Elimu ilifia Chuo Kikuu au ilizikwa chuo kikuu?

Elimu ilifia Chuo Kikuu au ilizikwa chuo kikuu?

Unategemea mijadala yenye tija kutoka UVccm? Utangoja sana.
Ccm ina strategy ya kuwapumbaza vijana kwa kuwakoleza na muziki na mpira wa miguu ili wapumbae hivyo kuwatumia kirahisi kuendelea kutawala!!
Mbinu kama hizo Wabeligiji walizitumia huko Congo kwa kuwapumbaza wananchi kwa muziki na starehe huku wao wakichota maliasili za nchi.
Bila majadiliano nitajua unawaza nini. Ni mpumbavu tu ndiye anayeweza kukebehe majadiliano na midahalo
 
ELIMU ILIFIA CHUO KIKUU au ILIZIKWA CHUO KIKUU?
Imeandikwa na ASKOFU BAGONZA


Mzee Jenerali Ulimwengu kasema vyuo vikuu vyetu ni kama Extended High School. Anayebishi anitafute. Sababu ni nyingi kama idadi ya wajinga wetu waliosoma vyuo vikuu.

1. Tulipokuwa na Chuo Kikuu kimoja, tulifuta ujinga kwa asilimia 85. Sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50, tuna wajinga wengi mitaani na maofisini kuliko enzi ya chuo kikuu kimoja.

2. Vyuo vilitengeneza wanasiasa na viongozi makini. Waliposhika madaraka wakapiga marufuku mijadala ya kisiasa na kijamii katika vyuo vikuu.

3. Wakati ule wanafunzi wa vyuo vikuu waliwahoji watawala, siku hizi watawala wanawahoji wanafunzi wa vyuo vikuu.

4. Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.

5. Kuna tofauti ndogo inayotenganisha uchawa na ujinga. Wote wanazalishwa katika vyuo vikuu. Mmoja anaishi ofisini na mwingine anaishi mitaani akiunga mkono asiyoyajua.

6. Elimu ya wakati ule ilichochea uasi mtakatifu (holy rebellion). Hii ya sasa inachochea woga na utii usiomnufaisha anayetii.

Nini kilitokea?

Waliohitimu chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia shule za msingi. Vyuo vikuu vikageuka kuwa mhanga wa mafanikio yake. Kwa hiyo elimu ilifia chuo kikuu na kuzikwa chuo kikuu.Shule za Msingi na sekondari ni vitalu vya uzalishaji unaoenda kukuzwa chuo kikuu.

View attachment 2822820
Hao Wazee ni wahafidhina tu. Badala ya kujadili kuboreshwa taaluma vyuo vikuu, wanataka mijadala ya kisiasa vyuo vikuu. Waache uhafidhina. Kila zama na kitabu chake. Hata kwa nchi zinazotuzunguka hakuna mijadala ya kisiasa vyuo vikuu. Tupambane kuboresha taaluma tupate wataalamu na siyo kuwaweka vijana wadogo wa vyuo vikuu katika ubusy wa kujadili siasa. Huko vyuo kuna nafasi ya mtu kujiunga na matawi ya vyama vya siasa. Hizo zibaki kama forums za yeyote kusema.
 
ndio maana waswahili husema ujana maji ya moto. Utumie vizuri kuepuka majuto na maumivu moyoni baadae.

Mzee ana mawazo mazuri sana. Lakini pia kama haridhiki na mawazo na uwezo wa kujieleza na kuhoji wa vijana wanaohitimu vyuo vikuu kwasababu hakuna mijadala hilo ni tatizo lake binafsi. Lakini vijana wa sasa wana ujuzi, umahiri na uwezo mkubwa sana wa kujieleza na kuhoji mambo.

Na mimi binafsi na mpa pole sana generali kama jambo hilo linamkwaza. Mambo yanabadilika wakati wake uliisha, awape fursa vijana wajiandalie kesho yao kulingana na mazingira yao yaliopo.

Vijana wanaohitimu vyuo vikuu mbalimbali nchini. Wanaohitimu na kutoka na maarifa, ujuzi na umahiri mkubwa sana wa kadre mbalimbali na wanasonga mbele kwa furaha na mikogo kama yote ama hamuhudhuriagi graduations, wameridhika na kwakweli inaridhisha na kutia moyo sana.

Babu jenerali tunampenda na tunamuheshimu sana. Anajaribu kufundisha na kuichochea jamii ya hususani ya wasomi ujasiri wa kubeza kama ilivyo hulka yake. Umri wake umesonga kidogo ni vigumu vijana kumuunga mkono kwenye pendekezo lake. Nashukuru vijana na wasomi makini wamekua wakimpuuzia kisomi zaidi ,Mzee wetu huyu ambae tunaempenda sana asijiskie vibaya, na kwakweli wamefanikiwa pakubwa na mambo yanasonga vizuri...

Mawazo yake mazuri ikiwa yanafaa basi atathiminiwe na yatekelezwe na vyuo husika kwa wakati wana ona unafaa na kama jambo lenyewe linamanufaa.

Ana uhuru wa kutoa maoni, kukosoa, kupendekeza mambo yawe vipi ili tusonge mbele kama Taifa, ila nia yake ya ndani inafahamika vizur sana muda mrefu. Na kwahivyo hasira na ghadhabu ndani ya maoni mazuri sana ya generali ulimwengu vinafahamika sio jambo geni humu nchini.

Maoni yangu kwenye pendekezo na na maoni juu ya mijadala.

Mijadala mbalimbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi iendeshwe na vyama vya kisiasa, kupitia jumuiya zake mathalani jumuiya za vijana, wanawake, wazazi, chipukizi n.k ili kuwajengea vijana uwezo wa kujieleza na kuhoji, ikiwa hilo ndio tatizo kama anavyodai Mzee general ulimwengu.

Platforms za mijadala ni nyingi mno si vyuo vikuu tu.

Kwako Tindo
Aiseee. Another foolish of the making of Lucas mwashambwa in the JF wilderness. So sad.
 
Bila majadiliano nitajua unawaza nini. Ni mpumbavu tu ndiye anayeweza kukebehe majadiliano na midahalo
Nyie chawa akili zenu zimeshikiliwa na mabwana zenu hamuwezi kuwa na mijadala yenye tija.
Ndio maana viongozi wenu wanashinda JF kuchota busara za wenye akili huku nyie chawa mnalabishwa asali!
 
Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.
Enzi za kina Dr Bashiru na Kina Prof Mkumbo.
Lakini leo akina Bashiru na Mkumbo wanafunga watu wanaohoji na kukosoa.

Kweli elimu ilifia huko.
 
Unategemea mijadala yenye tija kutoka UVccm? Utangoja sana.
Ccm ina strategy ya kuwapumbaza vijana kwa kuwakoleza na muziki na mpira wa miguu ili wapumbae hivyo kuwatumia kirahisi kuendelea kutawala!!
Mbinu kama hizo Wabeligiji walizitumia huko Congo kwa kuwapumbaza wananchi kwa muziki na starehe huku wao wakichota maliasili za nchi.
Miziki ya kina mondi ya Tema mate iteleze Pangoni na Kulamba Mitaroni.......ccm wanafundishana ushoga tupu
 
Hao Wazee ni wahafidhina tu. Badala ya kujadili kuboreshwa taaluma vyuo vikuu, wanataka mijadala ya kisiasa vyuo vikuu. Waache uhafidhina. Kila zama na kitabu chake. Hata kwa nchi zinazotuzunguka hakuna mijadala ya kisiasa vyuo vikuu. Tupambane kuboresha taaluma tupate wataalamu na siyo kuwaweka vijana wadogo wa vyuo vikuu katika ubusy wa kujadili siasa. Huko vyuo kuna nafasi ya mtu kujiunga na matawi ya vyama vya siasa. Hizo zibaki kama forums za yeyote kusema.
lakini sasa Mzee wetu huyu ambae kwakeli tunakapenda sana na tunamuheshimu sana ila sasa siasa imemchakaza sana phyisically and mentally na hatuna namna tutasonga nae tu pole pole...

Huko kwenye vyama ni platform pia vijana waanzishe mijadala iwasaidie kuongeza huo uwezo wa kujieleza na kuhoji anaodai Mzee wetu ati wahitimu wa vyuo vikuu hawana...

Mbona rahisi tu
 
Bila majadiliano nitajua unawaza nini. Ni mpumbavu tu ndiye anayeweza kukebehe majadiliano na midahalo
mkajadiliane kwenye vyama vyenu huko ni platform nzuri ya majadiliano na midahalo
 
Ofcourse there is no doubt that fools now prevail all over the country. That's mere truth. Tukubaliane tu na Askofu Bagonza.
if you don't want to take part in political administration don't blame to be ruled by a fool...

jamii imeathirika na siasa za mihemko na kuzira. Ujasiri wa kudhihaki na saa zingine kutukana na kubeza, haitasaidia.

Wazoefu katika siasa ndio wanasonga mbele zaid kujiimarisha kwenye nafasi zao, kijizatiti na kukita mizizi zaidi ili wasimame imara zaid na kutawala vizur zaidi....
 
Sahihi ni vyuo vya kuzalisha majambazi dhidi ya wananchi waliowasomesha.Elimu Yao imetufanya maskini zaidi ya miaka 60 ya uhuru.
 
Unategemea mijadala yenye tija kutoka UVccm? Utangoja sana.
Ccm ina strategy ya kuwapumbaza vijana kwa kuwakoleza na muziki na mpira wa miguu ili wapumbae hivyo kuwatumia kirahisi kuendelea kutawala!!
Mbinu kama hizo Wabeligiji walizitumia huko Congo kwa kuwapumbaza wananchi kwa muziki na starehe huku wao wakichota maliasili za nchi.
kama hakutakua na mijadala yenye tija CCM, bila shaka ya Bavicha au ngoma ya vija ACT inaweza kua na tija. Na hiyo ni kama ambavyo mijadala ya udsm na mzumbe haiwezi kuwa sawa na huwezi kusema ya huko ina tija ya kule hakuna, unless umeathirika spiritually na saikolojikali na siasa za vyama.

Hizo mbinu za vyama kuwafunda vijana ndizo zinazofanya vyama kutawala na kijizatiti zaidi mamlakani kwa uhakika zaidi. Itategemea uelewa
 
Ndio hao wajuu wake anawalea kwa kuwaambia wajirekebishe badala ya kujipendekeza kwa watawala.
hawaambii anawabeza kwa kebehi na madharau wao, walezi na wazazi wao.

Wajukuu waerevu wamechanuka, wako rada, wamestukia janja janja ya Babu
 
Ni nani aliyehalalisha na kuhimiza matumizi ya vitini (handouts) badala ya vitabu vyuoni?! Ni mwanafunzi au utawala?! Utawala wa Chuo usiohimiza wanafunzi kutumia vitabu kama rejea, mwanafunzi atapata wapi guts ya kutafuta maarifa nje ya vitini ambapo ndo mitihani inatokea humohumo? Tatizo ni kubwa, siyo kama ulivyoshauri hapo juu.
Hiyo Elimu ya Tz inahitaji kuijiongeza hata hao waliosoma zamani walikuwa wanajisomea vitabu kutoka Sehemu na sio kutegemea maarifa ya mwalimu tu.
 
Katika majadiliano jadidi huwa ndio chanzo cha kujenga hoja zenye ubunifu ndani yake. Lakini bila kujua unawaza nini ni vigumu kupata views zako. Hivyo basi tutafute jukwaa la vijana lenye maona endelevu kama wewe tujenge nchi yetu
Je huoni huyu mwanzilisha wa jf kafanya la maana kuanzia hili jukwaa na anafaa kupewa pongezi, huu ndio usomi ndio maana mwanzilisha wa Facebook alipata Phd kutokana na ubunifu zake.

Yule mzee ni educational ego han cha maana na hana mchango zaidi ya lopo lopo ....Kila siku kuona wenzie wajinga ila hana cha maana amefanya na elimu ya kizamani.
 
Sasa huyu anamlaumu nan ? Huyu ana point ila tatizo ni yeye na kama vile hajielewi ,tatizo lingine ana kitu kama educational ego ambayo haina maana.

Mijadala ya kisiasa ndio imekaa kichwani mwake ila hatambui katika nchi zetu sio mahali pake na ndio chanzo cha kupata viongozi wabovu...

Ukisoma hao maprofessor wengi kama yeye wamesoma elimu ya zamanu ila hakuna kitu wamefanya zaid kufanya kazi nje ya nchi...

Kama yeye na kundi la generation yake wameshindwa mpaka leo especially mtu kama Nyerere alishindwa kabisa na sera zake za kucopy na kupaste.

The man is full doubts but no single solution ...Moja kati ya wasomi wa hovyo kutokea ni hyu mzee hana cha maana wao na elimu yao wa ukoloni ndio walishinwa kuleta ukombozi ,kizazi chao za maprofessor hawana jipya na wamesoma hiyo elimu mjadala.

Badala mtu na akili zake akae chini aeleze mambo ya ubunifu ,kichwa kimejaa siasa mpaka mtu kazeeka ,kuna nchi wa hawana hizi mambo hata za kukosoa nenda Russia ,china, Korea ,iran still wapo far kiuchumi ...Instead watu wawe bussy kweny innovation yeye akili yake ni siasa tu ndio chanzo cha wezi.

Nchi zinazofanya mijadala kwa sasa kama USA wale wana haki ya kuwa na milumbano ya kisiasa kwa vile walishakuwa njema kweny uchumi miaka kiboo watu walishajikomboa tangu mwaka 1776..

Tanzania ijikomboe kwanza kweny uchumi ndio mje kweny siasa.
Inasikitisha na kushangazq kuwa ,licha ya kujifanyq unajua ,huelewi maana na umuhimu wa Siasa kwa Nchi!
 
Ni nani aliyehalalisha na kuhimiza matumizi ya vitini (handouts) badala ya vitabu vyuoni?! Ni mwanafunzi au utawala?! Utawala wa Chuo usiohimiza wanafunzi kutumia vitabu kama rejea, mwanafunzi atapata wapi guts ya kutafuta maarifa nje ya vitini ambapo ndo mitihani inatokea humohumo? Tatizo ni kubwa, siyo kama ulivyoshauri hapo juu.
😂😂Hapo umewashika ni hao hao maprofessor na wapiga dili ,sisi ilikuwa ukitaka kitini nenda stationary fulani hapo tunajaaa watu nyomi.

Hao waliopata elimu mwanzo mmoja wapo ndio huyo Ulimwengu wao ndio wameharibu elimu kwa tamaa zao ,kwa vile hawana uwezo zaidi ya kujua kingereza.

Zile handouts ukisoma sana unafaulu kwa alama za juu ila hamna kitu utafnya ukija kweny uhalisia mambo ni mengi.
 
Inasikitisha na kushangazq kuwa ,licha ya kujifanyq unajua ,huelewi maana na umuhimu wa Siasa kwa Nchi!
Kila mwanasiasa ni tapeli , nakuonea huruma dogo bado hujajitambua utakufa maskini kwa uchawa wa siasa...
 
Back
Top Bottom