Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Ule uchovu wa akili na mwili kutokana na uzee kweli Lowassa anaweza kazi hiyo unayodai.

Walianza kina Juma Volter Mwapachu na wengine kuonesha hawana uwezo wa kuhimili mikiki wakiwa upinzani na CHADEMA haikufa.

Hili la Edward Lowassa kurudi CCM ni dalili njama zote za kuimaliza CHADEMA zimeshindwa.

Katika wazee wote wa mabadiliko tutamkumbuka sana Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ambaye leo amesalitiwa na Mzee Edward Lowassa katika imani ya mabadiliko.

Tujikumbushe hotuba ya Mzee Kingunge Ngombale Mwiru tarehe 24 Oct 2015 viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam akizungumza na wana-Dar es Salaam kuhusu hatima ya nchi yetu wakati akimnadi Edward Lowassa.

Mzee Kingunge - "CCM imechoka na kuishiwa pumzi ya kuleta maisha bora kwa wa-Tanzania pamoja na ahadi nyingi za CCM..kutokana na sera mbovu.."

Source : Jamii Forums
 
Subiri upepo wa sumaye and co wakule kwao...
Kesho kaa karibu na Runinga yako kusikiliza bendera fata upepo kutoka pande zote za nchi hahaha...

Siasa za Tanzania bhana.
-ajira karibia na uchaguzi
-kuunga juhudi wakati wa uchaguzi
-kulipa wastaafu wakati wa uchaguzi

Yote hayo kwa kikundi cha watu chenye lengo moja yaani chama cha siasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja ya CCM kukamata mafisadi kwishneiiiiiiiiiiii hahahahahahahahah Raha sana Beberu limerudi zizini
 
Kilichotokea kwa lowassa ni ubinafsi,tena wa hali ya juu sana,Jinsi watanzania walivyompigania kwa kweli inauma sana.Ile imani ya kuwa na upinzani imara inaitaji manabii,chadema chaliiii,Aya mzee slaa alioji "lowassa ni asset or liability".......chadema walikiamishia choo sebuleni,sasa ccm wamekirudisha sehemu yake.This is tanganyika
 
Pamoja na mambo mengine siasa ni ujasusi, information is power, ni vyema kujua next move ya mpinzani wako. Kwa kuwa CCM imekula chumvi ya muda mrefu upande huu wako makini sana.
Lowassa atamkabidhi mwenyekiti wa CCM ripoti nzito ya miaka mitatu yenye kurasa 5000 muda wowote kuanzia kesho, ripoti hiyo imeshikiria ubunge wa wabunge kibao wa Chadema. Ripoti za vikao vyote vya Chadema kuanzia siku ya kwanza Lowassa anatambulishwa Chadema ,mikutano yote ya Chadema hasa ukizingatia Lowasa ndio alikuwa analipia ukumbi basi Chadema waliongea yote wakijua ni mwenzao kumbe jasusi.
Yajayo ni mengi [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbunge yupi wa kinondoni alijitoa CHADEMA mbona sijawahi kusikia hivo kinondoni kumeshawahi kuwa na Mbunge wa CHADEMA kweli?
Yule Mtulia wa UKAWA sijui alikua CHADEMA sijui CUF ila mimi nilimpigia kura sababu chama changu kilikua CHADEMA na yeye alikua anawakilisha huo Muungano wa UKAWA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli nimeamini watanzania ni wanafiki. Alipohama na kipindi chote alichokuwa CDM alikuwa ni fisadi na wanaccm wote walikuwa wanaimba wimbo huo wakati wanachadema wakisema hapana huyo ni safi. Leo karudi CCM tena wote Lumumba wanaimba mapambio ya kumsifu yule yule fisadi mmhh
 
Kuna ccm makalai wanafurahia lowasa kuludi ccm kumbe hawajuwi kua chadema inajiandaaa kuchukua Inch natayari washamuandaa Mh Lisu kuamgombea sasabasi huu nimpango maalum wa chadema ambao kamatikuu imekaa na kumpeleka mzee Lowasa lengo ni kutibua mipango ya ccm katika uchaguzi mkuu. (Yajao Yanafuraisha)

Sent using Jamii Forums mobile app

Hahahahaaaa

Unanichekesha sana mkuu!

Good theory though!

Inawezakua kweli kiutani utani hivi!
 
hili swali alijibu ndugu yetu Mwanakijiji....
Hili swali hata mimi linanipa wakati mgumu sana.

Wanasiasa wote wanafik, wapo kwa maslahi yao binafsi na si maslahi ya wananchi kama tunavyojitahidi kuamini.

Watanzania, tusiuane na kujiumiza kwa kushawishiwa na viongozi wa siasa au eti kwa mapenzi ya chama. Hili ni fundisho kubwa sana.
 
Ule uchovu wa akili na mwili kutokana na uzee kweli Lowassa anaweza kazi hiyo unayodai.
Haikuwa kazi ngumu kihivyo, Kila kitu alikuwa anawekea kwenye flashdrive tena kwa baraka za mwenyekiti
 
Back
Top Bottom