Egypt: Hii siyo sawa kuwafanyia ndugu zenu. Kuna nini Kinaendelea hapa?

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Nimeshangaa Egypt haitaki kabisa kuwa msaada kwa wanaGaza ili wapate mapumziko.

Unaona huu ukuta. Unaweza sema Trump katili sana kajenga huu ukuta kuzuia wapalestine wasiingie USA.

Unakuja kuambiwa ni ndugu wa Damu. Hakuna anayewataka Wapalestine. Sijui kwa nini. Huu mpaka wa Egypt na Gaza
 
Siasa zimeingia kati .. Muslim Brotherhood ni chama pinzani ambapo serikali ya Egypt inakichukulia kama chama cha kigaidi .. Muslims brotherhood Wana uhusiano wa karibu mno na Hamas ..hadi Idiology .. watu wa Ghaza walichagua hamas kwa kura nyingi mno kutawala Ghaza .. Huo ukuta ni product za Siasa za Kidunia na wamesahau Dini .. kwani mbele ya Allah hautaulizwa chama chako cha kisiasa bali dini yako ..
 
Kwao ni Gaza sio Egypty, hakuna atakae kubali watu wafukuzwe kwao , watabaki hapo hapo Gaza
 
Kwanini waende Egypt haliyakua kwao ni Gaza?. Na waunga mkono Misri au nchi yeyote nyingine kulazimisha wabaki gaza wakipigania aridhi yao.
Ardhi ya Wayahudi hiyo, hii vita tunayoishuhudia sasa hivi ya Wapalestina kuuwa iliwahi kutokea enzi za giza ambapo wafuasi wa Muhammad waliua watu Middle East kwa kuwalazimisha wawe Waislam. Ni Wayahudi pekee waligoma kubadili imani na kukimbilia nchi zingine duniani, mwaka 1948 waliamuq kurudi kwao
 
Hujui historia wewe. Kasoma Historia ya Ibrahim kutoka MESOPOTAMIA kuja Caanan ambayo ni Gaza ya sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…