Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Mwisho, kuhusiana na nini kifanyike baada ya siku kumi na nne kumalizika, naungana mkono na wewe, lakini niongezee tu kwamba chadema kimvue uanachama zitto LAKINI kimpe nafasi ya kuomba tena uanachama wa chadema na kikae na kushauriana iwapo itafaa kumruhusu tena awe mwanachama au hapana. Asipoomba, hilo litakuwa ni kosa lake, na umma utaliona hivyo kwani kwa waraka ule, hiyo ni adhabu stahili kwa mujibu wa katiba ya chama chake. Sasa chadema isimamie hilo.

Nini itakuwa madhara yake? Umejadili vyema kuhusiana na 2015 kwani kuna dalili kwamba chadema wamejipanga sana kuingia ikulu 2015, na hata Mbowe alishasema na kunukuliwa na vyomba vya habari kwamba, Chadema isipochukua nchi, basi atajiuzulu siasa. Kwa kauli hii, iwapo maamuzi ya CC baada ya siku kumi na nne kupita yatalenga zaidi malengo ya chama 2015, hakika chadema watafunika kombe mwanaharamu wapite.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Nikubaliana nawe katika masuala mengi uliyobainisha kwenye post hii, lakini hapa kwenye conclusion yako, iko vema lakini sidhani kama itazingatiwa na pande mbili zote. Kwamba possibility ya CDM kumtimua (kumvua uanachama) Zitto ni kubwa sana kwani squad yote ya CDM haina mtizamo kuwa na compromise na Zitto katika hili lakini sioni dalili za Zitto kuomba tena uanachama iwapo atavuliwa uanachama. Kwasababu ukijaribu kumsoma Zitto katika maelezo yake, anaamini kwamba yeye ni "Innocent" katika haya yanayoendelea na kwamba kinachofanywa na CDM ni kama kutotothamini mchango wake katika Chama.

Hata hivyo, akitokea kufuata ushauri huu wa kuomba tena uanachama, in the short run atakuwa looser ingawa in a long run anaweza kuwa Hero wa Siasa za baadaye. Kwa upande mwingine, iwapo CDM kumtimua uanachama na kumpa nafasi ya kuomba tena na kaomba, in the short run, baadhi ya wana CDM watakuwa winners ingawa in the long run watakuwa looser. Binafsi naona ikitokea ametimuliwa, ni vema ajiondoe kwenye siasa(kama Lamwai), lakini hii ni option ambayo siioni kwake. Nasema hivyo ni kwasababu naamini kwamba back-up ya Zitto iko kutoka pande zote tatu, baadhi ya wana CDM, wana CCM na wasio na vyama ambao wanaamini Zitto "akikomaa" anaweza kuisaidia sana nchi, hivyo possibility ya kupata uteuzi wa kitendaji kutoka Taasisi za Umma au binafsi ni kubwa.
 
Ditto,

Nakubaliana na hoja zako hapo juu. Tatizo lilipo ni kwamba wanaomuunga mkono zitto katika hili are nothing but "FANATICS" meaning - they are motivated by irrational enthusiasm and they will never change their mind and position in regards to the subject.

Zitto alifanikiwa sana kisiasa kutokana na aina yake ya uongozi, ujengaji wa hoja, uwezo wa kuchambua masuala yanayogusa jamii kisiasa na kiuchumi, uwezo wa kujieleza kwa lugha inayoeleweka kirahisi kwa mwananchi kutoka kada yoyoten kwa kiwango ambacho hakuna mwanasiasa ndani na nje ya ccm aliweza kukifikia. Kwa mwendo ule, taifa lilikuwa in the verge of getting kiongozi anayemkaribia mwalimu nyerere, na iwapo angekuwa mvumilivu, hakika angefika mbali. Ni kutokana na haya, ndio maana zitto alifanikiwa kufanya hata wanachama na baadhi ya viongozi ndani ya ccm kuwa "enthusiatic" - kwani walionyesha great excitment and interest kwa mwanasiasa huyu chipukizi. Nisisitize hapa kwamba naongelea baadhi ya viongozi wa ccm ambao ni "Rational Thinkers" - viongozi ambao hoja na mitazamo yao inaongozwa na intellect, na reasoning, na waliofanikiwa kutenganisha politics with private life. Binafsi nilikuwa najua wajumbe wachache wa kamati kuu (ccm) ambao walivutiwa sana na style of leadership ya zitto. Ni bahati mbaya yakaja mabadiliko katika kamati kuu husika ambapo sasa wakaletwa irrational figures na hawa wakaenda mbali ya wale rational thinkers ambapo, wakati the irrationals waliishia tu kumwa admire zitto na kutekeleza mengi ya anayojadili nje na ndani ya bunge at their different capacity kwa maslahi ya taifa, na inasemekama kwamba the irrationals wao wakaenda mbali na kuanza kumdanganya kwamba bila yeye hakuna chadema, huku baadhi wakimweleza kwamba wapo tayari hata kuhamia chadema ikiwa tu atatwaa uongozi wa chadema. Zitto ilitakiwa ajifunze kutoka NCCR kwani mapinduzi dhidi ya mabere marando yalifanikishwa na irrational thinkers pia kwa ahadi kwamba fulani akifanikiwa kumtoa katika uongozi, basi nccr itakamilika na wao watamfuata na kujenga chama.Mpaka leo hilo halijatokea na nccr kimebakia kuwa chama cha just a certain click.

Wanaomtetea zitto leo wana behave as if zitto ni independent candidate na kusahau kwamba anatokana na chama cha siasa chenye kanuni, taratibu na katiban vitu ambavyo ndio uongoza maamuzi na shughuli zote za chama. Binafsi nilikuwa mfuasi mzuri sana wa zitto lakini kwa vile ufuasi wangu hautokani na dhana ya independent candidate bali chama cha siasa chenye kanuni, taratibu na katiba, kwa manufaa ya kulinda na kujenga demokrasia yetu changa ndani ya taifa, siwezi kuwa upande wa zitto katika hili, hasa kwa vile I was not a fanatic bali follower katika misingi tajwa hapo juu. Na kwa vile hata zitto inasemekana alikubali ndani ya kikao cha cc kwamba ametenda kosa, this strengthens my position further from him on this controversy. Lakini haina maana kwamba zitto kapoteza uwezo wake kama kiongozi, bali ni amepotoka na kukosea, kwani ameenda kinyume na kanuni, taratibu na katiba za chama chake, hivyo kujitia doa. Nasema haya kwa vile, licha ya kuwa mwana ccm, naamini kwamba ukombozi wa wananchi walio wengi utatokana na aidha - kiongozi ndani ya ccm iliyoimarisha umakini kutokana na chadema kuwa madhubuti, au kiongozi huyu atatokana na chadema iliyoaminiwa na umma kuwa mbadala wa ccm katika uongozi wa taifa kutokana na ccm kukosa umakini, lakini iwe ni chadema ambayo viongozi wake wanatokana na kanuni, katiba na sheria ndani ya chama, na wanaosimamia kanuni hizo, kwani umakini wao katika hilo ndio utaaminisha umma kwamba kiongozi huyo ataweza kusimamia hayo ngazi ya taifa.

Mwisho, kuhusiana na nini kifanyike baada ya siku kumi na nne kumalizika, naungana mkono na wewe, lakini niongezee tu kwamba chadema kimvue uanachama zitto LAKINI kimpe nafasi ya kuomba tena uanachama wa chadema na kikae na kushauriana iwapo itafaa kumruhusu tena awe mwanachama au hapana. Asipoomba, hilo litakuwa ni kosa lake, na umma utaliona hivyo kwani kwa waraka ule, hiyo ni adhabu stahili kwa mujibu wa katiba ya chama chake. Sasa chadema isimamie hilo.

Nini itakuwa madhara yake? Umejadili vyema kuhusiana na 2015 kwani kuna dalili kwamba chadema wamejipanga sana kuingia ikulu 2015, na hata Mbowe alishasema na kunukuliwa na vyomba vya habari kwamba, Chadema isipochukua nchi, basi atajiuzulu siasa. Kwa kauli hii, iwapo maamuzi ya CC baada ya siku kumi na nne kupita yatalenga zaidi malengo ya chama 2015, hakika chadema watafunika kombe mwanaharamu wapite.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Unaposema wanaomtetea Zitto are driven by irrational enthusiasm naona unanitupia madongo. Mtu akisoma posti zako ataelewa kuwa your insider katika masuala ya siasa za Tanzania. Unaelewa viongozi wa CCM wana fikra gani kuhusu CDM na vyama vingine vya kisiasa. Vilevile una uzalendo na nchi yako na unaona CDM ni changamoto nzuri kwa CCM na taifa.

Kwa upande wangu naangalia matatizo ya CDM, CCM, na vyama vingine bila kuwa na inside information. Hivyo sipo hapa kumtetea Zitto. Nipo hapa kuonyesha kuwa kuna kasoro katika misingi ya uendeshaji wa demokrasia ya kuiga. Migogoro ya Zitto na CDM hipo ndani ya CCM, CUF..............

Hivyo tatizo sio Zitto. Kwa mujibu wa posti yako, unakubali kuwa Zitto ni mzuri lakini sio mvumilivu. Kwanini mtu mzuri avumilie mediocracy. Uvumilivu wa mediocracy sio ndio umeifanya Tanzania kuwa ilipo?

Kwanini watu wafikirie kufanya mapinduzi ndani ya chama, wakati chama kina taratibu? Ubora wa utaratibu sio kuwepo bali kufuatwa.
 
Nikubaliana nawe katika masuala mengi uliyobainisha kwenye post hii, lakini hapa kwenye conclusion yako, iko vema lakini sidhani kama itazingatiwa na pande mbili zote. Kwamba possibility ya CDM kumtimua (kumvua uanachama) Zitto ni kubwa sana kwani squad yote ya CDM haina mtizamo kuwa na compromise na Zitto katika hili lakini sioni dalili za Zitto kuomba tena uanachama iwapo atavuliwa uanachama. Kwasababu ukijaribu kumsoma Zitto katika maelezo yake, anaamini kwamba yeye ni "Innocent" katika haya yanayoendelea na kwamba kinachofanywa na CDM ni kama kutotothamini mchango wake katika Chama.

Hata hivyo, akitokea kufuata ushauri huu wa kuomba tena uanachama, in the short run atakuwa looser ingawa in a long run anaweza kuwa Hero wa Siasa za baadaye. Kwa upande mwingine, iwapo CDM kumtimua uanachama na kumpa nafasi ya kuomba tena na kaomba, in the short run, baadhi ya wana CDM watakuwa winners ingawa in the long run watakuwa looser. Binafsi naona ikitokea ametimuliwa, ni vema ajiondoe kwenye siasa(kama Lamwai), lakini hii ni option ambayo siioni kwake. Nasema hivyo ni kwasababu naamini kwamba back-up ya Zitto iko kutoka pande zote tatu, baadhi ya wana CDM, wana CCM na wasio na vyama ambao wanaamini Zitto "akikomaa" anaweza kuisaidia sana nchi, hivyo possibility ya kupata uteuzi wa kitendaji kutoka Taasisi za Umma au binafsi ni kubwa.

Naungana nawe; mimi nadhani hii ni Litmus Test for Chadema kubaini iwapo umaarufu wake mbele ya umma unatokana na "personalities" au ni itikadi, sera, imani, kanuni na misingi ya chama, huku viongozi wake wakipimwa kwa jinsi gani wanasimamia masuala haya. Katika sakata husika, for sustainability ya chama today and beyond, wanaomuunga mkono zitto ilitakiwa watazame suala hili kitaasisi zaidi na sio vinginevyo, kwani kinyume chake ni kwamba support yao kwa chadema ni suala la msimu tu. Kuna haja ya uongozi wa sasa kuanza kubadilisha haya ili warithishe vizazi vijavyo chama kinachosimama kama taasisi.

Kuna suala lingine ambalo kidogo linanitatiza - na linahusiana na hoja yako kwamba attitude ya zitto ni kama vile kaonewa. Je, kwa maana hii ndio maana amekaa kimya anapoona wananchama katika maeneo mbalimbali wanaleta fujo kufuatia maamuzi ya kamati kuu, amechagua kukaa kimya? Hivi anaelewa jinsi gani ange score political mileage kwa kutoa onyo kali kwa wale wanaofanya vitendo vya uharibifu n.k? Je, kwa wale wataalamu wa masuala haya yanayohusiana na kamati kuu, maamuzi yake, siku kumi na nne za kujieleza n.k, ni busara kwa zitto kukaa kimya badala ya kukemea vurugu zinazoendelea?

Mwisho, naungana na wachangiaji kadhaa huko juu kwamba kwa sasa, uongozi wa chama ungesitisha ziara za viongozi mikoani. Lakini nadhani uongozi uliopo ni makini na unalijua hilo, na uamuzi wa kwenda mikoani ulilenga kwenda kupima upepo wa siasa, first hand, kufuatia maamuzi ya kamati kuu.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kuna suala lingine ambalo kidogo linanitatiza - na linahusiana na hoja yako kwamba attitude ya zitto ni kama vile kaonewa. Je, kwa maana hii ndio maana amekaa kimya anapoona wananchama katika maeneo mbalimbali wanaleta fujo kufuatia maamuzi ya kamati kuu, amechagua kukaa kimya? Hivi anaelewa jinsi gani ange score political mileage kwa kutoa onyo kali kwa wale wanaofanya vitendo vya uharibifu n.k? Je, kwa wale wataalamu wa masuala haya yanayohusiana na kamati kuu, maamuzi yake, siku kumi na nne za kujieleza n.k, ni busara kwa zitto kukaa kimya badala ya kukemea vurugu zinazoendelea?

Mwisho, naungana na wachangiaji kadhaa huko juu kwamba kwa sasa, uongozi wa chama ungesitisha ziara za viongozi mikoani. Lakini nadhani uongozi uliopo ni makini na unalijua hilo, na uamuzi wa kwenda mikoani ulilenga kwenda kupima upepo wa siasa, first hand, kufuatia maamuzi ya kamati kuu.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
[SIZE=3 [USER=5165]Mchambuzi[/USER], Zitto angefanya hivi iwapo tu angejiridhisha kwamba kuondolewa kwake uongozi na kutakiwa ajieleze ni sehemu ya "deterrence". Lakini likely ana idea kwamba hii si deterrence bali ni "indication" ya kutohitajika (sio kujirekebisha). Na hili kosa linafanywa na washabiki na baadhi ya viongozi wa CDM ambao kwa wanayoyahubiri kabla ya vikao ndio yanakuwa kweli; na pia pamoja na kutolewa maelezo kwamba hili suala limefungwa, lakini lingali linajadiliwa kwenye mikutano au forums za CDM-iwe kwa uwazi au kwa mafumbo. Katika hali kama hiyo, kwa vile mtaji wa wanasiasa ni watu, naye anakaa kimya ili kupima support aliyonayo. lakini vilevile, si wote wanaofanya hivyo ni supporters wazuri wa Zitto, la hasha, wengine wanatake advantage ili kuzorotesha CDM.

Hapa kwenye red, labda unisaidie kuelewa jambo moja. Hivi wapiga kura wote nchi yoyote ni "rational" and "rigid" kweli? Mi nionavyo kama wapiga kura hawana sifa hizo hivyo perception zao haziko constant.

Lakini pia Mchambuzi mimi niko na hypothesis kwamba vyama vya siasa hasa kutoka upinzani hususan Afrika zinategemea sana "candidacy" sio misingi ya chama. Ila chama tawala uimara wake unategemea misingi ya chama si "candidacy". Kwamba, CCM (chama tawala) inaweza ikamsimaisha "Kibajaji" jimbo la Temeke na akshinda lakini sio rahisi kwa CDM au CUF kumsimamisha "nowhere" then akashinda bali haina budi kumsimamisha mtu ambaye ni "perfect" kwa wapiga kura. Hiyo ikitokea itakuwa ni kiwango cha juu sana cha watu kukata tamaa ambapo kwa Tanzania naona hali haijafikia huko.

Fanya simple survey kwa nchi za kiafrika zilizofanikiwa kukiondoa au kukipa upinzani wa kweli chama Tawala kilikuwa na candidate ambao wananchi waliwaona wanaweza kukidhi matakwa yao. Nasema hivi kwasababu, chama kabala hakijashika nchi, yoote miongoni mwa sera na kadhalika is "theories" ambazo mpiga kura anashawishika kuamini theory hizo ikiwa zinaendana na mtu anayeelekea kuzitumia. Any' way, naomba kusaidiwa hapa.[/SIZE]
 
Last edited by a moderator:
Unaposema wanaomtetea Zitto are driven by irrational enthusiasm naona unanitupia madongo. Mtu akisoma posti zako ataelewa kuwa your insider katika masuala ya siasa za Tanzania. Unaelewa viongozi wa CCM wana fikra gani kuhusu CDM na vyama vingine vya kisiasa. Vilevile una uzalendo na nchi yako na unaona CDM ni changamoto nzuri kwa CCM na taifa.

Mkuu Zakumi,

Kwanza, mimi sio insider, lakini nikiri kwamba ninafahamiana na wajumbe kadhaa wa kamati kuu za CCM za huko nyuma (sio kamati kuu ya sasa).

Hoja yangu haikulenga 'kukutupia madongo' bali kueleza kwa hoja kwanini nadhani wanaomtetea zitto are driven by irrational enthusiasm, na nimejadili kwanini nasema hivyo. Nadhani ingekuwa busara kwa wale wote wanaopingana na hilo waje na counter arguments. Nguruvi3 amejitahidi sana kuomba upande huo wa hoja wajadili kwanini wanadhani zitto kaonewa, efforts zake zimeishia kuwa futile.

Kwa upande wangu naangalia matatizo ya CDM, CCM, na vyama vingine bila kuwa na inside information. Hivyo sipo hapa kumtetea Zitto. Nipo hapa kuonyesha kuwa kuna kasoro katika misingi ya uendeshaji wa demokrasia ya kuiga. Migogoro ya Zitto na CDM hipo ndani ya CCM, CUF..............

Tatizo linakuja pale ambapo zitto amekuwa ni sehemu ya uongozi wa chama chake kwa muda mrefu, anayeelewa kanuni, taratibu na sheria, hivyo alikuwa na nafasi to raise hoja juu ya mapungufu anayoona kwa mujibu wa taratibu, kanuni na katiba iliyopo ambayo aliapa kuisimama kama mwanachama na kiongozi ndani ya chama. Iwapo anakwama kufanikisha hilo, hivi kweli ni sahihi kwa mtu wa level yake kukubali kuwa sehemu ya mkakati ule mchafu (waraka)? Mimi nadhani angetumia njia nyingine ndani ya kanuni, taratibu na katiba ya chama chake kujaribu fanikisha anayotaka fanikisha, na hata angekwama, ange sustain heshima yake na kujenga mazingira ya kufanikiwa huko mbeleni as long as harakati zake zipo ndani ya katiba, kanuni na taratibu zilizowekwa na chama chake.

Hivyo tatizo sio Zitto. Kwa mujibu wa posti yako, unakubali kuwa Zitto ni mzuri lakini sio mvumilivu. Kwanini mtu mzuri avumilie mediocracy. Uvumilivu wa mediocracy sio ndio umeifanya Tanzania kuwa ilipo?

Kwa mujibu wa kamusi, mediocrity means "Ordinariness as a consequence of being average and not outstanding". Unaweza ukafafanua hili kidogo katika muktadha wa kilichojiri hivi karibuni ndani ya Chadema? Au una maana kwamba viongozi walipo Chadema ni Mediocre? Kama una maana hivyo, ni muhimu utambue kwamba neno mediocrity is relative, so you cant treat it in absolute sense - kwamba once Zitto snatches leadership, tatizo la mediocracy litatatuliwa. Kwa maana nyingine, yawezekana waliopo kwenye uongozi wa chama wakawa ni 'mediocre', lakini kwa vile neno hili ni relative, hata zitto akipata madaraka, wapo ambao watamuona ni mediocre.

Kwanini watu wafikirie kufanya mapinduzi ndani ya chama, wakati chama kina taratibu? Ubora wa utaratibu sio kuwepo bali kufuatwa.
Katika hili sijakuelewa vizuri, kwani inasomeka kama vile unapingana na intent ya waraka husika, wakati huko nyuma haujasomeka hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3 Mchambuzi

Nakubaliana na uchambuzi wenu katika vipengele vyote kuhusiana na mapungufu kwenye huo waraka. Pia nakubaliana na nyie kwenye maeneo ambayo waraka umegusia ambapo kusingekuwa na nia mbaya, huenda hayo mapungufu yaliyoainishwa yangeweza kukisaidia zaidi chama katika kukijenga na kuonekana kwamba kinafaa kuongoza nchi.

Mimi binafsi ningependa kujikita katika maeneo mawili; Nini kitafuata baada ya siku 14 za akina Zitto kujieleza; na pili CDM ifanye nini katika kurudisha imani ya wananchi kama mbadala wa chama tawala.

Siku 14 za Zitto zikiisha
Mengi yameshasemwa na mengi yanategemewa kutoka kwenye pande zote mbili za huu mgogoro. Kama ambavyo Nguruvi3 alivyotanabahisha kwenye bandiko lake, ingawa busara haikutumika wakati wa kufanya maamuzi haya ya pupa na hasira ya kuwasimamisha uongozi, ni mategemeo yetu busara itatumika zaidi wakati wa kufanya maamuzi ya aidha kumbakishia au kumfukuza uanachama Zitto na wenzake.

Kwa maoni yangu, nafikiri namna pekee ya ku-handle hii situation kwa chama ni kumalizia walichokwisha kianza. Ni vyema kwa chama kuainisha makosa ya Zitto na wenzake, kuyaweka katika lugha nzuri inayoeleweka katika jamii, na kufuata taratibu za kikatiba na kikanuni kumvua uanachama. Nafahamu kutakuwa na wengi sana ambao watachukizwa na hayo maamuzi hasa hasa wale ambao ni wafuasi wa 'personalities' badala ya wafuasi wa chama lakini hiyo itakuwa ni namna pekee ya kulimaliza na kulizika kabisa hili tatizo. Kama itabidi chama kupoteza baadhi ya hao wafuasi, basi na iwe hivyo.
Kwa hili, litakifanya chama kuonekana kuwa na msimamo dhabiti katika kusimamia nidhamu katika chama na mimi binafsi nitakiamini kwamba kinaelekea kuonyesha kwamba kiko tayari kuongoza kitaasisi bila kuwa na woga na baadhi ya personalities.

Chama kifanye nini katika kurudisha imani ya wapenzi wake hasa hasa watakaokuwa wameumizwa na hayo maamuzi
Kwanza kabisa, chama kinatakiwa kijipange katika kujibu tuhuma zote zilizoelekezwa kwake kutoka kwenye huo waraka pamoja na hoja mbalimbali zilizojitokeza katika kipindi hiki. Naelewa mengi kati ya hayo mambo yaliyotamkwa kwenye waraka yanaweza kuhusishwa na propaganda za kuchafuana ili kugombea nafasi hiyo ya juu kwenye chama, lakini hizo hoja tayari zimeshaweka doa kwenye usafi wa chama. Wengi wa wapenzi wake wameanza kukiangalia chama kwa jicho la wasiwasi na hivyo basi, ni muhimu chama kuangalia namna ya kuzijibu hoja zote tena katika lugha inayoeleweka ikiambatanishwa na vielelzo mbalimbali ku-justify hoja zao.

Chama lazima kipitie muda wa kukaa kimya na kujitafakari. Matamko mbalimbali yakomeshwe na hata hiyo ziara ya katibu mkuu isimamishwe kwa muda. Pia iwape nafasi wapenzi na washabiki wake wajitafakari. Chama kinaweza kutumia kipindi hicho kujichunguza na kujiangalia kama kipo tayari katika kinyang’anyiro cha urais 2015. Wakati mwingine ni vyema kujikubali kwamba hauko tayari ili basi aina ya vita unayopigana uweze kuibadili. Chama kinaweza kubadili strategy ya badala ya kukimbilia ku-focus katika Urais, basi ijikite zaidi katika kuongeza viti vya madiwani na wabunge.

Chama lazima kijipange na namna ya kutoka upya na kusimama katika medani za kisiasa. Katika bandiko moja la Mchambuzi aligusia suala la kuhusisha vyama vingine vya upinzani katika umoja ambao ulionyesha mafanikio makubwa katika suala la katiba. CDM wanaweza hata kufikiria kuwahushisha baadhi ya wabunge wa vyama vingine vya upinzani katika kutengeneza baraza jipya la kivuli bungeni. Hilo la kujiunga na wengine linaweza kuipa tena presa ya kutosha CCM ambayo mpaka sasa pamoja na kelele zote inazopiga kuhusiana na hili Zitto, bado haijajielewa ni kwa namna gani linaweza kuwa na manufaa au likawa tatizo katika siasa zake.

Kuna mambo mengi sana ambayo yamegusiwa kwenye huo waraka ambayo yakifanyiwa kazi yanaweza kuwa na manufaa na kubadili aina ya siasa za chama. Chama kianze kutumia wasomi ili wakishauri namna nzuri zaidi ya kukoga nyoyo za watanzania katika siasa. Watanzania wanaonekana ni wapenzi wa siasa za matukio lakini tatizo ya siasa za namna hiyo huwa zinachuja mapema sana. Inabidi chama kiangalie ni aina gani za siasa ambazo zinaweza kukaaa kwenye mioyo wa watanzania kwa muda mrefu ni zikawasaidia katika kuchukua nchi. Mfano mzuri kabisa ni falsafa ya majimbo ambazo binafsi naona kwamba kama ikiweza kufikishwa vizuri kwa wananchi inaweza kuwa turufu nzuri sana katika uchaguzi. Inatakiwa iandaliwe katika lugha inayoeleweka na utaratibu ufanyike wa namna inavyoweza kunadiwa kwa wananchi ili na wenyewe waweze kuielewa.
Ahsante sana. Ditto umezungumzia hoja nyingi kwa undani.
Nisitize kuwa CDM na viongozi wanaonekana kupata kimuhe muhe na kulikuza tatizo badala ya kutumia tatizo kujitahmini.

1. Nimewaambia ziara Slaa haziwezi kuwa kipimo kizuri kutokana na wakati na mazingira yaliyopo.

2. CDM ielewe kama sehemu ya 'nature' lazima itapita katika chujio fulani bila kupenda.
Mgogoro huu unaweza kutumika kama chujio la wenye nia ya mabadiliko na wale wanaofuata watu
Kwanini wasiachwe wakajichuja? Kwanini wasilione chujio hili? Nani alijua kuwa mshauri wa chama ni msalaiti pia, nature ndio imeleta yote na kila siku wanazidi kujitokeza. Tumesikia brigedia zikianza kazi na wengine kujiuzulu. Hilo si jambo baya kama litafanyiwa kazi kwasababu ni majibu ya tatizo yaliyokuwa hayajulikani au hayaonekani.

Nimetoa mfano, mwenyekiti wa Singida amejivunia rekodi yake ya kuwa mawanachama wa 300 wa CDM na wa 1 mkoani Singida. Rekodi nzuri eh! Lakini angalia miaka 20 CDM haina sanduku la barua, miaka 20 CDM haina ofisi Singida.

Juzi kajiuzulu, kwanini CDM wadhani ni kudhoofika kwa chama na wala si fursa ya kupata mtu wa kukisogeza zaidi baada ya mika 20 ya kudumaa!

3. Nimewaambia CDM kuwa yapo ya kujitahmini ambayo wanatakiwa wajiulize yanatoa picha gani kwa jamii.
Tuhuma za mwenyekiti kuwa na conflict of interest za supply ni nzito na wanapaswa waziangalie.

Si tu waziangalie bali watafute mbadala wa uwazi utakaondoa wasi wasi. Jambo limesemwa sana ni wakati wakalifanyia kazi.

4. Kutokana na hali iliyopo kuna mistrust kubwa sana miongoni mwa watendaji. Wapo watakaogopa kutoa mawazo kwa kuhofiwa kuhusishwa na waraka wa embe kivurugwa. Wapo watakao toa kwa hasira za 'sterling' wao kuondolewa.
Wapo wasiotambua nini kinaendelea.
Wakati wanasbiri uchaguzi lazima wafanaye 'reset' ya haraka kujenga imani tena.
 
Last edited by a moderator:
[SIZE=3 [USER=5165]Mchambuzi[/USER], Zitto angefanya hivi iwapo tu angejiridhisha kwamba kuondolewa kwake uongozi na kutakiwa ajieleze ni sehemu ya "deterrence". Lakini likely ana idea kwamba hii si deterrence bali ni "indication" ya kutohitajika (sio kujirekebisha).


Umenielewesha kuhusiana na jambo muhimu sana, lakini unaniacha na maswali kuliko majibu. Kwa mfano, iwapo ni kweli zitto anajua uongozi wa chama haumuhitaji kama ulivyojadili, je:

*Lini alituambia hilo na alifanya nini kufuatana na katiba, kanuni na taratibu za chama?
*Je sababu zake kutotakiwa na uongozi wa chama msingi wake ni nini- zinalenga kujenga chama au kubomoa chama?
*Katika hoja za kutomtaka ndani ya chama, ni hoja zipi yeye ndie chanzo (kwa ushahidi) na ni hoja zipi yeye anaonewa (kwa ushahidi)?
*Je, katika hoja ambazo kaonewa, kuna ushahidi kwamba alitumia taratibu, katiba, na kanuni kupambana nazo?

Na hili kosa linafanywa na washabiki na baadhi ya viongozi wa CDM ambao kwa wanayoyahubiri kabla ya vikao ndio yanakuwa kweli; na pia pamoja na kutolewa maelezo kwamba hili suala limefungwa, lakini lingali linajadiliwa kwenye mikutano au forums za CDM-iwe kwa uwazi au kwa mafumbo.
Ni kweli lakini tatizo hili lipo kwenye vyama vyote (including ccm), but it doesn't justify anything badala yake ni ushahidi kwamba siasa zetu katika zama hizi zimevamiwa na watu wasiostahili kuitwa viongozi.
Katika hali kama hiyo, kwa vile mtaji wa wanasiasa ni watu, naye anakaa kimya ili kupima support aliyonayo. lakini vilevile, si wote wanaofanya hivyo ni supporters wazuri wa Zitto, la hasha, wengine wanatake advantage ili kuzorotesha CDM.
So hapa una maana kwamba mkakati wa zitto hivi sana ni kutafuta mtaji wa siasa kufuatia maamuzi ya kamati kuu badala ya to reconcile? Nijirudie tu kusema ushauri wangu kwa zitto ni kuanza kukemea machafuko yanayojitokeza mikoani, na ikibidi, aombe kuzunguka nchi nzima na uongozi wa chama kwenda kuomba reconciliation na aseme kwamba kwa vile alishasema ana mpango wa kwenda kufundisha chuo na kupumzika siasa, atafanya hivyo na kubakia kuwa mwanachama mwaminifu ambae atatumia muda wake mwingi kujenga chama kwa njia ambazo hazihitaji media kuonekana anafanya hivyo; kisha apumzike siasa kwa miaka kadhaa kama alivyosikika akitamka, na arudi katika siasa kwa wito huko mbeleni. Kitendo cha kuhama chadema kwenda hata chama kipya kabisa itakuwa ndio mwisho wake kisiasa kwani tafsiri itakuwa "anapenda maradaka kuliko suala lingine lolote"

Hapa kwenye red, labda unisaidie kuelewa jambo moja. Hivi wapiga kura wote nchi yoyote ni "rational" and "rigid" kweli? Mi nionavyo kama wapiga kura hawana sifa hizo hivyo perception zao haziko constant.
Kuwa rational maana yake ni kuongozwa na reasoning yenye intellect (capacity for rational thought), sio kuwa emotional. Tofauti na hii, wengi wanaomuunga mkono zitto katika hili kwa bahati mbaya wanaongozwa na EMOTIONS ambazo wanajaribu kuzijengea reasoning bila without scoring anything meaningful.

Lakini pia Mchambuzi mimi niko na hypothesis kwamba vyama vya siasa hasa kutoka upinzani hususan Afrika zinategemea sana "candidacy" sio misingi ya chama. Ila chama tawala uimara wake unategemea misingi ya chama si "candidacy".

Niungane na wewe katika hili, lakini vyama vyote vya siasa including ccm vimetokea huko. Hata demokrasia kubwa kama marekani, personalities zina sehemu yake - mfano the kennedies, clintons, obama, lakini tofauti yao na sisi ni kwamba - katika ratio baina ya personalities and issues, ni issues ndio zina dominate, hasa jinsi personalities zinavyojengea hoja issues husika, sisi ni the other way round;
Kwamba, CCM (chama tawala) inaweza ikamsimaisha "Kibajaji" jimbo la Temeke na akshinda lakini sio rahisi kwa CDM au CUF kumsimamisha "nowhere" then akashinda bali haina budi kumsimamisha mtu ambaye ni "perfect" kwa wapiga kura. Hiyo ikitokea itakuwa ni kiwango cha juu sana cha watu kukata tamaa ambapo kwa Tanzania naona hali haijafikia huko.

U think so? I would say kwamba moja ya mafanikio ya chadema leo ni kwamba katika maeneo mengi sana ya Tanganyika, ukifanyika uchaguzi wa jimbo, odds baina na ccm na chadema ni almost 50:50. Na ccm inalijua leo. Kinana ana akili sana, his theme akizunguka mikoani sasa hivi anawaambiwa wananchi kwamba ccm ilikosea, ilifanya maamuzi ya kipumbavu katika maeneo kadhaa, inaomba second chance. Huu ndio uongozi ambao chama haukuwa nao kwa muda mrefu sana - uongozi unaokubali mapungufu. Mkakati huu utaigharimu sana chadema majimbo 2015 iwapo hawatakuwa makini.
Fanya simple survey kwa nchi za kiafrika zilizofanikiwa kukiondoa au kukipa upinzani wa kweli chama Tawala kilikuwa na candidate ambao wananchi waliwaona wanaweza kukidhi matakwa yao. Nasema hivi kwasababu, chama kabala hakijashika nchi, yoote miongoni mwa sera na kadhalika is "theories" ambazo mpiga kura anashawishika kuamini theory hizo ikiwa zinaendana na mtu anayeelekea kuzitumia. Any' way, naomba kusaidiwa hapa.[/SIZE]
Nakubaliana na wewe lakini nadhani tatizo ni kwamba wananchi wana tabia to reward political positions kwa wagombea based on what they offer prior to electing them into office (rushwa), not based on what candidates promise once they get elected (policies and good use of tax payers money).wenzetu nje practice the latter.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3, Kosa kubwa la CCM ni kuingiza siasa kwenye katiba!.
Katiba iliweka wazi mipaka ya utumishi wa siasa na utumishi wa umma. Iliweka huru kila raia ana haki ya kushiriki uongozi tangu wa serikali za mitaa hadi serikali kuu!. Serikali ya CCM ikazipora haki hizo na kuzifungisha ndoa kisiasa kuwa ili ushiriki uongozi, lazima udhaminiwe na chama cha siasa!, na kuuingiza upuuzi huo ndani ya katiba yetu!.

Chadema kama chama mmbadala, kilitarajiwa kisiukumbatie huu upuuzi CCM kilioungiza kwenye katiba! kwa kuheshimu tofauti kati ya utumishi wa chama na utumishi umma.

Mtu akishadhaminiwa na chama kugombea nafasi fulani, mtu huyu anakuwa ni mteule wa chama na mtumishi wa chama, lakini akiisha shinda nafasi ile, sasa anabadilika na kuwa sio tena mtumishi wa chama bali ni mtumishi wa umma, waliomchagua sio tena wanachama wa chama chake bali ni umma wa Watanzania.

Ukiisha chaguliwa, unakuwa ni over and above party lines, unakuwa ni mtumishi wa umma!, ni zaidi ya chama!. Nilipo sema Zitto kwa alipofikia ni zaidi ya Chadema!, watu humu walitamani kunirarua!.

Kitendo cha Chadema kuutumia upuuzi ule ule wa CCM kumuondoa mtumishi wa umma kwa faida za chama, nililalamika it was wrong!. Walipofanya upuuzi huo kwa wale madiwani, nililalamika it was wrong!. NCCR walipomtimua Kafulila nililalamika it was wrong!. CUF walipomtimua Hamad Rashid nililalamika it was wrong!.
Sasa Chadema wanataka kumtimua tena mtumishi mwingine wa umma kwa manufaa ya chama!, its wrong!.Pasco
Pasco nakubaliana kabisa na hoja yako. Hata hivyo unachotaka kusema ni kuwa Zitto asichuliwe hatua kama Mbunge. Hili ni neno kutokana na hoja zako. Lakini huko nyuma umesema Zitto asiondolewe naibu KUB kutokana na kuwa mwanachama wa kambi ya upinzani ambayo inaundwa na CDM. Naona unakwenda mbele unarudi nyuma, nadhani katika jitihada za kumsaidia Zitto kila jambo litasemwa. Nakubaliana na hoja yako ya awali hapo juu, natatizika unavyolifanya. Unataka Zitto awe Yard stick, lakini CDM wamemwacha Shibuda pia, kwanini Shibuda asiwe yard stick?

Nadhani tatizo si CDM au CCM ni sisi wananchi ambao tumekubali kuwapa haki ya kuamua nini tunataka na sisi kujiamulia nini tunataka.
 
Mkuu Zakumi,

Kwanza, mimi sio insider, lakini nikiri kwamba ninafahamiana na wajumbe kadhaa wa kamati kuu za CCM za huko nyuma (sio kamati kuu ya sasa).

Hoja yangu haikulenga 'kukutupia madongo' bali kueleza kwa hoja kwanini nadhani wanaomtetea zitto are driven by irrational enthusiasm, na nimejadili kwanini nasema hivyo. Nadhani ingekuwa busara kwa wale wote wanaopingana na hilo waje na counter arguments. Nguruvi3 amejitahidi sana kuomba upande huo wa hoja wajadili kwanini wanadhani zitto kaonewa, efforts zake zimeishia kuwa futile.



Tatizo linakuja pale ambapo zitto amekuwa ni sehemu ya uongozi wa chama chake kwa muda mrefu, anayeelewa kanuni, taratibu na sheria, hivyo alikuwa na nafasi to raise hoja juu ya mapungufu anayoona kwa mujibu wa taratibu, kanuni na katiba iliyopo ambayo aliapa kuisimama kama mwanachama na kiongozi ndani ya chama. Iwapo anakwama kufanikisha hilo, hivi kweli ni sahihi kwa mtu wa level yake kukubali kuwa sehemu ya mkakati ule mchafu (waraka)? Mimi nadhani angetumia njia nyingine ndani ya kanuni, taratibu na katiba ya chama chake kujaribu fanikisha anayotaka fanikisha, na hata angekwama, ange sustain heshima yake na kujenga mazingira ya kufanikiwa huko mbeleni as long as harakati zake zipo ndani ya katiba, kanuni na taratibu zilizowekwa na chama chake.



Kwa mujibu wa kamusi, mediocrity means "Ordinariness as a consequence of being average and not outstanding". Unaweza ukafafanua hili kidogo katika muktadha wa kilichojiri hivi karibuni ndani ya Chadema? Au una maana kwamba viongozi walipo Chadema ni Mediocre? Kama una maana hivyo, ni muhimu utambue kwamba neno mediocrity is relative, so you cant treat it in absolute sense - kwamba once Zitto snatches leadership, tatizo la mediocracy litatatuliwa. Kwa maana nyingine, yawezekana waliopo kwenye uongozi wa chama wakawa ni 'mediocre', lakini kwa vile neno hili ni relative, hata zitto akipata madaraka, wapo ambao watamuona ni mediocre.


Katika hili sijakuelewa vizuri, kwani inasomeka kama vile unapingana na intent ya waraka husika, wakati huko nyuma haujasomeka hivyo.

The framing of the thread didn't exhort us to take positions. Kwanini katikati ya mjadala tunaombwa kutoa counter argurments?

Vilevile mpaka sasa waraka uliotumika hapa haujathibitishwa kuwa ni waraka wenyewe. Kwanini tutoe counter arguments wakati hatuna uhakika na waraka wenyewe? Vilevile hatujui kwa kiwango gani Zitto alishiriki katika kuuandika.
Vilevile hii sio isolated case. Wiki mbili kabla ya kutolewa kwa waraka, kulikuwa na mijadala mbalimbali ndani ya CDM kuonyesha kuwa mambo hayakuwa swari. Haiwezekani watu kutuletea matumizi ya ZZK wiki hii na wiki inayofuatia waraka.

Kuhusiana na katiba, a constitution is only as good as the people who follow it. Kula kiapo is just a commentary. Ndio Zitto ana makosa kutofuata katiba. Lakini waliomwachia kuendelea kufanya makosa nao wana makosa. Kwa mujibu Zitto ana makosa 11 ambayo kayafanya kwa vipindi tofauti.

Kuhusiana na matumizi ya mediocracy. Katika posti yake moja, Kichuguu alisema kuwa miaka ya chama kimoja, wasomi wengi hawakujiingiza kwenye mambo ya siasa. Matokeo yake ni siasa za Tanzania kutawaliwa na wajanja wajanja (mediocre). Huu ni utamaduni tuliojijengea na umeendelea katika mfumo wa vyama vingi. Na katika mjadala huu, kuna watu wanaokubali umoja wa CDM hili kuindoa CCM mwaka 2015 japokuwa gharama za umoja huo is to preserve mediocrity.

Ki takwimu, viongozi wa CDM au CCM ni taswira ya watanzania. Hivyo mabadiliko ya uongozi ya 2015 yatatokea pale watakaochukua nafasi hiyo kuhamua kufanya vitu above the average. Kwa sasa hivi, CCM and CDM wanafanya vitu vilevile. Tofauti ni kuwa CCM wapo madarakani na CDM ni wapinzani.
 
Zinedine;8007834]Asante Pasco, litakuwa suala la ajabu kama mtu atazungumzia tofauti na mtizamo huu kwa kile kinachoendelea CDM. Nadhani huu ndio mtizamo niuonao sahihi kuhus Waraka.

Vyovyote iwavyo maamuzi ya kumtimua Zitto na hao wenzake yatakiathiri Chama tukiwa tunaelekea 2015 na hasa kutokana na baadhi ya watu wenye mitizamo kama huu wa Pasco (Yaani hawaoni "empirical and srong" evidence za kuwatia hatiani walioandika waraka ule, unless kama waraka ungekuwa unazungumzia mageuzi ya uongozi nje ya Demokrasia(mapinduzi)). Tuacheni siasa, na political propaganda katika hili, ni vema mlio karibu na CDM mshirikiane kukirejesha chama kwenye right track.

Inatosha kuamini kwamba watanzania tulio wengi hatuna vyama lkn tuko serious kuona mabadiliko ya kisiasa ya kuingiza chama kingine zaidi ya hiki chama kilichopo madarakani. Kuyumba kwa CDM kilichoonyesha njia ya kuleta mabadiliko, ni hatua 100 nyuma katika kufikia lengo hilo. Tuliikosa fursa hii kwa NCCR, kwa CUF, si vema CDM nayo ikiipoteza, kwani athari zake ni hizo alizosema Pasco-itahitaji miaka mingi kwa watanzania kujenga trust kwa upinzani.
Ahsante
nguruvi3 umerejea kilichofanywa na CCM kwa Mansour na kukilinganisha na kilichofanywa na CDM kwa Zitto kwamba wote wana umaarufu unaolingana. Mwalimu wangu, rejea tena historia ya Mansour kabla hujamlinganisha hivyo. Lakini Pia tuelewe kwamba nguvu na uimara wa mwanasiasa wa Zanzibar ni ima kwa wananchi au kwa Serikali ya Muungano. Siasa za Zanzibar hata wewe Nguruvi3 ukisimama pale Kibandamaiti na kusema "tumeandika barua" ya Zanzibar Huru-basi jiandae kupewa wake hata 10 na siku hiyo unakuwa "mkombozi" wa watu wa Zanzibar na kuukwaa umaarufu. lakini Umaarufu wako huo hauna nafasi kama hauna backup ya Tanganyika. Pamoja na umaarufu huo kutoka kwa wapiga kura, ukitimuliwa hauna madhara yoyote kwa Chama (Chama hakitegemei watu). Hali hiyo kwa Tanganyika ni tofauti, kwani kukubalika kwa mtu kwa wananchi ni kete muhimu katika kujenga himaya yako ya kisiasa. Narudia tena, kaeni chini fikirieni kwa umakini. Siasa hazina "mtiifu" mumtafutaye, ni suala la kucheza na akili za watu kwa njia ya kuunganisha nguvu za wapiga kura kwa kutumia social, cultural and economic forces. Kitu ambacho CCM wanakijua vema
Mimi nisingependa vyama vya siasa viwe na watu watiifu. Ningependa vyama viwe na watu wenye maono na mipango hata kama inatofautiana.
Sipendi watiifu lakini sipendi zaidi wanafiki, wachochezi na wafitini kwasababu hawana definition yoyote nzuri ya kuwa fit katika vyama vya siasa.

Kuhusu Mansour, nikupe mfano mmoja kuwa sisimizi mmoja ndani ya sikio ni bughudha kubwa kuliko mafahali wawili ndani ya zizi ya ng'ombe. Mansour ana ushaiwishi sana katika siasa za Zanzibar. CCM walimuona kama kikwazo na kuamua kumchinjilia baharini. Wakati wanakamata kisu mashabiki walikuwa wanapiga kelele za achinjwe, achinje kwa jina la demokrasia. Tena mashabiki wa CCM.
Wengine tukasema Mansour hana kosa ana mitazamo tofauti na ni kosa kumvua uanachama.

Leo kisu kile kile che nembo ya demokrasia kimekamatwa na CDM mashabiki wanapiga kelele, muuaji, uonevu, haki za binadamua n.k. Hoja hiyo imeshikiwa bango kana kwamba demokrasia imekuja katika maboksi kila mtu ana lake. Ninachosema ni kuwa kosa la Zitto na waraka wa Embe kiburugwa haliwezi kulingana na la Mansour.
Adhabu ya Mansour ni kali kwa kuwa muwazi kueleza mawazo yake, vipi huyu aliyejificha akitumia watu mitandaoni adhabu yake inapaswa kuwaje? Na kwanini CCM wale wale walitumia kisu brand ya demokrasia leo wanaona kisu kile ni butu CDM wakitaka kukitumia? Kuna nini hapo ? Why Zidane.
Kama ni kosa limefanywa na CDM yenyewe kwa muda mrefu kwa kumpa nafasi zitto kubeba agenda za kitaifa na hivyo kujenga jina kwa jamii ya watu wengi sana Tanzania.

Nijuavyo watanzania na siasa za matukio, ni wazi "uasi" wa Zitto nje ya Chama ni mkubwa kuliko ndani ya Chama. CDM walitakiwa watumie cold politics kumuondoa Zitto kwenye connection sio hii iliyoanzia kwenye mitandao
Kosa zaidi ni pale CDM walipopewa maonyo kuhusu Zitto. Ushiriki wake katika mapinduzi ni wa kiwango cha kuridhisha sana. Hakuna jaribio la mapinduzi ya vurugu lililowahi kufanyika CDM bila Zitto kuhusishwa, hakuna!

Kwa ujanja wa Zitto yeye anabeba agenda halafu anatuma vijana kuvuruga mambo ili apake masizi upande mmoja upande mwingine aking'aa. Huyu hafai.

Ni ujanja huo huo aliutumia kuwatuhumu Barrick na kuwa kinara wa agenda ya ufisadi umma ukimwamini.
Kama alivyomtumia Juliana, Kafulila na Masalia kuleta vurugu, Zitto akawatumia halmashauri ya wilaya ya jimbo lake kujenga shule katika jimbo kwa kutumia Mlungula a.k.a Rushwa kwa kupokea milioni 10 kutoka Barrick.

Ndivyo aanavyotudanganya kuwa hakuhusika na kuandika waraka, wakati tunajua ametekeleza mambo yaliyomo katika waraka tena hadharani kabisa.

Huyu mtu CDM wamemlea leo wanavuna walichopanda.
Sasa umaarufu wa Masour na Zitto unaweza kuwa tofauti kwa hoja za hapo juu, mmo
 
The framing of the thread didn't exhort us to take positions. Kwanini katikati ya mjadala tunaombwa kutoa counter argurments?

Vilevile mpaka sasa waraka uliotumika hapa haujathibitishwa kuwa ni waraka wenyewe. Kwanini tutoe counter arguments wakati hatuna uhakika na waraka wenyewe? Vilevile hatujui kwa kiwango gani Zitto alishiriki katika kuuandika.
Vilevile hii sio isolated case. Wiki mbili kabla ya kutolewa kwa waraka, kulikuwa na mijadala mbalimbali ndani ya CDM kuonyesha kuwa mambo hayakuwa swari. Haiwezekani watu kutuletea matumizi ya ZZK wiki hii na wiki inayofuatia waraka.

Kuhusiana na katiba, a constitution is only as good as the people who follow it. Kula kiapo is just a commentary. Ndio Zitto ana makosa kutofuata katiba. Lakini waliomwachia kuendelea kufanya makosa nao wana makosa. Kwa mujibu Zitto ana makosa 11 ambayo kayafanya kwa vipindi tofauti.

Kuhusiana na matumizi ya mediocracy. Katika posti yake moja, Kichuguu alisema kuwa miaka ya chama kimoja, wasomi wengi hawakujiingiza kwenye mambo ya siasa. Matokeo yake ni siasa za Tanzania kutawaliwa na wajanja wajanja (mediocre). Huu ni utamaduni tuliojijengea na umeendelea katika mfumo wa vyama vingi. Na katika mjadala huu, kuna watu wanaokubali umoja wa CDM hili kuindoa CCM mwaka 2015 japokuwa gharama za umoja huo is to preserve mediocrity.

Ki takwimu, viongozi wa CDM au CCM ni taswira ya watanzania. Hivyo mabadiliko ya uongozi ya 2015 yatatokea pale watakaochukua nafasi hiyo kuhamua kufanya vitu above the average. Kwa sasa hivi, CCM and CDM wanafanya vitu vilevile. Tofauti ni kuwa CCM wapo madarakani na CDM ni wapinzani.
Zakumi , kulikuwa na uzi wa waraka ulioletwa na Rene. Uzio huo umeendelea kwa muda mrefu sana bila kauli ya uongozi wa CDM kuukubali au kuukanusha.

Pili, CDM walisema watausambaza waraka huo katika vyombo vya habari.

Tatu, kama utakumbuka waraka ulifuatia kukamatwa kwa Laptop

Nne, Katika bandiko langu la mwanzo nimesema wazi CDM waukane waraka, vinginevyo utakuwa halali kwasababu umekuja kwa jina lao na wanauona ukichambuliwa kwa jina lao.

Tano, Katika ushahidi wao ambao ulikuja baada ya waraka, si Zitto au Kitila aliyekanusha kuhusika na waraka.

Sita, tafadhali sana soma mashtaka 11 ulinganishe mashtaka na maudhui kama hayana uwiano kwa kiasi kikubwa sana.

Saba, Kitila amekubali kuandika waraka, akasema Zitto hakuhusika ingawa alikuwa mhusika mkuu. Soma waraka halafu ulinganishe na maneno ya Kitila

Na mwisho nilisema tutaujadili kama ulivyo.
Nadhani kuna kila jitihada za kuweka jambo hili wazi lakini pia kuna jitihada za kuzima mjadala kwa kuokoa baadhi ya watuhumiwa.

Vyovyote iwavyo Zitto na Kitila ni watuhumiwa wa jaribio la ‘mapinduzi ya demokrasia''.
Na hasa tukizingatia historia zao za ushiriki wa kuhujumu chama kuanzia huko nyuma.

Tuendelee
 
Last edited by a moderator:
Niseme tena hili labda, Kwa misingi na Kanuni za Demokrasia (sio za chama) kama kweli imedhihirika Zitto ni muhusika wa waraka, basi si uonevu kumuadhibu! Anastahili! Swali: Je, misingi hiyo ipo na inafuatwa ndani ya CDM? Kama zipo na zinatakiwa zifuatwe, nani angebaki salama?
Pili, Kwa mazingira yanayosemwa yapo ndani ya chama CDM (ambayo hakuna hoja ya wazi iliyotolewa na watuhumiwa kuyakanusha -turejee baadhi ya madai ya waraka), basi Zitto na wenzake walioandaa waraka huu wapo sahihi kabisa. Madai ya kwamba nao walikuwa viongozi hayana mashiko, kwani uongozi wako utakamilika kama hautakuwa violeted na chochote hasa na nguvu toka juu yako! Kusema wangejiuzulu, ingekuwa njia tu ya kuonesha kutokubaliana na hali fulani, lakini si njia bora ya kupambana na hali hiyo!
Personal attacks zilizomo ndani ya waraka, sidhani kama ni big deal kuuharamisha waraka, haviwezi kuficha hoja zilizopo!
Mkuu Zakumi anasema waliomuacha Zitto kuwa muasi kama inavyodaiwa, wanastahili kuadhibiwa nao. Ni sahihi, kwani kuna mazingira yaliyosababisha Zitto kuwa so. Na mazingira hayo hayakutokana na utekelezaji bali ukiukwaji wa kanuni! Nani amekiuka, na nini kimemkuta!

Sisi Demokrasia HATUIWEZI! Nimeona wengi mkihusisha kutetereka kwa CDM na Mustakabali wa Taifa, ni kitu kilicho wazi kabisa kwamba, kuyumba kwa CDM kiasi fulani kunaweza kuyumbisha Taifa! Mimi hili inaniuma moyo sana, NI KWANINI HATIMA YA TAIFA LETU TUIKABIDHI KWA VITAASISI UCHWARA KIASI HIKI? CHAMA CHA SIASA, CDM, CMM au CUF? How? Usije ukashangaa kataasisi kadogo kabisa, kakathubutu kuingiza Taifa kwenye matatizo makubwa! KWANINI TUNARUHUSU UPUUZI HUU? Kwanini watufanye kila siku tujadili vyama? Eti Chama kama nembo ya Ukombozi, mbaya zaidi under Democracy. Ni kujidanganya kwa kiasi gani huku!

TUNATAKA DIRA YA TAIFA KWANZA KABLA YA KATIBA NA VYAMA!!! TUNATAKA UTANZANIA WETU KWANZA! Kwa sasa vyama vya siasa vinakutana katika upuuzi tu wa kubomoa Taifa, si katika mema ya kujenga Taifa. Ni Ulimbukeni!
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani. Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Ahsante Mimi nisingependa vyama vya siasa viwe na watu watiifu. Ningependa vyama viwe na watu wenye maono na mipango hata kama inatofautiana.
Sipendi watiifu lakini sipendi zaidi wanafiki, wachochezi na wafitini kwasababu hawana definition yoyote nzuri ya kuwa fit katika vyama vya siasa.

Kuhusu Mansour, nikupe mfano mmoja kuwa sisimizi mmoja ndani ya sikio ni bughudha kubwa kuliko mafahali wawili ndani ya zizi ya ng'ombe. Mansour ana ushaiwishi sana katika siasa za Zanzibar. CCM walimuona kama kikwazo na kuamua kumchinjilia baharini. Wakati wanakamata kisu mashabiki walikuwa wanapiga kelele za achinjwe, achinje kwa jina la demokrasia. Tena mashabiki wa CCM.
Wengine tukasema Mansour hana kosa ana mitazamo tofauti na ni kosa kumvua uanachama.

Leo kisu kile kile che nembo ya demokrasia kimekamatwa na CDM mashabiki wanapiga kelele, muuaji, uonevu, haki za binadamua n.k. Hoja hiyo imeshikiwa bango kana kwamba demokrasia imekuja katika maboksi kila mtu ana lake. Ninachosema ni kuwa kosa la Zitto na waraka wa Embe kiburugwa haliwezi kulingana na la Mansour.
Adhabu ya Mansour ni kali kwa kuwa muwazi kueleza mawazo yake, vipi huyu aliyejificha akitumia watu mitandaoni adhabu yake inapaswa kuwaje? Na kwanini CCM wale wale walitumia kisu brand ya demokrasia leo wanaona kisu kile ni butu CDM wakitaka kukitumia? Kuna nini hapo ? Why Zidane.
Kosa zaidi ni pale CDM walipopewa maonyo kuhusu Zitto. Ushiriki wake katika mapinduzi ni wa kiwango cha kuridhisha sana. Hakuna jaribio la mapinduzi ya vurugu lililowahi kufanyika CDM bila Zitto kuhusishwa, hakuna!

Kwa ujanja wa Zitto yeye anabeba agenda halafu anatuma vijana kuvuruga mambo ili apake masizi upande mmoja upande mwingine aking'aa. Huyu hafai.

Ni ujanja huo huo aliutumia kuwatuhumu Barrick na kuwa kinara wa agenda ya ufisadi umma ukimwamini.
Kama alivyomtumia Juliana, Kafulila na Masalia kuleta vurugu, Zitto akawatumia halmashauri ya wilaya ya jimbo lake kujenga shule katika jimbo kwa kutumia Mlungula a.k.a Rushwa kwa kupokea milioni 10 kutoka Barrick.

Ndivyo aanavyotudanganya kuwa hakuhusika na kuandika waraka, wakati tunajua ametekeleza mambo yaliyomo katika waraka tena hadharani kabisa.

Huyu mtu CDM wamemlea leo wanavuna walichopanda.
Sasa umaarufu wa Masour na Zitto unaweza kuwa tofauti kwa hoja za hapo juu, mmo
Mkuu Nguruvi3, sorry umechanganya hapa kidogo issues kumfananisha Mansoor na Zitto.

Wakati wa mjadala wa mafuta ya Zanzibar, niliwahi pata fursa kwenda Zanzibar na nilizungumza na Mansoor na mazungumzo yale niliyaandika humu jf sikumbuki jina la thread!, Mansoor ni arogant kutokana na unasaba na Karume!. Kosa lake ni la ki sera!. Sera ya CCM ni serikali mbili!, yeye kama kiongozi wa CCM ana uhuru wa kutoa maoni yake kuhusu serikali 3 lakini sio kuyashadadia kama alivyoakifanya!.

Tukija kwa Zitto, si muandishi wa waraka wala sii mpangaji bali ni mlengwa tuu!, ila waraka ule sio wa uchochezi wala mapinduzi yoyote kinyume cha katiba sheria na taratibu za Chadema!. Umesema na hapa nanukuu, "kuhusu Zitto. Ushiriki wake katika mapinduzi ni wa kiwango cha kuridhisha sana. Hakuna jaribio la mapinduzi ya vurugu lililowahi kufanyika CDM bila Zitto kuhusishwa, hakuna!" hapa naomba tusaidiane, kueleweshana, kuelimishana na kukumbushana na ikibidi kufundishana, jee kumewahi kutokea jaribio lolote la mapinduzi ndani ya Chadema?!.
Pasco
 
Mkuu JingalaFalsafa
Kama utakumbuka tiliwahi kujadili kuhusu Tanzania kutokuwa na strong civil societies. Tukasema nchi ijenge vipi society hizo, from-top ot bottom-top.Tukazungumzia kuhusu umuhimu wa civil society zaidi ya vyama vya siasa.

Hatuwezi kukataa umuhimu wa vyama vya siasa hata kama ni uchwara.
CCM kinachukua bilioni 8 kwa mwezi kama ruzuku. Ni kiasi gani kinapelekwa Muhimbili hospitali kama ruzuku.

Rasimu nzima ya katiba imeondoka mikononi mwetu, inashughulikiwa na wabunge wa vyama ‘uchwara' .
Mwisho wa siku katiba hiyo itakuja kutuathiri sote.Pamoja na uchwara wake bado vinaathari katika maisha yetu.

Wanapokaa bungeni na kupitisha maamuzi mazito kama ya kodi, mishahara na miradi hizo ni fedha zetu.
Athari zake ni katika mfuko wako, je, hapo uchwara haujakuathiri.

Ninachokubaliana nawe ni kuwa agenda za nchi zichukuliwe na wananchi kwa kupitia civil society.
Swali ni je tunazo hizo society? Na je, hapo hatujaingia katika uchwara wa vyama? Au alternative ni ipi.

Kuhusu Zitto, unaposema waliomwachia waadhibiwe nakubaliana nawe kwa msingi wa kuacha kufuata taratibu hadi hali inakuwa kama ilivyo. Lakini utamwadhibu mtu vipi wakati amekuwa anayafanya vichakani? Je, hapo si uonevu.

Hakuna aliyejua ushiriki wa ZZK katika maalia hadi ‘Ben Saanane' alipojifunga mabomu.
Labda niseme wuongozi ulipaswa kuchukua hatua za awali kabisa bila kuogopa personality.
Swali, ni je, hiyo inaondoa tuhuma zinazomkabili ZZK.Je,makosa mawili yanaweza kusahihisha kosa?

Umedai waraka wa Zitto et al ni sahihi. Tumeuliza usahihi wake upo wapi?
Ndicho tunahitaji kujua kutoka upande mwingine na labda utusaidie kwa hilo.

Wengine tumesema hata kama kuna mchele katika waraka, ni ngumu kuupata kwasababu waraka umejaa kejeli, matusi na kashfa. Tumesema wazi si kila jambo ni la kupuuzia.Tumeuuliza uongozi kuhusu kile kilichomo chenye mantiki, lakini je, hiyo ndio sababu za kuufanya waraka uwe na maana.

Hoja kubwa hapa ni njia walizotumia kufikisha ujumbe wao. Kinachoonekana wazi ni jaribio la mapinduzi kama alivyofanya ZZK kwa kurusha kombora la ukaguzi wa fedha kwa kutumia umma ili kupata mradi wake.

Huyu ni kiongozi aliyepaswa kusaidia chama chake kuweka mahesabu vema na si kuwa mnafiki.
Huwezi kuwa sehemu ya maamuzi halafu ukakimbia upande wa pili na kujitoa.

Tunaomba kama una rekodi za ZZK kutoa malalamiko waliyoyaanisha utuwekee hapa.
Tuna rekodi za ZZK kuwa sehemu ya maamuzi ya CDM ambayo ameyapinga.
 
Mkuu Nguruvi3, sorry umechanganya hapa kidogo issues kumfananisha Mansoor na Zitto.

Wakati wa mjadala wa mafuta ya Zanzibar, niliwahi pata fursa kwenda Zanzibar na nilizungumza na Mansoor na mazungumzo yale niliyaandika humu jf sikumbuki jina la thread!, Mansoor ni arogant kutokana na unasaba na Karume!. Kosa lake ni la ki sera!. Sera ya CCM ni serikali mbili!, yeye kama kiongozi wa CCM ana uhuru wa kutoa maoni yake kuhusu serikali 3 lakini sio kuyashadadia kama alivyoakifanya!.

Tukija kwa Zitto, si muandishi wa waraka wala sii mpangaji bali ni mlengwa tuu!, ila waraka ule sio wa uchochezi wala mapinduzi yoyote kinyume cha katiba sheria na taratibu za Chadema!. Umesema na hapa nanukuu, "kuhusu Zitto. Ushiriki wake katika mapinduzi ni wa kiwango cha kuridhisha sana. Hakuna jaribio la mapinduzi ya vurugu lililowahi kufanyika CDM bila Zitto kuhusishwa, hakuna!" hapa naomba tusaidiane, kueleweshana, kuelimishana na kukumbushana na ikibidi kufundishana, jee kumewahi kutokea jaribio lolote la mapinduzi ndani ya Chadema?!. Pasco
Hapana Mansour hana kosa kutofautiana kwa sera na chama chake.

Wapo wabunge wa Republican waliounga mkono Obamacare na wapo Democrat waliokaa.
Mansour kushadidia ni kujenga hoja yake na hakuwa mnafiki wa kujificha na kusemea vichochoroni.
Kilichotakiwa ni CCM kumjibu hoja zake na wala si kumfukuza.

Zitto aliwahi kubaki bungeni wakati wenzake wametoka. Nilisimama hapa JF na kusema ingawa alitofautiana na msimamo wa CDM hapaswi kulaumiwa au kuonekana msaliti kwasababu alifanya kwa uwazi.
Kilichopaswa ni CDM kumuuliza sababu zake au kusikiliza sababu zake.

Nilimuunga mkono kuhusu hoja ya serikali 3 hata pale CDM ilipokuwa haina sera madhubuti au iliogopa kutetea sera hiyo. Nikasema ZZK alichokifanya ni kutumia uhuru wake wa kutoa maoni ambayo si lazima yawe sawa na kila mmoja.
Mwingine mwenye hoja tofauti na ZZK aje aeleze. Alifanya hivyo kwa uwazi kabisa.

Katika hili la waraka, Kafulila, Shonza na Masalia ZZK alijificha nyuma ya watu akiongoza uasi huku akikaa katika kamati zile zile zilizowaadhibu waasi. Huu ni unafiki na uzandiki wa kiwango bora na hatupaswi kuufumbia macho kwa manukato au manemane.

Lissu amesema ZZK hakushiriki kuandika ingawa ni mlengwa mkuu ili kumuokoa na matatizo kama kuvuliwa ubunge.
Ukweli usio na shaka ni kuwa ZZK alishaanza kuufanyia kazi waraka bila shaka ya aina yoyote.

Waraka umesema ‘warushe makombora' na ameyarusha tena akiwa naibu mtendaji mkuu.
Akatumia PAC kulaani kazi alizotakiwa azifanye kama naibu.
ZZK ameshiriki kampeni za hivi karibuni kama waraka ulivyosema.

ZZK hakumjibu Lema kama kawaida yake bali alifuata maagizo ya waraka ya kuchagua aseme nini na kwa wakati gani.

ZZK na wenzake walishaanza kutupa makombora kwa ID tofauti kama waraka ulivyoshauri.
Habari za tenda ndani ya CDM tumezisoma kabla ya waraka.
Hebu rejea bandiko #92 upate picha halisi. Mambo yalishaanza kufanyiwa kazi

Majaribio ya mapinduzi haram ni yale ya Juliana, Kafulila, Masalia ambaye ZZK ushiriki wake hauna shaka.

ZZK ni smart sana hawi mstari wa mbele anakuwa best supporter wa movie kwa nyuma.
Nikikueleza kuwa alishachukua kitu kutoka Barrick huwezi kuelewa lakini fikiria haya:

ZZK aliwananga sana Barrick na kuwa sehemu ya kamati ya JK na Bomani.
Barrick wakapeleka milioni 10 jimboni kwa ZZK kupitia halmashauri ya wilaya.

Tulimuuliza ZZK kama hana masilahi akasema hajui mpango mzima.
Baada ya kumbana tulibaini ni mjumbe wa kamati ya halmashauri .
Hivyo alijua mchango wa Barrick ulilenga kumtuliza.
Alikubali kuwa ni mjumbe lakini hahusiki na mshiko.

Kwa kiongozi makini yeye akiwa mjumbe wa kamati za halmashauri na mbunge angekataa pesa hizo zina conflcit of interest. Hakufanya hivyo.

Alijua Barrick walilenga nini lakini kwa vile alifahamu hatakuwa na direct contact akakubali zijenge shule jimboni kwake. Kuanzia hapo kimyaa hadi leo.

Ni rahisi kusema ZZK hajachukua kitu lakini je hakuchukua kwa mantiki?
Ndivyo ilivyo rahisi kusema si mlengwa hata kama anatekeleza wajibu wa waraka.
 
Hapana Mansour hana kosa kutofautiana kwa sera na chama chake.

Wapo wabunge wa Republican waliounga mkono Obamacare na wapo Democrat waliokaa.
Mansour kushadidia ni kujenga hoja yake na hakuwa mnafiki wa kujificha na kusemea vichochoroni.
Kilichotakiwa ni CCM kumjibu hoja zake na wala si kumfukuza.

Zitto aliwahi kubaki bungeni wakati wenzake wametoka. Nilisimama hapa JF na kusema ingawa alitofautiana na msimamo wa CDM hapaswi kulaumiwa au kuonekana msaliti kwasababu alifanya kwa uwazi.
Kilichopaswa ni CDM kumuuliza sababu zake au kusikiliza sababu zake.

Nilimuunga mkono kuhusu hoja ya serikali 3 hata pale CDM ilipokuwa haina sera madhubuti au iliogopa kutetea sera hiyo. Nikasema ZZK alichokifanya ni kutumia uhuru wake wa kutoa maoni ambayo si lazima yawe sawa na kila mmoja.
Mwingine mwenye hoja tofauti na ZZK aje aeleze. Alifanya hivyo kwa uwazi kabisa.

Katika hili la waraka, Kafulila, Shonza na Masalia ZZK alijificha nyuma ya watu akiongoza uasi huku akikaa katika kamati zile zile zilizowaadhibu waasi. Huu ni unafiki na uzandiki wa kiwango bora na hatupaswi kuufumbia macho kwa manukato au manemane.

Lissu amesema ZZK hakushiriki kuandika ingawa ni mlengwa mkuu ili kumuokoa na matatizo kama kuvuliwa ubunge.
Ukweli usio na shaka ni kuwa ZZK alishaanza kuufanyia kazi waraka bila shaka ya aina yoyote.

Waraka umesema ‘warushe makombora' na ameyarusha tena akiwa naibu mtendaji mkuu.
Akatumia PAC kulaani kazi alizotakiwa azifanye kama naibu.
ZZK ameshiriki kampeni za hivi karibuni kama waraka ulivyosema.

ZZK hakumjibu Lema kama kawaida yake bali alifuata maagizo ya waraka ya kuchagua aseme nini na kwa wakati gani.

ZZK na wenzake walishaanza kutupa makombora kwa ID tofauti kama waraka ulivyoshauri.
Habari za tenda ndani ya CDM tumezisoma kabla ya waraka.
Hebu rejea bandiko #92 upate picha halisi. Mambo yalishaanza kufanyiwa kazi

Majaribio ya mapinduzi haram ni yale ya Juliana, Kafulila, Masalia ambaye ZZK ushiriki wake hauna shaka.

ZZK ni smart sana hawi mstari wa mbele anakuwa best supporter wa movie kwa nyuma.
Nikikueleza kuwa alishachukua kitu kutoka Barrick huwezi kuelewa lakini fikiria haya:

ZZK aliwananga sana Barrick na kuwa sehemu ya kamati ya JK na Bomani.
Barrick wakapeleka milioni 10 jimboni kwa ZZK kupitia halmashauri ya wilaya.

Tulimuuliza ZZK kama hana masilahi akasema hajui mpango mzima.
Baada ya kumbana tulibaini ni mjumbe wa kamati ya halmashauri .
Hivyo alijua mchango wa Barrick ulilenga kumtuliza.
Alikubali kuwa ni mjumbe lakini hahusiki na mshiko.

Kwa kiongozi makini yeye akiwa mjumbe wa kamati za halmashauri na mbunge angekataa pesa hizo zina conflcit of interest. Hakufanya hivyo.

Alijua Barrick walilenga nini lakini kwa vile alifahamu hatakuwa na direct contact akakubali zijenge shule jimboni kwake. Kuanzia hapo kimyaa hadi leo.

Ni rahisi kusema ZZK hajachukua kitu lakini je hakuchukua kwa mantiki?
Ndivyo ilivyo rahisi kusema si mlengwa hata kama anatekeleza wajibu wa waraka.
Du!, Mkuu Nguruvi3!, hands down for a moment, ngoja nijipange maana tuhuma nyingine, japo not expressly, but impliedly!.
Pasco.
 
Naungana nawe; mimi nadhani hii ni Litmus Test for Chadema kubaini iwapo umaarufu wake mbele ya umma unatokana na "personalities" au ni itikadi, sera, imani, kanuni na misingi ya chama, huku viongozi wake wakipimwa kwa jinsi gani wanasimamia masuala haya. Katika sakata husika, for sustainability ya chama today and beyond, wanaomuunga mkono zitto ilitakiwa watazame suala hili kitaasisi zaidi na sio vinginevyo, kwani kinyume chake ni kwamba support yao kwa chadema ni suala la msimu tu.

Kuna haja ya uongozi wa sasa kuanza kubadilisha haya ili warithishe vizazi vijavyo chama kinachosimama kama taasisi.

Kuna suala lingine ambalo kidogo linanitatiza - na linahusiana na hoja yako kwamba attitude ya zitto ni kama vile kaonewa. Je, kwa maana hii ndio maana amekaa kimya anapoona wananchama katika maeneo mbalimbali wanaleta fujo kufuatia maamuzi ya kamati kuu, amechagua kukaa kimya? Hivi anaelewa jinsi gani ange score political mileage kwa kutoa onyo kali kwa wale wanaofanya vitendo vya uharibifu n.k? Je, kwa wale wataalamu wa masuala haya yanayohusiana na kamati kuu, maamuzi yake, siku kumi na nne za kujieleza n.k, ni busara kwa zitto kukaa kimya badala ya kukemea vurugu zinazoendelea?

Mwisho, naungana na wachangiaji kadhaa huko juu kwamba kwa sasa, uongozi wa chama ungesitisha ziara za viongozi mikoani. Lakini nadhani uongozi uliopo ni makini na unalijua hilo, na uamuzi wa kwenda mikoani ulilenga kwenda kupima upepo wa siasa, first hand, kufuatia maamuzi ya kamati kuu
Ndiyo Mchambuzi, tumeeleza miaka 2 iliyopita kuwa CDM haina sura ya taasisi bali mkusanyiko wa wananchi chini ya mwembe na lazima wabadilike ili iwe taasisi.

Mwaka 2011 nilisema hivi kwanini CDM hawawezai kujenga haoja hadi awepo Dr Slaa. Nikahoji huyu Slaa atafafanu au kujibu tuhuma zote kama nani. Kwani hakuna viongozi wengine? Hakuna idara nyingine? Kama yapo mabadiliko kuelekea kuwa taasisi inayosimama yenyewe ni kidogo. Ndio maana sasa hivi wanfanya litmus test badala ya kusimamia sheria, kanuni nataratibu.


Kuhusu ZZK, attitude kuwa anaonewa ndiyo silaha yake. Tena anaijenga kwa misingi ya kugombea uongozi kwamba anapigwa vita. Huyu ndiye aliyepanda mbegu ya ukanda inayochanua vema kama kinga pale anapofanya uharibifu. Kinga imemsaidia sana kiasi cha kufikia hatua nzuri ya kuvuruga CDM.

Swali ni je, kinga hiyo inakisaidia CDM na itavumiliwa hadi lini?


Nashangaa ZZK anakwenda katika maredio na vyombo vya habari kueleza jinsi alivyoisaidia CDM. Asichokisema ni wapi amejikwaa au amekosa kama alivyodai katika uetetezi hapo juu.


ZZK anafahamu vurugu katika kanda ni sehemu ya kazi yake na Kitila iliyotibuka prematurely.
Nadhani alikuwa na jukumu la kukaa kimya ili kupunguza tension na jamii imwelewe.
Anchokifanya ni kutumia media kwa kuelewa political platform hanayo,inatahari kwake hata hivyo


Kuhusu kufkuzwa uanachama na kwamba kutaathiri chama kuelekea 2015, ninachoweza kusema ni kuwa 2010 ZZK alizusha mtafaruku wakati CDM kikiwa katika harakati za uchaguzi.
Alifanya vile makusudi kabisa.

Historia yake ya uasi inatia shaka zaidi kuliko faraja kwa CDM

Sijui kama kubaki kwakwe kutakuwa na athari tena au la, sina uhakika


Kufukuzwa na kuomba uanachama upya:

Nadhani ni jambo la hatari sana kulifanya.
Likifanyika litashadidia dhana ya kuwa uongozi umemfukuza ili asiweze kugombea na hakukuwa na sababu za maana kumchukulia hatua bali mbinu za kumfunga mikono.

Baada ya 14 vikao halali vikae kukiwa na ushahidi usio na shaka wa kumtia hatiani. Kama hakuna ushahidi basi kesi ifutwe.


Hatua zichukuliwe kwa mujibu wa katiba, sheria na kanuni.

Endapo hana kosa arudishiwe nyadhifa zake.


The bottom line ni kuepuka jazba na hasira kama walizofanya hapo awali za kumuondoa na kuteua watu nusu nusu.


Hapa ndipo CDM watajilaumu kwasababu ili kuwe na haki na usawa ilibidi kuwa na chombo nje ya kamati kuu kutafuta ukweli.
Kwasasa itakuwa ni ngumu sana kwao kuaminika hata kama wana ushahidi.

Ningewashauri team ZZK kuwa badala ya kupita kueneza uongo hasa wa uenyekiti, ukanda n.k. wangejibu hoja


 
Niseme tena hili labda, Kwa misingi na Kanuni za Demokrasia (sio za chama) kama kweli imedhihirika Zitto ni muhusika wa waraka, basi si uonevu kumuadhibu! Anastahili! Swali: Je, misingi hiyo ipo na inafuatwa ndani ya CDM? Kama zipo na zinatakiwa zifuatwe, nani angebaki salama?
Pili, Kwa mazingira yanayosemwa yapo ndani ya chama CDM (ambayo hakuna hoja ya wazi iliyotolewa na watuhumiwa kuyakanusha -turejee baadhi ya madai ya waraka), basi Zitto na wenzake walioandaa waraka huu wapo sahihi kabisa. Madai ya kwamba nao walikuwa viongozi hayana mashiko, kwani uongozi wako utakamilika kama hautakuwa violeted na chochote hasa na nguvu toka juu yako! Kusema wangejiuzulu, ingekuwa njia tu ya kuonesha kutokubaliana na hali fulani, lakini si njia bora ya kupambana na hali hiyo!
Personal attacks zilizomo ndani ya waraka, sidhani kama ni big deal kuuharamisha waraka, haviwezi kuficha hoja zilizopo!
Mkuu Zakumi anasema waliomuacha Zitto kuwa muasi kama inavyodaiwa, wanastahili kuadhibiwa nao. Ni sahihi, kwani kuna mazingira yaliyosababisha Zitto kuwa so. Na mazingira hayo hayakutokana na utekelezaji bali ukiukwaji wa kanuni! Nani amekiuka, na nini kimemkuta!

Sisi Demokrasia HATUIWEZI! Nimeona wengi mkihusisha kutetereka kwa CDM na Mustakabali wa Taifa, ni kitu kilicho wazi kabisa kwamba, kuyumba kwa CDM kiasi fulani kunaweza kuyumbisha Taifa! Mimi hili inaniuma moyo sana, NI KWANINI HATIMA YA TAIFA LETU TUIKABIDHI KWA VITAASISI UCHWARA KIASI HIKI? CHAMA CHA SIASA, CDM, CMM au CUF? How? Usije ukashangaa kataasisi kadogo kabisa, kakathubutu kuingiza Taifa kwenye matatizo makubwa! KWANINI TUNARUHUSU UPUUZI HUU? Kwanini watufanye kila siku tujadili vyama? Eti Chama kama nembo ya Ukombozi, mbaya zaidi under Democracy. Ni kujidanganya kwa kiasi gani huku!

TUNATAKA DIRA YA TAIFA KWANZA KABLA YA KATIBA NA VYAMA!!! TUNATAKA UTANZANIA WETU KWANZA! Kwa sasa vyama vya siasa vinakutana katika upuuzi tu wa kubomoa Taifa, si katika mema ya kujenga Taifa. Ni Ulimbukeni!
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani. Anaita sasa!
kiongozi @jinga la falsafa kwanza naomba nikupongeze kwa bandiko zuri na lenye kujaa uzalendo.

kwa muda mrefu nilikuwa kimya kuhusu mgogoro ndani ya CDM kwasababu nilishindwa kuelewa jambo moja, hivi sisi kama watanzania tunataka nini kama first priority?? je tunataka chama/vyamna ama tunataka taifa kama taifa??

ikiwa nia yetu ni vyama basi naona mwisho wa tanzania ni mfupi sana manake vyama vyote vilivyopo hakuna ambacho kinaweza kusema kwamba kimeifanya tanzania kuwa taifa lenye neema ila cummulative efforts za watu wote zimelifanya taifa hili kuwa hapa lilipo hata nkama tuko nyuma sio nyuma sana kiivyo.

sioni sababu ya kuona kwamba CDM ikisambaratika basi nchgi imekwisha, kwann tuwe na fikra kama hizi?? istoshe mgogoro huu wa cdm ni mdogo sana haupaswi kumeza akili za watanzania wote kama ukweli kuna aina yyte ya hujuma na i9naonekana zitto ni threat basi wafanye kilichosahihi juu yake and thats all.

hakuna haja ya kuiona nchi kama haita piga hatua simply kwasababu ya vyama vya siasa ambavyo tunavipa nafasi tu ya kuratibu lkn sio watendaji.
 
Nguruvi3 rejea bandiko lakon #157 .................
sawa ZZK anatafuta huruma ya wananchi/raia na hii imjketokana na ukweli kwamba anajua anayo nguvu ya watu nyuma yake yaani anao uwezo mkubwa wa kushawish na kupata sympathy ya watu kuliko ambavyo baadhi ya wanategemea.

lakin najiuliza swali la msingi sana hivi CDM ni chama cha siasa, ama taasisi isiyo ya kiserikali ama ni kikundi cha wahuni tu ambao hujiendesha pasina taratibu zinazoeleweka ama nini??

Hivi kama ishu ni kugombea uongozi kwann basi wasiache kura ikawa mwamuzi?? na ishu ni ZZK kuongopa hivi CDM inaona tabu gani kumuwajibisha hadi wafanya media ndio hakimu na msikiliza mashtaka wao??

Tuliona mfano ambao Lowassa alituonyesha kiukweli kitendo cha yeye kukubali kuresign hata kwa mambo ambayo mengine yalikuwa ni tuhumu ama yalikuwa ya kweli halikusambaratisha ccm wala haikufanya ccm kushindwa kuendelea na harakati zake za kuongoza nchi. mfano huu ungetosha kuifunza cdm kwamba hata kama zzk kakosea na yy haoni kuwa kakosea basi wao waendelee kujenga chama na warekebishe baadhi ya makosa ambayo kwa namna moja ama nyingine ndio chanzo cha haya.

hakuna haja ya kunyenyekea watu kama miungu watu lkn pia hakuna haja ya kunyima taifa zima Usingizi kisa mgogoro ndani ya CDM.
 
Last edited by a moderator:
kiongozi @jinga la falsafa kwanza naomba nikupongeze kwa bandiko zuri na lenye kujaa uzalendo.

kwa muda mrefu nilikuwa kimya kuhusu mgogoro ndani ya CDM kwasababu nilishindwa kuelewa jambo moja, hivi sisi kama watanzania tunataka nini kama first priority?? je tunataka chama/vyamna ama tunataka taifa kama taifa??

ikiwa nia yetu ni vyama basi naona mwisho wa tanzania ni mfupi sana manake vyama vyote vilivyopo hakuna ambacho kinaweza kusema kwamba kimeifanya tanzania kuwa taifa lenye neema ila cummulative efforts za watu wote zimelifanya taifa hili kuwa hapa lilipo hata nkama tuko nyuma sio nyuma sana kiivyo.

sioni sababu ya kuona kwamba CDM ikisambaratika basi nchgi imekwisha, kwann tuwe na fikra kama hizi?? istoshe mgogoro huu wa cdm ni mdogo sana haupaswi kumeza akili za watanzania wote kama ukweli kuna aina yyte ya hujuma na i9naonekana zitto ni threat basi wafanye kilichosahihi juu yake and thats all.

hakuna haja ya kuiona nchi kama haita piga hatua simply kwasababu ya vyama vya siasa ambavyo tunavipa nafasi tu ya kuratibu lkn sio watendaji.

gfsonwin;

Jinga la Falsafa ana hoja zilizotulia sana. Ukisoma katiba ya Marekani, hakuna sehemu yoyote inayotaja vyama vya siasa. Inavyotaja ni haki ya wananchi kushiriki katika shughuli za kisiasa, haki ya kujikusanya kufanya majadiliano, na haki ya watu kuwakilishwa.

Mfumo wa vyama umekuja baadaye sana baada ya watu kutumia haki zao za kiraia zilizomo kwenye katiba. Hivyo vyama vya Republican na Democrat vipo kutimiza haki za kiraia. Na kiongozi wa chama, jukumu lake la kwanza ni kuhakikisha haki za kikatiba za wanachama zinatimizwa kwa sababu haki hizo ndizo zinazofanya chama kisimame. Katiba inaposema kuwa watu wana haki ya kukusanyika ina maana wanaweza kuanzisha makundi ambayo utaita chama au upinzani ndani ya chama.

Katiba ya Marekani haisemi Marekani iwe nchi ya kijamaa au kibepari. Wala haisemi Marekani liwe taifa tajiri au lenye nguvu duniani. Katiba inatoa muundo wa kijamii ambao unatoa haki za kisiasa. Kwa kifupi haya ndio malengo ya katiba ambayo yanapatikana katika jamii zote zilizoendelea na zenye taratibu.

Kwa upande wetu, tumeanza na matokeo (vyama vya kisiasa) bila kuwa na haki za kimsingi ambazo zingekuwa ni misingi ya kuwepo kwa vyama. Ukiwauliza wana CCM na CDM kwanini ni wanachama wa vyama hivyo, watakwambia ndio vyama pekee vyenye uwezo wa kuleta maendeleo. Na ili walete maendeleo na kufanya mabadiliko ni lazima waende Ikulu.

Ukweli wa mambo, ili kuleta mabadiliko ya kweli sio lazima CDM, CCM, au CUF iende Ikulu. Na matatizo ndani ya vyama vya kisiasa yangepungua kama viongozi wake wa juu wangeacha kutumia muda wao mwingi kutafuta njia ya kwenda Ikulu.
 
Back
Top Bottom