East African Federation (EAF) public Views

East African Federation (EAF) public Views

kinyang'anyiro hicho.CHADEMA na mgombea kwa pamoja walifanikiwa kuweka bayana kwamba katika masuala ya kitaifa, utanzania unakuwa kitu cha kwanza kabla ya vyama na tofauti za kiitikadi chini ya kauli ya kampeni „SIASA SI UADUI-TANZANIA NA AFRIKA KWANZA". Hivyo, timu inapenda kuchukua fursa hii kuwapongeza wabunge wachache waliotambua ubora huu na kumpigia kura Profesa Mwesiga Baregu bila kutanguliza kwanza maslahi ya chama chao.


b) TUMEBAINISHA MAPUNGUFU YALIYOMO KATIKA MCHAKATO WA UCHAGUZI NA TABIA YA WENGI YA WABUNGE KATIKA KUPIGA KURA: kwa ujumla mapungufu mbalimbali katika kanuni na taratibu za uchaguzi yameweza kubainika. Kwa upande mwingine tabia ya wabunge katika kupiga kura imebanika kama ambavyo imedokezwa katika mapungufu yaliyotajwa hapo juu. Hii ni hatua muhimu katika kuboresha mchakato wa uchaguzi wa bunge la Afrika katika chaguzi zijazo.


MAPENDEKEZO NA MWELEKEO:

(i) UCHAMBUZI UFANYIKE KUBAINI KIASI NA ATHARI ZA „SIASA ZA UNDUGU KWA MUSTAKABALI WA TAIFA: Suala la kuongezeka kwa viongozi wanaochaguliwa wenye uhusiano wa kindugu na wale waliokatika nafasi mbalimbali linapaswa kufanyiwa uchambuzi. Zipo hisia kwamba kama mtindo huu ukiendelea kutajengeka tabaka la nasaba za watawala(royal classes) na watawaliwa. Kama hali hii ikitokea ni hatari kwa umoja wa Taifa. Ni vyema wakati wote mfumo wa uchaguzi na kisiasa ukatoa haki na uhuru kwa watanzania wote.

(ii) UANGALIZI NA UTAZAMAJI WA UCHAGUZI UFANYIKE KATIKA CHAGUZI ZOTE KATIKA HATUA ZOTE: Uchaguzi wa bunge la Afrika Mashariki kama zilivyo chaguzi nyingine ni mchakato unaopaswa kuwa huru na haki katika ngazi na hatua zote. Kwa mantiki hiyo suala la haki kutendeka ni la muhimu lakini suala la haki kuonekana ikitendeka ni la muhimu zaidi. Hivyo jitahada za makusudi zifanywe na wote wanahusika kuhakikisha kuwa chaguzi zijazo za bunge la Afrika Mashariki zinakuwa na waangalizi(monitors) na watazamaji(observers). Hii ni muhimu hususani wakati huu ambapo jumuia ya Afrika Mashariki inaelekea kuchukua nafasi ya pekee katika maisha ya wananchi wa nchi wanachama.


(iii) KAMATI ZA VYAMA(PARTY CAUCUS) ZISITUMIKE KUBAKA DEMOKRASIA: Katika mazingira ya sasa kamati za vyama(party caucus) zimekuwa zikitumiwa vibaya na chama tawala. Suala la kuwa na kamati za vyama ama kambi(party/camp caucus) ni suala la kawaida katika demokrasia ya mfumo wa vyama vingi kote duniani. Hata hivyo katika mabunge yanayoheshimu haki na uhuru wa mawazo na maamuzi kamati za vyama/kambi ni fursa ya serikali ama mamlaka kutoa UFAFANUZI na KUSHAWISHI. Lakini hapa kwetu chama tawala kimekuwa kikitumia kamati ya chama kutoa SHINIKIZO na MAELEKEZO kwa wabunge. Na wabunge wengi kwa upande wao wamekuwa wakisukumwa na mashinikizo hayo na kufanya maamuzi kwa kuzingatia kile wanachokiita MSIMAMO WA CHAMA. Tunachukua fursa hii kuwakumbusha wabunge kwamba ninyi ni WAWAKILISHI WA WANANCHI hivyo mnapaswa kuweka mbele MASLAHI YA UMMA kabla ya maslahi ya chama ama maslahi binafsi. Kumbukeni kuwa mmechaguliwa na wapiga kura wa vyama mbalimbali na wasio wanachama wa chama chochote hivyo ni muhimu kwenu kuweka mbele maslahi ya Taifa.


(iv) UWAKILISHI WA BUNGE LA AFRIKA YA MASHARIKI UPANULIWE NA MFUMO WA UPATIKANAJI WA WABUNGE WAKE UBORESHWE: Idadi ya wabunge wa sasa(tisa kwa kila nchi) ni ndogo ukilinganisha na maslahi yanayojadiliwa katika bunge la Afrika ya Mashariki hususani wakati huu ambao tunaelekea katika soko la pamoja na hatimaye baadae shirikisho la kisiasa. Katika hali kama hiyo kuna haja ya kujadili suala la kupanua uwakilishi lakini pia kutengeneza daraja mwafaka baina ya bunge la Afrika ya mashariki na mabunge ya nchi husika. Aina mbalimbali za uwakilishi zitafakariwe ikiwemo suala la kuwa na sehemu ya wawakilishi ambao watapigiwa kura za moja kwa moja na wananchi wa nchi husika hususani katika hatua ya shirikisho. Pia kuna haja ya kuzifanyia marekebisho kanuni za bunge ili kuzingatia pia uwiano wa kura kwa upande wa Zanzibar pamoja na kutumia kura za ujumla badala ya kutumia idadi ya viti bungeni kama kigezo pekee.

(v) WANANCHI WAYAJADILI MASUALA YALIYOIBULIWA NA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KUTOA MAONI YAO KUHUSU MCHAKATO KUUNDA SHIRIKISHO LA AFRIKA YA MASHARIKI: Katika uchaguzi huu masuala mbalimbali yaliibuliwa kuhusu mambo ya kuzingatiwa katika muktadha wa uundwaji wa shirikisho la Afrika ya Mashariki. Ni wakati mwafaka sasa wa kuyajadili kwa kina masuala haya na kutoa maoni katika kamati iliyoundwa ya kukusanya maoni. Baadhi ya mambo hayo yamedokezwa katika sehemu ya mafanikio. Aidha tunatoa mwito kwa wote waliokuwa wagombea pamoja na vyama vyao kuendeleza mjadala wa masuala mbalimbali yaliyoibuliwa kwa maslahi ya watanzania, Afrika ya Mashariki na Afrika kwa ujumla. Hakuna kulala, Mpaka Kieleweke.

CHADEMA: Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Imetolewa na:



John Mnyika
Aliyekuwa Mratibu wa timu ya kampeni
Na Mkurugenzi wa Vijana Taifa
0754 694 553
www.chadema.net
18/11/2006
 
nashukuru kupata nafasi hii ya kuchangia uwepo/kutokuwepo kwa jumuiya hiyo.akumbuka hapo zamani nikiwa mdogo kulikuwa na jumuiya hii ambayo wazee wetu waliiunda ikawafaa lakini kuna wajanja wakafanya kaujanjaujanja wa kipuuzi tu wakauvunja,leo hii wapo!mimi nafikiri tuwaite!hatuwasuti la hasha ila ni kuwaomba watueleze nini walikiona mpaka wakapata mwazo yale!

Kwa kweli watanzania tuliumia sana maumivu hadi leo hii yapo,walituvuruga kabisa wenzetu kenya waliendelea na sera za kibepari wakawa na viwanda vingi vikiwemo vilivyokuwa kwenye jumuiya,sisi tukaanza mwanzo shilingi ilishuka ghafla thamani na uchumi ukaporomoka!

Tukajikongoja kusogelea uchumi imara ,kutengeneza caricula mpya za Elimu na kadhalika.Leo hii sisemi tupo pazuri sana ila hali inatia moyo"promising" ijapokuwa jinamizi la umeme limeingia!Hawa watu(Kenya na Uganda) wanaona ala kumbe eneo lao dogo!haliwatoshi watanzania wana mapori mengi ngoja tujiunge nao.HATUTAKI!

Naomba watanzania tuliangalie kwa kina hili!mengine tutachangia siku nyingine.
 
To my fellow Kenyans, i know there has been a silent agreement to ignore this site, but i want to seek your indulgence and write as hereunder:

Now, fellow East Africans, forget about this EAF. There is even a bigger problem in our midst that we need to adress before we come together; and this is the question of Zanzibar's independence. How can we talk about the Fed. when a part of Africa is still under mikono ya wakoloni, i.e. Zanzibar under TZ? Why are the Tanganyikas under this wrong illussion that Zanzibar is a poor colony of theirs and that the latter needs them more and not the other way round?

I have been to both TZ Bara and Zanzibar, and i can confidently say that Zanzibaris live a much better life than their mainland counterparts, even better than the rest of East Africans. They have such a booming tourism industry, and i can easily compare Zanzibar with the Seychelles in terms of size and natural wealth. My conviction therefore is that sahau EAF, let's all start agitating for Zanzibar's total independence, and thereafter we can think of the Fed. Tanganyika, SHAME ON YOU!!!!
 
Katika ulimwengu wa leo, kila nchi ina haki yakujiamulia mustakbal wake. Je Zanzibar haina haki ya kujiamulia mustakbal yake? Je wanzanzibari wataendelea kunyanyaswa na mali yao ghafi kunyonywa na mabepari watanganyika? Mbona hamna huruma jamani?

Tumeitwa kila aina ya mjina k.m. wasaliti, makuli, ngumbaru n.k. Lakini ukweli utasemwa, mahasid wapende waipende. Mpasuko Zanzibar umechochewa na mabaradhuli toka Tanganyika. Wengine wanaota ndoto kuwa Zanzibar ni koloni la tanganyika! wanajifanya kuwa wako tayari kukabiliana na yeyote anaye itakia mema Zanzibar! Zanzibar... hao waotao ita kuwa huru.

Katika akili zao, wanao kwamba wamekwisha kutumaliza, walakin hawajui kwamba tunawamulika. Kama alivyosema Mzanzibari .... Ipo Siku.....Ipo Siku... Zanzibar ita kuwa huru.
 
Dear Friends,

It has been long since I contributed to this forum. I have been away for all those who appreciate the need for careful analysis I say listen. East African Federation is a good idea, implementation is the challenge. Particularly for the people of Zanzibar.

Our thinking is largely eastern based, our culture and beliefs too. While our brothers on the mainland their thinking is southern. They tricked our businessmen into living COMESA for SADAC promising us big things! Yet some of our business relations are in Egypt and Libya which are in COMESA. Today our businessmen are suffering because of the hila mbovu of the mainlanders!

I agreed with Dr. Mohamed Kassam, we need to decide our fate (yaani mustakbal wa Zanzibar) because then we can rejoin COMESA and consequently EAF. It is true that some people in the mainland who recently became rich want to grab Zanzibar's wealth! (mali ghafi) These day dreamers keep asking Eti Zanzibar ina mali ghafi ipi? shocking!

Kwakweli hawana hoja, our relatives in Oman, Baharain, Libya, Egypt and Saudi Arabia send money back home for TRA and some vigogos to chew! We shall be free and we shall stop those parasites from sucking damu yetu!

Zanzibar is rich and can do well without the chains that are imposed by the muungano! Ukweli utasemwa kila siku! Tukidai haki zetu tuna pokea matusi chungu tele!

Mengine baadae.
 
[/B]
Dear Friends,

They tricked our businessmen into living COMESA for SADAC promising us big things!

Who was tricked to leave Comesa. If Zanzibar was tricked to leave COMESA who was representing them at that particular time? What are the facts?

Yet some of our business relations are in Egypt and Libya which are in COMESA. Today our businessmen are suffering because of the hila mbovu of the mainlanders!

Doesn’t Zanzibar have their own president and cabinet, why do they allow this hila mbovu?

It is true that some people in the mainland who recently became rich want to grab Zanzibar's wealth! (mali ghafi) These day dreamers keep asking Eti Zanzibar ina mali ghafi ipi? shocking!

What does ‘mali ghafi’ mean? I think you are confusing yourself with words check in the dictionary.

our relatives in Oman, Baharain, Libya, Egypt and Saudi Arabia send money back home for TRA and some vigogos to chew!

TRA is a big organisation if you can give us some details and proof of this will appreciate!


Zanzibar is rich and can do well without the chains that are imposed by the muungano!

Really, I and others are interested to know this chains imposed by muungano it will shade some light to Tanganyikans the way they profit from you?


Wacha
 
It is quite clear that we, Tanzanians, DO NOT want OUR country to enter in the East African Federation.

Those friends of ours who post something about Zanzibar problem actually UNDERLINES why we DO NOT WANT to enter the federation: we have problems to sort out in our EXISTING union. Until we do that, we cannot complicate the issues further by joining yet another Union. For that matter, we WISH Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi success in the east africa federation -- where we will be able to learn from THEM a thing or two on how to iron out problems in a union. They can go on without Tanzania, can't they?

Continue posting about Tanganyika-Zanzibar union problems, the posts help awaken some persons who somehow have forgorten union problems, and want to bring into Tanzania even worse woes of east africa federation.

Long live Tanzania
http://mlenge.blog.com
Mlenge
 
We Tanzanians DO NOT want OUR country to join the east africa federation. Somalia, Rwanda, Uganda, Burundi and Kenya, or anyone for that matter, can form the federation -- but Tanzania is staying out.

Mlenge
http://mlenge.blog.com
 
Continue posting about Tanganyika-Zanzibar union problems, the posts help awaken some persons who somehow have forgorten union problems, and want to bring into Tanzania even worse woes of east africa federation.

Long live Tanzania

Thank you brother! but si umesahau? inapaswa kuwa long live Tanganyika na Long Live the Great Zanzibar!

Naona watanganyika wameanza kuelimika taratibu. Zanzibar itakuwa huru na kupe kama kina WACHA itabidi waelekeze nguvu zao zaukandamizaji kule Malawi na Msumbiji. Mjadala uendelee..............
 
Continue posting about Tanganyika-Zanzibar union problems, the posts help awaken some persons who somehow have forgorten union problems, and want to bring into Tanzania even worse woes of east africa federation.

Long live Tanzania

Thank you brother! but si umesahau? inapaswa kuwa long live Tanganyika na Long Live the Great Zanzibar!

Naona watanganyika wameanza kuelimika taratibu. Zanzibar itakuwa huru na kupe kama kina WACHA itabidi waelekeze nguvu zao zaukandamizaji kule Malawi na Msumbiji. Mjadala uendelee..............

Lete facts kama hapo juu, Usipige kelele tu! haya ndio mambo ya uswahili tusiyotaka .............. unataka kukimnbilia matusi ni jadi yako siyo?
 
Zamani mabepari ndio walokuwa vibaraka, leo vibaraka ni kinanani si watanganyika: Kwakeli hiyo arrogance yako WACHA utakoma ukisoma yafuatayo:Tupe haki yetu natutawaacha kwa amani! Katika hii piece utaelewa wanyonyaji nikinanani, kupe wako wapi n.k. facts tupu.


Zanzibar's Political Instability

The roots of Zanzibar's political instability lie in a complex set of divisions that characterize the archipelago's relations with its African mainland federation partner -- the former Tanganyika -- and partially overlapping regional, ethnic and economic splits within its domestic society that are aggregated by its two contending parties.

Mainland Tanzania's population of approximately 40 million people dwarfs Zanzibar's one million. Their union came in 1964, a year after Zanzibar gained independence from Great Britain and a revolution generated by the country's African majority quickly overthrew the traditional Arab political class through which London had exercised its standard practice of indirect colonial rule. Having a left and even communist direction, the revolution excited the concern of Tanganyika's more moderate socialist regime, which had a vital interest in tamping down instability off its Indian Ocean coast.

In order to secure its interests, Dar es Salaam offered Abeid Karume, the leader of Zanzibar's revolution and the current president's father, a plan for a unique form of federation in which the archipelago would have control, through its own executive and legislature, of all policy areas except defense, foreign relations and high finance. There would be one president and parliament for the federation and no separate autonomous institutions for Tanganyika. The elder Karume accepted the deal in the interest of securing protection for his rule and fused the revolutionary movement with the C.C.M., which had governed Tanganyika since it won independence from Great Britain in 1961 and has ruled the Tanzanian federation since union was achieved.

The federal bargain has served the purpose of perpetuating the rule of the revolutionary leadership and the machine that it has constructed, but it opened up divisions between the archipelago and the mainland, and it did not heal the splits within Zanzibar, leading to chronic disaffection among supporters of the revolution's losing side that has spread to other segments of the population, particularly the country's majority of poor. In the four decades following union, Zanzibar's political forces have polarized, with the C.C.M. hanging on to power and discontent with the regime flowing into the C.U.F.

On the federation level, Zanzibaris share a general consensus that the archipelago has not received fair economic treatment from Dar es Salaam. During the 2005 electoral campaign, Hamad proposed that the federal bargain be revised to create a separate governmental apparatus for the mainland, leaving the federation's institutions competence over defense and foreign relations. Such an arrangement, which is opposed by Dar es Salaam, would presumably allow Zanzibar to retain more of its economic product.

Dissatisfaction with the federation within Zanzibar is complicated by the archipelago's domestic divisions, which have thus far stalled any initiatives to redress perceived imbalances. Most obvious is the regional split -- underlined by the recent election results -- between Unguja and Pemba, which has similar complaints about the C.C.M. regime in Unguja's Stone Town to those that Zanzibar has about the administration in Dar es Salaam.

Overlaid on the regional divide is the persisting split between the African population, augmented by migrants from the mainland, and the archipelago's other ethnic groups, particularly descendants of the Arab population. Adding to the picture is the divide between those who have benefited from the archipelago's growing tourist industry, which is centered in Stone Town, and the urban poor and agricultural workers on the government-owned spice plantations, which is the other pillar of Zanzibar's economy.

Although the complex divisions in Zanzibar's society do not fully overlap, they have compounded sufficiently over the decades to give the C.U.F. the support of at least half the archipelago's electorate and to embolden it to propose major reforms, most importantly privatization of the clove plantations.

The polarization of Zanzibar's politics and the instability that it creates would not awaken concern outside East Africa were it not for the fact that the persisting tensions and stasis have opened up a gap that has begun to be filled by Islamist movements appealing to the poor among the archipelago's 98 percent Muslim population. The C.C.M. regime has responded to the rise of Islamism by banning Islamic parties, which has driven the movement to give tacit and sometimes overt support to the C.U.F.

In turn, Hamad has warned that unless the C.U.F.'s demands are met, Islamism will spread. Karume has responded that the C.U.F. has been tainted by Islamism and is the stalking horse of the fundamentalists. Islamist leaders, meanwhile, keep up a drum fire of advocacy for an Islamic state as the only alternative to failed democracy.

The Bottom Line

With Western donor countries, most importantly Great Britain, firmly backing the C.C.M. regime in Dar es Salaam on the basis of its liberal economic reforms, its popularity on the mainland and its cooperation in the campaign against Islamic revolution, it is unlikely that strong external pressure will be brought to resolve Zanzibar's political tensions through mediation, as the C.U.F. desires.

Look for the confrontation between the C.C.M. and C.U.F. to deepen and for secessionist forces within the C.U.F. to gain more power in the party. Meanwhile, Islamism will make greater inroads in a region where it previously had little appeal, opening up a new trouble spot for Western powers.

Natumai umekwisha elewa, vibaraka, kupe na wanyanyasaji ni kinanani!
 
Mlenge umenifurahisha sana ndugu yangu. Tunahitaji watu wanaoweza kujenga hoja namna hii. Nimekuona juzi kwenye kipindi cha Sema Usikike ukihojiwa na Ayubu Rioba na nilihamasika sana. KAZA UZI, na ni wengi tunaokuunga mkono.

Pengine hunikumbuki lakini tulikuwa wote katika shule uliyosoma mwaka 1990 hadi 1992, na sote tulishiriki kikamilifu katika kujenga hoja kwenye malumbano mbalimbali, wakati huo tukizungumzia sana kuvunjika kwa iliyokuwa USSR na kuporomoshwa kwa ukuta wa Berlin.

Nilikuwa pro-socialism (sijaacha!), na japo matukio mawili ninayoyatolea mfano (kusambaratika kwa USSR na kuungana kwa Ujerumani) yanaelekea kupingana (kuvunjika kwa taifa moja na kujengwa kwa lingine) na kushabihiana kwa wakati huohuo (kusambaratika kwa mfumo wa kijamaa), ninayachukia yote mawili kwa sababu yalitoa mwanya kwa ustawi wa mfumo kandamizi uliobomoa misingi ya utu na kuneemesha mfumo dhalimu wa kibepari.

Ubepari ndio chanzo cha uovu wote ulioenea duniani sasa hivi, na ndio unaostawisha mambo maovu kama ugaidi, vita vya kugombea rasilmali n.k. Ubepari ni unyama! Ndio sababu yangu ya kukataa hili shirikisho la Afrika Mashariki, kwanza kwa sababu lina msingi wake katika ubepari na ukoloni mkongwe, ambao unataka kusambaa kama saratani. Sasa hivi tayari tuna magonjwa yaliyoletwa na ubepari katika Tanzania, sihitaji kutaja jinsi pengo la kipato na ubora wa maisha lilivyo kubwa kati ya maskin na tajiri, tunahitaji ufumbuzi wa matatizo haya.

Tumevamiwa pia na gonjwa lingine: utandawazi ambalo ni jina lingine la ukoloni mamboleo. Sasa mgonjwa huyu ananyemelewa pia na waathirika wa mifumo msonge ya kibepari (Kenya, Uganda) na wale wa maradhi nyemelezi ya mifumo dhalimu ya kibaguzi (Rwanda, Burundi), na ndipo atakapokuwa mahututi kabisa na pengine kufa, hii ni mbinu ya hawa wenzake (Kenya,Uganda, Rwanda, Burundi) kujipunguzia kwa namna fulani makali ya shida zao. Ni upanuzi wa himaya unaofanya kazi kama yale magugu-maji ya Ziwa Viktoria ambayo sasa hayaruhusu mimea mingine kustawi! Hayo ndiyo yatakayotukuta.

Hili sio shirikisho, ni sulubisho!
Shime watanzania, tuungane tulikatae hili jitu (monster) linalojiita Federation! Ni hatari kuliko UKIMWI!
 
Zamani mabepari ndio walokuwa vibaraka, leo vibaraka ni kinanani si watanganyika: Kwakeli hiyo arrogance yako WACHA utakoma ukisoma yafuatayo:Tupe haki yetu natutawaacha kwa amani! Katika hii piece utaelewa wanyonyaji nikinanani, kupe wako wapi n.k. facts tupu.


Zanzibar's Political Instability

I had seen this article before. (written on 15 November 2005) for those who haven’t seen it, the link is http://www.pinr.com/report.pnp .or type PNIR - Intelligence brief:Zanzibar This is what we call ‘copy and paste’ or plagiarism. Without giving credit to the person who wrote it in the first place.

Anyway my questions haven’t been answered and are still valid after reading what you claimed in your article before:

As you said before:
They tricked our businessmen into living COMESA for SADAC promising us big things!

Who was tricked to leave Comesa. If Zanzibar was tricked to leave COMESA who was representing them at that particular time? What are the facts?

Yet some of our business relations are in Egypt and Libya which are in COMESA. Today our businessmen are suffering because of the hila mbovu of the mainlanders!

Doesn’t Zanzibar have their own president and cabinet, why do they allow this hila mbovu?

It is true that some people in the mainland who recently became rich want to grab Zanzibar's wealth! (mali ghafi) These day dreamers keep asking Eti Zanzibar ina mali ghafi ipi? shocking!

What does ‘mali ghafi’ mean? I think you are confusing yourself with words check in the dictionary.

Our relatives in Oman, Baharain, Libya, Egypt and Saudi Arabia send money back home for TRA and some vigogos to chew!

TRA is a big organisation if you can give us some details and proof of this will appreciate!


Zanzibar is rich and can do well without the chains that are imposed by the muungano!

Really, I and others are interested to know this chains imposed by muungano it will shade some light to Tanganyikans the way they profit from you?

If it was an exam you have failed to answer the fundamental questions you raised in the first place. I mean 0%

And let me assure you that the majority of Tanzanian mainlanders wanted this union to break not today or tomorrow but yesterday.

Ndio tunarudi pale pale sisi wote tunafahamu kinachoendelea lazima tuwe wakweli na tujadili mambo haya kwa uwazi, ili kuyaweka sawa kama tukianza ubabaishaji hatufiki mbali.

Wacha
 
Jamani Ndugu zangu,

Kwanza najivunia kuwa Mtanzania, ukiondoa historia sijui Mkutano wa Berlin, enzi hizo uliosuruhisha ugomvi wa wakoloni na kupelekea mgawanyo wa bara la Afrika hadi tukawa na mipaka tuliyo nayosasa. bali nasifu na namshukuru Mungu kwa kuwajalia hekima viongozi wetu waliofanya juhudi za kila namna kutufukisha hapa tulipo. Leo hii naweza kutamba kujiita mimi ni Mtanzania (ukipenda Mtanganyika) zaid ya labda ya yeyote katika maziwa makuu kutamba yeye ni wa nchi yake, kwa nguvu na sauti kuu.. haya ni matokeo ya jitihada na mikakati dhabiti ya waanzilishi wa Taifa hili. Umoja wa Kitaifa!

Najua walibezwa, walidharauliwa, na kuonekana wakipoteza damu zao na rasilimali kuhakikisha amani inajikita kwa majirani zetu, lakini kumbe leo tumekuwa ni kisiwa cha amani, na tu wamoja, dini na ukabila bado hazijapata nguvu.

Jitihada hizo hazikuishia hapo, Mwalimu JK, kwa kutambua umuhimu na manufaa, alipigania Muungano wa Afrika Mashairiki, lakini ona jinsi ulivyokuja kuvunjika, tena kwa maumivu na hasara kubwa kwa Tanzania!

Siamini, labda mtu anieleze, tena kwa mifano na nia dhabiti, kwamba, makosa yale, vidonda vile, kweli vimepona, au ni uhafidhina tu na uchu wa watu wachache ambao wanataka kututumbukiza kwenye mtafaruku wa kiuchumi, kijamii na upotevu wa amani!

Naunga Ushirikiano, lakini naamani bado ni mapema mno, hasa kwa Tanzania, ndio kwanza tumeanza kujenga mfumo wa uchumi, tunahitaji uzalishaji wa bidhaa zetu, tunahitaji kusomesha watu wetu tena kwa wingi, tunahitaji kumalizia kuimarisha miundo mbinu, MKUKUTA ndio kwanza umeanza, SACCOS zinapamba moto (naambiwa raia wa nchi jirani wameanza pia kufaidika nazo!); kilimo chetu ni duni; haya ndio masuala ya msingi kwa sasa... Tujiandae.. tunahitaji muda. Tuna matatizo mengi chungu mbovu, yote haya yatamezwa na mbaya zaidi yakiongezeka pale tutakapochukua ya wengine!

Najua ulimwengu unaelekea kuungana, lakini hebu fikiria, je kuna muungano wa masikini kwa masikini? Tulishajaribu huo, tukashindwa, kwa nini hatujifunzi? Basi na tukae chini, tujenge nchi zetu, tupeane malengo, kwamba, bwana Uganda twakuhitaji fanya hiki na kile, maliza mapigano, acha kuvamia wenzako nk, hakikisha uchumi wako unafiki hapa, imarisha hiki na kile, Kenya vilevile, weka wazi nia yako, shughulikia ukabila na mengineyo, Tanzania nayo, uchumi wako ni duni, hebu vuta soksi hadi kiwango hiki!

Watu wengine wamechoka na matatizo ya nchi zao, wanatafuta kuvuta pumzi, jamani, tafadhali, tusaidieni kwanza hukohuko mliko, tunaogopa, na kwa nini msingingatie woga tulio nao, wakati mifano ni ya wazi na inaendelea? Hapa hakuna moshi unaofuka au mawingu kutanda, Kuna MOTO huko na MVUA zinanyesha!

Hatuhitaji "spidi 120" za makabrasha (eti FastTracking EAC!), tunahitaji KAZI, malengo, na viashiria, tupeane MUDA!

Tanzania inahitaji muda, historia imetuonyesha, tukiipuuza tutaumia!
 
Ano

Everybody is talking about 100million people but in the current setting we are 100 million people!!. The main difference between the two is that we are going to have more poor Kenyans move to TZ and live in TZ. This is because

1. We have more land to farm and to live. ( Our natural resources are cheaper)
2. We have fertile land (Our natural resources are fertile)
3. We have growing economy (Human resources are in high demand)
4. We have middle class-market ( Poverty level TZ 37% and Kenya 50%)
5. Tanzania in general is a better country to live than Kenya.

For Tanzania to join the union there's no benefit we should live our current setting because is working for our economy, if we join with the slowing Kenyan economy our economic growth is going to be slow.
 
We should not join with nobody at this point. For the first time Tanzania is experiencing a stable economical growth and we want to change that and join these loosers, this may sound funny in theory but is a dam idea.
 
0% kwakudai haki zawazanzibari!
Ndugu WACHA,

Natumai kuwa uhali njema. Lazma ni kwambie wazi,Wrong number, jaribu kwengine! kwasabu zifutazo.
1. Hayo maswali umeya misdirect, mwanzo kabisa the arguments unazotaja zimeletwa na CHUIWAMASHARIKI, though I fully support maoni yake, he is entitled to his opinion. Kwahivyo nakukosoa kuingwana, ume dial wrong number jaribu kwingineko rafki yangu!

2. Plagarism: inaokena wazi kwamba kisomo chako is just too low! kwani wewe umeona popote ilipotajwa kwamba this article ni by Dr. Mohamed Kassam? Nilidhani ni viroboto tu wenye mawazo hayo!

3. Je unajina? si wewe unatoka MARA, huku mwalana wenyewe kwa wenyewe kama samaki? Au lets put it clearly unadini? Mimi kwetu Mlandege. Hata leo ukiuliza utaambiwa Dr. Mohamed Kassam ninani! Laajabu nikwamba wewe unaona haya kuksema kwamba kwenu ni Mara na hivi sasa mwalana wenyewe kwa wenyewe kama samaki!

4. Kama alivyo sema contributor fulani, "Pilipili iko Zanzibar, wewe uko Mara, inakuwashiaani mtanganyika?

5. Kama unavyo argue wewe kweli huja safiri nje ya Tanganyika. Yendavyo unaona Dar-es-salaama kama New York! Njoo Zanzibar tukufunze ustaarabu hiyo Kibri yako ita koma!

6. 0% Kwa kudai haki zawazanzibari, strange very strange. Ni viroboto kama nyinyi na vibaraka wenu mtakao timuliwa wakti utakapowadia.
 
0% kwakudai haki zawazanzibari!
Ndugu WACHA,

Natumai kuwa uhali njema. Lazma ni kwambie wazi,Wrong number, jaribu kwengine! kwasabu zifutazo.
1. Hayo maswali umeya misdirect, mwanzo kabisa the arguments unazotaja zimeletwa na CHUIWAMASHARIKI, though I fully support maoni yake, he is entitled to his opinion. Kwahivyo nakukosoa kuingwana, ume dial wrong number jaribu kwingineko rafki yangu!

2. Plagarism: inaokena wazi kwamba kisomo chako is just too low! kwani wewe umeona popote ilipotajwa kwamba this article ni by Dr. Mohamed Kassam? Nilidhani ni viroboto tu wenye mawazo hayo!

3. Je unajina? si wewe unatoka MARA, huku mwalana wenyewe kwa wenyewe kama samaki? Au lets put it clearly unadini? Mimi kwetu Mlandege. Hata leo ukiuliza utaambiwa Dr. Mohamed Kassam ninani! Laajabu nikwamba wewe unaona haya kuksema kwamba kwenu ni Mara na hivi sasa mwalana wenyewe kwa wenyewe kama samaki!

4. Kama alivyo sema contributor fulani, "Pilipili iko Zanzibar, wewe uko Mara, inakuwashiaani mtanganyika?

5. Kama unavyo argue wewe kweli huja safiri nje ya Tanganyika. Yendavyo unaona Dar-es-salaama kama New York! Njoo Zanzibar tukufunze ustaarabu hiyo Kibri yako ita koma!

6. 0% Kwa kudai haki zawazanzibari, strange very strange. Ni viroboto kama nyinyi na vibaraka wenu mtakao timuliwa wakti utakapowadia.


COPY AND PASTE

Kama nilivyokuambia kwenye hii issue ilipo anza, tabia yako ya dharau na matusi ndiko unakokimbilia. Umetoa hoja ambazo huwezi kuzi-backup, hapa sio mahali pa majungu.

Kitu unachojua ni ‘copy and paste’, nafikiria ni vizuri uwe kama wengine kama huna point nyamaza na soma ya wenzio waliobobea.

Mimi ni Mtanzania na haina sababu yoyote kama natoka sehemu yoyote ile la msingi ni hilo. Unavyofikiri wewe sio ninavyofikiri mimi.

Jaribu plagiarism Mlandege maana huko ndio hawawezi kufahamu. Hapa umefika kwenye open world.

alamsiki

WACHA
 
Hakuna mpya Chadema, kwani unduguzaisheni hapo ndio nyumbani kwao.
Mtei alimpa uenyekiti rafiki yake aliyekuwa naye benki kuu-Bob Makani.
then akampa mkwe wake Bwana mbowe, nathani miaka ishirini atakuja mjukuu wa mtei kuwa mwenyekiti wa chama yaani mtoto wa Mbowe.
CCM hakuna uozo wa namna hiyo. tizama wenyeviti wanne wa CCM wametoka maeneo tofauti na hakuna hali kama ya chadema,Mnyika acha uzushi.

CCM ndio kwenye maslahi ya Taifa. lakini chadema ni ukaskazini zaidi. kila kitu huko tu.

Mwenyekiti KILIMANJARO, makamu mwenyekiti ndesamburo huko huko, tena hadi vitu maalum wamepewa watoto wa ndesamburo, mnyika hilo mbona husemi?

kuna katibu mkuu wa chama ambaye ni mkaskazini-DR-Slaa.
Udini-chadema.

kila kiongozi ni mkristu tu tena mapadri kama DR. Slaa na hata Mnyika aliyetakiwa kuwa padri na hata sauti uliyopewa mnyika ni kwa vile mama yako ni mpare-kilimanjaro.

kwa kifupi chadema ni NGO ya kaskazini na wala si chama cha kujifananisha na ccm, sasa hivi inajulikana kuna mshiko toka kwa David Cameroon, kwa hiyo ni NGO kama NGO zingine.

CCM ni muziki mkubwa,acha hizo MNYIKA,
MADAI YAKO YA eLIMU JIBU KWANZA, KABLA YA KUIVAMIA CCM,
kweli ccm kuna uozo si kama wa Chadema HATA viti MAALUM WAMEPEWA WATU WA VIGOGO. au unaleta hadithi ya nyani kuona ya mwenziwe huku yeye hajioni?
 
Jamani, mimi ningependa kujua Daktari wa Mlandege, hasa hasa udaktari huu ni katika vitu gani; maanake anatoa vitu vyake hasa!
Ile habari aliyoiweka kuhusu muungano sioni kuwa inawasuta hasa wale makupe; nadhani inafaa aisome vizuri kwa mara nyingine tena, na pengine atutafutie nyingine itakayoonyesha ubaya zaidi wa haya mafedhuri ya huko Bara.
 
Back
Top Bottom