Uchaguzi 2020 Embu tuambizane ukweli, CHADEMA inatumia kigezo gani kusema itashinda?

Vigezo vya CCM kishinda kwa kishindo ni pamoja na Lissu, Mgombea Urais kupitia CHADEMA kutokujua wapiga wanajua walikotoka walipo na wanapitaka kwenda, badala yake:
√ anaacha nyuma maswali mepesi yanayojibiwa na wagombea wa CCM ngazi ya Ubunge na Udiwani, kirahisi na wepesi;
√ anaacha hoja nzito zisizoweza kutetewa na wagombea wa chama chake, ngazi ya Ubunge na Udiwani; na
√ kuhubiri chuki na fitina kwa jamii ambayo inajua thamani ya amani.
 
Kwa hiyo, Chadema wanajisemea tu bila kuwa na Hesabu za uhakika kwamba watashinda?
 
Unajua mimi namuunga mkono mgombea wa JPM lakini nawapinga baadhi ya ccm ambao hawako serious kiasi wanamfanya mh anaonekana mwepesi sana.

Hoja ulizotoa hapa hazina mashiko kabisa kwa mtu yetote anaefuatilia hizi kampeni.

Wanatoa majibu mepesi kwa hoja nzito(kumbuka hoja zina tuhuma ambazo hazijibiwi)

Hoja zake amezipanga vema. usimdharau ,acha kutegemea msaada.

Hakuna fitina anazohubiri, ungesema analalamika ungeeleweka.

Mi ninasababu zangu za kumuunga mkono JPM lakini hazipo kabisa kwenye ambayo umeongea hapo juu.
 
Mkuu nakuunga mkono,

Mh Magufuli, yapo ambayo ki ukweli mtu ukiamua NDIYO yawe ni msimamo, huwezi kumpa Kura,

Jambo moja tu ambalo litamfanya apate Kura yangu ni kule kusema kwake na kufanya papo Kwa papo
 
Ahaaa! We jamaa vipi? Kwanza mwandiko wako mbaya. Pili, umeshindwa kuchambua kiuweledi namna CCM ilivyojiaminisha kushinda uchaguzi.
Labda uniambie mna uhakika wa kushinda uchaguzi sababu watangaza matokeo ni ngome yenu (Refa wa mchezoni mmemuandaa ninyi).
 
Kama kigezo ni kujaza watu ndio ushindi, basi, Magufuli ni mshindi wa Kura mara nne zaidi ya mpinzani wake mkuu

Kwani wanafunzi wanapiga kura? Kama idadi ya watu kwenye mikutano sio kigezo cha kupata kura, basi Lipumba ndio atashinda uchaguzi.
 

Chadema inaweza kushinda kwenye majiji makubwa mfano Dar, Mbeya, mikoa mingine kama Moshi, Arusha, Kigoma, Bukoba nk. Ila hata huko watagawana kura na CCM.

Wanachama wa muda mrefu wa CCM watakwenda kupiga kura kwa wingi ukilinganisha na vijana ambao wengi ndio wafuasi wa CDM.

Nilitegemea CDM watajikita kwenye Sera zinazowagusa Watanzania wengi washikilie hapo hapo kila siku. Wakisema wenyewe watafanya nini?

Kilimo - Nchi inahitaji kilimo cha kisasa cha umwagiliaji,mbolea pembejeo hapa wangeweza kutoa hata incentive kama Tax break kwa miaka kadhaa ili wawekezaji waanzishe viwanda hapa Tanzania.

Masoko ya bidhaa za kilimo hasa ya nje yaimarishwe na kuongezwa. Mahindi (Kenya) Mchele (Rwanda, Burundi, DRC, Comoro, South Sudan hadi Ulaya, USA,Uarabuni hadi Far East.

Avocado, machungwa, Tangarine, mananasi,mapapai, mboga mboga, hadi maua, yote yanaweza kutafutiwa masoko ya uhakika kwenye supermarkets za huko.

TRA :-- Hapa wangekuja na sera za kuhakikisha watu hawaonewi na kubambikiwa kodi ambazo haziendani kabisa na uhalisia, Camera kwenye Ofisi zote za umma, body camera kwa maofisa wote wa TRA, askari wa barabarani, Polisi ingewezesha kupunguza mambo ya rushwa kuongeza uwajibikaji makazini.

Kutumia zaidi IT kungeongeza ufanisi na kupunguza gharama. Kodi kwenye Bandari, Airports inabidi ziangaliwe kwa umakini upya, mfano gari sio luxury item, ni kama simu, necessity of life.

Uvuvi na ufugaji wenye tija, Mikopo kwa ajiri ya kununua boti za kisasa za uvuvi. Ufugaji wa kisasa, pamoja na kutafuta masoko ya uhakika ya ndani na nje kwa samaki na nyama zetu. To streamline process (kurahisisha, kuondoa ukiritimba) ya kupata export license.

Mfumo wa elimu inabidi ufumuliwe, ujikite zaidi kuwasaidia vijana kuwa tayari kukabiliana na changamoto za ajira na maisha kwa ujumla.

Afya:- hospitali, vituo vya Afya inabidi kuzidi kuimarishwa hasa vijijini.

Maji:- salama kila sehemu ya Tanzania itasaidia sana kupunguza magonjwa mengi, hivyo kuongeza nguvu kazi na kupunguza gharama za matibabu kwa serikali.

Miundombinu siyo vitu vya kubeza (barabara, bandari, reli, meli, umeme wa uhakika, ndege).

Hivi ni vitu ndivyo vitasaidia mazao kuchukuliwa vijijini na kupelekwa masokoni mijini na nje ya nchi hiyo itasaidia ku - improve utalii na uchumi wa watu.

Issue, discussion labda iwe asilimia ngapi?iwekezwe wapi? kwa muda gani? Kwa uwiano upi?
 
Kwa kuwa ilishawahi kushinda kwani wewe hujui.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu kubwa ya wanachama wa Ccm ni wale wanao nunuliwa kadi wakati wa mchujo wa ngazi mbalimbali za uongozi mf ubunge wakati huo. Wengine ni wale wanaopewa kadi ili wapewe kazi fulani wakati wa matukio kama vile kampeni. Kwa hiyo wanachama wa kweli hawafiki 4m. Tena katika hiyo idadi wapo wanachama waliosusa kutokana na mambo mbali mbali ikiwemo kuenguliwa katika chaguzi, wao wenyewe au watu wao. Na kuna wengine kadi za Ccm ni kama vitambulisho kutokana na hali ya maisha. Ingekuwa wapo 14m wasingepiga kampeni wala magoti mbele ya watoto. Zaidi wange gawana pesa.

Sent from my itel W6002 using JamiiForums mobile app
 
Kwa mjibu wa website ya CCM, na Kwa mjibu wa kauli ya mwenezi wa CCM ndugu Hamphuley Polepole, CCM inawanachama wa kudumu M.14+. Na kikawaida, ili uwe mwanachama wa Chama chochote, maana yake uwe umefikia umri wa miaka 18+
 
Tume, Tume, Tume, inaibeba CCM! Bado hamjapata jinsi ya kushinda? Mnatia aibu! Kwa maana hiyo CHADEMA kikipewa ridhaa ya kuongoza nchi kitashindwa kuilinda?
 

Chadema wana uhakika wa kushinda kwa sababu wanajuwa kwamba CCM na vibaraka wake hawajawahi kushinda. CCM lao ni kudanganya tu kama wanafanya uchaguzi lakini uhalisia ni kwamba wao wako madarakani kutokana na uchakachuaji wa kura. Hebu angalia hii link hapo chini!

https://www.facebook.com/
 
Hoja gani ya Lissu isiyo na jibu

Kwa mfano anadai vitambulisho vya wafanya biashara havina maana ni ghali. Mhusika ana jibu. Ati mjamzito anatozwa kodi akienda kujifungua. Mjamzito ana jibu. Kwamba pesa imetumika kununua ndege badala ya mahitaji mengine. Mfanya biashara anayetumia ndege ana jibu

Hoja yangu ni kwamba maswali anayouliza angekuwa na muda, au angetumia intelenjisia yake, angepata majibu kutoka kwa makundi anayoamini utawala wa Magufuli umeyakandamiza. Anaongea kwa hisia pasipo ukweli wowote. Baadhi ya maswali ya kisera, siyo utendaji, yanajibiwa kwenye kampeni na viongozi wa CCM km bima ya afya, maendeleo ya vitu, nk

Lissu ndiye mwenyewe anaingia kwenye chaka au choo cha jinsi tofauti
 
Huu ndio ukweli ambao CCM hawautaki kuukubali! Ila wanaujua sema wanajitoa tu ufahamu!
 
Eti hawajawahi kushinda!!

SASA kama hawajawahi kushinda mbona ndio huwa wanaapishwa na kuingia Ikulu?
 
Hao ni wapiga kura ni
wanahamasa na ni vijana ambao wanajaki ya kwenda kusikila kinacho nadiwa kwa maslahi mapana ya faida yao kama kizazi konachofata kumuka wapiga kura ni million 29 na kati ya hao 15million ni vijana.
Wakati CCM ikipanda mbegu, wengine bado wanaona bado kiangazi mbegu hazitaota,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…