Tarishi
Senior Member
- May 9, 2008
- 105
- 150
Vyombo vya habari vya Tanzania vinaonekana kuifuta mipaka kati ya uandishi wa habari na hadithi za mitaani, kwa ku-copy na ku-paste kila habari wanayopata bila kuchimba zaidi kutafuta ukweli.
Drama ya hivi karibuni inayowahusisha Madaraka Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, na Steve Mengele, anayejulikana kwa jina maarufu la Steve Nyerere, ni mfano halisi wa uvivu huu wa wanahabari. Badala ya kufanya kazi yao na kuchunguza kwa nini ghafla Madaraka ameamua kumwambia Steve aache kutumia jina la Nyerere, ilhali amekuwa akilitumia kwa miaka mingi, wanahabari wamekopi tu habari kama ilivyo bila kuuliza maswali ya msingi ama kuchunguza nini chanzo halisi ama kisababishi?
Ngoja niwasaidie wanahabari, kwa sababu baada ya kuwafanyia kazi yao ya kiuchunguzi, hatimaye nimegundua kiini cha sakata hili. Hapa kuna siri nzito ambayo inaweza kueleza vurugu hii. Na sio kwamba Steve anaiga sauti ya Mwalimu au anapenda sifa za kuiwa na jina la Nyerere.
Tatizo halisi linamhusisha Emma Lwaitama Nyerere, mwanaharakati maarufu na binti wa mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dr. Azavery Lwaitama, ambaye pia amekuwa akitumia jina la Nyerere kwa muda mrefu sasa. Emma si mwanaharakati wa kawaida; kwa miaka kadhaa amekuwa akidai kuwa ni binti wa Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jambo ambalo si kweli. Rekodi zinaonesha amekuwa hata akikaribishwa majumbani ama Ikulu kwa viongozi wanaompenda na kumthamini Mwalimu Nyerere. Kwao wao kuwa na “binti” wa Mwalimu ilikuwa furaha na fahari ilioje.
Awali alikuwa akijitambulisha kama mtoto wa Mama Maria, baada ya kuhitimu utamu wa jina na kuonja faida zake, akawa “binti” wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Soma Pia: Kumbukizi ya Nyerere: Familia ya Mwalimu Nyerere yawataka wasanii kuacha kutumia jina la Baba wa Taifa kama ubin wao
Sasa, hapa ndipo ulipo mwiba wenyewe, ambao hata Madaraka anaonekana kuuogopa usimchome: Emma amezaa mtoto na Kambarage Joseph Nyerere, ambaye ni mtoto wa kambo mdogo wa Mwalimu, Joseph Nyerere! Kimsingi, Emma angekuwa na haki kabisa ya kutumia jina la Nyerere iwapo wangekuwa wameoana, lakini hawajaoana bado.
Hivyo basi, uhusiano wa Emma na jina la Nyerere ni wa kulazimisha. Au angalau asingekuwa anafanya haya yafuatayo.
Sasa, mambo yalianza kuchafuka pale Emma alipoanza kujitokeza kwenye majukwaa ya kitaifa na kimataifa, akipigia debe ajenda zake za kisiasa, ikiwa ni pamoja na kuunga mkono taifa la Palestina huku akilaani vikali vitendo vya Israel.
Sio siri kwamba msimamo wake huu wa wazi kuhusu Palestina, hasa kwenye majukwaa ya kimataifa, umechokoza hisia za baadhi ya mataifa ya Magharibi.
Mataifa haya yanaona kama ni fedheha ya kidiplomasia kwamba mtu wa familia ya Nyerere anazua kasheshe kwenye masuala nyeti ya kimataifa.
Tuseme tu, "wakubwa" hawajaridhika kabisa. Na kutokana na diplomasia nyeti ya Tanzania ya kutofungamana na upande wowote, kuna dalili kwamba shinikizo limetolewa chini kwa chini. Na hapa ndipo hadithi inakuwa tamu.
Vyanzo vya ndani vinaashiria kwamba msimamo wa Emma kuhusu Palestina, unaoendelea kuakisi msimamo wa zamani wa Julius Nyerere aliyewaunga mkono Wapalestina waziwazi, umewaudhi "wakubwa.” wa magharibi.
Inaonekana wameishinikiza familia ya Nyerere kumvuta Emma chini, wakitaka jina hilo lisihusishwe kabisa na siasa hizo za kimataifa, huku wakipigwa mkwara wa “Hiyo ilikuwa zamani, sasa mchezo umebadilika. Kwa hiyo, mnyamazisheni! Vinginevyo…”
Sasa familia ya Nyerere inafanyaje? Badala ya kumkemea Emma moja kwa moja, wanamtuma Madaraka, msemaji wa familia. Lakini yeye, badala ya kukabiliana na chanzo halisi—Emma kutumia jina la Nyerere kwenye majukwaa ya kimataifa—wanaamua kumshambulia Steve Nyerere, ambaye utaamua mwenyewe kama ana ama hana hatia ya kupewa jina hilo na mashabiki wake kwa kuiga sauti ya Mwalimu.
Steve anakula za uso huku watu wengine wanaotumia jina la Nyerere.Mfano mwingine ni kama huyu Yericko Nyerere, anayejinasibu yu mtaalamu bingwa wa masuala ya ujasusi na dilomasia na uchumi na mwandishi wa vitabu vya masuala ya ujasusi ambao wanaendelea kula bata kwa jina la Mwalimu.
Yericko, ambaye anatokea Iringa (kama Steve), sii Mzanaki na hana uhusiano kabisa na Mwalimu. Lakini Madaraka kammezea!
Kuna dhana kwamba huenda kutoikana na umaarufu alio nao, imeonekana ujumbe utafika haraka zaidi endapo kama watamtumia Steve kama mbuzi wa kafara.
Wengine watamalizana nao baadae mmoja mmoja. Sasa basi, sina haja ya kuwatafunia kila kitu enyi wanahabari, habari ndiyo hiyo. Tafuteni ukweli. Muulizeni Madaraka yote haya. Na kwa upendo wa Mungu, acheni ku-copy na ku-paste! Jifunzeni kuchunguza mambo kama nilivyoiwasaidia hapa!
Alamsiki
Drama ya hivi karibuni inayowahusisha Madaraka Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, na Steve Mengele, anayejulikana kwa jina maarufu la Steve Nyerere, ni mfano halisi wa uvivu huu wa wanahabari. Badala ya kufanya kazi yao na kuchunguza kwa nini ghafla Madaraka ameamua kumwambia Steve aache kutumia jina la Nyerere, ilhali amekuwa akilitumia kwa miaka mingi, wanahabari wamekopi tu habari kama ilivyo bila kuuliza maswali ya msingi ama kuchunguza nini chanzo halisi ama kisababishi?
Ngoja niwasaidie wanahabari, kwa sababu baada ya kuwafanyia kazi yao ya kiuchunguzi, hatimaye nimegundua kiini cha sakata hili. Hapa kuna siri nzito ambayo inaweza kueleza vurugu hii. Na sio kwamba Steve anaiga sauti ya Mwalimu au anapenda sifa za kuiwa na jina la Nyerere.
Tatizo halisi linamhusisha Emma Lwaitama Nyerere, mwanaharakati maarufu na binti wa mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dr. Azavery Lwaitama, ambaye pia amekuwa akitumia jina la Nyerere kwa muda mrefu sasa. Emma si mwanaharakati wa kawaida; kwa miaka kadhaa amekuwa akidai kuwa ni binti wa Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jambo ambalo si kweli. Rekodi zinaonesha amekuwa hata akikaribishwa majumbani ama Ikulu kwa viongozi wanaompenda na kumthamini Mwalimu Nyerere. Kwao wao kuwa na “binti” wa Mwalimu ilikuwa furaha na fahari ilioje.
Awali alikuwa akijitambulisha kama mtoto wa Mama Maria, baada ya kuhitimu utamu wa jina na kuonja faida zake, akawa “binti” wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Soma Pia: Kumbukizi ya Nyerere: Familia ya Mwalimu Nyerere yawataka wasanii kuacha kutumia jina la Baba wa Taifa kama ubin wao
Sasa, hapa ndipo ulipo mwiba wenyewe, ambao hata Madaraka anaonekana kuuogopa usimchome: Emma amezaa mtoto na Kambarage Joseph Nyerere, ambaye ni mtoto wa kambo mdogo wa Mwalimu, Joseph Nyerere! Kimsingi, Emma angekuwa na haki kabisa ya kutumia jina la Nyerere iwapo wangekuwa wameoana, lakini hawajaoana bado.
Hivyo basi, uhusiano wa Emma na jina la Nyerere ni wa kulazimisha. Au angalau asingekuwa anafanya haya yafuatayo.
Sasa, mambo yalianza kuchafuka pale Emma alipoanza kujitokeza kwenye majukwaa ya kitaifa na kimataifa, akipigia debe ajenda zake za kisiasa, ikiwa ni pamoja na kuunga mkono taifa la Palestina huku akilaani vikali vitendo vya Israel.
Sio siri kwamba msimamo wake huu wa wazi kuhusu Palestina, hasa kwenye majukwaa ya kimataifa, umechokoza hisia za baadhi ya mataifa ya Magharibi.
Mataifa haya yanaona kama ni fedheha ya kidiplomasia kwamba mtu wa familia ya Nyerere anazua kasheshe kwenye masuala nyeti ya kimataifa.
Tuseme tu, "wakubwa" hawajaridhika kabisa. Na kutokana na diplomasia nyeti ya Tanzania ya kutofungamana na upande wowote, kuna dalili kwamba shinikizo limetolewa chini kwa chini. Na hapa ndipo hadithi inakuwa tamu.
Vyanzo vya ndani vinaashiria kwamba msimamo wa Emma kuhusu Palestina, unaoendelea kuakisi msimamo wa zamani wa Julius Nyerere aliyewaunga mkono Wapalestina waziwazi, umewaudhi "wakubwa.” wa magharibi.
Inaonekana wameishinikiza familia ya Nyerere kumvuta Emma chini, wakitaka jina hilo lisihusishwe kabisa na siasa hizo za kimataifa, huku wakipigwa mkwara wa “Hiyo ilikuwa zamani, sasa mchezo umebadilika. Kwa hiyo, mnyamazisheni! Vinginevyo…”
Sasa familia ya Nyerere inafanyaje? Badala ya kumkemea Emma moja kwa moja, wanamtuma Madaraka, msemaji wa familia. Lakini yeye, badala ya kukabiliana na chanzo halisi—Emma kutumia jina la Nyerere kwenye majukwaa ya kimataifa—wanaamua kumshambulia Steve Nyerere, ambaye utaamua mwenyewe kama ana ama hana hatia ya kupewa jina hilo na mashabiki wake kwa kuiga sauti ya Mwalimu.
Steve anakula za uso huku watu wengine wanaotumia jina la Nyerere.Mfano mwingine ni kama huyu Yericko Nyerere, anayejinasibu yu mtaalamu bingwa wa masuala ya ujasusi na dilomasia na uchumi na mwandishi wa vitabu vya masuala ya ujasusi ambao wanaendelea kula bata kwa jina la Mwalimu.
Yericko, ambaye anatokea Iringa (kama Steve), sii Mzanaki na hana uhusiano kabisa na Mwalimu. Lakini Madaraka kammezea!
Kuna dhana kwamba huenda kutoikana na umaarufu alio nao, imeonekana ujumbe utafika haraka zaidi endapo kama watamtumia Steve kama mbuzi wa kafara.
Wengine watamalizana nao baadae mmoja mmoja. Sasa basi, sina haja ya kuwatafunia kila kitu enyi wanahabari, habari ndiyo hiyo. Tafuteni ukweli. Muulizeni Madaraka yote haya. Na kwa upendo wa Mungu, acheni ku-copy na ku-paste! Jifunzeni kuchunguza mambo kama nilivyoiwasaidia hapa!
Alamsiki