TANZIA Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

TANZIA Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Taarifa zaidi itatolewa na familia na Serikali. Poleni wote


EDWARD NGOYAI LOWASSA AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Mtoto wake Fredrick Lowassa amethibitisha

Pia, Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2008 na kuweka rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzulu.

WASIFU WA EDWARD NGOYAI LOWASSA
Edward Ngoyai Lowassa anatoka katika jamii ya Wafugaji Kaskazini mwa Tanzania. Alizaliwa August 26 mwaka 1953 katika Kijijini cha Ngarashi Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha. Edward Lowasa ni mtoto wa tatu wa Mzee Ngoyayi.

Kitaaluma Lowasa ni msomi , akiwa na shahada kwanza kutoka chuo Kikuu cha Dar es salaam na shahada ya Uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Bath huko Uingereza (1983-1984).

Uzoefu katika siasa
Ingawa baba yake alikuwa mfugaji aliwahi pia kufanya kazi kama tarishi katika serikali ya wakoloni.

Alijiunga na chama cha CCM mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka wa 1977.

Kabla ya kugombea Ubunge , aliwahi kutumikia Jeshi la Tanzania na hata kupigana katika vita kati ya Tanzania na Uganda vilivyopelekea Idd Amin kuondolewa madarakani.

Baada ya hapo alikuwa Mtumishi wa Umma kwa miaka kadhaa kabla kuteuliwa kuwa Mbunge kuwajilisha Vijana na kujiunga rasmi na siasa.

Mwaka wa 1990 alijitosa ulingoni kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la uchaguzi la Monduli.

Alifanyikiwa kwa miaka yote hii Lowassa ameendelea kulishikilia jimbo hilo la uchaguzi hadi alipolazimika kuliachia ili kuwania Urais.

Mwaka 2015 alipowania Urais haikuwa mara yake ya kwanza kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwani mwaka 1995, alikuwa miongoni mwa watangaza nia 15, hata hivyo nafasi ikachukuliwa na Benjamin William Mkapa.

Hata hivyo tofauti na matarajio ya wafuasi wake, Mwaka 2005, Lowassa hakuwania nafasi hiyo, badala yake aliunga mkono rais anayemaliza muda wake Jakaya Kikwete.

Je Lowassa amewahi kuwa nani katika nyadhifa alizozipitia Kiserikali?
Edward Ngoyayi Lowassa amewahi, kuwa Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo, Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na nafasi nyinginezo.

Lakini pia nafasi za juu alizowahi kuzipata ni pamoja na kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Tanzania kuanzia mwaka 2005 mpaka Febuari 7 mwaka 2008, alipolazimika kujiuzulu baada ya madai ya kuhusishwa katika kashfa ya rushwa ya Kampuni ya Richmond, Madai ambayo bwana Lowassa aliyakanusha hadi sasa.

Katika siasa, Lowassa anafahamika kama mtu wenye misimamo mikali,kwa kile anachokiamini mwenyewe kama siasa zinazo ambatana na maamuzi magumu.

Licha ya kuwa mwanachama wa CCM kwa miaka 38, bwana Lowassa aliwashangaza wanachama wa CCM kwa uamuzi wake wa kukihama chama hicho. Hatua iliyochangiwa na yeye kutoridhrishwa na jinsi uteuzi wa wagombea urais wa kilichokuwa chama chake ulivyoendeshwa.

Alijiunga na chama cha kikuu cha upinzani cha CHADEMA. Kilichukuwa mojawapo ya vyama vinne vya upinzani vinavyounda umoja uitwao, UKAWA katika Uchaguzi wa mwaka 2015

Kufuatia uamuzi wake wa kubadili chama, Edward Lowasa amelazimika pia kubadili msimamo wake wa kisiasa na kuwa mpinzani wa chama tawala na sera aliziunga mkono na kuzitumikia awali, jambo ambalo linawatatanisha wakosoaji wake .

Hii ilikuwa mara yake ya pili kujaribu kuingia ikulu.
Kila nafsi itaonja mauti tutende mema tukiwa hai kifo ni ibada!
 
Nikiambiwa nitaje Wanasiasa BORA wa muda wote yaani pure Politicians hapa Tanzania nitawataja hawa:-

1) J.K Nyerere (R.I.P)

2) E. M. Sokoine (R.I.P)

3) Salim Ahmed Salim

4) E. N. Lowassa (R.I.P)
 

Nafsi wakati wa kifo

Kwa mujibu wa Hadith, mtu anapokufa, roho hutoka chini ya mwili kwenda juu kabla ya kuuacha mwili na macho yanakunja kama roho inaacha mwili. Kwa mujibu wa Hadith iliyopokewa na Umm Salama, amesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia kwa Abu Salamah (baada ya kufa) na macho yake yakafumbuka, akayafumba kisha akasema: 'Nafsi inapochukuliwa, macho huifuata.'” (Imeripotiwa na Swahiyh Muslim, 1528).

Nafsi baada ya kifo

Baada ya mtu kufa, roho hupelekwa mbinguni na malaika wawili na hatima yake inategemea hali yake ya uadilifu. Kwa mujibu wa Hadith ya Abu Hurayrah ambaye amesema: “Inapotwaliwa roho ya Muumini hukutana na Malaika wawili wanaoichukua…” (Msimulizi akasema: kisha akataja harufu yake nzuri na harufu ya miski). Watu wa mbinguni husema, 'Roho njema iliyotoka ardhini, Mwenyezi Mungu akubariki na mwili uliokuwa ukiishi humo. Kisha wanaipeleka kwa Mola wake Mlezi, ametakasika na kutukuzwa, kisha Anasema: Zungukai nayo mpaka mwisho wa dunia. Nafsi ya kafiri inapotoka… (msimulizi alitaja harufu yake iliyooza na laana). Watu wa mbinguni husema: Ni roho mbaya iliyotoka ardhini, kisha ikasemwa, 'Zunguka nayo mpaka mwisho wa dunia.' Abu Hurayrah akasema: kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaweka kipande cha kitambaa juu ya pua yake, hivi. (Imeripotiwa na Muslim, 5119).
Urongooo
 
Taarifa zaidi itatolewa na familia na Serikali. Poleni wote


EDWARD NGOYAI LOWASSA AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Mtoto wake Fredrick Lowassa amethibitisha

Pia, Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2008 na kuweka rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzulu.

WASIFU WA EDWARD NGOYAI LOWASSA
Edward Ngoyai Lowassa anatoka katika jamii ya Wafugaji Kaskazini mwa Tanzania. Alizaliwa August 26 mwaka 1953 katika Kijijini cha Ngarashi Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha. Edward Lowasa ni mtoto wa tatu wa Mzee Ngoyayi.

Kitaaluma Lowasa ni msomi , akiwa na shahada kwanza kutoka chuo Kikuu cha Dar es salaam na shahada ya Uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Bath huko Uingereza (1983-1984).

Uzoefu katika siasa
Ingawa baba yake alikuwa mfugaji aliwahi pia kufanya kazi kama tarishi katika serikali ya wakoloni.

Alijiunga na chama cha CCM mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka wa 1977.

Kabla ya kugombea Ubunge , aliwahi kutumikia Jeshi la Tanzania na hata kupigana katika vita kati ya Tanzania na Uganda vilivyopelekea Idd Amin kuondolewa madarakani.

Baada ya hapo alikuwa Mtumishi wa Umma kwa miaka kadhaa kabla kuteuliwa kuwa Mbunge kuwajilisha Vijana na kujiunga rasmi na siasa.

Mwaka wa 1990 alijitosa ulingoni kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la uchaguzi la Monduli.

Alifanyikiwa kwa miaka yote hii Lowassa ameendelea kulishikilia jimbo hilo la uchaguzi hadi alipolazimika kuliachia ili kuwania Urais.

Mwaka 2015 alipowania Urais haikuwa mara yake ya kwanza kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwani mwaka 1995, alikuwa miongoni mwa watangaza nia 15, hata hivyo nafasi ikachukuliwa na Benjamin William Mkapa.

Hata hivyo tofauti na matarajio ya wafuasi wake, Mwaka 2005, Lowassa hakuwania nafasi hiyo, badala yake aliunga mkono rais anayemaliza muda wake Jakaya Kikwete.

Je Lowassa amewahi kuwa nani katika nyadhifa alizozipitia Kiserikali?
Edward Ngoyayi Lowassa amewahi, kuwa Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo, Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na nafasi nyinginezo.

Lakini pia nafasi za juu alizowahi kuzipata ni pamoja na kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Tanzania kuanzia mwaka 2005 mpaka Febuari 7 mwaka 2008, alipolazimika kujiuzulu baada ya madai ya kuhusishwa katika kashfa ya rushwa ya Kampuni ya Richmond, Madai ambayo bwana Lowassa aliyakanusha hadi sasa.

Katika siasa, Lowassa anafahamika kama mtu wenye misimamo mikali,kwa kile anachokiamini mwenyewe kama siasa zinazo ambatana na maamuzi magumu.

Licha ya kuwa mwanachama wa CCM kwa miaka 38, bwana Lowassa aliwashangaza wanachama wa CCM kwa uamuzi wake wa kukihama chama hicho. Hatua iliyochangiwa na yeye kutoridhrishwa na jinsi uteuzi wa wagombea urais wa kilichokuwa chama chake ulivyoendeshwa.

Alijiunga na chama cha kikuu cha upinzani cha CHADEMA. Kilichukuwa mojawapo ya vyama vinne vya upinzani vinavyounda umoja uitwao, UKAWA katika Uchaguzi wa mwaka 2015

Kufuatia uamuzi wake wa kubadili chama, Edward Lowasa amelazimika pia kubadili msimamo wake wa kisiasa na kuwa mpinzani wa chama tawala na sera aliziunga mkono na kuzitumikia awali, jambo ambalo linawatatanisha wakosoaji wake .

Hii ilikuwa mara yake ya pili kujaribu kuingia ikulu.
Tangu augue, chadema hawajawahi kwenda kumsalimia
 
Taarifa zaidi itatolewa na familia na Serikali. Poleni wote


EDWARD NGOYAI LOWASSA AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Mtoto wake Fredrick Lowassa amethibitisha

Pia, Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2008 na kuweka rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzulu.

WASIFU WA EDWARD NGOYAI LOWASSA
Edward Ngoyai Lowassa anatoka katika jamii ya Wafugaji Kaskazini mwa Tanzania. Alizaliwa August 26 mwaka 1953 katika Kijijini cha Ngarashi Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha. Edward Lowasa ni mtoto wa tatu wa Mzee Ngoyayi.

Kitaaluma Lowasa ni msomi , akiwa na shahada kwanza kutoka chuo Kikuu cha Dar es salaam na shahada ya Uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Bath huko Uingereza (1983-1984).

Uzoefu katika siasa
Ingawa baba yake alikuwa mfugaji aliwahi pia kufanya kazi kama tarishi katika serikali ya wakoloni.

Alijiunga na chama cha CCM mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka wa 1977.

Kabla ya kugombea Ubunge , aliwahi kutumikia Jeshi la Tanzania na hata kupigana katika vita kati ya Tanzania na Uganda vilivyopelekea Idd Amin kuondolewa madarakani.

Baada ya hapo alikuwa Mtumishi wa Umma kwa miaka kadhaa kabla kuteuliwa kuwa Mbunge kuwajilisha Vijana na kujiunga rasmi na siasa.

Mwaka wa 1990 alijitosa ulingoni kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la uchaguzi la Monduli.

Alifanyikiwa kwa miaka yote hii Lowassa ameendelea kulishikilia jimbo hilo la uchaguzi hadi alipolazimika kuliachia ili kuwania Urais.

Mwaka 2015 alipowania Urais haikuwa mara yake ya kwanza kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwani mwaka 1995, alikuwa miongoni mwa watangaza nia 15, hata hivyo nafasi ikachukuliwa na Benjamin William Mkapa.

Hata hivyo tofauti na matarajio ya wafuasi wake, Mwaka 2005, Lowassa hakuwania nafasi hiyo, badala yake aliunga mkono rais anayemaliza muda wake Jakaya Kikwete.

Je Lowassa amewahi kuwa nani katika nyadhifa alizozipitia Kiserikali?
Edward Ngoyayi Lowassa amewahi, kuwa Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo, Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na nafasi nyinginezo.

Lakini pia nafasi za juu alizowahi kuzipata ni pamoja na kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Tanzania kuanzia mwaka 2005 mpaka Febuari 7 mwaka 2008, alipolazimika kujiuzulu baada ya madai ya kuhusishwa katika kashfa ya rushwa ya Kampuni ya Richmond, Madai ambayo bwana Lowassa aliyakanusha hadi sasa.

Katika siasa, Lowassa anafahamika kama mtu wenye misimamo mikali,kwa kile anachokiamini mwenyewe kama siasa zinazo ambatana na maamuzi magumu.

Licha ya kuwa mwanachama wa CCM kwa miaka 38, bwana Lowassa aliwashangaza wanachama wa CCM kwa uamuzi wake wa kukihama chama hicho. Hatua iliyochangiwa na yeye kutoridhrishwa na jinsi uteuzi wa wagombea urais wa kilichokuwa chama chake ulivyoendeshwa.

Alijiunga na chama cha kikuu cha upinzani cha CHADEMA. Kilichukuwa mojawapo ya vyama vinne vya upinzani vinavyounda umoja uitwao, UKAWA katika Uchaguzi wa mwaka 2015

Kufuatia uamuzi wake wa kubadili chama, Edward Lowasa amelazimika pia kubadili msimamo wake wa kisiasa na kuwa mpinzani wa chama tawala na sera aliziunga mkono na kuzitumikia awali, jambo ambalo linawatatanisha wakosoaji wake .

Hii ilikuwa mara yake ya pili kujaribu kuingia ikulu.
Very sad .
Apumzike kwa Amani.
 
Nenda kwa amani Mzee Edward Lowassa lakini pole kwa familia ila Mungu awatie nguvu wakati huu mgumu.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe.
 
Acha urongo. Tatizo la maji Chalinze lilimalizwa na JK Kwa kushirikiana na Wachina. Maana walikua jamaa anaenda kuukwaa ukuu wakafanya jambo
Hata kama una chuki na Lowassa lakini jaribu kuipunguza kidogo.

Wakati mradi wa maji wa mto Wami unajengwa Waziri wa maji alikuwa mh Edward Lowassa na mh Kikwete alikuwa Waziri wa mambo ya nje chini ya uongozi wa mh Benjamin Mkapa.

Hata kama mradi huo umefadhiliwa na wachina lakini kulikuwa na msaada wa aliyekuwa Waziri wake ambaye ni Lowassa.
Hata siku ya uzinduzi wa mradi huo marehemu mzee Mkapa aliwamwagia sifa kemkem askari wake wa miavuli hao wawili mh Lowassa na mh Kikwete.
 
Back
Top Bottom