Emirates yafanya maajabu uwanja wa ndege dar es salaam

Emirates yafanya maajabu uwanja wa ndege dar es salaam

Mabulangati

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2010
Posts
796
Reaction score
167
Wandugu jana nilienda kumpokea mgeni wangu toka Sri Lanka pale Julius Nyerere international Airort (Dar es Salaam). Saa 9.06 mchana Ndege ya shirika maarufu duniani Emirates iliwasili lakini ilipokanyaga ardhi tu ikapaa tena kurudi angani na kutua rasmi baada ya dakika kama 38 hivi. Sijui kilichotokea au ni kikwazo gani kilileteleza ndege hiyo kurudi angani ia mgeni aliposhuka alinieleza kuwa rubani aliomba radhi kwa kuchelewa kutua ila hakusema sababu za kutua na kupaa kwa haraka kiasi kile.

Jamani wenye taarifa zaidi za tukio hili hasa wa mamlaka ya viwanja vya ndege watujuze. Maana tumezoea mambo hayo yakifanywa na ndege za kijeshi siyo za abiria.

Journalists may wish to consult Emirates officers or TAA for elaborations on this.
 
Wandugu jana nilienda kumpokea mgeni wangu toka Sri Lanka pale Julius Nyerere international Airort (Dar es Salaam). Saa 9.06 mchana Ndege ya shirika maarufu duniani Emirates iliwasili lakini ilipokanyaga ardhi tu ikapaa tena kurudi angani na kutua rasmi baada ya dakika kama 38 hivi. Sijui kilichotokea au ni kikwazo gani kilileteleza ndege hiyo kurudi angani ia mgeni aliposhuka alinieleza kuwa rubani aliomba radhi kwa kuchelewa kutua ila hakusema sababu za kutua na kupaa kwa haraka kiasi kile.

Jamani wenye taarifa zaidi za tukio hili hasa wa mamlaka ya viwanja vya ndege watujuze. Maana tumezoea mambo hayo yakifanywa na ndege za kijeshi siyo za abiria.

Journalists may wish to consult Emirates officers or TAA for elaborations on this.

Mdau Mabulangati, hilo ni jambo la kawaida, hata mimi limeshawahi nitokea na rubani alisema ni tatizo la upepo. Ndege zina kifaa cha kupimia upepo wa chini (ground wind flow) ila sometimes due to several reasons hua hakipimi sawasawa mpaka pale ndege inapofika chini ndio rubani anagundua upepo ni mkali na si salama kwa ndege kutua in that direction so hua wanarudi angani na kubadilisha direction ya kutua then wanatua in different direction ila pia inategemeana na uzito wa ndege wakati huo.
 
Nashukuru nimeekewa. Lakini kwa mujibu wa mgeni wangu, hakukua na maelezo yoyote kuhusu hilo hivyo kwangu ilikua maajaby
 
Sidhani kama ni Maajabu? Mkuu itakuwa ni mara yako ya kwanza kufika viwanja vya Ndege.... kweli kwako lazima iwe Ajabu.... na huyo mgeni wako pengine....

Kipofu kumuelekeza kipofu mwenzie wote watatumbukia shimoni....
 
Duh! hata mimi hilo nilikuwa silijui! nilifikiri ni ndege za jeshi tu ndio zinaweza kufanya hivyo!
 
Mkuu mabungata, hilo sio jambo la ajabu bali ni la kawaida sana, sio hata wakati ndege ikiwa tayari imegusa ardhi bali hutokea hata ndege kuzunguka zunguka angani juu ya uwanja au kuupita kabla ya krudi na kutua. Hii inategemeana na hali ya uwanja kwa muda huo kama vile mwelekeo wa upepo na kasi yake, kutoa nafasi kwa ndege nyingine inayotaka kuruka muda huo. Wakati mwingine kabla hata ndege haijagusa ardhi unashtukia inarudi juu tena kwa kasi ya ajabu mpaka mnajisikia vibaya kama kizunguzungu vile; au ndege inatua, ikishapunguza mwendo na kuanza kuelekea eneo la kushusha inasimama kipindi kirefu halafu unaona inaendelea kwa hiyo hayo sio maajabu ni mambo ya kawaida na mara nyingi Cabin Crew unasikia wanaomba samahani lakini hawasemi kulikuwa na tatizo gani.
 
Last edited by a moderator:
Pia emergncy landing inasababisha ndege ya kwanza iliopewa ruhusa ku tua ikapewa amri ya kurruka tena ili kuipisha ndege nyengne kutua ilio request may day
 
inawezekana tembo alikuwa akikatisha na rubani akabadilisha uamuzi kwa kujuwa tembo atachelewa kukatisha barabara

Hiyo inatokea kwa ndege yoyote ile sio Emirate pekee kama ilivyoandikwa hapo juu ni missed approach au sababu nyengine hata CT anaweza kumuamuru rubani kurudi angani tena
 
kama walivyoelezea wadau hapo na ndio maana ndege hizi huwa na mafuta ya ziada ya kuzunguka huko juu au hata ya kwenda kutua kiwanja kingine iwapo hali ya hewa itakuwa bado hairidhishi....naipenda jf kwani kila uzi ni shule kwa baadhi ya watu kwani wataalamu wa sekta husika hufunguka bila kinyongo na kutafuta material ya kuwezesha somo kueleweka zaidi
 
Mdau Mabulangati, hilo ni jambo la kawaida, hata mimi limeshawahi nitokea na rubani alisema ni tatizo la upepo. Ndege zina kifaa cha kupimia upepo wa chini (ground wind flow) ila sometimes due to several reasons hua hakipimi sawasawa mpaka pale ndege inapofika chini ndio rubani anagundua upepo ni mkali na si salama kwa ndege kutua in that direction so hua wanarudi angani na kubadilisha direction ya kutua then wanatua in different direction ila pia inategemeana na uzito wa ndege wakati huo.

Acha uwongo wako wewe, hahahahaaaa! Air traffic controller ndio anaetoa wind direction ambayo imepimwa na ofisi ya mamlaka ya Hali ya hewa dakika chache kabla ya ndege kutua. Pia air traffic controller ndio anaemshauri rubani atue kwa njia ipi kulingana na upepo aliomtajia.
 
Back
Top Bottom