Elimu ilifia Chuo Kikuu au ilizikwa chuo kikuu?

Elimu ilifia Chuo Kikuu au ilizikwa chuo kikuu?

Inasikitisha sana.
Waambie Bagonza na Jenerali Ulimwengu kwamba wao ni mfano mzuri wa waliyoyaandika. Kwamba baada ya kumaliza chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia ya msingi na kuendelea kama wanavyodai kwani wao walimaliza mapema. Ikitokea kuwajibishwa wao ndio wa kwanza. Mkumbushe Jenerali Ulimwengu kwamba Joseph Sinde Warioba na yeye walipigwa/walichapwa bakora Ikulu na mwalimu Nyerere kwa kauli kama hizo, hivyo asisahau.
 
😂😂Hapo umewashika ni hao hao maprofessor na wapiga dili ,sisi ilikuwa ukitaka kitini nenda stationary fulani hapo tunajaaa watu nyomi.

Hao waliopata elimu mwanzo mmoja wapo ndio huyo Ulimwengu wao ndio wameharibu elimu kwa tamaa zao ,kwa vile hawana uwezo zaidi ya kujua kingereza.

Zile handouts ukisoma sana unafaulu kwa alama za juu ila hamna kitu utafnya ukija kweny uhalisia mambo ni mengi.
Sahihi kabisa
 
Hiyo Elimu ya Tz inahitaji kuijiongeza hata hao waliosoma zamani walikuwa wanajisomea vitabu kutoka Sehemu na sio kutegemea maarifa ya mwalimu tu.
Upo sahihi, mimi siku nikisikia vitini vimepigwa marufuku vyuoni kote nchini nitafurahi sana. Hiyo italazimisha wanafunzi kutafuta rejea hasa kupitia Google scholars, Amazon, etc etc
 
Tusiilaumu elimu bali tukubali tuna kizazi cha vijana wavivu, hawapendi kujiwajibisha iwe kutafuta maarifa hadi kufanya majukumu yao.

Mfano, unakuta kijana na digrii, ana smartphone ana bando hana kazi rasmi na bado hajui na wala hajishughulishi kutafuta kazi mtandaoni au kuongeza maarifa kupitia kurasa za mitandaoni.

Unakuta kijana mwenye digrii na bado hajui namna ya kutumia Microsoft word, akiambiwa aandike barua ya kuomba kazi anaomba kuandikiwa.

Mwisho kabisa, ni kawaida sana kukuta kijana wa chu na hata aliyemaliza chuo kikuu hajawahi kusoma kitabu chochote cha maarifa tangu ajue kisoma na kuandika. Yeye ni kusoma vitabu vya masomo tu ya shule na chuo akienda mbali atasoma biblia au quran
 
hawaambii anawabeza kwa kebehi na madharau wao, walezi na wazazi wao.

Wajukuu waerevu wamechanuka, wako rada, wamestukia janja janja ya Babu
Hamna Cha werevu, Bali wamepata ulemavu wa woga. Tunaona kinachofanyika huko vyuoni toka kwa watawala wanaolazimisha kupandikiza woga na nidhamu za kinafiki. Hayo ni baadhi ya madhara ya chama kulazimisha kubaki madarakani kwa shuruti, ni lazima waue uwezo wa wanafunzi kujieleza kwa uhuru.

Sioni shida ww ukipinga asemacho huyo mzee, maana ww ni zao la walemavu asemao huyo mzee kutoka kwenye elimu yetu. Inshort ww ni muhanga wa ukweli wa huyo mzee.
 
Waambie Bagonza na Jenerali Ulimwengu kwamba wao ni mfano mzuri wa waliyoyaandika. Kwamba baada ya kumaliza chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia ya msingi na kuendelea kama wanavyodai kwani wao walimaliza mapema. Ikitokea kuwajibishwa wao ndio wa kwanza. Mkumbushe Jenerali Ulimwengu kwamba Joseph Sinde Warioba na yeye walipigwa/walichapwa bakora Ikulu na mwalimu Nyerere kwa kauli kama hizo, hivyo asisahau.
Ni wapi Askofu Bagonza na Jenerali ulimwengu wamewahi kuwa policy makers Wa nchi hii?! Angalau Jenerali nasikia aliwahi kuwa Mbunge, lakini siyo Bagonza. Kwa hiyo hizo lawama zako haiwahusu.
 
ELIMU ILIFIA CHUO KIKUU au ILIZIKWA CHUO KIKUU?
Imeandikwa na ASKOFU BAGONZA


Mzee Jenerali Ulimwengu kasema vyuo vikuu vyetu ni kama Extended High School. Anayebishi anitafute. Sababu ni nyingi kama idadi ya wajinga wetu waliosoma vyuo vikuu.

1. Tulipokuwa na Chuo Kikuu kimoja, tulifuta ujinga kwa asilimia 85. Sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50, tuna wajinga wengi mitaani na maofisini kuliko enzi ya chuo kikuu kimoja.

2. Vyuo vilitengeneza wanasiasa na viongozi makini. Waliposhika madaraka wakapiga marufuku mijadala ya kisiasa na kijamii katika vyuo vikuu.

3. Wakati ule wanafunzi wa vyuo vikuu waliwahoji watawala, siku hizi watawala wanawahoji wanafunzi wa vyuo vikuu.

4. Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.

5. Kuna tofauti ndogo inayotenganisha uchawa na ujinga. Wote wanazalishwa katika vyuo vikuu. Mmoja anaishi ofisini na mwingine anaishi mitaani akiunga mkono asiyoyajua.

6. Elimu ya wakati ule ilichochea uasi mtakatifu (holy rebellion). Hii ya sasa inachochea woga na utii usiomnufaisha anayetii.

Nini kilitokea?

Waliohitimu chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia shule za msingi. Vyuo vikuu vikageuka kuwa mhanga wa mafanikio yake. Kwa hiyo elimu ilifia chuo kikuu na kuzikwa chuo kikuu.Shule za Msingi na sekondari ni vitalu vya uzalishaji unaoenda kukuzwa chuo kikuu.

View attachment 2822820
Kadri vyuo vikuu/nchi inavyozalisha wajinga/machawa ndivyo ccm wanashangilia maana kudumu kwao madarakani kunakuwa na uhakika. Uzalishaji wa machawa/wajinga ni mkakati wa muda mrefu wa ccm ili waendelee kutawala.

Hii nchi lazima tutafute ukombozi mara ya pili kwa kuing'oa ccm, maana hata ile hatua kidogo ya kujitambua tuliyokuwa tumeifikia ccm wamefanya kila mbinu kuirudisha nyuma
 
Hata wewe Elimu yako ni muhimu hapa jukwaani maana unaadika logic
Je huoni huyu mwanzilisha wa jf kafanya la maana kuanzia hili jukwaa na anafaa kupewa pongezi, huu ndio usomi ndio maana mwanzilisha wa Facebook alipata Phd kutokana na ubunifu zake.

Yule mzee ni educational ego han cha maana na hana mchango zaidi ya lopo lopo ....Kila siku kuona wenzie wajinga ila hana cha maana amefanya na elimu ya kizamani.
 
Hamna Cha werevu, Bali wamepata ulemavu wa woga. Tunaona kinachofanyika huko vyuoni toka kwa watawala wanaolazimisha kupandikiza woga na nidhamu za kinafiki. Hayo ni baadhi ya madhara ya chama kulazimisha kubaki madarakani kwa shuruti, ni lazima waue uwezo wa wanafunzi kujieleza kwa uhuru.

Sioni shida ww ukipinga asemacho huyo mzee, maana ww ni zao la walemavu asemao huyo mzee kutoka kwenye elimu yetu. Inshort ww ni muhanga wa ukweli wa huyo mzee.
usijiskie vibaya kukosa kuungwa mkono kwa ushawishi wa hoja zako au upande wako. Acha watu wawe huru, na haina haja kumbeza alie na wazo tofauti na lako na kuanza kusingizia vitu hata visivyo na maana.

Hoa vijana wasomi wa vyuo unaowaita waoga, wahanga, walemavu na waoga wenye nidhamu za kinafiki nikuhakikishie wako chonjo, wako makini na wako rada mbaya sana. Wanajitambua vizuri sana. Hawawezi kuwa driven mathalani kwa hoja kama zako Tindo, coz its full of mihemko na negativity. Hayupo wa kujisumbua kuambatana na wewe. Vijana hawa wataendelea kuunga mkono upande ambao akuna kejeli wala mabezo.

Na uzuri ni kwamba vijana hawa wametulia tuli, mentally na saikolojikali, hawana papara wala hawabughudhiwi na dhihaka,dharau na mihemko yenu wanasonga mbele vizuri sana na kuwaunga mkono wale wanowaskiliza na kuwaelekeza kwa heshima, utu, upendo na ungwana.

Nyie kuna engo wanawasubiria tu ili wawaadhibu na kuwanyorosha vizuri sana mpaka mseme yote, mtukane matusi yote na mihemko yote iwatoke ili hatimae akili ziwakae sawa na muwe na heshima, utu na nidhamu kwa wasio waunga mkono.
 
Kadri vyuo vikuu/nchi inavyozalisha wajinga/machawa ndivyo ccm wanashangilia maana kudumu kwao madarakani kunakuwa na uhakika. Uzalishaji wa machawa/wajinga ni mkakati wa muda mrefu wa ccm ili waendelee kutawala.

Hii nchi lazima tutafute ukombozi mara ya pili kwa kuing'oa ccm, maana hata ile hatua kidogo ya kujitambua tuliyokuwa tumeifikia ccm wamefanya kila mbinu kuirudisha nyuma
🤣umepanic Kinyungu relax bana

the impact ya CCM into you, saikolojikali na spiritually inaelekea kukufanya hata ukijikwaa barabarani pekeyako utasema ni CCM wamesababisha ujikwae
 
🤣umepanic Kinyungu relax bana

the impact ya CCM into you, saikolojikali na spiritually inaelekea kukufanya hata ukijikwaa barabarani pekeyako utasema ni CCM wamesababisha ujikwae
Mkuu hakuna anayefaidia na ujinga wa watz zaidi ya ccm.

Ukitaka kujua angalia watu waliokuwa timamu kabisa kama Kitila, Kabudi, walipoingia ccm wamekuwaje? Wamekana hadi vitu vya msingi kabisa walivyokuwa wakipigania.
Haishangazi Ulimwengu anasema vyuo vikuu vimekuwa sawa na extension ya form six. Unajua kwa nini? Ni kwa sababu kwenye vyuo vyetu hautakiwi kupingana na mawazo ya serikali, ya chama na hata ya walimu wako. Wamekuwa kama wanazalisha mazombie
 
Mkuu hakuna anayefaidia na ujinga wa watz zaidi ya ccm.

Ukitaka kujua angalia watu waliokuwa timamu kabisa kama Kitila, Kabudi, walipoingia ccm wamekuwaje? Wamekana hadi vitu vya msingi kabisa walivyokuwa wakipigania.
Haishangazi Ulimwengu anasema vyuo vikuu vimekuwa sawa na extension ya form six. Unajua kwa nini? Ni kwa sababu kwenye vyuo vyetu hautakiwi kupingana na mawazo ya serikali, ya chama na hata ya walimu wako. Wamekuwa kama wanazalisha mazombie
kwahiyo akina kitila wamekuacha unalalama tu bila kuchukua hata hatua?
sasa utafika kweli unapostahili?

wewe ni Chadema au?

naona unailaumu sana CCM na husemi hao unaowabeza na kuwaita mazombie wakufuate wapi na watanufaika na nini wakiwa upande wako angalau utakua umewasaidia kwa kiasi...

Lakini kuilaumu ccm na kuwadharau wanaoiunga mkono hakusaidii na wala haimvutii yeyeote kukuona wewe ni wa maana zaid ya kukushangaa tu....

Show the way kiungwana na kuhakikisha utapata watakao kuunga mkono
 
usijiskie vibaya kukosa kuungwa mkono kwa ushawishi wa hoja zako au upande wako. Acha watu wawe huru, na haina haja kumbeza alie na wazo tofauti na lako na kuanza kusingizia vitu hata visivyo na maana.

Hoa vijana wasomi wa vyuo unaowaita waoga, wahanga, walemavu na waoga wenye nidhamu za kinafiki nikuhakikishie wako chonjo, wako makini na wako rada mbaya sana. Wanajitambua vizuri sana. Hawawezi kuwa driven mathalani kwa hoja kama zako Tindo, coz its full of mihemko na negativity. Hayupo wa kujisumbua kuambatana na wewe. Vijana hawa wataendelea kuunga mkono upande ambao akuna kejeli wala mabezo.

Na uzuri ni kwamba vijana hawa wametulia tuli, mentally na saikolojikali, hawana papara wala hawabughudhiwi na dhihaka,dharau na mihemko yenu wanasonga mbele vizuri sana na kuwaunga mkono wale wanowaskiliza na kuwaelekeza kwa heshima, utu, upendo na ungwana.

Nyie kuna engo wanawasubiria tu ili wawaadhibu na kuwanyorosha vizuri sana mpaka mseme yote, mtukane matusi yote na mihemko yote iwatoke ili hatimae akili ziwakae sawa na muwe na heshima, utu na nidhamu kwa wasio waunga mkono.
Wala sihitaji kuungwa mkono na watu ambao tayari ni zao la elimu ya woga, na Sasa uchawa. Nimeunga mkono ukweli wa Ulimwengu. Na Sina sababu ya kuacha kuunga mkono ukweli huo wakati dhahiri naliona tatizo.

Hakuna kijana utasema Yuko chonjo kwenye mazingira ambayo tayari mfumo umeshaundwa kuaccomodate waoga, na akitokea yoyate anayetaka kuhoji mazingira hayo ni lazima apoteze nafasi yake ya masomo. Yaani mfumo wetu wa elimu huko vyuoni ni rafiki kwa wasio na uwezo wa kuhoji mambo ya msingi. Ili uwe salama kwenye elimu yako ni lazima kuwa kondoo. Na ukondoo kwenu chawa ni dalili ya utulivu na uelewa.

Wanasubiri watuadhibu wapi boss, kungekuwa na mazingira ya kweli ya kuadhibiana ungeona matokeo ambayo ingekuwa fedheha kwenu vibaraka wa watawala, na mnaoawasujudu. Sio ule upuuzi ambao vyombo vya Dola vinaona fahari kutumika kulinda mabox ya kura za wizi.
 
Aulize waliokuwa mstari wa mbele walianbulia nini,hata yeye mwenyewe aliishia wapi,all in all lazma mtu ajali maslahi yake kwanza hayo mengine ni ziada tu.
 
ELIMU ILIFIA CHUO KIKUU au ILIZIKWA CHUO KIKUU?
Imeandikwa na ASKOFU BAGONZA


Mzee Jenerali Ulimwengu kasema vyuo vikuu vyetu ni kama Extended High School. Anayebishi anitafute. Sababu ni nyingi kama idadi ya wajinga wetu waliosoma vyuo vikuu.

1. Tulipokuwa na Chuo Kikuu kimoja, tulifuta ujinga kwa asilimia 85. Sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50, tuna wajinga wengi mitaani na maofisini kuliko enzi ya chuo kikuu kimoja.

2. Vyuo vilitengeneza wanasiasa na viongozi makini. Waliposhika madaraka wakapiga marufuku mijadala ya kisiasa na kijamii katika vyuo vikuu.

3. Wakati ule wanafunzi wa vyuo vikuu waliwahoji watawala, siku hizi watawala wanawahoji wanafunzi wa vyuo vikuu.

4. Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.

5. Kuna tofauti ndogo inayotenganisha uchawa na ujinga. Wote wanazalishwa katika vyuo vikuu. Mmoja anaishi ofisini na mwingine anaishi mitaani akiunga mkono asiyoyajua.

6. Elimu ya wakati ule ilichochea uasi mtakatifu (holy rebellion). Hii ya sasa inachochea woga na utii usiomnufaisha anayetii.

Nini kilitokea?

Waliohitimu chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia shule za msingi. Vyuo vikuu vikageuka kuwa mhanga wa mafanikio yake. Kwa hiyo elimu ilifia chuo kikuu na kuzikwa chuo kikuu.Shule za Msingi na sekondari ni vitalu vya uzalishaji unaoenda kukuzwa chuo kikuu.

View attachment 2822820
Sasa Hv kuna vitabu vya kijinga vitupu vimetamalaki hakuna maarifa tena na ni kweli vyuo vikuu vinasikitisha sana,Taifa linakoelekea Sijui tuombe MUNGU atunusuru.
 
Wala sihitaji kuungwa mkono na watu ambao tayari ni zao la elimu ya woga, na Sasa uchawa. Nimeunga mkono ukweli wa Ulimwengu. Na Sina sababu ya kuacha kuunga mkono ukweli huo wakati dhahiri naliona tatizo.

Hakuna kijana utasema Yuko chonjo kwenye mazingira ambayo tayari mfumo umeshaundwa kuaccomodate waoga, na akitokea yoyate anayetaka kuhoji mazingira hayo ni lazima apoteze nafasi yake ya masomo. Yaani mfumo wetu wa elimu huko vyuoni ni rafiki kwa wasio na uwezo wa kuhoji mambo ya msingi. Ili uwe salama kwenye elimu yako ni lazima kuwa kondoo. Na ukondoo kwenu chawa ni dalili ya utulivu na uelewa.

Wanasubiri watuadhibu wapi boss, kungekuwa na mazingira ya kweli ya kuadhibiana ungeona matokeo ambayo ingekuwa fedheha kwenu vibaraka wa watawala, na mnaoawasujudu. Sio ule upuuzi ambao vyombo vya Dola vinaona fahari kutumika kulinda mabox ya kura za wizi.
basi sawa,
songa mbele kulaumu na kulalaama acha na wengine wasonge pia kwa uhuru...

Kumbuka kuna madhara kisaikolojia na kiroho ukikaza na kushupaza sana shingo kwa uchungu.

Usichakaze nafsi, akili na fikra kwa kuchochewa au kuhemshwa na mirengo ya kisiasa au utofauti wa fikra au kukataliwa kuungwa mkono.

Inauma ila itabidi uzoee tu
 
Waambie Bagonza na Jenerali Ulimwengu kwamba wao ni mfano mzuri wa waliyoyaandika. Kwamba baada ya kumaliza chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia ya msingi na kuendelea kama wanavyodai kwani wao walimaliza mapema. Ikitokea kuwajibishwa wao ndio wa kwanza. Mkumbushe Jenerali Ulimwengu kwamba Joseph Sinde Warioba na yeye walipigwa/walichapwa bakora Ikulu na mwalimu Nyerere kwa kauli kama hizo, hivyo asisahau.
Mkuu tupo kwenye mjadala kuhusu mada nyeti (seroius). Kwahivyo rejea tena kusoma hili bandiko, halafu rudi tujadili seroiusly. Madai ya Bagonza na Ulimwengu ni very serious na hivyo tujadili seriously.
 
Back
Top Bottom