Nilichonote hapa
1. Bado mwanakijiji haoni sababu ya kutomuunga mkono Magufuli.
2. Anaona CHADEMA walikosea kumpokea lowassa hivyo wawaombe radhi watz
3. Mbowe awajibike kwa kumpokea Lowassa.
4. Kuondoka kwa Lowassa upinzani ni uthibitisho kuwa CHADEMA walikosea kumpokea.
4. Anaamini ELna RA ni wachafu na mafisadi.
5. Haoni kama ukaribu wa RA na EL kama utamcorrupt Magufuli maana anaamini Magufuli ni strong enough kuwa collapsed.
6.Anaamimi JPM amefanya mabadiliko makubwa, amebaki njia panda kwenye iwapo JPM atafanikiwa kuibadilisha CCM.
7. Anaamini kuna majeraha Lowassa ameyaacha upinzani, wakati huohuo anakiri kuwa Lowassa hajawahi kuwatetea upinzani.
At this juncture ninakubaliana na Mzee Mwanakijiji kwenye hoja moja tu nayo ni kuhusu kujiuzuru kwa Mbowe au kutogombea maana mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi chamani na kama sikosei wapo ngazi ya mkoa. Mbowe asigombee siyo kama ishara ya kuwajibika bali kama ishara ya kusadifu ile demokrasia inayoimbwa CHADEMA hivyo tu basi.
Pia nimpongeze Mwanakijiji kwa kuendelea kumuunga mkono JPM na kukiri hilo waziwazi. Tofauti na watu kama chahali and the like ambao mwaka 2015 walikuwa kwa JPM sahizi wanajifanya wanatunafkia eti wapo upinzani. Kisingizio eti walimsapoti JPM sababu ya Lowassa. This is absurd, Lowassa anaweza kuwa sababu ya wao kutosapoti upinzani lakini hawezi kuwa sababu ya wao kumsapoti JPM waache kujificha kwenye visingizio wabaki huko na JPM wao.
Mawazo mengine ya Mzee Mwanakijiji siyapingi moja kwa moja lakini yanahitaji kuwa substantiated enough to convince any reasonable person. Nitapoint out mkanganyiko wa mawazo yake hapa chin.
i. Mzee Mwanakijiji hajaeleza kuondoka kwa Lowassa kunakuwaje uthibitisho wa kuwa CHADEMA (au mbowe kama anavyodai) alikosea kumpokea Lowassa? Hivi kuna uhusiano wa "Kupokelewa" na "kuondoka". Kama kuondoka ni uthibitisho wa kuwa walikosea kumpokea je inamaana CHADEMA walikosea kumpokea Kafulila kutoka nccr maana naye ameondoka? Je wasira alipokelewa upinzani kimakosa ndiyo maana akaondoka? Similar facts are to be treated equally. Mwanakijiji ameshindwa kueleza uhusiano uliopo hapa na kwamba je ili umpokee mtu unatakiwa ujiulize atadumu muda gani? Na je chama kina option ya kumnyima kadi mtu kwa sababu yoyote ile?
Na kama ni kumpa mtu ugombea je ukipewa kugombea Urais unatakiwa usiondoke? Vipi tuna guarantee gani kuwa akigombea Lissu au mbowe hataondoka baada ya uchaguzi? Na akiondoka ni uthibitisho kuwa tulikosea kumpa kugombea?
2. Hoja kwamba Lowassa ameacha majeraha CHADEMA wanayotakiwa wayatibu imekuwa conflicted na hoja yake Mwanakijiji mwenyewe kuwa Lowassa hakuwahi kuwa mpinzani wa kweli hivyo kwa maoni yake alikuwa mzigo maana hakuwatetea wapinzani. Mwanakijiji anmeshindwa kuondoa mgongano katika hoja hii.
3. Mwanakijiji ameshindwa kueleza ni kwa jinsi gani anatuguarantee kuwa JPM ataweza kudhibiti (mafisadi kwa mujibu wake Mwanakijiji) akina EL na RA wanaomkaribia kwa karibu. Na ameshindwa kueleza je kuna ulazima gani CCM na mtu (credible kwa mujibu wa Mwanakijiji) kama JPM awe karibu na "mafisadi" aache kazi zake ofisini aende Lumumba uongozi mzima wa chama kumpokea "Fisadi". Hii inamaana gani na wana umuhimu gani hawa Mwanakijiji anaowaona siyo "wasafi" kupewa heshima kubwa na "msafi" (asiyedanganyika kwa mujibu wa Mwanakijiji)?
4. Kuhusu mabadiliko na utendaji wa JPM ni very subjective inategemeana unatazama kutokea angle gani. Mwanakijiji ameshindwa kuonesha ni angle gani anayomtazama Magufuli maana wapo wanaomtazama kama Rais wa wizara ya "miundombinu na uchukuzi" pekee.
Nawasilisha!
Sent using
Jamii Forums mobile app