Elections 2015 Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...

Elections 2015 Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...

Hakuna mungu wewe tapeli.
Mkuu Kiranga na hakuna Mungu yako, haina mashiko!. Hili la kuitana tapeli nalo neno!.
Nakuomba nenda kanisome imani yangu HAPA hizi kauli zako za hakuna Mungu ni mafanikio makubwa sana ya kishetani kuwaaminisha the weaks ones kiimani kama wewe kuwa hakuna Mungu na mkaamini!.

Wether you like it or not Mungu yupo!, na umuamini au usumuami, yeye ataendelea kuwepo!. Thare is nothing new under the sun, kila linalotokea, limeishakuwepo na limeisha pangwa miaka milioni nyingi nyuma, hivyo rais wa Tanzania 2015, aliishapangwa na kuandikiwa siku nyingi, kinachosubiriwa sasa ni taratibu tuu, kusubiria kumtangaza na kuapishwa!. Whoever aliyeandikiwa ndiye atakaye kuwa and no ane can do anything kuzuia.

Kama walivyo wengine, na wewe subiri tuu siku ya siku, uushuhudie utukufu wa Mungu!.

Pasco.
 
Hivi huyu Mzee mnamuhangaisha kwa nini? hivi mali alizonazo azimtoshi mpaka anataka ulaji kupitia Urais, Umri wake umeenda muno kiasi kwamba kizazi cha digital kina kasi zaidi kitamsumbua.. Lowasa akalee wajukuu wa Mwanae Rich-m bwana. Kha!
 
Mkuu Kiranga na hakuna Mungu yako, haina mashiko!. Hili la kuitana tapeli nalo neno!.
Nakuomba nenda kanisome imani yangu HAPA hizi kauli zako za hakuna Mungu ni mafanikio makubwa sana ya kishetani kuwaaminisha the weaks ones kiimani kama wewe kuwa hakuna Mungu na mkaamini!.

Wether you like it or not Mungu yupo!, na umuamini au usumuami, yeye ataendelea kuwepo!. Thare is nothing new under the sun, kila linalotokea, limeishakuwepo na limeisha pangwa miaka milioni nyingi nyuma, hivyo rais wa Tanzania 2015, aliishapangwa na kuandikiwa siku nyingi, kinachosubiriwa sasa ni taratibu tuu, kusubiria kumtangaza na kuapishwa!. Whoever aliyeandikiwa ndiye atakaye kuwa and no ane can do anything kuzuia.

Kama walivyo wengine, na wewe subiri tuu siku ya siku, uushuhudie utukufu wa Mungu!.

Pasco.

Wala hakuna shetani. Na huna jipya katika habari zako za kutumia jina la mungu kuhalalisha matakwa yako ya kisiasa.

Hata wafalme wa zamani aana wa Kichina na mafarao wa Kimisri walitumia gia ya mungu.

Ishapitwa na wakati.
 
Mzee wa sumu..... Saizi next ni nani baada ya Zito kuruka kamba.... Ila we kweli mburula unawezaje kupanga kumuuwa mtu kwa sumu....

Hata ile ajali ya kibaha wewe ndiyo ulihusika kumuuwa yule rafiki yako. Wakuu muogopeni huyu jamaa kama ukoma ni hatari sana.

Kukushauri kuwa utumie kiswahili badala ya kutumia kiingereza kibovu ndio umezusha haya na panic zote hizi?
 
JP Magufuli ni chaguo la watanzania wengi, anecdotal evidence inaonyesha ivyo, anakubalika katika makundi yote, vijana, wazee, wanawake, hadi wapinzani..kizuri kinajiuza, hauitaji kutumia pesa nyingi kujitangaza kama matangazo ya biashara.
 
Huyu ndio Pasco ,eti patachimbika asipochaguliwa Edward Ngoyai Lowasa mmmmmh
1.Patachimbika kivipi?
2.Unauhakika gani?
3.Na umeshafanya maandalizi ya kuchimbika?
 
Last edited by a moderator:
...Yule Aliyepangiwa na Mungu!.

Wanabodi,

2015 ndio hii, mimi ni miongoni mwa tuliojibainisha wazi, kumkubali Edward Lowassa as "The One and Only" Best President this country can ever have apart from Nyerere!. Hii haina manna Lowassa ndio lazima awe rais. Rais wa Tanzania kwa 2015 ni yule tuu, aliyepangiwa na Mungu, sio lazima awe ni Lowassa, ila kwa vile Mungu bado hajatuambia amempangia nani, kama aliepangiwa na Mungu ni Edward Lowassa, basi ni lazima awe yeye!.

Nakiri nimekuwa inspred kuandika mada hii, kufuaria mchango wa mwana jf huyu kwenye uzi fulani!

Mkuu So Notorious, kwanza nakubaliana na wewe, Pasco huyu unayemjua sasa ni mshereheshaji tuu wa maonyesho ya Saba Saba na Nanenane, kwa nyie watu wa kisasa. Pasco aliondoka rasmi newroom mwaka 2002 na tangu hapo hajawahi kuajiriwa tena, sasa amebaki kama Mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea. Sasa ili kumjua Pasco, rudisha mawazo yako mwaka 2002 ulikuwa level gani, na kuanzia hapo ndipo turudi nyuma!.

Pasco hajawahi kuwa spokesperson wa Lowassa, hajawahi kufanya kazi yoyote kwa Lowassa, hajawahi kuhudhuria press conference yoyote ya Lowassa, hajawahi kuandika au kuripoti news yoyote ya Lowassa na wala hajawahi kufika Monduli, au kuhudhuria zile sherehe maarufu za Monduli!.

Kitu pekee alichofanya Pasco humu jf, ni kumkubali Lowassa, katika ukweli dhahiri usio na mawaa yoyote kuwa ndani ya CCM, Edward Ngoyai Lowassa, ndie the one and only best presidential candidate CCM has, na ikitokea asipitishwe, then asipitishwe kwa haki, vinginevyo patachimbika!.

Hata hivyo kumkubali kwangu Lowassa, ni personal tuu, tena kwa kujitolea, siko Team Lowassa!, sijawahi kuwepo!, wala sijawahi kupokea hata senti moja kutoka kwa Lowassa!, hivyo hoja ya kumlamba mtu miguu kwangu haipo!, ningekuwa mlamba miguu, ningemlamba Mkapa ambaye mtoto wake nimesoma naye darasa moja sekondari kwa miaka minne!, wakati kwa wengine wote Mkapa ni rais, mimi nimekwenda kwake kama baba fulani!. Ningekuwa ni mtu wa kujikomba komba na kujipendekeza, ningejikomba kwa Riz 1, nimekutana nae UDSM na tunaiva sana, hivyo angenishika mkono anipeleke kwa mshure wake!, why nilambe miguu ya mtu?!. Mimi niko kwenye lile kundi la "Maskini Jeuri" kama kina "Kozi mwana mandanda, kulala njaa kupenda!".

Ila pia nina mtu wangu wa karibu kwenye Team Lowassa, hii ndio timu yenye mkono mrefu kuliko team nyingine yoyote so far!. Tatizo langu na timu hii ni moja tuu, hali ya Afya ya Mzee wetu!, kwa vile rais wa Tanzania 2015, ameishachaguliwa na Mungu, then, alilolipanga Mungu, binadamu hawezi kulipangua!, ndio maana kule nyuma Mungu aliwahi kufanya muujiza wa "Jiwe walilolikataa waashi likafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!", na kuna mtu alielezwa kuwa "Wewe ni mwamba, na juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!", kwa Tanzania hapa tulipofika, tuna mwamba mmoja tuu, "Mwamba wa Kaskazini!"
Lazima awe!, na asipokuwa basi itakuwa Mungu hakumpangia!, hivyo atakayekuwa rais wetu, 2015, ni yule tuu Mungu aliyempangia!.

Wasalaam!.

Pasco.

Mungu yupi maana wako wengi sana
 
EL akipitishwa na ccm kwa ushabiki; tena kwa sababu ya vijisent tu! Tutakuwa tumepitisha dalali aliyepindukia kwenye mambo ya ufisadi. Nchi ilipo kwa sasa inataka rais msafi asiye na makundi.

Siasa ni mchezo unaochezwa kitimu na kawme si kama mtihani ambayo kila mtu hufanya kivyake kuwa na kundi ndio njia moja kufanya siasa. CCM ni kundi tayari. Lowasa ana kundi kubwa la ccm. Je hii ni dhambi? Mahakama kila siku zinawashughulikia wezi, mbona lowassa hashitakiwi? Mafanikio ya mtu yasiwe tabu
 
Ni ukweli ulio wazi bila kificho, kwa hali ilivyo sasa ukiweka unafikiri, uzushi, kejeli, matusi, kashfa pembeni Edward Lowassa ndiye chaguo la wengi isipokuwa wachache tu.

Kwa hali ilivyo, Lowassa ni raisi hata bila kuwepo na kupigiwa kura wala kampeni. Napredict BIG IMPACT endapo chama cha mapinduzi hakitampitisha kupeperusha bendera ya ccm.

Enyi ccm na wanaccm, mpetisheni Lowassa kwani ni chaguo la wananchi wengi bila kujali ushabiki wa vyama vyao. Hata wapinzani wanakiri hawana ubavu wa kupambana nae katika uraisi.

Twende na Lowassa 2015.com
 
safari yenye matumaini sima a uhesabiwe,!nakuunga mkono
 
Mkuu kusema ukweli mimi siwezi kwenda na huyu mwizi fisadi asiyekuwa hata na chembe ya huruma kwa mali za taifa hili wewe kama umeweza kunufaika nazo hizo za ufisadi wewe nenda naye mfanikiwe salama japo mungu hayupo upande wenu.
 
Twende nae huyu ndio mwenyewe anafaa hakuna mwingine zaidi yake
 
Mkuu kusema ukweli mimi siwezi kwenda na huyu mwizi fisadi asiyekuwa hata na chembe ya huruma kwa mali za taifa hili wewe kama umeweza kunufaika nazo hizo za ufisadi wewe nenda naye mfanikiwe salama japo mungu hayupo upande wenu.

wengi tuko nae, wewe pita kushoto
 
Ni ukweli ulio wazi bila kificho, kwa hali ilivyo sasa ukiweka unafikiri, uzushi, kejeli, matusi, kashfa pembeni Edward Lowassa ndiye chaguo la wengi isipokuwa wachache tu.

Kwa hali ilivyo, Lowassa ni raisi hata bila kuwepo na kupigiwa kura wala kampeni. Napredict BIG IMPACT endapo chama cha mapinduzi hakitampitisha kupeperusha bendera ya ccm.

Enyi ccm na wanaccm, mpetisheni Lowassa kwani ni chaguo la wananchi wengi bila kujali ushabiki wa vyama vyao. Hata wapinzani wanakiri hawana ubavu wa kupambana nae katika uraisi.

Twende na Lowassa 2015.com

Ndiyo maana wapinzani hawasemi chochote mpaka sasa. Wanasubiri atemwe CCM wampe nafasi huku
 
Back
Top Bottom