CCM ikazipora haki hizo na kuzifungisha ndoa kisiasa kuwa ili ushiriki uongozi, lazima udhaminiwe na chama cha siasa!, na kuuingiza upuuzi huo ndani ya katiba yetu!.

Chadema kama chama mmbadala, kilitarajiwa kisiukumbatie huu upuuzi CCM kilioungiza kwenye katiba! kwa kuheshimu tofauti kati ya utumishi wa chama na utumishi umma.

Mtu akishadhaminiwa na chama kugombea nafasi fulani, mtu huyu anakuwa ni mteule wa chama na mtumishi wa chama, lakini akiisha shinda nafasi ile, sasa anabadilika na kuwa sio tena mtumishi wa chama bali ni mtumishi wa umma, waliomchagua sio tena wanachama wa chama chake bali ni umma wa Watanzania. Ukiisha chaguliwa, unakuwa ni over and above party lines, unakuwa ni mtumishi wa umma!, ni zaidi ya chama!. Nilipo sema Zitto kwa alipofikia ni zaidi ya Chadema!, watu humu walitamani kunirarua!.

Kitendo cha Chadema kuutumia upuuzi ule ule wa CCM kumuondoa mtumishi wa umma kwa faida za chama, nililalamika it was wrong!. Walipofanya upuuzi huo kwa wale madiwani, nililalamika it was wrong!. NCCR walipomtimua Kafulila nililalamika it was wrong!. CUF walipomtimua Hamad Rashid nililalamika it was wrong!.

Sasa Chadema wanataka kumtimua tena mtumishi mwingine wa umma kwa manufaa ya chama!, its wrong!.

Malalamiko yangu kuhusu upuuzi wa CCM kuingiza politics kwenye katiba, nimeupigia kelele sana humu tangu kesi ya Mtikila. Jaji Mkuu Agustino Ramadhani aliwawateua kina Kabudi, Mwaikusa na kuwa "Amicus Curiea" niliamini Mahakama Kuu ingeutengea ule ujinga wa kuichezea katiba kisiasa, na ili inawe mikono, ikamteua Prof. Kabudi ambaye ni kada wa CCM na Prof. Jwani Mwaikusa ambaye ni neutral, ili hatimaye waitendee haki katiba, kumbe wapi!.

Chadema kama chama kilichopigania katiba mpya kutokana na madudu ya katiba iliyopo, haiwezi kujastify kuyatumia madudu hayo hayo for its advantage!, japo its legal right but its morally wrong na consciously unthinkable!.
Pasco
 
Chadema kama chama kilichopigania katiba mpya kutokana na madudu ya katiba iliyopo, haiwezi kujastify kuyatumia madudu hayo hayo for its advantage!, japo its legal right but its morally wrong na consciously unthinkable!.
Pasco

Nakubaliana na wewe kabisa katika suala zima la mapungufu katika katiba yetu ya nchi especially katika hicho kipengele cha kumuondoa mtumishi wa umma kwa manufaa ya chama.

katika suala hili, naomba nitofautiane na wewe kidogo. Chama kinahitaji kuonekana kama ni taasisi yenye wafuasi wenye malengo yaliyo sawa. Ndani ya chama, ili kiweze kujiendesha, kuna umuhimu sana kanuni na taratibu zake ilizojiwekea ziweze kufuatwa.

Ikitokea kwa namna yoyote ile, mmojawapo wa wafuasi akawa tofauti kwenye malengo ya kuendesha hicho chama, lazima chama kijitenge naye ili kiweze ku-protect u-taasisi wake. Hilo ni suala la kawaida kabisa. Haitawezekana hata siku moja mtu ambaye amejipambanua kuwa tofauti na mtazamo mzima wa chama akaendelea kubaki na kukivunja chama na wanachama wakaendelea kumvumilia simply kwasababu wanaogopa kumuondoa mtumishi wa umma.

Nafikiri utaratibu mwafaka ulikuwa kwa huyo mtumishi wa umma, pindi atakapoona haendani na utaratibu wa chama alichonacho, ajiengue na kuanzisha chama chake au kujiunga na kile kinachoendana na maono yake.

Ningependa sana kufahamu mawazo yako ndugu yangu (kama wakubaliana kulikuwa na makosa makubwa kiutaratibu na kikanuni katika kuandaa na ku-execute huo waraka), wewe ungeshauri utaratibu gani wa kinidhamu ungefaa kufuatwa?
 
Nakubaliana na wewe kabisa katika suala zima la mapungufu katika katiba yetu ya nchi especially katika hicho kipengele cha kumuondoa mtumishi wa umma kwa manufaa ya chama.

katika suala hili, naomba nitofautiane na wewe kidogo. Chama kinahitaji kuonekana kama ni taasisi yenye wafuasi wenye malengo yaliyo sawa. Ndani ya chama, ili kiweze kujiendesha, kuna umuhimu sana kanuni na taratibu zake ilizojiwekea ziweze kufuatwa.

Ikitokea kwa namna yoyote ile, mmojawapo wa wafuasi akawa tofauti kwenye malengo ya kuendesha hicho chama, lazima chama kijitenge naye ili kiweze ku-protect u-taasisi wake. Hilo ni suala la kawaida kabisa. Haitawezekana hata siku moja mtu ambaye amejipambanua kuwa tofauti na mtazamo mzima wa chama akaendelea kubaki na kukivunja chama na wanachama wakaendelea kumvumilia simply kwasababu wanaogopa kumuondoa mtumishi wa umma.

Nafikiri utaratibu mwafaka ulikuwa kwa huyo mtumishi wa umma, pindi atakapoona haendani na utaratibu wa chama alichonacho, ajiengue na kuanzisha chama chake au kujiunga na kile kinachoendana na maono yake.

Ningependa sana kufahamu mawazo yako ndugu yangu (kama wakubaliana kulikuwa na makosa makubwa kiutaratibu na kikanuni katika kuandaa na ku-execute huo waraka), wewe ungeshauri utaratibu gani wa kinidhamu ungefaa kufuatwa?
Mkuu Ditto,
Chadema inatatizwa tuu na uchanga wa siasa!, kilichofanyika sii kigeni kabisa katika medani za kisiasa wala hakuna mapinduzi yoyote waraka ule ulitaka kuyapanga, bali pale walikuwa wanatengeneza a "winning coalition" na winning coalition zote siku zote huwa siri mpaka kipenga cha uchaguzi kinapopulizwa!.

Ule usiri umezidishwa na culture ya Chadema kwamba Uenyekiti huwa unatolewa kwa idhini ya kina "fulani", wakati uchaguzi wa ndani ulikuwa bado, mnajua maoni ya wengi ni kupendekeza fulani aendelee na nyinyi mmeyaona wazi mapungufu ya huyo fulani, hamuwezi kumzunguzia au hata kumshauri asigombee kwa sababu ameipata hiyo nafasi kwa sababu ya "fulani!", kinachofanyika siku zote kwa wenye mapenzi mema na chama kwa mustakabali wa kukipeleka kwenye ushindi 2015, kwanza wataandaa "a winning coalition" na watamtafuta mtu capable kuliko aliyepo ambaye angeweza kuwapatia ushindi 2015!, then wakimpata na akikubali wanamgroom kwa siri na hatua ya pili ilikuwa kutengeneza "a lobby group" ya siri ndani ya chama kumpatia uungwaji mkono!.

Uchaguzi wa ndani ikiisha tangazwa, yeye hatakimbilia fomu kabisa wala hata fanya kampeni yoyote ila achukue fomu last minute na kufanya a surprise ambush hivyo kuchaguliwa kihalali na sio kufanya mapinduzi yoyote kinyume cha katiba, kanuni na taratibu za Chadema!.

Mfano mimi niko Jimbo la Mdee, naujua uwezo wake, capabilities zake, strength na weaksneses zake na posibilities za kulitetea jimbo la Kawe kwa 2015. Tayari nimeishajua Mbatia akiwa stronger na akisupportiwa na CCM atajaribu tena kwa NCCR!, nimeishajua this time CCM haitafanya makosa, itamsimamisha a very strong candidate kama Joseph Kusanga, sasa mimi kama mwana Chadema wa jimbo hili, najua wazi kwa uwezo wa Mdee, hawezi kufua dafu kwa hao niliowataja, kuliko kulipoteza kabisa jimbo,ni heru tutafute mtu wa kutuleta ushindi!, tutachaguana kwa makini na kufanya silent internal search ya watu wetu wote waliokatika jimbo lile!, wanamuona jamaa mmoja anaitwa Pascal Mayalla ni strong and capable kutuletea ushindi kwa kumaliza Mbatia na kumbomoa Joseph Kusaga hata kama Clouds itapiga kampeni kutwa kucha kwa siko zote 90 za kampeni!. Tatizo Pascal Mayalla ana mambo yake na hana mpango wowote wa kugombea!. Inaandaliwa "a winning coalition" kwa siri, inamshawishi Pascal Mayalla akubali kugombea, akikubali ina mgroom kisirisiri bila kumwambia Mdee, uchaguzi ukitangazwa, Mdee atachukua fomu na Pascal Mayalla atachukua fomu!, by that time a lobby group inakuwa tayari imeishamtonya member wake kwenye vikao vya maamuzi!. Kwa vile Mdee ni incumbent of course ndie atakaepewa preference na vikao vya maamuzi, yule member wa lobby group atakieleza kikao cha maamuzi why Pascal Mayalla and not Halima Mdee, ataeleza ni kwa nini?!. Ikitokea mmoja wa ile "a winning coalition" au "the lobby group" akalikisha siri kwa Mdee, then Mdee anakiarifu chama kuwa ametaka kufanyiwa uhaini wa kupinduliwa na chama kikamsikiliza!, hiki kitakuwa ni chama cha ajabu kabisa kama ambavyo Chadema wanataka kutuaminisha kuhusu ule waraka!, pale hakuna uhani wowotw wala mapinduzi yoyote bali mabadiliko kwa afya ya chama!

Inaonekana Uenyekiti kwa Chadema ni copyright ya watu fulani fulani tuu!, kuuzungumzia na kupanga kugombea kwa mwingine yoyote ni "uhaini!!.

Kiukweli kumfukuza Zitto kutakuwa na matokeo hasi kwa Chadema as far as 2015 is concerned!. Chadema ina udhaifu mkubwa sana wa ukosefu wa "political tolarance!", na ikipita salama, viongozi wakuu wa Chadema lazima waende semina ya "managing political divesity", vingenevyo its neither 2015, nor 2020, labda 2025 by that time hao kina "fulani" would have long time been gone!.
Pasco.
 
Mkuu Ditto,
Chadema inatatizwa tuu na uchanga wa siasa!, kilichofanyika sii kigeni kabisa katika medani za kisiasa wala hakuna mapinduzi yoyote waraka ule ulitaka kuyapanga, bali pale walikuwa wanatengeneza a "winning coalition" na winning coalition zote siku zote huwa siri mpaka kipenga cha uchaguzi kinapopulizwa!.

Mkuu Pasco,
Kwenye uchanga wa kisiasa uko sahihi kabisa na katika uchanga huo sidhani kwamba ni sahihi kwa baadhi wanachama wake kuanza kuandaa hizo "winning coalitions" kwa usiri! CDM ndio imepata mafanikio makubwa lakini ultimate goal haijafikiwa ambayo ni kuchukua nchi.
Lakini lengo hilo haliwezi kufikiwa kukiwa na makundi ya aina yoyote ndani ya chama na hiyo mikakati ya wachache kuunda "coalition" lazima ingezaa makundi zaidi. Hebu fikiria ikiwa mpango wao ungefanikiwa na wakachukua usukani unafikiri kina Mbowe nao wangekaa kimya na kukubali matokeo hivi hivi tu bila kuleta mpasuko?

Hizi biashara za minyukano ya makundi wanaziweza CCM wenyewe sababu mwisho wa siku huwa wana uhakika wa ushindi kwa back up ya dola nyuma yao....CDM move za namna hii haziwafai na zitawaagharimu zaidi!
 
Last edited by a moderator:
Kaka Pasco

Kwenye suala la uchanga kisiasa, hilo naliafiki 100%. Lakini pia, chama hakiwezi kukua bila kupitia changamoto za aina hii. Changmoto za aina hii huwa na results za aina mbili, kuvuka salama na kuwa chama chenye mvuto zaidi kuliko ilivyokuwa hapo mwanzo; au kufa kibudu kama ilivyotokea kwa vyama vingine kama NCCR. Yote haya yatategemea zaidi busara na namna watakavyoweza kutatua huu mgogoro wao wa ndani. Lazima chama kipite kwenye tanuri hili la moto ili kiweze kujichuja na "makapi".

Katika suala la kutengeneza the "winning coalition", hilo nalo naliafiki lakini kwa kiasi kidogo. Sababu za kutofautiana na wewe ni hizi tatu;

  1. Siku zote kama utapanga haya mambo na yakabakia siri baina yenu, haitakuwa na shida. Lakini pia, kwavile inajulikana kwamba huo utaratibu sio wa kikanuni na kikatiba, lazima muandaaji ajiandae na consequences zozote zitakazotokea pindi hiyo siri ikaja kugundulika. Kwa kawaida mambo kama hayo yakitokea, utaratibu sahihi ni kurudi kwenye vitabu na kuangalia kanuni na taratibu zinasema nini kuhusiana na makosa ya aina hiyo. It is just a matter of principles!
  2. Utaratibu huo wa ushindi ulihusisha kutengeneza mtandao. Pamoja na nia njema ya kubadili uongozi wa juu wa chama kidemokrasia, huo utaratibu ungeletelezea uongozi mpya kuchaguliwa kutokana na matakwa ya watu wachache na sio wanachama wote kwa ujumla wao. Ni sawa na kuleta taratibu zisizo za kidemokrasia katika mwamvuli wa demokrasia. Hapo ndipo ingekuwa mwanzo wa mwisho wa hicho chama kwa maana kingegawanyika katika vipande viwili right away.
  3. Waraka huo ungeandaliwa kisomi zaidi, bila kutumia lugha chafu, zenye maudhi pamoja utaratibu ambao ungekuwa hauhusiani na kutengeneza mtandao ndani ya chama, mimi ningekuwa wa kwanza kuu-support. (hapa nakubaliana na ndugu yangu Nguruvi3 kwamba huu waraka naamini kabisa haujaandaliwa na wasomi).
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ditto,
Chadema inatatizwa tuu na uchanga wa siasa!, kilichofanyika sii kigeni kabisa katika medani za kisiasa wala hakuna mapinduzi yoyote waraka ule ulitaka kuyapanga, bali pale walikuwa wanatengeneza a "winning coalition" na winning coalition zote siku zote huwa siri mpaka kipenga cha uchaguzi kinapopulizwa!.

Ule usiri umezidishwa na culture ya Chadema kwamba Uenyekiti huwa unatolewa kwa idhini ya kina "fulani", wakati uchaguzi wa ndani ulikuwa bado, mnajua maoni ya wengi ni kupendekeza fulani aendelee na nyinyi mmeyaona wazi mapungufu ya huyo fulani, hamuwezi kumzunguzia au hata kumshauri asigombee kwa sababu ameipata hiyo nafasi kwa sababu ya "fulani!", kinachofanyika siku zote kwa wenye mapenzi mema na chama kwa mustakabali wa kukipeleka kwenye ushindi 2015, kwanza wataandaa "a winning coalition" na watamtafuta mtu capable kuliko aliyepo ambaye angeweza kuwapatia ushindi 2015!, then wakimpata na akikubali wanamgroom kwa siri na hatua ya pili ilikuwa kutengeneza "a lobby group" ya siri ndani ya chama kumpatia uungwaji mkono!.

Uchaguzi wa ndani ikiisha tangazwa, yeye hatakimbilia fomu kabisa wala hata fanya kampeni yoyote ila achukue fomu last minute na kufanya a surprise ambush hivyo kuchaguliwa kihalali na sio kufanya mapinduzi yoyote kinyume cha katiba, kanuni na taratibu za Chadema!.

Mfano mimi niko Jimbo la Mdee, naujua uwezo wake, capabilities zake, strength na weaksneses zake na posibilities za kulitetea jimbo la Kawe kwa 2015. Tayari nimeishajua Mbatia akiwa stronger na akisupportiwa na CCM atajaribu tena kwa NCCR!, nimeishajua this time CCM haitafanya makosa, itamsimamisha a very strong candidate kama Joseph Kusanga, sasa mimi kama mwana Chadema wa jimbo hili, najua wazi kwa uwezo wa Mdee, hawezi kufua dafu kwa hao niliowataja, kuliko kulipoteza kabisa jimbo,ni heru tutafute mtu wa kutuleta ushindi!, tutachaguana kwa makini na kufanya silent internal search ya watu wetu wote waliokatika jimbo lile!, wanamuona jamaa mmoja anaitwa Pascal Mayalla ni strong and capable kutuletea ushindi kwa kumaliza Mbatia na kumbomoa Joseph Kusaga hata kama Clouds itapiga kampeni kutwa kucha kwa siko zote 90 za kampeni!. Tatizo Pascal Mayalla ana mambo yake na hana mpango wowote wa kugombea!. Inaandaliwa "a winning coalition" kwa siri, inamshawishi Pascal Mayalla akubali kugombea, akikubali ina mgroom kisirisiri bila kumwambia Mdee, uchaguzi ukitangazwa, Mdee atachukua fomu na Pascal Mayalla atachukua fomu!, by that time a lobby group inakuwa tayari imeishamtonya member wake kwenye vikao vya maamuzi!. Kwa vile Mdee ni incumbent of course ndie atakaepewa preference na vikao vya maamuzi, yule member wa lobby group atakieleza kikao cha maamuzi why Pascal Mayalla and not Halima Mdee, ataeleza ni kwa nini?!. Ikitokea mmoja wa ile "a winning coalition" au "the lobby group" akalikisha siri kwa Mdee, then Mdee anakiarifu chama kuwa ametaka kufanyiwa uhaini wa kupinduliwa na chama kikamsikiliza!, hiki kitakuwa ni chama cha ajabu kabisa kama ambavyo Chadema wanataka kutuaminisha kuhusu ule waraka!, pale hakuna uhani wowotw wala mapinduzi yoyote bali mabadiliko kwa afya ya chama!

Inaonekana Uenyekiti kwa Chadema ni copyright ya watu fulani fulani tuu!, kuuzungumzia na kupanga kugombea kwa mwingine yoyote ni "uhaini!!.

Kiukweli kumfukuza Zitto kutakuwa na matokeo hasi kwa Chadema as far as 2015 is concerned!. Chadema ina udhaifu mkubwa sana wa ukosefu wa "political tolarance!", na ikipita salama, viongozi wakuu wa Chadema lazima waende semina ya "managing political divesity", vingenevyo its neither 2015, nor 2020, labda 2025 by that time hao kina "fulani" would have long time been gone!.
Pasco.


Asante Pasco, litakuwa suala la ajabu kama mtu atazungumzia tofauti na mtizamo huu kwa kile kinachoendelea CDM. Nadhani huu ndio mtizamo niuonao sahihi kuhus Waraka. Nionavyo, something must be done kuokoa "Uhai" wa Chadema. Ubaya wa Siasa ni kwamba wapiga kura hawana "all times permanent decision" linapokuja suala la mtu na Chama. Kwamba, wako wapiga kura wanaotumia mgombea na wengine wanatumia Chama na mawazo hayo yanabadilika kutegemea na muda unavyokwenda na matukio yanayopita baina ya kipindi husika na demographic and economic factors zinavyochenge . Na siku zote Siasa haina "mtiifu". Haya mambo CDM wayajue vema sana. Kwahiyo slogan ya kusema kuondoa wasio "watiifu" katika chama ni kitu ambacho falsafa yake haieleweki sawasawa.

Vyovyote iwavyo maamuzi ya kumtimua Zitto na hao wenzake yatakiathiri Chama tukiwa tunaelekea 2015 na hasa kutokana na baadhi ya watu wenye mitizamo kama huu wa Pasco (Yaani hawaoni "empirical and srong" evidence za kuwatia hatiani walioandika waraka ule, unless kama waraka ungekuwa unazungumzia mageuzi ya uongozi nje ya Demokrasia(mapinduzi)). Tuacheni siasa, na political propaganda katika hili, ni vema mlio karibu na CDM mshirikiane kukirejesha chama kwenye right track. Inatosha kuamini kwamba watanzania tulio wengi hatuna vyama lkn tuko serious kuona mabadiliko ya kisiasa ya kuingiza chama kingine zaidi ya hiki chama kilichopo madarakani. Kuyumba kwa CDM kilichoonyesha njia ya kuleta mabadiliko, ni hatua 100 nyuma katika kufikia lengo hilo. Tuliikosa fursa hii kwa NCCR, kwa CUF, si vema CDM nayo ikiipoteza, kwani athari zake ni hizo alizosema Pasco-itahitaji miaka mingi kwa watanzania kujenga trust kwa upinzani.


nguruvi3 umerejea kilichofanywa na CCM kwa Mansour na kukilinganisha na kilichofanywa na CDM kwa Zitto kwamba wote wana umaarufu unaolingana. Mwalimu wangu, rejea tena historia ya Mansour kabla hujamlinganisha hivyo. Lakini Pia tuelewe kwamba nguvu na uimara wa mwanasiasa wa Zanzibar ni ima kwa wananchi au kwa Serikali ya Muungano. Siasa za Zanzibar hata wewe Nguruvi3 ukisimama pale Kibandamaiti na kusema "tumeandika barua" ya Zanzibar Huru-basi jiandae kupewa wake hata 10 na siku hiyo unakuwa "mkombozi" wa watu wa Zanzibar na kuukwaa umaarufu. lakini Umaarufu wako huo hauna nafasi kama hauna backup ya Tanganyika. Pamoja na umaarufu huo kutoka kwa wapiga kura, ukitimuliwa hauna madhara yoyote kwa Chama (Chama hakitegemei watu). Hali hiyo kwa Tanganyika ni tofauti, kwani kukubalika kwa mtu kwa wananchi ni kete muhimu katika kujenga himaya yako ya kisiasa. Narudia tena, kaeni chini fikirieni kwa umakini. Siasa hazina "mtiifu" mumtafutaye, ni suala la kucheza na akili za watu kwa njia ya kuunganisha nguvu za wapiga kura kwa kutumia social, cultural and economic forces. Kitu ambacho CCM wanakijua vema.

Kama ni kosa limefanywa na CDM yenyewe kwa muda mrefu kwa kumpa nafasi zitto kubeba agenda za kitaifa na hivyo kujenga jina kwa jamii ya watu wengi sana Tanzania. Nijuavyo watanzania na siasa za matukio, ni wazi "uasi" wa Zitto nje ya Chama ni mkubwa kuliko ndani ya Chama. CDM walitakiwa watumie cold politics kumuondoa Zitto kwenye connection sio hii iliyoanzia kwenye mitandao.
 
Nguruvi3 Mchambuzi

Nakubaliana na uchambuzi wenu katika vipengele vyote kuhusiana na mapungufu kwenye huo waraka. Pia nakubaliana na nyie kwenye maeneo ambayo waraka umegusia ambapo kusingekuwa na nia mbaya, huenda hayo mapungufu yaliyoainishwa yangeweza kukisaidia zaidi chama katika kukijenga na kuonekana kwamba kinafaa kuongoza nchi.

Mimi binafsi ningependa kujikita katika maeneo mawili; Nini kitafuata baada ya siku 14 za akina Zitto kujieleza; na pili CDM ifanye nini katika kurudisha imani ya wananchi kama mbadala wa chama tawala.

Siku 14 za Zitto zikiisha
Mengi yameshasemwa na mengi yanategemewa kutoka kwenye pande zote mbili za huu mgogoro. Kama ambavyo Nguruvi3 alivyotanabahisha kwenye bandiko lake, ingawa busara haikutumika wakati wa kufanya maamuzi haya ya pupa na hasira ya kuwasimamisha uongozi, ni mategemeo yetu busara itatumika zaidi wakati wa kufanya maamuzi ya aidha kumbakishia au kumfukuza uanachama Zitto na wenzake.

Kwa maoni yangu, nafikiri namna pekee ya ku-handle hii situation kwa chama ni kumalizia walichokwisha kianza. Ni vyema kwa chama kuainisha makosa ya Zitto na wenzake, kuyaweka katika lugha nzuri inayoeleweka katika jamii, na kufuata taratibu za kikatiba na kikanuni kumvua uanachama. Nafahamu kutakuwa na wengi sana ambao watachukizwa na hayo maamuzi hasa hasa wale ambao ni wafuasi wa 'personalities' badala ya wafuasi wa chama lakini hiyo itakuwa ni namna pekee ya kulimaliza na kulizika kabisa hili tatizo. Kama itabidi chama kupoteza baadhi ya hao wafuasi, basi na iwe hivyo.
Kwa hili, litakifanya chama kuonekana kuwa na msimamo dhabiti katika kusimamia nidhamu katika chama na mimi binafsi nitakiamini kwamba kinaelekea kuonyesha kwamba kiko tayari kuongoza kitaasisi bila kuwa na woga na baadhi ya personalities.

Chama kifanye nini katika kurudisha imani ya wapenzi wake hasa hasa watakaokuwa wameumizwa na hayo maamuzi
Kwanza kabisa, chama kinatakiwa kijipange katika kujibu tuhuma zote zilizoelekezwa kwake kutoka kwenye huo waraka pamoja na hoja mbalimbali zilizojitokeza katika kipindi hiki. Naelewa mengi kati ya hayo mambo yaliyotamkwa kwenye waraka yanaweza kuhusishwa na propaganda za kuchafuana ili kugombea nafasi hiyo ya juu kwenye chama, lakini hizo hoja tayari zimeshaweka doa kwenye usafi wa chama. Wengi wa wapenzi wake wameanza kukiangalia chama kwa jicho la wasiwasi na hivyo basi, ni muhimu chama kuangalia namna ya kuzijibu hoja zote tena katika lugha inayoeleweka ikiambatanishwa na vielelzo mbalimbali ku-justify hoja zao.

Chama lazima kipitie muda wa kukaa kimya na kujitafakari. Matamko mbalimbali yakomeshwe na hata hiyo ziara ya katibu mkuu isimamishwe kwa muda. Pia iwape nafasi wapenzi na washabiki wake wajitafakari. Chama kinaweza kutumia kipindi hicho kujichunguza na kujiangalia kama kipo tayari katika kinyang'anyiro cha urais 2015. Wakati mwingine ni vyema kujikubali kwamba hauko tayari ili basi aina ya vita unayopigana uweze kuibadili. Chama kinaweza kubadili strategy ya badala ya kukimbilia ku-focus katika Urais, basi ijikite zaidi katika kuongeza viti vya madiwani na wabunge.

Chama lazima kijipange na namna ya kutoka upya na kusimama katika medani za kisiasa. Katika bandiko moja la Mchambuzi aligusia suala la kuhusisha vyama vingine vya upinzani katika umoja ambao ulionyesha mafanikio makubwa katika suala la katiba. CDM wanaweza hata kufikiria kuwahushisha baadhi ya wabunge wa vyama vingine vya upinzani katika kutengeneza baraza jipya la kivuli bungeni. Hilo la kujiunga na wengine linaweza kuipa tena presa ya kutosha CCM ambayo mpaka sasa pamoja na kelele zote inazopiga kuhusiana na hili Zitto, bado haijajielewa ni kwa namna gani linaweza kuwa na manufaa au likawa tatizo katika siasa zake.

Kuna mambo mengi sana ambayo yamegusiwa kwenye huo waraka ambayo yakifanyiwa kazi yanaweza kuwa na manufaa na kubadili aina ya siasa za chama. Chama kianze kutumia wasomi ili wakishauri namna nzuri zaidi ya kukoga nyoyo za watanzania katika siasa. Watanzania wanaonekana ni wapenzi wa siasa za matukio lakini tatizo ya siasa za namna hiyo huwa zinachuja mapema sana. Inabidi chama kiangalie ni aina gani za siasa ambazo zinaweza kukaaa kwenye mioyo wa watanzania kwa muda mrefu ni zikawasaidia katika kuchukua nchi. Mfano mzuri kabisa ni falsafa ya majimbo ambazo binafsi naona kwamba kama ikiweza kufikishwa vizuri kwa wananchi inaweza kuwa turufu nzuri sana katika uchaguzi. Inatakiwa iandaliwe katika lugha inayoeleweka na utaratibu ufanyike wa namna inavyoweza kunadiwa kwa wananchi ili na wenyewe waweze kuielewa.
Ditto,

Nakubaliana na hoja zako hapo juu. Tatizo lilipo ni kwamba wanaomuunga mkono zitto katika hili are nothing but "FANATICS" meaning - they are motivated by irrational enthusiasm and they will never change their mind and position in regards to the subject.

Zitto alifanikiwa sana kisiasa kutokana na aina yake ya uongozi, ujengaji wa hoja, uwezo wa kuchambua masuala yanayogusa jamii kisiasa na kiuchumi, uwezo wa kujieleza kwa lugha inayoeleweka kirahisi kwa mwananchi kutoka kada yoyoten kwa kiwango ambacho hakuna mwanasiasa ndani na nje ya ccm aliweza kukifikia. Kwa mwendo ule, taifa lilikuwa in the verge of getting kiongozi anayemkaribia mwalimu nyerere, na iwapo angekuwa mvumilivu, hakika angefika mbali. Ni kutokana na haya, ndio maana zitto alifanikiwa kufanya hata wanachama na baadhi ya viongozi ndani ya ccm kuwa "enthusiatic" - kwani walionyesha great excitment and interest kwa mwanasiasa huyu chipukizi. Nisisitize hapa kwamba naongelea baadhi ya viongozi wa ccm ambao ni "Rational Thinkers" - viongozi ambao hoja na mitazamo yao inaongozwa na intellect, na reasoning, na waliofanikiwa kutenganisha politics with private life. Binafsi nilikuwa najua wajumbe wachache wa kamati kuu (ccm) ambao walivutiwa sana na style of leadership ya zitto. Ni bahati mbaya yakaja mabadiliko katika kamati kuu husika ambapo sasa wakaletwa irrational figures na hawa wakaenda mbali ya wale rational thinkers ambapo, wakati the irrationals waliishia tu kumwa admire zitto na kutekeleza mengi ya anayojadili nje na ndani ya bunge at their different capacity kwa maslahi ya taifa, na inasemekama kwamba the irrationals wao wakaenda mbali na kuanza kumdanganya kwamba bila yeye hakuna chadema, huku baadhi wakimweleza kwamba wapo tayari hata kuhamia chadema ikiwa tu atatwaa uongozi wa chadema. Zitto ilitakiwa ajifunze kutoka NCCR kwani mapinduzi dhidi ya mabere marando yalifanikishwa na irrational thinkers pia kwa ahadi kwamba fulani akifanikiwa kumtoa katika uongozi, basi nccr itakamilika na wao watamfuata na kujenga chama.Mpaka leo hilo halijatokea na nccr kimebakia kuwa chama cha just a certain click.

Wanaomtetea zitto leo wana behave as if zitto ni independent candidate na kusahau kwamba anatokana na chama cha siasa chenye kanuni, taratibu na katiban vitu ambavyo ndio uongoza maamuzi na shughuli zote za chama. Binafsi nilikuwa mfuasi mzuri sana wa zitto lakini kwa vile ufuasi wangu hautokani na dhana ya independent candidate bali chama cha siasa chenye kanuni, taratibu na katiba, kwa manufaa ya kulinda na kujenga demokrasia yetu changa ndani ya taifa, siwezi kuwa upande wa zitto katika hili, hasa kwa vile I was not a fanatic bali follower katika misingi tajwa hapo juu. Na kwa vile hata zitto inasemekana alikubali ndani ya kikao cha cc kwamba ametenda kosa, this strengthens my position further from him on this controversy. Lakini haina maana kwamba zitto kapoteza uwezo wake kama kiongozi, bali ni amepotoka na kukosea, kwani ameenda kinyume na kanuni, taratibu na katiba za chama chake, hivyo kujitia doa. Nasema haya kwa vile, licha ya kuwa mwana ccm, naamini kwamba ukombozi wa wananchi walio wengi utatokana na aidha - kiongozi ndani ya ccm iliyoimarisha umakini kutokana na chadema kuwa madhubuti, au kiongozi huyu atatokana na chadema iliyoaminiwa na umma kuwa mbadala wa ccm katika uongozi wa taifa kutokana na ccm kukosa umakini, lakini iwe ni chadema ambayo viongozi wake wanatokana na kanuni, katiba na sheria ndani ya chama, na wanaosimamia kanuni hizo, kwani umakini wao katika hilo ndio utaaminisha umma kwamba kiongozi huyo ataweza kusimamia hayo ngazi ya taifa.

Mwisho, kuhusiana na nini kifanyike baada ya siku kumi na nne kumalizika, naungana mkono na wewe, lakini niongezee tu kwamba chadema kimvue uanachama zitto LAKINI kimpe nafasi ya kuomba tena uanachama wa chadema na kikae na kushauriana iwapo itafaa kumruhusu tena awe mwanachama au hapana. Asipoomba, hilo litakuwa ni kosa lake, na umma utaliona hivyo kwani kwa waraka ule, hiyo ni adhabu stahili kwa mujibu wa katiba ya chama chake. Sasa chadema isimamie hilo.

Nini itakuwa madhara yake? Umejadili vyema kuhusiana na 2015 kwani kuna dalili kwamba chadema wamejipanga sana kuingia ikulu 2015, na hata Mbowe alishasema na kunukuliwa na vyomba vya habari kwamba, Chadema isipochukua nchi, basi atajiuzulu siasa. Kwa kauli hii, iwapo maamuzi ya CC baada ya siku kumi na nne kupita yatalenga zaidi malengo ya chama 2015, hakika chadema watafunika kombe mwanaharamu wapite.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom