Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Lowassa atufunze sie Vijana tupende na tushike Itikadi ya Vyama sio Mtu, poleni wote mliohamaVyama vyenu kwa sababu ya Lowassa
 
Shukrani kubwa sana kwa mzee Lowasa.

Ulichotufanyia kama ukawa ni mambo makubwa sana, Umetuongezea wabunge na madiwani wa kutosha sana bila kusahau Halmashauri nyingi ambazo chadema au CUF wanaziongoza.

Nakutakia mafanikio mema uko uendako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wana nd
tulikuwa tukifunga na kuomba fisadi kuu liondoke ajiunge na alikozaliwa. Mungu katujalia ameondoka kajiunga na RA kubwa lao. Sasa ni wakati wa kumweleza Sumaye na wengine waondoke na Freeman Mbowe muuza chama. Zitto arudi cdm aongeze nguvu upinzani. Lisu tayari kashapata njia nyeupe kumkabili JP. Mbowe umefanya mengi tunakushru sana kwa ili la lowasa kwa kweli ulituumiza sana. Hata Dr. SLAA ANAWEZA KURUDI SASA na John kapata raha kwani sera ya ufisadi inarudi Mrsa ni
1. Karudi baba mmoja,
toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,
na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja,
ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli iwafae maishani.

2. Akatamka mgonjwa,
ninaumwa kwelikweli,
Hata kama nikichanjwa,
haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa,
kifo kimenikabili,
Semeni niseme nini,
kiwafae maishani.

3. Yakawatoka kinywani,
maneno yenye akili,
Baba yetu wa thamani,
sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani,
mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali,
itufae maishani

4. Baba aliye kufani,
akajibu lile swali,
Ninakufa maskini,
baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni,
kama mnataka mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

5. Wakazidi kumchimba,
baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba,
hatujui fumbo hili,
akili zetu nyembamba,
hazijajua methali,
Kama tunataka mali,
tutapataje shambani?

6. Kwanza shirikianeni,
nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani,
mwisho mtapata mali,
haya sasa buriani,
kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

7. Alipokwisha kutaja,
fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja,
roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

8. Fumbo wakatafakari,
watoto wale wawili,
wakakata na shauri,
baada ya siku mbili,
wote wakawa tayari,
pori nene kukabili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

9. Wakazipanda shambani,
mbegu nyingi mbalimbali,
tangu zile za mibuni,
hadi zitupazo wali,
na mvua ikaja chini,
wakaona na dalili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

10. Shamba wakapalilia,
bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia,
wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

11. Wakanunua na ng'ombe,
majike kwa mafahali,
wakapata na vikombe,
mashine na baiskeli,
Hawakuitaka pombe,
sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

12. Wakaongeza mazao,
na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao,
wakaihubiri mali,
Wakakiweka kibao,
wakaandika kauli...

"KAMA MNATAKA MALI
MTAIPATA SHAMBANI".
 
EL ndiye mshindi! CCM na CDM wote ni aibu tu....kwa walio timamu. Hakuna mwenye afadhali. Tena anasema "amerudi nyumbani"....na CCM top brass yote inampigia makofi! Aibu sana. Kama ilivyokuwa kwa CDM mwaka 2015. Ngoja tuone sasa "sifa" atakazo mwagiwa na ccm ma "kashfa" atakazomwagiwa na CDM!.
Nimependa hiyo aliposema, nanukuu, "amerudi nyumbani"...sikuwahi kumsikia akiita Chadema nyumbani. Nadhani kwa kauli hiyo na ile ya wana CCM waliomwimbia Kikwete kwamba wana imani na Lowassa akiwemo Waziri Mkuu Majaliwa, Guninita, Sophia Simba n.k. inajibu maswali kadhaa.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Amerejea Rasmi CCM Leo.

Amepokelewa Lumumba Makao Makuu Madogo Ya Chama Cha Mapinduzi Na Katibu Mkuu Dr Bashiru Ally.

Aidha, katika mapokezi hayo walikuwepo Rais Magufuli, Rostam Aziz, Mzee Phillip Mangula, Waziri Mkuu Majaliwa Kassim, Humphrey Polepole n.k

Habari zaidi...

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa amerejea Chama cha Mapinduzi (CCM) Ijumaa, nchini Tanzania. Lowassa alikuwa mgombea wa kinyang’anyiro cha urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na vyama vinavyounda umoja wa UKAWA katika Uchaguzi mkuu 2015.

Kurejea kwa Lowassa kulikuwa kukitabiriwa na baadhi ya watu, lakini mara kadhaa Lowassa alikanusha kuwa anampango wa kurudi katika chama hicho.

Vyanzo vya habari vinasema hatua hiyo imewashitua watu wengi, kwa sababu ya kile ambacho kilisababisha yeye kuhama chama hicho.

Lowassa baada ya kuitumikia CCM kwa kipindi kirefu alikihama chama cha hicho kufuatia mvutano uliotokea baada ya kutoidhinishwa na chama hicho kuwa mgombea wa urais.

Sherehe za mapokezi yake wakati akirejea rasmi Ijumaa zilifanyika katika ofisi ndogo ya CCM iliyoko Lumumba Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa chama hicho John Magufuli.

Lowassa mara kadhaa amefanya mazungumzo na Rais John Magufuli, Ikulu ya Tanzania.

Kumekuwa na wimbi la wanachama wa upinzani kuingia CCM tangu Magufuli achaguliwe 2015, kitu ambacho kimekuwa kikizungumziwa katika duru za siasa kwamba kinadhoofisha upinzani.



View attachment 1035375
View attachment 1035459
View attachment 1035448

Unaweza soma pia:

Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM - JamiiForums

Edward Lowassa: Wanaodhani nitarudi CCM wanapiga porojo na kuota ndoto - JamiiForums

Lowassa hana namna zaidi ya kuipigia magoti CCM, Mkwewe Sioi Sumari mpaka sasa yupo lockup - JamiiForums

USED FROM KINONDONI.
 
King maker RA ndani ya nyumba, kuna kitu kizito bila shaka kinaendelea woga umetanda lazima wahuni watafutwe wapambane na mhuni mwenzao maana hasomeki na inaonyesha kama anacheza karata zake vizuri hivi kupitia vijana wake.. Ngoja tuone mchezo sasa..
 
Safi sana. Huyu mzee alitunyima pumzi kwa hakika. Leo nakula maji hadi asubuhi.
 
Back
Top Bottom