East African Federation (EAF) public Views

East African Federation (EAF) public Views

Kamundu,
Ndugu yangu tupeni na sisi wa Mwanza hizo Ajira jamani!...
Labda kuwepo kwa hayo makao makuu ya EAC, Mwanza kunaweza kutuletea maendeleo zaidi. Mwanza ya toka uhuru ndiyo ile ile haijabadilika zaidi..
 
Shirikisho la afrika mashariki ni jambo jema lakini huu si wakati muafaka kwa kuundwa shirikisho hilo.

Tatizo hapa si kwamba ni uelewa mdogo wa watanzania bali uelewa mkubwa na mtanzamo wa khari ya juu watanzania tulionao ndio maana tunalikataa shirikisho hilo lilo na mtazamo hasi kwa watanzania.
Mimi ni mwanafunzi ktk chuo kikuu cha tekinolojia nchini Poland nashuhudia jinsi Nchi ya kenya inavyotanganza maliasili za tanzania kua zipo nchini kenya,mfano ml.kirimanjaro,mbuga za serengeti .hivyo basi kumbe hapa tunapata picha ya shirikisho hili lina malengo tofauti zaidi ya muungano ulio makini na mathubuti, bali upokonyaji wa mali

Pili kuna viongozi ambao kwa mtanzamo mwepesi kabisa endapo watakosa uraisi ndani ya shirikisho EAC lazima wataingia mstuni kuusaka uraisi wa shirikisho hilo

Tatu siasa za kenya ,uganda ,Rwanda Burundi ni siasa zilizojaa mabavu ,ukabila ,kwa nini turudishwe ktk ukabila na mitafaruku ambayo watanzania tumefanikiwa kuidhibiti?

Viongozi wasifanye shirikisho kwa masilahi ya watu wa chache bali kwa taifa letu, shirikisho hilo kwa sasa hatulihitaji maana shirikisho hilo linatakiwa li asisiwe miaka isiyopungua 20 ili kutona taswira iliyo dhabiti na imara zaidi.
cha muhimu zaidi viongozi wetu watoe sababu zilizopelekea kuanguka ile jumuia ya mwanzo na sababu zake harafu wawaeleze wananchi kua sababu hizo leo zimetatuliwa na si kuwatisha wananchi kwa kuwaita wanauelewa mdogo
PETER MKAMA -POLAND
 
Adai bila ridhaa ya wananchi ni uhaini
*Adai Kibaki, Obote walilikataa miaka ya 60
*Asema ni mfumo wenye gharama kubwa
Na Hassan Abbas

HUWEZI kulizungumzia vyema suala la shirikisho ambalo linagusa muungano wa mataifa mbalimbali bila kuwa manju katika sheria za kimataifa na ufahamu mpana wa siasa na historia za nchi husika, hivyo ndivyo ilivyobainika Jijini juzi.

Mmoja wa watu muhimu ambao wanaweza kulizungumzia
kwa ufasaha suala la shirikisho linalotolewa maoni sasa la nchi za Kenya, Tanzania na Uganda (na baadaye Rwanda
na Burundi) ni Profesa Palamagamba John Kabudi.

Huyu ni Mkuu wa Idara ya Sheria za Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambaye juzi aliamua kuvunja ukimya kuhusu mwenendo wa shirikisho hilo.

Alisisitiza kuwa iwapo Shirikisho la Afrika Mashariki ambalo mchakato wake unaendelea hivi sasa litafikiwa bila ridhaa ya wananchi, huo utakuwa sawa na uhaini kwa sheria za Tanzania.

Msomi huyo aliyebobea katika maeneo anuai ya sheria za kimataifa, anasema pia kwamba kitendo cha sasa wananchi kutakiwa wajadili shirikisho ni makosa makubwa kwani wananchi walitakiwa kwanza waamue nchi zao ziungane kwa muundo gani kati ya mifumo mbalimbali ya muungano inayojulikana duniani ndipo mambo mengine yafuatie.

Alisema kuna aina mbali mbali za muungano ambazo taifa moja linaweza kuufanya na jingine na akazitaja baadhi ya aina hizo kuwa ni Union, Federation, Confederation na Community. Akasema wananchi wa Afrika Mashariki wangeamua kwanza juu ya aina hizo.

Profesa Kabudi aliyekuwa akichangia mada kwenye kipindi cha This Week In Perspective kinachorushwa na Televisheni ya Taifa (TvT), akizungumzia uhalali wa kuundwa shirikisho hilo alisema chini ya sheria za kimataifa, maamuzi hayo mazito hayawezi kufanywa na marais tu.

" Kanuni zinasema bayana kwamba ni wazo ambalo lazima lifikishwe kwa wananchi waamue kupitia kura ya maoni muundo na hata taratibu zake," alisema mtaalam huyo.

Akaongeza katika hilo akisema kwa sasa tayari makosa yamefanywa kwa wananchi kutoshirikishwa na badala yake viongozi ndio wameshaamua jumuiya hiyo iwe ya shirikisho.

" Kabla hata ya kuamua muungano huo uwe wa shirikisho au la, hilo ni moja ya maswali ambayo wananchi walitakiwa kuyaamua kwanza. Ni kosa kuamua halafu ndipo unakwenda kuwauliza wananchi kama wanakubali," alisema Profesa Kabudi.

Akizungumzia kanuni za Tanzania kujiunga katika shirikisho hilo, mtaalam huyo ambaye pia ni Mhadhiri Mwandamizi wa sheria wa UDSM, amesema chini ya mkataba wa Vienna, Tanzania haiwezi kuingizwa katika shirikisho bila pia maamuzi ya wananchi kupitishwa na Bunge.

" Itatakiwa theluthi mbili ya wabunge wa Bunge la Muungano na lile la Zanzibar wapitishe uamuzi huo ndipo uwe umekidhi matakwa ya kisheria.
" Kuiingiza Tanzania katika shirikisho bila ridhaa hiyo ya wananchi na mabunge yao itakuwa sawa na uhaini," alisisitiza.

Akijibu swali la kama Tanzania iko tayari kuingia katika shirikisho hilo alisema hilo kwa sasa haliwezekani na si jambo la busara.
" Kama ningetakiwa kutoa maoni yangu ya kitaalamu kuhusu hilo, ningesema bila kinyongo kwamba labda baada ya miaka 25 hivi ndipo tutakuwa tayari," alisema.

Akifafanua zaidi na kujibu hoja juu ya iwapo wananchi wa Tanzania ambao wengi wanaonekana kuwa na hofu dhidi ya shirikisho hilo kama wana mantiki, Profesa alisema hofu waliyonayo Watanzania inaeleweka.
" Lazima wawe na hofu na hofu yao iko wazi, Tanzania haiko tayari kuingia katika shirikisho kwa sababu nyingi. Shirikisho lazima liangalie mambo mengi.
" Tanzania inasifika kwa amani na utulivu ambao umeipa taswira kubwa hata kwenye Umoja wa Mataifa. Utawahakikishia nini Watanzania unapoungana na watu kama Rwanda na Burundi (zenye mapigano ya kikabila)?" alihoji.

Akasema pia kiuchumi nchi hizi hazilingani na ndio maana hata kabla ya kuundwa Jumuiya ya kwanza ya Afrika Mashariki mwaka 1967, suala la shirikisho lilishindikana huku Kenya na Uganda ndizo zilizokataa baada ya kujiona hazikuwa tayari.
" Kwanza kabisa mkataba wa Tanganyika kuwa koloni chini ya udhamini wa UN ulizuia nchi hiyo isiingie katika aina yoyote ya shirikisho. Lakini mwaka 1961 lilipokuja wazo hilo tena Milton Obote (aliyekuwa Waziri Mkuu) wa Uganda akakataa.
" Wazo hilo lilipoibuka tena mwaka 1963, mwanasiasa aitwaye Emilio Stanley Mwai Kibaki (akiwa mbunge wa jimbo ambalo kwa sasa linaitwa Makadara) alilipinga wazo hilo. Huyu nadhani sasa ndiye rais wa Kenya. Sasa kwa nini leo Tanzania inataka kukimbilia suala hilo," alisema akionesha kuwa wenzetu mwanzo walikataa kwa sababu waliona hawakuwa tayari, sasa wamejiandaa.

Akizungumzia shirikisho hilo, Profesa Kabudi alisema makosa mengi yamefanyika ikiwa ni pamoja na wananchi kutoshirikishwa katika mikataba ya awali na ya msingi sana kama ule wa kuunda shirikisho la kiuchumi, soko la pamoja na pia muungano wa sarafu.
" Hakuna kitu kigumu na kitakachowaathiri sana wananchi wa Tanzania kama soko huria, kitu ambacho mara nyingi huchukua miaka kati ya 10 hadi 15 kuundwa. Lakini katika hili watu hawakupewa nafasi kujadili, wameingizwa tu kujadili hatua ya mwisho ya shirikisho," alisema msomi huyo.

Anasema huwezi kuzungumzia shirikisho la kisiasa wakati kitu cha muhimu kama muungano wa kiuchumi na sarafu wananchi hawakuelimishwa.
" Kwanza shirikisho la kisiasa ni gharama sana kuliendesha kwa sababu nchi kama Tanzania itatakiwa kundesha serikali tatu; Kuchangia katika serikali ya Muungano, Zanzibar na ya shirikisho. Maoni yangu shirikisho ni muundo wenye gharama kubwa sana," alisisitiza.
Kilichojitokeza katika mjadala huo pia ni kuhusu ulazima wa kuharakisha kuundwa kwa shirikisho hilo na namna wananchi wanavyopewa fursa ya kujadili faida na hasara za shirikisho.

Katika hilo Profesa Kabudi, ambaye pia amepata kuwa mwandishi wa hotuba za rais katika awamu ya pili ya Alhaji Ally Hassan Mwinyi, anasema hakuna sababu za kuharakisha shirikisho hilo na akasikitika kuona hata namna ya kulijadili shirikisho lenyewe wananchi wanapotoshwa.
" Ukiangalia faida na hasara wanazozijadili baadhi yao utabaini si za shirikisho la kisiasa. Wananchi wengi wanajadili faida na hasara za muungano wa kiuchumi ambao umeshapita.
" Wengi wanaonekana hawakuelimishwa kuhusu shirikisho na hawalielewi ni kitu gani hatimaye wanajikuta wanajadili vitu ambavyo vilishaamuliwa," alisisitiza.
Maoni haya ya msomi huyo ambaye pia ni mahiri katika Sheria za Mazingira, Ndoa, Madhara, Juriprudensia (falsafa za sheria) na Sheria za mambo ya kale, kati ya nyingine nyingi ambazo amebobea, yanazidi kuibua mjadala na kuunga mkono kilio na hofu ya Watanzania wengi.

Mpaka sasa mchakato wa kutoa maoni unaendelea jijini Dar es Salaam chini ya Kamati iliyoundwa na serikali kushughulikia masuala hayo.
Kinachojitokeza ni kwamba pamoja na suala la mataifa kuungana kuwa ni la muhimu katika zama hizi za utandawazi, Watanzania kutoka kada za wasomi au raia wa kawaida, wote wana hofu kuu ya je, ukiangalia vurugu za kisiasa katika nchi tutakazoungana nazo, mifumo yao ya kiuongozi na mipasuko ya kijamii iliyopo, shirikisho kwa sasa litatusaidia au kutuingiza matatizoni?
|
Tatizo kubwa jingine wakati kamati hiyo ikiendelea kukusanya maoni, imebainika, ni wananchi wengi kutofahamu wanachokitolea maoni, kama pia alivyobaini Profesa Kabudi.

Wengi kati ya wanaotoa maoni wamejikuta wakijadili na hata kuzungumzia masuala ambayo hayahusu shirikisho, lakini kwa ujumla, wengi wao, ukisikiliza walichokisema na taarifa za vyombo vya habari vinavyoripoti, utabaini wanasema Tanzania haijawa tayari na wengi wanasema hilo, tena waziwazi. Tunakaribisha makala kuhusu mjadala huu. - Mhariri
 
Mkanda, ninakubaliana na wewe kabisa, lakini baadhi ya ofisi zifunguliwe Mwanza, Mwanza ni mji wenye pesa na watu wachapakazi lakini serikali yetu imeitupa Mwanza sana. Mwanza inatakiwa ijengwe kwa mpangilio na pesa ipo na kama haipo iombewe msaada.

Watu wa Mwanza wanatakiwa waongee na kupush serikali iweze kuuweka huu mji uwe wa kitalii. Mkanda nakubaliana na wewe lakini makao makuu hayawezi kuwa Mwanza kwa sababu Ujenzi wa makao makuu umeshaanza Arusha lakini idara nyingine na ofisi zifunguliwe Mwanza.
 
Guys

Sasa nyie mnahalalisha tume na Muungano wa jumuiya ya Afrika Mashariki?
 
Kuna kila dalili za Mwanza kuwa Makao Makuu ya hiyo Shirikisho, Mf. Mwaka jana kulikuwepo na vikao viwili ambavyo vilikwa vinahusu shirikisho, na zaidi Kikwete na Museven, walionekana Mz wakiketa kuhusu Shirikisho.

Mz sasa inakarabatiwa kwa kasi kubwa, na kwa hesabu ya benki Maendeleo ya Afrika, Mwanza ndio ulikuwa mji unaokuwa kwa kasi kwa mwaka jana katika Afrika.
 
Ukishauriwa jambo la kijinga usikubali,utaonekana zuzu
Juma Mohammed
HabariLeo; Monday,January 22, 2007 @00:02

Juma Mohammed
La mgambo limelia…kuna jambo Tanzania tena kubwa, mchakato wa kukusanya maoni ya wananchi wa Afrika Mashariki kuhusu kuharakishwa au kutoharakishwa kwa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki umeanza kwa nchi za Uganda, Kenya na Tanzania.

Ningepanda Watazania wenzangu tujadili na kutafakari kwa makini matamshi haya ya Baba wa Taifa, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoyatoa mwaka 1994, alisema: “Mtu akikushauri jambo la kijinga, huku anajua jambo hilo analokushauri ni la kijinga, na wewe ukakubali, basi atakuona, wewe zuzu!”

Nimelazimika kunukuu matamshi hayo ni kwa sababu kwa maoni yangu si wakati Muafaka kwa Taifa letu kujiunga katika Shirikisho la aina hiyo. Nasema hivyo kwa sababu, Tanzania ni zao la Mataifa huru mawili, Zanzibar na Tanganyika ambazo ziliungana Aprili 26, 1964.

Kwa kuwa ni Muungano wa nchi mbili, kuna mambo yalikubaliwa katika hati ya Muungano ambayo na hakika suala la Shirikisho la Afrika Mashariki halimo, sasa swali liko hapa je nafasi ya Zanzibar katika mambo yasiyokuwa ya Muungano nani msimamizi wake?

Kwa Mujibu wa mkataba wa Muungano, kutakuwa na Serikali mbili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatakayokuwa na kujumu la kusimamia mambo ya Muungano na yale yasiyokuwa ya Muungano kwa upande wa Tanganyika( Tanzania Bara) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakayosimamia masuala ya Zanzibar yasiyokuwa ya Muungano.

Tanzania kujiunga katika Shirikisho yatakuwa ni maafa makubwa kwa Watanzania iwapo tutajiunga hasa kwa mpango wa "fast track". Wenzetu wanadhani kwamba Watanzania kutokana na upole wao, ukarimu ni mazuzu tunaoendekeza wema wa mshumaa kuwaangazia wengine huku wenyewe tunateketea, kwa minajili ya kupata sifa isiyokuwa na tija, hilo haliwezekani.

Ulipoanzishwa umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki miaka iliyopita, iliyokuwa Tanganyika kwa wakati huo haikujiunga harakaharaka hadi ilipofahamu maslahi yake, lakini suala hilo halikuzuia nchi za Kenya na Uganda kuanzisha Umoja wao wa Forodha.

Tanganyika ilijiunga baadaye! Hata ile Jumuia ya Afrika Mashariki iliyovunjika mwaka 1977 ilianzishwa baada ya kupita miaka 50 tangu kuanzishwa Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki. Sasa hii haraka ya sasa hivi ya nini? Ni faida gani itapatikana ? Mbali na ngonjera za kisiasa, pengine na watu fulani kupata posho za vikao vya EAC na baadhi kuandikwa kwenye vitabu vya historia, vipi hasa vinatakiwa kutusukuma katika fast track?

Huo Mkataba wa EAC uko wapi ili tuweze kuuona na kuusoma? Ni Watanzania wangapi waliousoma na kuuridhia ikawa sasa tunaanza kuwa kwenye mchakato wa kuelekea kwenye Shirikisho? Je wale waliosababisha Jumuiya ya kwanza ya Afrika Mashariki kuvunjika hawatarudia makosa waliyoyafanya mwaka 1977 kwa kutuacha bado tunafurukuta? Mimi naona kujiunga kwetu kwafanana na Punda wa kwenye hadithi moja iliyochapishwa Tanzania ambamo Simba baada ya kujeruhiwa, alishindwa kuwinda; na Sungura, Fisi na Punda wakaenda kumpa pole.

Kumbe Fisi na Sungura walikuwa na lao jambo, punda akawa kitoweo.


Kwa nini mkataba unafichwa? Tuonyeshwe hiyo DRAFT ya huu muungano?
 
Mimi naona tunahitaji muda bado kabla ya kulikubali shirikisho hili. Mimi ni mTanzania na kwa ninavyoona bado Tanzania haiko tayari kabisa kukabiliana na changamoto za shiriokisho hili. Ni kweli kwamba linaweza kuleta maendeleo na faida kubwa lakini sisi waafrika ni wabinafsi na hatuna uwezo wa kuwa na shirikisho la kudumu.Lazima kwanza tujiulize sababu za kuvunjika shirikisho lililopita(1977) ndio tukubaliane kuunda shirikisho jipya.

Sidhani kama sababu zilizopelekea kuvunjika shirikisho lililopita zimeshafanyiwa kazi na kuonekana kwamba hazitaibuka tena katika shirikisho hili. Watanzania ndio tulioumia zaidi tulipovunja shirikisho mwaka 1977 na ni lazima tuwe makini sana zaidi wakati huu. Viongozi wetu wanaonekana wanashabikia sana shirikisho hili kwa sababu ya maslahi yao binafsi.

Watanzania tusidanganyike, bado hatuko tayari kwa ajili ya shirikisho jipya. Tupewe kwanza sababu za kuvunjika lile la mwanzoni. Sio mambo yote wanayoongea viongozi yanafaa kukubaliwa!!
TUTAKULA HARAMU!!

Lwendo G.G
 
Kwanza napenda kusema kuwa siungi mkono uundwaji wa shirikisho la Afrika mashariki. Nasema hivyo kwa sababu kitendo hicho kitasababisha watanzania kuja kujuta siku za usoni. kwanza hawa jamaa tunaotaka kuungana nao hawana amani katika nchi zao, hivi tunataka kuweka amani yetu tuliyoijenga kwa zaidi ya miaka 45 rehani?. Pili tabia za watanzania ni tofauti kabisa na hawa wenzetu. Watanzania ni watu wapole na wenyekuvumiliana na wenzetu ni wakorofi na wenye kupenda fujo na machafuko, sasa unaunganishaje vitu viwili ambavyo havifanani?

Sera za ubepari zimeanza siku nyingi nchini Kenya, wakati sisi tukiwa na sera za ujamaa. Sera hizo za kibepari ziliwafanya kila mtu kukusanya mali bila kujali jamii nyingine ina hali gani. Si rahisi nchini Kenya kukuta ARDHI ambayo haina mtu na ardhi hiyo kwa sehemu kubwa imehodhiwa na watu wachache.

Nadhani watanzania tujipe muda wa kutosha kulekebisha mapungufu yetu ambayo yalisababishwa na mfumo wa kiuchumi na kisiasa wa wakati ule. Hizi block politics kwa sasa hazitusaidii na badala yake tuelekeze nguvu zetu katika kujenga uchumi.
 
Nimejaribu kutafakari maoni ya watanzania kwa muda sasa juu ya kujiunga na shirikisho. Maoni ya watanzania wengi ni kuwa hatujawa tayari. Nami najiuliza ni lini tutakuwa tayari? Halafu hoja kwamba wakenya wapo mbali kiuchumi, hivi ni nani amesema kuwa wakati sisi tukijiweka sawa wakenya watakuwa wanatusubiri ili tuwe sawa?

Maoni yangu ni kuwa kutokuwepo usawa ndio hasa ingekuwa sababu ya kuungana. Kila nchi ina mapungufu na mazuri yake, tunajiunga ili kupiga hatua pamoja. Hata huo umoja wa ulaya ambao watu wanatolea mfano sana, mbona nchi nyingi tu hazifanani kiuchumu, kisiasa, n.k.

Hao ndugu zetu wa Burundi na warwanda wakija tutawaambukiza ustaraabu na pengine upuuzi wao wa kupigana ukaisha maana katika muungano itakuwa hamna cha mtusi wala mhutu. Na sisi Tanzania tutafaidika sana hasa katika maeneo mengi, kwa mfano:
i) kuchangamka kibiashara na katika kazi maofisini. Hii longolongo ya watanzania kupiga story maofisini badala ya kuchapa kazi itaisha
ii) kuvipiga msasa vyombo vyetu vya habari. Ilivyo sasa vyombo vyetu vingi vya habari kazi yake ni kuitukuza serikali tu kama vile viongozi wa serikali ni malaika. Shirikisho litawaamusha waandishi wetu waweze kuandika with a critical mind na waache kulamba viatu vya viongozi.
iii) Kukuza demokrasia: Sio siri wenzetu wa Kenya wametuacha katika hili. Angalau sasa wamefikia hatua ya kuwa na uwezo wa kubadilisha serikali kwa njia ya kura. Sisi tupo nyuma katika hili. Tunafikiri hakuna maisha nje ya CCM. Yaani tunaogopa mabadiliko. Shirikisho litatuamsha tupende mabadiliko. Hii itakuwa nzuri maana chama chochote kitakachokuwa madarakani kitakaa sawa kikijua kuwa tukicheze atakuja mwingine. Leo ilivyo, CCM wanajua iwe mchana au usiku ni wao tu hata wakifanya makosa namna gani. This is not healthy.

Having said that I must warn Kenya contributors in this forum who come by unergistered identity. Why you guys like swearing, you can't finish your contributions without the word f***k. Can't you do better than this? Again, stop cheating yourself that you are far better than us. We are all poor. Carefully examine who is owning the wealth you claim to possess in Kenya, and you will realise that it is a handful of people. At the end of the day the majority of our people in all sides (Kenya, TZ and Ug) are miserably poor. There is nothing to be proud of. it is this mentality of yours that scare most of Tanzanians to join this noble body.
 
Mi binafsi nafkili Mengi anafaa kuangaliwa na kuchunguzwa ikiwezekana kuhakikiwa kwasababu yeye tayari amekuwa akipambana na watu ambao kwa namna moja au nyingine wanafaida na jamii hap kunnani

Kwa mfano sakata la Kilimanjaro Hotel aliwazubaisha watu sana na kutaka kuleta sura ya rushwa ati mnunuzi wa Hoteli ile hakuzingatia sifa na ametumia Rushwa kupata Hoteli lakini baadae mwishoni tulioona hakuna kitu kama icho na sasa wananchi wanafidika kutoka na kodi mbalimali zinazo kusanywa kutokea pale kaika Hoteli ile

Sasa ameingia kwa Manji na analeta sura ya uzawa ili kujipatia watu watakao mkubali katika maslahi yake na hii ni baada ya kushindwa katika sura ya kwanza ya udini

Lakini vile vile leo pia tayari ameingizwa na waziri mkuu katika sakata kisa maslahi yake

Mi binafsi sitaki kusema Mengi Hafai au Anafaa kwasababu kuna sekta maalum za kazi hizo lakini ningeshauri hili lishughulikiwe mapema kabla halijaleta makundi makubwa na hatimaye mvurugiko wa sifa na mihimili ya amani ya nchi yetu kama Mengi ana haki yake basi apewe asinyimwe kwakuwa hayupo serikalini kwwa namna yeyote ile iangaliwe haki yake apewe kama hana basi aangaliwe kwa kina asijekuwa chanzo cha tatizo
Naamini wahusika ujumbe utawafikia na mtaangalia nini cha kufanya kwa kutumia kanuni na utaratibu wa kazi yenu

Mwisho ujumbe umetokana na maoni ya kichwa changu ambacho kinaubinadam hivyo si hukum wala support kwa mtu yeyote bali ni mchango katika kutafuta suluhu na mafanikio ya taifa kwa nguvu za umoja wa kitaifa
 
Hivi hapa ni mazungumzo baada ya habari au mambo ya muunganao? Tanzania mbona hadi leo mmeshindwa kutatua matatizo ya muungano wa zanzibar na Tanganyika. Tusidanganyane hapa watu wameishaona watapata vyeo basi wanaanza kutukurupusha wote.

Nani alitoa hili wazo? Alikuwa anataka nini hasa kifanyike? Iko wapi katiba ya huu muungano? EU katiba yao iligawanywa watu waisome mpaka leo wanashindana nayo na hivi juzi tu BBC walionyesha jinsi inavyotupwa kwenye majalala, ya kwetu iko wapi? Je hii ni nyenzo ya kuwapa wakenya kazi Tanzania?

JK, Kibaki na Museveni tunataka kuiona katiba ya hili limuungano lenu.
 
Nimejaribu kutafakari maoni ya watanzania kwa muda sasa juu ya kujiunga na shirikisho. Maoni ya watanzania wengi ni kuwa hatujawa tayari. Nami najiuliza ni lini tutakuwa tayari? Halafu hoja kwamba wakenya wapo mbali kiuchumi, hivi ni nani amesema kuwa wakati sisi tukijiweka sawa wakenya watakuwa wanatusubiri ili tuwe sawa?

Maoni yangu ni kuwa kutokuwepo usawa ndio hasa ingekuwa sababu ya kuungana. Kila nchi ina mapungufu na mazuri yake, tunajiunga ili kupiga hatua pamoja. Hata huo umoja wa ulaya ambao watu wanatolea mfano sana, mbona nchi nyingi tu hazifanani kiuchumu, kisiasa, n.k.

Hao ndugu zetu wa Burundi na warwanda wakija tutawaambukiza ustaraabu na pengine upuuzi wao wa kupigana ukaisha maana katika muungano itakuwa hamna cha mtusi wala mhutu. Na sisi Tanzania tutafaidika sana hasa katika maeneo mengi, kwa mfano:
i) kuchangamka kibiashara na katika kazi maofisini. Hii longolongo ya watanzania kupiga story maofisini badala ya kuchapa kazi itaisha
ii) kuvipiga msasa vyombo vyetu vya habari. Ilivyo sasa vyombo vyetu vingi vya habari kazi yake ni kuitukuza serikali tu kama vile viongozi wa serikali ni malaika. Shirikisho litawaamusha waandishi wetu waweze kuandika with a critical mind na waache kulamba viatu vya viongozi.
iii) Kukuza demokrasia: Sio siri wenzetu wa Kenya wametuacha katika hili. Angalau sasa wamefikia hatua ya kuwa na uwezo wa kubadilisha serikali kwa njia ya kura. Sisi tupo nyuma katika hili. Tunafikiri hakuna maisha nje ya CCM. Yaani tunaogopa mabadiliko. Shirikisho litatuamsha tupende mabadiliko. Hii itakuwa nzuri maana chama chochote kitakachokuwa madarakani kitakaa sawa kikijua kuwa tukicheze atakuja mwingine. Leo ilivyo, CCM wanajua iwe mchana au usiku ni wao tu hata wakifanya makosa namna gani. This is not healthy.

Having said that I must warn Kenya contributors in this forum who come by unergistered identity. Why you guys like swearing, you can't finish your contributions without the word f***k. Can't you do better than this? Again, stop cheating yourself that you are far better than us. We are all poor. Carefully examine who is owning the wealth you claim to possess in Kenya, and you will realise that it is a handful of people. At the end of the day the majority of our people in all sides (Kenya, TZ and Ug) are miserably poor. There is nothing to be proud of. it is this mentality of yours that scare most of Tanzanians to join this noble body.


Yote uloongea YOU ARE RIGHT MAN! The prob is not Kenya... Not Uganda! No... Why Tanzanians fear Uganda? Labda hiki ndo wengi wanashindwa kuelewa. Ukisoma mawazo ya wengi utaona wanawapenda waganda kama waganda lakini HAWAMPENDI MU7. Wanamjua huyu kiumbe! Si wa kumchekea. Ajabu ndo anahaha ili tuungane aone kama anaweza kutimiza ndoto yake ya kuwa rais wa Afrika Mashariki. Hana maana huyu!

Kuhusu Kenya: Nilikuwa naangalia EATV na nikawa nasikiliza mawazo ya watanzania walio wengi. Wengi walionekana kutopenda kuungana na wakenya sababu zikiwa kuu 3.

a) Wakenya hawana UTU. Hii imeongelewa na wengi wakidai wakenya dhamira yao kwenye muungano huu si kuwa na udugu na kusaidiana kuinuana kiuchumi. Wanadai wakenya kwao ardhi imekuwa aghali sana na ajira ni mzozo. Wanatamani wahamie kabisa Tz lakini bado wanaona kuna kiwingu. Hapa wanafanya kila liwezekanalo tuwe sote ili wajidunge Bongo kirahisi kwakuwa firms nyingi ambazo zimetokea Kenya zinapenda kuwaajiri wakenya kwa kigezo kuwa WAMESOMA SANA.

b) Wakenya wametuzidi kielimu: Hapa naona watanzania wanashindwa kuelewa maana ya ELIMU. Kama elimu wanayoiongelea watanzania ni Kiingereza (kama watangazaji wa kipindi husika walivyoonekana kusema) basi wamepotea sana. Kuna haja ya kuwafanya wajue maana ya elimu. Pia nasi ni wasomi sana hadi kuwa na lugha moja inayoweza kuongeleka nchi nzima hadi nje ya nchi. Kiswahili ni lugha ya kujivunia. Nilitarajia watanzania waone kuwa hii ndo fursa ya kuwafanya hawa watu wakithamini kiswahili na waache kuutukuza u-kiingereza ili kwa sauti moja tuweze kupiga hatua kubwa kimaendeleo.

3. Kuwa wakenya ni wajanja sana kuliko sisi: Hapa bado napingana na wenye mwelekeo huu. Huu ni woga ambao sijui nani kawajengea watanzania. Mara zote niendazo Nairobi huwa nawaona vilaza hawa wakiwa hawajui mambo mengi hasa ya teknolojia. Wale wanaoiona Kenya imeendelea sana au wanadai wana ujanja kuliko sisi basi wanashindwa kuelewa maana ya ujanja. Hawa si wajanja NI WEZI. Tena wizi wao wanakuibia kwa wewe kutojua lugha ya kiingereza (udhaifu wa watanzania walio wengi). Aidha wao si wasomi kama wadhaniavyo walio wengi. Hawa ni wasanii tu na ukiwajulia basi unawaliza kila siku.

Nasikitika watanzania hawajithamini na kujiona wao wanyonge. Ni kweli polepole ya kobe humfikisha mbali. Wanachofanya wakenya si ujanja... Ni usanii tu ambao mwisho wake daima huishia kama walivyo sasa. Hawana uhakika na ajira. Halafu kwa usanii huu ndo wanaishia kuonana ubaya. Ki-demokrasia sidhani kama wao ni wajanja kwa njia wazitumiazo kudai haki. Mwanasiasa naona huenda hawa jamaa hujajua upungufu wao. Kushinda kwa Kibaki kumekuja baada ya SOTA NDEFU SANA. Najua una background yote. I believe hata Freeman akiendelea hivi we can beat these Kenyans tena kwa njia ambayo wewe utakubali watanzania wana akili kuliko wadhaniwavyo!

Anyway, yote ni kheri... Mimi sipendi kuwa na muungano na jamaa hawa lakini kwakuwa wakubwa wameshaamua hatuna jinsi... Ni kelele za vyura baba!
 
Yote uloongea YOU ARE RIGHT MAN! The prob is not Kenya... Not Uganda! No... Why Tanzanians fear Uganda? Labda hiki ndo wengi wanashindwa kuelewa. Ukisoma mawazo ya wengi utaona wanawapenda waganda kama waganda lakini HAWAMPENDI MU7. Wanamjua huyu kiumbe! Si wa kumchekea. Ajabu ndo anahaha ili tuungane aone kama anaweza kutimiza ndoto yake ya kuwa rais wa Afrika Mashariki. Hana maana huyu!

Kuhusu Kenya: Nilikuwa naangalia EATV na nikawa nasikiliza mawazo ya watanzania walio wengi. Wengi walionekana kutopenda kuungana na wakenya sababu zikiwa kuu 3.

a) Wakenya hawana UTU. Hii imeongelewa na wengi wakidai wakenya dhamira yao kwenye muungano huu si kuwa na udugu na kusaidiana kuinuana kiuchumi. Wanadai wakenya kwao ardhi imekuwa aghali sana na ajira ni mzozo. Wanatamani wahamie kabisa Tz lakini bado wanaona kuna kiwingu. Hapa wanafanya kila liwezekanalo tuwe sote ili wajidunge Bongo kirahisi kwakuwa firms nyingi ambazo zimetokea Kenya zinapenda kuwaajiri wakenya kwa kigezo kuwa WAMESOMA SANA.

b) Wakenya wametuzidi kielimu: Hapa naona watanzania wanashindwa kuelewa maana ya ELIMU. Kama elimu wanayoiongelea watanzania ni Kiingereza (kama watangazaji wa kipindi husika walivyoonekana kusema) basi wamepotea sana. Kuna haja ya kuwafanya wajue maana ya elimu. Pia nasi ni wasomi sana hadi kuwa na lugha moja inayoweza kuongeleka nchi nzima hadi nje ya nchi. Kiswahili ni lugha ya kujivunia. Nilitarajia watanzania waone kuwa hii ndo fursa ya kuwafanya hawa watu wakithamini kiswahili na waache kuutukuza u-kiingereza ili kwa sauti moja tuweze kupiga hatua kubwa kimaendeleo.

3. Kuwa wakenya ni wajanja sana kuliko sisi: Hapa bado napingana na wenye mwelekeo huu. Huu ni woga ambao sijui nani kawajengea watanzania. Mara zote niendazo Nairobi huwa nawaona vilaza hawa wakiwa hawajui mambo mengi hasa ya teknolojia. Wale wanaoiona Kenya imeendelea sana au wanadai wana ujanja kuliko sisi basi wanashindwa kuelewa maana ya ujanja. Hawa si wajanja NI WEZI. Tena wizi wao wanakuibia kwa wewe kutojua lugha ya kiingereza (udhaifu wa watanzania walio wengi). Aidha wao si wasomi kama wadhaniavyo walio wengi. Hawa ni wasanii tu na ukiwajulia basi unawaliza kila siku.

Nasikitika watanzania hawajithamini na kujiona wao wanyonge. Ni kweli polepole ya kobe humfikisha mbali. Wanachofanya wakenya si ujanja... Ni usanii tu ambao mwisho wake daima huishia kama walivyo sasa. Hawana uhakika na ajira. Halafu kwa usanii huu ndo wanaishia kuonana ubaya. Ki-demokrasia sidhani kama wao ni wajanja kwa njia wazitumiazo kudai haki. Mwanasiasa naona huenda hawa jamaa hujajua upungufu wao. Kushinda kwa Kibaki kumekuja baada ya SOTA NDEFU SANA. Najua una background yote. I believe hata Freeman akiendelea hivi we can beat these Kenyans tena kwa njia ambayo wewe utakubali watanzania wana akili kuliko wadhaniwavyo!

Anyway, yote ni kheri... Mimi sipendi kuwa na muungano na jamaa hawa lakini kwakuwa wakubwa wameshaamua hatuna jinsi... Ni kelele za vyura baba!

Hapa umegonga nyundo. Our core problem is lack of confidence, may be low self-esteem as well. Nimeshafanya kazi na wakenya katika maeneo mbalimbali, hawana wanachotuzidi kama wakenya. Na ukikaa nao katika anga za academia utagundua wana shida sana katika elimu yao. Watanzania lazima tukatae kujidhalilisha. kama ni kiingereza, nani amesema kwamba sisi watanzania hatuwezi kujifunza kiingereza. tena Mungu katujalia lafudhi nzuri, mtanzania anayekijua kiingereza akiongea utatamani aendelee. Hao wakenya kwanza accent zao sio kiingereza.

Jamani ehee, tuacheni woga. Kukataa kujiunga hakutufanyi tuwafikie hao wakenya katika hiyo elimu, uchumi, n.k. Swala hapa ni kukabiliana na ukweli wa mambo. Tupambane na tukubali kubadilika. Tatizo letu tunaogopa sana mabadiliko. Tukikataa future itatupita, tutaiacha nyuma. Yangu macho.
 
JAMANI MBONA SIJASIKIA CHOCHOTE KUHUSU KATIBA YA MUUNGANO WA EAC...?? SASA WANANCHI WATAJADILI NINI BILA KUJUA KILICHOKUBALIWA AU KUKATALIWA...??
 
Hey
Watanzania wezangu kitu muhimu kuna tofauti kati ya shirikisho na jumuia
shirikisho la sasa linalotaka kuundwa yani ni kutokomeza jina kenya jina tanzania jina rwanda jina uganda jina burundi na kuwa nchi moja inayoitwa shirikisho ya afrika mashariki.

ile jumuia ya mwanzo ilikua inajumuisha mambo kadhaa na mambo mengine yalikua yanashugulikiwa na nchi husika ,hivyo basi kutakua hakuna wizara ya tanzania ila wizara ya shirikisho,kutakua hakuna hospital ya tanzania ila ya shirikisho

Sasa basi watanzania tunachokataa ni ikitokea Raisi akatokea kenya wizara zote na sehemu nyeti zote si watajaa wakenya si kwamba eti wakenya wamesoma wanatuzidi hakuna hilo halipo mbona wako shallow balaa si tunao ila watatumia ukabila na ukenya

Kama mnataka kukubali hili, saizi wanauchaguzi angalieni kampeni zinavyoendeshwa yani ni unakuru ,ukarejing u kisumu,u lift valley ndio siasa zao, ukirudi rwanda kama ni mtusi vigongo wa juu ni watusi ,uganda da burundi ndio basi.

Jumuia ya ulaya hii ni jumuia tu na haikuvunja nchi na kua na raisi mmoja kila nchi inafanya kama nchi ila wana mambo machache wanayoshirikiana
hili swala lakua nchi moja jamani watanzania tuliangalieni kwa makini
ukiangalia babu, mama na bibi zetu wana mashamba na nyumba lakini hawana hati miliki za mali hizo.

Upande mwingine wewe mwenyewe huna dokomenti inayokubainisha kua ni mtanzania jamani mtanyaganywa kila mlichonacho kuweni makini
hawa manyang'au wa kikenya na kiganda wamejiaandaa siku nyingi kutuvamia wao ardhi yote wameigawa na hati miliki pia wanavitambulisho
jeje wewe mtz ?

Tukaeni pamoja tulikatae shirikisho bila hivyo watanzania tumeliwa
Asili ni asili tu hakuna asili mbovu ikiwa nchi moja bado kuna LRA watataka kuingia madarakani kwa silaha ,bado wanyarwada watataka kutawala ,warundi maana asili haipotei kabisa na bado watakua na ushawishi maana
wana majeshi mwisho wa mwisho tutashangaa na sisi tunakua wakimbizi
wa kivita kongo au malawi
Peter Mkama -Poaland
 
Peter unaweza kuwa ndo unanijua... Naomba tuwasiliane HARAKA. Kama ni wewe Electrical Engineer. If yes I need your attention... Jisajili then tuma PM
Muhimu kaka
 
naomba unitumie ktk email yangu maana nitajisajili baadae
harafu sijakuelewa pia wewe ni nani
naomba ufanye vivyo
 
Back
Top Bottom