East African Federation (EAF) public Views

East African Federation (EAF) public Views

Kujiunga kwa Rwanda na Burundi itakuwa ni faida kubwa kwa Jumuiya kwani soko litakuwa na zaidi ya watu millioni mia moja. Kiwanda kilichopo ndani ya umoja mfano Mtwara hilo ni soko lake bila vikwazo. Pia wawekezaji watavutiwa zaidi kuwekeza ndani ya jumuiya ukizingatia ukubwa wa soko, China ni mfano hai wa hili.
 
Kujiunga kwa Rwanda na Burundi itakuwa ni faida kubwa kwa Jumuiya kwani soko litakuwa na zaidi ya watu millioni mia moja. Kiwanda kilichopo ndani ya umoja mfano Mtwara hilo ni soko lake bila vikwazo. Pia wawekezaji watavutiwa zaidi kuwekeza ndani ya jumuiya ukizingatia ukubwa wa soko, China ni mfano hai wa hili.

Faida kubwa sio kuungana. Sasa hivi nani amekuzuia kuuza bidhaa zako Rwanda, Burundu au popote pale duniani - no one. Angalia picha kubwa China wapo wengi lakini bidhaa zao zinauzwa kwa nchi tajiri; USA, Europe na sasa nchi zote maskini wananunua kotoka kwao kwa sababu makampuni makubwa walienda kuinvest kule kufuata cheap labour. Uwingi haupanui soko bali watu waliosoma wenye kufanya mambo yao kutumia akili na new technology. watu wenye uwezo wa kununua bidhaa na kutafakari kuweza kutatua matatizo yao.

Watu wengi sasa hivi wanataka kuja kupora mali za Tanzania ambayo ukiangalia ni bado bikira katika development hivyo wanataka kujiwahi.

Education is the key here - sio miungano isiyokuwa na mpango.


Wacha
 
Has the time come!!!!!

quote from uganda Monitor

EAC ministers meet over Rwanda, Burundi
ZEHANIA UBWANI
ARUSHA

East African ministers responsible for the East African cooperation are meeting in Arusha tomorrow to make clear their position on entry of Burundi and Rwanda in the organisation.
The closed-door ministerial meeting will be preceded by high-level discussions the whole of today with senior officials from the two land-locked states which applied to join EAC in the late 1990s but yet to be admitted.
EAC Secretary General Juma Mwapachu was not clear when contacted yesterday whether Burundi and Rwanda would at last be admitted to the regional body during the EA Heads of State Summit on Thursday.
"Negotiations are still going on. It is the Summit which will make a declaration on that" he said in affirmative, countering reports that the process was being deliberately delayed.

I hope the ministers are going to be truthful to the views expressed, although I am sure the majority as seen on this forum from Tanzania are against this move. when people questioned Kagame's legitimacy people where angry but at the moment he is on time clock.


____________________________
Dua la kuku halimpati mwewe
 
Ukishaanza kuone jazba, na maneno makali, hapo ujue mtu anaanza kupoteza mwelekeo.

Mimi naamini elimu ya mtu na ujuvi wake vinajionyesha, ikiwa ni pamoja na kukomaa kimjadala. Pale mtu anapooanza mashambulizi, ooh sijui we watoka wapi, mi sijui wote wananijua, sijui visiwa vya wapi na wapi... yote haya ya nini?

Stick to your guns, but when you start going astray by start chipping irrevant issues, that raises questions on your credibility, and education.

Cha msingi, toa hoja, yenye uchambuzi, acha watu wajadili, na SI lazima wakubaliane na wewe, hata hivyo, si tena wewe kurudi na kuanza kuporomosha.

Tunapenda kusoma michango yenu, mkumbuke pia hilo, hivyo jaribuni kujipanga, weka jazba kando.

Kuna matatizo Zanzibar, kuna matatizo Tanganyika, huo ndio mjadala. Ikumbukwe pia kuna Masuala ya Muungano, na Masuala ya Zanzibar pekee. Huo ndio ukweli.

Naamini, Zanzibar inafaidika zaidi na muungano huu kuliko hata Tangayika.

Nina hakika, ukipitisha kura ya maoni ya wazi kabisa, bara itaitema Zanzibar!

Huu ni mtazamo wangu.
 
watanzania wanasukumwa kiujanjaujanja ili wakubali shirikisho la afrika mashariki kwa faida ya watu wachache.ukweli watanzania halitufai shirikisho hili kwa sasa kwa sababu zifuatazo.

1 nchi zote zinazotuzunguka zina makabila machache hivyo silka ya ukabila imeingia katika roho za raia wao na hivyohivyo silka ya ubaguzi wa kikabila na kitaifa wanayo tofauti na watanzania kila binaadamu ni sawa.kutokana na tabia hii leo wageni nchini wanao uhuru mkubwa na haki kubwa kuliko wabogo wenyewe hivi tukijiunga na shirikisho si tutafukuzwa kabisa nchini.wala serikali isidai kuwa itahakikisha hili na lile kwani wageni wangapi wanaishi kiholela na wanafanya kazi kiholela hatua gani dhiidi yao zimechukuliwa

2. kwa bahati mbaya tofauti na nchi jirani ardhi ya tanzania haina mwenyewe lakini nenda kkwa ndugu zetu kama utapata ardhi kiholela mano mzuri katika ujenzi wa barabara ya msoma hadi migori kenya udongo,kokoto na mali asili nyingine zilitoka tanzania kujenga kenya kwa sababu kule kila kipande kilikuwa cha mtu mkandarasi ilibidi anunue lakini bingo ilikuwa bwelele.

2 kwakuwa raia wa nchi hizi tunafanana kote kuna vitambulisho vya uraia lakini watanzania hatuna hivi tukiungana watanzania watajulikana kweli.usinieleze kuwa viatayarishwa kama matayarisho ya vitambulisho imechukua miaka kadhaa kweli ifuatiliaji wa nani raia na nani si raia utafanyika haraka kweli.

4Rushwa imeota mizizi hapa nchini uchaguzi rushwa polisi rushwa mahakama rushwa watanzania tutasalimika kweli.hoja ya kudai eti uchumi wetu utaimarika kwa kuungana ni hoja ya fisi kuufata mkono wa mwanadamu. ona watanzania wanavyopata taabu wakipeleka mali au bidhaa kuuza kenya au ugganda na ulinganishe urahisi wanaopata wenzetu wanapoleta bidhaa hapa nchini.

mimi nawawasa tusiige fasion tusioijua tutakuwa kioja na watumwa tufikirie hatma ya watotoi wetu
 
JK anatakiwa kuwa makini sana na EAF kwasababu ikiharakishwa italeta maandamano sana Tanzania. Watanzania hawataki huu muungano na si kwa sababu hawapendi majirani lakini ni kwasababu wanaona inafanywa kwa pupa sana bila kuangalia madhara yake kwa Taifa. Wakati taifa letu linaendelea na misaada mingi imeongezeka ni wakati wa kuwa makini kuchanganywa na Kenya kwani nchi nyingi zinazosaidia zinaamini kenya inaenda nyuma kwenye swala la rushwa 50% ya watu wanaishi chini ya kiwango cha umasikini!. Kwasasa Tanzania uchumi unakuwa kati ya 6%-7% na nawasiwasi kama utaendelea kukuwa kwa kiasi hicho kama tukiingia kwenye jumuia hii. Tanzania inatakiwa kama 20 years kabla ya kufanya hizi nchi kuwa moja kwani wakati huo uchumi wetu utazidi mbali sana ule wa Kenya, tuna mafuta gold na tutakuwa na skilled workers. Ningemshauri kikwete kuacha mambo kama yalivyo sasa kwani uchumi wetu unakua na hatuhitaji ujanja ujanja wa Kenya na uganda.
 
The Daily Nation of the 18th November splashed its headline with "Kenya's Maasai Mara named among the most spectacular place on the planet" and later in the article in smaller print "The Maasai Mara and Serengeti and the Wildebeest migration were selected as one of the new wonders" etc. So The American Broadcasting Corporation and a group of panelists, hosted by our neighbours, told the world what we have known all along. The annual migration is a "Wonder of the World."


THE PRESS IN KENYA AND ITS READERS JUST ENJOYING WHAT THEY WANT TO SEE. THEY DARE COMPARE MAASAI MARA IN KENYA WITH SERENGETI.


AND YET THESE PEOPLE WANT TO JOIN WITH US IN EA FEDERATION; ITS ONLY A STUPID IDIOT WHO WILL AGREE WITH THEM. LET THEM CONTINUE IN DREAM LAND!
 
watanzania wanasukumwa kiujanjaujanja ili wakubali shirikisho la afrika mashariki kwa faida ya watu wachache.ukweli watanzania halitufai shirikisho hili kwa sasa kwa sababu zifuatazo.

1 nchi zote zinazotuzunguka zina makabila machache hivyo silka ya ukabila imeingia katika roho za raia wao na hivyohivyo silka ya ubaguzi wa kikabila na kitaifa wanayo tofauti na watanzania kila binaadamu ni sawa.kutokana na tabia hii leo wageni nchini wanao uhuru mkubwa na haki kubwa kuliko wabogo wenyewe hivi tukijiunga na shirikisho si tutafukuzwa kabisa nchini.wala serikali isidai kuwa itahakikisha hili na lile kwani wageni wangapi wanaishi kiholela na wanafanya kazi kiholela hatua gani dhiidi yao zimechukuliwa

2.kwa bahati mbaya tofauti na nchi jirani ardhi ya tanzania haina mwenyewe lakini nenda kkwa ndugu zetu kama utapata ardhi kiholela mano mzuri katika ujenzi wa barabara ya msoma hadi migori kenya udongo,kokoto na mali asili nyingine zilitoka tanzania kujenga kenya kwa sababu kule kila kipande kilikuwa cha mtu mkandarasi ilibidi anunue lakini bingo ilikuwa bwelele.
2 kwakuwa raia wa nchi hizi tunafanana kote kuna vitambulisho vya uraia lakini watanzania hatuna hivi tukiungana watanzania watajulikana kweli.usinieleze kuwa viatayarishwa kama matayarisho ya vitambulisho imechukua miaka kadhaa kweli ifuatiliaji wa nani raia na nani si raia utafanyika haraka kweli.

4Rushwa imeota mizizi hapa nchini uchaguzi rushwa polisi rushwa mahakama rushwa watanzania tutasalimika kweli.hoja ya kudai eti uchumi wetu utaimarika kwa kuungana ni hoja ya fisi kuufata mkono wa mwanadamu. ona watanzania wanavyopata taabu wakipeleka mali au bidhaa kuuza kenya au ugganda na ulinganishe urahisi wanaopata wenzetu wanapoleta bidhaa hapa nchini.
mimi nawawasa tusiige fasion tusioijua tutakuwa kioja na watumwa tufikirie hatma ya watotoi wetu

Ndugu zangu Dua na Saidsabke, poleni, na ogopeni zaidi!
Mwelekeo wa mambo unavyojionyesha sasa hivi, inaelekea uamzi umekwishafikiwa wa Tanzania kuingia katika shirikisho hili; iliyobaki ni wakati tu uwadie. Sijui kama mmefanikiwa kusoma hotuba saaafi ya Mh. Rais aliyoitoa alipoalikwa na M7. Naibu Waziri wetu wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki hana wasiwasi wowote na nafasi ya waTanzania ktk ushirikiano huu, kwani anaamini kabisa sheria zilizopo zitawalinda! Naona anayo imani kubwa zaidi na utekelezaji na ufuatiliaji mzuri wa sheria hizi kuliko wananchi wengi wa kawaida walio na hofu kubwa ya kunyang'anywa hata hicho kidogo walichonacho sasa hivi!

Na hata sio ajabu tena ukimsikia Meya wa Kisumu akisema anataka wavuvi wafuatilie samaki waliozaliwa eneo la Kenya na kukimbilia sehemu ya Uganda au Tanzania bila kizuizi chochote kile. Waziri Kitui yeye anasema anataka waTanzania walime pamba, Uganda waichambue na kui-gin ili viwanda vya Kenya viifanyie kazi! Halafu sasa tunafahamishwa kwamba Maasai Mara ni 'Wanda ya saba' serengeti ikiisindikiza!

Kwa ujumla, hata tuseme kwa nguvu vipi kuwa sisi sote watu wa Afrika Mashariki ni wamoja na ndugu; lakini ukweli uliopo na usioweza kuepukika ni kwamba tabia zetu na mienendo yetu imekwishabadilika mno katika hii miaka iliyopita baada ya kuachana katika ushirikiano wetu wa mwanzo ulioharibika, kiasi kwamba tunahitaji tahadhari kubwa na busara nyingi, na tuchukue wakati na kuwashirikisha wananchi zaidi na kwa dhati tupu kabla ya kujitumbukiza zaidi katika ushirika huu. Wenzetu waKenya wamekwishajiwekea katika mawazo yao kwamba wao katika eneo hili la Afrika ni zaidi mno; na ndio maana hata mawaziri wao wa Ushirikiano huu wanaonekana kutokuwa na subira.

Mawazo ya namna hii yanazidi kuimarishwa na baadhi ya waandishi wa magazeti kama yale yatolewayo na Ernest Mpinganjira, ambaye yeye huona kila lifanyikalo na serikali ya Tanzania kuwa halina maana yoyote, na kama lina maana kidogo, basi limeigwa kutoka serikali ya Kenya! Jeshi la Tanzania kumbe halikumng'oa Nduli, ni Waingereza ndio waliomwondoa Amin.; na mwandishi wa habari huyo anahakika kabisa bila chembe ya wasiwasi yoyote kuwa jeshi hilo hadi sasa halina lolote! Majenereta yote ya umeme na ndege ya Rais ni mitumba tupu! Anadiriki hata kuanza kutoa majungu yanayowahusu watoto wa mawaziri Mramba na wengineo wanaojihusisha na mikataba ya uongo na kweli!

Utadhani anatafuta njia ya kuwachochea wananchi waone kuwa serikali yao haina maana. Mimi nilijua Waziri Mkuu aliyepita anayo mashamba makubwa ya kulima, lakini sikujua kuwa hili lilikuwa tatizo lililosababisha waTanzania wengine wakose mashamba ya kulima! sijui huyu mwandishi habari zote hizi yeye huzipata wapi!

Waandishi wa habari wa Tanzania wasipotoa majungu kama hayo, wanaambiwa sio "Waandishi" wa kwelikweli hao. Ukweli ni kwamba si waandishi wa habari tu, kati ya Kenya na Tanzania wasioshabihiana, bali hata tabia za wananchi wa kawaida wa nchi zetu hizi kwa ujumla zimekuwa ni za tofauti sana. Sasa uje uwachanganye katika hilo shirikisho bila ya kuwa makini, unaweza kujikuta kwamba yule ambaye alikuwa anaonekana kuwa mpole, anaweza akageuka kabisa, na hata kufikia hatua ya kuanza machafuko yasiyokuwa na maana yoyote ikiwa ni njia ya kujihami, na kuacha mambo ya mhimu yanayoleta maendeleo.

Matumaini yangu makubwa ni kwamba viongozi wetu walisha yatafakari vizuri mambo yote haya, na kwamba kwa moyo wa dhati kabisa, bila ya kuwa na ajenda nyinginezo, watawapatia nafasi nzuri na ya wazi watanzania waweze kushiriki kikamilifu kabisa katika kufikia uamzi wa mwisho kuhusu jambo hili.
Wasalaam
 
the idea is welcoming and it's...ok! a good thing is that always africans east africans in particular say karibu mgeni lakini hatutaki vita na tribalism🙂
 
Rwanda, Burundi join East Africa Community
By Marie-Louise Gumuchian
ARUSHA, Tanzania (Reuters) - Rwanda and Burundi have been accepted as members of the East African Community (EAC), expanding the regional economic bloc to five nations, the EAC said on Thursday.
Rwanda has struggled to rebuild an economy shattered after a 1994 genocide in which 800,000 people were killed.
"This decision opens a new chapter in our cooperation. I congratulate Rwanda and Burundi for joining our family of EAC members," Tanzanian President Jakaya Kikwete told an EAC summit in the northern Tanzanian town of Arusha.
REUTERS PICTURES

Editors Choice: Best pictures
from the last 24 hours.
View Slideshow
The EAC previously grouped Kenya, Uganda and Tanzania, which hope to transform the region into a political federation.
Tiny neighbors Rwanda and Burundi had applied to join the economic community, relaunched in 1999 to boost regional trade.
The EAC agreed a customs union last year and plans to launch a common market for its population of about 90 million by 2010. The countries also plan to have a monetary union and a common president and parliament by 2010.
The first attempt at east African cooperation ended acrimoniously in 1977 because of the three partners' widely divergent political and economic thinking.
The summit in Arusha also launched a 2006-2010 development strategy to achieve the bloc's goals.
The EAC previously told Burundi to hold democratic elections and tackle insecurity that plagued the African nation during a civil war that killed 300,000 people.
Donors now support the government of President Pierre Nkurunziza, elected in 2005, which is trying to boost its fragile economy after the 12-year conflict.
"There is no doubt that our accession to the community will be a stabilizing factor," Nkurunziza said.
REUTERS PICTURES

Editors Choice: Best pictures
from the last 24 hours.
View Slideshow
Rwanda has been keen to join since the EAC's early days.
"My country is ready to join you in building a more and better integrated region," Rwandan President Paul Kagame said. The membership is to be formalized and concluded by July 2007.
At a meeting in April, the presidents of Kenya, Uganda and Tanzania called for more public campaigns in their countries about the planned political federation. The leaders said on Thursday more needed to be done to speed this up.
"The process needs to be fast-tracked," Kikwete said. "If we continue this way we may lose the momentum."
The customs union, which began setting common external tariffs for goods entering the region in January 2005, is seen as a first step toward a common market and single currency modeled on the European Union
The future of east Africa lies in the establishment of a solid single market," Kenyan President Mwai Kibaki said.
Kibaki said the EAC needed to address issues regarding membership to other African economic blocs and their planned customs unions. No country can belong to two customs unions: "We need to finalize this matter so that negotiations toward an economic partnership can be concluded."
Although trade and investment among EAC members has increased in the last five years, some analysts say there remains mistrust between the citizens of the three countries, although they share a common language and culture.
Kenya is by far the biggest economy in the region and businesses in Tanzania and Uganda often complain that they need support from their Kenyan counterparts. [quote/]
 
Rwanda na Burundi zimekubaliwa kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Ni matumaini yangu kuwa huu ni mwanzo wa ushirikiano mpya wa kujenga jamii moja ya watu wa Afrika ya Mashariki!! Karibu ndugu zetu!!
 
Waambiwa wajifunze Kiswahili fasaha
Na Omari Shaaban, Arusha

HATIMAYE wakuu wa nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) wamezikubalia uanachama Rwanda na Burundi.

Nchi hizo zilitangazwa kujiunga rasmi na Jumuia hiyo jana na Rais Jakaya Kikwete kwenye ukumbi wa mikutano wa Simba, uliopo kwenye jengo la AICC mjini hapa.

Wanyarwanda na Warundi waliokuwemo ukumbini, walipiga makofi na kutoa machozi ya furaha baada ya kipindi kirefu cha kuomba uanachama katika Jumuia tangu mwaka 1996 na kukubaliwa jana.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete alisema hiyo ni siku ya historia kwa Jumuia ya Afrika Mashariki, na kuwepo kwa Rwanda na Burundi ni kuleta changamoto kwenye Jumuia.

“Tumepanua wigo wa Jumuia yetu…katika kuelekea kwenye shirikisho la Afrika Mashariki…Rwanda na Burundi sasa ni wanachama halisi wa Jumuia hii,” alisema Kikwete.

Alisema nchi hizo zilikuwa zikitumia bandari, barabara kwa muda mrefu za Jumuia kupeleka ama kutoa bidhaa zao, lakini sasa watafurahi zaidi wakitumia miundombinu hiyo wakiwa ndani ya Jumuia ya Afrika Mashariki.

Kikwete alisema ingawa nchi hizo zimekubaliwa rasmi, taratibu za kisheria za nchi hizo kuingia kwenye Jumuia hiyo zitakuwa zimekamilika Julai mwakani.

Akizungumzia upungufu wa maji katika Ziwa Victoria, matatizo ya umeme na mabadiliko ya hali ya hewa, Rais Kikwete alisema hayo ni matokeo ya kuharibu mazingira na hilo ni somo kwa wananchi wa Afrika Mashariki, kuhakikisha wanatunza mazingira kikamilifu.

Akizikaribisha Rwanda na Burundi, Rais Mwai Kibaki wa Kenya alisema wameridhishwa na jinsi nchi hizo zilivyotekeleza masharti wakati wakiomba kuingia Jumuia ya Afrika Mashariki.

Alizitaka nchi hizo kuanza kujifunza kwa ufasaha lugha za Afrika Mashariki ambazo ni Kiswahili na Kiingereza.

Naye, Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika hotuba yake alisema ili nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki ziwe imara kiuchumi ni lazima ziwe na soko la pamoja.

Alisema nchi za jumuia zikiwa na soko la pamoja zitaweza kupambana na masoko mengine makubwa ya kimataifa na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Afrika mashariki.

Alisema nchi jumuia ya Afrika Mashariki zimetawaliwa na ‘blaa blaa’ za siasa huku kukiwa hakuna maendeleo wanayofanya kwa wanachi wa nchi wanachama na kutaka kuachwe mizaha kwenye kuendeleza gurudumu la jumuia.

“Kila mara katika nchi za Afrika Mashariki utasikia masuala ya vyama vingi na mwenzake demokrasia, mara haki za binadamu…hakuna lolote juu ya hilo kwani zipo nchi hazina vyama vingi na zimepiga hatua, ” alisema Rais Museveni.
Baada ya hotuba za wakuu hao, Rais wa Rwanda, Paul Kagame alisema atahakikisha anashirikiana na wanachama wenzake katika kuwaletea wananchi maendeleo kwenye nyanja zote.

Rais wa Burundi, Jean Pierre Nkurunziza alisema amefurahishwa na maamuzi ya wakuu wa nchi ya kuwa wanachama wa jumuia hiyo na yupo tayari kuhakikisha Jumuia inasonga mbele kwa kasi zaidi.

“Rais Kibaki amenifurahisha sana….kwani sisi Burundi sasa hivi, wanafunzi wa darasa la kwanza hadi kuendelea wanajifunza Kiingereza na elimu ni bure nchini kwangu. Sisi tulishaanza muda mrefu tukijiandaa kuingia Jumuia,” alisema Rais Nkurunziza na kuacha umati wa watu ukicheka.

Pia katika mkutano, waliwaapisha majaji wawili wapya wa Mahakama ya Jumuia ya Afrika Mashariki ambao ni Harold Nsekela wa Tanzania na Marystella Amogo wa Kenya.

Majaji hao wanachukua nafasi za majaji waliomaliza muda wao, Joseph Warioba wa Tanzania na Salome Rosa wa Uganda.
 
Arusha yaandika historia nyingine

na David Frank, Arusha


NCHI za Rwanda na Burundi, zimekubaliwa uanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Kwa maana hiyo, jumuiya hiyo sasa itakuwa na nchi tano wanachama. Waasisi wa jumuiya hiyo ni Tanzania, Kenya na Uganda.

Pia kujiunga kwao kunaifanya jumuiya hiyo sasa iwe na idadi ya watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya milioni 120; idadi ambayo inaweza kuwashawishi wawekezaji kuja kuwekeza katika ukanda huu.

Uamuzi wa kuzikubali Rwanda na Burundi ulitangazwa jana na Mwenyekiti wa EAC, Rais Mwai Kibaki wa Kenya.

Shughuli hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), na kuhudhuriwa na marais Pierre Nkuruziza wa Burundi na Paul Kagame wa Rwanda.

Nkuruziza na Kagame, walionekana kujawa na furaha baada ya uamuzi huo kutangazwa.

Rais Kibaki aliuchangamsha ukumbi, baada ya kuwaagiza wanachama hao wapya, wajifunze Kiswahili, lugha ambayo inazungumzwa na wananchi wengi wa Afrika Mashariki.

"Tumekaa na kupitia maombi yenu kwa muda mrefu, sasa napenda kuwafahamisha kwamba tumekubali.

"Nawaagiza mjifunze Kiswahili - lugha inayotumika zaidi Afrika Mashariki," alisema Rais Kibaki na kuifanya hadhira ishangilie.

Rais Jakaya Kikwete, katika hotuba yake, alisisitiza ushirikishwaji wa wananchi kwa kusikiliza mapendekezo yao ili waweze kushiriki katika jitihada za nchi hizo za kukuza uchumi na hatimaye kufikia Shirikisho la Afrika Mashariki.

Alisema uzinduzi wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Jumuiya hiyo wa mwaka 2006 hadi 2010, utasaidia kuimarisha jumuiya na kuinua kiwango cha uchumi kwa nchi wanachama.

"Hatua ya Rwanda na Burundi kukubaliwa kuwa wanachama wa jumuiya hii, ni kitendo cha kihistoria kinachofungua ukurasa mpya wa ushirikiano na uhusiano katika Bara la Afrika," alisema Kikwete.

Kwa upande wake, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, alisisitiza katika maendeleo ya kiuchumi, maliasili na rasilimali watu.

Alisema katika nchi za Afrika wamekuwa wakizungumzia masuala ya demokrasia zaidi wakati Jamhuri ya Watu wa China wanazungumzia maendeleo.

Alisema wananchi wanahitaji akili za watu zitakazosaidia kukuza maendeleo yao.

Alitoa mfano wa Korea Kusini na kusema katika miaka ya 1950, wananchi wake walikuwa wakiwanyoa nywele wanawake na kuzisafirisha nchi za Ulaya, ambako zilitumika kutengeneza ‘wigi'.

Alisema nchi hiyo ambayo ilikuwa na hali hiyo katika miaka hiyo, leo ni matajiri sawa na Saudi Arabia yenye kuongoza kwa uuzaji wa mafuta duniani, licha ya umaskini wa maliasili nyingine.

"China inategemea teknolojia na akili za watu wao pamoja na soko kubwa la ndani na nje ya nchi hiyo, hali iliyozifanya nchi za magharibi kukimbilia soko katika nchi hiyo, na sasa uchumi wao unakua kwa kasi kubwa," alisema.

Marais Nkurunziza na Kagame, wakizungumza kwa nyakati tofauti, waliwashukuru wakuu wa jumuiya hiyo na wananchi kwa kuwakubalia uanachama.

Waliahidi kutoa ushirikiano wa hali na mali ili kuhakikisha jumuiya inapata nguvu zaidi, na wananchi wananufaika.

Rais Nkuruziza, akitumia Kiswahili fasaha, alisema Rais Kibaki, amewahimiza wajifunze Kiswahili, lakini wao walianza kujifunza mara baada ya kuomba kujiunga katika jumuiya hiyo, ikiwa ni maandalizi na vigezo vya kuwa wanachama.

Rais Kagame alieleza kufurahishwa kwake kwa hatua hiyo na kuahidi kutoa ushirikiano wa dhati katika kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Aliwahakikishia wakuu wenzake kuwa wapo pamoja katika mchakato mzima wa kuinua uchumi wa nchi wanachama.

Kikao cha jana kilizindua Mkakati wa miaka mitano (2006-2010) wa Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Suala la ushirikiano na ukuzaji uchumi lilitawala sehemu ya mazungumzo ya mkutano huo.

Rais Kibaki alisema kuna umuhimu wa kutoa nafasi kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi endelevu.

Alisema Sekretarieti ya Jumuiya hiyo ni muhimu ikajikita katika ngazi ya chini kwa kuwashirikisha wananchi.

Hata hivyo, uzinduzi wa Bunge la Afrika Mashariki haukufanyika jana kutokana na kesi iliyofunguliwa na walalamikaji 12 kutoka Kenya wakiongozwa na Profesa Peter Anyang' Nyong'.

Walalamikaji wanapinga utaratibu mzima wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka nchini mwao. Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Januari mwakani.

Kukubaliwa kwa Rwanda na Burundi, kutapokewa kwa hisia tofauti na wananchi wengi, hasa katika mikoa ya magharibi mwa Tanzania.

Kwa nyakati tofauti, wananchi wengi walionyesha wazi kupinga nchi hizo kupewa uanachama, wakisema kabla ya kukubaliwa, zipewe masharti.

Masharti yaliyotajwa ni pamoja na kudumisha amani na utawala bora katika nchi zao, kuacha mauaji, kuacha vitendo vya ujambazi vinavyodaiwa kufanywa na raia kadhaa, na kuhakikisha wakimbizi wanarejea katika nchi zao.

Kimsingi, wananchi hao hawakuonyesha kupinga nchi hizo kupewa uanachama, lakini hoja kuu ilikuwa kwamba zipewe masharti, na zikiyatekeleza ndani ya miaka kadhaa, na viongozi na wananchi wa Kenya, Uganda na Tanzania wakishajiridhisha, ndipo zikaribishwe.

Wananchi walitaka Rwanda na Burundi pia zihakikishe zinawanyang'anya silaha wananchi wake, ambazo sasa zimezagaa na hivyo kuongeza matukio ya ujambazi, uporaji na mauaji.

Adha za ujambazi na kero zinazosababishwa na wahamiaji haramu, majambazi na wahalifu wengine kutoka Rwanda na Burundi, ni mambo yanayowakera Watanzania wengi waishio magharibi mwa nchi.

CHANZO (Source): Tanzania Daima Newspaper
 
Tusipookoa Kigoma, Kagera, Mungu atatuhukumu

Manyerere Jackton

HIVI karibuni niliandika makala iliyokuwa na kichwa kisemacho: Kagera, Kigoma si Tanzania tena!

Wengi waliowasiliana nami, walisema hawakujua chochote kilichokuwa kikiendelea katika ukanda wa magharibi mwa nchi yetu, hadi waliposoma makala hiyo. Walinishukuru kwa kuwafumbua macho.

Majibu haya yalinisaidia kujua mambo kadhaa muhimu. Mosi, ili tatizo lifahamike kwa wengi, si lazima liwe kubwa. Kwa kutotambua matatizo yanayowakabili Watanzania wenzetu katika mikoa ya magharibi, hii haina maana kwamba tatizo la ujambazi, utekaji, uporaji na mauji katika ukanda huo, ni dogo.

Ni kubwa, lakini kwa kuwa semina zote zinafanywa Arusha, Dar es Salaam, Bagamoyo, Mwanza, Dodoma, Zanzibar (Unguja) na Morogoro; hakuna anayeyajua haya.

Laiti kama siku moja semina hizi zingepelekwa Kibondo, Ngara, Kasulu, Biharamulo, Karagwe au Muleba; kisha basi la wanaojiita wanaharakati likatekwa, leo ujambazi ungekuwa kwenye vitabu vya hadithi.

Pili, maneno ya wanasiasa wetu yamewaingia sana Watanzania. Maneno kama Tanzania ni kisiwa cha amani, Tanzania hakuna mapigano, Watanzania wanapendana; yote haya na mengine, yamewafanya Watanzania wengi waamini kuwa nchi hii ni tulivu. Tanzania ina wavumilivu tu.

Majuzi tu, Jeshi la Polisi liliposema limedhibiti ujambazi kwa asilimia zaidi ya 50, wananchi wengi walipiga makofi. Wakashangilia. Wakatamani IGP Mwema ajitokeze-wambebe-wampe ofa kutokana na kazi kubwa na nzuri.
Waliokuwa wa kwanza kuondoka kwenye baa na sehemu nyingine za starehe, wakawa na sababu ya kuwafanya wakeshe! Wawahi kwenda wapi, ilhali nchi imeshatulia?

Wanasiasa wakadakia. Unaona Serikali ya Ari mpya, Kasi mpya, na Nguvu mpya? Ujambazi kwisha! CCM oyeeee!
Hata wale tunaowajua wazi kwamba wanaikwamisha Serikali ya Awamu ya Nne, wakawa wa kwanza kutamba. Kwa wanasiasa, na Watanzania wengi, Tanzania maana yake ni Dar es Salaam! Ujambazi ukipungua Dar es Salaam, basi Tanzania yote iko shwari!

Ujambazi, uporaji na mauaji yanayotokea Kigoma na Kagera, si ujambazi! Na kama ni ujambazi, basi ni mdogo sana! Tunajidanganya.
Kwa bahati mbaya, sherehe na mbwembwe hizi ni vitu vinavyoonekana upande mmoja tu wa nchi. Kiongozi anayetaka kutoa tambo hizo, ahakikishe anatumia majukwaa yote, isipokuwa majukwaa yaliyopo Kibondo, Kasulu, Kigoma, Karagwe, Ngara, Biharamulo, Muleba, Kahama na kwingineko.
Kusema kwamba ujambazi umepungua kwa asilimia zaidi ya 50 nchini, maana yake ni kwamba hiyo asilimia 50 iliyobaki, ipo Kagera, Kigoma na maeneo jirani. Huu ni ukweli usiopingika.

Ndugu zangu Watanzania wanaoishi nje ya Kagera, Kigoma, Rukwa na sehemu za mikoa ya Mwanza na Shinyanga, watambue kuwa nchi yetu si salama kama tunavyojilazimisha kuamini.

Mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo ina matukio machache ya ujambazi, wananchi wajue kuwa ndugu zao wa Kigoma, Kagera na sehemu za mikoa jirani, hali ni mbaya. Wanataabika. Wanaporwa. Wanajeruhiwa. Wanauawa, na wengine juzi ndiyo wamesikika wake wakibakwa mbele ya waume zao! Fikiria wanaume sita wamefungwa kamba, wanashuhudia wake zao wakibakwa! Unyama gani kuuzidi huu?

Haya ni mambo ya maharamia kutoka nchi jirani wanaoshirikiana na Watanzania wachache. Hawa ni maharamia waliomwaga damu za watu wasio na hatia, kiasi kwamba sasa wamewageukia Watanzania.

Kinachowaponza Watanzania hawa ni uungwana wao. Kuwakubali wageni wanaotumia kivuli cha ukimbizi. Wakimbizi ndio chanzo kikuu cha yote haya.
IGP Mwema kafanya jambo la maana. Kamteua Kamanda Venance Tossi kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera. Tossi tunamjua, ni mchapakazi, ni aina ya polisi adimu katika nchi yetu. Kilimanjaro ilisifika sana kwa ufedhuli, iligeuka ikawa kama Kagera na Kigoma. Ilisifikia kwa ujambazi na uhalifu wa kila aina.

Miezi michache ya Kamanda Tossi mkoani humo, ilitosha kurejesha amani. Majambazi, wezi na wahalifu wengine, wanamtambua Tossi kama adui yao mkuu.

Sasa amepelekwa Kagera. Hapo IGP Mwema, na wote waliobuni mabadiliko hayo, wanastahili kupongezwa.
Tossi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi, serikali na wananchi, sasa ana kazi kubwa. Dhima aliyopewa kamanda huyu, ni kubwa na ya hatari.

Ndiyo, amepelekwa Kagera. Je, ana vitendea kazi? Ana askari wa kutosha? Ana vifaa maalumu vya usalama kwa askari wanaopambana na majambazi? Anawezeshwa kupata mafuta ya magari kwa saa 24? Je, askari na yeye wametengewa posho kulingana na ugumu na hatari ya mazingira ya kazi hii waliyopewa na taifa?

Tosi huyu bila magari ya kutosha, bila pikipiki, bila askari wa kutosha, bila motisha kwa askari, bila mahema, bila mlo mzuri kwa askari, bila viburudisho kadha wa kadha, atayamudu mabazazi haya kutoka nchi jirani?

Bila vifaa vya kuwawezesha kuingia ndani ya misitu kufanya doria na kuwasaka wauaji hao, Tossi ataweza kuleta mabadiliko? Hawezi.
Je, wenzake aliowakuta katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na sehemu za Shinyanga, wana hayo niliyoyataja hapo juu?

Hii ina maana kwamba bila kumwezesha Tossi na wenzake kwa kila hali, vita dhidi ya majambazi na waporaji katika ukanda huu itakuwa kama Israel na Palestina. Haitakwisha.

Kama nilivyosema katika makala iliyopita, suala la ujambazi katika mikoa ya Kagera, Kigoma, Rukwa na maeneo ya mikoa jirani, ni tatizo la kitaifa. Hili si jambo la kuwaachia watu wachache.

Kama wakimbizi wanatumia bunduki nzito nzito na mabomu, hii maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba hii ni vita! Kama ni vita, inabidi vyombo vya ulinzi na usalama vya Tanzania navyo viingie kivita.

Hakuna diplomasia kwa wauaji waliojipenyeza ndani ya ardhi yetu, wakaifanya misitu yetu kuwa ngome zao, kisha watu wa aina hiyo, tukawaondoa kwa mapanga au marungu! Wamekuja kivita, sharti washughulikiwe kivita.

Nchi haiwezi kutunza vifaru na magari ya deraya, ilhali kuna sehemu ya Tanzania imetwaliwa. Si busara kuwalea makamanda na wapiganaji, wakaota vilibatumbo, ilhali kuna kazi ya kufanya huko Kigoma na Kagera.
Viongozi wenye uchungu na Watanzania wenzao wanaotaabishwa magharibi mwa nchi, hawawezi kuafiki suala la ukosefu wa fedha kama sababu ya kuwaruhusu majambazi kuanzisha jamhuri ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kuna pesa nyingi zinatumiwa vibaya. Kuna ufujaji wa ajabu. Wananchi wanaachwa wafe, huku wengine wakitumia mabilioni katika semina na makongamano yasiyoisha. Kama ni fedha za wafadhili, wafadhili gani hawa wanaofadhili milo na vinywaji kwenye semina, wakakataa kuwafadhili maskini wanaouawa au kuishi kwa taabu katika jamhuri yao?

Nchi hii kuna meli kubwa ambayo jina lake limefichwa! Meli hii imebeba watu wengi, maarufu kwa ubunifu. Meli hii inaitwa mv Ulaji!
Miongoni mwa abiria wake ni Idara ya Takwimu. Idara hii imepanga kutumia sh bilioni 3.6 kufanya tathmini ya mapato na matumizi ya kaya 896! Haya ni maajabu.

Unakwenda Kibondo, Kasulu, Ngara, Biharamulo, Muleba, Karagwe, Kahama, kuuliza mapato na matumizi ya kaya? Wana muda wa kufanya kazi wananchi hawa? Watafanya kazi vipi ndani ya wimbi kubwa la ujambazi? Wafanyabiashara wa huku watasafiri vipi, ilhali hawawezi kwenda sokoni bila mitutu ya polisi, na hata wakiwa na polisi, wanatekwa na kuuawa?

Hayo mapato na matumizi kwa kazi ipi? Je, kwa nini fedha hizo zisitumike kununua vitendea kazi na kutoa motisha kwa polisi na askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanaoshinda na kukesha wakiwa wameweka roho mikononi?

Pesa hizo kwa nini zisitumike kununua japo baiskeli kuwasaidia polisi wanaohangaika kwenye mapori ya Kyamisi, Biharamulo, Benako, Lugufu na kwingineko? Pesa hizo kwa nini zisitumiwe kuhakikisha magari ya polisi yanakuwa na mafuta muda wote wa kazi?

Tuna raha gani ya kutumia sh bilioni 3.6, kufanya kazi ambayo ilifanywa katika Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2002? Haya ya mapato na matumizi, mbona yalikuwa kwenye dondoo za sensa hiyo? Nani hataamini kuwa huu ni mpango wa ulaji uliobuniwa kwa makusudi kabisa? Je, viongozi wa aina hii, wana uchungu kweli na Watanzania wenzao wanaotaabika? Mv Ulaji itazuiwa lini kusafiri?

Nimetoa mfano huu kuonyesha kuwa si kweli kwamba nchi yetu haina uwezo wa kumaliza tatizo la ujambazi magharibi mwa nchi yetu. Uwezo huo upo. Tena ni mkubwa kuliko mahitaji.

Wakati kina Tossi, Kanali Mfuru, Kanali Simbakalia, Luteni Kanali Mzurikwao na wengine wakipewa dhima ya kuwashughulikia majambazi, tunapaswa kujiuliza maswali kadhaa.

Nini maana halisi ya neno mkimbizi? Je, kwa tafsiri hiyo, Tanzania ina wakimbizi? Tujiulize.

Kamusi:
Mkimbizi: 1. Mtu akimbiliaye nchi nyingine kutokana na vitendo vya kidhalimu au vita. 2. Mtu mwenye tabia ya kukimbia mahali anapotakiwa awepo.
Kamusi ya Kiswahili Sanifu, toleo la II (Oxford).
Wanyarwanda walipoingia nchini mwaka 1994 kutokana na mauaji ya kimbari, walistahili kuitwa wakimbizi, kwa sababu wanakidhi maana ya kwanza iliyotolewa kwenye tafsiri ya neno mkimbizi.
Kadhalika, Burundi nao wakati wakipigana na kuchinjana wenyewe kwa wenyewe kama kuku, walistahili kupokewa, kuhudumiwa na kutunzwa kama wakimbizi.

Je, baada ya Rwanda kuwa nchi inayoendeshwa kidemokrasia, baada ya Burundi kuwa na kiongozi aliyechaguliwa na Warundi wenyewe, bado kuna sababu ya watu wa mataifa hayo kuishi kama wakimbizi katika ardhi ya Tanzania?

Hawa waliopo Kigoma, Kagera na kwingineko magharibi mwa nchi yetu, si wakimbizi. Wanaotoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), hao ni wakimbizi, lakini siku si nyingi, nao tutawaomba warejee kwao.
Warundi na Wanyarwanda ni watu wenye tabia ya kukimbia mahali wanapotakiwa wawepo.

Hawa wako kwenye tafsiri ya pili ya neno mkimbizi. Wanastahili kwenda kwao ili Watanzania wapumue. Wamemaliza wanyama na misitu, sasa wameingilia maisha ya raia wetu. Watatumaliza hawa.

Wamebweteka. Wanaponda maisha. Wapo walionunua magari. Wapo wenye daladala, lakini ni wakimbizi wanaoishi makambini. Wapo wanaishi kama wafalme walioandikwa kwenye vitabu vitakatifu.

Tujiulize, ukwasi wote huu wanautoa wapi katika ardhi isiyokuwa yao? Wana biashara gani? Je, si kweli kwamba hawa ndio wafadhili wa ujambazi na uhalifu mwingine?
 
Mbona ujambazi mwingi unatokea karibu na kambi? Kwa nini utokee kama wafadhili na washiriki wakuu hawaishi kwenye kambi hizo?
Je, si kweli kwamba hawa ndio wezi wa misaada inayotolewa kwa wakimbizi wa kweli? Lazima maswali haya tujiulize na tuyapatie majibu. Waeleze utajiri wao wameupataje ilhali hawaruhusiwi kutoka nje ya kambi?

Hawa wanajua wazi kuwa wakirejea kwao, hawatakuwa na mrija wa kuupata ukwasi walionao sasa. Wanangangania Tanzania ili waendelee kuchuma.
Na kama wanachuma, wanajenga wapi? Je, ni haki Tanzania kuwa kituo cha kuchuma kupitia damu za Watanzania?

Hawa wanaoitwa wakimbizi, wanatetewa sana na mashirika yaliyojipa kazi ya kuwahudumia wakimbizi. Kama nilivyopata kusema, mashirika haya yanaongozwa kihuni, na yamejaa wahuni tu wa maisha.

Wakimbizi ni chanzo kikuu cha ajira kwa Wazungu. Bila shaka serikali yetu inalijua vema hilo, kwa sababu imeshawafukuza baadhi ya wahuni waliothubutu kuzuia wakimbizi kurejea makwao.

Nihitimishe kwa kusema, wakimbizi wanapaswa warejee kwao. Wale wenye sababu za kutaka kubaki nchini, watumie mikondo halali kisheria, maana ni ukweli ulio wazi kuwa hawa ni ndugu zetu, lakini wenye tabia mbaya.
Kambi za wakimbizi zipunguzwe. Wawekwe kambi chache, ili iwe rahisi kuwadhibiti. Kambi nyingi zitawafanya wazidi kuja, na hivyo itakuwa vigumu kuwadhibiti.

Tossi na makamanda wenzake, wapewe ushirikiano wa dhati. Wapo pia Watanzania wanaoshirikiana na majambazi. Hao nao wanapaswa washughulikiwe.

Muhimu zaidi, tujue kuwa Watanzania wenzetu katika mikoa ya magharibi, wanataabika mno. Wao sasa ndio wakimbizi katika nchi yao.
Wametekwa na wageni. Hawana sauti. Hawana uhuru wa kutembea au kufanya kazi za kuboresha maisha yao. Hata wanapokwenda kukata ndizi shambani, wana sali wasiuawe. Haya ni maisha gani? Miaka 45 baada ya uhuru, wana cha kusherehekea? Tushirikiane kuwakomboa wenzetu.
E-mail: manyerere@hotmail.com
Selula: 0713 335 469
 
Hili shrikisho ni la viongozi au vipi? Mbona mambo yanaenda pasipo kuzingatia maoni ya wanachi? Hizi ziara za Kamala za Kuzinguka nchi nzima kutambulisha ziara yake na kuchukua maoni zina maana gani? Yale maoni ni kiini macho?

Maaana moja ya mambo ambayo watu walikuwa wakijadili naskutoa maoni yao lilikuwa suala la Kujiunga kwa Rwanda na Burudi.Kadri ilivyokuwa ikiripotiwa,wananchi wengi waliofikiwa na Waziri Kamala walipendekeza Burundi na Rwanda zipiwe muda kutatua migogoro yao ya ndani.

Hii,kasi ni kiu ya viongozi wetu kuwekwa kwenye vitabu vya historia? Au wananchi hawaoni kile ambacho viongozi wetu werevu wanaoana?
 
Hili shrikisho ni la viongozi au vipi? Mbona mambo yanaenda pasipo kuzingatia maoni ya wanachi? Hizi ziara za Kamala za Kuzinguka nchi nzima kutambulisha ziara yake na kuchukua maoni zina maana gani? Yale maoni ni kiini macho?

Maaana moja ya mambo ambayo watu walikuwa wakijadili naskutoa maoni yao lilikuwa suala la Kujiunga kwa Rwanda na Burudi.Kadri ilivyokuwa ikiripotiwa,wananchi wengi waliofikiwa na Waziri Kamala walipendekeza Burundi na Rwanda zipiwe muda kutatua migogoro yao ya ndani.

Hii,kasi ni kiu ya viongozi wetu kuwekwa kwenye vitabu vya historia? Au wananchi hawaoni kile ambacho viongozi wetu werevu wanaoana?

Well said Mr Ongara...to add up...

Hata mimi nina mashaka sana kuhusu hii kasi ya kuunganisha EA. Mbona wananchi wanaburuzwa buruzwa tuuu...hiyo tume ya kukusanya maoni ndio juzi juzi tu JK ameizindua rasmi...leo hii tunaambia Rwanda na Burundi wameruhusiwa kujiunga. Watanzania babdo hata hawana uhakika au hawajapewa muda kutoa mawazo yao iwapo wamekubali/kukataa muungano kati ya Tz, Kenya na Uganda, na bado leo tunaambiwa ahh...Rwanda na Burundi nao wamo....!!!!

Hiyo tume kazi yake ni kuwaambia wananchi kuwa Tanzania imejiunga au inatakiwa kuchukua maoni ili watanzania waamue kujiunga au kutojiunga??? Kama serikali tayari iliamua kujinga mbona tunapoteza hela za walipa kodi bure; tume ya nini????!!!

Mwisho wanabodi naomba nielekezwe mahali panapopatikana Katiba ya hii jumuiya (natumai kuna draft mahali kama katiba kamili bado); natumai kutakuwa na referandum ya kukubali au kukataa katiba kamili hii kabla maraisi na jumuiya yao hawajaamua kuipitisha halafu waje watuambie Tanzania sasa inafuata Katiba ya EA pamoja ya Tanzania.
 
POLENI NDUGU ZANGU


Tangu jana baada ya habari hii kupatikana kutoka shirika la habari la UK Reuters kwa wale walio nje ya bongo, wengi wamebutwaa na wanaomboleza ndio maana huoni posting nyingi. Lakini wewe subiri - kimya kikubwa kina mshindo.

watanzania wanalitafakari hili suala kwa kila upande pamoja na mizengwe yote hii.


Wacha
 
sawa sawa! Rwanda na Burund- hongera sana-!! hili jambo lime nifurahisha sana...Sasa ni wakati wa Congo-zambia- malawi- Msumbiji- somalia kuangalia uweze-kano wa kujiunga!! na sisi-!!

Hasa Congo!!
 
Back
Top Bottom