Ebu niambie unapoona hii kitu unamkumbuka nani katika mahusiano

Ebu niambie unapoona hii kitu unamkumbuka nani katika mahusiano

Mie kuna sister mmoja nikiwa lasaba pale Tabora nilikuwa nampenda sana kumwambia nashindwa, siku moja nikamwambia mshkaji wangu kwamba nimemuota yule dem si akamwambia! Dah niliepuka skuli wiki zima siku niliporejea nikamfata yule dem nikamwambia aniazime daftari la sayansi kilimo kumbe nilikuwa napima kina cha maji!
 
View attachment 204940

Najua utakataa lakini ulipo kuwa shule ya msingi kuna mtu alikuwa anakuumiza nafsi na hatimaye ukatengana naye mara baada ya kumaliza. Sasa basi napenda upate fursa ya kuieleza jamii nini unakumbuka unapoiona hiyo kitu hapo juu katika hadithi yako ya mahusiano. Maana wengi wetu tumeanza kubarehe tukiwa shule za msingi na kama unavyo jua mihemko pindi tunapo barehe.

Mmmm unanikumbusha mbali sana charii. Kuna dada nilikuwa nampenda sana alikuwa akiitwa editor kaolewa sahv ila still your in my memory
 
nakumbuka wakati niko mwaka wa pili mzumbe university nilichaguliwa kuwa timekeeper, ilikuwa kazi ngumu sana kugonga kengele chuo kizima wasikie.
 
Nilikuwa time keeper primary enzi hiyo. I thought i was part of the school administration!
 
sioni uhusiano wowote hapo na sikumbuki kitu chochote
 
mkuu you took me very back ic namkumbuka dadaa mmoja alikua anitwa khadija alikuja akawa sijui miss nini huko daaah!! nilikua namkubaali kinyama hadi bro wangu akawa ananitania eti mie mchafumchafu nakuaje na kitotoo kisafi lakin mie kilikua kinanielewa coz nikua mcheshcheshi kiaina na story zisizokua na mwisho...
 
Mmh...std 7 na mambo ya ngono wapi na wapi? Mie hata form IV nilikuwa nayasikia tu.

mmmmh! nyie ndo mlikuwaga akina mama kwenye kibabababa na kimamamama alaf mnacheza kamchezo kaleeeeee:A S-rap:
 
Nilikupenda sana MWAJABU MBATA,tulipokuwa shule ya msingi buzebazeba miaka ya 2004-.2006. popote ulipo pokea salam zangu!
 
Da nilikuwa mtaalam wa zomari kwenye blas band... hahahaha mapumziko saa sita kwenda kula nyumbani,... uji wa buruga, kwenda shule na kidumu cha kumwagilia maua, kimfuko cha mbolea.... tena mama ndio ananiandalia (ubarikiwe sana Mama yangu uwe na maisha marefu)...maua yenyewe maua saa sita na mengine vimbegu vyake vilikuwa ninanasa kwenye nguo ...

umenikumbusha umishumita nikitimua mbio 100m na 110m kupokezana vijiti, umikumbusha nilipokuwa golikipa wa kutumainiwa au mkoba hahahah was so real ujamaa life.
 
Aisee mi nakumbuka huyo kaka alikuwaga time-keeper alikuwaga ananifukuzia mi kipindi hicho nlikuwa la tano ye la saba. Nilikuwa nampenda ila nlikuwa naogopa kumkubalia.Bas hiyo kengere ilikuwa karibu na darasa letu kila akienda kugonga kengele ya mapumziko lazima nimchungulie daaah... Alipomaliza alienda kusoma boarding akawa kila akirudi likizo haachi kunifukuzia.....badae nlimkubalia tukawa tunaandikiana barua ila kumsogelea hivi nlikuwa naogopa kama nini. Siku hizi nasikia ni dereva wa halmashauri fulani ktk wilaya fulani hivi.....
yeah it was MWANDU PR.SCHOOL somewhere in central tanzania,guess what....
 
Back
Top Bottom