Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Kweli nimekubali mwnasiasa yoyote yule haaminiki. Halafu nasikia dirisha dogo la usajili limefunguliwa tena. Naona na Rostam muda si mrefu tutasikia nae amerejea bungeni.
 
Kuondoka kwa Lowasa kume uongezea upinzani nguvu, hivyo tutarajie uchaguzi wenye upinzani kuliko 2015 , zaidi ya yote Babu wa watu amesoma alama za nyakati kuwa asingepata nafasi ya kugombea tena.
Kwa heri Babu huu muziki tuachie tuucheze siye na tutahakikisha kuwa hatuta lala iwe jua iwe mvua hadi CCM ing'oke.
Babu kwa taarifa tu nikwamba upinzani hakuhitaji watu wenye nia mbili mbili, upinzani hauitaji watu wenye kufikiria sana madaraka, badala yake upinzani unahitaji zaidi watu wanaofikiria ukombozi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya kula na kushiba, ndipo usingizi ulipoanza kunishika. Kweli ni sawa kwa jinsi ambavyo waungwana wanasema "et, shibe ni mtoto wa malevya na njaa ni mtoto wa malegeza!" Kwa kweli inastaajabisha mno, katika kuamini jambo hili, hata hivyo nimeshiba kweli kweli. Nikiwa nimeamka tayari kwa kuelekea kitandani.... Mara anakuja Asia, ambaye ni dada yangu, huku akiniita "Billieeee!!! Bibi anakuita, Fanya haraka ujeee...". "Nakujaaa..." Nikamuitikia.

"Naam Bibi, nimekuja tayari." Nikamuitikia huku nikipapasa kutafuta mahala pa kuketi kwenye mkeka. "jamani wajukuu zangu, kwanza ninayofuraha kubwa kuwaiteni ninyi mahala hapa, kwani nimeona ni vema kuwaeleza jambo la msingi na lenye umuhimu mkubwa kwenu" alianza kuzungumza kwa kuanza na maneno hayo. Akaendelea huku akisema "kwa maneno machache sana, napenda niwashirikishe jambo lifuatalo: Ni kwamba... Ni jambo la hekima kubaki katika usalama wa watu walio salama, chini ya uangalizi wa Baba anayejali, anayependa na anayejua kutunza, badala ya kwenda kutafuta raha katika mahala pa mbali.... Na kwa wakati mmoja wafurahieni wale wote waliowarudia ninyi kwa hiari yao wenyewe kwa lengo la kutimiliza malengo ya pamoja yaliyo na tija kwenu ninyi na kwa wenzi wenu." Baada ya kusema maneno hayo machache sana, akainuka kisha akautaaga akisema "Chilo mwaka!" Kwa pamoja tukamjibu tukisema, "Chilo mwaka nagwe!" huku nasi tukielekea kwenda kulala kila mtu chumbani kwake. Kesho yake asubuhi ikawa ndio siku ambayo niliweza kufahamu maana ya maneno ya bibi, aliyotueleza usiku wa jana.

Karibu sana mzee Lowassa, CCM na Serikali ilikuhitaji na inakuhitaji kwa ajili ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa lengo la kuwahudumia watanzania.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!!
 
Kweli nimekubali mwnasiasa yoyote yule haaminiki. Halafu nasikia dirisha dogo la usajili limefunguliwa tena. Naona na Rostam muda si mrefu tutasikia nae amerejea bungeni.
Ndiyo ukweli Kafumu anafumuliwa mwenye jimbo anarudi kama Trump
 
Siku zote sina mashaka na mzee Lowasa, ila nina mashaka na uwezo wa viongozi wa cdm. Ni watu ambao hawajui hata wanachopigania au hawajui misimamo ya chama chao.
Lowasa ana akili kubwa sana kuliko ma-cdm wote. Katika list of shame, lowasa alikuwepo na waliokuwa wanahubiri ni cdm, walimtukana na kumdharirisha. Baada ya kutoka mwembeyanga wakazunguka mikoani kutukana watu na kudharirisha.
Lowasa akatumia msemo usemao " mchawi mpe mwana alee." Wakaazunguka tena kumsafisha na kumtukana Slaa.
Leo Lowasa karudi kwao akiwa msafi na moja ya mchawi mkuu akiwa katimuliwa kwa kutaka kumroga mwana.
 
Watu wa Mungu habari zenu..

Tetesi za ndani za CDM ni maumivu makali baada ya Mh Lowassa kurudi nyumbani kumenoga..!! Yaani ni sawa kuvunjika kwa uti wa mgongo, haiwezi tena kujitutumua hata kidogo kisiasa..!! Poleeeeni..!

CCM haishindwi chochote huwa nasema hivi kila mara.. Sasa mmeona na kudhibitisha..! Chezea kitu kingine sio CCM..!! CHADEMA leo bado wako ktk maruweruwe hawajui nini kimetokea, hawaamini bado..!! Siasa mchezo mchafu sana..!! 😜😂😂
Safi tu
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimesema kuondoka kwa mwanachama wake, Edward Lowassa na kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) hakutakuwa na madhara yoyote.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa Machi 1, 2019 na Katibu Mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Dk Vicent Mashinji alipozungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya Lowassa ambaye ni waziri mkuu wa zamani kutangaza uamuzi huo.

“Tunamtakia maisha mema huko aendapo, yeye ni mtu mzima anajua anachokifanya,” amesema Dk Mashinji.
Alipoulizwa iwapo uamuzi wa Lowassa unaweza kukitetelesha chama hicho kikuu cha upinzani Dk Mashinji amejibu kwa kifupi “It will never happen"(haiwezi kutokea).

Na Tausi Mbowe, Mwananchi
CHADEMA YAFUNGUKA LOWASSA KUREJEA CCM..."YEYE NI MTU MZIMA ANAJUA ANACHOKIFANYA"

Neno la Sumaye baada ya Lowassa kurejea CCM

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye ameeleza maoni yake baada ya kusikia Edward Lowassa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Sumaye amesema "Mimi haunipi shida, mtu akiamua kuhama chama na kwenda kingine ni uamuzi wake,” alisema Sumaye.

"Kama kaamua acha aende, sisi tutaendelea kujenga chama na hicho unachokisema cha kuhama ni ndoto ambayo haipo,” amesema Sumaye alipoulizwa kama na yeye ni miongoni mwa watakaorejea CCM.

Edward Lowassa alijiunga CHADEMA Julai 2015 baada ya jina lake kuenguliwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa Urais ndani ya CCM


Neno la Sumaye baada ya Lowassa kurejea CCM - MUUNGWANA BLOG
Magufuli alipo waalika wastaafu,sumaye alitamka kuwa kwenda kwako cdm ni faida kwa ccm.
Asiaminike

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom