Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Na wafanyakazi wa serikali Lowassa ndie alikuwa anawapa mishahara? Maana hadi Leo hawajawahi kuongezewa mishahara tangu Lowassa asepe


Yaan umeniwahi haswa................ na huyo huyo Lowasa ndio aliyekuwa akitoa mafao ya wastaafu maana nao hali yao tete kabisa hali si hali na huyo huyo Lowasa ndio aliyekuwa anapandisha madaraja ya Serikali. Next time utulie ndio uanzishe thiredi hapa maana unadhani kuanzia thread ni rahisi
 
Nimepitia maoni yako hata hivyo hoja zako nyingi ni self centred,ni mawazo yaliyosheheni hisia binafs!!!Kwa maoni yangu umeonesha udhaifu mkubwa kuaanda maada iliyojaa hisia zako binafsi!!!!Sijaona objectivity kwenye hoja zako hata hata hvyo naheshimu maoni yako!!

Sasa si ndio maana ya maoni; sikuwa nafanya academic research; lakini ndani yake utaona madai yangu ya objectivity.
 
Brother najua watu ambao hamkupenda yale maamuzi mnafikiri huu ndio wakati muufaka kuonyesha hayakuwa sahihi,lakin unajua kampen za arumeru lowassa alikuwa target kwa sababu na yeye alishiriki zile kampen moja kwa moja,japokuwa hakuna aliyenionyesha ni kwa jinsi ghani chadema waliathirika na uchaguzi wa 2015 kwa kumuweka lowassa kama mgombea
Yaani, hadi sasa kweli kabisa huoni jinsi gani CHADEMA iliathirika? au hutaki kuona?
 
MWEMBESI ONE Hoja yangu ni rahisi sana. Kuna baadhi ya wana-CHADEMA tena wengine ni viongozi wa ngazi ya Kamati Kuu waliwaaminisha watanzania kwamba Lowassa ndiyo alama ya ufisadi na ndiyo ufisadi wenyewe...

Of course. Japo mimi si mwana-CDM, lakini nimeegemea upande wa upinzani. Nilikwazika kuona CDM wanampokea Lowasa na kumfanya mgombea wao wa uraisi. Nilikwazika zaidi kumuona Slaa akjiengua. Hilo lilikuwa kosa lliliofanywa na viongozi wa CDM, labda na washirika wao katika UKAWA.
Pamoja na kukwazika huko, bado nilichagua upinzani kwa sababu naona ccm kama chama kimechoka kupindukia; na kinaumwa kifafa
 
Nilichonote hapa

1. Bado mwanakijiji haoni sababu ya kutomuunga mkono Magufuli.

2. Anaona CHADEMA walikosea kumpokea lowassa hivyo wawaombe radhi watz

3. Mbowe awajibike kwa kumpokea Lowassa.

4. Kuondoka kwa Lowassa upinzani ni uthibitisho kuwa CHADEMA walikosea kumpokea.

4. Anaamini ELna RA ni wachafu na mafisadi.

5. Haoni kama ukaribu wa RA na EL kama utamcorrupt Magufuli maana anaamini Magufuli ni strong enough kuwa collapsed.

6.Anaamimi JPM amefanya mabadiliko makubwa, amebaki njia panda kwenye iwapo JPM atafanikiwa kuibadilisha CCM.

7. Anaamini kuna majeraha Lowassa ameyaacha upinzani, wakati huohuo anakiri kuwa Lowassa hajawahi kuwatetea upinzani.

At this juncture ninakubaliana na Mzee Mwanakijiji kwenye hoja moja tu nayo ni kuhusu kujiuzuru kwa Mbowe au kutogombea maana mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi chamani na kama sikosei wapo ngazi ya mkoa. Mbowe asigombee siyo kama ishara ya kuwajibika bali kama ishara ya kusadifu ile demokrasia inayoimbwa CHADEMA hivyo tu basi.

Pia nimpongeze Mwanakijiji kwa kuendelea kumuunga mkono JPM na kukiri hilo waziwazi. Tofauti na watu kama chahali and the like ambao mwaka 2015 walikuwa kwa JPM sahizi wanajifanya wanatunafkia eti wapo upinzani. Kisingizio eti walimsapoti JPM sababu ya Lowassa. This is absurd, Lowassa anaweza kuwa sababu ya wao kutosapoti upinzani lakini hawezi kuwa sababu ya wao kumsapoti JPM waache kujificha kwenye visingizio wabaki huko na JPM wao.

Mawazo mengine ya Mzee Mwanakijiji siyapingi moja kwa moja lakini yanahitaji kuwa substantiated enough to convince any reasonable person. Nitapoint out mkanganyiko wa mawazo yake hapa chin.

i. Mzee Mwanakijiji hajaeleza kuondoka kwa Lowassa kunakuwaje uthibitisho wa kuwa CHADEMA (au mbowe kama anavyodai) alikosea kumpokea Lowassa? Hivi kuna uhusiano wa "Kupokelewa" na "kuondoka". Kama kuondoka ni uthibitisho wa kuwa walikosea kumpokea je inamaana CHADEMA walikosea kumpokea Kafulila kutoka nccr maana naye ameondoka? Je wasira alipokelewa upinzani kimakosa ndiyo maana akaondoka? Similar facts are to be treated equally. Mwanakijiji ameshindwa kueleza uhusiano uliopo hapa na kwamba je ili umpokee mtu unatakiwa ujiulize atadumu muda gani? Na je chama kina option ya kumnyima kadi mtu kwa sababu yoyote ile?

Na kama ni kumpa mtu ugombea je ukipewa kugombea Urais unatakiwa usiondoke? Vipi tuna guarantee gani kuwa akigombea Lissu au mbowe hataondoka baada ya uchaguzi? Na akiondoka ni uthibitisho kuwa tulikosea kumpa kugombea?

2. Hoja kwamba Lowassa ameacha majeraha CHADEMA wanayotakiwa wayatibu imekuwa conflicted na hoja yake Mwanakijiji mwenyewe kuwa Lowassa hakuwahi kuwa mpinzani wa kweli hivyo kwa maoni yake alikuwa mzigo maana hakuwatetea wapinzani. Mwanakijiji anmeshindwa kuondoa mgongano katika hoja hii.

3. Mwanakijiji ameshindwa kueleza ni kwa jinsi gani anatuguarantee kuwa JPM ataweza kudhibiti (mafisadi kwa mujibu wake Mwanakijiji) akina EL na RA wanaomkaribia kwa karibu. Na ameshindwa kueleza je kuna ulazima gani CCM na mtu (credible kwa mujibu wa Mwanakijiji) kama JPM awe karibu na "mafisadi" aache kazi zake ofisini aende Lumumba uongozi mzima wa chama kumpokea "Fisadi". Hii inamaana gani na wana umuhimu gani hawa Mwanakijiji anaowaona siyo "wasafi" kupewa heshima kubwa na "msafi" (asiyedanganyika kwa mujibu wa Mwanakijiji)?

4. Kuhusu mabadiliko na utendaji wa JPM ni very subjective inategemeana unatazama kutokea angle gani. Mwanakijiji ameshindwa kuonesha ni angle gani anayomtazama Magufuli maana wapo wanaomtazama kama Rais wa wizara ya "miundombinu na uchukuzi" pekee.

Nawasilisha!

Sent using Jamii Forums mobile app

Very good counter attack arguments....

Hata hivyo, alichokiandika MwanaKijiji hakiwezi kuwa ni "facts" bali yatabaki kuwa ni "maoni" yake tu....

Hii ni kwa sababu na kama ulivyosema, inategemea sana unayatazama mambo haya katika engo gani kwa kuzingatia siasa zetu za Kiafrika na hususani za Bongo yetu hii....

Na kwa mtazamo wangu, issue ya Mbowe kujiuzulu eti tu kwa kuwa alifanya kosa hili la kumpokea EL kwa mazingira na siasa zetu hizi za Kibongo, binafsi sikubaliani nalo 100%....

Bado naona kabisa kuwa, kwa mazingira tuliyo nayo ingalau kwa kipindi hiki, Freeman Aikael Mbowe ndiye Mwenyekiti anayestahili kuendelea kuongoza harakati za mapambano hayo kwa CHADEMA....

Nakuhakikishia kuwa, likifanyika kosa la Mbowe kutangaza kuwa anaachia ngazi kwa sababu hii iliyotajwa na Mzee MwanaKijiji, ndiyo itakuwa mwisho wa CHADEMA na hakuna jambo muhimu lenye kuashiria kuua rasmi upinzani kabla 2020 wanalosubiri CCM kwa hamu kutokea upesi na kwa haraka isipokuwa mambo matatu haya yafuatayo:

1. Tundu Lissu kupotezwa kabisa ktk siasa za Tanzania aidha iwe kwa KIFO rasmi cha roho na mwili na cha aina yoyote ile ama asije kabisa Tanzania awe mkimbizi wa kisiasa huko huko aliko...

2. Freeman Aikael Mbowe haendelei kuwa M/kiti na Mbunge wa CHADEMA iwe kwa mbinu yoyote ama hata kwa KIFO cha mwili cha kawaida ama hata kisicho cha kawaida.....!!

3. Maalim Seif Sharrif Hamad na CUF ya Zanzibar wanapotezwa kisiasa kabisa iwe kwa KIFO cha kawaida ama hata kwa njia zozote zile. Rejea marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa juzi kati. Lengo ni hili hili.......

• Si ajabu maandiko haya ya kina Mzee Mwanakijiji yaliyoandikwa kwa mpangilio wa dizaini ya "Kimalaika wa nuru" kumbe ndani yake ni " utekelezaji wa kiapo cha ushetani na mkakati wa kufuta upinzani kabla ya 2020" mtupu.....

Soma tu ndani between lines utaligundua hili mara moja na utadhani kuwa ni full chembechembe za "nia njema", kumbe it's part of the strategic plans to lead the opposition to the road heading to hell before 2020 general Election...!!

Kama wanabisha, wanaopewa ushauri huu wenye "nia njema", wajaribu kuutekeleza waone impact yake....

In my opinion, acha Lowassa aende zake. Na nakubaliana kabisa na Mh. Freeman Mbowe, kuwa haya maisha yawe ktk nyanja ya kisiasa ama dini nk hayako "constant" kwamba ikiwa hivi basi inakuwa vilevile.....

It's like a Train Safari to Kigoma whereby on the way there will be get off and get in passengers....!!

Wanaoshuka hawawezi kuzuia Gari Moshi kuendelea na safari hadi mwisho wa Reli Kigoma....


Na haiwezekani kumshusha abiria kwa nguvu njiani mahali ambapo siyo Kituo chake cha kushukia....

Kumlazimisha Mbowe ajiuzuru kwa sbb ya EL, ni kumlazimisha abiria mwenye tiketi ya hadi mwisho wa safari - KIGOMA achukie Tabora junction na kumhadaa kuwa hapa ndo Kigoma .....!!
 
Of course. Japo mimi si mwana-CDM, lakini nimeegemea upande wa upinzani. Nilikwazika kuona CDM wanampokea Lowasa na kumfanya mgombea wao wa uraisi. Nilikwazika zaidi kumuona Slaa akjiengua. Hilo lilikuwa kosa lliliofanywa na viongozi wa CDM, labda na washirika wao katika UKAWA.
Pamoja na kukwazika huko, bado nilichagua upinzani kwa sababu naona ccm kama chama kimechoka kupindukia; na kinaumwa kifafa

Ulikubali kucompromise principles zako ili tu upinzani uende Ikulu. Kwamba, haikujalisha yote uliyosimamia kabla na kiu yako ya mabadiliko ikakufanya ufumbe macho usione kilichokuwa nikitoka mbele yako. My friend haukuwa peke yako.
 
Back
Top Bottom